NAINGIZA KICHWA TU
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Chapter 1
“Haitopendeza kabisa nichepuke,”
“Ni kweli, jaribu kumzoesha taratibu atazoea,”
“Hataki hata kusikia hizo habari,”
“Mh! Hapo pagumu, mimi mke wangu alinigomea lakini mwisho wa siku alikubali,”
“Ulitumia mbinu gani?”
“Kumuomba sana, ilifikia wakati aliondoka nyumbani, lakini aliporudi niliendelea kumuomba mpaka akakubali,”
“Yaani kaka napata tabu sana, huu mchezo sio mzuri kabisa, ukiuanza hauwezi kukuacha salama,”
“Sasahivi tunafurahia tu,”
“Nayatamani maisha hayo sana,”
“Komaa, anaweza akakiachia.”
Maongezi hayo yaliwahusisha marafiki wawili waliokuwa wakishirikishana mambo mengi sana. Multaza ndiye aliyekuwa akipata ugumu juu ya mkewe, aliyekuwa akimshauri aliitwa Ndukanza.
Multaza alporejea nyumbani alimkuta mkewe aliyeitwa Nisha, alikuwa amenuna mno.
“Mke wangu! Hii hali mpaka lini?”
“Mke wangu naongea na wewe, kama kuna tatizo tuliongee,”
“Naomba uniache, kama umenichoka niache!” alisema Nisha kwa hasira
INAENDELEA

