MPANGAJI
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Sehemu Ya 11
“Kwa hiyo unataka kusema kuwa unajilinda juu yangu kwa kuwa unahisi nina ugonjwa au magonjwa”.
“Hapana.Hapa nakulinda wewe kwa kila kitu,si magonjwa tu!Bali hata mimba zisizotarajika”.Nilimjibu na kumtania miguu yake ili asiendelee kuuliza maswali zaidi.
Nilipomtanua,nikaachia mzee mzima kuingia uwanjani ili asakate kabumbu alilotegemea kufunga magoli mawili kama dhana alizokuja nazo.
“Mbona hunipi yale mavitu ambayo ulikuwa unanipa wakati umevaa nguo?”.Nilimuuliza swali baada ya kuona najishughulisha peke yangu.
“Mimi siwezi kufanya wakati umevaa hayo,hapa hata sijisikii hamu wala raha,ni kama unanipapasa tu!”.Aliongea Tuse na kunifanya nibaki nimeduwaa kwa maneno yake. Hadi hapo nikajua chale zangu zilikuwa sawa. Yule demu hakuwa bure. Nitakwambia mbele nini kilitokea na ndiyo sababu ya mimi kuondoka pale Dar nilip[okuwa naishi na kaka.
Baada ya kuona ana lake jambo,niliamua kumuacha na kuvaa nguo zangu kwa ajili ya kufanya mambo mengine. Kifupi alikuwa hana radha wala nini,ndo maana niliamua kuachana naye.
“Kwa hiyo unaniacha hivi hivi?”.Aliongea Tuse huku akiwa bado pale juu ya meza.
“Sasa wewe ulitakaje?”.Nikamtupia swali.
“Nipe changu ndiyo mambo yote yataenda sawa”.Alinijibu huku ananioneshea vidole vyake kuwa anahitaji hela.
“Kwani tuliambiana kuwa kutakuwa na malipo?”.Na mimi nilimuuliza baada ya kugundua nia yake.
“Kwani dukani ukienda unaulizia kama kuna malipo au hakuna?Si wajua kabisa naenda dukani na lazima nitalipia”.Aliongea.
“Kwani wewe ni duka?”.
“Hilo halikuhusu,ila jua hapa hela ndiyo kila kitu,hutaki lazima utajuta kuingia kwenye mwili huu”.
“Ha ha haaa,naona unajaribu kutishia kujamba wakati unatumbo la kuhara. Utajiharishia mdogo wangu”.
“Unadhani nakutishia,sikuishi wala sikudanganyi,utaniona mimi ni mbaya. Hivi vimeundwa babu,usione vyaelea tu!”.
“Okey.Kwa hiyo unataka shilingi ngapi?”.
“Laki moja”.
“Zinaokotwa hizo laki moja?Kwa lipi ulilonifanyia?Kwa kipi ulichokifanya wakati mimi nimeingia kwenye dimbwi lako”.
“Mi hayo sijui. Nachotaka hapa ni changu tena fasta.Huna huo mpunga,basi unatakiwa kunisikiliza mimi nachotaka”.
“Sikiliza wewe kuku,mimi siyo wakunipelekesha pelekesha kama mpira wa miguu,na kamwe usinitishie maisha yangu”.
“Unajidai mbishi si ndio eeh. Sasa ngoja uone kuwa hapa umeingia sipo penyewe”.Aliongea Tuse na kushuka pale juu yameza kisha akavaa nguo yake na kutoka nje.
Nilimpuuzia na kumuona ni mwanamke tu! Hana jipya kwangu na wala hanitishi hata kidogo.
Baada ya dakika chache nikasikia geti la kuingilia kwangu likifunguliwa na sekunde kadhaa mwili wa Tuse uliingia ukifuatiwa na mama yake,na nyuma kabisa alifuatiwa mwanaume aliyekuwa amejaa haswa.Kwa kukuelekeza tu! Ni kwamba mwanaume yule alikuwa ni baunsa.
“Huyu hapa anataka anidhurumu”.Aliongea Tuse huku akimuoneshea yule baunsa kuwa mimi ndiye nataka nimdhurumu. Yule baunsa alinisogelea na kunikata kofi moja la maana hadi nikapepesuka. Sijakaa vizuri,akanisindikiza na konde lingine la uso na kunifanya nidondokee kwenye kochi.
“Kijana hizi mali haziliwi bure kama ulivyodhani,hizi mali zinajitunza kwa njia hiyo. Kama ulidhani kuna vya bure,hapa andika maumivu”.Aliongea baunsa yule huku akiwa kauwekla mguu wake kifuani kwangu.
“Umeiona hii?”.Aliendelea yule baunsa na kutoa bastola moja ndogo aina ya revorva na kunielekezea usoni kama akinionesha.
“Baba muache,usimfanye chochote,tutaongea naye na kama akitusikiliza,tutamalizana”.Aliongea Tuse akimsisitiza yule baunsa aliyekuwa baba yake,asifanye aliyokuwa anataka kuyafanya.
“Haya mwambie unachotaka kumwambia,na kama akikataa basi namfinyanga hapa hapa”.Aliongea baba Tuse huku akitoa mguu wake kifuani na kuniachia ili nisikilize nitakachoambiwa na wanae.
Nilikuwa napumua kwa kasi kama nimetoka mbio ndefu au kufanya kazi nzito. Pale nilipopigwa ngumi palikuwa panapwita balaa kwa maumivu,huku shavu langu la kushoto likiwa limetengeneza alama za vidole vya yule Baba Tuse. Achana na hayo tu!,tayari tumbo la kuhara lilikuwa linakaribia kufanya yake,na endapo angeendelea kunichimba mkwara na kunioneshea ile bastola yake,basi mwenzenu sasa hivi ningesema siku ile nilijiachia haja kubwa.
“Si nilikwambia Prince. Heri tungemalizana wenyewe huku huku,sasa ona yanayokukuta. Mimi sikutetei na wala sina huruma,kama utakataa nachosema,naruhusu baba akufanyie na huyo kaka yako si kitu kwetu,akileta uboya boya wake na yeye anakaushwa tu!”.Aliongea Tuse huku akiwa kasimama mbele yangu na kikanga chake.
“Mwambie unachotaka kumwambia siyo unaanza kumpigisha stori hapo”.Sauti ya Baba Tuse iliamrisha.
“Sikiliza Prince. Umeingia mwilini mwangu na kufanya yako. Hivyo hapa kama kawaida,nataka changu kama nilivyokwambia”.Aliniambia Tuse huku akiwa na uso usiyo na utani.
“Shilingi ngapi unataka?”.Niliuliza huku natetemeka.
“Nimeshakwambia laki moja,sishushi wala sipandishi”.Alijibu Tuse.
“Lakini mbona sikufanya muda mrefu na wewe,na vilevile hata sikutoa goli”.Nilijaribu kujitetea ili nieleweke na wanipunguzie ile hela waliyoniambia.
“Mimi sijui hilo,nachojua umeingia mwilini mwangu tena kwa kondom. Unajua ghalama ya kuingia mwilini mwangu kwa kondom?”.Aliniuliza Tuse.
“Sasa mimi ningejuaje wakati hukuniambia kama unafanya biashara?”.Na mimi nikatupa swali.
“Kumbe alikuwa hajui kama unafanya biashara?”.Baba Tuse aliuliza baada ya kusikia maneno yangu yale.
“Ndiyo mzee.Yeye alikuja humu na kuanza kuchagua CD, mara akaona CD yangu ya ngono,akaanza kuing’ang’ania. Mara tukaanza kugombania ndiyo tukajikuta tayari tumeingia katika kufanya mapenzi. Nilikuwa sijui kuwa mwenzangu anafanya biashara”.Niliongea kwa upole ili japo kidogo nieleweke,na kweli yule mzee alianza kunielewa.
“Sasa kama hukumwambia huyu mjinga kuwa unafanya biashara,ya nini useme anakudhurumu?Huoni kama huo ni ujinga?Si nilishakukataza kujiingiza mwenyewe kufanya mapenzi na kuanza kuwadai watu kwa kisingizio wamekufuck kwa maelewano?Si nilishakukataza hiyo tabia?”Baba Tusea alimuijia juu mwanae ambaye alikuwa kimya wakati simba ananguruma.
“Lakini Baba Tuse,hata hivyo huyu kijana ana makosa,kwa nini afanye mapenzi na mwana wetu bila mawaelewano naye?Kwa nini asingemuuliza kabla hawajaanza mchezo?”.Mama Tuse naye akawa anajaribu kumtetea.
“Si hivyo tu Baba.Mimi nilikuwa tunataka kufanya kama kufurahishana,sema yeye akaanza kuwa na kiburi na maneno ya kashfa na kusema eti naweza kuwa na ugonjwa,hadi akaamua kutumia kondom”.Tuse alijaribu kujitengenezea mazingira mazuri kwa baba yake. Na baba yake aliingiwa na maneno yale na kuanza kunipiga tena.
“Wewe wa kumwambia mwanangu ana magonjwa wewe?Unajua huyu katoka wapi hadi hapa alipo. Haya nieleze ana ugonjwa gani ulioutambua. Nieleze kabla sijakugawanywa maisha yako,kwenda kaburini na mengine jehanamu”.Aliongea kwa hasira Baba Tuse baada ya kunipiga kwa ngumi na mateke mwilini mwangu. Huku nikiwa natetemeka na mwingi wa kilio,nilianza kujitetea.
“Hapana mzee. Mimi sijamwambia kuwa ana magonjwa,ila nilimwambia tutumie kondom kwa sababu hatujuani,wote tumekutana huku huku. Yeye hajui mimi nimetokea wapi na nina magonjwa gani,na wala mimi simjui yeye. Hivyo ni vema kulindana katika hilo,na si hilo tu! Hata mimba zisizotarajiwa nazo twaweza kuzuia kwa mtindo huo,lazima tujali”.Niliongea huku nikijaribu kuonesha hali ya huruma kwenye uso wangu,na maneno yale yaliwaingia vizuri sana wazazi wa Tuse.
“Hivi wewe Tuse una akili kweli?Ni mwanaume gani katika maisha yako anaweza kuwa kama huyu kijana?Anakusihi na kukushauri kwa vitu vya muhimu kama hivi,mwanaume gani kawahi kukufanyia hayo? Mimba ngapi umetoa wewe mtoto?Leo unaushauriwa vizuri,eti unajidai unakuja kwetu na kusema umedhurumiwa. Sasa hapa umemdhurumu huyu kijana?,au yeye ndiye kakudhurumu wewe. Embu nijibu”.Mama Tuse aliongea huku anamwangalia mwanaye.
“Mama huyu si kala kuku,amlipie tu!.Mimi sitaki zengwe na nyie,si mnanijua nikiamua hapa eeh. Nitawafanyia kama juzi,na mtahama na hapa. Mwambieni huyu fala anipe changu,kama hana,tumpe masharti kama ya wengine wa nyuma”.Tuse aliongea kwa kujiamini hadi hata wazazi nao wakanywea.
Sikujua ni kwa nini Tuse alikuwa mbabe vile hadi wazazi wake wakanywea na kuwa kama mkate uliowekwa kwenye chai.
“Una hiyo laki moja kijana?”.Baba Tuse aliniuliza huku akiweka bastola yake kwenye mkanda wa suruali aliyoivaa.
“Mzee mimi sina hiyo laki moja,labda mnipe masharti”.Nilijibu huku nikijifuta damu zilizokuwa zinatoka kwenye paji langu la uso.
“Utaweza au unataka kutufia sisi tu!”Mama Tuse aliingilia ombi langu kabla halijapitishwa.
“Aah,mama muache,si kataka masharti?Ngoja nimpe,na baba utamalizia yale mengine”.Tuse hakuwa nyuma kubishana na wazazi wake.Akaendelea,
“Ipo hivi wewe fala.Inatakiwa kila baada ya siku mbili,uwe unakuja kwetu na kufanya mapenzi na mimi kwa jinsi navyotaka.
Nitakuelekeza jinsi ya kufanya na wewe utafanya hivyo hivyo. Na sipo mimi peke yangu,kaa ukitambua hilo. Akitokea mtu anataka mambo,na mimi nikiridhia,utafanya naye tu!. Ni kila baada ya siku mbili ndani ya mwezi mzima,yaani namaanisha utafanya mapenzi na mimi na watu wangu kwa siku kumi na tano kuanzia leo,hayo ndio malipo ya laki moja yangu”.Aliongea Tuse na kunifanya nitabasamu kimoyo-moyo huku nikiamiami kazi hiyo ni rahisi sana kwangu.
“Na kama ukijaribu kutoroka,nitaifanya familia yako kitu kibaya sana ambacho utajutia maamuzi yako. Si unakaa na kaka yako hapa?Basi yeye ndiye atakuwa malipo ya wewe kutoroka. Umenisikia?”.Aliongea Baba Tuse huku akiniangalia kwa macho makali na ya kuogofya.
“Nimekusikia na nimekuelewa mzee.Ila nina ombi moja”.
“Ombin gani?”.
“Kwenye hayo aliyosema Tuse,naomba yawe yanafanyika kwa dhana,kama haiwezekani,basi niuweni sasa hivi tu!”.Nilitoa ombi langu na kuifanya ile familia ya wajinga na wasio na akili yoyote,kubaki kuangaliana kama majogoo yaliyotoka kupigana halafu wakatoka droo.
“Poa, Hamna tatizo kuhusu hilo. Limepita”.Tuse alipitisha hoja na kuwafanya wazazi wake kuanza kuondoka mle ndani kwangu na kuniacha mimi na Tuse.
“Umeona sasa Prince?Nilikwambia tuyamalize,ukajidai mgumu kama nazi,ona ulivyoumizwa”.Tuse alijidai ananionea huruma,lakini sikujali huruma yake kwa sababu katimiza nia aliyokuwa kaipanga.
“Hayo masharti yako yanaanza kutimizwa lini?”.Nilimuuliza Tuse.
“Kesho ndiyo kazi inaanza rasmi.Ntakufaidije”.Alijibu Tuse huku akijishongo-shongo macho na mwili wake.
“Basi toka ndani kwangu kama kazi inaanza kesho,sikutaki humu”.Nilimwambia kwa hasira na kumfanya acheke kwa kejeri na kuanza kutoka zake nje.
Sikuamini kabisa kama kuna wazazi kama wale duniani. Wanawafanya watoto wao ni biashara na wala hawaomi shida kwa maamuzi wanayoyachukua.
Yule Tuse au Suzy,siyo mtu wa kutamka mbele ya wazazi wake kuwa atafanya ngono na mimi kwa mwezi mzima halafu wazazi wake wanakubali tu!. Na pia maswali kwangu ni lazima yapite,kwa nini imetokea vile,yaani ni kwa nini adhabu yangu iwe ni kufanya ngono na yule binti?.Jibu nilikuja kulipata baadae.
**************
Nilikaa siku ile huku nikiwa na mawazo mengi sana. Nilijitibia maumivu yangu,na yalipopona,niliweza kulala kwa ajili ya kuamka kesho.
Nilipoamka,nilifanya kazi zangu za kila siku,hasa kusafisha nyumba na mazingira yake pamoja na kuosha vyombo vyangu,na baada ya kumaliza nilitulia zangu na kuweka filamu ya Rambo na kuanza kuiangalia hadi mida fulani ambapo nilisikia geti la nyumba nayokaa likianza kugongwa kwa nguvu kidogo. Nilipotoka,nilikutana na sura ya Yesaya mdogo wa Tuse. Aliniambia kaja kuangalia video,na kwa kuwa nilikuwa sina tatizo na yule dogo,nilimuachia aingie ili aangalie.
Baada ya kimya kidogo,niliamua kuanza kumpeleleza yule dogo kuona kama anajua chochote kuhusu familia yake. Na kweli,nilipata chochote kutoka kwake,japo hayakuwa mengi sana.
Aliniambia kuwa kule walipohama,walihama kwa sababu Tuse aliwadhurumu watu halafu akawasingizia wazazi wake ndiyo wamemtuma kufanya vile. Nilipomuuliza dogo,kama anajua ni kazi gani aliyokuwa anaifanya Tuse hadi adhurumu watu,dogo alijibu kuwa hajui.
