Mchungaji Auawa Saa Chache Baada ya Kushiriki Mjadala wa Waislamu na Wakristo – Imamu ni Miongoni mwa Washukiwa
Mchungaji Bernard Mulongo alishiriki katika mazungumzo ya kidini kati ya Wakristo na Waislamu kabla ya kuonekana katika kipindi cha redio ya eneo hilo.
Inaripotiwa kuwa wanawake wawili Waislamu walibadili dini na kuwa Wakristo wakati wa mjadala huo, jambo ambalo ni wachache walilitegemea.
Mulongo alikutwa amefariki dunia akiwa na majeraha mengi baada ya washambuliaji waliokuwa kwenye pikipiki kumzuia njiani.
Mchungaji mwenye umri wa miaka 25 anadaiwa kuuawa saa chache baada ya kushiriki katika mjadala wa kidini unaohusisha imani tofauti, huku wachunguzi wakiripotiwa kumchukulia mmoja wa washiriki wa tukio hilo kama mshukiwa mkuu.
Mchungaji Bernard Mulongo wa Kanisa la New Restoration Church of Christ alihudhuria mjadala wa wazi kati ya Wakristo na Waislamu katika Wilaya ya Butebo kabla ya kushiriki katika kipindi cha redio ya eneo hilo ili kuendeleza mazungumzo hayo.
Mchungaji mwenzake, David Omala, alisema hali ya mjadala huo ilianza kuwa ya taharuki baada ya wanawake wawili Waislamu kubadili dini na kuwa Wakristo hadharani wakati wa tukio hilo.
Kwa mujibu wa gazeti la Christian Post, Omala alidai kuwa mmoja wa washiriki Waislamu alionyesha dhahiri kukasirishwa na tukio hilo.
Imam huyo anaripotiwa kumtuhumu Mchungaji Mulongo kwa kuwapotosha Waislamu na kutumia Quran kuwavutia watu kujiunga na Ukristo.
Mulongo alikuwa amesafiri kwenda Mbale mahususi kwa ajili ya tukio hilo la kidini, na anaamini kuwa uhasama uliofuatia mjadala huo na kipindi cha redio huenda ulichangia katika matukio yaliyofuata usiku huo.
Rafiki wa mchungaji huyo marehemu, Robert Mukisa, alieleza kuwa wawili hao walikuwa wakisafiri pamoja kwa pikipiki kuelekea mahali pao pa malazi wakati kundi la wanaume waliokuwa kwenye pikipiki lilipowazuia njia katika kijiji cha Jami, takriban maili tisa kutoka Mbale.
Mukisa alisema mmoja wa washambuliaji alimtuhumu mchungaji huyo kwa kuwavutia watu kuacha Uislamu. Mukisa alikimbia eneo hilo na kutoa taarifa kwa polisi mara moja.
Maafisa wa polisi na viongozi wa kanisa walipofika eneo la tukio, walimkuta Mchungaji Mulongo akiwa amefariki dunia, huku akiwa na majeraha mengi kichwani, kifuani, mgongoni na mkononi.
Mwili wake ulihamishiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Mbale City kwa uchunguzi kabla ya kuachiliwa kwa familia yake kwa mazishi katika Wilaya ya Butebo.
Vyanzo vinavyofahamu uchunguzi huo vinasema imamu huyo ni miongoni mwa wanaochunguzwa na inadaiwa amejificha.
Polisi walianzisha uchunguzi, lakini hakuna aliyekamatwa wakati ripoti za tukio hilo zilipochapishwa.
Katiba inalinda uhuru wa kuabudu, kutia ndani haki ya mtu kubadili imani yake na kufuata imani yake waziwazi.
Kifo cha Mulongo kimeibua upya wasiwasi kuhusu usalama wa viongozi wa kidini wanaojihusisha na uenezaji wa dini mbalimbali na mazingira mapana ya uvumilivu wa kidini katika eneo hilo.
Kwingineko, video ya Mchungaji Victor Kanyari akiongea kwa dharau kuhusu marehemu mke wake wa zamani, Betty Bayo, katika kanisa lake mwenyewe imewakasirisha Wakenya.
Katika klipu hiyo, kasisi huyo alidai kwamba Betty alikataa maombi yake na kukataa kuwa naye kabla ya kufa.
Wakenya walionyesha kutoamini kwamba pasta angetumia mimbari yake kumdhihaki mwanamke aliyeaga dunia, na ambaye pia alikuwa mama wa watoto wake.
Chanzo: TUKO

