LOVE AND SEX
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Sehemu Ya 11
“Weee mtoto lazima nikuue leo lazima nikupasue ukome”samson aliniambia kwa hasira huku akinipiga ngumi mfululizo zingine za masikio kwa Lengo la kutaka niachie ili anipige usoni ambapo nilikuwa nimeziba kwa mikono yangu miwili ili ngumi zake zisinipige usoni.Samson baada ya kuniona naanza kuishiwa nguvu haraka haraka akaninyanyua na kunigeuza nyuma kisha akanipiga robo kali na kunipeleka tena chini huku akiwa amenikaba shingoni kwa kutumia mkono wake ukisaidiwa na mwingine ambayo ilitosha kabisa kuninyong’onyesha kwa maumivu.Ukali wa roba ile ulipelekea nianze kukohoa huku macho yakinianza kunitoka hata nilipotaka kujaribu kumng’ata sikufikia mkono wake uliokuwa shingoni mwangu.
↓
“aaa…aaa….aaaa….u..na..niuaa mw..anaanguu unan..niumizaa b..anaaa yalaaa unaniumizaaa..” Nililamika kwa tabu huku nikiendelea kurusha rusha miguu yangu huku mikono yangu ikiwa juu ya mikono yake shingoni nikijaribu kuitoa hapo shingoni mwangu ambao ndio samson alikuwa kanishikilia kwa nguvu akanikaba na wala hakutaka hata kuniachia.
“Eeeewe utakoma…Nakuuuliza utakoma yani mpaka nikufundishe Adabu f**** wewe” Samson akaongezea huku akiwa amezidisha kabisa kunikaba hakika alionekana kabisa kudhamiria kuniua nilipaparika kama kuku kuitoa mikono yake udenda ulikuwa unanitoka na kumwagikia yeye mikononi mwake lakini wala hakushtuka yeye aliendelea kunishikilia na kukaza mikono yake kwa nguvu za hali ya juu.Ghafla nguvu zikanijia nikaangaika mpaka mdomo wangu ukakaribia karibu na Mkono wangu ambapo bila ya kuchelewa nikamng’ata kwa nguvu na kusababisha samson atoe ukelele wa nguvu wa maumivu na kuniachia kutokana na jinsi nilivyong’ata kwa nguvu na kusababisha Maumivu makali
“Aaaaa Mjinga wee yani unaning’ata” samson akalalama na mimi nikanyanyuka Haraka haraka samson akanivaa tena lakini safari nilimkwepa kwa ufundi kisha nikamkamata na kumsukumiza kwa nguvu ambapo yeye moja kwa moja akaenda kuvaa ukuta na kujigonga kwa Nguvu kichwani na Papo hapo akatulia kimya.
“Heeee nimeuaaaaa!!!”…
jasho jembamba likaanza kunitiririka mwili mzima baada ya kumuona samson amelala chali hata nilipojaribu kumuita alikuwa kimyaa haongei wala kutingishika uoga ulionivaa ulinifanya nishindwe hata kumsogelea kumtingisha niliaanza kutetemka kama mtu anayesikia baridi hakika lilikuwa baridi ambalo na Majasho yalikuwa yanachuruzika mwili mzima.
” Sa…aa..mson br..oo a.mka..” kwa sauti ya chini kama mtu ananisikia vile nikalalama machozi nayo yakaanza kunitiririka hakika nilitamani ile ingekuwa ndoto lakini nilipokuja kuona sio ndoto bali ni kweli hakika nilichoka ndipo nilipozidi kulia na machozi yakanitoka kwa wingi zaidi kilio ambacho hakikuwa na sauti kubwa kilikuwa ni cha kawaida chenye simanzi nzito hakika usifanye masihara kuua bila ya kudhania au kukusudia ni kitu kingine na usiombee hali kama hiyo ikutokee
“Weee kimbiaaa” sauti ya ghafla ikanijia katika kichwa changu ikiniambia nikimbie na hata sikutaka kukataa na kupinga licha ya kuwa nilipotaka kunyanyua mguu kukimbia miguu yangu kukimbia ilikuwa mizito si kawaida ilikuwa kama imewekwa sumaku flani hivi ambayo ilikuwa ikinivuta pale nilipotaka kujaribu kukimbia.Nilimuangalia samson aliyekuwa amelala kwa huzuni kubwa na bila ya kujiuliza nikaanza kukimbia kushuka chini ya jengo lile ya shule ambalo ni ghorofa mbili ndefu zilizojengwa vizuri.Kwa mwendo wa haraka nikaanza kuzishuka ngazi kwa spidi ya hali ya juu lakini ghafla nikajikuta nikiganda kama mtu aliyepigwa shoti ya umeme au sindano ya ghafla hamadi!!!
“Begi langu!!” Nikalikumbuka begi langu nililoliacha darasani wakati na jisomea mimi na samson na lilikuwa kulekule juu ya ghorofa shauri yakutaka kuliacha lilikuwa ngumu kwa sababu atakapokuja kuchukuliwa samson na kutakapofanyiwa uchunguzi na kukutwa begi langu lingekuwa kosa na kukamatwa kwangu.Nikakata shauri ya kurudi juu kwa kasi tena kwa mwendo wa kusua sua mara nijikwae mara nigongane miguu nikafanikiwa kufika na Moja kwa moja nikaelekea katika darasa tulilokuwa tunajisomea Mimi na samson na kuchukua begi langu kisha nikatoka tena haraka haraka kushuka tena huku safari nikiwa siuangalii tena Mwili wa samson aliyekuwa chali pale.
“Kohooo!!!,kohoooo……!!!” kabla hata sijaanza kuzishuka ngazi sauti za mtu kukohoa nikazisikia kabisa kwenye tundu za masikio yangu nakunifanya nigande nigeuke nyuma kwa hofu kuangalia anayekohoa ni nani tena.Macho yakatua kwa samson ambaye alikuwa akikohoa na kuanza kutingishika Jambo ambalo lilinifanya nidondoshe begi langu kwa Mshangao wa furaha ya hali ya juu furaha ambayo ilikuwa imepotea ghafla nakuingia dosari ya hatari.Nikajikuta nikirudi mpaka pale kwa samson nakumuangalia alikuwa akikohoa huku akihema kwa nguvu majasho yakiwa yanamtiririka kama Maji huku akiwa anahema haraka haraka nikavua shati langu la shule na kubaki na vest kisha nikaanza kumpepea kwa kutumia shati langu huku nikiwa siamini kilichotokea Niliona kama miujiza mingine kwa sababu nilihisi samson atakuwa amekufa kutokana na kumsukumiza vibaya ukutani.Nikajikuta nikishusha pumzi za furaha na kumkombatia kwa nguvu sana
“Oooooo vipi broo vipi samson upo fresh kaka??”
“Mmmh vipi pablo nipo wapi aaaa kumbe shule nilizimia eee aaaa ulinisukumiza ukutani” samson akawa anauliza maswali huku akiwa anajijibu mwenyewe huku akiwa ananiangalia mimi ambaye nilikuwa bado nikimpepea huku nikimuangalia yeye.
“Samahani sana samson halikuwa kusudi langu samahani sana”
“Daaah kichwa kinauma balaa hivi pablo kwanini umemchukua halimaa”
“Daa mwanangu nyanyuka tuondoke kaka Tutayaongea vizuri” hakika samson alikuwa anampenda sana halima alikuwa ni chizi kwake jina la halima lilijaa katika daftari lake kutokana na kumpenda bila ya kupoteza muda nikamsaidia samson kunyanyuka kisha haraka haraka nikaenda darasani tena na kumchukulia samson begi lake kisha nikamshika bega huku nikimsaidia na begi lake na kuanza kushuka ngazi za lile jengo.Nikamsindikiza mpaka kituoni na kuhakikisha Mpaka anapanda gari kisha na mimi nikapanda gari la kuelekea nyumbani.Hakika mawazo ndio yaliendelea kuniandama sana nikiwa katika gari na nilipokumbuka vuguvugu lilotokea nyuma nilibaki kumshukuru Mungu huku nikiwa siamini kabisa kuwa samson ni mzima kutokana na Kipigo kile nilichompa.Nilifika nyumbani Na breki yangu ya kwanza ilifikia kwenye simu yangu ya mkononi ambayo nilikuwa nimeizima Nikaiwasha kisha nikaiandika namba ya samson iliyokuwa kichwani na kuipiga haikuita sanaa ikapokelewa.
“Nambie Man pablo” nikajikuta nikishusha pumzi ndefu huku nikitabasamu kwa furaha baada ya kusikia sauti ya Samson ambaye mchana wake nilipigana naye kisa Halima.
“poa sam vipi unaendeleaje kaka??”
“Fresh Mwanangu kichwa kilikuwa kinanisumbua mida flani lakini sasa fresh kaka”
“Aaaaaa daa safi sana vipi sam unapiga msulu nini”
“Kama kawaida pablo lakini nini kaka naomba unisamehe kwa yale yote ya mchana yaliyotokea unajua hasira tu za hapa na pale”
“Aaaa nishakusamehe kaka tena kitambo tu halafu vitu vile vya kawaida chakumshuruku mungu tu tumebaki wazima Maana mwanangu Nilijua umekufa kaka”
“Aaaa mimi jembe siwezi kufa kizembe sasa unajua nini pablo nakuomba uendelee kumueleza Halima jinsi gani ninavyompenda nampenda sana nipo radhi kumpa kila kitu atakachokihitaji katika Maisha” samson aliongea kwa hisia na kuniambia na kunifanya nitulie kimya kidogo na kutathimini kwa kuchekecha ubongo wangu.
