NYETO NYETONI
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Sehemu Ya 21
Cynthia akawa yupo hoi lakini alionekana kuwa mbishi
Ndipo Chinoge alipoiamuru Nyundo imalize kazi
Nyundo ikakita tumboni mwa bibie alitapika damu na nyongo Nyundo
Ikazunguka na kwenda kukita magotini Mabonge ya damu yalizidi kumtoka bibie akawa amelala chini
Licha ya purukushani na kelele zote zilizokuwa zikitokea hapo Sebreni Lucy hakuweza kusikia chochote hata waliokuwa nnje hawakuskia
Nyundo ikarudi mkononi mwa Chinoge iliporudi tu! Akatoweka
Songa nayo
Sasa
Mda wote Lucy alikuwa amekaa kitandani akiendelea kuperuzi kwenye mtandao wa Facebook pasipo kufahamu kuwa Dada yake kuna kisanga kimemkuta
“naomba vocha ya elfu tano basi”
”mtandao gani?”
“nimekwambia naomba vocha”
“ndiyo nakuuliza mtandao gani?”
“nitumie kwenye tigopesa”
”sawa nipe namba basi”
Lucy akaandika ile namba kisha akafungua mesegi ya Mwanaume mwingine
”mambo mrembo”
”safi tu nambie mkaka”
”mmh”
”sasa mbona unaghuna?”
“nilishakata tamaa mwenzako kutokujibiwa mesegi yangu”
”ndiyo ishajibiwa sasa nambie”
”upo pande zipi?”
”Tabata bima”
”whaoo mi naishi Viwege huku”
”mmh Viwege ipo mkoa gani?”
”Dar es Salaam yani unapanda gari mpaka Gongo la Mboto kisha unapanda la Viwege”
”sawa nimekupata”
”sema nini mrembo kiukweli nimetokea kukupenda yani kila nionapo picha zako nakuwa hoi taabani”
“mmh”
”usighune bwana nikubalie mtoto wa Mwanamke mwenzio nina teseka juu yako”
“nikuulize kitu mkaka?”
”niulize tu! Sema usiniite mkaka jina langu si umeliona hapo kwenye Profile?”
“hivi mpaka Sasa ushatongoza Wanawake wangapi humu mitandaoni?”
”ni wewe tu!”
”mmh sio kweli”
”niamini bibie”
“sawa nimekuamini”
“baby tayari nimekutumia elfu kumi”
Ni mesegi iliyotoka kwa jamaa aliyeombwa vocha ya elfu tano
”whaoo asante baby”
Lucy aliandika hivyo huku akisimama na kuelekea Sebreni kuifata simu yake ambayo aliiacha sofani
Laa haula ile anafungua mlango tu! Wa chumbani hakuweza kuamini macho yake kwakile akionacho mbele yake
Dada yake alikuwa kalala chini huku baadhi ya vitu vikiwa shaghara baghara
”dadaa jamani dada yanguuu”
Alipiga kelele na kumkimbilia Dada yake akawa anamtikisa kelele zake ziliweza kusikiwa kule nnje kwakuwa mlango ulikuwa wazi baadhi ya majirani na Wapangaji wenzao wakaingia
“khaa wee Lucy kitu gani tena kimemtokea Dada yako? Mlikuwa mnapigana au?”
“jamani Dada yangu hiiiiiiii,, haaaaa,,”
Lucy alilia huku akimtikisa Dada yake
Tukija kwa wale vibaka siku hiyo walikuwa maeneo ya Tegeta Kibaoni katika harakati za kuiuza ile simu
“oyaa wee Pimbi”
”nani Pimbi sasa?”
”embu lete hiyo simu”
”sio lete simu nakuuliza nani Pimbi?”
“pimbi si wewe hapo!”
”wee kweli matako kuku kishingo”
”sema nini jeshi yule Bwege kasema ana elfu tisini tu!”
“ninii?”
”ujaskia au dharau?”
”sio dharau yani Samsung Galaxy s6 edge toleo la kwanza kabisa hili aitake kwa hela hiyo kweli kama vipi mwambie akaushe tu!”
”sasa kichaa wangu hii simu hata tukiuza elfu sita kuna hasara gani tuipatayo si tumeikwapua tu!”
”hata kama
“embu acha mambo yako wewe”
”kuanzia Sasa mpo chini ya ulinzi jisalimisheni wenyewe, haya wekeni mokono yenu juu”
Wakati vibaka wale wakibishana kuhusu bei ya kuiuza simu ile ndipo wakashtushwa na sauti kari ikiwataka wajisalimishe. Binafsi walishtuka sana kuona Polisi takribani
Sita wakiwa na mitutu ya Bunduki wamesimama mbele yao wakatii amri kwa kupiga magoti chini wakanyoosha mikono juu kabra ya kufungwa pingu walianza kuchezea kichapo cha kufa mtu walipigwa ile kisawasawa mpaka wanapakizwa kwenye Difenda walikuwa hawatamaniki walichakazwa ni damu tu zilikuwa zikiwachuruzika midomoni na puani
”ndiyo mkuu tayari tumewanasa”
”mko nao hapo?”
”ndiyo mkuu tupo nao”
”basi hakikisheni mnawafikisha kituoni mkishafika pale nijurishe nije kuwafata”
”sawa mkuu haina shida”
Mmoja kati ya Maafande wale alisikika akizungumza kwa simu na bwana mkubwa Madebe
Waliweza kuwasili maeneo ya kituo cha polisi watuhumiwa wakabebwa msobemsobe na kushushwa chini wakakokotwa mpaka Selo na kutupiwa humo
Dakika si nyingi Madebe akiwa kaongozana na Cooper waliwasili pale akaomba kuwaona hao Vibaka alipowaona tu! Akatoa amri wachukuliwe na kupelekwa Lugalo
Wakati wanajiandaa kutoka eneo lile la kituo cha polisi
Ghafla bin vuu upepo mkali misiri ya Kimbunga ulianza kuvuma
Vumbi lilitimka huku miti na majani yakipukutuka Makaratasi na manaironi vilipeperushwa kufumba na kufumbua kuna kiumbe mfano wa Ninja Ice aliibuka sema kiumbe hiki alionekana ni mtoto mdogo nakama sio mtoto mdogo basi ni Mbilikimo
Sura yake
haikuweza kuonekana vyema ila mwili wake wote ulikuwa ni barafu lenye kung’aa yule kiumbe alikaza macho yake yenye kutoa kitu kama shoti za umeme kuwaangalia wale Vibaka waliokuwa wamepakizwa kwenye Gari wakati akiwa bize kuwaangalia wale Vibaka akashtushwa na vitu vya moto vikidunda mwilini mwake kumbe Maafande walishaanza kummiminia Risasi ambazo zilikuwa zinadunda tu bwana mkubwa Cooper akachomoa kisu chake kidogo akakimbia kwa kasi kumfata yule kiumbe
”Coopeeeeeer”
Madebe alipiga kelele kumwita Cooper huku akishuhudia Cooper mwenyewe akirudishwa kwa kurushwa juu baada kutandikwa zinga la teke akafikia kujibamiza kwenye Gari
Risasi zilizidi kumiminika mwilini mwake kiumbe ndiyo kwanza kilisimama imara
Baada kumtandika teke Cooper halafu akazunguka na kujitawanya viumbe wenye sampuri yake wasiokuwa na idadi waliibuka na kuanza kuwashambulia maafande huku
Yeye akichumpa na kwenda kutua kwenye Gari ambayo walipakizwa wale Vibaka alimshika mmoja na kumchinja huku mwingine akimmalizia kwa kumchomeka kisu cha koromeo unajua mpaka hapo Madebe hakujua afanye nini alibaki akiwa ameduwaa tu
Baada kuwachinja wale Vibaka yule kiumbe akatoweka pamoja na wafuwasi wake wenye kufanana naye
Cooper alikuwa kalala chini haliyakuwa akitetemeka unaweza ukasema labda kagusishwa nyaya ya Umeme
Ajabu hakuna hata Askari mmoja aliyeuwawa zaidi ya kujeruhiwa waliuliwa ni wale Vibaka
“wauweee”
Ni kelele alizopiga bwana mkubwa Chinoge akiwa amekaa sebreni kwake tukio zima la kule kituo cha polisi aliweza kulishuhudia kupitia Tv yake kubwa iliyopo ukutani hakika alishangilia sana akafungua friji na kutoa chupa ya maji akanywa funda kadhaa akapiga hatua kadhaa kuusogelea mlango baada kusikia ukigongwa akashika kitasa na kuufungua
“habari yako kaka yangu”
Mgongaji mwenyewe alikuwa ni bibie Salome yule Binti aliyekuwa akimuhitaji kimapenzi Marehemu Gulam
“safi tu nambie Mrembo”
“mmh nilikuwa naiomba ile cd niliyokuona nayo jana”
“ohoo ile ya Fifty Shades?”
”ehee ndiyo hiyo hiyo”
Chinoge akarudi chumbani muda akatoka na kumkabidhi ile cd
“ohoo Asante sana”
Salome alishukuru huku akiipokea ile cd
”vipi lakini unaenda kuangalia na shemu au?”
”hapana nipo tu! Mi mwenyewe kwani hii movie ina Minyanduano?”
”hahahaha, embu liangalie vizuri cover lake”
Salome akaliangalia lile cover kulikuwa na picha ya wapenzi wawili wakinyonyana denda”
”mmh wacha nikaiangalie kama nikizidiwa nitapiga Nyeto Nyetoni”
“shida yote ya nini bibie ingia basi humu tukaicheki pamoja”
Salome pasipo kujivunga aliangalia kushoto na kulia kuona kama kuna Soo kisha akajitoma chumbani kwa Chinoge mlango ukafungwa.
Mziki ulianzia Sebreni yani walipoingia tu cd ikawekwa pembeni wakashikana na kuanza kubadirisha mate
********
Cooper na wale Maaskari waliweza kuwahishwa hospitali
“kwanini unayaacha yote haya yakitokea tena mbele ya macho yako. Kumbuka wewe ni Jeneral Wananchi wote wanakutegemea wewe ndiyo utakae simama mstari wa mbele kwaajili ya kuliongoza Jeshi kwenda vitani ajabu leo hii
unabung’aa tu!”
Yote yalikuwa ni maneno kutoka kwa mkuu wa majeshi akimsema Madebe ilionekana kafanya uzembe mkubwa Sana kumuacha yule kiumbe akiwashambulia Maaskari muda wote Madebe alibaki kimya akimsikiliza mkuu wake simu iliyopo mezani ikawa inaita ambapo mkuu wa Majeshi akaipokea na kuiweka sikioni
“what!?”
Mkuu wa Majeshi alitamka hivyo baada kuambiwa kitu na mtu aliyekuwa kapiga simu akairudisha simu mahara pake kisha akamkazia macho Madebe kwa sekunde kadhaa
“hii sasa ni hatari inavyosemekana kuwa yule Agent wakike aitwae Cynthia amejeruhiwa vibaya sana”
“ninii?”
Madebe aliuliza kwa hamaki huku akisimama kutoka kwenye kiti
”ndiyo hivyo kijana”
Madebe akatoka ofisini pasipo kuaga binafsi alishachanganyikiwa alimuomba kijana mmoja ampeleke hospitali ya Aghakan
”mamaa,,Ducha amerudi”
Zilikuwa ni kelele za Kitwana akimwita mama yake baada kuona Ducha akifunguliwa geti na kuingia ndani Mariam alitoka ndani na kusimama kwenye kizingiti cha Mlango nikweli Ducha alikuwa karejea tena akiwa mzima wa hafya
Baada Ducha kuingia ndani aliwaangalia wale Wanajeshi halafu akafanya kuwapigia Saruti kitu ambacho kiliwafanya Wanajeshi watabasamu
”whaoo mwanangu huyo”
Mariam alitanua mikono na kumraki Ducha akamkumbatia kwa muda
Ducha alijiskia kufarijika sana kukumbatiwa na Mariam wakaingia ndani ambapo kina Milfat walianza kumdadisi maswali ya hapa na pale
”Ducha kwani ulipelekwa wapi na yule jini?”
“ajakunyonya damu kweli embu nione shingo yako”
“isijekuwa na wewe umekuwa zombie kama yule aliyekuchua”
”tujibu basi ulipelekwa wapi na yule Jini?”
”nyie watoto embu shikeni adabu zenu kaka yangu sio Jini yule”
Mariam akawakalipia watoto wake kwa kuwaambia hivyo
Ducha alishangazwa Sana na kauli ya Mariam kusema Chinoge ni kaka yake
”kha! Inamaana yule ni Mjomba etu?”
Ahmad akauliza
”ndiyo maana yake au ukumbuki sikuile nilizungumza naye kitu gani embu subirini niwaonyeshe kitu”
Mariam alizungumza hivyo akaelekea zake chumbani alirejea haliyakuwa kabeba Albaam ya kuhifadhia picha akaiweka mezani
Alianza kuwaonyeshea picha za kifamilia
“haaaa! Kumbee ni Ankor wetu kudadeki nami natamani siku moja niwe kama yeye”
Ahmad alizungumza hivyo baada kujiridhisha kuwa yule kiumbe ni Mjomba wao.
Ducha naye alishapata picha kwanini siku ile Chinoge alimuokoa Madebe asiuwawe kumbe ni Shemeji yake
*********
Tukija kuzimu siku hiyo kwenye tawala ya Duchani kulikuwa na kikao nyeti Makuhani na majini wote wenye kuhusika na tawala hiyo waliitwa
“kha!kha!kha!
Hatimae leo hii ule muda tuliokuwa tukiusubilia kwa haamu umetimia ghriiiii,,ngriiii,, Tunaitaka damu ya Ducha lazima atolewe kafara hahahaha mizimu inataka nyamaa nendeni mkamlet….
Hata hakuweza kumalizia kuzungumza kisu kilikuja kwa kasi na kuzunguka Shingoni mwake
Kichwa kikatengana na kiwiliwili
Majini wote walishtuka
Kuja kutahamaki Ducha mwenyewe akaibuka
Akifatiwa na bwana mkubwa Chinoge Nyundo mkononi aisee
”kamata yule”
Amri ikatoka kwa Duchani akiwaamrisha majini wamkamate Ducha ambaye alifanya kuchenji muonekano wake kumbe ni yeye aliyekinukisha kule Kituoni majini waliojaribu kumsogelea Ducha walijikuta wakitembelewa na Nyembe za hatari ni silaha ambazo alikuwa akizitumia Marehemu Ninja Ice kwa sasa Ducha ndiyo anazitumia ubaya wa Silaha hizo ikikugusa tu unapukutika Kama karatasi liunguapo na Moto
Duchani baada kuona wanazidiwa ndipo akaamua kukimbia lakini hakuweza kufika mbali alijikuta akinaswa na mzee mzima Ibnuwas
Kuzimu kulikuwa na hekaheka ya aina yake miale yenye kuambatana na moto ilizidi kutatarika huku Majini wengi wakipukutika kama vile nyasi kavu ziunguapo kwa moto
Nyundo zote mbili zilionekana zikizunguka huku silaha kali aina ya Star alizokuwa akizitumia Bwana mkubwa Ninja Ice zikiwapukutisha maelfu ya Majini Ducha alionekana kuzitumia vyema silaha hizo.
Utawala wa Duchani ulikuwa umezidiwa nguvu kwa kiasi kikubwa tena na watu wawili tu! Kibaya zaidi mmoja kati ya watu hao ni mtoto wao ambaye kwa upande wao walimuona kama ni mtoto wa haramu kisa tu! Kazaliwa nnje ya ndoa.
Baadhi ya majini waliweza kupata upenyo wa kukimbia huku
Bwana mkubwa Duchani akinaswa na kutiwa kwenye kifaa kimoja wapo ambacho ndani yake kulikuwa na Barafu siku zote majini kwenye baridi wanateseka na kutaabika kupita kiasi ni sawa na Binadamu kuwekwa kwenye moto
”agriiiiiiii,,,hiiiiiii”
Duchani akiwa amefungiwa ndani ya kile kifaa alianza kuunguruma huku akibadirika ngozi ya mwili wake kutoka ya kibinadamu aliyojitwika na kuwa ya kijani. Sio kama alifanya hivyo kwa hasira bali baridi lililopo mule lilianza kumuasiri
”Duu,,du! Duchaaa,, niokoe,, tafadhari fanya kunitoa humu kumbuka Mimi ni baba yako, Ducha, usiniache mwanangu”
Duchani alipiga kelele huku machozi ya damu nyeusi tii yakianza kumchuruzika
Ducha alimuangalia baba yake kama ujuavyo siku zote damu nzito kuliko maji hisia za kumuhurumia baba yake zikamjia sema hakuwa na la kufanya,
”twende kijana”
Sauti ya Chinoge akimtaka waondoke ndiyo iliyo mgutusha
Wakashikana mikono na kutoweka
Simanzi na Majozi iliweza kutawala kwenye ukoo wa Duchani majini waliosalia kwenye vita hiyo walikusanyika kwa pamoja
Wakafanya taratibu za kuwazika wenzao kisha wakakaa kikao na kuanza kujadiriana juu ya wao kwenda kumuokoa kijana wao Duchani pamoja na kulipa kisasi juu ya vifo vya wenzao
Wakati kikao kikiendelea kuna kikosi cha majini kilionekana kuja maeneo hayo
Kwanza walishikwa na uwoga wa aina yake wakidhani ya kwamba kikosi hiko kinachokuja ni cha wale wabaya wao
“kila mmoja akamatie silaha yake vyema. Tujiweke tayari tayari kukabiliana nao hakuna kuogopa”
Mmoja kati ya majini aliyeonekana kuwa ni kiongozi wao alizungumza hivyo
“ohoo! Poleni sana ndugu zanguni”
Alikuwa ni bibie Ozzi
Ndiyo aliyekuwa akiuongoza msafara ule
Waliwasili pale wakafanya kutua chini
Kuna msafara mwingine ukawasili hawa ni wale ambao wakati wa sekeseke hawakuwepo ukichanganya na wale waliokimbia basi Walizidi kumiminika hakika walikuwa wengi kupita kiasi
”kama makosa tumeyafanya wenyewe, hatuna budi kujirahumu kwa maana Ducha ndiyo alitakiwa kuwa ngao yetu silaha yetu,
Ajabu sisi wenyewe tukataka kuiangamiza kwa kisingizio kuwa ya haramu,
Ona sasa ilivyoshiriki kutushambulia”
Ozzi alizungumza hivyo baada ya kupewa nafasi ya kuchangia hoja juu ya nini kifanyie ili kumuokoa Duchani
”nikweli usemavyo Binti yangu Ozzi lakini tulitaka kufanya kitu pasipo kufikiria hata hivyo hatujachelewa tunaweza kusahihisha makosa yetu”
Baba yake Ozzi mzee
Makanga alizungumza hivyo
”unamaamisha kitu gani baba kusema hatujachelewa?”
