MWALIMU ALITAKA MWENYEWE
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Sehemu Ya 1
Mwalimu alitaka mwenyewe, ni mkasa mfupi ambao unausiana na kisa ambacho siwezi kusema moja kamoja ni chakweli, ila nusu ya mambo yaliyo andikwa yanaegemea kwenye ukweli, lakini tahadhari kwa majina yaliyo tumika, ayaja tumika kwa ubaya, wala siyo tabia halisi za wenye majina, hayo kama itatokea ukatajwa kwa bahati mbaya, basi natanguliza samahani, japo wapo watu halisi nilio wataja, na pengine walisha tangulia mbele za haki, mungu awalaze mahali pema peponi
Mwaka 1999 mwezi wa saba, ndani ya mji wa Songea uliopo mkoani Ruvuma, kusini kabisa mwa nchi ya Tanzania, kwenye mji mdogo wa Bombambili, mtaa wa kanisani, mtaa wenye nyumba nyingi ndogo ndogo, zinazoleta picha harisi ya wakazi wa mtaa huo ambao ni watu wenye kipato cha chini kabisa, vilikuwa ni vijumba vidogo vidogo, vilivyo jengwa kwa tofari za udongo, na kuezekwa kwa vibande vya mabati chakavu
Ilikuwa ni mida ya saa kumi na mbili za jioni, juwa linazama na giza kuchukuwa nafasi yake, kijiubaridi kikali cha jioni, kulipuliza huku kikiambatana na upepo uliotulia japo ulikusanya vumbi linalokera, na kupausha ndozi za wakazi wa mtaa huu, ambao walilazimika kupaka mafuta ili kujinusuru. na kwa wale ambao walikosa mafuta ya Ngozi walitumia mavuta a kupikia, hivyo usiongeona ajabu kupishana na mwenye au mkaazi wa mtaa hu una kusikia akinukia samaki, mandazi au vitumbua, (kile cha kunywea chai) na pengine dagaa au kitu chochote ambacho kilitangulia kupikiwa mafuta yale, ili kuzinusuru Ngozi zao.
Watu walionekana wanakatiza mtaani hapo au wengine, wakiwa wame kaa vibarazani, aiza wakiota moto, au wamejikunyata kwa baridi, huku wengi wao wakiwa wame valia makoti na mweta makubwa makubwa ya naridi, ya kila aina yakupendeza na yakuchukiza, wapo walio kosa majacket, yani makoti na masueta, wakitaniawa kuwa wanakufa na fasion, kwamba awakutaka kuficha nguo zao mpya walizo vaa, pia wapo walio wakinamama walio jitanda vitenge vikubwa vikubwa, si unajuwa wakazi wa mkoa huu, uvaaji waoni kama ndugu zao toka kusini mwa afrika, nyumba ya mwisho kabisa mtaa huu, wa kanisani, nyumba ambayo ilikuwa imepakana eneo moja kubwa sana lenye ghara la kuifadhia nafaka, na kiwanda cha kukoboa na kusaga nafaka hizo, ambazo mmiliki uwa na anunua toka kwa wakulima, na kuzikoboa pamoja na kuzikaga, kisha kuzifunga kwenye vifungashio na kuzisambaza mikoa yenye watu wasio penda kulima nafaka hizo, kama vile Dar es salaam na mikoa mingine unayo ifahamu.
Nje ya nyumba ile ya mwisho alionekana dada mmoja, alie valia gauni ambalo tunge shindwa kulitathmini kama ni zuri au chakavu, sababu alikuwa amelificha kwa pande mbili za kanga, ambazo, zilikuwa zina saidiana kuficha matundu ilikuzuwia baridi, akiwa amekaa kwenye gazi za nyumba ile aki mtazama mtoto wakiume mwenye umri wa miaka miwili, alie kuwa anacheza mpira, wa kufumwa na vitambaa chakavu na Kamba nazo chakavu, alekuwa anacheza pembezoni mwa sturi ilibebeshwa beseni dogo la plastick, na kufunikwa na hungo, juu yake, huku vipande vya gazeti, na kipande cha stiki ya kwenye matairi ya baiskeri yani spoker ikichungulia kwa toka ndani ya beseni lile lile, vilivyo kaa pembezo kabisa mwa barabara hii nayo tumika kama njia ya mkato ya kwenda kwenye kiwana chenye bango kubwa, lililosomeka M.Mills Company.