“Usijali mwanangu nishaweka vocha sasa hivi namsaundisha”
“Poaa kaka” Nikajikuta nikitikisa kichwa baada ya kusikia maneno ya samson aliyeniambia Kuwa bado niendelee kumshauri halima awe naye.Nilimuonea huruma samson kutokana na jinsi anavyompenda halima ambaye eti alikuwa akinitaka mimi.Nikachukua tena simu yangu nakumpigia halima na kumuambia mkasa mzima uliotokea na kumshauri kuwa awe na samson ndiye mwanaume anayemfaa jambo ambalo halikupita kabisa katika masikio mwa halima na alikataa kata kata.
“Jamani tena ndio nimezidi kumchukia yani anadiriki kukupiga wewe mpenzi wangu yani mwambie simtaki simpendi na sitompenda tena na aondoe kuwa na Mimi katika maisha yake Pablo sikia Mimi nakupenda wewe nitakupa chochote utakachotaka Baby hata ukitaka kusikostahili baby i love you nakupenda sana” Maneno yakamtoka halima na kuzidi kuniudhi na Kunikera na kunivunja Nguvu bila ya kumjibu nikakata simu yake kwa hasira kisha nikajibwaga kitandani na kuanza kufikiria Mchezo unavyokwenda ghafla mlio wa messeji ukalia katika simu yangu na nilipochukua kuangalia na nani tena alikuwa si Mwingine bali ni Samson kwa hofu nikaifungua.
“Nambie kaka vipi ushamwambia mwambie Bana Nampenda sana yani hapa nasoma lakini hata haviingii namuanza yeye tu” Messeji ya samson ikazidi kunichanganya na wala sikumjibu nikakata simu nakutuliaa kitandani.
“Mmmh yani rebecca,dada tuse,rukaiya,zureiya na huyu halimaa kweli kazi ninayo…..”…
. Asubuhi na mapema bila ya kuchelewa siku ya jumatatu nikahamka na kujitayarisha kwenda shule ilikuwa ni siku muhimu mno kwa sababu ilikuwa ni siku ambayo kila mwanafunzi wa kidato cha nne alikuwa akiisubiri kwa hamu na hofu kubwa kwa sababu ilikuwa ni siku ya kupanda mazao tuliyoyanunua na kusubiri kuyapanda kwa kipindi cha miaka minne.Mwanaume nilikuwa nishajiandaa vya kutosha tena bila ya kuogopa nikiwa nimeshika compass langu mkononi lilikuwa na dhana zote kama pen,penseli na mambo kibao.Nikaingia shuleni na moja kwa moja nikaanza kumtafuta Samson rafiki yangu ambaye siku mbili za nyuma tulikwaruzana kisa mwanamke ambaye alikuwa ananitaka mimi lakini mimi nilikuwa simuhitaji lakini mdomo wangu ulikuwa mzito sana kumwambia kutokana na kuogopa kumuumiza.Nilikutana na Samson ambaye alifurahia sana kuniona akiwa na washikaji wengine ambao nao baada ya kuniona wakaishia kunipa hai tu ‘’Inakuaje Samson mambo vipi umejiaandaaje na mtihani mshikaji’’ ‘’daa fresh tu Pablo kazi kazi oya vipi mwanangu uliiongea na Halima roho yangu maana nampenda sana’’samson akinichomekea ya Halima jambo ambalo lilianza kunikera lakini sikutaka kumuonyesha zaidi ya kutabasamu tu na kumpa moyo Samson ambaye alifurahi baada ya kumuambia Halima anamfikiria kwa mara ya pili.baada ya kuonana na Samson mwanaume nikaanza kuzunguka zunguka tu shuleni nikisubiri muda muafaka ufike ghafla nikiwa katika mizunguko yangu pale pale shuleni nikaasikia naitwa na nilipoangalia nani ananiita alikuwa si mwingine bali ni Halima alikuwa ndani ya tabasamu pana baada ya kuniona mimi sikutaka wala kumfuata mwanaume nikajifanya kama simuoni na kuondoka na kumuacha huku akiwa na mshangao wa hali ya juu.Kengele ikagongwa kuashiria mtihani ulikuwa tayari kufanya na sikuwa na budi kuelekea katika mistarini tuliyoelekezwa kwa lengo la kwenda kupewa maelekezo ya hapa na pale na kukumbushiwa sharia za mtihani ambayo tayari tulikuwa tunazijua sema mwalimu mkuu msamamizi wa mitihani alikuwa akitukumbushia.Ilipotimia saa mbili kamili tukaingia katika vyumba vyetu vya kufanyia mitihani hali iliyosababisha presha kupanda na kushuka kwa muda huo kila mtu alikuwa kimya kuwaza na kuwazua je mitihani itakuwa migumu kama walimu walivyokuwa wakituhusia kuwa mitihani ya mwisho ya kidato cha nne si lele mama kama wanafunzi wengi wanavyotegemea.siku zikasogea kwa kasi sana mitihani ilikuwa migumu hatari na hatimaye tukamaliza yote na kufanya hadi practical kwa sisi tuliokuwa tunachukua sayansi.kila mtu alikuwa na furaha na huzuni katika siku hiyo ilikuwa ni siku ya kuagana kwa sisi wanafunzi na hata walimu ilikuwa ni siku ya graduation ambayo shuleni hapo tuliamua kufanya baada ya kumaliza mitihani ili tuagane vizuri kila mtu alikuwa na furaha yebye majonzi ya hapa na pale kwa sababu tulikuwa tumezoeana sana sema ilikuwa graduation ambayo ilikuwa ni wanafunzi tu wazazi hawakualikwa kutokana na mambo flani ya kifedha ambayo ilikumba shuleni wakiwa na lengo la kuboresha Maabara yetu ya shule.wanafunzi tulikusanyika na kuanza kupewa husia na maelekezo ya kukabiliana na maisha ya mtaani huku kila mwalimu alikuwa akiisisitizia kutokana na vijana wengi wakati huu walikuwa weni wavuta bangi na wakabaji hali iliyosababisha wengi wao kuuliwa na wananchi wenye hasira kali na wengine hata kukamatwa na mapolisi ulikuwa ni wosia uliomgusa kila mwanafunzi aliyekuwa
akiisikiliza.Baada ya kuhitimisha graduation hiyo iliyokuwa fupi wanafunzi wote tukaruhusiwa kuondoka huku tukipewa na wosia wengine kwamba tusisahau kwenda kusalimia shule.Siku hiyo Samson alikuwa hajaja shuleni na sikujua sababu ya kutokuja kwake shuleni mwanaume nilikuwa mpweke na kuagana na wengine na kubadilishana namba za simu kama wengine wanavyofanyaga ‘’PABLOOOOOOOOOOOOOOOO’’Ghafla nikasikia jina langu likiitwa na kusababisha nisimame na kugeuka nyuma kuangalia nani aliyekuwa akiniita Macho yangu yakakutana na halima aliyekuwa amependeza sana kwa nguo zake alizokuwa amevaa na kuonyesha umbo lake maridhawa lenye shepu nzuri na nene yenye kumvutia kila mwanaume aliyekuwa akimpitia karibu hakika alionekana mrembo hasa na si kama mwanafunzi alionekana mdada mwenye kazi zake aliponifikia karibu bila ya haya akanikombatia mbele ya wanafunzi wengine waliokuwa nao wanaondoka na kusababisha minong’ono flani kuanza kutokea na kusababisha mimi nimtoe haraka ‘’vipi sasa mbona ulikuwa unataka kuondoka bila hata ya kunishtua jamani au umesahau’’ ‘’hamna nimekutafuta sana sijakuona leo sasa unasemaje’’ ‘’Jamani baby ilo ya kuuliza tena twende gesti tu ukanipe kitu roho inataka roho inapenda baby’’ ‘’oooooooo basi twende me sina maneno’’bila ya uoga nikamshika kiuno Halima na moja kwa moja tukatoka shuleni na kuanza kushaka gesti ya kwenda kubanjuka mimi na halima ambaye alikuwa anamchukia sana rafiki yangu Samson bila ya sababu za msingi.safari yetu ikagota barabarani ambapo tulikuwa tukisubiri gari la kuelekea mitaa ya maeneo ya kwetu ambayo ndio nilimwambia kulikuwa na gesti nyingi zenye utulivu mkubwa na tunaweza kuenjoi kwa raha.nikiwa pale barabarani Halima akaona baiskeli ya mtu anayeuza koni na kutokana na kupenda akaniaga anakwenda kununua na mimi nikamruhusu akaenda huku nikiwa na msindikiza kwa macho kisha akanunua na kugeuka nyuma na kuanza kurudi huku akiniangalia kwa furaha iliyojaa kifani.ghafla bila ya hata ya kutegemea nikakumbatiwa na mtu nisiyemfahamu kwanza alinikombatia ghafla bini vuu na kusababisha hofu unitande nilipojaribu kutaka kumtoa akanizidi nguvu na kupeleka mdomo wake kwangu na kuanza kuninyonya denda mbele ya watu pale kituoni barabarani.nikatumia uanaume wangu kumsukumiza kwa nguvu ambapo alisukumizika lakini macho yangu yakatua moja kwa moja kwa rukaiya dada yake zureiya na kusababisha roho ianze kudunda ghafla kwa sababu rukaiya anafahimika vizuri sana na Halima ambaye shoga yake ni zureiya ‘’vipi wewe unaogopa nini baby??’’ Maneno yakamtoka rukaiya na kuniambia mimi niliyekuwa natetemeka kwa uoga wa halii ya juu ‘’Heeeeee makubwa rukaiya hadi weewee unamzunguka mdogo wako??’’ kwa nguvu Halima akayatamka maneno yaliyomshtua sana rukaiya ambaye alipogeuka naye akashtuka na kupigwa na butwaa baada ya kumuona Halima aliyekuwa ameshika koni ambazo akazidondosha kutokana na kitu alichokiona machozi yakaanza kumtiririka na bila ya kuangalia Halima akaingia barabarani akiwa na hasira na majonzi ya hali ya juu ‘’PAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA!!!!!!!!????’’……
‘’maaaaamaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!’’ ukulele wa nguvu ukasikika pale barabarani yakiambatana na mlio mkubwa wa gari ambayo iliyokuwa imefunga breki.macho yangu yakanitoka roho ikaanza kudunda hakika macho yangu hayakutaka kabisa kushuhudia kile nilichokiona.maneno ya malalamika yakamtoka Halima baada ya kugongwa na gari ambalo baada ya kumgonga halikuondoka lakini kugongwa huko kulisababisha Halima arushwe mbali sana na alipotua alibaki kimya palepale damu zikaanza kusambaa barabarani.akili ikaniruka haraka na mimi bila ya kuchelewa nikajikuta nikikimbilia na mimi barabarani pale alipogongwa Halima ambapo na watu nao walikuwa tayari washajikusanya wakimsaidia Halima ambaye alikuwa hajitambua damu zikiendelea kumvuja kichwani.kelele zikaanza kushamiri na kila mtu akaanza kuongea lake.