”namaanisha ya kwamba kuwa juu ya hili swala tunaweza tukamtumia Ducha kwenda kumuokoa baba yake.
Kama sikosei binti yangu Ozzi ni mmoja kati ya marafiki zake Ducha sasa kwanini tusiitumie nafasi hii
Kumteka kiakili?”
Alizidi kuzungumza mzee Makanga akatoa kichupa fulani hivi na kumkabidhi Binti yake
“nikitu gani hiki?”
Ozzi aliuliza baada kukipokea kile kichupa
”usiulize kitu gani unachotakiwa kufanya kwasasa ni kwenda kumnywesha Ducha hicho kinywaji
”nawezaje kwenda kufanya jambo ambalo sijui kama lina faida kwangu au ni hasara kwa upande wetu. Ni vyema ukaniweka wazi”
Ozzi akang’ang’ania kufahamishwa kwanza
”sawa binti yangu kwanza kabisa naomba ufahamu ya kwamba ndani ya hiko kichupa kuna Kipapatio cha Nani? Ni dawa mujarabu ya kumpumbaza na kummiliki kiumbe yoyote yule yani ukimnywesha tu atakuwa chini ya tawala yako utaweza kumtumia vile utakavyo”
Mzee Makanga alitoa ufafanuzi juu yakile kilichomo ndani ya kile kichupa Majini wote walikenua meno ya furaha kwa matumaini ya kwamba mda si mrefu Ducha atakuwa wao.
“ohoo sawa nimeweza kukuelewa ewe baba yangu lakini ningeomba nipewe muda kidogo juu ya kuikamirisha hii kazi. Maana sio kitu rahisi kama mfikiriavyo’’
Ozzi alizungumza hivyo akapatiwa na maelekezo mengine pale kisha Ozzi akaaga na kuondoka zake wala hakusema ni mda wa siku ngapi atakuwa tayari kuikamirisha hiyo kazi. Alipotoweka pale akafunga safari moja kwa moja mpaka Duniani akafikia sehemu moja hivi yenye njia panda akasimama katikati ya njia hiyo alikaza macho yake ya kijini kuangalia kushoto na kulia
“hii dawa inaitwa Kipapatio cha nani? Mmh mbona kama sielewi inamaana gani kuitwa hivi? Heti nikamnyweshe kipenzi changu Ducha, hapana siwezi kumfanyia kitu kama hiki isijekuwa ikawa ni plani moja wapo ya kutaka kumuangamiza Mwanaume nimpendae katika maisha yangu mmh kwanza inawezekana vipi Ducha kuweza kupambana na ukoo wa Mzee Ibnuwas wakati Chinoge bado yupo na vipi yule Ninja Ice? Ehee nishapata wazo kwanini hii dawa nisiende kumnywesha Chinoge ili nione kitatokea kitu gani juu yake? Kwanza hata akifa sio mbaya kitu kingine cha kujiuliza hapa je nitawezaje kumfikia kiumbe hatari kama Chinoge?’’
Binti Ozzi alijiuliza maswali mengi pamoja na kuwaza na kuwazua mwishoe akapata jawabu la majibu yake kuwa Chinoge yupo kwenye mahusiano ya kimapenzi na binti ajulikanae kwajina la Salome baada kufahamu hilo akakenua meno ya furaha na kuona kazi yake imekuwa nyepesi
************
Siku ya siku hiyo bwana mdogo Ducha alikuwa maeneo ya shule ya msingi Mbezi Beach akiangalia mpira
“oyaa wee dogo hutaki kucheza?’’
“mimi au?’’
“ndiyo wewe hapo’’
“nataka lakini sina jezi’’
“wee vua fulana hiyo kuhusu Jezi utapata kwani unacheza namba ngapi?’’
“namba saba’’
Basi Ducha akavua fulana na kuiweka pembeni akapatiwa Jezi namba saba mgongoni
“oyaa refa tunataka kufanya sabu’’
Yule jamaa aliyemtaka Ducha acheze akapaza sauti huku akipunga mikono juu kwakuwa mpira ulikuwa wa kurushwa sabu ikafanyika mtoto aliyetolewa alikuwa kachukia kishezi
“yani Mwalimu unanitoa mimi super star sio na kumuingiza yule Mkurungwa sijui umemuokotea wapi huko”
Yule mtoto alizungumza kwa udadisi
“una ustaa gani wewe zaidi ya kuleta ubishoo tu yani wewe na goli unakosa mpuuzi mmoja wewe embu angalia vyenga vile kudadeki’’
Mwalimu wa vijana wale alizungumza hivyo huku akitumbua mimacho kumuangalia Ducha aliyekuwa akichanja mbuga na mpira kufika sehemu akatisha kama anapiga shuti ajabu akatoa pasi ya kisigino aliyepasiwa naye hakufanya makosa akaachia zinga la shuti mpaka goli watu wewe kuingia kwa Ducha mpira ulichangamka balaa
“mwalimu kwani yule mtoto anaitwa nani?’’
Kuna mtoto alitoka mbio nnje na kuja kuulizia jina la Ducha Mwalimu wake kwanza akakuna kichwa maana hata yeye hamjui
”anaitwa Ducha Duchani’’
Jibu likatoka kwa Madebe aliyefika hapo naye kuangalia mechi hiyo ya mchangani baina ya watoto watokao Tegeta na hao wa Mbezi Beach kabra ya Ducha kuingia Tegeta walikuwa wanaongoza kwa goli tatu kwa moja sasa alipoingia Ducha ubao ukabadirika ikawa Tano kwa zile tatu
“Duchaaa huku huku Ducha’’
Basi walipolifahamu jina lake ukawa ni mwendo wa kuomba pasi tu uwanja mzima Ducha Duchaa
“mwalimu mbona yule mtoto akatiki wala hakabiki?’’
“akatiki kivipi inamaana umekuja kucheza mpira au kukata wenzako? Embu acha uzembe wako unamuachia anakupita kizembe pale yani misifa yote ile niliyokuwa nakupatia kuwa wewe ndiyo beki wangu bora kwenye timu hii ajabu leo hii unakuja kupigwa matobo na kuvishwa mikanzu unajiabisha kijana’’
“haya basi tufanye mi sio beki bora aingie umuonae beki bora mi nakwambia yule mtoto akabiki wala hakatiki’’
Kuonyesha kuwa kachukia akavua Jezi yenyewe na kuitupa chini wakati huku mpira ukiendelea hapa tunamuona bibie Salome akiandaa chakula muda kidogo akawasili Binti Ozzi kwenye muonekano ambao hawezi kuonekana kwa macho ya kawaida akapiga hatua kadhaa mpaka pale jikoni akakitoa kile kichupa na kuimimina ile dawa kwenye jagi ambalo ndani yake kulikuwa na juisi alishafahamu kuwa hiko kinywaji kimeandaliwa spesho kwaajili ya Chinoge baada kufanya yake akaitikisa kwa kuichanganya sawa Masikini ya Mungu Salome wala hakufahamu chochote kile muda kidogo kila kitu kilikuwa tayari chakula kilishaandaliwa mezani bibie akaingia Chumbani kwenda kumuamsha kipenzi chake
“baby hamka bwana chakula tayari’’
Salome alizungumza kwa kudeka Chinoge akaamka na kumkisi mpenzi wake wakaongozana na kuelekea sebureni kitu cha kwanza alichokifanya Salome ni kumimina Juisi kwenye glasi na kumnywesha funda kadhaa kipenzi chake hata hazikupita dakika mbili tokea ameze ile juisi Chinoge alianza kujiskia vibaya alijishika kichwani na kubana meno
“vipi tena mbona hivyo?’’
Salome aliuliza kwa uwoga
“yani Madebe wewe wa kunipiga mimi kweli wakati mi nilikushika kwa niya ya kutaka kukuzuia ili usiendelee kupigana,,,
Ilikuwa ni kumbukumbu ya tukio la Dada yake Chinoge alipopigwa kibao cha nguvu na Madebe kule Uwanjani
Ni moja kati ya kumbukumbu zilizoweza kupita kichwani mwa Chinoge kumbukumbu ambayo ikafatiwa naile siku ya yeye kuchomwa kisu na Ducha akakumbuka alivyopigwa na bibie Cynthia yani Bwana mkubwa Chinoge alikumbuka mambo mengi mabaya yaliyowahi kutokea nyuma pasipo yeye kuchukua hatua
“baby vipi tena kichwa kinakuuma au?’’
Pasipo kujibu lile swali la mpenzi wake Chinoge akasimama akatembea kuelekea chumbani hakupiga hata hatua mbili akadondoka chini chali na kuwa kimya Salome alipiga kelele kwa kuchanganyikiwa
Sehemu Ya 22
“yani Madebe wewe wa kunipiga mimi kweli wakati mi nilikushika kwa niya ya kutaka kukuzuia ili usiendelee kupigana,,,
Ilikuwa ni kumbukumbu ya tukio la Dada yake Chinoge alipopigwa kibao cha nguvu na Madebe kule Uwanjani
Ni moja kati ya kumbukumbu zilizoweza kupita kichwani mwa Chinoge kumbukumbu ambayo ikafatiwa naile siku ya yeye kuchomwa kisu na Ducha akakumbuka alivyopigwa na bibie Cynthia yani Bwana mkubwa Chinoge alikumbuka mambo mengi mabaya yaliyowahi kutokea nyuma pasipo yeye kuchukua hatua
“baby vipi tena kichwa kinakuuma au?’’
Pasipo kujibu lile swali la mpenzi wake Chinoge akasimama akatembea kuelekea chumbani hakupiga hata hatua mbili akadondoka chini chali na kuwa kimya Salome alipiga kelele kwa kuchanganyikiwa
Songa nayo
Sasa
“wee Salome nini tena kimemkuta mwenzako?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa mama mwenye nyumba aliyeingia chumbani humo akiwa kaongozana na baadhi ya majirani
“mi sijui mamaa”
”embu pisha kwanza”
Mama mwenye nyumba akamtaka Salome akae pembeni alianza kumkagua Chinoge kwa kusikilizia mapigo yake ya moyo akamshika kiganja cha mkono
”nenda kalete maji”
Akaomba aletewe maji yalipoletwa akayapokea na kumnyunyuzia Chinoge kichwani kisha akamnawisha usoni dakika si nyingi bwana mkubwa Chinoge alizinduka akapiga chafya mfurulizo
”pole sana baba yangu”
Alipewa pole na mama mwenye nyumba
”asante”
Chinoge aliitikia ile pole akanyanyuka na kwenda kukaa kwenye sofa muda kidogo Mama mwenye nyumba na wale wapangaji waliaga baada ya kujiridhisha kuwa mgonjwa Yuko sawa bin sawiya pale sebureni wakabaki wapenzi wawili
”mke wangu kipenzi unaweza ukaenda kuendelea na shukhuri zako nyingine acha mi nipumzike kwasasa”
”unapumzikaje sasa wakati chakula chenyewe ujala?”
”ohoo kumbe nilikuwa sijala haya fanya unipakulie nile”
Chinoge alizungumza kwa furaha na kumfanya Salome atabasamu basi chakula kikapakuliwa
”mmh hiyo juisi siitaki tena”
”haaa kwanini tena kipenzi changu?”
Salome aliuliza kwa mshangao
“au nimekosea kuitengeneza?”
Salome aliuliza huku akitaka kunywa yeye Chinoge akafanya haraka kumpokonya ile glasi juisi yenyewe yote akaimimina kwenye maji
”baby Sasa mbona unafanya hivyo? Jamani juisi yangu”
Salome alizungumza kwa kunung’unika
“nikuulize kitu kipenzi?”
“staki”
“basi kama utaki”
“ndiyo Staki wee utaimwagaje juisi yote ile kama ulikuwa huitaki si ungesema ningeenda kumpa Mama Tabu”
“kwani tatizo liko wapi kipenzi?”
Chinoge akauliza haliyakuwa akinyanyuka na kuelekea chumbani
”unaenda wapi sasa?”
”kulala”
”inamaana hata kula umesusa?”
Chinoge wala hakutaka kuendelea kuzungumza akaingia zake Chumbani japokuwa alionekana kujikaza kutokana nakile kinacho msumbua kichwani kwake binafsi hakuwa sawa kabisa
Salome alishindwa kuendelea kula kile chakula haliyakuwa yuko peke yake naye akanyanyuka na kuelekea chumbani
“baby nisamehe basi kama nimekuuzi”
Salome aliomba msamaha akajilaza kifuani mwa Chinoge alipojilaza tu! Chinoge akaupitisha mkono wake Shingoni mwa Salome palepale Bibie alinyong’onyea akapitiwa na usingizi mzito bwana mkubwa akaitumia nafasi hiyo kutoweka
Tukirudi huku uwanjani mpira ulikuwa tayari umeshaisha kulikuwa na shamra shamra za kushangilia ushindi wa kishindo walioupata unaweza kusema ni Come back ya maana kutoka goli tatu moja mpaka kushinda Saba kwa nne si kitu kidogo
”Ducha wee noma aisee unacheza kama Ronaldo unapiga vyenga kama Messi”
Basi kila mmoja alitoa pongezi kwa Ducha
Basi Ducha alivimba mbichwa huo kutokana na kumwagiwa sifa kemu kemu za kufananishwa na Wacheza soka mahiri hapa duniani
“sasa kijana uwe unakujaga mazoezini”
“sawa mkuu nitakuwa nafika bila kukosa”
Ducha akaitikia
“khaa yule jamaa vipi mbona kafikia kumpiga refa?”
Ilikuwa ni kauli kutoka kwa mtoto mmoja wapo aliyeweza kushuhudia refa aliyechezesha mechi hiyo akichezea kichapo kutoka kwa mtu ambaye usoni alikuwa kavaa Barakoa kivazi ambacho kimeshika hatamu kuvaliwa duniani baada Gonjwa hatari la Corona kuingia ile kauli ikawafanya wote
Wageuka na kuangalia songombingo hiyo nikweli Refa alikuwa akichezea vitasa japokuwa alionekana kujaribu kurudisha mashambulizi lakini mbele ya mtu yule hakuweza kuambulia kitu
”oyaa wee jamaa vipi mbona unatupigia mtu wetu?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa mmoja kati ya vijana mashababi kutokea timu hiyo ya Mbezi Beach swali likajibiwa kwa kijana yule kutandikwa ngumi moja tu iliyomfanya apepesuke na kujibamiza kwenye mti kama haitoshi akaongezewa zinga la teke Kama sio Madebe kuwahi kumdaka jamaa angedondokea Nondo ambazo zilikuwa zimepigiliwa zege
“kaka mkubwa embu mshuhurikie huyo”
Madebe akatakiwa kumdhibiti yule jamaa naye alimsogelea kwa dharau kitendo cha kumsogelea kiliweza kumkosti kwani
Jamaa alichumpa kwa kulibetua jiwe kubwa kiasi na kulipiga teke likatua usoni mwa Madebe na kumpasua Damu nyingi zilimtiririka
Ducha akajiandaa kuingilia maana aliona huyu mtu anatisha ile Barakoa si ikavuliwa
Mtu mwenyewe hakuwa mwingine bali ni bwana mkubwa Chinoge
Si Ducha wala Madebe wote walishtuka baada kuona muonekano wa Chinoge umebadirika kwanza ana Meno mawili marefu utasema reki
Huku macho yake yakiwa meusi tii yakifuka moshi
“kakaa tukimbie”
Ducha alipaza sauti akimtaka Madebe wakimbie binafsi alishaweza kufahamu kuwa Mwalimu wake kabadirishwa kiakili na pale alipo
Yupo kisasi zaidi si vinginevyo kuonyesha msisitizo Ducha alimshika mkono Madebe na kuanza kumvuta lakini Madebe hakuwa tayari kukimbia kisa tu Chinoge wakati yeye ni Komando wa kutumainiwa jamii itamchukuliaje iwapo atakimbia huku akiacha raia wakiuwawa
Bwana mkubwa Chinoge Alikuwa ameshachafukwa alimfata kwa kasi yule refa ikawa kufumba na kufumbua mtu kuzungurushwa kichwa akadondoka chini puuh
Madebe akatoa kitambaa na kujifunga sehemu yenye jeraha
Hata ngumi hakujiandaa kukunja alishtukia akipigwa na kitu kizito nyuma ya uti wa mgongo ilikuwa ni Nyundo iliyokuja kwa kasi Madebe alipepesuka huku akitema Damu kule kupepesuka aliongezewa na mateke ya Dabodabo
“kakaa,,”
Sauti ya bibie Mariam ilisikika ikiita hivyo huku akija mbiombio na kumfikia kumlalia Madebe aliyekuwa kalala chini akiugulia maumivu alifanya hivyo kama kumkinga maana Chinoge alishaipa ishara Nyundo yake ikite Shingoni mwa Madebe
Kule Mariam kumlalia mumewe kwa juu Nyundo yenyewe ikasita kufanya hivyo Ducha alionekana amesimama kwa mbaali akikodoa macho tu!