Aliongeza kwa kusema kuwa,baada ya kuwataja wazazi wake kuwa ndo wamemtuma,wale majamaa walienda hadi polisi na kuwafungulia mashitaka ya dhuruma familia ile. Ilibidi walipe hela fulani ili ile kesi iishe,na walifanikiwa katika hilo.
Pia dogo alisema baba yake anatokaga usiku na kurudi mida ya saa nane mchana. Na mara nyingi akirudi,anakuwa na vitu mbalimbali vizuri na vya kuvutia kama vidani vya madini ya ghalama na siomu za kila aina.
Niliposikia hayo,nilijua moja kwa moja,baba wa Tuse ni jambazi au mwizi.Nilitulia kimya na kuendelea kuangalia filamu niliyoiweka hadi ikaisha,ambapo baada ya kuisha,Yesaya alitoka nje,na aliporudi,aliniambia kuwa dada yake ananiita ndani kwao.Hadi hapo,nikajua tayari mambo yamewiva.Yaani ile adhabu niliyokuwa nayo,nilitakiwa kwenda kuanza kuitumikia. Adhabu yenyewe ni kufanya ngono na binti yule kwa jinsi atakavyo.
Nikatoka zangu ndani na moja kwa moja nikaenda kule nyumbani nilipoitwa na Tuse,ambapo nilikaribishwa kwa mbwembwe nyingi na Tuse aliyekuwa kavaa nguo moja ambayo ilionesha maungo yake vizuri kabisa.
Baada ya mimi kuingia,akaanza kujichekesha-chekesha pale kama kakalia kitu kinachotekenya. Nilimuangalia kwa dharau kisha nikamuomba tufanye jambo lililonileta ili niondoke mle ndani haraka sana.
Ni kweli Tuse alikuwa ana Inye Gwedegwede,lakini kwa alichonifanyia,nilimuona kama vile sijui kitu gani. Kwa kifupi naweza kusema kuwa alinitoka kabisa akilini,yaani alikuwa hanipi mizuka hata kidogo.
Baada ya kumwambia tufanye alichoniitia,alitoa lile vazi lake linaloongaza hadi vitu vya ndani ya mwili wake vinaonekana.Na kisha alikuja pale nilipokuwa nimesimama na kunitoa nguo zangu zote.Baada ya hapo akamshika nanihii wangu,ee,huyo huyo nanihii. Akawa anamvuta kama kamba ya farasi au ngamia,na mimi nikawa namfata hadi tukafika chumbani kwake.
Tulipoingia,akanisukumia kitandani,nikadondokea kifudi-fudi. Kwa mbwembwe nyingi,alinifata pale kitandani na kuanza kumpikicha Prince huku anapaka mikono yake mate. Hakuishia hapo,akamweka mdomoni Prince na kuanza kumnyonya kwa uangalifu na taratibu bila wasi-wasi. Hapo kidogo alinipatia,kwa sababu utamu nilioukosa kwa muda mrefu,sasa ulikuwa laivu unaniingia mwilini.
Nilijiahidi kimoyo-moyo kuwa akinipa nafasi ya mimi kumchezea,nitamfanya kitu ambacho hatakuja kisahau maishani mwake. Kitu hicho niliwahi kuwafanyia wanawake wawili tu! Hapa duniani,nao ni kwa sababu walikuwa wanajifanya manunda sana katika mapenzi. Sasa nilimpangia na huyu Tuse nimfanyie.
Baada ya kufanya mautundu yake kwa muda kidogo,nilihisi kama wazungu wanaanza kutaka kunitoka,na kama ingetokea hivyo,basi ishu niliyoipanga ingesipofanyika ipasavyo.
Nilichoamua ni kumtoa mdomo wake kwenye kipaza sauti changu,na kisha nikamlaza yeye kifudi-fudi. Kwa utaalam wangu wa mapenzi,nikaingiza kidole changu kikubwa na kirefu kwenye pango lake,hapo sikuona kama kahisi utamu wala nini.
Nikaingiza viwili mzee. Kisha nikaanza kutoa na kuingiza kwa kasi ya ajabu hadi nikamuona anaanza kufungua mdomo na kufumba macho kuonesha kuwa utamu unaingia haswaa. Hapo nilizidisha ile kasi zaidi ya mara ya kwanza. Toto likawa kama linataka kupaa,kudadeki zake.
Nilipoona kakorea,nikaacha zoezi na kumuuliza kuhusu dhana. Kwa haraka aliinuka na kwenda kwenye kimkoba chake alichokuwa kakitundika mle ndani,kisha akafungua na kutoa dhana aina ya raha,na kuniletea. Aliponipa akajilaza mkao uleule,kisha akaniomba niendeleze kale kamchezo ka kuchokonoa nyoka shimoni.Nikatabasamu moyoni,kisha nikajisemea,subiri babu kubwa inakuja.
Nikavaa ile dhana na kisha nikaendelea na shughuri niliyokuwa nimeipigia debe hapo mwanzo. Sasa hivi niliongeza kasi zaidi na zaidi na nilipoona kakolea,nilianza kutumia kidole kimoja,lakini kwa kasi ile-ile. Mtoto hoi bin taabani. Sasa hapo ndipo nilikuwa kama napasubiri,niliingiza kidole chote na kisha nikaanza kubofya sehemu ya juu ndani ya pango lake,ambapo mimi najua huko ndipo penye G.Spot.
Sehemu Ya 12
(G.Spot ni sehemu ambayo inaamsha hisia za mwanamke au mwanaume.Sehemu hiyo kwa mwanamke,ipo ndani kwa juu ya uke. Na mara nyingi ukitaka kuipata,ni lazima utumie kidole kikubwa kwani ndicho kiwezachacho kufika huko. Na huwa ina uhali fulani hivi kama sponji. Kwa mwanaume,G.Spoti yake ni ngumu sana kuitambua,ila wanasema ipo chini ya makoro-koro).
Basi na mimi Prince baada ya kuingiza kidole changu mle ndani,nikaanza kuisugua na kuibofya G.Spoti ya toto lile la kinyakyusa. Weweee,ha ha haaaa,acha kabisa harifu. Toto lilikuwa jeusi tii,lakini lilianza kubadilika rangi na kuwa sijui rangi ile.
Lenyewe likaanza kutoa makelele. Na mimi sikuacha hata kidogo,nikazidi kubonya na kusugua kama vocha aina kumbe ni G.Spoti
Nilianza kuhisi ushindi taratibu kwani toto lilikuwa hoi taabani huku likinivuta kwa ajili ya kutaka kulianzisha gemu. Lakini nilikuwa mgumu haswa,nilichokuwa nakitaka ni kuona kalainika kabisa ndiyo nimpe mambo ambayo hawezi kuyasahau na atajuta kwa nini alinipa adhabu kama ile.
Nilianza tena kuingiza na kutoa kidole changu kwa kasi,jambo lililofanya sasa Tuse kuanza kujipinda pinda na kujigeuza geuza huku bado dole la kati likiendeleza shughuli pevu.Ilifikia muda,alikuwa hajiwezi kabisa,yaani alikuwa tayari kwa mchezo,lakini na mimi sikutaka kuingia hadi nihakikishe jambo langu limetimia.
Baada ya mwendo mrefu,sasa nikaona Tuse yupo tayari kumwaga ile kitu yake. Na mimi hapo-hapo,nikazidisha kasi kidogo ya kidole changu,na baadae nilikitoa haraka kile kidole na kuingiza kipaza sauti changu kwa kasi ile-ile. Nilipiga mipigo kama sita hivi ya haraka,halafu nikamchomoa Prince kwa nguvu na kwa kasi pia.
Ha ha haaa,hapo nilimpatia hasaa. Alitoa uyowe mmoja mkubwa sana,ule mama wee.Kilichofata hapo ni yeye kuanza kuchafua mashuka yake kwa kimiminika kilichokuwa kinatoka kwa wingi kama maporomoko ya Victoria.
Kimiminika kile kilipokata,ndiyo nilisikia akiaanza kuhema. Kwani muda wote wakati anatoa kile kimiminika,alikuwa ni kama kakabwa na jinamizi.Niliangalia hali ya mashuka yake,na sehemu mbalimbali za kile chumba,kisha nikatabasamu kwa kuweza kuumaliza mchezo bila kashi-kashi.
“Tuendelee”.Nilimuuliza Tuse baada ya kumuona karudi katika hali yake.
“Hapana Prince,unataka uniue?”.Alinijibu huku amerembua macho yake.
“Mimi mbona sijaridhika?”.Nilimuuliza swali kwa utani tu!.
“Mi sitaki tena,we nenda zako. Unajua nimetumia nguvu kiasi gani kumwaga hiyo?.Unaweza kufa kama si mzoefu,we nenda tu!”.Niliendelea kutabasamu kimoyo-moyo kwa ushindi ule. Na hapo hapo,nilinyanyuka bila hata kuvua dhana na kutoka nje ambapo nilipita sebuleni kwao na kuvaa nguo zangu,kisha ile dhana niliitoa na kwenda kuitupa kwenye jalala kwa ajili ya usalama wa afya za watu wanaozunguka eneo lile.
***********
Baada ya kitendo kile,sikumsikia tena Tuse akinitaja-taja wala kuniita,hata pale siku mbili zilipopita. Na uhakika nilimpa dozi ya nguvu hadi akawa hana hamu tena ya kufanya kale kamchezo katamu ila kenye kunyong’onyeza baada ya kukamaliza.
Ikapita hadi siku ya tano,ikawa kimya kwa Tuse. Hadi kaka yangu akarudi,bado alikuwa kimya tu!. Kwangu ilikuwa furaha kwani nilikuwa simpendi hata kidogo,alikuwa analazimisha mapenzi tu.
Baada ya kaka kuja. Tulienda madukani na kununua vyombo vingine,na tena safari hii,tulinunua vikali zaidi ya vya mwanzo. Kama mziki,basi ulikuwa ni mziki hasaa. Ukifunguliwa ni kero kwa pale nyumbani na mtaa nzima. Nyumba ikarudi kama zamani.Na kwa kuwa kaka naye alikuwa ni mtu wa mziki,basi ilikuwa ni kelele mwanzo mwisho.
************
Siku zikakata na kaka akaondoka tena,safari hii alisema atakaa huko mwezi mzima,hiyo ni kutokana na kazi aliyopewa. Siku hiyo hiyo alipoondoka,Tuse akavamia nyumbani kwangu na kuanza kuangalia vifaa tulivyonunua. Sikupenda sana ujio ule,kwa sababu ya kuhisi kuwa atamwambia baba yake,ambaye mimi nilimuona kama jambazi.
Baada ya kuzama mle ndani,akaanza kusifia-sifia bidhaa zetu mpya huku akiwa kavaa makhanga yake kama kawaida. Nilikuwa kimya tu!,kwani ningemuongelesha au kumfanya kitu chochote,kungezuka kesi nyingine,hasa ya kunifanyisha ngono.
“Mbona huongei?Au hujapenda sifa zangu”.Aliongea Tuse alipoona sina hata mpango wa kujibu maongezi yake.
“Mimi nakuelewa na nimekusikia vizuri tu!. Nataka umalize ili nikushukuru”.Nilijitetea.
“Ndiyo hivyo bwana. TV inchi thelethini na moja,deki ya maana kabisa hii kutoka Marekani. Hapo naona kuna mziki mnene wa Sony,yaani daah!Mmejitahidi sana”.Alizidi kusifia mwanamke yule ambaye kwangu nilikuwa namuona kama shetani tu!.
“Asante Suzy. Tumegharamikia sana hapo. Ni kama laki saba hivi”.
“Mh!Kweli gharama. Kwa hiyo na laki moja yangu kakuachia?”Tuse aliingiza mada nyingine.
“Kwani si tulishafanya mara moja? Ina maana bado imesimama pale-pale laki moja?”.
“Imebaki elfu tisini,na hiyo ni huruma yangu tu!Ilitakiwa ibaki elfu tisini na tano”.Tuse alinijibu.
“Hajaniachia hela nyingi,ipo kama elfu ishirini. Labda nikupe hiyo halafu siku zilizobaki tutamalizana kibingwa”.Nilimwambia kistaarabu zaidi.
“Hapo umenena P. Embu nipe kwanza ili leo tukale kiepe”.Aliongea tena Tuse na kunifanya ninyanyuke pale kochini na kwenda chumbani ambapo nilitoka na elfu ishirini.Lakini kabla sijampa,nilimuuliza anakata ya siku ngapi kwa kuwa hadi muda ule,zilibaki siku kumi na nne.
“Wewe sikuwezi,unaweza kunikosesha hela. Unajua tangu siku ile sijafanya tena. Yaani sijisikii kabisa. Sasa kwa mtindo huo,utafanya nisiende kutafuta hela”.Aliongea Tuse lakini bila kunijibu swali langu.
“Kwa hiyo umenisamehe kosa au?”.Nilimuuliza.
“Hapana. Nashusha siku,zinabaki siku tano,lakini hizo tano,tatu kati yake,sitaki kukuelezea”.Tuse aliongea huku akianza kubadilika na kuweka msisitizo kwa akisemacho.
“Mbona umeniacha kwenye koma?”.Nilimuuliza.
“Kwani kaka yako anarudi lini?”.Na yeye akauliza swali.
“Baada ya mwezi mmoja”.
“Basi zikibaki wiki mbili kabla ya kaka yako kuja,ndio utaanza kumalizia adhabu yako. Sasa hivi,wewe jipange”.Aliongea Tuse na kuchukua zile hela mkononi mwangu na kuondoka mle ndani huku akiniacha na wingi wa viulizo.
*************
Niliendelea kuburudika na maisha yangu huku mawazo ya Tuse,kiasi fulani yalikuwa yameanza kunitoka. Nikarudi katika hali yangu ya zamani ambayo nilikuwa nayo,na sasa niliweza hata kula na kulala kwa raha kwani sikubugudhiwa.
Hatimaye zikabaki zile wiki mbili kabla ya kaka yangu kurudi. Siku hiyo nilikuwa naangalia filamu kama kawaida. Mawazo yote yakiwa yameelekea kwenye filamu ile,mara nilisikia mlango unagongwa. Nilipotoka,nilikutana na mdogo wake Tuse yule mdogo kabisa,wakati huo yule wa kiume alikuwa karudi shuleni.
“Dada anakuita”.Aliniambia mtoto yule,na mimi nikarudi sebuleni na kuzima vifaa vyangu na kwenda ndaani kwao.
Niliingia sebuleni lakini sikuona mtu hadi pale niliposikia sauti ya Tuse ikinitaka niingie chumbani kwake. Ile kuingia tu!,wala sikutegemea kama ningekutana na kitu kile,na wala sikuwahi kufikiria.
Alikuwa ni Tuse na mama yake na wote walikuwa kama walivyozaliwa. Kurudi nyuma nilishindwa,kwenda mbele ikawa kazi.
Taratibu mama Tuse akanyanyuka pale kitandani na kuanza kunifuata pale nilipokuwa nimeganda kama mnara wa barafu ule uliogongwa na meli ya Titanic.
“P. Leo zamu yangu maana nasikia ulimkata Tuse kiu chake chote cha kufanya ngono. Na mimi nataka maana nahisi nina pepo la ngono, hakuna mwanaume aliyewahi kunifanya nikajihisi hilo pepo limetoka. Ila baada ya Tuse kunihadithia kitu kilichotokea,nikahisi wewe ndiye hasa utakayelifanya ili pepo litulie japo kwa wiki”.Alianza mama yule kuongea huku macho na sauti yake vikiwa vimelegea kama kasikia habari nzuri kutoka kwa mumewe.
“Sasa mama,wewe si una mume?.Si mume tu! Huyu si ni mtoto wako?Mbona huoni aibu? Yaani unajianika ukiwa uchi na mtoto wako,nini maana yake? Kha! Nyie ni watu gani aisee,hata kama ni biashara,hii yenu ni too much,loh!”. Niliongea kwa hamaki huku bado nikiwa nimeganda pale-pale mlangoni,na mama Tuse akiwa mbele yangu”.
“Jambo usilolijua,ni kama usiku wa giza Prince. Nilikuwa sikuhitaji hata kidogo katika mapenzi,ila nilichoambiwa na Tuse,kimenifanya niwe muhitaji wa penzi lako”.Mama yule aliendelea kuniongelesha kwa sauti yake ya puani,lakini na mimi bado nikawa naendelea kupambana naye kwa maswali.