‘’nani anayemjuaa huyuuu??’’ mara nikasikia sauti ya mmoja akisema vile na bila ya kuchelewa nikaitikia na kupenya kwa watu ambao walinipisha baada ya kunisikia mimi namjua.
‘’weee nani yake.’’
‘’eeeeee mimi ni mwanafunzi wenzake’’
‘’anhaaa basi panda gari twende hospitali haraka halafu tutajua cha kufanya.’’ilikuwa ni sauti ya dereva ambaye alikuwa na wasiwasi huku naye akiwa analowa jasho akiwa na wasiwasi wa kuua.haraka haraka katika lile lile gari tukapanda mimi na mwananchi mmoja ambaye alikuwa kipaumbele kumpakiza Halima katika lile gari haraka haraka tukapanda lile gari na kukaa siti ya nyuma tukiwa tumempakata Halima aliyekuwa hajitambui.mwanaume nikajikuta nikianza kutoa machozi huku nikiwa nimemshikilia Halima maeneno ya miguuni na mwingine akimshika maeneo ya maeneo ya kichwani ambapo alikuwa anavuja damu nyingi zilizokuwa zinaendelea kumtoka na kuchuruzika ndani ya mule mule katika gari.haikuchukua hata muda mwini tukafika hospitali na kupokelewa na madaktari ambapo walimchukua Halima haraka haraka na kuingia naye katika chumba maalumu na kutuacha tukiwa bado tupo nje ya chumba alichoingizwa Halima.ghafla tukiwa bado katika kusuburia nikajikuta nikitumbua macho yangu baada ya kushuhudia ugeni mkubwa ukiiingia hapo ugeni uliokusanya mama yake Halima akiwepo rukaiya,zureiya ambao wote walikuwepo na kusababisha mwanaume niinamie chini huku wasiwasi ukiniingia sana na hadi kujikuta nikitetemeka kama mtu aliyemwagia na maji ya baridi huku akiwa amevaa nguo tena ikiwa asubuhi.
‘’uwiiiiiiii jamani mwanangu yupo wapiiiiii amekufaaa au yupo wapiiii uwiiii mwanangu wa pekeee mimiii’’maneno yakamtoka mama Halima baada ya kufika pale tulipokuwepo na kusababisha madaktari waanze kumtuliza na kumuambia atulie kwa kumbembeleza kwa maneno ya kutulia yaliyosababisha nay eye kutulia huku akiendelea kulia chini chini.macho ya zureiya na rukaiya yalikuwa yananitazama huku kila mmoja akiwa ananiangalia mimi kwa kuibia ibia na hata mimi nilikuwa nawaangalia kwa macho ya kuibia na kuwapotexea kiaina kama siwajui vile.tukiwa wote tumetulia ghafla madaktari waliokuwepo katika chumba alichoingizwa Halima wakatoka ghafla na kusababisha sisi wote kunyanyuka na kuwavaa.
‘’jamani mwanangu anaendeleaje’’mama Halima huku akiwa na jazba nzito akauliza huku machozi yakiendelea kumtiririka na kuzidisha huzuni itawale kwa kila mmoja aliyekuwepo pale.
‘’mama binti yako amepoteza damu nyingi sanaa kichwani kwa hiyo tumemuwekea damu safi na mpaka sasa hali yake ni mbaya na mpaka dakika hii wala hajarudiwa na fahamu zake kilichobakia ni kumuomba mungu na kusali ili Mwenyezimungu aweze kumsaidia ninachopenda kuwambia tu wengine mnaweza mkarudi nyumbani wabaki wana ndugu tu na Yule aliyemgonga abakie hapa’’maneno ya daktari yalisikika vizuri tu katika masikio ya kila mmoja aliyekuwepo pale.sikuwa na budi la kukaa tena taratibu nikanyanyuka zangu nakuanza kutoka na hakuna hata aliyeshangazwa na hali ile.
Sehemu Ya 12
‘’paablo nisubiri’’sauti nyororo ya zureiya mwaname niliyekuwa nampenda kweli ikasikika vizri katika masikio yangu sikuwa na budi la kusimama niliendelea kutembea sikutaka kusimama niliona majanga onyo kutoka kwa dada yake lilinipitia kichwani mwangu na hata vitendo alivyonifanyia rukaiya na kupelekea mpaka Halima kugongwa na gari viliendelea kunitesa katika kichwa changu.zureiya akanikaribia na kunisamamisha kwa kunishika macho yake maregevu aliyokuwa ananiangalia macho yaliyokuwa na machozi yal;itosha kabisa kuniregeza huruma ukaniingia nilipomuangalia zureiya na taratibu nikajikuta nikinyanyua mikonono yangu nakuanza kumfuta machozi yaliyokuwa yakimtiririka.
‘’pabloo umekuaje siku hizi simu zangu haupokei,messeji zangu hauzijibu,tulipanga tuonane lakini nilipokuwa nakupigia simu ulikuwa unakata Pablo nimefanyaje tatizo liko wapi niambie nambie sasa bado haujanisamehe lile kosa nililokufanyia please naomba unisamehe unautesa moyo wangu Pablo.kumbuka nilishakupa penzi langu nakukukabidhi moyo wangu kwanini sasa umeamua kunitesa namna hiii??’’maneno yakamtoka zureiya huku akiwa analia na kuzidi kunitia simanzi ya moyo wangu na kubaki nikimuangalia kwa macho ya huruma sana.
‘’zureiya sio mahala pake kuzungumza mambo kama haya unajua kabisa umekuja kumuangalia rafiki yako Halima please tutaongea kwenye simu’’
‘’jamani kwenye simu nikikupigia haupokei unakata tutaongea saa ngapi kwa nini unanitesa’’
‘’sikia nisikilize leo nitakupigia tuongee umwenisikia hapa nilipo akili yangu imechoka niache nikapumzike’’
‘’poaa bana Pablo ila naomba unibusu unikumbushie zamani najua kuna watu lakini busu lako litathibitisha kwamba unanipenda please naomba unibusu’’nikamsika vizuri uso wake zureiya ambaye baada ya kumsika vile na kusababisha zureiya afumbe macho tayari kabisa nimbus taratibu nikataka nipeleke mdomo wangu kumbusu nikajikuta nikisita na kujikuta nikigeuka nyuma baada ya kuhisi kitu.macho yangu yakagongana na rukaiya dada yake halali wa tumbo moja zureiya ambaye baada ya kukutana naye macho kwa macho akaninyooshea kidole cha onyo kilichopelekea nimuachie zureiya bila ya kumbusu na nilipomuachia rukaiya haraka akaondoka pale na kurudi alipotokea kisha na mimi nikaanza kuondoka na kuendeleaa na safari yangu na kumuacha zureiya katika hali ya mshangao huku akiwa analia baada ya kuona mimi nikimfanyia vile jambo ambalo kwake niliona kabisa lilikuwa linamuuma kutokana na kutotegemea mimi kumfanyia vile.mwanaume nikatoka hospitali huku nikiwa na mawazo mengi kichwani yaliyokuwa yakinisumbua kichwa cha nguvu na kwenda kupanda gari la kuelekea nyumbani ambapo kwa bahati nzuri nikapata gari papohapo ambalo kutokana na kutokuwa na foleni haraka likanifikisha mahala nilipokuwa napataka na haraka nikashuka nakuelekea nyumbani huku nikiwa bado na mawazo ambayo yalisababisha hadi kichwa kizidi kuniuma.nikafika nyumbani na kuingia kwa kufungua mlango wa kuingia ndani lakini ghafla bila ya kutegemea ghafla nikakumbatiwa na msichana ambaye sikumjua mpaka nilipomsukumiza na kusababisha nishushe pumzi na kujitahidi kutabasamu baada ya macho yangu kukutana na mwanamke ambaye nilishawai kufanya naye mapenzi kwao na tukafumwa na dada yao wa kazi ambaye naye alikuwa anataka naye penzi alikua si mwingine bali ni Rebecca.