Chinoge akatoweka
“jamani mume wangu hiii,, msaidienii”
Mariam alilia kwa sauti huku akimtikisa mumewe aliyeonekana kuanza kupumua kwa shida watu walishajazana pale kuna wale waliokuwa wameuzunguka mwili wa Marehemu wengine wakawa wamekaa pembeni wakiulizana na kuzungumza hili na lile
“hatimae leo hii kaka mkubwa Madebe kakutana na kisingi cha mpingo. Yani kapigika kama vile mtoto”
”sio kisiki cha mpingo yule jamaa aliyekutana naye ni Jini”
”jini wapi wakati jamaa anaonekana wa kawaida tu! Au ulichanganyikiwa naile Barakoa yenye chata la mzimu?”
“sasa Binadamu gani anaweza kulibetua jiwe kubwa Kama lile Kisha akalipiga shuti kama vile mpira pasipo yeye kuumia?”
“usikute jamaa atakuwa kavaa viatu vya chuma”
”sio viatu vya chuma kudadeki yule ni Jini tu kitu kingine ile Nyundo ilitokea wapi?”
“khaa inamaana jamaa Alikuwa kashika Nyundo sio?”
“sio kuishika yani ile Nyundo sijui ilitokea wapi yani iliibuka ghafla tu! Na kufikia kumshambulia Brother pale yani mi nilivyoiona tu ile kitu ilibaki kidogo nijikojolee maana inatisha”
“Mmh wewe isijekuwa unatusimulia movie la Thor hapa yule jamaa mwenye Nyundo kubwa hivi?”
“wee kweli fala tulichokiona hapa mwanangu sio movie ni uharisia kabisa yani live bika chenga ningekuwa na Simu yangu kubwa ningeshot video sema nimeiacha nyumbani kwenye chaji.
”kwakweli mi hata siamini”
”basi usiamini kwani umelazimishwa”
Basi pale kila mmoja alikuwa anazungumza la kwake
“mi nilishawahi kumwambia Akida maswala ya kujifanya kimbelembele kuchezesha mechi za mchangangani sio kitu kizuri ipo siku huu mchezo utakuja kumtokea puani.
Mwenzangu wala hakutaka kunisikiliza Angalia sasa umauti umemfika”
Alizungumza kwa sauti ya majonzi mmoja kati ya ndugu wa yule kijana aliyeuwawa akili yake iliwaza kuwa mtu aliyemuua ndugu yake ni mmoja kutoka kwenye timu iliyofungwa hawakufahamu kama Muuwaji aliwasili hapo akiwa na mambo yake.
”baby fumbua macho yako hiiiii”
Mariam aliendelea kulia muda kidogo gari za kijeshi zipatazo tatu ziliweza kuwasili pale wakashuka wazee wakazi wakiwa na mitutu kitendo pasipo kuchelewa walimbeba mkuu wao na kumpakiza kwenye Gari
Mariam alipotaka kupakia akazuiwa Gari zikaondoka kwa kasi ndugu jamaa na marafiki wa Marehemu nao wakafanya taratibu za kuubeba mwili wa yule kijana wao
Mariam alirejea nyumbani kwake haliyakuwa akiwa kachanganyikiwa walinzi walijaribu kumtuliza kwa kumbembeleza pamoja na kumtoa hofu kitendo cha mama yao kulia kiliwauma Sana kina
Ahmad walimuangalia mama yao kwa huruma alichokifanya Kitwana mtoto mdogo kabisa ni kuingia jikoni akatoka haliyakua kashika kisu mkononi
“wee Kitwana unaenda wapi sasa huko? Embu rudi huku”
Mariam alipaza sauti kumwita mwanaye
“siwezi kurudi Mimi naenda kumchinja chinja mtu aliyempiga Baba yangu haiwezekani baba angu apigwe hiiiiiii haaaa”
Kitwana alizungumza hivyo huku akiangua kilio
“Ducha embu nenda kamrudishe Kitwana hapa!”
Ducha alikuwa kaegemea ukuta uso kaunyanyua kuangalia mawinguni alishtuliwa na sauti ya Mariam akimtaka akamzuie Kitwana Ducha pasipo kuchelewa akafanya hivyo kwa kumfata Kitwana
”Duta usinisogelee nitakuchinja kudadeki zako nasema usinisogelee “
Kitwana alipiga kelele kumwambia Ducha huku akimnyooshea kile kisu siku zote inajurikana Kitwana akishika silaha ni vigumu kumzuia hasa awapo na hasira mtu pekee anaemuwezea ni Baba yake Sasa kutokana na Mariam kusimuliwa kuwa Ducha ana talenti kubwa ya mapigano ndipo akataka kuiona moja ya hiyo Talenti je ataweza kumzuia Kitwana
Maana kuna siku yeye mwenyewe alichomwa na Bisibisi siku hiyo Kitwana sijui nani alikuwa kamtibua huko mtaani akarudi nyumbani kwao na kubeba Bisibisi alipojaribu kumzuia alijituta hata kumzaa bahati nzuri Madebe alikuwepo.
“Bucha ntakuua hiyaaa”
Kitwana alipiga kelele huku akitaka kumchoma kisu cha Tumbo Ducha aliyezunguka kwa kasi na kuukita mkono wa Kitwana kisu kikadondoka chini Kitwana akashtukia akipigwa zinga la kofi lilimpata vyema shavuni
“yalaaa mama Duta kanipigaa hiiiiiiii”
Kitwana alilia huku akirejea kwa mama yake akakaa chini kuna mda anamwita Duta mara Bucha ili mradi tu awe kapatia
Mariam alimuangalia Ducha haliyakuwa akitabasamu
********
Bwana mkubwa Duchani bado alikuwa amefungiwa kwenye kichumba kidogo chenye ubaridi wakutisha ndani yake aliugulia maumivu pamoja na kupiga kelele za kuomba msaada lakini hakuna kiumbe chochote kilichoweza kumsikiliza
Walinzi wa Ibnuwas walikuwa wametanda Kila kona kwa kukizunguka chumba hicho cha mateso Duchani alibaki akihesabu siku za yeye kutoweka ulimwenguni
Alijiuliza maswali mengi Sana kuhusu Ukoo wake wenye nguvu na uwezo wa kutosha
Kwanini wamemtelekeza kwa kipindi chote hicho tokea atekwe hakuna jitihada zozote zinazofanyika kwa yeye kuja kuokolewa? Kama kulia alilia kama kelele alipiga mpaka sauti imemkauka
Mwisho akapata jibu huwenda wamemtelekeza kisa kuzaa na Mwanamke wa kibinadamu kibaya zaidi nnje ya ndoa
Huku nnje shukhuri zilikuwa zikiendelea Kama kawaida
Hata upepo ulipoanza kuvuma kutokea upande wa Kaskazini hakuna hata Jini mmoja aliyekuwa na habari maana walifahamu ni mtu wao.
walikuja kushtuka baada bwana mkubwa Chinoge kuibuka na kuanza kushambulia walinzi waliokuwa wanalinda upande huo
“vipi tena huyu si mwenzetu mbona amekuja kwa shari?”
Baadhi ya majini wanaomfahamu Chinoge waliulizana kwa wakati
Wakajiweka tayari kukabiliana naye
“Hafidhi mjukuu wangu unafanya nini wewee? Mbona unaangamiza watu wako?”
Bibi mtu alienda kuitwa alipowasili pale hakuweza kuamini macho yake baada kumuona Chinoge akiwaangamiza watu wake alipaza sauti kuuliza
Chinoge alikuwa kawakaba majini wawili akawanyongelea mbali akapiga hatua kumfata Bibi yake
Ghafla alishtukia akirudishwa nyuma baada kupigwa kifuani na kijinga cha Moto Ibnuwas naye alishawasili akamkinga Mama yake
Chinoge alirudi nyuma mita kadhaa akajipangusa kifuani akanyoosha mikono yote miwili
Ibnuwas naye alijikuta akirushwa juu
Alipotua chini hakuwa na Miguu
Nyundo zilishafanya kazi
Zikarudi mikononi mwake yani nyundo zake unaweza kusema ni Automatiki akinyoosha mkono mmoja inakuja moja miwili zinakuja zote
Ibnuwas alikuwa kalala chini haliyakuwa akitapatapa hakuweza kusimama kutokana na Miguu yake kusambaratishwa vipande vipande
“Hafidh,,,,
Bibi mtu sijui alikuwa anataka kuzungumza kitu gani alishtukia akipigwa na Nyundo ya tumbo iliyomfanya ashindwe kuzungumza Akajikaza na kuanza kurusha makombola ya Moto kumuelekezea Chinoge aliyekuwa akizunguka kwa kasi na kufanya yale makombola yazimwe na ule upepo
Chinoge akachumpa kwenda juu
Akatua chini kishindo kizito kilitokea na kumfanya Bibi yake apeperushwe juu kama vile kishada
Nyundo ikaenda kumshusha kwa kukita kifuani
Masikini wee Bibi wa watu alifikia kujibamiza sehemu mbaya
Alibaki kuhema juu juu.
Nyundo nyingine ikataka kukita kichwani Chinoge akawahi kuizuia kwa kuidaka
“muiuwe huyo unasubilia nini Sasa?”
Sauti ya Ozzi ilisikika ikimwambia hivyo
”hapana mjukuu wangu usimsikilize huyo binti wa Kishetani Hafidhi kumbuka bila mimi leo hii usingekuwa na uwezo huo tafadhari usiniuwe”
Bibi mtu alijikaza kuzungumza hivyo
Chinoge akaiachia ile Nyundo kwa kuielekeza kwenye kile kichumba alichofungiwa Duchani ikakisambalatisha kwa kukivunja vunja akapiga hatua kumsogelea Duchani aliyekuwa kajikunyata kama vile kifaranga cha kuku kilichonyeshewa na Vua
Alipomfikia akamshika na kutoweka naye alipotoweka Malkia Kaisi akiwa na Jeshi lake wakawasili
Miili ya majini ilikuwa imelaliana hovyo kuna wale waliopoteza maisha na waliojeruhiwa kelele nyingi zilisikika kutoka kwa majini ambao walikuwa wamejeruhiwa walipiga kelele za kuomba msaada Malkia Kaisi akiwa na jeshi lake waliangaza macho huku na kule yote ilikuwa ni katika kumtafuta Bibi mtu kwa maana yeye ndiye wa umuhimu kuliko majini wote
”mukuu mbibi muhuyu huku”
Mmoja kati ya majini alipaza sauti kumwambia Malkia Kaisi akimaanisha kuwa mkuu Bibi huyu huku
Malkia Kaisi alikimbilia mbio mbio ile sehemu nikweli Bibi mtu alikuwa kalala chini haliyakuwa akiwa hoi taabani
“ohoo Mungu wangu”
Malkia Kaisi alitamka hivyo haliyakuwa akiinama kwaajili ya kumnyanyua Bibi yule kwake nikama mama kwa maana Ibnuwas na Kaisi ni watoto wa Mamkubwa na Mdogo Yani Ibnuwas mama yake ni Mkubwa
Wakati anamnyanyua mara ikaonekana taswila ya Ninja Ice akitabasamu
Bibi mtu alipata nguvu ghafla za kusimama mwenyewe pasipo kusaidiwa na mtu akakaza macho kuiangalia ile taswila iliyokuwa juu mawinguni
“wee mwehu unacheka cheka kitu gani? Umefurahi kuona alichotufanyia mpuuzi mwenzako ehee washenzi kabisa nyie”
Bibi mtu alizungumza kwa hasira huku akinyooshea kidole ile taswila.
Ninja Ice alizidi kutabasamu mwisho akaangua kicheko kisichokuwa na sauti alionekana akicheka mbavu hana
”wee cheka tu! Embu muangalie baba yako tayari kashakuwa kilema hana Miguu tena”
Bibi mtu aliendelea kuzungumza akanyoosha mkono kumuonyeshea Ibnuwas aliyekuwa kajikunyata pale chini
Malkia Kaisi alishtuka pindi alipoweza kumuona kaka yake
“kakaaa,,jamani kaka yanguu”
Alimkimbilia na kumuinamia ajabu ile taswila wala haikujari ndiyo kwanza iliendelea kucheka halafu ikatoweka ilipotoweka mara akaonekana yule binti ambaye alimpatia Mzee wa Nyapu kipawa cha Uninja Ice akija kwa mwendo wa madaha yani tembea yake unaweza ukasema akanyagi chini.
Unajua mpaka sasa huyu binti haijurikani katokea sayari ipi sema muonekana wake ni kama Malaika
Alipowasili pale Bibi mtu na wafuwasi wake wote walitoa heshima kwa kuinamisha nyuso zao chini naye akafanya hivyo kama ishara ya kuitikia
Kisha akanyoosha mkono kuelekezea sehemu ambayo kulikuwa na mifupa pamoja na nyama nyama za Miguu ya Ibnuwas aliponyoosha tu Upepo mkali ulianza kuvuma pale ile mifupa na zile nyama nyama zilianza kujikusanya na kujiunga ikaenda kujipachika kwenye magoti ya Ibnuwas na kujiunga
Ibnuwas hakuweza kuamini aisee kama amerudishiwa miguu yake
”unaweza ukasimama sasa”
Yule binti alizungumza hivyo huku akipaa juu
Alipofika sentimita kadhaa kule juu akapuliza upepo kuja chini ikawa kufumba na kufumbua majini wote waliokuwa wameuwawa na kujeruhiwa kuwa wazima
Si Bibi wala Malkia Kaisi aliyeweza kuamini hakika binti yule alionekana kuwa na uwezo wa Ajabu kupita kiasi
”khaa umewezaje kufanya yote haya?
Ibnuwas alimuuliza yule binti
Ambaye alibaki kutabasamu pasipo kujibu swali
“yani Chinoge wa kutushambulia sisi kweli mtoto niliyemkuza na kumtukuza kwakila kitu!”
”hapana usizungumze hivyo embu chekecha akili yako na uwezo wako uweze kubaini kitu juu ya mjukuu wako”
Yule binti alizungumza hivyo akimtaka Bibi asianze kumrahumu Chinoge pasipo kutafakari
Bibi mtu akatumia uwezo wake wa kijini
“yani,yani huu ukoo wa Duchani sijui ukoje wameiteka akili ya mjukuu wangu pumbavu kabisa hawa”
Bibi mtu alizungumza kwa jazba baada ya kubaini kile ambacho alifanyiwa Chinoge taswila ya Video ikaja mbele yao ikawa inaonyesha ile siku ya kikao ambacho Binti Ozzi alikabidhiwa ile Dawa mpaka alipobadirisha maamuzi na kwenda kumpatia Chinoge
Kila mmoja alisikitika
”kwanini wameamua kumfanyia hivi?”
Ibnuwas aliuliza swali ambalo hakuna aliyeweza kumjibu
“kitu cha kujiuliza kwasasa ni nani atakaeweza kumzuia huyu kichaa?”
“hakuna atakaeweza kumzuia kumbukeni ya kwamba Chinoge anajeshi kubwa la Masokwe ambao hawafi wala kudhurika na silaha ya aina yoyote ile.
Tukiachana na zile silaha zake hata Ninja Ice asingeweza kumdhibiti si mnakumbuka Ninja Ice aliwahi kupigwa kwenye mpambano wao mpaka Mimi nilikuja kumuongezea uwezo?”
“ndiyo nakumbuka”
Bibi mtu aliitikia niule mpambano ambao yeye aliingilia kati na kuwatenganisha
“je wewe huwezi ukamdhibiti?”
Malkia Kaisi alimuuliza yule binti
“hapana siwezi”
Binti akakataa
“kwanini Sasa wakati unaonekana unauwezo mkubwa kupita sisi”
”uwezo niliobarikiwa ni kutibia Viumbe wa aina yote kuwapa nguvu kitu nilichonyimwa ni kupigana tu! Siwezi na sitoweza kamwe”
“sasa kama huna uwezo wa kupambana unajilinda vipi na Maadui zako watokeapo ghafla kutaka kukushambulia?”
“ninao walinzi wenye nguvu na uwezo wa kutosha naweza kusema mmoja kati ya walinzi wangu ni zaidi ya Chinoge na Ninja Ice”
“khaa Sasa kwanini usimtumie huyo kumdhibiti Chinoge?”
”je unataka mlinzi wangu auwawe?”
“sasa atauwawa vipi wakati uwezo wake ni mkubwa?”
”hakuna kitu kama hicho. Chinoge kwasasa kawa ni Jiniasi asieweza kushikika Nyundo yake moja inauwezo wa kunisambalatisha Mimi na walinzi wangu wote”
”daah Sasa tutafanyaje aisee”
”sio mtafanyaje hapa njia ya kumdhibiti ni moja tu!”
”njia ipi hiyo?”