“Wewe una mume au hauna?”.Nilimuuliza.
“Huo ndio usiku wa giza nao-uzungumzia”.Akanijibu kimafumbo.
“Nitoe sasa,nipeleke mchana”.Mama Tuse alimwangalia Tuse aliyekuwa kitandani,na Tuse naye akamuoneshea ishara yule mama kuwa aendelee kuongea na mimi,yaani aniambie ukweli ambao yeye anauita giza.
“Nakwambia kwa sababu nahitaji huduma yako,kama si hivyo,ungeendelea na mambo yako huku ukiwa una mawazo hayo hayo kuhusu mimi na hii familia. Ila kabla sijaanza kukwambia chochote,niahidi hii kuwa siri”.
“Nakuahidi itakuwa siri”.
“Na niahidi kuwa utanipa nachohitaji baada ya kuujua ukweli”.
“Kama nikiridhika,nitafanya ila si kama kwa Tuse”.
“Si kama kwa Tuse kivipi?”.
“Itabidi Tuse anisaidie kufanya hivyo ili hata nikiondoka,msinisahau na mnienzi”.Baada ya maneno hayo,Mama Tuse aliinama chini kama anafikiria kitu na kisha akanyanyua uso wake,akanishika mkono na kunivuta hadi pale kwenye kitanda alichokuwepo Tuse.Akanikalisha na yeye akakaa na kuanza kuongea na mimi.
“Sikiliza Prince. Hakuna anayejua maisha ya mwenzake hadi pale jambo litakapomkuta. Haya maisha yaonage hivi-hivi kuliko yakukute wewe. Maisha tunayoishi sisi,siyo maisha ya kuishi binadam hata kidogo,nasema tena,si ya kuishi binadamu hata kidogo. Lakini kwa kuwa tumeumbiwa maisha haya,basi hatuna budi kushukuru hata kwa hichi tunachoishi.
Wewe ni kijana mzuri na muelewa sana.Tangu ile siku baba wa huyu alivyokupiga,roho yangu ilijaa huruma sana. Hakupasa kukufanyia vile kwani umebarikiwa sana we kijana. Unajua jinsi ya kumlegeza mtu kwa maneno na kumfanya ajisikie mwenye hekima. Kama si tabia za ajabu tulizonazo sisi,ningekuomba umuone Tuse,lakini haiwezekani,sisi ni kama Mashetani wadogo.
Najisikia aibu sana kukaa na wewe hivi nikiwa uchi,lakini nitafanya nini na hii ndiyo kazi yangu?Nitafanya nini na wakati nahitaji mambo yatakayonifanya nipumzike kulanda na wanaume kila kukicha.Nitafanya nini na wakati watoto wanahitaji kwenda shule na kula?
Prince,usinifikirie vibaya. Na usinichukulie mimi kama ndugu yako yoyote wa kike,bali niangalie mimi kama wanawake wengine wa mtaani”.Mama Tuse hadi anamaliza kuongea hayo,alikuwa tayari kishaiva uso vya kutosha.Alikuwa mwekundu sana,na ule mkorogo anaoutumia,basi ndiyo mama wee,unaweza kusema ni andazi.
“Lakini Mama Tuse,wewe si una mume?Licha ya hayo,mimi nishatembea na mtoto wako,huoni aibu? Huoni aibu mimi kufanya mapenzi na mtoto wako na wewe unata……”.Sikumalizia sentensi niliyokusudia,Mama Tuse akawa kadakia maongezi yale niliyokuwa nayaongea.
”Tuse si mwanangu,na yule si mume wangu. Ngoja nikutoe gizani sasa,lakini ndio iwe siri yako. Tumeamua kukwambia haya yote karibu kabisa na kaka yako kuja ili akija wewe uondoke uende popote,kwa sababu hatuwezi kuvumilia kuendelea kumuangalia mtu anayejua siri zetu.
Hapo nyuma,yule aliyegundua siri zetu,tulimfutilia mbali,ila wewe tunakuomba uondoke baada ya kujua haya”.Mama yule aliongea kwa uchungu sana hadi nikajihisi kitu fulani kama huruma kikinikaba kwenye koo. Akaendelea kueleza.
“Baada ya maisha ya Mbeya kuwa magumu kwangu,niliamua kujiingiza kwenye biashara ya kuuza mwili,huko nilikutana na marika mbali-mbali ya watu wenye kazi kama mimi niliyokusudia kwenda kuianza.
Nilijitahidi sana ili hawa watoto wawili ambao ni Yesaya na Tumpare wapate chakula hasa huyu Tumpare aliyekuwa na miezi kama sita hivi.
Tumpare na Yesaya.Hawa ni watoto wa dada yangu aliyefariki wakati anajifungua huyu Tumpare. Alipoteza damu nyingi sana,na kwa kuwa tulikuwa tunaishi maisha ya kubangaiza,tulikosa hata hela ya kununulia damu hiyo,hivyo dada yangu aliaga dunia kihivyo. Nikaachwa na hawa watoto.
Nikawalea hivyo-hivyo huku maisha yangu yakiwa ya tabu sana tena sana. Huyu Tumpare muone hivi-hivi,kapita kwenye mabonde ambayo wewe hutokuja kuyapitia. Akiwa na mwezi mmoja tu! Alishazijua shida kama mtu mzima. Maji yasiyochemshwa huyu mtoto kabwia kama hana akili nzuri,hiyo ni sababu mimi sikuwa na maziwa wala hela ya kuyanunua.
Huyu Yesaya,na miaka yake minne,nilikuwa namtuma aende kutungua maembe au maparachichi ili tuje kula kama chakula cha mchana. Hakuna ajuaye sababu za sisi kufanya miili yetu maduka,bali yule muelewa pekee anaweza akakuelewa nini usemacho”.Mama Tuse japo aliongea kwa uchungu sana,lakini kamwe hakujaribu kutoa chozi.
“Prince. Mimi baada ya kuona watoto hawa watanishinda,ndio nikaamua kuingia kwenye biashara hii ya kuuza mwili,na baada ya kuingia tu!. Ni kama soko lilikuwa linanisubiri,haikuwa taabu kwangu kulala na wanaume wawili au watatu kwa siku moja. Na saa nyingine nililala na wanaume watatu kwa wakati mmoja.
Nilichokumbuka cha msingi,ni kwenda kutoa kizazi changu ili nisipate mimba zisizotarajika na wakati bado na watoto wengine,na ndiyo maana siku ile uliposema unajilinda kwa dhana ili mzuie mimba,nilikuona mtu mmoja makini sana”.Bado Mama yule aliendelea kunipa hadithi maisha yake.
“Kazi ilinilipa sana tu!Watoto sasa wakawa wanakula na kulala mahala panapoeleweka. Mavazi pia yakawa mazuri kwao.
Mwaka mmoja ukapita na maisha kwangu yakawa mazuri tu!. Katika mwaka huo,ndio nikakutana na huyu Tuse ambaye yeye alipenda kujiita Suzy,lakini mimi nilimuita Tuse ili aendane na hali ya kule Mbeya. Huyu na yeye ana historia yake binafsi ya kwa nini aliingia kwenye shughuli hii,sintomsemea moyo.
Camp ikaongezeka baada ya ujio wa huyu,na hela zikawa zinaingia haswa. Hapo ndipo tulipata wazo la kuamia Dar kwa sababu kule kuna soko zuri kuliko Mbeya.
Tulipofika Dar,tukasaka nyumba moja kubwa,na kuanza maisha yetu kwa kazi ile-ile. Hapo sasa,ndiyo kama uchangudoa ukafika mahala pake.Kwani Tumpare akawa kidogo anaanza kutembea na kuongea,huyu Yesaya ikabidi tumpeleke shule za bweni maana tayari alishaanza kuelewa baya na zuri kwa umri wake wa miaka mitano.
Kazi ilipokuwa inazidi kunoga,ndipo tukakutana na huyu baba. Najua huwezi kuamini kwa muonekano wake,waweza kuhisi ni jambazi au mtu fulani mwizi. Lakini naye ana historia yake binafsi ya kuwa vile”.Akanyamaza kidogo na kumuangalia tena Tuse ambaye alikuwa kimya wakati wote Mama yule anasimulia.
Baada ya kumuangalia sana Tuse. Nikaona Tuse akinyanyua mgongo wake pale alipokuwa kakaa na kuanza kuongea.
“Prince tunakwambia haya kwa sababu unaonekana huna mambo ya ajabu wala nini. Na kwa kuwa una-idea ya muziki na sanaa nyingine,tunaomba haya uyafikishe katika jamii. Baada ya mama kukwambia historia yake,na mimi nitakutafuta nikupe historia yangu na ya baba pia. Tunataka ujumbe ufike kwa kila mtu,ila tunaomba uondoke baada ya kujua haya. Nenda huko mbali kabisa,ndiyo katuelezee tulichokifanya. Hatukupenda hata kidogo,ni maisha tu! Mama endelea”.Tuse aliongea na kumpa mama yake ruhusa ya kuendeleza gurudumu la hadithi aliyoianza.
“Huyu baba ni shoga,Prince”.Mama Tuse aliongea na kuangalia chini kwa aibu kubwa,na wakati huo mimi nilibaki kinywa wazi nisijue ni nini niulize au kujibu.
“Mwili wote wote ule,maguvu yote yale na mikwara kibao,kumbe si ridhiki? Daah! Kweli dunia ni tambara bovu”.Nilijiwazia kichwani na kushindwa kuvumilia kabisa kwa nilichokisikia.
“Sasa kwa nini kawa vile?”.Niliwauliza.
“Hiyo ni historia nyingine ndefu sana aliyoipitia baba. Wala usijali,kabla ya kuondoka utakuwa umeipata”.Alijibu Tuse na kuniacha bila swali.
“Ndiyo hivyo Prince. Na yeye nilikutana naye katika harakati hizi hizi za kutafuta maisha. Tena yeye naweza kusema ana bahati japo afanyacho si chema. Watu wake ni watu wakubwa na wenye fedha sana. Hawa wazungu na watu wa nchi za nje,ndiyo wanaomweka mjini”.Mama Tuse aliongea huku bado akiwa ameangalia chini.
“Kitu pekee ambacho nakifanya katika maisha yangu,ni kuwawekea watoto wa dada yangu amana ya fedha ambazo zitawasomesha hadi watakaporidhika. Na najua watasoma sana baada ya kujua mama yao mdogo naangaika kwa kujiuza ili wao wasome. Sina kingine cha kuwapa zaidi ya elimu,na nina amini,ipo siku watasema asante mama kwa msaada wako hata kama nikiwa kaburini.
Hata baada ya kufanikiwa kwao,labda mmoja akawa Rais,basi mimi nitamuita Rais aliyesoma kwa fedha za kujiuza mwili. Au shujaa wa changudoa. Nawapenda sana wanangu”.Alimaliza mama yule kwa kachozi kadogo kaliko mtiririka bila yeye kujijua.
Nilichukua shuka la pembeni yake,nikamfuta lile chozi na bila kutegemea,nilijikuta namkumbatia yule mama akiwa vilevile bila nguo na mara taratibu nilianza kumchezea chezea. Hapo Tuse aliamua kutoka zake nje na kutuacha watu wazima tukijiandaa na mchezo.
Niliamua kwa roho moja kufanya mapenzi na mama yule ambaye hakuwa mama kabisa,yaani hata yule shangazi yake Stela alikuwa mkubwa sana. Sasa kama niliweza kufanya na mama kubwa kama Shangazi wa Stela,ya nini nimshindwe huyu ambaye alikuwa si mkubwa japo alinizidi.
Nilimpa mambo mengi sana ambayo sidhani kama kuna mwanaume mwingine aliweza kuyafanya hapo kabla. Yale niliyomfanyia Tuse na Shangazi yake Stela kule Morogoro hadi akazimia,basi niliyachanganya kwa pamoja na kumfanya Mama Tuse yule kuwa hoi taabani huku akiniahidi kumwambia Tuse anisamehe kwa adhabu iliyokuwa inanikabiri.
Hakuacha kuniambia kuwa ameenjoy sana mambo niliyomfanyia,na alisema atanikumbuka sana,kwani ni mimi pekee ndiye niliweza kukata kiu yake ya ngono.
Kesho yake mama yule ambaye alijitambulisha kwangu kwa jina la Khadija,aliniita ndani kwao na moja kwa moja niliitikia wito ule kwa kwenda,ambapo kama kawaida nilimkuta na Tuse,lakini siku ile walikuwa wapo kistaarabu zaidi.
“Prince. Nimekuita hapa kwa ajili ya kulijadiri lile suala letu la kutolewa ile adhabu ya kufanya ngono ambayo ilikuwa kama tunakulazimisha kufanya vile,hukupenda nadhani. Na kama ungependa basi ungekuwa una furahia sana sisi tukikuita au wewe mwenyewe ungekuwa unamuita Tuse ndani kwako na kufanya naye ngono. Hivyo baada ya kugundua kuwa hupendi,tumeona bora tukuite na kukupa taarifa za kuisitisha adhabu ile,lakini tukiwa na masharti machache sana kwako”.Mama Khadija au Mama Tuse alianza kwa kusema hayo.
“Nakusiliza dada”.Nilimpa uhuru kwa kumuita dada,jIna ambalo alitabasamu kidogo baada ya kulisikia. Akajivuta kwa mbele kutoka kwenye lile kochi alilokuwa amekalia,na kisha akaendelea na maongezi yake.
“Tunachoomba. Baada ya kuitoa hii adhabu kwako,ni wewe kufanya haraka iwezekanavyo kuondoka hapa,kwani yule baba akijua kuwa tumekwambia siri zetu,ni lazima atakutafuta na kukufanyia kitu kibaya. Hivyo nakuomba sana Prince,ondoka na nenda kokote lakini si kukaa hapa. Na pia,siri zile tulizokwambia jana,usijaribu kumwambia hata kaka yako. Wewe ukiondoka,sisi tutamtetea kaka yako,na huyu baba anatuamini sana,hawezi kumfanya chochote. Ni hayo tu jembe langu”.Mama Tuse alimaliza kwa kijisifa cha kijinga,hadi akanifanya nitabasamu na wakati si tabia yangu hasa napokuwa nao.
“Sawa dada,nimekusikia na naufanyia kazi ushauri wako”.Nilimjibu kifupi na kumsikiliza atasema nini.
“Sawa,basi wewe kaendelee na shughuli zako halafu baadae nadhani huyu Tuse atakuja nae kusema na wewe,uongo mama?”.
“Ndiyo Prince. Nitakuja tuagane kwa kukupa historia ya maisha yetu”.Tuse alimjibu Mama yake huku ujumbe ukiwa unakuja kwangu.
“Hamna tatizo. Nakukaribisha bibie”.Niliwajibu na kisha nikanyanyuka na kurudi kwangu kuendelea na mambo yanayonihusu.
Mida ya jioni,Tuse alikuwa sebuleni kwangu huku akiwa na sura ya majonzi sana usoni kwake. Na mimi pia nilikuwa vivyo hivyo kutokana na hadithi aliyokuwa amenisimulia. Ilikuwa imeshika hisia zangu sana,na niliahidi kufanya jambo ili aliyonihadithia Tuse,yafike kwa kila mtu.
(Aliyonihadithia Tuse,nitayafanya kama hadithi nyingine. Bado nafikiria iweje. Kuwa na mimi).
“Basi ndiyo hivyo P. Si kila changudoa,kapenda kuwa changudoa,bali kuna watu au vitu vimesababisha sisi kuwa hivi. Nakuomba P,usiwe na kinyongo na mimi,na nakuomba sana tena sana,kaelimishe haya niliyokwambia,usiyafutike moyoni mwako”.Tuse aliongea kwa uchungu na baada ya hapo alihisi kama machozi yanataka kumtoka,kwa haraka sana,alitoka nje na hakurudi tena.
************
Nilikaa wiki nzima pale nyumbani huku nikipanga mkakati wa kumdanganya kaka ili niondoke pale nyumbani kwake.
Baada ya kuwaza na kuwazua,nilipata jibu moja ambalo nadhani lingemfanya kaka kutofikiria vibaya mimi kuondoka pale kwake. Nilimsubiri kaka kwa zile siku tano zilizobakia,na baadae alikuja na wala sikuwa na wasiwasi,moja kwa moja nikamueleza nia na madhumuni yangu.