‘’rebecca vipi mambo??”
‘’Poa tu mzima mpenzi nimekuja baby kuja kukuona pia nije nikuambie pia nina mimba yako.’’
‘’heeeeeee mimba???”………
Nikajikuta nikitumbua macho kwa mshangao na hofu kubwa baada ya kusikia maneno ya Rebecca akisema eti ana mimba yangu.majasho yakaanza kunichuruzika taratibu nikajisogeza mpaka katika kochi na kukaa chini na kutulia kidogo.
‘’rebecca sijakuelewa unasema una nini??’’
‘’jamani Pablo hujanielewa nimekuambia nina mimba yako’’
‘’wewe unaumwa nini hiyo mimba yangu yako.??’’
‘’heee jamani Pablo si wewe ndio umenipa kwa leo hii ushasahau kama mimi na wewe tulifanya mapenzi nyumbani kwetu??’’
‘’sasa ndio mara moja tu uwe na mimba hii mimba sio yangu kwanza mimi bado sina uwezo wa kukupa mimba mimi bado mtoto’’nikajikuta nikisema vile na kusababisha kuzidi kumshangaza Rebecca ambaye akanisogelea karibu lakini aliponifikia mimi nikahamia pembeni kwa hasira ya hali ya juu.
‘’pablo jamani hii mimba ni yako baby.’’
‘’sasa utapataje mimba na sisi tulifanya mapenzi kwa siku moja tu yaani na hata hatukumaliza raundi nyie wanawake wahuni saana mimi naona hiyo mimba sio yangu’’nikajikuta nikilalama na kusababisha Rebecca aanze kulia baada ya mimi kumuambia maneno yale.
‘’sasa Pablo hii mimba mimi nikaitoe.’’rebecca akaniambia huku mikono yake akishika tumbo yake na kuniangalia mimi huku akidondosha machozi yalionisababisha nianze kumuone huruma.nikajikuta nikinyanyuka na kumsogelea karibu kisha nikamfuta yale machozi yake yaliyokuwa yakimbubujika kwa wingi.
‘’sikia Rebecca nikuambie usiitoe mimba ni dhambi kwa mungu ujue.’’nilimuambia Rebecca kwa unyonge lakini nikashangaa kumuona ana tabasamu kwa furaha jambo ambalo lilianza kunishangaza na kubaki nikimuangalia.
‘’hahahhaa kumbe unanipenda eeee sina mimba bana baby’’nikajikuta nikishusha pumzi baada ya kusikia rebbeca akaniambia kuwa hana mimba nikajikuta na mimi nikicheka na kumuangalia Rebecca ambaye naye alikuwa kashabadilisha macho sasa alikuwa akiniangalia kwa macho ya kimahaba akiniangalia kwa macho ya mtu anayehitaji kitu Fulani.
‘’baby mama yangu na mama yako wametoka nilikuja hapa na mama wameenda kwenye biashara zao baby naomba tuitumie hii nafasi adimu ya kipekee mimi na wewe tufanye yetu.’’kabla hata sijaanza kutaka kumjibu Rebecca akanivamia kwa pupa na mdomo wake akapeleka katika papi za mdomo wangu na mimi sikuwa na budi ya kuukataa nikaupokea taratibu nakuanza kunyonyana naye denda haraka haraka huku mikono yangu ikaanza kumpapasa papasa sehemu nyeti tofauti zilizoanza kumpagawisha taratibu Rebecca ambaye naye akaanza kuhema kwa kasi ya ajabu.kama kawaida yake presha ilipoongezeka akanivua t-shirt yangu niliyovaa kimahaba huku mimi nikiwa nampapasa katika mapaja yake meupe yasiyokuwa hata na mchubuko huku mkono wangu mwingine ukiwa unatalii katika kifua chake kilichobeba nido nzuri sana za kuvutia na kusababisha nizide kupagawa na kumpagawisha Rebecca ambaye tayari alionekana kulainika na mimi nilishaanza kukolea.ghafla tukiwa katika presha milio ya hatua za viatu vikasikika haraka haraka nikajikuta nikimsukumiza Rebecca na mimi nikachukua shati yangu haraka na kuvaa ile namaliza kuvaa tu macho yangu yakatua kwa mama Rebecca na mama yangu ambao wote walishangazwa kidogo na jinsi hali ilivyokuwa na kuwa na shauku ya kutaka kujua kumetokea nini.
‘’nyiee watoto vipi Rebecca kuna nini mbona mpo kimya sana Pablo haujambo.’’
‘’aaaa nani mimi n…a….a sijambo mama shikamooni’’
‘’marhaba mwanangu mpo kimya sana vipi.’’
‘’hamna bana maa tulikuwa tunapiga story za mitihani sasa Pablo kuna swali flani hizi tulikuwa tunalifikiria lipi lilikuwa gumu katika somo la mathematics.’’rebecca akatunga uongo ambao hata mimi niliupenda maana ndio ulisababisha mama zetu wote wakae pale na kuanza kutuuliza uliza maswali ya hapa na pale kuhusu mitihani ilivyokuwa nani changamoto zipi tulizokutana nazo.hakika mama Rebecca na mwanae walikaa sana siku hiyo na kuondoka majira ya jioni na mimi na mama tukawasindikiza mpaka katika kituoni ambapo walipanda gari na kuondoka nyumbani kwao.tuliporudi nyumbani ilinibidi nimueleze mama ajali ya Halima ilivyotokea huku nikimuambia wakati tulipotoka shule ndio hali ile ikatokea.hakika hata yeye akasikitika na kunipa pole mimi na mimi nikamchomekea kuwa nitakuwa naenda kumuangalia kwa sababu shule kwa wakati huo tulikuwa tushamaliza kidato cha nne na pili yeye aliniambia nipumzike kwa mwezi mmoja na nusu kisha ndipo atakaponipa pesa ya kwenda kujisomea computer kama miongoni mwa wanafunzi wengi tunavyofanyaga.kama kawaida siku hiyo ikapita na kesho yake mishale ya tatu nilikuwa nishajiandaa kwenda kumuona Halima ambaye kwa siku hiyo nilikuwa nikiambatana na rafiki yangu Samson rafiki ambaye alikuwa naye akimpenda sana Halima na kupata ajali kwa Halima kulimuumiza sana na kujikuta wakati nilipokuwa naongea naye kwenye simu jana yake usiku alikuwa akilia kabisa kutokana na mapenzi aliyokuwa nayo kwa msichana huyo.hakika wala sikuchelewa sana kufika katika hospitali aliyolazwa Halima lakini nilipofika nilikuta muda muafaka wa kuangalia wagonjwa ulikuwa ushafika na mimi sikuwa na budi nikaingia na moja kwa moja nikaelekea katika wodi aliyelazwa Halima ambapo baada ya kufika nikakaribishwa na watu wengi sana ambao wengine walikuwa ndugu zake,mashoiga zake wa shule hadi na walimu akiambatana Samson ambayde alikaa karibu na rukaiya dada yake zureiya aliyekuja huku nilipomuangalia zureiya sikupata kuona sura yake ikiashiria alikuwa hajafika siku hiyo.mwanaume nikaenda kuwasalimia wote pale waliokuwepo kisha nikamuangalia Halima ambaye alikuwa haongei lakini alikuwa akiwaangalia watu kisha sikukaa sana nikadanganya kuna sehemu nilikuwa nimetumwa ambapo wote wakaniruhusu na mimi haraka nikaondoka pale akifatiwa na rukaiya ambaye baada ya kuniona mimi nimeaga naye akazuga anaaga na kunifuata mimi baada ya kunifikia karibu bila aibu akanikombatia mbele ya macho ya watu hospitalini jambo ambalo lilisababisha baadhi ya watu kuniangalia kwa shauku kubwa na wengine wakichukulia kawaida.
‘’jana ulinifurahisha ulivyokaata kumbusu zureaiya pale nilijisikia raha sana’’
‘’anhaaa lakini si mdogo wako Yule mbona haumpendi ??’’
‘’walaaa sio kama simpendi sema yeye bado michezo hii mikubwa aniachie mimi dada yake.’’
‘’bado vipi sasa wakati anajua kila kitu Yule.’’
‘’bwana tuachane na bwege huyo sasa sikia mimi na wewe hapa mguu wako mguu wangu ukanipe haki yangu uliyonipa siku zile jamani nina hamu na wewe mimi wee acha tu baby.’’