(NYETO NYETONI)
Binti alizungumza kauli moja tu! Akatoweka zake
”Nye,,,Nyeee,,,to”
Ibnuwas alijaribu kulitamka hilo neno
Bwana mkubwa Chinoge baada kutoweka na Duchani pale alimpeleka sehemu moja hivi ni sehemu ile ambayo Mwanzoni kabisa tuliona Ducha akifundishwa na Mwalimu wake wa awali aliyepoteza maisha baada ya kuwawa na Duchani. Sijui kwanini alimfikisha sehemu hiyo akamlaza juu ya mbao kubwa iliyoandaliwa kama kitanda halafu Chinoge akapiga mruzi wa kumwita yule Sokwe mwenye kutembea nakile kibuyu chenye dawa ya maajabu
Ajabu zilipita dakika kama tano Sokwe hakuweza kutokea kitu ambacho kilimshangaza Sana Chinoge maana sio kawaida kutotokea ikabidi arudie kumwita licha ya kumwita kwa mara ya pili Sokwe hakutokea
”ohoo Shit!
Akapiga mruzi mara ya tatu safari hii upepo mkali ulianza kuvuma si akaibuka Ducha mkononi akiwa kashika kile kibuyu
Chinoge alimuangalia Ducha kwa jicho kali huku akinyoosha mkono ili apatiwe kibuyu hiko
Ducha akapiga hatua za Tahadhari kumsogelea Chinoge akampatia kile kibuyu ambapo kilichukuliwa kama vile kinapokonywa
Duchani akatakiwa kufumbua mdomo akanyweshwa ile Dawa haikuchukua sekunde hata kumi ilianza kufanya kazi ndani ya Dakika tatu Duchani alijishangaa kujiona yu mzima wa hafya
”bila Shaka kwasasa ushapona naomba uniulie yule”
Chinoge alizungumza hivyo kumwambia Duchani akamtaka amuulie Ducha kitu ambacho kilimshtua Duchani
”khaa kwanini unataka nimuuwe Kijana wangu sipo tayari kufanya hivyo”
Duchani alizungumza hivyo
Alichokifanya Chinoge kilikuwa ni kitendo cha ghafla mno kwenda kumtandika zinga la teke Ducha aliyebimbilika na kwenda kujibamiza kwenye mawe makubwa
Ducha akainuka kwa staili ya kuchenji muonekano wake maana alifahamu kuwa akizubaa atauwawa akawa katika umbo la Ninja Ice akazunguka kwa kasi kumfata Chinoge hata hakuweza kumfikia alijikuta akirushwa juu baada kutandikwa teke lingine
Ambalo lilimuingia ile kisawasawa
Akafatwa kulekule juu na kushikwa Shingoni akawa amekabwa kwa kuning’inizwa
Akashushwa mpaka chini kwa kubamizwa kwenye mbao
Duchani akaona ehee Kijana wake anaweza akauwawa mbele ya macho yake
Akachumpa na kwenda kumvamia Chinoge akabimbilika naye alipokuja kumuachi Baba na mwana wakawa wamekunja ngumi kumzunguka Chinoge wakapeana Ishara ya kumshambulia
Ducha alianza kuachia zile silaha zake za nyota hakuna hata Nyota moja iliyoweza kumfikia Chinoge maana Nyundo zake zilikuja kwa kasi na kuanza kuzizuia zile nyota
Zikawa zinasambalatika
Kwa mara nyingine Chinoge alichumpa na kwenda kumtandika Ducha teke la Shingo masikini Ducha alipepesuka kwa mawenge
Nyundo ikaja kukita kwenye sikio la kushoto mawasiliano yakawa sio tena
Maana aliona Dunia inazunguka
Duchani alitumia uwezo wake kwa kumkumbatia Chinoge ili asiendelee kumshambulia Kijana wake
“Ducha kimbia mwanangu”
Alipiga kelele akimtaka Ducha akimbie huku akiwa kamshikilia Chinoge ile kisawa sawa kumbe ukimshika Chinoge Nyundo zake hazifanyi kazi zilikuwa zinaambaa ambaa tu!
Ducha alikuwa kalala chini damu nyingi zilikuwa zinamtoka aliweza kushuhudia Baba yake akiuwawa kwa kung’olewa kichwa yani Chinoge alivyojitoa mikononi Mwa Duchani akakishika kichwa na kukizungusha kama haitoshi aliking’oa aisee
Ducha alitetemeka kwa uwoga akatoweka
_____________
“umefanya nini Ozzi ni upumbavu waaina gani ulioutenda binti yangu?”
Mzee Makanga alizungumza huku akimnasa makofi ya nguvu binti yake kisha akaamuru Ozzi akamatwe na kwenda kufungiwa kwenye chumba cha mateso
“babaa kwanini unantendea hivi mwanao?”
Ozzi aliuliza huku akikukuruka ili aweze kujinasua kutoka mikononi mwa walinzi waliomkamata
“Makanga embu achana na huyo binti yako siku zote maji yakimwagika hayazoleki Ozzi ni mtoto mdogo sana asieweza kutambua kile kilichopo mbele yake
Kijana wetu Duchani amenyanyasika kupita kiasi ameuwawa kikatiri mwili wake umechezewa na kudharirishwa vya kutosha embu angalieni anachokifanya Chinoge hii sio haki kabisa,
Chinoge amekuwa ni mshenzi wa washenzi ni unyama waina gani kamtendea Kijana wetu?”
Mmoja kati ya wazee wa Ujinini alizungumza kwa hisia huku machozi yakimtiririka Majini wote walikaza macho yao kuangalia tukio zima la kuwawa kwa Duchani
Alionekana Chinoge akikipiga danadana kichwa cha Duchani Kisha akawa anapasiana na Nyundo zake utasema watu watatu wanacheza kodroo walikichezea kile kichwa kisha Chinoge akakifata kiwiliwili cha Marehemu akafanya kukisimamisha ikawa wanakipiga kile kichwa kuelekezea kwenye kiwiliwili
“wee Mshenzi kwanini unaufanyia hivyo mwili wa Kijana wangu? Ipo siku nitakuja kukuua kwa mkono wangu”
Mzee Makanga alizungumza kwa uchungu vitendo alivyokuwa anavifanya Chinoge juu ya mwili ule ni unyama wa kupitiliza
“kwasasa Chinoge hafai amekuwa ni kirusi chenye kuangamiza kila kiumbe kiitwacho Jini”
Yule mzee alizungumza hivyo
“kwanza samahanini Sana wazee wangu na ndugu zangu kwa hiki kilichoweza kutokea ila naomba nipatiwe nafasi ya mwisho ya kwenda kumuangamiza huyu Mshenzi”
Ozzi alizungumza hivyo na kufanya Majini wote wamuangalie yeye
”hivi unadhani swala la kwenda kumuangamiza Chinoge ni sawa na kunywa damu ya paka embu nenda kampatie Matibabu Ducha maana naye haliyake ni mbaya
Yule mzee alizungumza hivyo
”hali yake ni mbaya kivipi yani?”
Ozzi aliuliza alichokifanya yule mzee ni kulirudisha lile tukio nyuma kidogo ndipo wakaweza kuona jinsi Chinoge akitaka kumuangamiza Ducha
”inamaana Chinoge amekuwa ni adui wakila mtu! Yani mpaka Ducha kamshambulia?”
Mzee Makanga aliuliza kwa mshangao
”kama nilivyoweza kuelezea hapo awali kuwa Chinoge kwasasa anauwa na kushambulia kila kiumbe kiitwacho Jini kwake yeye ni adui hii yote tumesababisha sisi wenyewe na hatuna budi kupambana kwa pamoja
Vinginevyo wote tutaangamia kama utitiri waunguzwapo kwa moto
Twendeni tukaungane na wenzetu hii ni vita vitani.
*********
Siku mbili ziliweza kupita hali ya bwana mkubwa Madebe ilikuwa bado ni mbaya ikabidi asafirishwe kupelekwa nnje ya nchi
Kwa upande wa Ducha naye hali haikuwa hali kabisa maana kuna muda akikaa hua atakohoa na kutapika damu kitu ambacho kilimuogopesha Sana bibie Mariam akafanya haraka kuwasiliana na Mwanaidi ambaye alifika na kumchukua mdogo wake
Ducha akarudishwa nyumbani kwao hali yakuwa akiwa hoi taabani
Siku moja Ducha akiwa chumbani kwake amejilaza kitandani akatembelewa na bibie Ozzi
“pole sana kipenzi kwa yote yaliyokukuta”
Pasipo kutoa salamu Ozzi alizungumza hivyo Ducha alikaza macho kumuangalia tu
“pia nisamehe Mimi kwa maana ndiyo msababishaji wa yote haya”
”unamaanisha nini kuzungumza hivyo?”
Ducha akauliza huku akijiziba mdomo ili asiweze kukohoa ikabidi Ozzi amsimulie kila kitu hata akumalizia kuzungumza alishtukia kitu kizito kikimpitia kwa hewa na kwenda kujibamiza ukutani kilikuwa ni kisturi kilichorushwa na Ducha
”nilijua ni jinsi gani utanichukia ndiyo maana nikatanguliza kuomba msamaha. Ducha nisamehe mimi”
Ozzi alizungumza huku akipiga magoti na kukinga viganja vya mikono yake ni ishara ya kuomba msamaha
Ducha alimuangalia Ozzie kwa ghadhabu
”inamaana huwezi hata kuzungumza
Ducha nitamkie kauli yoyote ile ili niweze kuisikia tena sauti yako”
Ozzie alizungumza kwa sauti yenye kuambatana na kwikwi
Ducha alionekana kujikakamua ili aweze kuzungumza lakini wapi mwishoe damu zilianza kumchuruzika mdomoni na Puani kauli pekee aliyoitamka niile ya kumuuliza Ozzie unamaanisha nini kuzungumza hivyo kitendo cha Ducha kutapika Damu binti Ozzi akafanya haraka kwenda kumshika Ducha begani ikawa kufumba na kufumbua kutoweka naye
Hapa tunamuona bwana mkubwa Chinoge akiwa amekaa chumbani kwake akichezea simu alionekana kuwa sawa bin sawia muda kidogo akawasili bibie Salome na kumpatia bahasha ambapo Chinoge aliipokea na kuifungua ndani ya ile bahasha kulikuwa na karatasi kadhaa
Chinoge alizitupia macho kwa dakika kadhaa wakati huo Salome alikuwa kaichua simu ya Chinoge na kuanza kuperuzi
”mmh”
Salome alisikika akighuna sijui aliona kitu gani kwenye simu
“hivi baby mtu kama huyu utamsaidiaje yani kiushauri?”
Salome aliuliza huku akimsogezea simu Chinoge ili aone kilichoandikwa
”subiri kwanza nimalizane na hizi Document
Inamaana pale unapofanyia kazi kunavunjwa sio?”
Alizungumza hivyo Chinoge kisha akauliza swali
“ndiyo walivyosema kuwa pale lazima pavunjwe ili kupisha upanuzi wa barabara”
”na vipi kulipwa fidia?”
“kuhusu swala la kulipwa fidia kwakweli sijajua tulichoambiwa kila mmoja aende Serikali ya mtaa akiwa na hizi karatasi”
Salome alizungumza hivyo Basi Chinoge akaipokea ile simu na kuanza kuusoma ule ujumbe
Naombeni msaada wenu ndugu Zanguni mimi ni binti Mwenye umri wa miaka kumi na Tisa. Mzaliwa wa Njombe nimezaliwa katika familia ya kimasikini sana
Kutokana na umasikini wetu nimetaftiwa kazi za Ndani jijini Dar es Salaam maeneo ya Namanga mabosi wangu ni Wahindi kitu kilichonifanya niombe msaada kwenu ni kutokana na mateso na manyanyaso niyapatayo kutoka kwa mke wa Bosi wangu yani najitahidi sana kufanya kazi zangu lakini Mama akija analalamika na kusema nirudie tena kufua nguo zote kwa maana hazijatakata zinatoa harufu Mashine za kufulia zipo hataki nizitumie akidai mikono ninayo nikipika Chakula anakimwaga anaweza kumwaga ilimradi tu mimi nisipate mda wa kupumnzika pia anatuma tuma kitu hata kama kipo miguuni pake bado atakuita uche kazi yako uje umpe nikichelewa hata sekunde moja naangushiwa kipigo ananijeruhi kwa mikucha yake mirefu
jambo ambalo linaukwaza sana moyo wangu na kunifanya nijutie kuzaliwa katika familia duni isiyo na uwezo pia kwa sasa sina Baba nna mama tu na mama yangu anaishi na Baba yangu wa kambo ambaye ni mkali alishawahi kunibaka ndio sababu ya mm kuja kufanya kazi za ndani
lakin huku nako nateseka ila inanibidi kuvumilia yote maana sina pa kwenda
Muda mwingine natumikishwa kingono pindi wanapokuja wageni wake wenye kunihitaji kimapenzi
Nafosiwa kukizi haja zao??????????
Post iliishia na emoji ya binti akilia
Chinoge alikunja ndita
Sehemu Ya 23
nizitumie akidai mikono ninayo nikipika Chakula anakimwaga anaweza kumwaga ilimradi tu mimi nisipate mda wa kupumnzika pia anatuma tuma kitu hata kama kipo miguuni pake bado atakuita uche kazi yako uje umpe nikichelewa hata sekunde moja naangushiwa kipigo ananijeruhi kwa mikucha yake mirefu
jambo ambalo linaukwaza sana moyo wangu na kunifanya nijutie kuzaliwa katika familia duni isiyo na uwezo pia kwa sasa sina Baba nna mama tu na mama yangu anaishi na Baba yangu wa kambo ambaye ni mkali alishawahi kunibaka ndio sababu ya mm kuja kufanya kazi za ndani
lakin huku nako nateseka ila inanibidi kuvumilia yote maana sina pa kwenda
Muda mwingine natumikishwa kingono pindi wanapokuja wageni wake wenye kunihitaji kimapenzi
Nafosiwa kukizi haja zao
Post iliishia na emoji ya binti akilia
Chinoge alikunja ndita
Songa nayo
Sasa
“ehee baby mwenzako kuna kitu nimekikumbuka embu Subiri kwanza nakuja Sasa hivi”
Salome alizungumza hivyo akasimama na kutoka nnje Chinoge bado alikuwa amekunja ndita kuonyesha ni jinsi gani kachukia
”jamani majirani uwiii Salome jamani umefanya nini?”
Sauti ya mmoja kati ya wapangaji akilia huku akilitaja jina la Salome ndiyo iliyomshtua bwana mkubwa Chinoge akatoka chumbani mbiombio hakuweza kuamini macho yake baada kumuona Kipenzi chake kalala chini
“kitu gani kimemtokea jamani embu pisheni”
”mi hata sijui maana nilikuwa zangu chumbani nikawa natoka ili nielekee msalani ile natokezea tu! Ukumbini ndiyo nikashtuka kumuona Salome akiwa kalala hapa halafu kulikuwa na mtu kamsimamia pembeni yake”
Yule mpangaji alizungumza hivyo
”yuko wapi huyo mtu?”
Mpangaji mwingine akauliza wakati huo Salome alishafunikwa na shuka mwili mzima kumbe tayari alishapoteza maisha yani kiutani utani tu! Alimuaga mpenzi wake kuwa Subiri narudi Sasa hivi kumbe ndiyo kwa heri
Chinoge alikuwa akibubujikwa na machozi alikaa pembeni kwa kuegemea ukuta muda kidogo polisi walifika na kuingia ndani
Walianza kufanya uchunguzi wao pamoja na kumuhoji yule mpangaji pamoja na Chinoge
Mwili wa Marehemu ukabebwa na kupelekwa hospitali kwaajili ya uchunguzi
“pole sana baba yangu siku zote mipango ya Mungu haina makosa”
Mama mwenye nyumba alitoa pole kwa Chinoge simu zilipigwa kwa ndugu wa Salome ambapo waliweza kufika
Yule mpangaji alichukuliwa na polisi kwaajili ya mahojiano kamili ikawa kila akiulizwa ni mtu gani huyo? Yeye akawa anajibu kuwa hamjui maana sura yake ilikuwa ni ngeni machoni mwake.
“sasa kama humjui inawezekana ikawa wewe ndiyo mshukiwa namba moja wa tukio hili”
“hapana afande Mimi sihusiki kwa lolote lile”
“kama uhusiki basi tutajie ni mtu gani huyo?”
”sasa kama simfahamu nawezaje kumtaja?”
“Afande Mwakanyege”
”naamu mkuu”
”kamata hii weka ndani”
Basi afande Mwakanyege akaja kumchukua yule mpangaji na kwenda kumfungia Selo
Ndugu zake Salome walijigawa wengine wakaelekea hospitali wakati wengine kituo cha polisi
Mwili wa marehemu ulipochunguzwa ikaonekana amefariki kutokana na Mshtuko
”kitu gani kilichosababisha Dada yangu kupatwa na Mshituko wakati enzi za uhai wake hakuwahi kuwa na tatizo lolote la Presha si ya kupanda wala kushuka?”
Kaka yake Salome alizungumza hivyo wakati wakiwa ndani ya Hospitali
”siku zote Ugonjwa unapoamua kukuvaa hauwangalii historia yako kitu kiitwacho Mshituko humtokea mtu yoyote yule sio mpaka awe mgonjwa wa presha”
Daktari akatoa ufafanuzi
Yule mpangaji aliachiwa huru mwili wa Marehemu ukachukuliwa na ndugu zake
Kama ujuavyo tena Uswahili hakukosi kuwa na vijimaneno ndivyo ilivyokuwa kutoka kwa baadhi ya majirani kuanza kuteta kuwa Mama mwenye nyumba ile ni Mchawi tena Mwanga wa kutupwa itakuwa wapangaji wake anawaweka misukule maana juzi juzi tulimzika
Yasri yule mtoto wa muuza Samaki wabichi
Tukamzika yule kijana Mzuri mzuri leo hii Tena anauwawa Salome
“tatizo lako Ashri wewe kitaani umehamia juzi tu! Humjui vizuri yule bi mdashi ni noma kwa Uchawi”
”wee umejuaje kuwa ni Mchawi kama nawe sio Mchawi mwenzake?”