Tukimtazama vizuri mschana huyu, ambae aliekaa peke yake, anamtazama mtoto yule alie valia nguo chakavu huku akiwa amechafuka kwa vumbi, unge gundua kuwa akuwa anamwona,mtoto sababu macho yake yalikua yame jaliwa na machozi, mengi sana, ambayo mala kwa mala alikuwa anayawai yasi fike mashavuni na kuya futa kwa haraka, ni wazi kuwa mwanadada huyu mwenye umri wa miaka kama ishilini na tatu au ishilini na nne hivi, alikuwa katika maumivu makubwa ya rohoni mwake, yani nikama nafsi ilikuwa ina msuta, na wakati huo huo kuna jambo alikuwa analijiutia, “mama mama ona piga kudhuti mpaka kule” ilikuwa ni sauti ya yule mtoto wa kiume, ambae ata kutembea kwake ilikuwa ni shida, kutokana na umri wake, mwana dada yule akujibu kitu, Zaidi aliendelea kumtazama huku mawazo yakimsokota.
Sehemu Ya 2
Ukweli kilicho mfanya mwana dada huyu ambae mpaka umtazame vizuri ndio, unaweza kutambua kuwa ni wana dada mwenye uzuri wa hasiri, ni juu ya huyu mtoto, alie mbele yake, ambae akujuwa jioni hii ata kula nini, maana mchana alibahatika kumpatia vitumbua vitatu, ni kati ya vile anavyo viuza, ambavyo toka jana aliuliza vitumbua sita tu! kati ya vitumbua hamsini, na kama vitumbua alobaini na moja vilivyo bakia, visinge za kuuzwa siku inayo fuata wala kuweza kuliwa na mwanae, “sasa atakura nini usiki huu?” alijiuliza mwana dada huyu, ambae akujifikilia mwenyewe, pengine alisha zowea Maisha aya ya shida, japo ukimtazama vizuri mwanamke huyu, unaweza kutambua kuwa, Maisha aya yamemkuta ukubwani.
Kitu kingine kilicho kilicho mfanya atokwe na machozi ni kuhusu afya ya mama yake, ambae mida hii alikuwa amelala ndani, akiugua homa kali sana ya malaria, mama ambae siku za nyuma alikuwa ndie msaada wake mkubwa, maana alikuwa anajiusisha na biashara ndogo ndogo, kama vile zile za kutembeza mboga za majani, matunda ikiwa na hii biashara ya vitumbua, ambayo alimlisisha binti yake, baada ya kupata ujauzito, ulio kwamisha ndoto za mschana huyu, “mama tazama bwana navyo piga gushuti” alisikika tena yule mtoto akimsisitiza mama yake, ambae alifuta chozi kwenye jicho la kushoto, na kumtazama mwanae, “aya baba cheza nakutazama” alisema yule mwanamke, huku akimtazama mwanae ambae kiukweli, ni harama kubwa sana katika Maisha yake, maana kupatikana kwake, ni Zaidi ya simulizi ya kutisha, “aya piga sasa alafu ukaoge” ambae sasa alikuwa ameinuwa usowake na kufanya uzuri wake onekane vyema, na kulazimisha tabasamu huku akiendelea kumtazama mwane, pasipo kujuwa mwanae huyu atakula nini usiku ule.
Mwana dada aliweza kumwona mtoto wake wa kiume, akiweka mpira wake chini na kurudi hatua kadhaa nyuma, kisha akakimbia na kupiga ule mpira, ambao uliseleleka kidogo na kugonga ile sturi ambayo ilikuwa imebeba beseni la vitumbua, “Eric unafanya nini sasa?” alipiga kelele mwana dada yule huku anainuka na kufwata sturi ambayo ilikuwa imezungukwa na vitummbua vilivyo taka chini kwenye vumbi, huku mwanae alie mwita kwa jina la Eric, akiwa anaukimbilia mpira uliokuwa una seleleka kuelekea kwenye ile barabara ya vumbi, wakati huo huo vikasikika vicheko toka kwenye nyumba za jirani, kwa watu waliokuwa wamekaa vibarazani, “hahahahaaaaaa! vyajuzi vime mwagika” zilikuwasauti za kike zilizo jaa umbea, “ona sasa umemwaga vitumbua vyote” mwana dada akuwajari Zaidi alianza kuokota vitumbua vile, huku akisikia vicheko vikiendelea, kwakweli hali ilikuwa ngumu kwake, roho ilimuuma, alishindwa kuwalahumu kaka zake, ambao walikataa kabisa kumpa msaada wa kumwuguza mama yake, alishindwa kumlahumu baba yake, ambae ni kawaida yake kutelekeza wanawake na Watoto kama alivyo fanya kwa mama yake na mwanamke ambae alimwacha kwa ajili ya mama yake, ambae nae aliachwa kwaajili ya mwanamke mwingine ambae bado anaishi na baba yake mpaka sasa, sijuwi Kwanini dada huyu akuwaza juu ya baba wa mtoto huyu.