“Bro unajua nimekaa sana kwako,halafu nimepakumbuka sana nyumbani. Si wajua nyumbani ni nyumbani hata kama mnakunywa chai kwa maharage kila asubuhi?”.Nilianza kuongea na kaka kiutani kama simaanishi nachosema.
“Aaa dogo,mara hii unataka kuondoka?Tulia kwanza hata miezi miwili mingine ili nikipata kiasi fulani,nikupe umpelekee na mzee,si wajua sijamtumia mshiko siku nyingi”.Kaka aliniomba lakini na mimi nilikuwa nimejiandaa vyema katika mabembelezo yangu.
“Basi nitaenda kwa Bro George kule Arusha ili ukishapata huo mshiko nirudi nyumbani moja kwa moja kwa maana nikitoka hapa bila kwenda kwake,atamind sana”.
“Hilo nalo wazo zuri,kwa kuwa na yeye alikuwa anakuhitaji uende kwake,ni vema ukamcheki halafu mimi nitakutunia hela hiyo ya mzee,ndiyo na wewe utaondoka,sawa?”.Bro aliingia line mwenyewe bila kujua nia na madhumuni yangu ya kuondoka pale.
Akapanga siku ya kuondoka ambayo ilikuwa ni siku mbili zijazo. Na hata alipompigia kaka yangu wa Arusha,hakuwa na kinyongo zaidi ya kufurahi ujio wangu kwani pale kwake anasema kulikuwa papweke sana.
Nilifurahi sana kuhusu hilo,kwani nilijua sasa ile kadhaa inaeleka kwenda kaburini. Nilimshukuru sana kaka kwa msaada na uvumilivu wake pale mimi nilipoibiwa,na sikuacha kumpa moyo kwa kumwambia MUNGU ndiye muweza na atamlipa kwa yote aliyonifanyia.
Kesho yake,nilikutana na ile familia ya akina Tuse,nikawaaga kwa kuwaambia kuwa naondoka kesho yake.Nao wakiwa wanamasikitiko kiasi fulani,waliniaga huku wakiniachia mawasiliano yao ambayo hadi wakati huu napowahadithia mkasa huu,niliwahi kuongea nao kama mara nne tu! Na ni miaka mingi sana imepita tangu niachane nao.Kilichowapata,ni mkasa mwingine wa kusisimua.
Hatimaye siku hazigandi bali zinaenda kama moshi utakao kwenye kuni na kubebwa na upepo uvumao wakati wa mvua. Siku hiyo kaka alinisindikiza hadi Ubungo na kunikatia tikiti ya kwenda Arusha kwa basi la Shabiby.
Kwa kuwa basi lenyewe lilikuwa ni luxury,mnamo mida ya saa tano likawa linapiga honi kuashiria kuwa linaanza kuiacha ardhi nzuri iliyopo pale Ubungo. Naam,sasa safari yangu ya Arusha,ikawa imeshika hatamu.
*************
Mida ya saa mbili za usiku,mimi na abiria wenzangu,tukawa tumekanyaga ardhi ya jiji la Arusha ambapo kwangu mimi,ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kufika.
Nilitabasamu kwa furaha pale nilipochungulia dirishani na kumuona kaka yangu akiwa anatazama kila abiria anayeshuka katika basi lile. Hapo hapo na mimi nikaanza kuzihesabu hatua taratibu na kuelekea zilipo ngazi za basi lile. Nikazikanyaga kwa uangalifu huku nashuka chini,na kitendo cha furaha kikatokea kwangu.Kitendo hicho kilikuwa furaha sana wakati kinatokea muda ule,ila kama ningelijua,wala nisingelisema na kufurahia kuwa kile ni kitendo cha furaha.
Kitendo chenyewe kilikuwa ni kuikanyaga ardhi ya Arusha. Jiji ambalo linasifika kwa kuwa na vitendo vingi vya kihalifu kulikoni miji yote ya nchi hii pendwa ya Tanzania. Jiji lile pia,lilisifika kwa kuwa na bei za juu katika vyakula kuliko kitu chochote.
Jiji lenye mahoteli na kumbi kubwa na za kuvutia. Na ni jiji lenye madini hadimu ya Tanzanite pamoja na vivutio vya kitalii. Welcome to Arusha,ndivyo kibao cha kile kituo cha mabasi kilivyosomeka.
Kaka aliponiona,alitabasamu na mara moja alikuja pale nilipokuwa nimesimama kabla sijaanza hatua zangu kumuelekea. Alipofika alinikumbatia kwa furaha na kunisalimia kwa amani tele. Na mimi nikarudisha fadhira hizo sawa na alivyofanya yeye. Akachukua begi langu la nguo,kisha akaanza safari ya kutoka katika eneo lile la kituo cha mabasi yatokayo mikoani.
Kaka yangu huyu,yeye alikuwa ni mchuhuzi wa madini mbalimbali yanayopatikana Arusha. Kwa kazi hiyo,ilimfanya awe bize sana katika kutafuta madini na wateja wa kununua madini anayoyapata kutoka kwa wachimbaji wa pale Arusha.
Hivyo ilikuwa ni nadra sana kukaa nyumbani hata kwa siku mbili. Kwa kifupi alikuwa yupo bize kila muda. Kwa ujio wangu,ilikuwa ni ahueni kwake,kwani sasa angekuwa ana uhuru wa kufanya kazi zake hata kwa miezi kadhaa bila kuonekana pale nyumbani.
“Dogo karibu sana skani. Hapa ndipo kwangu”.Kaka alinikaribisha kwake baada ya safari iliyochukua kama dakika thelathini kutoka pale kituo cha mabasi.
“Bonge la hause mzee,upo peke yako au na watu?”.Nilimuuliza baada ya kushuhudia ule ukubwa wa nyumba kwa kule nje.
“Aaah,nipo na baba mwenye nyumba. Yeye anakaa kule na familia yake”.Kaka akanijibu.
“Na nyie ma-bro kwa kupanga tu!Kha! Si mjenge sasa?”.Niliongea huku nikionesha nakerekwa na wao kupanga panga.
“Mi nyumba yangu ipo Fire pale,nimeinunua,sema bado naikarabati. Nadhani baada ya miezi mitatu,itakuwa tayari kwa mimi kuingia”.Kaka alinijibu na kunifanya niridhike kwa hatua yake aliyofikia kwenye kujitafutia makazi yake binafsi.
Kaka alikuwa kajipanga kweli kweli ndani kwake. Alikuwa anakila kitu ambacho kijana wa kileo alitamani kuwa nacho. Kwa kifupi alimzidi yule kaka yangu wa Dar hasa kwa thamani za ndani.
Sehemu Ya 13
Alinionesha lilipo bafu,na mimi nikanyanyuka na kwenda bafuni humo na kuoga.Kisha nikajipiga mambo katika mavazi na manukato,na baadae nikaelekea sebuleni ambapo nilikuta chakula kimeandaliwa.
“Dogo piga msosi huo,mimi tayari”.Kaka alinikaribisha,nami nikavuta kiti kwa nyuma na kuanza kujipakulia chakula kile.
“Sasa Bro,huu msosi nani kakupikia?Mbona sioni mtu hapa wa kupika menyu ya ukweli kama hii”.Nilidadisi kaka kwa swali.
“Huyo shemeji yako,sema huwa ashindi hapa. Nilimwambia leo unakuja ndo maana akaja kunisaidia kupika”.Kaka naye hakuwa na kificho,aliniji na mimi nikakosa swali wala kauli ya kuendelea kudadisi.
Baada ya kumaliza chakula na kujiona kuwa nimeridhjka,nilimuaga kwa kumwambia kuwa naenda kulala. Naye kaka akaniruhusu,basi maisha ndiyo yakawa yameanza hivyo pale Arusha.
********
Kesho yake asubuhi na mapema,kaka aliniamsha kwa kuniambia kuwa anaenda kazini hivyo aliona ni vyema kwenda kunitambulisha kwa baba mwenye nyumba yake na familia yake kwa ujumla.
Nikanawa uso wangu haraka,na kisha nilimfuata kaka mgongoni hadi kwenye mlango ambao kaka aliugonga na baadae ukafunguliwa na mzee mmoja ambaye hakuwa mzee kiasi kwamba alihitaji fimbo,bali uzee wake,ni kwa sababu alikuwa kaenda umri mkubwa kushinda sisi.
“Shikamoo mzee”.Kaka aliamwamkia mzee yule na mimi nikafanya vivyo hivyo. Mzee akaitikia na kutega sikio kaitiwa nini asubuhi ile.
“Mzee huyu ni mdogo wangu,kaja jana. Naomba umtambue,anaitwa Prince. Leo atakuwa hapa na nyie”.Kaka alinitambulisha kwa mzee yule kwa haraka,kisha akasubiri majibu kutoka kwenye mdomo wa mzee yule.
“Ahaa.Prince. Karibu bwana. Mimi naitwa Mchungaji Donyo,na nina familia nyingine utaiona baadae,sasa hivi,rudi kapumzike kwanza maana safari ina uchovu wake”.Mzee yule alijitambulisha na kutupa ruhusa ya sisi kwenda kupumzika huku kaka yeye akiwa kama kapewa mbawa za kwenda kazini kwake.
Mida ya saa sita,kijana mie mpole na mtulivu lakini muuaji wa chinichini,nilikuwa naswaki katika bafu la nyumba yetu lililo mle mle ndani.
Baada ya kumaliza kuswaki,nilifungua jokofu na kukutana na maziwa fresh yakiwa kwenye box. Nikagida kwa ajili ya kuifanya afya yangu izidi kuwa imara,wakati huo nilikuwa sina tena wazo na wakina Tuse ambao niliwaacha na maisha yao ,na mimi nikaendelea na yangu. Nilichokumbuka ni kuwatumia meseji tu! Kwa kuwaambia kuwa nimefika salama Arusha.
Kaka yangu kama kawaida nilim-bipu,na alipopiga nikampa hali halisi ya safari yangu na sikuacha kumshukuru kwa ukarimu alionionesha wakati nipo kwake.Hayo ndiyo niliyoyafanya kabla sijatoka nje kuangalia mazingira.
Nilipotoka nje sasa. Aisee Arusha kuna baridi nyie,dah! Yaani nilijikuta natoka mara moja na kuingia ndani haraka. Nilivyofanya vile,nilisikia vicheko vya kike nyuma yangu. Niliguna na kujiuliza ni wakina nani hao walionicheka?
Kwa kuwa P nilikuwa si mtu wa kuogopa sana watoto wa kike,nikarudi ndani na kuchukua sweta la kaka,nikaliweka mwilini. Miguuni nikaweka soksi ndefu kabisa na sendro juu yake,na mikononi nikamaliza na grovu zile za sufi ambazo kaka alikuwa nazo za kutosha ndani kwake.
Baridi ya Arusha ilikuwa kama mateso kwangu kwani kule Dar es Salaam,kulikuwa hakuna hali ya vile hata mara moja. Kwa kifupi Dar,baridi yake ilikuwa inakuja na joto fulani hivi.Hali ile inaitwa jotoridi ,kwa wale wanajografia,kama nimekosea samahanini.
Na hali ile huja kwa sababu ya uwepo wa bahari ambayo kuna kipindi inavukishwa(Hali ya kutengeneza mvuke),na ule mvuke unaenda angani na kutengeneza wingu ambalo linasababisha mvua,au kama sijakosea,mvuke ule unaenda angani na kulainisha hali ya hewa ya kule na kuifanya iwe ya mvua. Hapo tunapata mvua.
Sasa ule mvuke wa bahari,ndiyo haswaa unaleta joto katika jiji la Dar es Salaam,na ndiyo maana mikoa ambayo ipo mbali na bahari,huwa na baridi la hatari. Kama Mbeya,Rukwa na Iringa,huko achana napo aisee.
Hayo ya wasomi,na mimi nilikuwa nataka niwaoneshe kuwa sipo nyuma katika elimu yangu japo sijafika mbali. Turudi kwenye mada.
Basi nilipovaa yale mavazi,nilitoka nje na kuanza kuangaza ni wapi vicheko vile vilitokea,sikuchukua hata dakika mbili,niliona kuna chumba ambacho moja kwa moja akili yangu ilisema kule ni jikoni. Nikanyoosha mwanaume hadi kwenye kile chumba,nikaita hodi nayo hodi yangu ikaitikiwa na sauti moja hivi ambayo ilinifanya nitabasamu kwa faraja kimoyo-moyo.
“Kumbe kuna demu hapa?”Nilijiwazia moyoni baada ya sauti ile ambayo wala sikuifikiria mara mbili kuwa labda itakuwa ya mwanamama. Kwa utaalamu wangu,nilikadiria ile sauti ni ya binti wa miaka kumi na saba hadi tisa.
Kamanda baada ya kuitikiwa hodi yangu nikasukuma mlango kwa utaratibu na kuingia kwenye kile chumba,na kama mawazo yangu yalivyoniambia,kule kulikuwa ni jikoni,sema miaka nilikosea kukadiria,ila iligusa kiasi fulani.
Eee bwana nilikutana na wasichana watatu. Mmoja alikuwa mdogo mdogo,kwa kumkadiria alikuwa anamiaka kama kumi au kumi na moja,mwingine alikuwa ndiyo anaanza kuja kuja ukubwani,alikuwa na miaka kumi na tano au kumi na sita. Halafu kulikuwa na mkubwa wao sasa,tena nahisi yule ndiye alijibu hodi yangu,huyu kwa kumuangalia alikuwa na miaka ishirini hadi ishirini na mbili.
Ngoja sasa nikwambie kitu kilichonifanya nishindwe kwenda mbele wala kurudi nyuma baada ya kuingia mle ndani.Hapa nitakwambia sifa za yule mkubwa na huyu wa kati,yule mwingine achana naye,alikuwa bado mtoto sana. Haniwezi.
Yule mkubwa alikuwa na weupe wa asili,weupe ambao kwangu ulikuwa ni silaha tosha ya kunifanya nidondoshe kila kitu nilichonacho na kumuachia yeye. Usoni alikuwa kabeba macho legevu na ya uviringo kama ya samaki lakini yenye ukubwa fulani hivi wa bashasha. Nashindwa kuyaelezea,ila kama unataka kuyapata yalikuwaje,mwangalie Ray C.
Tuache macho,ee bwana sijawahi kumsifia mwanamke hadi shingo,ila yule bwana alikuwa ni kiboko wa yote. Ile shingo ilikuwa haina michirizi wala nini,halafu imetoka kwenda juu kidogo na baadae ikarembwa na kicheni cha silva yenye herufi ya F.
Sasa pale kati sasa,mitaa ya kifua,ohooo,nyie acheni masela,tena acheni kabisa,mwnaume nilishikwa na uchu wa ngono kama nimekula juisi ya pweza,au supu ya pweza kama hujanielewa.
Kifua kilikuwa kimebetuka kwa juu,na kubeba mtindi wa maana,yaani umevimba na kutanuka. Nilidhani labda kayapiga jeki,lakini nilivyomzoea,niligundua hakuwa mzee wa jeki,kitu kilikuwa orijino kutoka kwa mpendwa MUNGU. Hiyo ni mitaa ya kifuani,ngoja niishie hapo,halafu baadae nitarudi kummalizia pale aliposimama.
Sasa yule mdogo wake wa kati. Yeye alikuwa hana tofauti sana dada yake,nasema ni dada yake kwa sababu walifanana,yaani kwa kuwaangalia tu! Huwezi kukataa hili nalokwambia.
Walikuwa wanafanana sana,lakini tofauti yao ni huyu mdogo kuwa na macho ambayo yaliregea zaidi ya dada yake.Huyu dada yake alikuwa na macho regevu lakini yalikuwa yamekaza,ila huyu mdogo alikuwa anarembua bwana,yaani sijui akipata mafua au malaria inakuwaje yale macho. Tukiacha hilo,huyu mdogo alikuwa pia na chuchu konzi,yaani titi jembamba halafu limechongoka kwenda mbele kama ncha ya mshale. Nani asitamani mazaga kama hayo,kwanza nilipiga na magoti kimoyomoyo na kumshukuru maulana kwa kunileta jiji la Arusha.