”wee fala nini kwani kumjua Mchawi mpaka nawe uwe Mchawi?”
“ndiyo maana yake”
”basi tufanye yule Mmama ni mwenzako haiwezekani umaindi kisa kumtaja kuwa ni mchawi”
“mi sijari wala nini”
Ashri alitamka hivyo akasimama na kuondoka zake
”yani kale kajamaa sijui
kakoje yani kitu kidogo tu anamaindi”
”usikute yule anamla yule Mmama ndiyo maana kachukia”
”ohoo kumbee Ashri mtu mbaya wakupenda mijimama ehee?”
”ehee ndiyo zake anapenda kulelewa kama nini”
”sema nini mazee twenzetu Msibani”
Basi vijana wale waliokuwa wakimjaji mama mwenye Nyumba wakanyanyuka na kuelekea Msibani kumbe familia ya Marehemu Salome ilikuwa inaishi mitaa kadhaa tu kutoka hapo
Ashri naye baada kutoweka pale kijiweni akiwa amechukia akaelekea Ghetto kwake
”whaoo Ashri wangu huyo”
Alilakiwa kwa furaha siku zote lisemwalo lipo nakama halipo basi laja Ashri alipokelewa kwa furaha na Mama mwenye nyumba aliyekuwa amejilaza kitandani kwa staili ya kifudi fudi na kufanya matako yake makubwa yabiduke kimtindo
Sijui Ashri aliacha mlango wake wazi au vipi maana ile kuufungua tu anamkuta Mtu kajilaza kitandani Basi Ashri akavua shati na vest akabaki kifua wazi
Mwili wake ulionekana kuwa ni mtu wa mazoezi kwa maana alikuwa na Sixpack kifua kilichotanuka mikono iliyojazia
Akavua na suruwali akabaki na Boxa
Iliyooneka imetutumuka kwa mbele
Ashri akapiga hatua kadhaa na kwenda kujipweteka Sofani mama mwenye Nyumba akaona usintanie akajinyanyua pale kitandani na kumfata Ashri pale Sofani akamkalia
Yani alipakatwa kama mtoto sema sasa hiyo staili ya kupakatwa ilikuwa yenyewe haswaa. Ashri alikaa kwa kuulaza mgongo wake kidogo hapo mtoto wa kiume alikuwa na boksa pekee iliyotuna ile kinomanoma mama mwenye Nyumba akajilaza kiubavu kisha miguu yake aliikunja,ule mguu mmoja wa Ashri ulipita katikati ya mapaja ukizingatia mama mtu alijibakiza na taiti pekee iliyombana na kukifanya kitumbua chake kichoreke vyema na kushawishi hasa
Vidole vyake laini vilikuwa vikimpitia Ashri kifuani mwake taratibu mpaka kidevuni palipo na ndevu za kichokozi, jamaa alikuwa akighuna tu,naye mkono wake ulikuwa ukitembea mgongoni taratibu mpaka kwenye kiuno kwa makusudi aliuingiza kabisa ndani ya taiti na kumshika matako yake yaliyokuwa laini hasa
“mmh jamani una makusudi wewe!”
Mama mwenye nyumba alizungumza kimahaba mkono ulipowasili matakoni mwake na kuanza kupekenyua
“makusudi gani Asma jamani, aaaah yaani una matako laini kama ya mtoto”
Ashri alizungumza kwa kuyasifia matako hayo huku akiyaminyaminya
Ilifika wakati mkono wake ukawa unatembea ndani ya taiti kuelekea kwenye kitumbua,hapo ndipo utamu ulipoanzia, hakuufikisha mkono kwenye kitumbua ila alikuwa anafanya kama anaupeleka mbele hivi na kurudisha matakoni tena.
Asma mwenyewe alianza kuonyesha dalili ya kuhitaji mboo aliushusha mkono wake laini mpaka kwenye boksa kwa taratibu aliuingiza ndani ya boksa na kulishika Dudu
“mmmmh”
Ashri Alighuna kimahaba kwani mikono ya Asma ilikuwa laini ina joto, na alimjua Asma kuwa mauno yake na mambo yake kwenye mchezo huwa ni balaa hivyo hakutaka mchezo ufanyikie pale Sofani,alimbeba na kumbwaga kitandani yaani alivyombwaga tu,kwa makusudi alijigeuza na kulala kifudifudi hapo kitandani.Kitanda kilikuwa ni kikubwa sana
“njoo nitoe taiti mpenzi wangu, unitombee”
Asma aliongea kwa sauti ya kutokea puani huku akijifanya anahangaika kuivua taiti hiyo kumbe lengo lake ambinulie tu matako Ashri
aliivua boksa yake na kulibakiza dudu inchi tisa urefu,lilikuwa nene hasa,yaani jamaa utadhani alikuwa ana ovasaizi.Na hiyo sababu pekee iliyomfanya Asmah kutulia kama maji ya mtungini mpaka kukubali kumlipia kodi na kumgharamikia kila kitu Ashri
Kwa mwendo wa taratibu alipanda kitandani na kumsogelea jimama hilo kwanza ule mtuno wa matako ya Asma daah,,,halafu taiti yenyewe aliishusha mlegezo kidogo alipokuwa akihangaika kuitoa kimakusudi, mdomo ulishafika kwenye kiuno cha Asma na kuanza kukinyonya taratibu
”mmmmmmmmmmh,,,aaaaassssssssssss”
Alisikika Asma akilalamika huku akitaka kama kujipindua hivi,muda huo alikuwa ameshika pindo la taiti, kwa hiyo akaanza kukishusha huku ulimi nao ukishuka taratibu,kwa makusudi aliufuatisha ule mstari wa ikweta unaogawa tako na tako ambapo Asma alihisi kama anatekenywa, alitamani kucheka huku akisikia raha kwa wakati mmoja.
Ashri alimvua taiti na kuendelea kumnyonya matako, Asma alifurahi sana kwani anapenda kunyonywa matako, alighuna kimahaba mpaka kitumbua kikalowa kabisa kwa ajili ya kunyonywa matako maana jamaa aligusa mpaka kwenye mpododo bila kuona kinyaa na kuingiza ulimi kabisa, basi Asma wa watu alimwaga kabisa,ila ghafla alimpindua Ashri baada ya kuona ameshamkojolesha,kisha alimlaza chali yani lile dudu la jamaa lilikuwa shida hasa, alilishika kwa mkono mmoja,ulimi wake mchokozi ukawa unazitekenya kende zake na kuzinyonya “aaaaaaaaaasssssssssssssssss,,”
Alilamika Ashri ambapo mkono ulikuwa unafanya kama unampigisha punyeto,mzigo ulisimama imara ambapo lengo la Asma lilikuwa ni kulipiza kumkojolesha,ila mambo yaligeuka Ashri akawa anataka amsugue kabisa maana tako tayari lilishampandisha nyege,,,
Mdomo wa Asma ulipotaka kuhamia kwenye dudu maana Ashri alijua tu mama huyo alivyomtaalamu wa kunyonya dudu,huwezi kuacha kukojoa kwa muda mfupi tu
“Ashri Subiri jamani”
Asma aliongea kwa sauti ya upole baada ya kuona Kibenteni wake amemlaza tena kifudifudi
“nilijua janja yako,unataka nimwage nje eeh?”
Alipoongea hivyo Asma aliishiwa pozi, alibaki kutabasamu tu
Wote wawili walibaki uchi wa mnyama, Asma alivyolala hapo kitandani kifudifudi ni hatari maana alijibinua kidogo matako yake,hivyo matundu yote yalionekana vyema,basi Ashri akiwa na mzinga wa dudu,alimfuata kwa nyuma,kisha akampanua vizuri matako na kulielekezea dudu lake kwenye tundu la haja kubwa
************
Huku kuzimu sasa kulikuwa na mkusanyiko wa majini wasiokuwa na idadi yani Koo takribani Ishilini ziliitana na kukusanyika pamoja Ukoo wa Ibnuwas peke yake una Majini million sabini elfu wakati ukoo wa Duchani million tisini na kitu
Achana na koo kumi na nane zilizoweza kuuzulia kwenye mkusanyiko huo na sio kama wamekuja na Watu wao wote ni baadhi tu
Lakini walionekana kuwa ni wengi balaa
“habari zenu ndugu zanguni? Kwa heshima na taadhima ningependa kuzungumza nanyi nakila mmoja wetu atapata nafasi ya kuchangia kile ambacho nitakizungumza hapa.
Kitu ambacho kimetufanya tuitane na kukusanyika pamoja pasipo kujari itikadi zetu uhasama uliopo baina yetu.
Kwasasa hatuna budi kushikamana tuwe kitu kimoja kwaajili ya kupambana na huyu kidudu mtu aitwae Chinoge Chinogae ni Mwanadamu ambaye ni kirusi kibaya Sana kwetu
Wangapi wapo tayari kuwa pamoja nasi?”
Mzee Makanga alizungumza hivyo kwa kupaza sauti iliyokuwa kali asilimia kubwa ya Majini walikubariana naye kwa kunyoosha mikono Juu
Miongoni mwa waliokubari ni Ibnuwas na Malkia Kaisi
Mzee Makanga alifurahi sana ajabu mama yake Ibnuwas alikataa katakata kuungana nao
“Makanga wewe ni mmoja kati ya wapumbavu yani kitu Cha hatari mkitengeneze nyinyi wenyewe halafu mtake kutushirikisha sisi kukiangamiza. Sasa nasemaje hakuna hata mtu mmoja atakaeweza kumuangamiza Chinoge kiumbe ambaye amebalikiwa kuwa na nguvu”
Bibi mtu alizungumza kwa kujiamini
“mamaaa”
Ibnuwas aliita
”na wewe unataka kusema kitu gani si umeamua kuungana naye huyu Mpuuzi wakati unafahamu zile sio Akili za Chinog,,,,,
Hata akuweza kumalizia kulitaja jina la Chinoge upepo mkali ulianza kuvuma
”huyo anakuja Sasa”
Bibi mtu alitamka hivyo Kisha akatoweka nikweli bwana mkubwa Chinoge akaibuka akiwa anahema mpaka Cheche za moto zilionekana kutokea puani
”nani aliyethubutu kuniulia mpenzi wangu?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Chinoge aliyeonekana kujiamini kupita kiasi wakati Binadamu wa kawaida Akikutana na Jini mmoja tu anaanza kujamba Jamba.
“mimi hapa!”
Mzee Makanga akajitoa kimasomaso na kutamka hivyo
Chinoge alimuangalia mzee Makanga kwa jicho kali ikawa kufumba na kufumbua Nyundo kufyatuka iliwapita Majini takribani Elfu mbili na kwenda kutua mdomoni kwa mzee Makanga
Alipepesuka huku akiachia mghuno wa maumivu
Wakati huo huo tetemeko lilianza kutokea kukawa na patashika nguo kuchanika mara
Jeshi la Masokwe wasiokuwa na Idadi wakaibuka nyuma ya Mfalme wao ni Masokwe ambao hawafi kirahisi yani hata Kama itatokea mmoja wao akafa Basi wanaibuka wawili kushika nafasi ya mmoja unaweza kusema ni Masokwe wa Ujinini maana hayo maumbo yao na nyuso zao ni za kutisha vibaya mno walionekana wakitoa pumzi za moto
Ibnuwas na Malkia Kaisi wakaamrisha Jeshi lao kuwa wakimbie maana walishafahamu hakuna atakaeweza kupona hapo
Kitendo cha Ibnuwas na Malkia Kaisi kukimbia kikafatiwa na tawala ya Makata wa Makatani kutoweka Subiani nao wakakimbia zikabaki tawala tatu ikiwa na maana tawala kumi na Saba zimetoweka Mzee Makanga alivimba kwa hasira wakati huo Chinoge alikuwa akiwavutia pumzi tu! Kabra ya kuliamrisha jeshi lake kuanza mashambulizi.
Mzee Makanga akaliweka vyema jeshi lake.
Patashika kivumbi jasho kikaanzia hapo Masokwe walikuwa wanatema moto. Wenye asidi kali sana
Chinoge yeye alikuwa akipiga hatua za taratiibu kumfata mzee Makanga
Baadhi ya majini wakawa wanajaribu kumzuia
Nyundo zikawa na kazi ya kusafisha njia
Mzee Makanga naye akawa anapiga hatua kumfata Chinoge pasipo kufahamu ya kwamba anajipeleka kwenye mdomo wa mamba
Mara akaibuka Binti Ozzie na kufikia kumshika mkono baba yake
“babaa usiende huko utakufa baba yangu tukimbiee”
Ozzie alizungumza kwa sauti yenye kuambatana na kilio huku akijaribu kumvuta baba yake
”niachieee, Siwezi kuuliwa na Binadamu kwa maana sisi ni viumbe bora kuliko wao Jini mmoja ni sawa na Binadamu mia moja iweje leo hii tumuogope Chinoge? Hiiiii,,ghaaaa,”
Mzee Makanga alizungumza na kuanza kuunguruma
Yani kuna mnyororo ulikuja kwa kasi na kumvilingisha Shingoni akaanza kuvutwa kupelekwa upande ule aliopo Chinoge
”babaa”
Ozzie alipiga kelele huku akijaribu kumkimbilia baba yake
“kimbia binti yangu kimbiaa Mimi ndiyo nakufa hivi”
Mzee Makanga alipiga kelele huku akipunga mkono wa kwaheri kumpungia binti yake
Chinoge mwenyewe alishangaa kuona mmoja kati ya Masokwe wake akiwa amemkaba mzee Makanga kwa mnyororo wenye moto
Haikuchukua hata dakika tano kushuhudia Makanga akianza kupukutika
Ozzie alilia na kupiga magoti chini
“niuweni na Mimi niuweniii,,hiiiii,,hiiiii”
Ozzie alilia kwa uchungu
Chinoge akatoa ishara kuwa Nyundo moja wapo ikamuangamize yule Binti Nyundo pasipo kuchelewa ikawa inaenda kwa kasi ghafla bin vuu Bwana mdogo Ducha Duchani akaibuka na kuidaka ile nyundo yani alifanya kuizuia
Nyundo ikawa inakukuruka kujitoa pale kwenye kizuizi Mara sauti kubwa ya kishindo ilisikika sauti ambayo iliwafanya waliokuwa wakipigana kuacha kupigana wote wakageuka kuangalia sehemu ambayo hiyo sauti imetokea alionekana Ducha akijipangusa mikono Kama vile katoka kushika vumbi kumbe aliisambaratisha ile Nyundo vipande vipande na ndiyo iliyotoa kishindo hiko
Ducha akawa anarudi kinyume nyume baada kumuona Chinoge akipiga hatua za kumfata alichokifanya Ducha ni kumuwahi bibie Ozzie na kutoweka naye
“angamizeni wote hao”
Chinoge alizungumza kwa hasira binafsi yeye hakuwa na kazi yoyote maana Masokwe waliifanya kazi yao vyema maana kule kutema moto kwa Sokwe mmoja ikawa kuangamia kwa majini si chini ya mia mbili
Chinoge akayasogelea mabaki ya nyundo akanyoosha mkono vitu vilianza kujikusanya Nyundo ikajiunga upya
Kuzimu kuligeuka kuwa ni uwanja wa machinjio
Majini wengi walipoteza maisha hakuna majeruhi hata mmoja aliyeachwa hai wote waliangamizwa lilikuwa ni tukio baya Sana kuwahi kutokea hata Ninja Ice enzi za uhai wake hakuwahi kuuwa Majini wengi kama hivyo
Baadhi ya majini waliamua kukimbilia Duniani kwa maana kuzimu kwasasa sio sehemu salama ya kuishi
Ni mapambano yaliyochukua takribani masaa manne kazi ilikuwa imeisha Tawala ya Duchani na nyinginezo zilikuwa zimeangamizwa
Masokwe waliopoteza maisha ni wenye kuhisabika tofauti na wale walioongezeka kuziba nafasi zao
Chinoge akatafuta sehemu na kukaa alivuta pumzi na kuzishusha
Masokwe wakatoa heshima na kumuaga Mfalme wao ambapo alitikisa kichwa kuwatakia safari njema,
***********
“mmmh wewe unatakaje hivyo jamani”
Asma alishtuka na kuongea kwa ukali kidogo baada kuhisi kichwa cha Dudu kikigusa kinyeo chake
”hamna bwana,siwezi kukufanyia hivyo baby ujuwe nataka unizalie mtoto mzuuri”
Ashri alizuga kwa kuzungumza hivyo wakati lengo lake lilikuwa kuingiza kwenye Mpododo basi akalielekeza Dudu kwenye kitumbua kilichokuwa kimelowa hasa, japokuwa mama huyo alishazaa lakini Mboo ndefu na nene ilienea vyema kabisa kwenye kitumbua chake.