‘’hata mii pia twende’’hakika penzi la rukaiya lilikuwa lishanikolea kwa namna moja ama nyingine na nilikuwa siwezi kabisa kuliepuka taratibu tukaagiza taxi ambayo mlipaji alikuwa ni rukaiya na tulipoingia tu ndani ya taxi hiyo Yule mwenye taxi akatuuliza tunaelekea wapi rukaiya akamtajia sehemu ya hoteli kubwa na kujikuta mwanaume nikifurahi kwa sababu nilikuwa nazidi kuzijua sehemu nyingi baada tu ya kuwa na rukaiya ambaye alikuwa akimpiku mdogo wake ambaye mara ya kwanza nilikuwa naye mimi kwa msaada mkubwa wa Halima ambaye naye alikuwa akinihitaji mimi tena akiwa kasahau alivyokubali kunionganishia mimi na zureiya……………………………
Sehemu Ya 13
Safari yetu ikagota katika jengo kubwa ambapo sisi tulishuka na rukaiya akamkabidihi pesa yake Yule dereva kisha taratibu huku tukiwa tumeshikana kimahaba mimi na rukaiya tukaingia ndani ya hoteli ile ambayo ilikuwa na madhara mazuri mno haswa ya kuvutia yenye kumpendezesha kila mtu atakapo angalia .baada ya kuingia ndani ya ile hoteli tukapokelewa pale mapokezi ambapo rukaiya akamaliza kila kitu kisha akapewa funguo na kuelekezwa mahali ambapo ilitaki tuende kutokana na malipo ya pesa yetu tuliyotoa.kwa mwendo wa kama dakika nane tukafika mahala usiku na sote tukaingia ndani ya chumba ambacho kilikuwa na kila kitu kikiambatana hadi na choo.mwanaume haraka haraka nikavua nguo zangu na kubaki na nguo ya ndani tu kibukta kisha nikazama chooni nakuanza kuogo bomba la mvua lilikuwepo ndani ya choo kile ambacho kilikuwa kimesheni vitu vizuri vya thamani vya kuvutia.nikiwa katika hali ya kuogo pale bafuni ghafla nikaanza kusikia msisimko mkubwa baada ya rukaiya kuingia na moja kwa moja akanikombatia kisha akazungusha mkono wake wa kulia kupitia katika kiuno changu na kuishika karoti yangu taratibu ikaanza kuinuka kwa kasi ya ajabu na kujikuta mwanaume nikianza kutoa miguno hafifu ya kimahaba kutokana na jinsi ya rukaiya alivyokuwa ananichua karoti yangu ambayo ilizidisha kasi ya kutuna kutokana na hali ile kuzidi kunipagawisha kabisa.mwanaume sikukaa bure tu nikamgeuza rukaiya na kumuweka mbele yangu na kuanza kumvua sidiria yake huku tukinyonyana wote ndimi kwa pamoja kisha baada ya kumaliza kumvua nikamvua na nguo yake ya ndani na kwa pupa nikaanza kuichezea ikulu yake kwa kuisigua kwa kasi iliyosababisha naye rukaiya aanze kutoa miguno ya mahaba huku akinisifia kwa jinsi nilivyokuwa nikimpagawisha.
‘oooo……….aaaaaaa assssss…..oooo ba…by ….jamani tuoge kwanza.’’maneno ya shida yakamtoka rukaiya ambaye alionekana kama kuzidiwa kwa jinsi nilivyokuwa nikiendelea kumpa mambo adimu yaliyokuwa yakimpagawisha sana.maneno yake nikayatii nikamuachia nakuanza kuoga haraka baada ya rukaiya kuzidi kunitega kwa staili yake ya mara anapaka sabuni mguuni kwa kuinama na kuzidisha maumivu yazidi kuongezeka katika karoti yangu.baada ya kumaliza kuoga haraka mwanaume nikambeba rukaiya moja kwa moja na kwenda kumbwaga kitandani ambapo yeye alipenda hali ile kisha mimi taratibu nikapanda kitandani na kumvaa rukaiya kwa kuanza kumnyonya kila sehemu ya mwili wake kisha kabla hata sijamalizia rukaiya akanyanyuka na kunilaza chali kisha akaniwekea mto kichwani mwangu kisha taratibu akainama na kuanza kuinyonya karoti yangu kama mwanamke anayekula ndizi na kunisababisha nijisike raha ambazo sikuwai kuzisikia utamu ukazidi kuongezeka hadi kusababisha mwanaume kuhema kama simba vile baada ya kuridhikak kunyonya karoti yangu rukaiya akanyanyuka na hata mimi nilipotaka kunyanyuka akanizuia na kunibakisha mimi nikiwa palepale huku nikiwa nimelalia mto.
‘’leeo nataka nikuonyeshe mambo baby hakika hotu juta kuwa na mimi.’’maneno yakimaha yakamtoka rukaiya huku akipanua miguu yake na kunisogelea karibu kisha taratibu akakamata mkono wake na kushika karoti yangu na kuisogeza katika ikulu yake kisha mwenyewe akaikalia na kusababisha nigune kidogo kisha akaanza kukalia na kufanya mfumo wakukaa na kuinuka akikaa kisha anainuka tena.hakika rukaiya siku ile alitaka kunionyesha baada ya kuanza kuzungusha nyonga kwa kuikatika karoti yangu na kuzidi kunipagawisha nakujikuta nikipagawa kabisa na kwa muda ule sikuwa na ujanja kabisa utamu wa pale niliokuwa nikiusikia nilikuwa sijawai kuusikia sehemu hata mara moja.rukaiya aliamua hakika kunionyesha kuwa yeye alikuwa vizuri sana katika sekta ile.hakika baada ya kuridhika akainuka tena lakini nilipotaka na mimi kuinuka nikazuiliwa tena kisha rukaiya akageuka na kunipa mgongo nikiwa kisha akachuchumaa kwa kuishika karoti yangu tena na kuipeleka katika ikulu yake ambapo alikuwa akiinuka tena kisha anasimama huku akizungusha kiuno chake laini kwa nguvu zote
na kusababisha mwanaume nisiwe na kazi nyingi zaidi ya kushika kivhwa changu na kusikiliza utamu ulikuwa ukija na kuingia.baada ya kufanya vile rukaiya nguvu zikaanza kuishia na mimi haraka nikamtoa nakumlaza chali yeye kwa kumuwekea na mtu katika kisogo cha kichwa chake kisha nikakamata mguu wake na kuupeleka mpaka katika bega langu na mwingine nikiuvuta kidogo kisha nikapeleka karoti yangu katika ikulu nakuanza kuwasha moto kwa spidi ya hali ya juu uliyomuacha hoi rukaiya ambaye akaanza kutoa miguno ya mahaba kwa nguvu kutokana na raha ambazo zilizidi kifani baada ya mimi kumpa haki yake ambayo alikuwa mwenyewe akiililia kwa muda wa kipindi kirefu kidogo.mwanaume sikutaka kufanya utani kabisa hata rukaiya alivyolalama eti nipunguze nifanye taratibu niliona kama alikuwa akinipigia kelele kwa kuniambia niongeze na mimi sikuwa na huruma nikawa naendelea kumpa haki yake kwa nguvu na haraka sana bila ya kuchoka.niliporidhika na mkao ule taratibu nikainama chini mpaka nikawa naangalia na ikulu yake kisha nikaanza kuinyonya kidogo kisha nikamuinua rukaiya na kumgeuza na kumuweka mkao wa staili ya kama mbwa na kuanza kumsugua tena kwa kasi iliyosababisha rukaiya mtoto wa kiarabu kuanza kuomba maji.baada ya purukushani ndefu tukafika roundi ya kwanza ambayo licha ya uchovu ulioanza kujitokeza kuonekana lakini hakuna aliyetaka kusimama wala kulala mwanaume nikaendelea kumpa dozi yke.bahati ya purukushani za hapa na pale katika mtanange usikuwa na referee wote tukajikuta tukipitiwa na usingizi mzito sana ambao ulisababisha tuchukue muda mrefu kidogo.nilikuja kushtuka baadae kidogo baada ya kuota ndoto mbaya sana iliyopelekea nishtuke kwa kupiga mekelele yaliomshtua sana rukaiya ambaye baada ya kushtuka kule akaanza kunifuta futa majasho yaliokuwa yanazidi kunitoka.
‘’jamani baby kuna nini umefanyaje.??’’yalikuwa maneno ya rukaiya yalionichanganya na haraka nikanyanyuka na kwenda mpaka katika mfuko wangu wa suruali ilikuwa chini kisha nikatoa simu yangu ya mkononi nakuisha na kukuta kuna messeji mbili.haraka haraka nikaifungua moja nakujikuta nikitumbua macho kwa wasiwasi.
‘’NATUMAINI WEWE NI PABLO DANIEL NAPENDA KUKUTAARIFU KUWA MWANAFUNZI MWENZAKO SAMSON HATUNAYE TENA DUNIANI’’ Nikajikuta nikipata mawenge na kizunguzungu baada ya kusoma messeji ile ambayo ilinichanganya na kuona kwamba ilikuwa imekosewa labda Halima ndio amekufa kutokana na kupata ajali na si rafiki yangu.haraka haraka bila ya kujishauri nikavaa haraka na kutoka nje nikifuatiwa na rukaiya ambaye hakuwa na lolote la zaidi la kusema.tulipotoka nje ya ile hoteli tukaanza kutafuta taxi huku mimi nikiwa bado nimechanganyikiwa machozi yananilengalenga.
‘’vipii Pablo mara ya pili hii tunakuja unakuwa na hali hii una matatizo gani??’’ yalikuwa maneno ya rukaiya.ghafla rukaiya akanikombatia huku akiwa ananiuliza maswali kadha wa kadha lakini ghafla macho yangu yakakutana uso kwa uso nay a Rebecca ambaye………………
Taratibu Rebecca akaanza kutosegelea na kusababisha mwanaume niwe na tetemeke hali iliyosababisha hata rukaiya kushangaa taratibu nikamtoa rukaiya pale kifuani na kusababisha aanze kushangaa hali iliyosababisha pia ageuke nyuma kuangalia sehemu niliyokuwa naangalia.
‘’wee vipi’’rukaiya akaniuliza lakini sikuwa na jibu la kumpa kwa wakati huo nikabaki nikimuangalia Rebecca kwa shauku kubwa ya kutaka kujua kama akifika pale atasema nini na itakuaje.baada ya kufika pale Rebecca akabaki akituangalia kwa umakini na kuzidi kumstaajabisha rukaiya ambaye akageuka naye na kumuangalia Rebecca aliyekuwa ameshika kiuno chake akiwa amebebetua mdomo wake kwa hasira kali huku machozi yakitaka kumlenga mikono yake ilikuwa imekunja ngumi hakika ilikuwa balaa juu ya balaa.