“Mbona umesimama mlangoni?”.Sauti ya yule dada mkubwa ilinitoa katika ule mshangao wangu na kunirudisha duniani.
“Mimi sikujua kama hapa ni jikoni. Siwezi kukaa humu”.Nilimjibu huku bado nikiwa naendelea kumtathimini yule binti aliyeumbika kupita malaika wa shetani.
“Ahaa,pole aisee. Karibu Arusha bwana”.Dada yule aliendeleza maongezi.
“Asante aisee. Naona kuna baridi kama nipo Antakatika”.Na mimi nikajibu na kuingiza kiusomi changu cha kuzugia.
“Ha ha haaa. Tulikuona ulivyokimbilia ndani,mbona kuna joto sasa hivi?”.Alijibu huku akitabasamu na kunipa moyo kuwa kuna joto wakati mimi nilikuwa nahisi naweza kuganda muda wowote.
“Wewe,masikhara hayo. Huu ubaridi unaingia hadi kwenye kucha,halafu wewe unasema kuna joto”.Nilimjibu kwa kupingana naye.
“Utazoea tu! We Sheila,mpe stuli mgeni akae”.Binti yule akamwambia yule mdogo wake wa kati anipe stuli nikae maana tayari alishaanza kunogewa na sauti ya gharama kutoka kwa Prince Mukuru.
“Aaag. Mwache akae bwana,mimi wala si wa kukaa hapa. Sijui mzee yupo?Maana niliongea naye asubuhi sana kisha nikarudi kulala”.
“Baba yupo sebuleni,twende nikupeleke maana ni wewe ndiye alikuwa anakusubiria ili aende mihangaikoni kwake”.Alijibu yule binti na kutoka nje,kisha akatangulia mbele kwenda ilipo nyumba yao.
Alikuwa kavaa khanga kiheshima kabisa,lakini bado umbo lake ambalo lilijengwa kwa makalio madogo na ya kichokozi,lilionekana vema kwa mvuto na kwa hamasa ya kila mwanaume kutaka kuona kilichofichika ndani ya nguo ile aliyovaa. Sikuona miguu yake kwa sababu khanga aliishusha hadi chini.
“Karibu kaka”.Nilikaribishwa na yule binti,na mimi nikavua sendro nilizokuwa nimevaa na kubaki na soksi. Nikaingia ndani na kumkuta yule mzee akiwa katika mavazi ya kichungaji. Nikamsalimia kwa heshima zote,na baadae aliniomba nikae kwenye kochi moja lililopembeni ya nyumba ile. Nikatii ombi lake kwa kukaa,na kisha nikatega sikio kumsikiliza mzee yule.
“Umesema unaitwa Prince eeh”.Alianza yule mzee kwa kujikumbusha jina langu,wakati huo yule binti alikuwa hayupo,kishatoka nje.
“Ndiyo Mzee,naitwa Prince Mukuru”.Nilimjibu kwa ufasaha zaidi.
“Sawa Prince,karibu sana Arusha na karibu sana nyumbani kwangu. Sasa nataka nikutambulishe kwa familia yangu ili ujuane nao,na wakija watu tofauti na hawa,basi uweze kuwauliza wanataka nini,maana kuna wezi sana hapa jijini”.Mzee yule aliongea huku kakunja nne ndani ya kanzu yake ya kichungaji.
“We Faridaa”.Aliita mzee yule.
“Abee”.Ikaitika sauti ya yule binti mkubwa.
“Njoo na wenzako”.Akaamrisha mzee kwa sauti ileile.
Baada ya dakika kadhaa,wale mabinti walikuwa kwenye kochi kubwa lile la watu watatu.
“Huyu ni mgeni,ni mdogo wake George,katoka Dar. Kafika hapa jana usiku wa saa tatu. Anaitwa Prince”.Mzee yule akanitambulisha kwa wanawe ambao mimi nilishaanza kupiga nao stori kidogo kidogo.
Sehemu Ya 14
“Karibu Prince”.Nikakaribishwa na mabinti wale kwa wao kupokezana kusema karibu Prince.
“Ehee. Prince. Hawa ni wanangu,huyu mkubwa anaitwa Farida Donyo,huyu anaemfata anaitwa Sheila naye ni Donyo na huyu wa mwisho anaitwa Lilian.
Wote naishi nao hapa na ninaomba uishi nao kwa amani sana. Uwalinde kwa kila kitu. Pia na nyie mfanye vivyo hivyo,mumuheshimu huyu kijana,sawaa?”.Mzee Donyo akatoa wosia huo mfupi kisha akawaruhusu wanawe waende kuendelea na shughuli huko nje.
“Najua utajiuliza kuhusu mke wangu. Sina mke,alishafariki miaka kumi iliyopita wakati anajifungua Lilian. Huyu Lilian nimempa jina la mama yake,yule pale”.Mzee Donyo aliongea huku akionesha picha moja ya ukutani kwa kusema yule ndiye mkewe.
“Pole sana mzee. Na nadhani tutakuwa pamoja sana”.Nilimfariji mtakatifu mimi.
“Sawa kijana. Wewe ukiwa na shida,ongea na hao watakusaidia. Kama unataka kwenda sokoni,kupika au jambo lolote la kike,waombe hao.Ila heshima muhimu,sitaki ujinga ujinga ufanyike,sawa kijana?”.Mzee Donyo aliendelea na ushauri wake.
“Nimekusikia mzee,na nimekuelewa. Ondoa shaka kuhusu mimi”.Nilimpa moyo Mzee Donyo japo nilijua ni lazima mwanae mmojawapo atafia kifuani kwangu. Watoto wazuri vile halafu unaleta habari za kuwaheshimu. Kanifanya mimi sina nanihii eeh,na baridi lile la Arusha,kama ni kesi na iwe,wakijirengesha natungua hata wote wawili.
“Sasa ngoja mimi niende huko kanisani,nadhani tutaonana baadae mida ya jioni,ukae salama”.Mzee Donyo aliniaga na mimi pia nikatoka mle ndani kwake na kuelekea kwangu ambapo moja kwa moja nikafikia kwenye TV na kuanza kucheki chaneli zilizopo kwenye king’amuzi kile cha DSTV.
Nilipata stesheni moja ambayo ilikuwa inapenda sana kuonesha mpira. Na siku hiyo,ilikuwa inaonesha mechi moja nzuri sana ya marudio kati ya Manchester United na Arsenal. Enzi zile Arsenal alikuwa hajapoteza michezo karibu Arobaini na Tisa.Alikuwa yupo vizuri sana. Kule mbele alikuwa TH-14 au Thiery Henry,halafu kulikuwa na kapteni mmoja mkorofi sana anaitwa Viera,huyo alikuwa hana utani. Aliwahi kumtandika vipepsi Rud Van Nistorooy au Rud Van Magoli,kisa Rud alijidondosha eneo la hatari na kupata penati ikiwa bado dakika kama mbili za nyongeza kuisha,kwa bahati mbaya penati ile United walikosa,hivyo ikawa suluhu.
Katika mechi ile niliyokuwa naiangalia,diyo ilikuwa ni mechi ya hamsini kwa Arsenal,yaani angeshinda ile,alikuwa anaweka historia ya kucheza mechi hamsini bila kufungwa. Lakini enzi hizo unawakuta watu kama Roy Keane katikati,kwa mbele Paul Scholes,kuna Giggs pembeni,mbele kuna York na Cole,thubutuuu. Utapita uende wapi,tulipigwa kimoja cha afya. Mimi ni Arsenal damu,ila ile mechi tulipigiwa kandanda bwana.
Kweli tulikuwa wafalme wa soka,lakini mimi sifa nazipeleka kwa Manchester United kwani alituvua ule ufalme wetu. Tutajigamba tuwezavyo kuwa tulicheza mechi arobaini na tisa bila kufungwa,ila pia tusisahau kuwapa pongezi waliofanya historia yetu kukatishwa. Kwani tusipofanya hivyo,ni sawa tunakuwa kama tunajisifia kuwa sisi ni wakali na wakati wakali ni wale waliotugonga.
Hayo ni ya kimechezo zaidi. Ila nilinywea sana baada ya kukatishwa mbio zile na timu kama Manchester,timu ambayo sasa hivi inatishia sana amani hapa duniani. Ila na sisi tunakuja vizuri,mjipange wapinzani.
Baada ya mechi ile kuisha,nilielekea kwenye jokofu la mle ndani kama kawaida na kuchukua juisi moja ya box inaitwa Cares. Ile ilikuwa ni ya Zabibu. Nikaanza kuinywa taratibu kijana mie,wala nilikuwa sina na wasiwasi na mtu,sijaua wala sina deni,basi acheni nienjoy maisha ya Arusha. Juisi ilikuwa ni nyingi na ni tamu sana.
Nikaamua utamu ule niende nao hadi nje kwenye kibaraza kimoja pale nyumbani. Nikaendelea kuburudika na kile kinywaji huku natumiana meseji na rafiki yangu mmoja niliyesoma naye Tabora Boys,wakati huo yeye alikuwa anaingia mwaka wa kwanza chuoni. Aliniambia mengi sana,na alinisihi nirudi darasani kwa ajili ya kujiendeleza kimasomo. Ila mimi kwa kuwa niliamini kaka na wazazi wangu wana uwezo,basi hata bila elimu, naweza kuishi kwa mgongo wao. Nikasahau kuwa mambo yanabadilika na kuna kipindi kila mtu hukaa pembeni na kujali maisha yake.
Hayo sikuyajua,ila nilikuja kuyajua na kuyapitia baada ya kutoka pale Arusha. Arusha hiyo hiyo iliyonifanya wanawake niwaone wachungu katika maisha yangu. Na ni Arusha hii,iliyonifanya nigundue mengi ambayo niliyaacha huko nyuma. Hii ndiyo Arusha iliyonifanya niuite mkasa huu mpangaji,na mwisho kabisa,Arusha ndiyo ilinifanya nikapige magoti kwa wazazi wa Maimuna. Utanielewa nachomaanisha,kuwa na subira.
Taratibu P wa watu nikawa najinywea Cares yangu huku nikijikita zaidi kwenye kutuma meseji nyingi kadiri niwezavyo. Mawazo yale niliyoyaweka kwenye simu,yakanifanya nisahau ya duniani kabisa.
“Wewe,khaa! Hata kusema upo bize,wewe too much pilipili”.Nuilishtuliwa na sauti ya kike iliyoambatana na kofi moja dogo ambalo ni kama lilinitoa mawazoni.
“Ahaa,Farida. Samahani Bibie. Nilikuwa nachat na baba bwana,halafu alikuwa ananipa mikakati mizuri sana,na ndio maana akili yangu ikaamia hapa”.Nilijitetea kwa mtoto yule mzuri.
“Okey. Sisi tunataka kwenda sokoni mara moja”.Farida aliniambia huku pembeni akiwa na yule Lilian,mdogo wake wa mwisho.
“Poa. Mimi nipo hapa,naendelea kuchat”.Nilimjibu Farida na kuendelea kubofya-bofya simu yangu.
“Kwa hiyo hutaki kulijua jiji au?”.Farida aliniuliza na kunifanya nijione kama mjinga vile.Yaani mwanamke anakuja kwangu na kuniambia anaenda mahala,eti namwambia poa. Hanijui wala simjui,sikuweza hata kujiuliza kwa nini kaja kuniaga?
Hapa na maana kwamba,mwanamke asiyekujua akaja kwako na kukuaga au kukuuliza kama unaenda sehemu fulani,basi ujue anataka kitu. Eidha umsindikize au akuagize kitu fulani.
“Dah! Aisee kweli. Embu nichekie hiyo juisi,ngoja nikavae koti kwanza”.Nilimwambia Farida na kisha nikaingia ndani. Nilipotoka,nilikuwa nimevaa koti moja jeusi la leiza ambalo nililinunua Dar es Salaam pale Karume.
“Daah! Umendeza kweli mwenzetu”.Farida alinisifia baada ya kuniona nimevaa lile koti. Wakati huo,huku kwa ndani nilikuwa nimevaa tisheti moja iliyonikamata vizuri kama mwanamiereka. Halafu suruali nilipiga modo moja matata sana,ilikuwa ya buluu. Nyie niacheni mazee,mimi nilikuwa napiga pamba balaa. Hawa unaowaona sasa hivi,wanakurupuka tu!
“Mbona hata wewe umependeza tu! Tena umetoka ile mbaya. Kama Mary J Bridge au Keisha Cole”.Na yeye nilimsifia huku tukianza kutoka eneo lile la uzio wa nyumba ile na kuitafuta njia ya kutupeleka tutakapo.
“Ha ha haaa,sifa za kitoto hizo. Ila siriazi kaka umetoka”.Alisitiza kauli yake Farida.
“Haya bwana. Au nikupe umetishe na kofia nini?”.Nilimuuliza kwa kumtega kwa sababu na yeye alikuwa kavaa kofia ya leiza,ambayo ilikuwa imempendeza balaa. Wakati wote,yule mdogo wake alikuwa kimya tu!.
“Nitafurahi wewe,hayo makoyi nayapendaje?”.Hakuwa nyuma kuonesha hisia zake. Basi na mimi si mwajua navyopenda misifa,sikujali kama nimevaa kujikinga baridi lile la Arusha au vipi. Nikatoa lile koti na kumvisha mtoto yule mzuri,mzuri, mzuri,mzuri kupitiliza.
“Kumbe zito hivi?”.Aliuliza baada ya kulivaa.
“Ha haa,kwani hujui hilo?”.Na mimi nikauliza kama kumjibu.
“Mmh!Nilikuwa sijui mwaya”.Alijibu huku anarembua kiaina.
“Mmh”.Nikaguna kamanda.
“Nini tena?”.Akauliza.
“Kwani nini?”.
“Mbona umeguna?”.
“Ha haa. Hayo macho yako bwana. Eti sijui mwaya. Macho kama yanadondoka”.
“Ha haaa,kumbe na wewe wamo eeh”.
“Aaah wewe. Mimi nimesema tu!”.
Haya bwana. Palee ndiyo sokoni”.Farida alinioneshea sehemu moja kwa kuniambia ndiyo sokoni. Sisi hatukuenda huko,tukaingia chocho moja na baadae tukatokea sehemu moja iana maduka sana kwa pale mtaani.
Watu wengi walikuwa wanatuangalia mimi na Farida wakati tunatembea. Tulikuwa tunaendana sana. Kuanzia urefu,mavazi na maumbile yetu. Wale wasiyonijua,wengi wao walishindwa hata kumsalimia Farida kwa kuhofia labda mimi ni mpenzi wake.
“Farida ndiyo Shem nini”.Dada mmoja alimuuliza Farida baada sisi kuanza kuondoka kwenye duka mojawapo la mtaa ule.
“Aaah,huyu kaka yangu tu!Kaja jana”.Farida alimjibu dada yule na hapohapo tukaanza kuondoka.
“Kwa hiyo ndo unasepa mwenyewe hata kunitambulisha? Tabia mbaya hiyo Farida”.Dada yule alimwambia Farida na kumfanya Farida arudi na mimi pale alipokuwepo dada yule.
“Kaka mimi naitwa Cindy au Cinderela.Farida ni best wangu tangu O-Level”.Dada yule mchangamfu alianza kujitambulisha.
“Na mimi naitwa Prince au kifupi,niite P yatosha. Nipo kwenu mara moja”.Nikamjibu huku nampa mkono wa salaam.
“Basi karibu handsome. Nadhani tutazidi onana”.Dada yule aliniambia huku akiniachia mkono wangu.
“Poa Cindy. Tutaonana”.Nilimjibu.
Baada ya salaam ile,tulianza kutokomea eneo lile huku tukiacha masharobalowa mtaa ule mimacho kodo kama wanacheki filamu ya ngono.
“Kaka P,naomba uninunulie ubuyu”.Lilian,yule mdogo wa mwisho wa Farida aliomba ubuyu baada ya kuuona unauzwa mitaa ile.
Nikajipekshina kutoa mia tano na kumpa akanunue.Akaipokea na akakimbia mara moja kwenda kununua ubuyu huo.
“P. Kuwa makini na midada ya huku,itaanza kuja kuja kwako halafu baadae itakuibia. Jichunge sana,usilete mazoea nao hata kidogo”.Farida alinikanya baada ya mdogo wake kuondoka.