Mwanadada huyu, aliokota vitumbua taratubu, maana vinge faa kwa mlo wa usiku kwake yeye na mama yake, na ikibidi ata mwanae Eric, huku akitokwa na machozi, kwa fedhea aliyokuwa anaipata, toka kwa majirani ambao kiukweli akujwa ata chanzo cha kumfanyia vile ni kitugani, maana toka mwanamke huyu na mama yake walipoamia nyumba hii miaka zaidi ya miwili iliyopita, majirani awa walianza kuwatenga na kuwa simanga, kwa Maisha yao ya hali ya chini, na sababu nyingine kadha wakadha, ambazo azikuwa na ukweli wowote wala umuhimu, kama vile baadhi walivyosema kuwa, mwanamke huyu analinga sana kwakuwa ni mzuri.
Naam lakini kabla ajafikisha ata vitumbua vitano, mwanadada yule akashatuliwa na ngurumo ya gari, ambalo lilionekana kilikuwa linakuja kwa kasi ya ajabu, mwana dada akageuka kutazama barabarani, akaliona gari moja aina range rover lakisasa kwa kipindi hicho, gari ambalo lingendeshwa na watu wenye fedha nyigi, likija kwakasi ya ajabu upande ule wa kwao, kilikuwa ni kitendo cha ghafla na chakushtukiza, sababu ni mala chache sana, kuona gari lina kuja upande huu, maana ukiachilia kutokuwa na mtu yoyote mwenye uwezo wakumiliki gari, pia ata magari ya M mills, uwa yana tumia geti kubwa lililo tazamana na barabara kuu ya lami, iendayo mikoa ya Ilinga Mbeya na Morogoro.
Mwana dada huyu, akiwa ameshakata tamaa ya kupona kwa mwanae Eric, ambae ndio kwanza alikuwa anaufikia mpira, na kuinama kwaajili ya kuuokota, hapo zika sikika honi kali za mfululizo, zikiashilia kuwa gari lilikuwa karibu sana, na bado lilikuwa katika mwendo kasi, mama Eric akuwa na uwezo wa kumtazama mwanae akiwa anakutwa na kile ambacho, alizania kuwa kunakuja kutokea kwa mwanae Eric, ambacho kikungongwa na gari, na kwa kasi ile ambayo gari lilikuwa lina tembea, alimini kuwa Eric asinge weza kupona, hivyo akaamua kujitosa barabarani amwokoe mwanae, ikibidi wafe wote, lakini kabla ajafanya lolote, akashuhudia dereva wa lile gari, akisimamisha gari kwa breack za gafla na zanguvu huku akijitaidi kukata kona upande wapili wa barabara, na kulifanya gari lile la kifahari, lisoteshe magurudumu yake, ambayo yalilalamika kwa msoto yaliyo upata, na mpaka gari lina fanikiwa kusimama, tayari vumbu na lilisha jaa eneo lile huku majirani wakiamini kuwa tayari mtoto Eric amesha gongwa na gari, hivyo wakaanza kusogea kuja kushuhudia,
Naam vumbi liliondoka baada ya dakika mzima, mwanamke yule masikini, alisha mkimbilia mwanae na kumwona akiwa mzima kabisa, akuamini macho yake, na wakati huo milango mitatu ya gari lile kifahari, ikafunguka, ikiwa ni ya mbele miwili na mmoja wanyuma, na wakashuka watu watatu, wanaume wawili, na mwanamke mmoja, ambao walionekana wazi jinsi walivyo valia kinadhifu, kasoro, mmoja ambae alikuwa ndie dereva alie valia suruali ya jinsi, na tishrt ya kubana, kuonyesha mwili wake wa mazoezi, ambae alienda moja na kuchuchumaa mbele ya Eric alie kuwa ameshikwa na mama yake, “vipi dada mtoto ajadhurika na chochoche?” aliuliza yule