Basi kilianza kichwa kupenya taratibu kwenye kitumbua ambapo Asma alilipokea kwa shangwe za mighuno ming ya kimahaba
“uuuuuuuuuushiiiiiiiiiiiiiii,,,aaaaaaaaaassssssssssssss,,,aaaaaaaaaaaaaaaaah”
Asma alilalamika hivyo huku akijichezesha matako yake ili dudu lipate kuingia vyema,
Ashri naye taratiibu akiunguruma alilikandamiza mpaka likazama lote, laiti kama ungepata bahati ya kushuhudia mauno aliyokuwa anayazungusha Asma ungesema hakuna Mwanamke kama yeye maana alikuwa fundi kweli kweli
Ashri alipoanza kupampu Asmah alimjia kwa juu kama ugomvi kwa hayo mauno, Mwanamke alizungusha kiuno taratibu kwa ujuvi wa hali ya juu,alikibana kitumbua chake na kufanya kama anarudisha nyuma kidogo ili dudu lizame vyema na kumkuna zaidi,uzuri wa dudu refu kwenye mtindo huo huwa halichomoki ovyo, kwa hiyo Asmah alikuwa ana uwezo wa kucheza nalo vyovyote atakavyo, Ashri aliishiwa maujanja kabisa,alibakia akimshika matako na kuyaminyaminya mpaka kidume kilimwaga kabisa bao lake ndani ya kitumbua
“aaaaaaaaaaah,,,mmm,,ohooooooo,,,asssssss”
Alighuna kwa utamu wa kumwaga Ashri ambapo alijilaza chali kwa uchovu,basi Asmah jinsi anavyojua kupetipeti, alimlaza juu ya kifua na kumbembeleza kama mtoto.
“poleee babaaa eeh,pole kwa kazi nzitooo nakupenda sana pumzika kijana wangu ehee”
Yaani alimbembeleza kama mtoto mdogo kifuani mwake huku akimshikashika nywele za kichwani,wakaanza kupiga stori
“hivi Ashri hii Mboo ulirithi,ulichanjia au ulilipata wapi?”
Asmah aliuliza hivyo huku akiishika shika
“nimerithi bwana”
kwa hiyo baba yako alikuwa na zinga la dudu inaelekea?”
“itakuwa, ila sina uhakika,ila Asma wewe unanimalizaga sana”
Ashri alijibu hivyo na kuzungumza kiuchokozi
“nakumalizaga wapi hapo?”
“kwenye mauno!,yaani ujanja wote huwa unaniishia, sijui ulifundwa wapi Mwanamke wewe?”
Alicheka kidogo Asma huku akimfinya Ashri shavu
Siku tatu baadae ndugu wa Salome wapatao sita waliwasili pale nyumbani alipokuwa anaishi
Tena walikuja na gari kubwa aina ya Fuso bila shaka ujio wao hapo nikwaajili ya kubeba vitu vya Marehemu
Nikweli maana waliomba kuonana na mama mwenye Nyumba
“sawa nimeweza kuwaelewa ila funguo ya chumba cha marehemu anayo Mchumba ake aliyekuwa akiishi naye chumba kile pale”
Mama mwenye Nyumba alizungumza hivyo huku akipiga hatua kuelekea mlangoni mwa chumba alichopanga Chinoge alipoufikia mlango ule alianza kubisha hodi
Zilipita kama dakika tano pasipo mtu wa ndani kuitikia
”sijui itakuwa kalala au ametoka?”
Mama Mwenye nyumba alijisemea hivyo
Akaelekea chumbani kwake akatoka akiwa kashika simu akabofya bofya na kuiweka sikioni
Simu ikawa inasikika ikiita chumbani mwa Chinoge na ndiyo aliyekuwa akimpigia Mmoja kati ya ndugu wa marehemu aliyeonekana kuwa kama kaka mkubwa akausogelea mlango na kukishika kitasa akajaribu kukizungusha mlango si ukafunguka
Mama Mwenye nyumba akawa wa kwanza kuchungulia ndani huku akiita
“Azizi,,wee Azizi upo humu ndani”
Kumbe Chinoge alijitambulisha kwa jina la Azizi
Mama mwenye nyumba alipatwa na mshituko baada kuingia mule Sebuleni na kumkuta mpangaji wake akiwa kalala chini ajitambui
“jamanii njoeni hukuu”
Mama mwenye nyumba alipiga kelele kuwaita watu
Ambapo waliingia ndani mbio mbio
Kila mmoja alishtuka kumuona Chinoge akiwa kalala chini
”mbona mtu mwenyewe anaonekana ameshafariki mda mrefu tu!”
Mmoja kati ya Majirani alizungumza hivyo baada kumchunguza Chinoge
“hapana hapana jamani kwanini imekuwa kwa wapangaji tu!
Kila kukicha wanakufa ajafa huyu ni mzima”
Mama mwenye nyumba alipiga kelele na kuanza kugalagala chini Mwili wa Chinoge ulifunikwa ukabebwa na kupelekwa hospitali
taarifa za mpangaji mwingine tena aliyehamia juzi juzi tu kupoteza maisha ziliwashtua watu wengi sana.
Taarifa zilitangazwa nchi nzima
**********
Hapa tunamuona Chinoge akiwa kuzimu amekaa pale pale kwenye Uwanja wa mapambano alionekana kuwa ni mwingi wa mawazo mara Ghafla alishtukia kiumbe kikimuibukia na kumchoma kisu chenye ncha kari kisu kilikita sehemu ileile yenye Moyo
Chinoge alinyoosha mkono na kumkaba yule kiumbe ambapo alikukuruka ili kujinasua lakini Chinoge hakutaka kumuachia alikaza macho kumuangalia huku akizidisha kumkaba
Sekunde si nyingi yule kiumbe alipoteza maisha kwa kupukutika
Chinoge alianza kutembea kwa mwendo wa kupepesuka hakufika mbali alidondoka chini puuh akalala chali kuangalia juu
“hahahahaha,,,hahahaha,,huhuhuhuhu”
Yani alicheka kicheko ambacho kilisambaa kuzimu kote mwishoe akawa kimya ikimaanisha naye kapoteza Maisha
Mwili wake ukiwa umelala pale Nyundo zake zilikuja na kuanza kumzunguka Masokwe waliibuka wakahitaji kumpatia ile dawa ya uzima lakini walikuwa wamechelewa siku zote Dawa haiwezi kufanya kazi kwa kiumbe ambacho kimepoteza maisha kwa maana hawezi kulimeza funda la Dawa.
Sauti ya vilio kutoka kwa Masokwe zilisikika wakimlilia Mfalme wao
Kwa mbaali alionekana Bibi mtu akiwa amesimama huku akilia
mwili wa Chinoge ulianza kumung’unyuka kama vile udongo ulionyeshewa na vua ilikuwa ni ishara ya kwamba kuzimu tayari alishatoweka
“mwanangu jamani jamani Hafidhi wangu hiiiiiii,,,”
“jamanii,,yanguu,,,hiiii”
“babaa,,”
Vyote vilikuwa ni vilio vilivyotanda kutoka kwa familia ya Bwana mkubwa Chinoge kuanzi mama yake Dada zake hadi mtoto wake wakiume aitwae Ikram
Ducha naye alikuwa analia Mwili wa Marehemu ulishawasili nyumbani kwao
Ukaoshwa na kuvishwa sanda ulisaliwa na kwenda kupumzishwa kwenye Nyumba ya milele
“nenda mwanangu nenda binafsi ulikuwa huitaji kuishi nasi ulizurula pa kuzurula mpaka tulifikia hatua ya kukurehemu tukidhania ulishapoteza maisha. Lakini leo hii umetudhihirishia
Kuwa unatuacha moja kwa moja
Kwanini uliamua kutufanyia hivi”
Baba yake Chinoge alizungumza kwa uchungu baada kushuhudia kijana wake akifukiwa
Huo ndiyo ukawa mwisho wa Mzee wa Nyundo
Chinoge Chinogae
Bila shaka ameenda kuungana na kaka yake
“oyaa wee Mama hiyo nyama mnailia wapi leo?”
Mmoja kati ya vijana wa kijiweni alipaza sauti kumuuliza mama Mwenye nyumba ni swali ambalo kama sio kulisikia basi lilimshtua
”nakuuliza wewe Mchawi mkubwa hiyo nyama mnailia wapi?”
Kuonyesha msisitizo yule jamaa akauliza Tena
“hivi wee mtoto una kichaa au uwendawazimu umekushika?”
Mama Mwenye nyumba alizungumza kwa kupaniki
“hakuna Cha ukichaa wala uwendawizimu acha nikupe makavu yako wewe mama ni Gwiji la Wachawi wote hapa mtaani
Unawaweka wapangaji wako Misukule mwisho wa siku mnawala nyama.”
Mama mwenye nyumba alikereka Sana kutokana na kauli za kiwaki kutoka kwa kijana yule
”wee jamaa vipi mbona unaleta Mambo ya kiwaki kwa wamama wa wenzio?”
Ashri hata alipotokea alifika pale na kuanza kufoka
Yule jamaa alimuangalia Ashri kwa sekunde kadhaa kisha akajikataa zake
”hiiiii,,haaaaa,,”
Mama mwenye Nyumba alijifanya kulia si alishamuona basha wake basi Ashri akamsogelea na kumkumbatia
*********
Katika jiji la Karachi nchini Pakistan ndani ya Jumba moja hivi la kifahari tunamuona binti Mrembo mwenye Asili ya kiarabu akifanya mazoezi ya kuruka kamba hakuwa mwingine bari ni Bibie Zauji ni mmoja kati ya wapiganaji hatari kwa wale walioweza kuisoma MFALME WA MASOKWE wataweza kumkumbuka vyema katika zile hekaheka zake akiwa na Chinoge wakati anaendelea kurukaruka kamba mara akashtuka baada ya kuona Madirisha na milango ikifunguka yenyewe akajiweka tayari tayari ili kukabiliana na chochote kitakachotokea Mbele yake.
“Zaujiaa”
Sauti kali na yenye kuumiza masikio ilisikika nyuma yake akafanya haraka kugeuka
Daah aliyekuwa anamwita si mwingine ni Bibie Laya ambaye alishapoteza maisha kwenye yale mapambano baina ya Chinoge na Kopang enzi za uhai wake alikuwa na uwadui mkubwa na bibie Zaujia
“huna haja ya kuniogopa rafiki Mimi na wewe tulishakuwa kitu kimoja”
Laya alizungumza hivyo huku akipiga hatua kumsogelea Zaujia
“ujio wangu hapa ni kwamba nahitaji msaada wako”
Laya alizungumza hivyo alishamfikia Zaujia akafanya kupita mwilini mwa Zaujia ambaye aliishia kushika hewa tu Laya alishakuwa mzimu usioweza kushikika wala kukamatika
“ni msaada gani unaouhitaji kutoka kwangu?”
Zaujia aliuliza kwa kupaniki
“nahitaji uwende kumsaidia mtoto wangu”
Laya alizungumza hivyo haliyakuwa akinyoosha kidole kuonyeshea ukutani mara nyingi Mizimu au Majini hupenda kuzungumza kwa kuonyesha vitendo vyenye uharisia
Basi aliponyoosha kidole kuna mtoto wakike mwenye umri wakama miaka kumi na miwili alionekana akiwa kafungwa kamba kwa kuning’inizwa juu yule Binti alionekana kafanana kila kitu na Laya
“unaemuona pale ni Binti yangu kipenzi ni Binti ambaye nilizaa na Chinoge kipindi kile nilipoenda kufanya misheni ya Mauwaji nchini Tanzania,,,
”Dadaa,,njoo uwone huku,,”
Wakati wanazungumza walishtushwa na sauti ya mtoto wakike akiita Dadaa njoo uone Zaujia akatoka mbiombio kwenda kumsikiliza mdogo wake
“wee Naah kuna nini?”
Zaujia alimuuliza mdogo wake
”Shemejiii,,hiiiiiii”
Naah alijibu hivyo huku akianza kulia Zaujia akakaza macho yake kuangalia kwenye televisheni kulikuwa na taarifa ya habari ikitangaza juu ya kifo cha bwana mkubwa Chinoge kwanza Zaujia hakuweza kuamini macho yake ikabidi aisogelee televisheni kwa ukaribu
Naye machozi yalishaanza kumchuruzika
Mara televisheni yenyewe ikabutuka na kutoa sauti kama vile bomu Zaujia alirudi nyuma kwa Uwoga
“watalipa”
Laya alizungumza hivyo Zaujia alipojaribu kugeuka kumuangalia Laya alishangaa Sana kuona Laya akiwa anazungukwa na Shoti ya umeme
“hatimae nimebarikiwa kipawa cha kuweza kushika na kukamata kitu chochote kile na ndiyo maana nikafanya yangu majaribio kwa kuifinya hiyo Televisheni samahani Sana rafiki nitailipa
Kwasasa naenda kufyeka Washenzi wote Kisha tukutane Tanzania kwaajili ya kulipa kile ambacho amefanyiwa Chinoge wetu”
Laya alizungumza hivyo Kisha akatoweka
*********
Nyumbani kwa kina Chinoge kulikuwa na hali ya Majozi ndugu jamaa na marafiki walihuzunika Sana juu ya kifo cha kijana wao mpendwa sema ndiyo hivyo hawakuwa na jinsi kila nafsi itaonja umauti.
Hapa tunamuona Ducha akiwa sehemu moja hivi akitembea kwa mwendo wa taratiibu ni sehemu ambayo haijurikani wapi umetokea wala unapoelekea. Lakini yeye alikuwa anatembea tu mara kwa mbaali aliweza kuonekana mtu akiwa kajiinamia ikabidi Ducha aongeze mwendo ili kuweza kumfikia mtu yule
Licha ya kuongeza mwendo alijikuta akitembea zaidi ya masaa sita pasipo kumfikia yule mtu Ducha akawa amechoka hoi akakaa chini kupumzika
”vipi kijana mbona umekaa juani?”
Akiwa kakaa pale kwa kujipumzisha akashtuliwa na sauti ikimuuliza akanyanyua uso wake ili kumuangalia huyo mtu ile kumuona tu Ducha alishtuka si kidogo
”nani wewe?”
Ducha aliuliza kwa uwoga kwanza yule mtu alitabasamu pasipo kujibu swali akanyoosha kiganja cha mkono akimaanisha kutaka kumshika Ducha
”simama kijana ili tuweze kujadiriana kitu”
Yule mtu alizungumza hivyo
Ducha akanyoosha mkono wake akanyanyuliwa
”wee ni nani kwani?”
”Ninja Ice hapa”
Ducha alishtuka zaidi alitamani hata kukimbia sema alikuwa kashikwa mkono
”huna haja ya kuniogopa embu twende tukazungumze na yule mtu pale”
Ninja Ice alizungumza hivyo
“mtu gani? Ahaa kama ni yule mi siwezi kumfikia maana najikuta natembea kwa mda mrefu pasipo kumfikia”
Ducha alizungumza hivyo
”nifate”
Ninja Ice akamtaka Ducha amfate walitembea hatua kadhaa tu! Wakawa tayari wamemfikia yule mtu aliyekuwa kawapa mgongo
”kwani nani huyu?”
Ducha aliuliza kwa sauti ya kunong’oneza swali likajibiwa baada ya yule mtu kugeuka Aisee kumbe alikuwa Marehemu Chinoge
”khaa! Mwalimu wangu jamani kumbe umzima ujafa, bado unaishi”
Ducha alimrukia mwalimu wake kwa furaha
”kumbe Mwalimu uko huku Sasa yule waliyemzika ni nani?”
”ni Mimi”
Chinoge akajibu
”kama ni wewe mbona hapa ni umzima?”
Ducha aliuliza haliyakuwa akiwa bado kamkumbatia Mwalimu wake
“Ducha”
Ninja Ice aliita hivyo
”naamu mkuu”
“kwanini uko hapa?”
Chinoge akauliza yani kaitwa na Ninja Ice kaulizwa swali na Chinoge
“nipo hapa kwaajili ya kufuzwa vile ambavyo sijawahi kufundishwa”
Ducha akajibu na kumfanya Ninja Ice ampigie makofi wakati Chinoge akitabasamu
Mara ghafla Chinoge akafanya kumsukumiza Ducha pembeni kitendo
Kilichomshangaza Sana Ducha
“mwalimu vipi tena,,
Ducha alipaza sauti kuuliza akajibiwa na kimondo kilichokuwa kinakuja kwa kasi akafanya kuinama chini kile kimondo kikapita
“pambana kijana ukizubaa utauwawa”
Ilikuwa ni kauli kutoka kwa Ninja Ice Ducha hakuweza kuamini macho yake baada kuliona jeshi la Viumbe wa Ajabu wakija mbiombio kumfata yeye.
Akadhani labda Ninja Ice na Chinoge watamsaidia kumbe wapi wenzake ndiyo kwanza wakatoweka naye alipojaribu kutoweka kipawa kikamgomea
“ohoo Shit! Nini hiki?”
Ducha alijiuliza hivyo huku akizunguka si akachenji Muonekano nakuwa kama Ninja Ice
Vile viumbe vikafunga breki na kusimama wakabaki kumuangalia Ducha wakawa kama vile wanaulizana na kupanga mikakati ya kumvamia
Sehemu Ya 24
baada kuliona jeshi la Viumbe wa Ajabu wakija mbiombio kumfata yeye.
Akadhani labda Ninja Ice na Chinoge watamsaidia kumbe wapi wenzake ndiyo kwanza wakatoweka naye alipojaribu kutoweka kipawa kikamgomea
“ohoo Shit! Nini hiki?”