“Zuga tu ile. Unadhani ataniona tena?Hapa ndio kaula,sitoki tena nyumbani. Nimekuja kupumzika na si kuzurura huku”.Nilimjibu huku tunaendelea kwenda kidogo kidogo kwa nia ya kutomuacha sana Lily.
‘Haya bwana.Ukiwa na shida utatuambia”Farida alimaliza maongezi na hapo,stori nyingine zikaanza kushika nafasi yake.
“Hivi juisi yako ipo wapi?”.Farida akaniuliza.
“Ishi! Halafu kweli,si niliwaachia pale?”.Na mimi nikamuuliza huku nikiwa nataka aniambie ukweli.
“Mimi sijui,labda umuulize huyu”.Farida alinijibu huku akicheka na kumuoneshea kidole mdogo wake ambaye tayari tulishaungana katika safari ile.
“Muongo dada. Wakati yeye mwenyewe alikunywa”.Dogo akajibuna kumsababishia kicheko kikubwa Farida hadi yale meno yake yaliyopangana kwa ustaarabu mdomoni mwake,yakaonekana.
Nilisimama huku namshangaa Farida ambaye alikuwa anaenda huku anazidi kucheka.Nikaanza kumfata kwa kasi kumuelekea. Alipoona hivyo,akaanza kukimbia huku anaendelea kucheka. Na mimi nikaanza kumkimbiza.
Yaani ungeona wewe tulivyokuwa,kama picha la kihindi,tena lile la mapenzi. Mtoto anakimbia na mimi namfuza kwa nyuma. Nilipomkaribia,nikashika lile koti lakini kwa bahati mbaya,Farida akadondoka,lakini si kivilee hadi labda aumie au achafuke.Kwanza alikuwa hakimbii kama Mrisho Ngasa bali kama kinyonga,na kile kisketi chake kifupi alichovaa na kumkaa vema,basi mtoto ni kama malaika. Kila kijungu kidogo kwa nyuma,daah! MUNGU anipe nini P?
Basi ile kudondoka,akachubuka kidogo sana kwenye goti. Akawa anadeka mwenyewe.
“P,umeniumizaa”.Hapo jicho lake lipo kama mrenda.
“Hamka bwana. Pole eeh”.Nilimjibu huku namnyanyua ambapo alinyanyuka na kuanza kutembea kama anachechemea.
“Umeniumiza kweli P”.Alizidi kudeka,hapo bado kama nyumba mbili ili tufike nyumbani.
“Ndani ipo spirit,ntakupa upake”.Nikampa moyo.
“Weee,spirit nini?Sipaki”.Alikuja juu hadi nikacheka.
“Sasa si kidonda hicho?”.Nikamwambia.
“Weweee,hata kama,ndio upake spirit”.
“Poa basi. Ntakupa bandeji”.
“Hapo sawa,hayo maspiriti yako,paka vitoto vyako vya ndevu”.Alinijibu na muda huo tulikuwa tayari tumefika nyumbani.
Wakati wote tunatembea baada ya kujidondosha,nilikuwa nimemshikilia vizuri kutokana na maumivu ambayo alisema anayasikia. Hivyo nilipofika nyumbani,nilimuachia na kuingia ndani kwa ajili ya kumletea bandeji. Sikujua nini kiliendelea kule nje,ila baada ya dakika mbili ya mimi kuingia mle ndani,Farida naye alisukuma mlango wangu na kisha akaingia kunikuta mimi nipo sebuleni napekua kutafuta zile bandeji.
Nilipogeuka kuangalia nani kaingia,ndipo macho yangu yalitua kwa mtoto Farida. Sikujua alibadili zile nguo saa ngapi,ila nachojua alibadili nguo na kuja kwangu. Na alifanikiwa kwa mavazi yale.
Alikuwa kavaa khanga ambayo aliivaa kiheshima sana tu!. Ila kwa huku juu sasa,dah! Nyie acheni tu! Wanaume tuna kazi kubwa sana ya kuepuka haya majaribu.
Alikuwa kavaa sijui niseme gauni au nini. Ila ni kama gauni,sema lenyewe lilikuwa lina vifungo kwa mbele. Yaani vifungo vyake vilianzia kifuani hadi lilipoishia lile gauni ambalo lilikuwa katika mtindo wa jinzi. Nashindwa kueleza jinsi lilivyokuwa lile vazi,lakini kwa kukusaidia tu,lipo kama ovaroli,sena lenyewe ni gauni.
Sasa kitu nilichoona kama mtego kwangu ni pale kifuani,ha ha haaa,nyie watu dunia hii wamebarikiwa sana kwa maujanja. Alikuwa hajafunga vifungo hadi juu,hivyo alifanya yale matiti yake makubwa yanaonekana vizuri sana. Yalikuwa yamevimba halafu yanang’aa kutokana na ule weupe aliokuwa amebarikiwa na MUNGU.
Nilibaki nimechutama pale nilipokuwa natafuta bandeji,lakini sikuchutama bure,bali nilikuwa namuangalia yeye na uzuri wake aliopewa na muumba.
“Mbona umetulia?”.Aliniuliza huku akiwa ametabasamu.
“Nakuangalia wewe unayeingia nyumba ya watu bila hodi”.Nikamjibu.
“Hamna bwana. Samahani kwa hilo. Vipi umepata bandeji”.Aliniuliza.
“Yap. Ndiyo hii hapa nimeipata”.Nilimjibu baada ya kufungua droo moja ya kabati lile lililobeba TV na kukuta hiyo bandeji.
“Okey. Sasa si unanisaidia kubandika?”.Aliniuliza swali la mtego huku anatoa ile khanga yake na kumbakiza na lile gauni la jinzi.
Teheee. Acheni Adam adanganyike tu! kwa Hawa, wanawake wanavishawishi bwana.
Unajua nini? Lile gauni alilivaa lilikuwa linaishia magotini.Kitendo cha kutoa khanga na kisha kukaa kwenye kochi,kilifanya lile gauni kuvutika kwa juu na kuonesha upaja wake ulionona kama umepakwa mafuta ya kula.
“Nitakubandika tu!Mbona rahisi”.Nilimjibu na kumfuata pale alipo na kuibandika ile bandeji.Wakati nambandika alikuwa natoa visauti fulani sijui ni vya raha au maumivu au uchokozi tu! sababu vilikuwa kama vina nisisimua kamanda. Nilipomuangalia usoni,alikuwa kalegeza macho utadhani ananyonywa pango.
Nilijifikiria kwanza kabla sijafanya maamuzi. Kwanza kabisa,ni siku ya kwanza tu!ndo nimefika,lakini huyu manzi anaanza kuleta ishu zake mazee.
Pili nikaona huyu anataka aniletee kesi kama za wakina Tuse,na zaidi nikaona labda ni kicheche hivyo anakitu anataka anifanyie au labda ni mtego ili nifumaniwe.
Mawazo hayo yalipitishwa kwa haraka na bunge la kichwa changu,na nikaona njia mbadala ni kumuacha kama alivyo,kisha nianze kutafuta marafiki ambao watanipa data za familia ile.
Niliichukua khanga yake na kumfunika maungio yake mazuri na mororo.Kisha kamanda nikatabasamu na kukaa karibu yake ili asihisi vibaya.
“Nikuwekee filamu gani”.Niliongea naye kwa upole ili ajisikie amani ya moyo.
“Hauna ile ya Romeo and Juliet?”.Aliniuliza huku akiwa na aibu kidogo.
“Ile ninayo. Kuna CD nilitoka nazo Dar,ipo hiyo. Si ile ya Leonard Decaprio?”Nilimjibu na kumuuliza ili nipate uhakika.
“Sijui ndio huyo. Yule aliye-act Titanic”.Alinipa uhakika zaidi.
“Okey. Ndio huyo. Ninayo collection yake”.Nilimjibu na kunyanyuka pale kochini na kuelekea chumbani ambapo baada ya dakika kadhaa nilitoka na albamu ya kuhifadhia CD.
Niliitoa CD anayohitaji na kisha nikaiweka na kuanza kuangalia naye tukiwa wote pale kwenye kochi.Yahitaji uvumilivu sana kuwa karibu na mtoto kama yule ambaye unajua wazi alikuja kwa ajili ya mchezo lakini ukamzingua.
Nilimshukuru MUNGU sana pale mdogo wake alipomuita kwenda kuandaa chakula cha usiku kwani angesipoitwa,nahisi uvumilivu ungenishinda. Mapozi niliyokuwa nawekewa,daah! Kama mtego basi niliutegua hasaa. Namshukuru MAULANA kwa kunifanikishia hilo.
****************
Ni baada ya wiki mbili sasa. Tayari nilikuwa mwenyeji wa Arusha hasa eneo lile la fire. Kule ilipo shule ya Themi ndipo nilikuwa na marafiki wengi,huku kule Daraja Mbili nikiwa naenda sana kuangalia wasanii wadogo ambao kwa pale Arusha walikuwa wengi sana kwa kule.
Pale karibu na nyumbani,nilikuwa nimepata rafiki wengi sana,lakini Gasper ndiye alikuwa rafiki yangu mkubwa kutokana na umri wake na hata alipokuwa anasoma. Alikuwa ni kijana mdogo tu! Lakini alikuwa mjanja sana. Yeye alikuwa anasoma shule moja ya kimataifa pale Arusha,kwa hiyo zile tabia za kichalii chalii alikuwa hana. Tabia kama kujiingiza kwenye makundi ya kihuni na uvutaji bangi ambayo ilikuwa kitu cha kawaida sana kwa wana Arusha,Gasper alikuwa hana.
“Kaka vipi. Ushakula mtoto hata mmoja hapo?”.Siku moja jioni Gasper aliniuliza baada ya Farida na wadogo zake kutoka kuangalia filamu.
“Ha ha haaa. Mimi hata sijui tabia zao dogo. Wasije wakanidhuru bure”.Nilimjibu Gasper.
“Hamna,uoga wako tu! Mbona wasafi hao. Yaani kama pesa mpya”.Alinijibu kwa kunipa moyo.
“Ina maana wewe unawajua hawa tabia zao?”.Nikamuuliza.
“Mimi tena. Data za huu mtaa wote ninazo”.
“Acha bwana. Embu niambie kuhusu huyu dada mtu,kwa sababu ndiye anayenitega-tega”.
“Huyo ni kicheche,siwezi kukudanganya,ila haka katoto kengine,kametulia balaa”.
“Ukicheche wake nini huyu Farida,mbona sijawahi kumuona?”.
“Ha ha haa. Huyu katulia sasa hivi tu! Baba yake alimtishia kumpeleka kijijini kwao ndo maana katulia. Anakikundi kimoja cha wenzake,wanajiita MADUU WA UKWELI,wapo wanne, wanaongozwa na dada mmoja anaitwa Cindy. Hao ni nouma,wakivaa hivi wakiwa wanatafuta mabwana,utasema wanaenda bichi”.Gasper alikuwa akiongea huku akiwa siriaz kitu kilichonifanya niamini asilimia zote.
“Daaah! Kwa hiyo ningeuingia hapa eeh. Maana alikuwa ananitega,sema nilikuwa nategua”.Nikamwambia Gasper.
“Hapo umejitahidi,ila si wa kumuacha huyu. Batua kichizi,tena anaonekana anahamu balaa. Ujue muda ajatoka mtaani,yaani katulia sana. Baba yake aliwafata wale wanamuharibu na kuwapiga mkwara,hadi leo wakimuona wanamkimbia. Nasikia ilikuwa mshikemshike balaa. Wanasema dingi ana bastola,ila bado sijaamini hilo”.
“Ha ha haaa,awe na bastola atolee wapi mchungaji huyu?”.Niliongea kwa dharau.
“Ha ha haaa,mimi mwenyewe nilicheka sana. Ila nitafatilia nijue kama kweli. Ila haka kakati,kenyewe kametulia sana,hakana tatizo. Ningekuwa mimi,ningepiga wote”.Alikuwa bado Gasper.
Nilitabasamu kimoyomoyo na kujisemea kwa kejeri.
“Ungejua malengo yangu. Ungesipotoa siri zao”.Niliwaza hivyo.
“Ndiyo hivyo kaka. Watoto wa Kimasai hawa,wanajua mambo hatari. Piga mizigo. Halafu usiofu kuhusu magonjwa,ndomu zipo. Tumia ujilinde”.Gasper alizidi kumfundisha mwalimu jinsi ya kujibu mtihani.
“Haya kaka. Ngoja nimsubiri anitege tena sasa. Napiga bila kukwepesha. Kumbe cheche bwana”.Nilidhamiria kweli kupiga Farida.
“Kazi ni kwako kaka”.Gasper alinijibu na tukaanza kupiga soga nyingine hadi mida ya jioni ambapo aliondoka na kuniacha mimi nikijipumzisha kitandani kwangu.
Sehemu Ya 15
Siku hiyo nakumbuka ilikuwa ni Jumatatu. Kaka kama kawaida alikuwa kaenda mzigoni kwake ambapo alikuwa anarudi siku za wiki endi. Baba wa Farida alikuwa naye kaelekea kanisani afanyapo kazi.
Nikiwa bize na kuacheza play station ambalo nilimuomba kaka anunue,mara akaingia Farida akiwa kavaa koti langu lile nililompa wiki tatu zilizopita.
“Ayaaa,na wewe umekuwa mtoto?”.Alianza Farida baada ya kuniona nacheza game.
“Aaah,kawaida bwana”.Nilimjibu na kuacha kucheza ili nimkaribishe.
Alikuwa kapendeza sana,kila siku alikuwa anajaribu kujiweka mpya. Hicho ndicho kitu nilichokuwa namsifu. Siku hiyo alikuwa kavalia sketi kama ya kutereza,ni kama mpira hivi,au leiza. Halafu ilikuwa si ndefu sana bali imeishia juu ya magoti,basi na ule urefu wake,haki ya MUNGU sikuweza kujizua kumsifia.
“Mmmh!Leo mama yangu umetoka. Kama Jojo vile”.Nilimsifu.
“Embu toka hapa. We kazi yako kunifananisha na huyo msanii tu”.Alijibu huku tabsamu halimuishi midomoni mwake.
“Ndo umeniletea koti langu nini,maana nimelimiss”.Niliachana na mada za utani na kwenda kwenye kitu changu.
“Wewee,hapa hupati kitu. Hili umenipa mwenyewe”.Alinijibu huku bado kasimama karibu na mimi. Wakati huo nilikuwa bado sijaamka pale chini nilipokuwa nacheza game.
“Embu acha masihara hayo. Koti elfu arobaini hilo”.Nilimjibu huku bado nikiwa palepale.
“Ndo nshakudhurumu hivyo”.Alinijibu na kisha kugeuka kama anaondoka. Hapo nilinyanyuka haraka na kuanza kumfata.
Kitendo kile cha kunyanyuka haraka vile,kilimfanya kama ashituke na kutaka kukimbia,ila tayari kamanda nilikuwa karibu yake nikivuta koti langu.
Ikawa vuta nikuvute,mimi huku,yeye kule. Lakini wasichana wana nguvu za kipekee. Niliona kama litachanika tukiendelea kulivuta. Hivyo nikaamua kumwachia.
Kitendo cha kumuachia,alianza kujigamba na kujiona kashinda. Basi kwa hasira nikamfata hadi pale alipokuwa amesimama kisha nikalianzisha tena.Yaani nilianza kulitaka tena koti langu.
Basi ilikuwa nikifata mkono huu,analeta mkono ule.Nikiufata mkono ule,analipeleka kwa nyuma. Dah!Ilikuwa mshikemshike hatari lakini hatimaye nililibamba kwa mikono yangu miwili. Lakini mikono hiyo ilikuwa imepita kiunoni kwake,na kulikamatia koti kwa nyuma kwa sababu ndipo lilipokuwepo.
Hekaheka nyingine zikaanzia hapo.Koti lipo kwa nyuma,na mimi nimelikamatia hukohuko.Hapo ikawa balaa,kwani alijipapatua na mwisho wake tukajikuta tunadondokea kwenye kochi,yeye kwa chini mimi kwa juu.
Kile kifua chake kilikuwa sawa kabisa kwenye kifua changu. Hapo sasa nikapata mihemko minginee.