dereva mwenye kuvalia suruali ya jinsi, huku majirani wakiwa wamesha jaa kulizunguka gari, “hapana ajaumia” alijibu yule mwanamke, ambae alisha sahau habari ya kuokota vitumbua vyake, kwasauti ya kinyonge na kuto amini, huku bado anamtazama mwanae kama vile anamkagua, “acha ujinga we mwanamke, kwanini unakosa umakini kiasi hicho, unamwacha mtoto anacheza barabarani, unazani gari linge mgonga angepona huyu…?” aliongea kwa ukali yule mwanamke alie shuka kwenye gari, alie onekana ni mwanamke mwenye kufanya kazi kwenye ofisi kubwa, kutokana na mwonekano wake wa uvaaji wa suit ya kike, na jinsi alivyo jitengeneza nywele na rangi za mdomo na kucha, ata viatu vyake alivyo vivaa, huku arufu nzuri ya marashi ikisikilika kwenye pua za watu waliokuwa karibu yake, hakika mama Eric alianza kuogopa na kuinua usowake kwa uoga, kumtazama yule mama kwa macho ya wasi wasi, huku baadhi ya majirani wakianza kuachanua nyuso zao kwa tabasamu. “samahani mama yangu, sikutegemea kama angekimbilia barabarani” alisema mama Eric, kwa sauti iliyojaa uoga na unyenyekevu.
Ukweli ilizidi kuudhunisha, kama unge kuwa na moyo wa huruma, na unge mtazama mama Eric, hakika roho yako inge sononeka, lakini pale pale yule dereva ambae alionekana wazi, kuwa ndie mwenye umri dogo kuliko wenzake, akamtazama yule mwanamke, mwenye kuvalia suti yakike kinadhifu, ambae kama ungetazama kwa haraka haraka unge kujuwa kuwa ndie boss, au mwenye wadhifa mkubwa kuliko wale wengine, kwa macho ya ukali yojaa hasira, na kila mmoja aliona, jambo lile, “weeee! Sophia! ebu kuwa na busara kidogo, unazani nilikuwa sahihi kuendesha gari kwa speed kama ile, si haraka zatu ndizo zilizo tufanya tukimbize gari” alisema yule jamaa, ambae kama unge kuwa ni kadiliaji mzuri wa umri ungegundua kuwa alikuwa na miaka ishilini na mbili, “samahani boss” alijibu yule mwana dada ambae ungeweza kusema kuwa umri wake unalingana na mama Eric, kwasauti ya unyenyekevu na heshima kubwa.
Sehemu Ya 3
Kila mmoja alishangazwa na jambo lile, wakamtazama mtu alie itwa boss, ambae uvaaji wake wa tishet na jinsi, japo ulimpendeza kutokana na mwili wake, uliojengeka kimazoezi, lakini usingesema kama ni boss mbele ya wale wawili, ata mama Eric pia alimtazama kijana huyu mwenye busara ambae sasa aliweza kuisikia sauti yake na kuifananisha, na sauti ya mtu ambae alikutana nae kwa muda mfupi sana miaka zaidi ya miwili iliyopita, hapo ungeweza kumwona mwanamke huyu, akimtazama yule kamaa kwa macho ya mshangao bado alikuwa anamtazama Eric aliekuwa na mama yake, huku ameshikilia mpira wake wakufumwa ka makaratasi na kamba, kwa kuubana kwapani, “pole sana, mchezaji wangu” alisema kijana yule, kwa sauti ambayo, ilionekana kuzidi kumchanganya mama Eric, huku ana mkagua yule mtoto, yani Eric, ambae akujibu kitu Zaidi alimtazama mama yake, ambae bado alikua anamtazama kijana yule kwa macho ya mshangao, “unaitwa nani vile, kesho nakuletea mpira zuri, tena wadukani?” aliuliza kijana yule alieitwa boss.
