Msomi wa PHD asimama Barabarani na Bango akiomba Ajira Kutoka kwa Rais
Chanzo: TUKO
Mwanamume mmoja amejitokeza barabarani kuelezea kufadhaika kwake baada ya kukosa kupata kazi licha ya kuwa na sifa za kuvutia za masomo. Mtumiaji wa TikTok Ayomide Alokun alijiunga na wahitimu wengi wa chuo kikuu ambao walikua wakiamini kuwa elimu ndio ufunguo wa mafanikio, hata hivyo bado hana kazi. Alionyesha sifa zake kwenye bango huku akiomba kazi kwa rais, akionyesha nia yake ya kufanya kazi na kuleta tija.
“Tulipokuwa wadogo, tuliambiwa tusome vitabu vyetu ili tuwe viongozi siku moja. Sasa tuna sifa zote duniani, lakini hakuna ajira. Inasikitisha sana,” aliandika video yake.
Akiwa amevalia mavazi rasmi, Alokun aliomba kazi kutoka kwa mkuu wa nchi, akitarajia fursa ambayo inaweza kubadilisha maisha yake. Ayomide Alokun ana umri gani? Akiwa na umri wa miaka 27, Alokun alifichua kwamba ana shahada ya kwanza, shahada ya uzamili katika Sayansi ya Siasa, na PhD katika Uhusiano wa Kimataifa.
“Bwana Rais, bwana, nipe kazi. Sijui jinsi ya kutumia Yahoo. Sijui kuimba kama Burna Boy, na sijui kucheza kandanda kama Victor Osimhen, lakini nina sifa,” bango lake lilisomeka. Alipotafuta nafasi ya kazi, sura yake ya uso ilionyesha huzuni na kukata tamaa alipokuwa akiomba msaada aliohitaji sana. Watu na magari yalipita huku akiinua bango lake kwa fahari, akitarajia mafanikio au muujiza.
TAZAMA VIDEO
@ayomidealokun Thank you Africa for the massive support 🙏. Day 3 of my job hunt on the streets of Abuja until I bag a job. #unemployed #africa #trending #foryoupage #goviral @CNN @BBC News ♬ sonido original – YOSELIN♥️✨️