‘’pablooo huyu nani??’’rebecca akavunja ukimya kwa kuuliza swali ambalo halikupata jibu kutoka kwangu kwa sababu nilikuwa kimya nikikodoa macho kumuangalia yeye.
‘’weee unaliza kama nani sasa??’’rukaiya akavunja naye ukimya swali nililotaka kujibu mimi akalijibu yeye kwa kuuliza swali lingine lilisababisha Rebecca acheke kicheko cha nguvu kikejeri.
‘’siongei na mbwa naongea na mwenye mbwa umenisikia wewe kikaragosi.’’
‘’weee ishia hapo hapo nani mbwa hivi unavyoojiona unaweza kufikia uzuri wangu wewe eeee unaweza Malaya wewe.’’
‘’haaaa ushie hapo hapo hebu Pablo mwambie mimi ni nani Pablo mwambie nyang’au wako mimi ni nani??’’katika hali nisio itegemea ghafla Rebecca na rukaiya wakaanza kurushiana maneno ya nguoni yaliosababisha kiwe kivutio kwa watu waliokuwa wakipita sehemu ile licha ya kuwa na watu wachache lakini kila aliyepita na kusikia hali ile alikuwa akisimama kuangalia kinachoendelea na nini kiliku wa kisababishi cha hali ile kutokea.
‘’hebu jamani wee Rebecca na rukaiya hebu acheni kutukanana kumbukeni nyie ni watu wazima sasa mnataka kujaza watu hapa.’’mwanaume nikajikuta nikitumia uanaume wangu kuwaambia kwa sauti ya kupaza na kibesi lakini hakuna lilisaidia na hakuna hata mmoja aliyetumia masikio yake kunisikiliza.katika hali nisiyoitegemea ghafla rukaiya akamsogelea karibu kabisa Rebecca.
‘’weee mbwa tu halooo kwa uzuri gani wakujifananisha na mimi wewe.’’
‘’PAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA’’ Nikajikuta nikitoa macho baada ya kusikia kibao kikali kutoka kwa rukaiya kwenda kwa Rebecca ambaye kibao hicho kilimpata barabara katika paji la uso wake na kusababisha nibaki nikitumbua macho kwa kutoa amini nilichokiona.hakika kile kibao kilimuingia barabara Rebecca ambaye akainama chini huku akilia na kulalamika kibao kile kwa maumivu ya hali ya juu.lakini ghafla Rebecca bila ya kuuliza akanyanyuka na konde kali sana lililoenda moja kwa moja katika uso wa rukaiya ambaye akaachia ukulele mkali wa maumivu nakudondoka chini mzima mzima.baada ya rukaiya kudondoka chini haraka Rebecca akamsogelea kwa kumkalia juu na kuanza kumshindilia mangumi yasiyokuwa na idadi ya uso nakusababisha damu kuanza kumtoka rukaiya ambaye kutokana na ngozi yake nyeupe ya kiarabu kuruhusu kuutoa damu haraka.hali ikiaanza kuwa mbaya kwa rukiaya na mimi nikapiga hatua ndefu na kwenda kumtoa Rebecca alipokuwa amemkalia rukaiya ambapo ndio alikuwa akimshindilia mangumi rukaiya na kumtoa.
‘’paaablooo niachie nimfundishe adabu huyu Malaya wa kiarabu niache nakwambia niaaache.’’kwa hali ya hasira Rebecca akalala kwa hasira huku akiwa anahangaika kujitoa mikono mwangu nilipokuwa nimeshika baada ya kumtoa.
Sehemu Ya 14
‘’hebuuu tulia bwana.’’nikajikuta nikipayuka kwa kumuambia Rebecca ambaye kumuambia vile ilikuwa ni kama sawa sawa nakumpandisha hasira akajikunjua nakuanza kunishindilia mimi makonde mfululizo bila ya huruma lakini kutokana na kuwa mwanaume mwanaume tu nikamzuia kwa kumshikilia vizuri huku nikiendelea kumpandishia sauti ya kuwa anyamaze.lakini kama ilikuwa mchezo vile ile nahangaika kumtuliza Rebecca rukaiya naye akajikusanya nakunyanyuka na kumvamia Rebecca na kuanza kumshindilia makonde ya mgongo kwa nguvu huku akimtukana.nikajikuta nikichoka na hata nilipojaribu kuwagombelezea hali ilikuwa ile ile hakuna aliacha kutaka kupigana na mwenzake kila mtu alikuwa na shauku ya kutaka kumfundisha mwenzake adabu haswa.uzalendo ukanishinda nikajikuta nikiwaacha na taratibu nikaanza kuondoka na kuwaacha pale huku moyo ukiwa unanienda kwa kasi kama mtu aliyekimbia mbio ndefu.nikiwa nimeshafika mbali na sehemu waliyokuwa wakipigana Rebecca na rukaiya ghafla nikamshuhudia mzee mmoja akiwa na kuanza kuwagombelezea jambo ambalo mzee Yule akalifanikisha na kupelekea kila mtu Rebecca na rukaiya achukue njia yake.mwanaume haraka nikaenda kupanda gari la kuelekea nyumbani gari ambalo nilipata mapema nakujikuta nikishusha pumzi ndefu baada ya kufanikiwa kupata siti ya kukaa.mawazo yakazidi kuniandama na kunisumbua mara kwa mara nikawa naisoma messeji niliyotumia ikiwa na taarifa ya habari ya kifo cha rafiki yangu kipenzi Samson rafiki ambaye alikuwa ni wa pekee niliyempenda licha ya kuwa na mikwaruzano ya hapa na pale baina yangu na yeye na kisa kikubwa kilikuwa ni mwanamke ambaye alikuw akinitaka mimi na kumkataa yeye Samson.sikuchukua hata muda mrefu sana nikafanikiwa kufika nyumbani ambapo nikamkuta mama akiwa nje na kuonekana akiwa na nyuso za majonzi sana na baada ya kuniona chozi likamdondoka taratibu katika paji lake la uso na kusababisha niwe na shauku ya kujua nini kilichokuwa kikiendelea.
‘’vipii mama shikamoo mbona unalia.??’’
‘’marhaba mwanangu kwani ulikuwa wapi mwanangu maana uliniaga unakwenda kumuona mgonjwa hospitali na hautokawia kurudi sasa nashangaa ulienda wapi kwani??’’
‘’hamna mama kuna sehemu flani nilipitia baada ya kutoka hospitali.’’
‘’anhaa sawa natumaini messeji ya taarifa ya kifo cha Samson uliipata maana kabla hajafa alikuja hapa nakuniachia bahasha ya kaki ambayo alisema wewe ukirudi uifungue na kuisoma lakini haikupita hata lisaa simu yangu ikaita alikuwa ni mama yake anakuja kunipa taarifa kuwa Samson hatunaye tena duniani eti ameejinyongaaa’’maneno ya mama yakanishtua na kujikuta na mimi machozi yakaanza kunitiririka na haraka nikaingia ndani nilipofika sebuleni nikakutana na bahasha ya kaki iliyowekwa kwenye meza haraka nikaichukua na kwenda nayo chumbani kwangu na kukaa katika kitanda kisha nikaichukua ile bahasha nakuifungua nakukutana na karatasi nyeupe iliyoandikwa maneno kwa wino wa bluu ambayo taratibu nikaanza kuyasoma kutaka kujua yalikuwa yanasemaje.
‘’RAFIKI YANGU KIPENZI PABLO NATUMAINI HAUTOKASIRIKIKA KWA MAAMUZI AMBAYO NAENDA KUYACHUKUA KWA SABABU PABLO MIMI NAJIUA KWA SABABU MOJA TU HALIMAA ANITAKI,ANIPENDI.HANIITAJI KATIKA MAISHA YAKE NA PIA ANAKUPENDA WEWE NA ANATAMANI UMUOE NAPENDA KUTHIBITISHA ILO KUWA ANAKUPENDA KWA SABABU LEO ALIPOANZA KUONGEA TU HAKUTAJA JINA LINGINE LOLOTE HAKUMTAJA HATA MAMA YAKE AKAKUTAJA WEWE NA ANATAKA AKUONE PABLO MIMI NAJIUA KWA SABABU SIWEZI KUVUMILIA KUONA WEWE UNATOKA NA MWANAMKE AMBAYE NAMPENDA KWA HERI NDUGU NITAKUMISI SANA’’yalikuwa ni maneno kutoka katika ile karatasi na kusababisha nianze kuangua kilio cha nguvu sana.niliumia kwa sababu rafiki yangu kajiua kisa mwanamke ambaye mimi sikuwa na mipango naye,
‘’noooooooooooooooooooooooooooo’’nikajikuta nikilalamika sana huku nalia hali iliyosababisha mama haraka kuja na kuingia moja kwa moja chumbani kwangu na alipoingia akaiona karatasi ile ambayo mimi kutokana na uchungu nikajikuta nikiiweka palepale.akaichukua ile barua nakuanza kuisoma kisha akaniangalia nakushusha pumzi ndefu huku akiniangalia.