Ducha alijiuliza hivyo huku akizunguka si akachenji Muonekano nakuwa kama Ninja Ice
Vile viumbe vikafunga breki na kusimama wakabaki kumuangalia Ducha wakawa kama vile wanaulizana na kupanga mikakati ya kumvamia
Songa nayo
Sasa
Baada ya wale viumbe kuonekana kama wakijadiriana kitu Ducha akaitumia nafasi hiyo kuwatupia zile Star zake zilizokuwa zikifyatuka na kwenda kutua kwenye miili yao wale viumbe ambapo kila aliyeguswa naile Silaha alipukutika na kutoweka
Kama haitoshi Ducha akaamua kuwafata yeye mwenyewe kwa kuchumpa kwenda juu alipowafikia tu! Viumbe vilianza kumshambulia kwa kwa pamoja kwa kutumia silaha zao za ajabu yani mapanga si mapanga mashoka si mashoka ni silaha zenye Kutisha Ducha akawa anakwepa huku akiachia mateke na ngumi za maana yani aliserereka huku na kule
Ajabu wale viumbe badara ya kupungua kutokana na wengi wao kuteketea ndiyo kwanza walionekana kuzidi kuongezeka kitu ambacho kilionekana kuanza kumkatisha tamaa
“tumia kibadach shen hung hoo”
Sauti ya Chinoge iliweza kusikika masikioni mwake ndipo alipoamua kuchenji staili kwanza alirudi nyuma yani alifanya kama vile kutaka kuwakimbia kisha akabimbilika na kuruka juu. Alipotua chini sauti kubwa ya kishindo ilisikika huku eneo zima likianza kutetemeka Amini usiamini Ducha alikuwa kakamatia Nyundo moja wapo kati ya zile Nyundo za Chinoge
Kwanza wale viumbe walionekana kujiziba masikio yao kutokana naile Sauti ya kishindo kuwaumiza kadri walivyoendelea kujiziba masikio ndivyo wakawa wanapasuka vipande vipande kama vile tikiti maji ulipigapo kwa Nyundo
Ducha alibaki kushangaa Sasa wakati anashangaa shangaa si akamuona mama yake akija mbiombio kumfata huku mkononi akiwa kashika Jagi
”utaenda shule au huendi?”
Mama yake alipomfikia alimuuliza hivyo
”khaa! Shule tena”
“nijibu kabra sijakumwagia haya mafuta ya moto”
”khaa! Mama yani uniunguze kisa staki kwenda shule”
Mara mwaaa Ducha alimwagiwa yale mafuta alitatarika huku akipiga kelele
”mama wee nakufaa yalaa”
Ghafla akashtuka na kujikuta yupo kitandani sema ameloana na maji chapa chapa
”sasa mama Mambo gani ya kumwagiana maji asubuhi Asubuhi?”
Ducha alimuuliza mama yake aliyekuwa kamsimamia pembeni ya kitanda
“embu hamka huko ukajiandae ili uwende shule. Hivi wee ni mtoto waaina gani usiependa Shule jamani”
Mama yake alizungumza hivyo
Kiunyoonge Ducha alinyanyuka na kutoka zake nnje muda kidogo akawa tayari amejitaarisha
“hivi wee kibwengo lini utaacha tabiya ya ukojozi?”
Lilikuwa ni swali kutoka kwa Mwanaidi akimuuliza Ducha
“hivi wee mshenzi wa tabiya aliyekwambia hiyo ni mikojo nani? Au hujui kutofautisha harufu ya maji na mikojo?”
Naye akatwangwa maswali mawili mfurulizo kutoka kwa mama yake
Ducha yeye alikuwa amenuna si kidogo
“hoya masela tutaonana mida basi”
Ducha aliwaaga hivyo
Mwanaidi na mama yake wakabaki kuangaliana inamaana wao ni masela
Ducha alikatiza mitaa miwili mitatu
“shikamoo mama”
“ohoo! Mwanangu Sudi huyo ahaa Ducha marhabaa ujambo mwanangu?”
Mama yake Sudi aliitikia salamu kwa kuchanganya majina bila shaka alipomuangalia Ducha nikama aliona taswila ya Sudi
“sijambo ewe mama yangu”
Ducha aliitikia
Kuna Mwanadada alifika pale alionekana tu ujio wake pale sio wa kheri maana alipofika tu! Alianza kumporomosha matusi na kauli za shombo kwa mama Sudi
“hivi wee kigagura Mwenye uchi kama ukoma deni langu utanilipa lini? Sasa kwa taarifa yako leo utake usitake utanilipa vinginevyo nitakuanzishia mtiti sio wa nchi hii muone Kwanza miziwa kama ganda la ndizi kazi kuomba omba tu! Bora hata ungekuwa na uch,,
“hivi wee Dada una Wazazi?”
Ducha akamkatisha yule Binti kwa kumuuliza swali kwanza yule Binti alimuangalia Ducha mara mbili mbili alimshusha na kumpandisha
“unaniulizaje wee kibwengo?”
Kwa dharau binti alitema mate chini kisha akauliza hivyo
“Ducha mwanangu wee nenda zako shule usije ukachelewa mi niache na huyu binti nitamalizana naye”
Mama yake Sudi alizungumza hivyo
“unamalizana naye vipi wakati amekutusi na kukudharirisha mbele yangu?”
”ndiyo Sasa nishamtusi wewe na mama yako ni Vibwengo tu mnanuka shid,,yalaa mama nakufaa, uwiii”
Binti hata hakumalizia kuzungumza alipiga kelele za maumivu huku akijishika mdomoni
Ducha alishatafuta Silaha si akalipata Gongo la ufagio wa kufagilia nnje pasipo kujiuliza mara mbili alimzibua la uso Binti akiwa analia huku kainama akaongezewa lingine kwa kutandikwa mgongoni
“yalaaa,, nakufaa nisaidieeni”
Kelele zake ziliweza kuwavuta baadhi ya majirani
”Ducha mwanangu acha, achaa Ducha”
Ilibidi mama yake Sudi amzuie Ducha kwa kumshikilia Binti akapata upenyo wa kukimbia peku peku hata viatu hakukumbuka kuvaa baada ya yule Binti kukimbia ndipo Ducha akaachiwa akiwa amefura kwa hasira akalifata begi lake na kulivaa huyo akaelekea zake shuleni
“mmh kumbe kiboko yao amerudi kitaani?”
Kuna mwanamama mmoja aliuliza hivyo
”ndiyo maana yake wale wenye vidomo domo wote wafunge mibakuri yao Mwenye mtaa wake kashaingia ehee watajamba”
Mwingine akadakia na kuzungumza hivyo
”kuna wale wa kujiita Wakaanga maji wanajifanyaga watata kama nini Sasa tuone kwa Ducha watakaanga hayo maji au kuyachemsha”
“mi nnacho mpendeaga Ducha hanaga maneno meengi yeye vitendo tu!
“kwani aliendaga wapi? Maana mtaa ulikuwa umepoa kweli kweli?”
”hata sijui mwenzangu”
Basi kila mmoja alizungumza lake pale
Ducha aliwasili maeneo ya shule nikweli alikuwa amechelewa mda huo wanafunzi wote walikuwa madarasani wakiendelea na masomo Ducha aliangaza macho huku na kule akapiga hatua za taratibu kulisogelea darasa ambalo alikuwa anasoma
“kudadeki zenu Mimi ndiyo kidume pekee niliyebakia humu wengine wote Mademu zangu”
Musa alizungumza kwa kujigamba
”wee fala nini! Nani demu wako humu?”
”oyaa Mose acha dharau za kichoko hizo”
”tatizo lako Musa unajikutaga John Cena ehee wee subiri siku ukiingia kwenye kumi na nane za Wakaanga maji watakubaka”
”nani abakwe Mbuzi nyi,,
Musa akanyamaza kuzungumza akabaki kutumbua macho kuangalia mlangoni hakuweza kuamini macho yake kumuona rafiki yake kipenzi amerejea Shuleni alienda mbiombio na kumkumbatia
”Ducha ni wewe?”
”ndiyo ni mimi”
”ohoo karibu Sana kichaa wangu hakika nilikumiss Sana oyaa wee pimbi pisha kwenye hilo Dawati ili wanaume tukae”
Musa alimtaka mmoja kati ya Wanafunzi atafute sehemu ya kukaa
Lakini Ducha alimwambia yule mwanafunzi asitoke wakae tu pamoja
”huyu jamaa anajamba kama nini ni vile tu! humjui”
Musa akakandia
“vipi Ally yuko wapi?”
Ducha alimuulizia Ally
“ahaa unamuulizia yule kiande?”
“mmh kiande tena?”
“ndiyo maana yake yule Ally ni fara kama mafara wengine tu haiwezekani animaindi Mimi kisa yule Malaya wake”
Musa alizungumza hivyo
“basi nyamaza mwalimu yulee anakuja”
Ducha akamtaka Musa anyamaze
Muda wa mapumziko ulipofika wakatoka na kwenda kupata juisi pamoja na sambusa
”inamaana Ally leo hajaja shule?”
Ducha akakumbushia kumuulizia Ally
”unajua nini Ducha kiukweli kabisa mimi na Ally tulikuwa ni zaidi ya marafiki yani nikama ndugu wa damu yote hii nikwaajili yako pale ulipotuunganisha sema ulipoondoka tu wewe tukaja kuzinguana kisa demu”
Musa akizungumza hivyo
”mmezinguana kivipi? Mbona sikuelewi?”
Ikabidi Musa aanze kumsimulia kisa na mkasa
”aisee yani mpaka mkafikia hatua ya kupigana kisa Mwanamke?”
Ducha aliuliza kwa mshangao baada ya Musa kumaliza kusimulia
”ndiyo hivyo”
“sio ndiyo hivyo watoto wakiume mnagombanaje kisa mwanamke?”
Ducha alishakasirika Musa hakuwa na cha kuzungumza akabaki kimya
“sasa sikia tukitoka hapa Shule tunaenda moja kwa moja nyumbani kwao”
”sawa kaka”
Musa aliitikia kiunyonge wakanyanyuka na kurejea darasani
*********
Bibie Zaujia aliwasili nchini Tanzania na kufikia kwenye hoteli moja wapo zilizopo Jijini Dar es Salaam
Ndani ya chumba alichofokia alionekana kuwa bize kuperuzi kwenye Website moja hivi iliyokuwa ikizungumzia swala zima la watu wasiojurikana wenye kuteka watu
Kuwapiga kuwabaka na kuwapoteza kwenye uso wa Dunia kila alichokuwa anakipitia alikiandika kwenye kidaftari
Mara simu ya mezani ikaanza kuita kwa fujo, akaiangalia kwa sekunde kadhaa akanyoosha mkono kuichukua
“haloo”
Zaujia alitamka hivyo
”samahani bosi kwa usumbufu Mimi ni yule Binti wa mapokezi”
”ohoo nambie Chiby”
”safi tu! Sema boss kuna mgeni wako hapa”
Zaujia akashtuka baada kusikia kuwa kuna mgeni wake
”yukoje?”
”ni binti wa kipemba mrefu wa wastani,
”ni Mimi hapa”
Sauti ya Laya ikasikika kumbe alimpokonya simu yule Muhudumu na kuzungumza yeye
”waweza ukamuelekeza chumba nilichopo
Zaujia alizungumza hivyo ajabu Laya alianza Kuondoka pasipo kuelekezwa
”wee Dada wee Dada Sasa unaenda wapi huko? Wakati hata sijakuelekeza”
Kwa hali ya uwoga muhudumu aliuliza na kumwita Laya aliyekuwa akibofya vitufe kadhaa vya lift Laya wala hakuitikia akaingia zake ndani ya Lifti taratiibu lifti ilijifunga na kuanza kupanda juu
Alichokifanya muhudumu nikwenda kutoa taarifa kwa meneja wa hoteli hiyo
“ndiyo bosi yani alipofika pale mapokezi pasipo kunisalimia aliniuliza swali tu! Kuwa Zaujia binti Sultan yuko hapa, hakika nilimshangaa sana yule binti ameshindwaje kuanza na salamu, kitu kingine kilichonishangaza kutoka kwake nikile kitendo cha kunipokonya mkonga wa simu akazungumza na mtu wake”
”khaa inamaana alikupokonya simu?”
”ndiyo bosi”
”bila shaka huyu Mwanamke atakuwa sio mtu Mzuri fanya haraka kutoa taarifa kituo cha polisi ili waweze kufika hapa”
Meneja akatoa amri kuwa polisi wataarifiwe huwenda huyu binti akawa ni mmoja kati ya Magaidi
Bibie Zaujia alikaza macho yake kuangalia mlangoni huku akiwa kaishikilia Vyema Bastola yake japokuwa alifahamu kuwa Laya ana uwezo wa kupitia sehemu yoyote ile sio mlangoni tu!
“ohoo my dear”
Sauti ya Laya ikitokea pembeni yake ndiyo iliyomgutusha na kumfanya amgeukie kwa kasi na kumnyooshea Bastola
“yani wee mshenzi umeamua kunifatiria mpaka huku?”
Zaujia aliuliza kwa ghadhabu
”sio kukufatiria kumbuka mi nawe tulipanga kitu gani kipenzi?”
Laya akauliza swali
”sikia nikwambie kitu wee kijuso siku zote katika maisha yangu sikuwahi kuwa na urafiki na Mpakistani waaina yoyote yule, na sitegemei kuwa naye naichukia Pakistan na watu wake”
Zaujia alizungumza hivyo
”kwanini unatuchukia? Kitu gani kibaya tulichokufanyia mpaka inafikia hatua ya kutuchukia hivyo,
“shatapu!”
Zaujia aling’aka pasipo kutegemea akafyatua Risasi sijui alisahau kufunga kiwambo cha kuzuia sauti maana sauti ya Risasi iliweza kusikika ndani ya hoteli nzima mpaka nnje watu walianza kushikwa na taharuki
”sikia nikwambie kitu Zaujia wewe sio kama unawachukia Wapakistani bali unanichukia Mimi kwa kosa la kukuulia mumeo mtarajiwa, hata hivyo nilishaomba Samahani mbele ya Hafidhi maana sikukusudia kumuua yeye,, Kama ungekuwa unaichukia Pakistan na watu wake usingeweza kumfunza maswala ya kijasusi yule Nustaty Kisha ukaenda naye vitani.
Unampenda Sana yeye kuliko hata mdogo wako wa Damu aitwae Naah”
Wakati wanaendelea kuzungumza mara waliweza kusikia ving’ora vya magari ya polisi
Laya akasogea dirishani na kuchungulia nnje
”ohoo shit!”
Zaujia alitamka hivyo baada ya kuona magari ya Polisi yakiwasili eneo hilo alishatambua kile kitendo cha yeye kufyatua risasi ndicho kilichowafanya polisi wawasili hapo
Alipogeuza uso wake kumuangalia Laya mwenzake alishatoweka zamani yani Laya alipochungulia tu! Akasepa zake kama msala abaki nao Zaujia mwenyewe.
Zaujia akawa anahaha mule chumbani mara akae kitandani mara asimame atembee tembee akatoa raba zake na kuzivaa kisha akaiweka ile bastola kwenye Begi akapiga hatua za kunyata kuusogelea mlango kumbuka yeye ni Komando aliyefanya misheni nyingi tena kwenye nchi za hatari kama
vile Marekani Urusi Irani Afghanistan Korea kusini na Kaskazini na nyinginezo nchi zote hizo aliingia kwa oda maarumu ya kuua.
Alipoukaribia mlango akakishika kitasa na kuufungua
Akatoka nnje ya chumba hicho kwa kuambaambaa Ukutani akapiga mahesabu atelemke chini kwa Lift au Ngazi?
Jibu alilolipata kuwa njia zote mbili kwake si salama akaangalia kushoto na kulia akawa anarudi kinyume nyume akachumpa kwa kupitia Dirishani alipopitia tu Dirishani na Lifti nayo inafunguka Aisee kumbe kikosi kazi cha ma FBI kilishawasili wakiwa na mitutu mkononi walinyata kwa kukisogelea Chumba alichofikia Bibie Zaujia pasipo kufahamu kuwa mwenzao anashuka chini taratiibu kwa kutumia kifaa maarumu alichokivaa mkononi ikawa kama Vile Spider anavyokamatia Ukuta ilikuwa ni Gorofa ya tisa
Baada ya FBI kuvamia chumbani humu na kumkosa
Wengine wakafanya haraka kutoka mpaka kwenye Korido wakawasiliana na wenzao waliokuwa wakipandisha juu kwa kutumia ngazi
Kama ujuavyo Kariakoo watu ni nyomi ile sauti ya mlio wa Risasi mwanzoni iliwafanya watu kukimbia hovyo Sasa baada kuona Polisi na kikosi kazi kimewasili kikawafanya Raia nao wajivute eneo hilo
”jamani, mnaemtafute yule kulee”
Mmoja kati ya Wananchi alipaza sauti kuwaambia polisi huku akinyoosha kidole kwa juu
Polisi nao si wakamuona Bibie Zaujia alivyokuwa anateremka
Risasi mfurulizo zilianza kuftatuliwa kuelekezwa juu Zaujia akawa anazikwema ile kiteknik
Akajiachia kutoka kule juu huku akichomoa Bastola zake mbili naye alianza kujibu mashambulizi
Siku zote Komando ni Komando tu haijarishi wakiume au wakike.
Baadhi ya Polisi walianza kudondokeana kama vile kuku wenye mdondo Zaujia alikuwa na target ya hatari Risasi alizokuwa anaziachia zilikita kwenye mapaji ya Uso.
Wananchi wakaona ehee hii sehemu sio ya kukaa walianza kukimbiana upya
Zaujia akatua chini kwa kishindo pasipo kuchelewa alikimbia kwa kasi kuelekea kwa Mtoro alipokaribia eneo la Msikitini akadunda na kwenda juu Gorofani akabiduka sarakasi na kutua upande wapili akazidi kuchochora
Hakika alionekana kuwa na mapafu ya Mbwa sasa hakufahamu kuwa anakimbilia wapi maana jiji la Dar es Salaam hakuwa analifahamu vyema akajikuta akiwekwa mtu kati baada ya kuwasili maeneo ya Polisi msimbazi
“shambuliaa”
Amri ikatoka ya kumuua Angalia ujinga wa Maaskari kwanza walikuwa wamemzunguka wote wakataka kumfyatulia Risasi
Zaujia naye alishawasoma akafanya haraka kulala chini huku akitambaa kwa kasi Kama vile Mjusi kenge
Maaskari wakajikuta wakichapana wenyewe,
Kisha akasimama imara na kuingia ndani ya kituo cha mwendo kasi
Akafyatua Risasi mbili tatu Kariakoo ikawa haitoshi si Machinga wala wanunuzi kila mmoja alikimbia kuokoa roho yake.
