SHUSHA NYEGEZI
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Chapter 2
Dorini alipelekwa mpaka kwa Renatusi ambapo palikuwa ni umbali wa dakika tano tu. Kwa bahati nzuri walipata uwazi dirishani wakachungulia, Dorini alipoona kwa macho yake ndio akaamini, alilia kwa sauti kubwa mpaka Renatusi na mpenzi wake walishtuka.
“Nani analia usiku huu?” Renatusi alihoji
“Sijui, sauti inatokea hapo dirishani.”
Aliamka huyo mwanamke na kuchungulia dirishani, akamuona Kiboro,
“Ni yule bodaboda aliyenileta,”
“Ah! Sasa mbona sauti ni ya kike?”
“Hapo sijajua. Namuona yeye tu.”
Renatusi aliamka na kutoka nje akijiamini maana alimjua Kiboro.
“Dogo vipi?”
“Ni kubaya aisee,”
“Nini tatizo usiku huu?”
“Dorini amekuja na amejua kila kitu, yupo hapo nje analia,”
“Dorini shemeji yako?”
“Ndiyo, nimekupigia sana simu, nimekutumia jumbe nyingi mno lakini hukujibu,”
“Yesu wangu! Kajua kama kuna mwanamke mwingine?”
“Ndiyo.”
Wakiwa wanateta hayo wenyewe wawili pembeni, Dorini kwa sauti ya kwikwi aliipaza,
“Kiboro tuondoke!”
“Sasa nakusikiliza, nifanyeje?”
“Kaka nimechanganyikiwa, dah!”
Renatusi alipojaribu kumfuata Dorini, alichimbwa mkwara mmoja akanywea kama pilitoni.
“Washa pikipiki tuondoke,”
“Dorini lakini…”
“Kaa kimya, wewe si unajua kuto…sasa endelea na umalaya wako,”
“Kiboro hebu washa tuondoke mbona sikuelewi na wewe?”
Basi Kiboro aliwasha pikipiki huku akiwa hajui ni wapi aelekee. Lakini alipokuwa njiani wazo dogo likamjia kuwa anaweza akatumia hasira za Dorini kuingia katikati ya mapaja yake.
Akampeleka mpaka nyumbani kwake, Dorini alikuwa akilia tu, kwikwi kwa wingi zilimtawala.
“Dorini, kwa usiku huu huwezi kurudi ulipotoka, utapumzika hapa kwangu na naomba uache kulia.”
Kiboro alimbembeleza Dorini huku akimkumbatia, Dorini alianza kujieleza jinsi alivyokuwa akimpenda Renatusi, alijitunza kwa muda wote huo ili kulinda heshima yake, aliongea mengi sana.
Wakaingia ndani huku Kiboro obo lake likiwa imara, muda wote alikuwa akimwangalia Dorini kwa macho ya matamanio sana. Kiboro aliendelea kumbeleza tena kwa kumuweka karibu. Akamchemshia maji ya kuoga, akaoga, mwanaume akaingia jikoni akamchemshia maziwa, alimkaangia na mayai matatu kisha akampa, alimbeleleza mpaka akala. Kiboro alimnyenyekea Dorini ambapo alimuonyesha chumba cha kulala, Kiboro akalala sebuleni.
Dorini hakulala kwa muda huo, yalipofika majira ya saa kumi aliamka na kuja sebuleni. Akamkuta Kiboro akiwa amelala anakoroma. Kha! Alishangaa hivyo baada ya kuona obo la Kiboro likiwa limechungulia kwenye uwazi wa paja. Akarudi kitandani, muda huo alikuwa amevalia khanga moja tu. Usingizi ukamchukua.
Asubuhi Dorini alipoamka alikuta tayari supu imeshaandaliwa, pembeni chapati. Dorini aliahukuru, walishiriki wote ambapo Dorini alivalia skini nje khanga. Juu blauzi fulani iliyombana vyema na kufichua chuchu zake zilizochomoza.
Walipomaliza kula. Waliketi hapo sebuleni, wakaanza kucheza karata,
“Leo kazini huendi?”
“Hapana, sijihisi vizuri,”
“Pole, unaumwa?”
“Nahisi, ila usiwaze, cheza nikufunge,”
“Huwezi…”
Wakiwa wanazungumza hivyo, mara Renatusi alibisha hodi, ile sauti yake ni kama ilikuwa msumari kwa Dorini,
“Samahani, naomba nimkomeshe na yeye,”
“Kivipi,”
“Kaa hivyo hivyo, niruhusu tu,”
“Sawa. Nimekupa ruhusa.”
Basi Dorini alipopewa Ruhusa aliitoa ile khanga na kubaki na skini, e bwana eeh! Hilo umbo lilivyojichora vyema, skink yenyewe ilikuwa nyepesi, ilionyesha mistari ya nguo yake ya ndani. Hapo kwenye kei palijichora vyema. Wote walikuwa wameketi kwenye kochi, basi Dorini alipanua miguu yake na kumkalia Kiboro.
“Dogo upo kweli?” Renatusi alizidi kuita
“Usitusumbue bwana.”
Renatusi aliposikia hivyo akaingia ndani moja kwa moja, akamshuhudia Dorini akiwa amemkalia Kiboro, mikono ya Kiboro ikawa inamshikashika makalio.
“Dorini! Kweli?”
.
ITAENDELEA