‘’pablo mwanangu nataka unijibu maswali nitakayo kuuliza lakini kabla sijakuuliza nihadithie mkasa mzima mwanangu.’’mama akaniambaia nimuhadithie na mimi sikuwa na budi ya kudanganya kwa sababu hali ilikuwa ni tete mwanaume nikajifuta machozi nakuanza kumuangalia mama aliyekuwa ananiangalia kwa shauku ya kutaka kujua……
“Mama kusema ukweli samson alikuwa anampenda sana halima kitambo sana na mara kwa mara alikuwa akinituma sana kwake kwa lengo la kwenda kumuambia habari hizo za kama yeye alikuwa akimpenda halima taarifa ambazo hata mimi nilizifikisha kwa huyo halima kwa sababu halima ni rafiki yangu sana tunashauriana kwa mambo mengi sana.lakini sasa hali ni tofauti sana kwa halima mara nyingi alikuwa ananikanya mimi kumuambia habari hizo huku akinisisitizia kuwa alikuwa hampendi samson jambo ambalo lilimuumiza sana samson ambae kuna siku moja tukajikuta tukipigana kabisa baada ya halima kuja kunikombatia mimi.lakini cha kushangaza zaidi ni kwamba mwisho wa siku halima akaja kuniambia mimi ananipenda lakini hata nilipojaribu kumkataa alikuwa akilia na kutishia kujiua na mwisho akajipeleka makusudi kwa kujigongesha katika gari baada ya kumwambia siwezi kuwa naye na ndio huyu niliyeenda kumuangalia jana Mama.kiufupi samson ameamua kujiua eti kwa sababu leo halima baada ya kuzinduka akataja na jina..l…..”kabla hata sijamaliza kuongea maneno yale ambayo yalikuwa ni ya ukweli yaliochanganyika na uongo kibao nikajikuta nikishindwa kujizuia machozi kibao yakaanza kunitoka na kusababisha mama ambaye hakuna na neno sasa lolote la kusema akanisogelea na kunikombatia nakuanza kunifariji.
“Sikia mwanangu kumbuka kazi ya Mungu haina makosa na Mungu ndio mpangaji wa kila jambo na ndio alipanga hivyo itokee” yalikuwa ni baadhi ya maneno ya mama yalionifariji mimi niliyekuwa bado naendelea kulia.siku ilikatika na kesho yake asubuhi na mapema tukadamka mimi na mama kuelekea kwa rafiki yangu kipenzi samson kwenda katika msiba wake ambao baada ya kufika tukapokelewa na vilio vya hapa na pale kutoka kwa ndugu na jamaa na sisi tukajiunga nao wakiambatana na mamia ya wanafunzi ambao wengine tulihitimu nao kidato cha nne ambacho ilikuwa si siku nyingi tumalize.
“Iiiiiiiii..ooooooook jamani samson mwaaaaanangu baba umeetuachia ukiwaa mimi na dadaaa yako umetuaacha peke yetu na kumfuata baabaaa y….akkkoooo mwa…nangu mamamama weeeee Eee mungu”yalikuwa ni maneno ya mama samson yaliosababisha mamia ya watu waliomsikia kuhuzunika sana na wengine kulia kabisa wakiambatana na mimi ambaye nikajikuta nikiangua kilio cha nguvu na kusababisha nianze kubembelezwa na wanafunzi wenzanfu ambao wengi walikuwa wakijua mimi na samson tulikuwa ni marafiki wa kushibana shuleni hapo.taratibu za ratiba ya maziko zikatajwa na kutangazwa kuwa mwili wa marehemu utaagwa hapo hapo kwao nyumbani na kuzikwa maeneo karibu na hapo nyumbani.kweli muda muafaka ukawadia na mamia ya watu waliojumuika tukaitwa kwenda kuaga mwili wa marehemu samson.hakika nguvu zikaniisha kabisa baada ya kushuhudia mwili wa samson aliyekuwa na ndoto za kuwa daktari wa baadae akiwa na lengo la kuisaidia familia yake kuondokana na umaskini akiwa ndani ya jeneza pamba zikiwa puani na masikioni alikuwa ametulia kama sio yeye.kwa uchungu nikajikuta nikiangukia jeneza lake huku nikilia kwa uchungu zaidi hakika inauma kumpoteza rafiki yako kipenzi ambaye ulikuwa upo naye bega kwa bega kwa mambo mengi yakushauriana.
“Sammmson amka haliima anakuita sammmm daaaa samson amkaaaaaa” nikajikuta nikimlalamikia amke baada ya kumuona amelala hakika niliona kama ni ndoto fulani lakini wapi ulikuwa ni ukweli mtupu.Miongoni mwa watu wakiambatana mama yake samson ambaye alikuwa akinifahamu vizuri na mama yangu na baadhi ya wanafunzi wakanisogelea na kwenda kuninyanyua pale nilipokuwa nimeegemea katika mwili wa samson ambaye alikuwa wala hanisikii na wala alikuwa hanioni roho yake ilikuwa ishatangulia sehemu husika.
“Nyanyuka Pablo kazi ya Mungu haina makosa” niliyasikika maneno ya mwanafunzi mmoja akiniambia lakini hakuniingia niliendelea kubaki palepale lakini nguvu za watu waliweza kuninyanyua na kunipeleka pembeni hakika ilikuwa ni majonzi juu ya machozi kwangu mimi na kila miongoni mwa watu walioudhuria na kweli ilipotimia mida ya saa tisa jeneza lile likabebwa na wote tukajumuika kumsindikiza samson katika safari yake ya mwisho katika maisha yake hapa duniani.katika hali ya sintoamini jeneza likadumbukizwa shimoni katika kaburi lake na kisha yule mchungaji akatoa wosia flani watu wakaanza kulifukia lile kaburi.
“daaaaa sam kwa heri” nikajikuta nikijisemea kimoyomoyo baada ya watu kumaliza kulifukia kaburi lile la samson kisha wakaitwa watu kwenda kuweka maua baada ya pale yule mchungaji akatoa wosia wa mwisho wa kutukumbusha kuacha madhambi kwa kumrudia Mungu na baada ya kumaliza wakaambia wabaki wanandugu tu kisha sote tuliobakia tukaruhusiwa tuondoke.mama akanishauri niondoke nyumbani kisha yeye akabaki kwa lengo la kusaidia saidia kazi zilizokuwa hazijaisha katika ule msiba huku akinisisitizia kuwa nisipitie sehemu nyingine yoyote zaidi ya kuelekea nyumbani.mwanaume nikaenda kupanda gari la kuelekea nyumbani ambapo kama vile mchezo wa kuigiza nikakutana na dada yule niliyemgonga kule serena hoteli siku ya kwanza ambayo nilienda kufanya mapenzi na rukaiya kisha yule demu alionekana kunipenda na kunipa na namba yake na siku ya pili nilionana naye katika gari siku hiyo tulipotoka kwa akina rebecca.baada ya kuniona tu haraka akanisogelea mpaka katika siti niliyokaa mimi kwa sababu kulikuwa hamna mtu mwingine yeye akakaa.
“Jamani nimefurahi kukuona Mambo”yule dada akajikuta akivunja ukimya na kuamua kunisalimia.
“Poa tu”
“Unaonekana haupo sawa vipi kuna tatizo gani wangu niambie mpenzi halafu jamani hata ujanipigie simu tangia siku zile kwanini lakini??”
“Nilikuwa sina vocha”
“Jamani basi hebu nipe namba yako maana mimi sina”
“Sina simu sasa”
“Hee jamani…” Ghafla yule dada akanisogelea karibu kabisa nakunikamata mikono yangu nakunishika kwa mahaba sana na kusababisha nigeuke na kumuangalia kwa hasira iliyosababisha aniache kwa uoga nakubaki akiniangalia lakini mimi sikuwa na haja ya kuongea naye baada ya kituo changu cha kushikia nikasimamisha gari na kushuka lakini cha kushangaza na yule dada akashuka na kuanza kunikimbilia aliponifikia karibu akazunguka mbele na kuniekea mkono kwa lengo la kunisimamisha lakini mwanaume nikautoa mkono huo kwa nguvu kwa kumsukumiza lakini hali ikarudi ile ile akanisogelea tena na kunisimamisha.
Sehemu Ya 15
“Weee mwanamke unataka nini nitakufumua ujue”mwanaume nikang’aka kwa hasira zaidi na kusababisha yule dada atishike.
“Unajua mimi tangia nikuone nimekupenda ghaf…..”
“Weeeeee acha ujinga hapa ntolee utumbo wako bwege wewe” kabla hata ajamaliza kuongea nikamzuia na kumuambia vile kisha nikamsukumiza tena na kuanza kuondoka haraka na kumuacha akiwa anajiuliza maswali mengi.nikafika nyumbani nakujibwaga kitandani kisha nikaichukua simu yangu ambayo baada ya kuiwasha messeji tatu zikaingia lakini nilipotaka kufungua simu yangu ikaita na nilipoangalia jina alikuwa ni rebecca.haraka haraka nikaipokea nakuiweka sikioni.