Zaujia alibaki amesimama pale pale kwenye kituo cha mwendokasi akatoa kikaratasi fulani hivi na akakitupia macho kwa sekunde kadhaa ilikuwa ni ramani yenye kutoa maelezo ya jiji zima la Dar es Salaam akawa anakimbia kuelekea upande wa stendi ya Gerezani polisi na
FBI iliwawia vigumu kumkimbiza yote ni kutokana na wingi wa watu uliokuwa umetawanyika huku nakule
”mmh shogaangu embu angalia kulee”
Mmoja kati ya mabinti alizungumza hivyo kumwambia Mwanaidi kumbe na wao walikuwepo Kariakoo sijui walienda kufanya nini? Bila shaka ununuzi wa Madera
“ohoo Mungu wangu wee Stumai tukimbie shogaangu”
Mwanaidi alitamka hivyo sasa wakati Stumai akigeuka ili aanze kutimua mbio ghafla akajikuta akipigana kikumbo na Zaujia kikumbo ambacho kilimfanya Stumai apepesuka na kwenda kudondokea barabarani
Mara puuh
Stumai aligongwa na Pikipiki
”yaaa Stumaiii”
Mwanaidi alipiga kelele huku akimkimbilia Zaujia aliyekuwa anatembea kwa mwendo ule wa haraka haraka kule kupigana kikumbo na Stumai kwa upande wake alichukulia Kama bahati mbaya wakati Mwanaidi aliona yule mtu ndiyo kamsukumiza rafiki yake si akamfikia na kumshika Begani
Zaujia akazunguka kwa kuutoa mkono kilikuwa ni kitendo cha haraka Mwanaidi kujikuta akiwa kanyooshewa Bastola kichwani
Ujuwe mpaka mda huo Zaujia alikuwa amevaa mavazi ya Kiume chini alivaa suruwali ya kijeshi flana nyeusi
Wakati usoni alikuwa kajifunga nikabu nyeusi
Mwanaidi alianza kutetemeka kwa uwoga
Zaujia alimuangalia yule binti kisha akageuka na kupiga hatua za kuondoka
”wee mshenzi kum**mako”
Lilikuwa ni zinga la tusi kutoka kwa Mwanaidi akimtukana Zaujia tusi ambalo lilipenya moja kwa moja kwenye mtima wa Zaujia
Akageuka na kumrudia
“yaaa yalaa mama yangu wee nakufaa
Mwanaidi alishtukia akipigwa Risasi ya bega alipiga kelele na kudondoka chini
*********
Ilikuwa yapata majira ya saa kumi kasorobo ya alasir kengere ya kutoka Madarasani ilisikika ikilia kila mmoja alibeba Begi lake wenye mifuko walibeba mifuko yao
Ducha na mwenzake Musa waliongozana kuelekea kwa kina Ally
Alichokuwa anakitaka Ducha ni kufahamu kwanini wametengana japokuwa Musa alimuelezea kila kitu. Lakini yeye alitaka kumsikia na Ally
“jamani jamani Kariakoo kumenuka”
Ilisikika sauti ya jamaa mmoja akizungumza hivyo
”kivipi mpaka kumenuka watu wamejinyea nini?”
”sio hivyo yani iko hivi kuna Jambazi kavamia moja kati ya Benki sasa katika harakati za kukimbizwa na Polisi si akaanza kufyatua risasi hovyo
Watu kibao wamededi”
Yale mazungumzo yaliweza kusikika vyema kwenye ngome ya masikio ya Ducha alichokishika yeye ni neno Jambazi watu ambao anawachukia kishenzi
”au basi wewe nenda tu nyumbani kwenu acha Mimi nikazungumze na Ally”
Ducha alibadirisha maamuzi
”mambo si ndiyo hayo kichaa wangu mi yule jamaa staki hata kuonana naye wee Kama vipi kachonge naye”
Musa alizungumza kwa furaha wakapeana tano kitendo cha Musa kugeuka tu Ducha akatoweka
Yani alipompa mgongo
”Ducha wee Ducha umepitia wapi wewe?”
Musa aliuliza huku akimtafuta rafiki yake
*******
“wee niuwe tu!
Haiwezekani umsukumize rafiki yangu mpaka amegongwa na Pikipiki yalaaa unaniumiza”
Mwanaidi alizungumza kwa sauti ya kilio wakati huo huo Upepo mkali ulianza kuvuma bila shaka ni ujio wa Ducha nikweli alikuwa ni yeye Tena kaibukia eneo lilelile
Kwakua Zaujia alikuwa kamuinamia Mwanaidi akilikandamiza lile jeraha kwa Bastola akashtukia
Akikumbwa na kitu Kama upepo
Uliomfanya arudi nyuma sema hakudondoka alisimama imara akakaza macho kumuangalia yule kiumbe aliyeibukia hapo
Wakawa wanasogeleana yani Zaujia alishajisahau kuwa yeye ni Wanted ni vyema angeendelea kukimbia tu!
Walipokaribiana walianza kushambuliana kwa mateke na ngumi zile za Dabo dabo uzuri kwa sasa Ducha amerefuka alishatimiza miaka kumi na nne so ana kimo
Cha wastani navile alivyokuwa ametinga kipawa cha Ninja Ice basi alionekana kama vile mtu mzima
Ikawa piga nikupige kama Zaujia aliwahi kupambana na Chinoge japokuwa alizidiwa uwezo Sasa kwa Ducha ndiyo ilikuwa balaa
Bibie akarudi nyuma tena baada kupigwa ngumi nzito ya kifuani huku yeye akiachia teke zito lililotua kichwani mwa Ducha
Wakawa wanaangaliana
Ducha akatoa ishara fulani Nyundo ikaja ikaelekezwa kwa Zaujia ajabu Nyundo iligoma kwenda
Zaujia naye akazitoa Bastola zake na kumuelekezea Ducha
Kama mkono kwa mkono walishazichapa wakaona Sasa watumie Silaha
Ducha alizunguka kwa kasi na kuachia zile Star zake zilizokuwa zikimfata Zaujia kwa Spidi ile ile
Zaujia akajiandaa kuzikwepa lakini alijikuta akitandikwa Risasi ya mguuni iliyomfanya apepesuke akapigwa nyingine iliyotua begani nikabu ikamvuka sura yake Sasa ilionekana dhahiri machoni mwa Ducha aliyeshtuka baada kuiona sura ya mrembo yule akafanya haraka kuzizuia Silaha zake
“na huyu je ni nani?”
”huyu anaitwa Zaujia naweza kusema ni mmoja kati ya Wanawake majasiri na wenye uwezo wa ajabu katika nyanja nzima ya Mapigano,”
Chinoge alijibu hivyo
”ohoo unataka kusema ni Shemeji yangu?”
”ndiyo maana yake ukiachana na ushemeji tambua ana mtoto wetu”
”ohoo Mwalimu wee ni noma yani umekula mbunye hadi ya Muarabu”
”hahahahaha Umemuona na huyu anaitwa Laya naye ni mzazi mwenzangu”
”khaa! Hadi huyu umemjaza kitumbo?”
”ndiyo”
”duuh kweli wee noma Sasa mwalimu hawa Mademu zako wako wapi?”
”huyu mmoja ameshafariki na kuhusu huyu yupo Misri
”daah kumbe huyu mrembo ameshafariki na vipi kuhusu mwanetu?”
”kabra ya umauti kumfika Laya aliniambia ya kwamba Binti yetu yupo kwenye kituo kimoja wapo alichowahi kulelewa yeye nchini Marekani ni kituo ambacho kinawafunza watoto wadogo maswala ya kijasusi”
Zote zilikuwa ni kumbukumbu za Ducha akikumbuka siku moja wakiwa wamekaa kule Kibaha Chinoge alikuwa na Arbaamu ya picha Sasa ile kuiona Sura ya Zaujia akamkumbuka alichokifanya Ducha ni kuwageukia FBI waliokuwa wakipiga hatua kumsogelea Zaujia aliyekuwa kajiinamia pale chini
Upepo mwingine mkali ulianza kuvuma upepo wa safari hii ulikuwa zaidi ya kimbunga
Maana vitu vilipeperushwa huku nakule
Bunduki walizokuwa wamezikamatia FBI ziliwaponyoka ikawa mbele hawaendi nyuma hawarudi
Upepo ulipokuja kutulia
Hakuonekana Ducha wala Zaujia
Mwanaidi naye sijui alipotelea wapi
FBI wakabaki Kubung’aa macho
Sehemu Ya 25
Zote zilikuwa ni kumbukumbu za Ducha akikumbuka siku moja wakiwa wamekaa kule Kibaha Chinoge alikuwa na Arbaamu ya picha Sasa ile kuiona Sura ya Zaujia akamkumbuka alichokifanya Ducha ni kuwageukia FBI waliokuwa wakipiga hatua kumsogelea Zaujia aliyekuwa kajiinamia pale chini
Upepo mwingine mkali ulianza kuvuma upepo wa safari hii ulikuwa zaidi ya kimbunga
Maana vitu vilipeperushwa huku nakule
Bunduki walizokuwa wamezikamatia FBI ziliwaponyoka ikawa mbele hawaendi nyuma hawarudi
Upepo ulipokuja kutulia
Hakuonekana Ducha wala Zaujia
Mwanaidi naye sijui alipotelea wapi
FBI wakabaki Kubung’aa macho
Songa nayo
Sasa
Polisi pamoja na FBI walibaki kuhaha huku na kule kile kitendo cha bibie Zaujia kutoweka kimiujiza kiliwachanganya sana walikuna vichwa na Sharubu zao
”hivi ule upepo ulitokea wapi?”
Mmoja kati ya maafande alimuuliza mwenzake
”aisee hata mi mwenyewe sijui”
Basi msako uliendelea pale waliingia mtaa kwa mtaa Gorofa kwa Gorofa kote huko Bibie Zaujia hakuweza kuonekana
Kumbe kilichofanyika pale baada ya ule upepo kuvuma aliibuka Bibie Laya akafanya haraka kutoweka na Zaujia wakati Ducha aliyejivika taswila ya kutoonekana kwa macho ya kawaida akitoweka na Mwanaidi kila mmoja alimchukua mtu wake hapa tunamuona Laya akiwa katikati ya msitu mgongoni akiwa kambeba Zaujia
“nimekwambia nishushe”
Zaujia alisikika akitamka hivyo basi akashushwa chini kwa kulazwa kwenye majani
Baada ya Zaujia kulazwa chini alichokifanya Laya ni kupiga mruzi
“ohoo kuja kuja baby fanya haraka wewe”
Zaujia alitamka kwa furaha huku akipunga mikono yake kumpungia Sokwe aliyeonekana akija mbio mbio haliyakuwa mkononi akiwa kabeba kile kibuya Sokwe alipofika pale akamkabidhi kibuyu Laya
”wee Ghost nipatie basi hiyo dawa”
Zaujia alitamka hivyo
”nani Ghost?”
”si wewe hapo”
”ohoo kumbe mi ghost ehee Sasa kwa taarifa yako hii Dawa sikupatii wala nini”
”hapana Laya hutakiwi kufanya hivyo tambua mwenzako nipo katika hali Mbaya nipatie bana”
”umeniitaje?”
”Laya”
”ohoo kumbe jina langu unalifahamu ehee haya fumbua mdomo nikunyweshe”
Laya alizungumza huku akifanya kumringishia kile kibuyu Zaujia akakiputa kibuyu chenyewe kikadondoka chini ajabu ile Dawa wala haikumwagika Zaujia akakichukua Kisha akagwida funda kadhaa wala haikuchelewa kufanya kazi majeraha yenyewe yalianza kufuka moshi Risasi zikachomoka majeraha yakatoweka Zaujia akawa sawa bin sawia
”asante”
Zaujia alitoa shukrani kwa yule Sokwe aliyekuwa kakaa pembeni akiwaangalia tu
”unaweza ukaenda Sasa embu kamata hii”
Laya alimtaka yule Sokwe aondoke Sokwe akakipokea kile kibuyu akakimbia hatua kadhaa mbele akatoweka
”inamaana Mimi hutaki kunishukuru?”
Laya aliuliza swali
“nikushukuru kwa kipi?”
Zaujia naye akauliza
”bila Mimi kukuondoa pale Ungenaswa leo”
”ha!ha!ha! Wakunaswa Zaujia mimi au mwingine?”
Mara upepo ulianza kuvuma na kufanya majani yapeperuke miti iliyumba
Laya akataka kutoweka lakini Zaujia akawahi kumshika mkono
”wee nini embu niachie huko”
”inamaana unataka kuniacha hapa peke yangu?”
”embu niachie”
Laya akautoa mkono wake lakini hakuweza kutoweka zaidi ya yeye kukaza macho kumuangalia kiumbe ambaye aliibuka mbele yao
Hakuwa mwingine zaidi ya Ducha Duchani akiwa kwenye vazi la Uninja Ice
Zaujia alimkumbuka vyema kiumbe yule
Akajiweka tayari tayari kupambana naye
Lakini walishangaa kumuona yule kiumbe akijivua ule muonekano kisha akaonekana kuwa ni kijana mdogo
“shikamooni”
Ducha akatoa salamu kwa kuwaamkia kwa pamoja Laya na Zaujia Lugha ya kiswahili wanaifahamu vizuri
”mmh marhabaa hujambo mtoto mzuri?”
Laya ndiyo aliyeitikia na kuuliza swali
”sijambo je naweza kufahamiana nanyi?”
”bila shaka karibu tuzungumze”
Zaujia aliitikia
Basi wakakaa chini Ducha ndiye aliyeanza kujitamburisha
“ha!ha!ha,huhuhuhu inamaana wewe ni kijana wa Chinoge Chinogae”
Zaujia alicheka kifala baada ya Ducha kumaliza kujitamburisha pamoja na kusema kuwa anawafahamu kupitia Chinoge
”ndiyo Maadam”
”daah yani hata siamini aisee mtoto mdogo ulivyonitoa jasho la meno”
”hahahahaha”
Ducha na Laya wakacheka
Hakika lilikuwa ni jambo la furaha sana baina yao walizungumza mambo mengi mwishoe Ducha akaomba asaidiwe kitu kutoka kwa Laya
”haya nambie Mume wangu nikusaidie kitu gani?”
”kuna kazi moja hivi
Sijaweza kuikamirisha bado Sasa nilikuwa naomba ukanikamirishie hiyo kazi Madam”
”nikazi ipi hiyo Mume?”
”wee naye mara hii kashakuwa mumeo kumbuka bado mtoto huyu usitake Kumbemenda bure”
“hahahaha”
Ducha akacheka baada ya Zaujia kumwambia hivyo Laya
”tulia wewe mtoto kwa mama yake huko”
Laya akazungumza na kumfanya Ducha azidi kucheka
”haya nambie kuhusu hiyo kazi na mshahara wake”
Laya alizungumza kiutani Ducha akanyoosha kidole mbele na kuwaonyeshwa tukio la kina Snop kuuwawa
Ile video ilipotoweka tu na Laya naye akatoweka hakika alishikwa na hasira
Baada ya Laya kutoweka Ducha akamshika mkono Zaujia ikawa kufumba na kufumbua Zaujia kujikuta akiwa Misri yani karudishwa Nyumbani kwao kwake aliona kama vile ni Ndoto lakini ndiyo hivyo haikuwa ndoto
Wakati jeshi la polisi wanahaha kumtafuta Muuwaji aliyeuwa Askari polisi wapatao kumi na tatu mara wanapokea taarifa kuwa wanajeshi wawili wamekutwa wameuwawa kinyama kwa kukatwa Vichwa wakati huohuo
kituo cha polisi kimoja wapo kilichopo Jijini Dar es Salaam Kikilipuliwa na Bomu huku ndani yake kukiwa na majambazi wanne na Askari watatu
Wananchi wakapaza sauti kuwa Nchi imevamiwa na Alshababu msako ulikuwa mkali Wanajeshi FBI Usalama wa taifa wote waliingia mzigoni ili kuwatafuta Wauwaji vizuri zaidi waliouwawa ni walewale waliokuwepo Dar Live siku ambayo
Snop na Sudi walipoteza maisha
Binafsi yalikuwa matukio ya ajabu Sana kuwahi kutokea Tena kwa siku moja kilichopishana ni Masaa tu kumtafuta Muuwaji au wauwaji ikawa kama vile kuutafuta upepo ili uweze kuukamata Laya hakuwa anaonekana
(DUCHA DUCHANI
NIKO VITANI HATA SIJUI ADUI YANGU NI NANI
NNA NYEMBE MKONONI NNA NYETO NYETONI
Ducha alisikika akiimba hivyo kwa furaha ya ajabu Huku akilichezea Dudu lake Kama vile analipigisha NYETO kisasi chakina Snop kiliweza kukamilishwa na Laya baada kuimaliza hiyo kazi akaagana na Ducha huyo akasepa zake Ally na Musa waliweza kupatanishwa wakawa kitu kimoja
”Duchaaah
“naamu Mwalimu”
“embu muangalie yule Binti”
Ducha akainua uso wake kumuangalia huyo Binti
Alipomuona tu Ducha alikunja ndita huku akimuangalia Mwalimu wake
”nitamsaidiaaa”
Ducha alitamka hivyo
***MWISHO***