Tuliangaliana kwa muda,na tukajikuta wote tunacheka,na tulipoacha kucheka,tuliacha sawia.Hapo kamanda nikaanza kusogeza midomo yangu taratibu kwenye midomo yake. Ile mishe ya koti,nikawa nimeisahau.
“Aaah, shit!. Nataka kufanya nini hapa?”.Nilijikuta nalalama peke yangu na kujitoa kwenye kifua cha Farida kwa kukaa pembeni.
Farida naye kwa aibu akainuka bila kusema neno na kukaa pembeni ya kochi lile kama mimi. Wakati huo nilikuwa nimejiinamia huku nimejishika kichwa kuonesha kama kujilaumu kwa kitu nilichokuwa nataka kufanya,na kumbe ilikuwa chezo tu!. Kamanda nilikuwa nataka kubembelezwa ili mtoto ajilengeshe mwenyewe.
Baada kama ya dakika moja na nusu,nilisikia kama kuna msukumo kwenye kochi kuja kwangu. Msukumo ule ulikuwa ni wa Farida akijivuta kuja kwangu.
“Sasa mbona umepoa hivyo P?”.Aliniuliza kwa sauti ya puani.
“Hamna. Ujue nilitaka kufanya jambo la ajabu sana”.Nilimjibu.
“Kwani vibaya?Au jambo la ajabu lipi?Kuna jambo la ajabu kama mtu mzima kunya kitandani au kujikojolea?. Au kusikia Rais kampiga mkewe hadharani. Kuna jambo la ajabu kushinda hayo?”.Aliongea Farida kwa sauti yake ileile.
“Najua hayo,ila hata hili lilikuwa ni jambo la ajabu sana”.Nilimjibu huku nainua kichwa changu kumwangalia.
Daah!Alikuwa kalegeza macho utadhani labda tayari nishamuingizia mdudu. Niliguna kimoyomoyo na kujifanya sina habari na yeye. Kumbe nilikuwa natega akiingia tu!,nifanye yangu. Na kweli akaingia.
“Bwana Piii,maneno gani hayo? Mwenzako sitaki”.Aliamua kujitoa mhanga na kunikumbatia kwa nguvu huku kifua chake kilichobetuka kwa juu kikigusa maeneo yangu ya mgongoni.
Safari hii sikujivunga tena. Si alikuwa mgongoni. Basi kamanda nikageuka,palepale nikiwa nimekaa,nikaingiza mikono yangu kwenye makwapa yake na kumnyanyua. Naye akanyanyuka kilainiiiiii,kama nanawa vile. Nikambeba,halafu nikamleta kwa mbele.
Kile kisketi chake,nikakirudisha kwa nyuma,sasa nikawa nayaona mapaja yake yaliyonona kama mnofu wa kitimoto,ule mbichi. Nikampakata,yaani miguu yake ilipita kiunoni kwangu.
Baada ya hapo,nikashika kiuno chake na kumvuta zaidi kwangu. Sasa kile kisehemu cha mbele cha kwenye chupi yake,kikawa kimegusa hadi kwenye zipu yangu. Bado miguu yake ilipita hadi nyuma mgongo wangu. Si wajua mtoto alikuwa mrefu kama mimi?. Basi ile miguu kwa huku nyuma akawa kaikunja na kuibana vizuri mgongoni kwangu.
Hapo kamanda nikanyoosha mikono yangu na kuzigusa zile nazi za kwenye kifua. Mautamu yakaanza kusambaa mwilini mwangu,kutoka kwenye mikono hadi kwenye boxer na kufanya mzee ananyuke kidogo na kukugusa kieneo cha chupi ya Farida. Kumbe kiligusa palepale kwenye pango. Ha ha haaaa,hapo mtoto alitoa mguno wa mahaba na kuanza kusotea kwenda mbele kwenye ile sehemu alipo Prince tena huku akiakatika.
Mimi kama mnijuavyo. Sina papara wala kokoro. Nipo taratibu lakini ndo naenda hivyo. Nikanyofoa kile kitopu chake na uso kwa uso nikakutana na nazi zilizovimba haswaa. Zilikuwa zimevimba vya kutosha halafu chuchu zilikuwa zime Dar es Salaam Stand Up,put your hands up. Kama ule wimbo wa Chid Benz.
Chuchu zilikuwa zimesimama balaa,na ule mtuno wa pembeni,ulinifanya niseme, Oooh My GAAAASH,kwa nini umenileta kwenye hii dunia ambayo kila kitu kizuri? Kwa nini umenikutanisha na binaadam kama huyu?. Daah! Nyie acheni MUNGU aitwe MUNGU.
Baada ya kumtoa ile topu,huku yeye akiendelea kukatikia ile sehemu ambayo kwa muda ule ilikuwa imefunikwa kwa suruali. Mimi nilizivamia nazi kama mkwezi na kuanza kuzisorola byee. Nilizinyonya kwa hamasa kubwa na baadae nikaanza kuzitafuna chuchu zake kama mtoto mwenye magego.
Hapo mtoto Farida akazidisha mauno huku akijikandamiza zaidi kifua chake kwenye mdomo wangu. Kitendo bila kufikiri,nikambinua na kulala naye kwenye kochi,mimi nikiwa juu na yeye chini. Nikaingiza mikono yangu ndani ya sketi yake,na moja kwa moja nikaelekea hadi kwenye zile lastiki za chupi zinazokaa kiunoni. Nikazishika na kuzivuta,nazo zikakubali sheria.Zilipofika pale kwenye makalio,zikagoma kutoka kwa sababu zilikuwa zimebanwa kwa chini ya makalio. Hivyo Farida alibinua kiuno chake kwa juu,basi ile chupi nikaitoa mahala pale. Pia ilipofika miguuni,alinyanyua miguu juu,basi na mimi nikanyoosha mikono juu na kuinyofoa ile chupi.
Sasa Farida alikuwa kabaki na sketi tu! Ile sikushughulika nayo kwani ilikuwa uinanipa hamasa sana nikiigusa,si mwajua nilisema ilikuwa ni ya Leiza?. Basi ndo hivyo jamani.
Mwenzenu nikaipandisha ile sketi kwa juu na hapo nikalala zaidi kifuni kwake na kuanza kula kinywa chake. Kwa utashi wake,na yeye akanibinua fasta,nikawa chini yeye juu kanikalia yale maeneo. Akanivuta kuja juu,na mimi nikaenda,hivyo tukawa tunaangaliana. Akanitoa fulana yangu,nikabaki kifua wazi,kifua ambacho kilikuwa kimekatika kwa katikati na kubeba nywele kiasi ambazo Farida kwake alizifanya kama foronya,kila saa alilala kifuani huku akizipapasa.
Ule uwanja ulikuwa mdogo sana. Na Farida alionekana kuwa fundi,hivyo katika galagazana tungeweza kudondoka hata chini. Basi nikanyanyuka naye tukiwa vilevile,nikambeba hadi chumbani kwangu huku miguu yake ikiwa imepita kiunoni kwangu na mikono yake shingoni mwangu,na tendo la kubadilishana mate ndilo lilikuwa linajiri wakati ule.
Kama kawa nikafika gheto na kumbwaga manzi yule akiwa na kisketi ambacho nacho nilikivuta na kukitoa mwilini mwake. Hapo live live mzee naona pango lililokuwa limenona na safi hata kwa kula. Nilimeza funda moja la mate kwa tamaa iliyokuwa imenikaba. Basi na yeye akanyanyuka na kukaa pale kitandani kisha akafungua mkanda wa suruali yangu na kuitoa maungioni mwangu. Kamanda nikabaki na boxer moja.
Nayo bila uoga wa kukutana na nyoka akaitoa. Sasa hapo na yeye uso kwa uso alikuwa anatazamana na joka lenye jicho moja. Akakamata kwa mkono wake wa kuume,kisha kwa mbwembwe akaanza kuipikicha kwa kuipeleka mbele na kuirudisha nyuma. Akaona haitoshi,akaiweka mdomoni na kuanza kuifanyia mautundu yake.
Ile raha nilikuwa sijaipata muda mrefu sana. Hivyo baada ya kuweka mdomoni,nilianza kuhisi hali ya kutoa wazungu. Kwa haraka nilimtoa ili nisimchafue,na yeye nadhani aligundua hilo. Akachomoka na kisha ukabaki mkono wake ukiwa unafanya kile kitendo kama cha kujichua. Basi hapo nilihisi kama nataka kupaa,kumbe ndio mambo yalikuwa yanakuja.
Ndiyo maana yake,kamanda nilirushwa stimu na manzi. Yaani nilitoa nje kwa mara ya kwanza. Alitabasamu kidogo baada ya kuona vile,kisha akaniambia sasa hapo tutaenda sawa.
Basi tulienda hadi bafuni,kwa kuwa lilikuwa mlemle ndani,wala hatukupata shida,ni kama tumefunga ndoa. Tukaanza kuogeshana,huku miili yetu tukiwa tunachezeana hapa na pale. Punde P tayari akawa karudi katika hali yake. Sasa hapo sikutaka mchezo tena.
Nikamuanzia mlemle bafuni. Nikauweka mguu wake juu ya sinki,na kisha nikainama na kuwa kama nachungulia kitu kwenye pango lake. Kidume nikapeleka mdomo wangu pale kunako. Teheeeee,mtoto alichonambia nakumbuka alisema maneno machache tu! Alisema eti anataka kudondoka. Basi mimi nikajaa kichwa,nikazidi kula pango ,heeee. Mtoto si akaanza kulegea bwana,ikabidi nimuache.
Hayo macho asee,dah! Sijui hata nisemaje ili unielewe. Nikamkokota hadi kwa bed. Sikutaka kumchelewesha saana. Nilichokumbuka ni kuvuta droo ya kitanda changu na kuchukua dhana ambazo nilitoka nazo Dar. Nikatinga tayari kwa mechi.
Yaonekana alikuwa hajafanya kweli kwa muda mrefu kwani nilipoingia alinilaki kwa kunikumbatia kwa nguvu kisha akawa ananiminya mgongoni yaani anamaanisha nizame zaidi,na mimi wala sina tatizo. Kitu nikawa nazama hadi mwisho,si mwajua kifo cha mende unavyokuwa huru kuzama hadi unagusa ndani kabisa. Basi habari ndo hiyo. Kuja kutahamaki,tayari nilikuwa nimefunga goli mbili za hatari.
“We mwanaume ni balaa”.Alianza sifa za kijinga na wakati mimi najua kabisa sijampa ule mzigo wenyewe.
“Kawaida hiyo. Siku moja ntakupa dozi yenyewe”.Nilimtania lakini ilikuwa ni kweli.
“Hapa umenikata kiu kabisa. Nikija tena nataka nikukate wewe”.Aliniambia.
“Usijali. Karibu sana”.Hapo alikuja kinywani kwangu na tukashare mate kama dakika mbili na kisha alinyanyuka na kuvaa mavazi yake na kupoa mle ndani.
Huo ndio ukawa mwanzo wa mchezo wetu,ambao utotoni tuliuita mchezo mbaya.
***************
Wiki mbili zilikata huku kale kamchezo tukizidi kukaendeleza kati yangu na Farida.
Nakumbuka siku hiyo Farida alikuwa ametoka tangu asubuhi na ilisemekana atarudi jioni sana. Kwa hiyo pale tulibaki watu watatu. Yaani mimi,Sheila yule wa katikati na Lilian yule wa mwisho ambaye alikuwa kaenda kucheza huko anapojua yeye.
Yule Sheila alikuwa yupo pale nyumbani na muda ule alikuwa anafua nguo sijui za familia zile au za kwake.
Basi mimi nikatoka zangu nje kama kawaida na box la juisi. Nikaanza kunywa huku najipigia mruzi ambao hata sikumbuki ulikuwa unahusu wimbo gani.
Yule mtoto kusikia nipo pale,ni kama alifarijika na moja kwa moja akazuga anaenda kuanika nguo kwenye kamba ambayo ilikuwa mbele ya kibaraza ambacho mimi nilikuwepo.
Baada ya kuanika akanifata pale nilipo na kisha akaanza kuongea maneno ambayo,dah! Sikudhani mtoto kama yule angeweza kuyanena.
“Nasikia unamla dada”.Alianza.
“Mh!We Shei unawehuka?”.Ilibidi niulize.
“We sema tu! Unamla dada?’.Alikazia.
“Embu kaendelee kufua”.Nilimkatisha maswali yake.
“Basi sasa,mimi nilikuwa nataka kukusaidia jambo lakini yaonekana huna mpango”.Aliongea huku ananiacha pale peke yangu.
“We Shei embu rudi rafiki yangu”.Nilimwita.Naye bila hiyana akarudi.
“Niambie kuna nini?”.Nilimuuliza.
“Sema kwanza. Unamgonga au humgongi”.Kicheko kilinibana hasa nikiangalia anayeniambia hayo.
“Poa. Nimefanya naye. Kuna nini kwani?”.Nilimjibu na kumtupia swali.
“Ulitumia ndomu?”.Swali lingine lilikuja kwangu.
“Sasa wadhani mimi namuamini msichana kama yule hadi nisitumie kinga?Kinga sitatumia kwa mtu nayejua hana tabia za ajabu”.Nilimjibu.
“Ahaaa. Hapo basi,hilo muhimu sana. Yule ni dada yangu lakini kuwa makini naye,unaweza kuzikwa. Hapo kaenda viwanja,akirudi yupo bwii”.Aliongea Sheila na kuondoka eneo lile kwa ajili ya kwenda kumalizia kufua.
Maneno yake yalikuwa kama yameamsha jambo na kutaka kulijua zaidi. Nikasema lazima nijitahidi ili nihakikishe maneno yale kutoka kwa Sheila.
Basi siku hiyo nilikaa nje kwa muda mrefu kuliko siku zote ili tu! Nimuone huyo Farida na muda anaorudi na kuhakikisha maneno ya Sheila.
Ndipo mida ya saa nne na nusu za usiku,nilisikia mtu kama ananyata kuingia eneo lile la nyumbani. Na mimi niliposikia hivyo,nilijificha kwa pembeni kidogo ili nisionekane pale atakapotokeza.
Mara nilimuona Farida akiwa kavalia kimini kimoja matata sana na brazia moja ya ajabu mno.
Kile kimini kiliishia juu ya mapaja,hali ambayo kama akiinama basi nguo yake ya ndani ingeonekana,wakati huo ile brazia ilikuwa ni kama chandarua,yaani ilikuwa inamatobo matobo halafu ndani hakuvaa kitu chochote. Hali hiyo ilifanya chuchu zake zitoke nje kupitia yale matobo ya brazia aliyovaa.
Aliangalia huko na huko kisha alitoa kimkoba chake na kunyofoa khanga mbili. Moja aliivaa chini na nyingine aliitanda kwa juu. Na baada ya kufanikiwa hilo,alienda hadi lilipo-dirisha lao na kuanza kumuita Sheila kwa sauti ya chini,na baada ya Sheila kuitika,aliulizwa kama baba yake yupo. Akajibiwa hayupo,na ndipo ahueni ya Farida iliposikika kwa kushusha pumzi moja ndefu.
Mimi kama kawaida yangu,huwa sipendi sana kumficha mtu. Baada ya Farida kutoka pale dirishani,alienda hadi ulipo-mlango wao wa sebuleni. Na mimi niliona huo ni muda muafaka wa kujifichua mahala nilipokuwepo.
Kwa mbwembwe nyingi nilianza kwa kupiga mruzi wangu uleule ambao haulewekagi ni wimbo gani unaimbwa katika ara ile ya mruzi.
Nilimuona kama kashtuka lakini alijitahidi kuficha hisia zile na kunifata hadi pale nilipokuwa nazuga napiga mruzi.
“Kwani P ulikuwa hapa muda mrefu eeh”.Aliniuliza swali ambalo wakati linakuja lilikuja na harufu ya pombe.
“Unakunywa na pombe mwenzetu?”.Nilimuuliza swali badala ya kujibu swali.
“Aaagh. Imetokea tu leo,nikajikuta nimekunywa”.Alinijibu huku akiangalia pembeni kama mtu atafutaye kitu pale nje.
“Mmmh,kwa hiyo na hayo mavazi ya ndani nayo utasema umetokea tu! Kuyavaa,si ndio mama?”.Nilimuuliza swali lingine.
