MWANAMKE ALIYECHORA TATTOO YA RAIS RUTO, ACHOMWA MOTO HADI KUFA – TAZAMA VIDEO YAKE WAKATI AKIWA HAI
Chanzo: TUKO
Rachel Wandeto aliungua vibaya kutokana na shambulio la petroli na kuaga dunia alipokuwa akipokea matibabu. Klipu ya hivi majuzi ya Wandeto inayosimulia kwamba tattoo ya Rais Ruto iligharimu ndoa yake iliibuka tena baada ya kifo chake. Mwimbaji huyo alifichua alichofanya mumewe baada ya kujichora tattoo hiyo licha ya ndoa yao ya muda mrefu.
Video ya Rachel Wandeto akisimulia jinsi tattoo ya Rais William Ruto ilivyogharimu ndoa yake imeibuka tena mtandaoni baada ya kifo chake.
Mwimbaji huyo wa nyimbo za injili ambaye alijitokeza hadharani kuunga mkono kuchaguliwa tena kwa Rais Ruto, alizungumzia madhara ya kujichora tattoo kwenye uso wa rais na kauli mbiu zake za kisiasa kwenye mwili wake. Wandeto alifariki alipokuwa akipokea matibabu katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta baada ya kupata majeraha mabaya ya moto kutokana na shambulio hilo la kinyama la petroli.
Je, mume wa Rachel Wandeto alimtupa kwa sababu ya tattoo ya Ruto? Katika mahojiano ya awali na mshawishi wa Akorino, Wandeto alifichua kuwa mumewe alimtelekeza.
“Kwa sasa nipo singo kwa sababu mume wangu alinitupa kwa sababu ya tattoo hii, najua ni nzito kwa mume wangu, lakini haiwezi kutenduliwa, nilipofanya hivyo sikujua kungekuwa na matokeo, lakini hadi kufikia hatua ya ndoa yetu kuvunjika, bado ni mume wangu na ninampenda, tumekuwa pamoja kwa zaidi ya miaka 10… singeweza kufuta tattoo hii kwa sababu nampenda Ruto,” alisema.
Wandeto alieleza kuwa mapenzi yake kwa Ruto hayana uhusiano wa kimapenzi, na kuapa kutoondoa tattoo hiyo, jambo ambalo lilimkosoa kwenye mitandao ya kijamii. “La sivyo, mtu akija kunilipia mahari, sijui kitakachotokea kwa sababu kwenye bega langu, Ruto yuko tayari, na hatuwezi kutengua. Hata hivyo, kumbuka kuwa simpendi kimapenzi; yeye ni mwanamume aliyeoa na familia,” alisema.
TAZAMA VIDEO