“Hivi wewe ni mwanaume wa aina gani maana nimekufumania na hata kuniomba msamaha umeshindwa eee sasa basi kuanzia sasa naomba tuachane tusijuane kabisa wala sikuhitaji tenaa”yalikuwa ni maneno ya rebecca ambaye alionekana akiongea kwa jazba kubwa ambayo hata nilipotaka kujaribu kuongea akakata simu na nilipopiga mimi simu haikupokelewa ikakatwa na nilipopiga tena niliambia haipatikani.nikajikuta nikipotezea huku mawazo ya kifo cha samson kunitawala kichwa changu ghafla mlio wa ujumbe wa messeji ukasikika kwenye simu yangu na haraka nikaungalia alikuwa ni rukaiya taratibu nikaufungua nakuanza kuusoma
“Sikiaaa pablo nikuambie baba amenibana na kuniuliza ni nani aliyeuharibu uso wangu sasa sikia nikutaarifu pablo kama nikikutaja wewe na mbwa wako yule mmjue wote mmekwisha kabisa”…………
Nikajikuta nikishusha pumzi baada ya kusoma ujumbe ule wa rukaiya ambaye hata nilipojaribu kumpigia simu ikakatwa na nilipojaribu kupiga tena ikawa haipatikana.akili yangu ikaanza kuchanganyikiwa flani mwili ukaanza kutoa majasho mwili mzima hofu kubwa ikanitanda na kusababisha hata moyo uanze kunidunda sana.hakika siku hiyo hata usingizi haukuja kutokana na mawazo yaliyokuwa yakiniandama.hakika maneno ya rukaiya yalikuwa yakinitisha sana kutokana na ukweli kwamba baba yake alikuwa ni mtu anayejiweza mno hakika kujiweza kwake kulisababisha kuniogopesha kwa sababu anaweza kunifanyia chochote kutokana na hela zakeambazo zilizidi kupendezesha wanae.kesho yake mwanaume nikaamka mapema nakuanza kufanya usafi wa nyumbani kwetu na kumsaidia mama kazi kazi ambazo mara nyingi alikuwa akizifanya yeye na kumaliza kwangu shule ilikuwa ni msaada tosha kwa mama ambaye mara nyingi kazi hizo alikuwa akizifanya yeye pekee.ghafla nikiwa nakunywa chai simu yangu ikaaita na nilipoangalia alikuwa ni zureiya ambaye ilipita kitambo sana tukiwa katika kutoelewana haraka haraka mwanaume nikaipokea haraka na kuipeleka sikioni.
‘’halooo mpenzi.’’nikajikuta nikianza kwa mbwembwe zote hali iliyosababisha mshangao mkubwa kwa zureiya ambaye alikaa kimya kisha akaachia tabasamu ambalo lilinifurahisha na mimi pia.
‘’jamaani leo unanitaa mpenzi pabloo wewe bana haya nambie sasa.’’
‘’aaaaa jamani sasa unataka nikuitaje zureiya mke wangu.’’
‘’hahahahaha jamani basi nakuomba leo tukatane kama ukiwa na muda maana nimekumiss sana.’’
‘’jamani usijali hata sasa hivi.’’
‘’heee naomba tukutane mmmh kule beach yani palm beach.’’
‘’jamani shaka ondoa sasa hivi nakuja honey.’’mwanaume nikajikuta nikipata furaha ya ghafla.hakika kilikuwa ni kipindi change kigumu kwa sababu nilishagombana na Rebecca na dada yake zureiya rukaiya ambaye jana yake alikuwa amepata dhahama kubwa ya kupigana na Rebecca ambao wote wakiwa wananigombania mimi.mwanaume haraka nikamaliza kunywa chai na kumuaga mama ambaye naye akakubali na kuniruhusu huku akanisisitizia kuwahi kurudi.nikaenda haraka haraka mpaka stendi na kupanda gari ambalo lilikuwa limejaa lakini kutokana nilikuwa nataka kuwahi nikapanda hivyo hivyo huku nikibanana na watu ambao nao walikuwa wamepanda gari hilo.siku hiyo haikuwa na foleni haraka nikafika na kukutana na zureiya ambaye alionekana kuwa na furaha sana baada ya kuniona haraka akanisogelea na kunikumbatia kwa mahaba ambayo yalikuwa kivutio kwa watu waliokuwepo pale stendi ambao wakaishia kutuangalia kwa maswali mengi yakujiuliza.
‘’jamnai Pablo nimekumisi sana mpenzi na hakika sasa umenisamehe kabisa.’’zureiya akafungua mazungumzo baada ya kutafuta sehemu nzuri na kukaa huku tukiwa tunakunywa kinywaji cha juice ya mapenseni.
‘’nisakusamehe wala usijali zureiya mimi ni wako haina haja ya kuogopa kwa sababu wewe ndio peke yako nimekuweka moyoni.’’
‘’jamani Pablo asante sana kwa kusikia hivyo kwa sababu nilikuwa nina wasiwasi wa kukupoteza kwa wasichana wengine ambao wengi wao wanakutamani kutokana na ukarimu wako,ustaarabu uliokuwa nao pablo.’’
‘’hahaha hamna bana nambie.’’
‘’pablo dada yangu rukaiya anaumwa jana amepigana sijui nani basi amemuharibu uso.’’moyo wangu ukaanza kudunda baada ya kusikia maneno yale ya zureiya maneno ambayo kisa chote na chanzo nilikuwa nakijua mimi pekee.nikajikuta nikionyesha uso wa mshangao kwa zureiya ambaye aliongea kwa kusikitika.
‘’jamaani kisa nini.??’’
‘’basi najua baba amembana sana ujue lakini kakataa kusema so baby tufanye haraka mimi niwahi kurudi nyumbani.’’
‘’mmmmh tufanye nini tena zureiya jamani.’’
‘’wewe bana situkumbushie kale kamchezo tuliofanya siku ile.’’nilimwangalia zureiya aliyesema maneno yale huku akiwa ameregeza macho yake yalionipandisha mzuka na kusababisha mwanaume mzuka upande ghafla na kujikuta uchu ukinipanda na mimi nikawa namuangalia zureiya kwa macho ambayo hata yeye yalimuonyeshea kitu.
‘’twende basi’’zureiya akaniambia huku akinyanyuka na mimi nikamfuata alipokuwa akielekea na safari yetu ikaanza na kuingia katika hoteli ya palepale palmbeach.lakini baada ya kuingia katika hoteli ile iliyokuwa imesheheni waarabu na watu weusi kama mimi wachache nikamshuhudia zureiya akiwa ana jificha ficha kama anamkwepa mtu asimuone jambo ambalo lilinishangaza sana na kujikuta nikimuuliza.
‘’mmmh baby vipi mbona unajificha jificha.??’’
‘’mmmh bby kuna humu ndugu zetu wengi ila usijali wala nini.’’nikajikuta na mimi nikipotezea na tukalipia chumba na tukaingia katika chumba ambacho kulikuwa ni kizuri sana.
‘’unajua bby hii ndio mara yangu ya kwanza kuingia gesti.’’zureiya akaniambia vile huku akianza kuvua nguo zake alizovaa nikifuatiwa na mimi ambaye nilipoangalia pembeni nikakutana na box kubwa la kondomu.nikalisogelea lile boxi na kulifungua kisha nikatoa pakti moja kwa lengo la kuvaa lakini cha kushangaza zureiya akanifuata na kunipokonya.
‘’heee vipi zureiya mbona unaninyang’anya kondomu.??’’
‘’wee za nini sasa.??’’
‘’khaaaa si tunafanya mapenzi au tumekuja kupiga stori??’’
‘’najua kama tumekuja kufanya mapenzi baby lakini mimi sitaki na kondomu mimi nat…’’kabla hata zureiya hajamaliza sentensi yake nikamsogelea na kuanza kumnyonya denda jambo ambalo hata yeye lilimshangaza na yeye akajikua akinipokea vizuri na wote tukaanza kudendeka taratibu.
‘’aaaaasssss ooooooo Pablo mume wangu nimekumiss maana kitambo sana,’’zureiya akazidi kunipagawisha kwa sauti yake mwanaume nikajikuta nikijisahaulisha majanga yote ambayo yamenitokea kufumwa na Halima kama natembea na rukaiya,pia kutojuwa zureiya kama mimi natembea na dada yake.hakika miamko ilikuwa inakuja ilinisahaulisha kama nilikuwa nimepoteza rafiki yangu kipenzi kwa sababu ya Halima ambaye ndio rafiki yake mkubwa zureiya na ndio yeye ambaye aliniyenionganishia na zureiya mpaka nampata na baadae eti anakuja kusema kwamba ananitaka jambo ambalo lilipelekea yeye kugongwa na gari kisa baada ya kutufuma na rukaiya akiwa ananibusu,hakika pia nikajikuta nikijisahau kwa muda kama nilikuwa nimegombana na msichana mwingine mrembo anayefahamika kwa jina la Rebecca ambaye alipigana na rukaiya ambaye kwanza alinipa kitisho kwamba akinitaja mimi kwa baba yake basi nitakwisha pili nikajikuta nikisahau tena onyo kubwa kutoka kwa rukaiya ya kwamba nisitembee tena na mdogo wake ambaye kwa muda huu nilikuwa nabanjuka naye.mihemiko iliendelea kuchukua nafasi yake mwanaume nilionekana kuwa na uchu sana na zureiya ambaye hakika nilimuona mpya tena na mapenzi yake yakarudi na kujikuta nikizidisha mbwembwe nyingi.nikamsukumiza kitandani zureiya ambaye tayari alishakuwa mtupu hana hata alichovaa kujistili.mwanaume nilikuwa tumbo wazi huku nikiwa nimevaa suruali tu baada ya kuvua shati tu.mzuka ukanipanda sana macho yakiwa yanaumangalia zureiya alikuwa naye akiniangalia mimi huku akiyashika maembe dodo yake mawili na kuzidisha kunipa mzuka mkubwa.taratibu nikashusha suruali yangu na kumvamia kitandani kwa kumkandamiza mabusu mbali mbali ambayo yalimpagawisha sana zureiya ambaye alionekana kuvimisi vitu vile adimu.
INAENDELEA