“Daah! Yaonekana ulinisubiri kitambo,kama mzazi wangu vile”.Alinijibu Farida kwa maneno ambayo yalikuwa yana nia ya kuanzisha vurugu.
Sikuwa na wasiwasi na shombo zake bali nilimchukulia kama mtu asiyejielewa afanyalo. Nilimuangalia usoni kwa macho yaliyojaa hasira zilizochanganyika na huruma juu ya maisha yake, na yeye aliniangalia kwa macho yake ambayo yalikuwa makavu na tayari kwa ajili ya vurumai. Wakati huo Sheila alishafungua mlango na kubaki mlangoni akitutazama tunachofanya.
“Hongera kwa maneno yako matamu. Lakini nimeona kila kitu. Umependeza sana kwa yale mavazi,ila nashangaa kwa nini uliamua kuvaa mikhanga”.Niliongea huku bado macho yangu yakiwa usoni pake.
“Hayo hayakuhusu babu wee. Jali biashara zako na si kukaa kwa kaka yako na kusubiri kumuona Farida kavaaje au anafanya nini. Baridi limekupiga kutwa nzima,kisa unamsubiri mwana wa Donya. Utakufa na Athima mtoto wa kiume,unaelelewa na ndugu zako. Tafuta vyako bwege wewe,msyuuu”.Aliongea Farida kwa nyodo na kunifanya nichanue tabasamu la kejeli kutokana na maneno yake yaliyomalizika kwa msonyo mrefu kutoka kinywani kwake.
“Ohooo. Kumbe na wewe una kidomodomo eeh. Pole sana binti,kama ulidhani mimi nitakuja juu,umebugi sana. Na jambo usilolijua,litakusumbua sana. Na mwisho wa siku utabaki unasonya misonyo tu!. Endelea na kazi yako ya umalaya,si ndio inakufanya ulete dharau na kuniona mimi bwege?Kwa kuwa wewe unatafuta kwa kutumia mwili wako na mimi nakaa kwa kaka yangu bila kazi,si ndio eeh”.Niliongea huku nampa mgongo kwa ajili ya kuingia ndani kwangu.
“Wewe unadhani Mwana FA aliimba bure? Ingekuwa vipi kama kungekuwa hakuna malaya,si ubakaji ungeongezeka kwa kasi ya ajabu. Acha niwe malaya ili niwalinde wadogo zangu wasibakwe kwa kuwamaliza hamu wanaume wenye tabia hizo. Usidhani malaya kaumbwa ili awe malaya,saa nyingine ni maisha tu!”.Maneno hayo yalinikumbusha maneno ya Mama Tuse na Tuse mwenyewe.
Niligeuka nikamwangalia sana Farida,kisha nilitikisa kichwa kwa masikitiko na kurudi tena pale niliposimama mwanzo.
“Hivi wewe Farida,hapa kwa baba yako umekosa nini wewe?Utake nini usipewe? Utake uende wapi ukataliwe? Na wewe unadiriki kusema eti hukupenda kuwa malaya?Unafanya kwa sababu ya jambo?
Jambo gani ambalo unalifanya linaleta faida kwa baba yako? Hao uanaosema unawalinda wasibakwe,wewe uliwahi kubakwa hapo mwanzo?Wewe ulilindwa na nani ili usibakwe?Embu acha chenga,tena bahati yako,ungekuwa anga zangu ningekuchapa viboko kwa kuwashushia heshma wazazi wako waliokulea kwa kila hali huku wakihakikisha unapata kila kitu muhimu.
Nimekutana na malaya mimi,malaya ambao kama wangekuwa ni wewe,sidhani kama wangefanya yale. Wanamalengo kuliko hata ya mtu ambaye si malaya. Eti na wewe unasema hukupenda,tamaa za mwili na vitu vikubwa,zitakuponza wewe”.Niliongea kwa hasira sana maneno hayo,na yeye alitambua kuwa nimepata moto hivyo alikaa kimya bila kusema chochote hadi pale nilipoingia ndani kwangu na kusikia mlango wao ukifungwa.
****************
Kesho yake Farida hakutoka nje kwa sababu ya aibu. Na mimi nilishukuru sana kwani maneno yangu yawezekana yalimuingia ipasavyo.
Siku ikapita bila kumwona na hatimaye wiki ikakata pia bila kumwona bali kumsikia akimuita mdogo wake,ila nahisi alikuwa anatoka,sema akiniona anakimbia au kujificha.
“Atajua mwenyewe.Meseji sent”. Ni maneno niliyojisemea siku moja baada ya kuona kimya chake kikiwa kikubwa.
******************
Kwa upande wangu, muda wa kukaa pale nyumbani kwa kaka,ulibaki kama wiki mbili na nilikuwa tayari kwa kuondoka baada ya wiki hizo.
Nilianza kuwaaga pale nyumbani hasa wale niliyokuwa nawaona. Tulikuwa tumezoeana sana,hasa utani wangu ndiyo kama chachu kwao ya kuwa wanyonge baada ya kusikia naondoka.
Wakati nimebakiza wiki moja niondoke pale nyumbani,likatokeza tatizo kubwa jingine. Hili ni tatizo kubwa kuliko matatizo yote niliyowahi kuyapata maishani mwangu. Tatizo hili naweza sema ndilo haswaa,lililonifanya nione Arusha chungu na mbaya sana kuliko mikoa yote niliyowahi kutembelea.
“SHEILA”.Acha nimtaje kwa herufi kubwa kwani bila yeye,leo mimi sijui ningekuwa wapi katika maisha haya mazuri ya kuajiriwa na serikali pamoja na makampuni makubwa duniani. Huyu kasababisha mimi nisiwe tena na maisha hayo. Najua wajiuliza kivipi,ila ngoja nikuhadithie sasa.
************
Ikiwa imebaki wiki moja mimi kuondoka pale nyumbani. Huyu Sheila alianza kunitega. Tena mitego yake ile ya Farida ilikuwa cha mtoto. Si mwajua huyu alikuwa kama chipukizi vile,yaani chuchu ziwa konzi,kiuno kilichoingia ndani kama dondora na huku chini kuna matufani yaliyokuwa yamejipanga kinoko-noko hasaa. Yaani mmmmh! Acheni jamani.
Siku hiyo asubuhi na mapema niliamka kama kawaida yangu na kuanza kutalii mazingira ya pale nyumbani. Wakati nashangaa shangaa,mara nikamuona Sheila anatoka nyuma ya nyumba na fagio kubwa la kufagilia uwanja. Sikushangaa kwani ilikuwa ni tabia yake kila asubuhi kufagia uwanja. Alinipita bila hata kunisalimia na kuingia ndani kwao.
Nahisi siku hiyo baba yake hakurudi nyumbani,maana alipoingia alitoka tena,lakini safari hii alivyotoka kwa kweli sikumuelewa hata chembe.
Alikuwa katoa ile sketi yake anayoitumia kufanyia kazi na alivaa khanga moja tu!. Khanga ambayo ukiingalia sana,utagundua kuwa inaonesha hadi maungo yake. Sasa ni kheri angekuwa anaenda labda bafuni,lakini haikuwa hivyo. Alikuja kwangu moja kwa moja.
“Leo P sijakusalimia jamani”.Alianza kihivyo huku macho yake yakiwa yanazunguka zunguka kiurembo zaidi.
“Nashangaa”.Nilimjibu na kuendelea kuwa bize na mambo yangu.
“Na wewe hata unishtui bwana”.Bado aliendelea kuniongelesha huku yale macho yake yakizidi kuranda randa na kurembuka.
“Mi nishawazoea. Mbona hata dada yako naye simuoni”.
“Aaagh,huyo achana naye. Kwanza unajua siku ya tatu leo halali ndani?”.
“Ama nini?Ina maana kajihalalisha tabia yake?”.Nilimuuliza.
“Huyo kishazoea mambo hayo. Mimi sitaki hata kumsikia”.Alinijibu.
“Mtajua wenyewe bwana. Ili mradi kaniacha salama na nimemuacha salama”.Na mimi niliongezea.
“Aaah!.Prince nikwambie kitu”.Ghafla Sheila alitoka kwenye yale maongezi.Akaanza kama kujikuna mguu,na baadae aliongea huku macho yake yakiwa yamerembuka kupita kawaida.
“Nini mdogo wangu?”.Nilijua nia yake.Ili kumkatisha nilimuita mdogo wangu.Lakini haikufua dafu. Sheila alikuwa kadhamiria hasaa.
“Naomba unisaidie P. Hapa kwenye mguu wangu pawasha”.Aliongea hayo huku anakuja pale kwenye kibaraza nilipo na kunipa mgongo kisha akafunua khanga yake na kuonesha sehemu ambayo anasema inawasha.
Ile khanga aliifunua vizuri kwelikweli,ingekuwa midume mingine kama huyu anaesoma,palepale angeanza mambo mengine. Ila kwa P,ilikuwa kitu cha kawaida sana.
“Hapa au?”.Nilishika lile eneo analosema linawasha na kumuuliza kama ndipo pale.
“Hapo kwa juu kidogo”.Aliongea kwa sauti ya chini huku mguu wake nimeushika mimi.
“Hapa?”.Niliuliza tena baada ya kugusa kwa juu yake.
“Kidogo tena juu”.Aliziidi kupanda. Hadi hapo tayari tulishavuka maeneo ya maungio ya mguu,na sasa alionesha sehemu inayowasha kuwa ni paja lake. Paja nono,paja jeupeee.
Kidume nikameza mate ya uvumilivu na kupiga moyo konde. Na nilichukulia yale ni majaribu tu!
Nikapanda hadi juu alipotaka. Mmmh! Kama majaribu ndio yapo vile,basi yale yalizidi kipimo.
Eti nilipogusa pale aliposema,mara akapandisha khanga yake hadi juu ya mapaja. Ha ha haaaa,wajua nini mpenzi msomaji?. Hawa watoto wa kike waacheni kama walivyo,wakiwa wamepandwa na maruhani yao sijui wanakuwaje.
Kumbe ndani bwana alikuwa hajavaa chupi wala nini. Mi nilidhani labda pale mwanzo niliona uongo maungio yake,lakini wala,ilikuwa ni kweli. Alikuwa hajavaa chupi aisee.
Basi ile kupandisha khanga yake juu,eeh bwana si nikaona pango lake!. Tena likiwa ndiyo kwaanza linaanza kuota vinyweleo. Pango lipo safi kichizi,halafu limejibana hatari. Hata pale aliponiambia hapa ndio panawasha huku anatanua miguu yake,bado lile pango lilikuwa limefungika,yaani ule mlango ulikuwa bado hauonekani.
“Shei. Unanizingua bwana. Mimi huko siwezi”.Ilibidi kamanda nijidai bwege tu!Maana ningejidai naendelea kuuliza,mara ningegusa na lile pago.
“Bwana P,ndio hapohapo,we nikune tu!”.Aliongea sauti ya puani hadi nikahisi huyu mtoto anaweza kufa kwa sauti hii ilivyobadilika.
Basi kwa haraka,nikakuna pale aliponiambia na kisha nikanyanyuka ile sehemu niliyokuwa nimepiga goti na kuingia zangu ndani kwangu bila kuaga wala nini.
Nadhani hali ile ilimtia mashaka Sheila,alihisi labda tayari nilikuwa nimepata hasira au nimemuhisi vibaya.Lakini hiyo yote ilikuwa sivyo,nilikuwa namvutia ndani makusudi. Mtoto kama yule na uzuri kama ule hawezi kupita hivihivi kwa Master P bila kupewa mdudu. Unacheza na mimi nini?
“P nimekukera?”.Sheila alikuja hadi sebuleni muda uleule nilioingia na kuniuliza swali hilo ambalo kwangu nilitegemea sana kuja kutokea na nilifurahi kwani mtego wangu ulikuwa umekamilika.
Huku nabofya bofya simu yangu nikiwa pale kochini,nilimuangalia kwa macho ya tabasamu na kumjibu.
“Hamna hujanikera wala nini. Sema simu yangu ilikuwa inaita ndio maana nilikuja haraka kuipokea”.Nikamjibu huku bado nikimuangalia kwa macho yale yale ya ushindi. Wakati huo alikuwa kasimama kwenye ule mlago wetu wa kuingilia.
“Ahaaa. Mi nilidhani nimekukera kwa tabia yangu”.Naye alionesha ahueni baada ya majibu yangu.
“Hamna. Si ulikuwa unaumwa bwana,ilibidi nikutibu tu!”.Nilimchokonoa kwa vijimaneno vyangu ambavyo naye alionesha nia ya kuendelea kuchokonolewa.
“Hata bado hujanitibu,mi bado nawashwa mwenzako”.Mambo kama hayo kwa kweli huwaga silazagi damu. Ilibidi nifanye kama kila mwanaume anachotakiwa kukifanya.
“Njoo basi niendelee kukukuna mtoto mzuri”.Nilimwambia huku naweka simu yangu kwenye meza moja ya kioo iliyokuwa sebuleni pale.
Mtoto akasogea hadi pale nilipo,kisha akanipa mgongo na kufunua khanga yake hadi pale aliposema panawasha ambapo palikuwa karibu kabisa na tako.
Kamanda nikameza funda moja la mate ambalo lilionesha kabisa kuwa ni la kutamani mchezo mbaya. Sasa badala ya kumkuna ikabidi nifanye maepe yangu.
Kwanza nikaongezea kuifunua ile khanga hadi uso kwa uso nikakutana na kalio moja jeupe na lisilo na vinyweleo hata vya kusingiziwa.
Nikalikamata lile kalio kitaalamu kabisa na kuanza kulifanyia maseji. Mtoto akawa katulia tu! Nilikuwa sioni uso wake kwa hiyo siwezi sema alikuwaje usoni wakati mimi nafanya yale.
Basi niliporidhika na ile maseji nikahamia moja kwa moja kwenye kile kisima cha buradani ambacho napenda sana kupaita pangoni. Lakini sikuingia kabisa pangoni bali nilibaki pale nje yake.
Nilipaka mate kidogo kwenye kidole changu cha kati,kisha nikakipeleka kidole kile kwenye sehemu ya juu ya kisima kile cha burudani. Nikaanza kukiterezesha kidole changu kwenye kile kidude cha juu ya pango.
Hapo mtoto hakuvumilia ile hali,akajikuta mwenyewe anakaa kwenye mapaja yangu na kunilalia kifuani huku akitweta kwa mihemo ya mahaba. Hapo kamanda nikaendelea kuonesha maujuzi yangu ya kusugua lile eneo.
Nilipoona mate yangu yamekauka kwenye kidole changu,nikaingiza kidogo kidole changu kile kwenye pango lake na kuchota ute ambao tayari ulikuwa umekuja vya kutosha pale kisimani.
Nilipoingiza kidole kile,ilikuwa kama nimemuamsha kitu fulani hivi,kwani kifua chake alikipandisha juu na kilio cha utamu kikaongezeka akiwa palepale kifuani kwangu.
“Baby nataka tena,nataka tena hiyo”.Ni sauti ya Sheila ilikuwa inaninong’oneza sikioni baada ya kutoa kile kidole changu.
Nilitabsamu na kucheka kimoyomoyo baada ya kusikia naitwa baby kwa kamuda kale ka dakika kumi.
Basi kamanda nikafanya kama nilivyoambiwa. Nikaingiza kidole kwenye kile kisima cha burudani ambacho kilikuwa kina utamu kuliko asali.
Safari hii sikuingiza kidogo,nilikiingiza chote na kukitoa haraka nje na kukiingiza tena kwa kasi ileile niliyokitolea nje. Hapo mtoto alianza kulia kama ana wendawazimu au kasikia habari ya msiba. Nilipomuangalia usoni alikuwa kama kadata kabisa,macho kayafumba huku mdomo ukiwa wazi na ulimi ukitoka nje na kuingia ndani kila napotoa kidole na kukiingiza.
Ulimi ule niliutamani kwelikweli,kwa sababu ndio hasa ubovu wangu katika mapenzi. Ninyime vyote lakini ulimi,kamwe usithubutu.
Basi nikaudaka ule ulimi wake uliokuwa unaingia na kutoka nje. Naye kwa utaalamu akupokea wangu na kitendo bila kuuliza akaanza kuenjoy nao huku akigugumia kwa raha ya dole langu la kati huku chini.
INAENDELEA