Naam na sasa siyo mama Eric pekee, alie kuwa anamtazama kijana huyu kwa mshangao, yani kila dakika zilivyoenda ndivyo ata wale wengine waliokuwa wanamtazama boss kijana na Eric, walionekana kumtazama kijana huyu kwa mhangao, ata wale wawili aliokuja nao, “aitwa Eric” alisema Eric kwa sauti yenye rafudhi ya kitoto, iliyoshindwa kuumba maneno vizuri, hapo wale watu wawili walioshuka kwenye gari moja na boss, wakacheka chini chini, baada ya kusikia jina la mtoto yule, ata yule kijana nae alitabasamu, “hooo! Eric, ni jina la baba yangu pia” alisema yule boss kijana, huku akigeuka kuwatazama wale jamaa wawili, wakacheka pamoja, “ilipangwa ukutane na baba yako boss” alisema yule mwanaume, huku akiendelea kucheka.
Hapo wale majirani ambao, waliotegemea kuwa balaha linamkuta mama Eric, walionekana kukunja midomo yao kwa chuki za wazi kabisa, “inaonekana anapenda sana mpira wamiguu kama mimi….” alisema yule boss kijana huku anainuwa uso wake kumtazama mama Eric, na hapo yule boss kijana aka sita ghafla, na kutumbua macho kwa mshangao, akimtazama mama Eric, ambae bado alikuwa anamtazama kwa mshangao wa kuto kuamini, “ni wewe mwalimu Jack?” aliuliza boss kijana kwa sauti ya chini, iliyojaa mshangao, huku anamtazama mama wa mtoto Eric, kabla aja mtazama tena mtoto Eric, kisha akamtazama tena mama Eric, kama vile anataka amwulize kitu, lakini akashindwa, akabakia kuinuka na kumtazama mama Eric kwa mshangao, “Michael! Ni wewe kweli, yani siamini kama niwewe Michael,” alisema mama Eric, ambae boss kijana alimwita mwalimu Jack, kwa sauti iliyo onyesha wazi kuambatana namshangao mkubwa, huku akizuwia kitu kifuani kwake,
…..
“ni mimi mwalimu….” alijibu yue boss kijana alie fahamika kwa jina la Michael, ambae alionekana wazi anatamani kuuliza jambo lakini alisita pengine ni swali ambali alipaswa aulize wakiwa wawili, ilionyesha wazi kuwa ni watu wanao fahamiana kabla ya kupotezana kwa muda mrefu. ****
Jackline Peter Mbilinyi, au Jack Peter kama wengi walivyo weza kumwita asa akiwa shule, ni mtoto wakike pekee kwa baba na mama yake, n ani mtoto wapekee kwa mama yake Devotha, huku akiwa ni mtoto wa tatu kwa mzee Mbilinyi, mwenye Watoto wegine wawili wakiume, ambae alimtelekeza Watoto wake wakiwa na umri wa miaka sita na tisa, kipindi ambacho bwana Mbilinyi alikutana na mschana mwenye mchanganyiko wa Kihabshi toka Ethiopia na mngoni toka Tanzania Songea.
Mbilinyi mwenye hasiri ya makete Njombe, mkoani Iringa (kipindi hicho), akiwa mfanya kazi wa kampuni kubwa sana, ya usafirishaji, aliilea familia yake hii mpya vyema kabisa, akiipatia matunzo mazuri yanayopaswa, kwa kutegemea kazi yake ambayo ilikuwa inamlipa fedha nyingi sana, huku akiitelekeza familia yake ya kwanza, ambayo ni mzazi mwenzie na watoto wake wawili, yani Richard na Godfrey, ambao walianza kuojna radha ya fedha za baba yao, baada ya Jackline ambae kwa kumtazama ungejuwa kuwa ni chotara kama mama yake, kufikisha miaka kumi na tano na kuwatambua kaka zake, ambao walikuwa wanasoma kwa shida kubwa, na kuanza kuwapatie fedha alizo kuwa anapewa na baba yake, ambazo kwakiasi kikubwa sana, kuweza kumudu Maisha ya shule, na kuachana na misaada hiyo, pale wawili awa walipopata kazi katika kampuni ya kiserikali ya uchukuzi, ya mkoa wa Ruvuma. KAURU, japo urafiki wao na dada yao mdogo Jackline aukuisha.
Jakline alijaliwa uzuri wa sura na umbo, ukiachilia mbali rangi yake ya chungwa, pia usowake wa duara ulibeba pua ya kihabeshi, na midomo midogo yenye lips pana, ambazo zilificha meno nazuri meupe, ambayo yalionekana pale tu alipotabasamu, ambapo na vijisima vidogo vingeonekana mashavuni mwake, alikuwa na shingo ndefu kiasi, yenye pingiri pingiri, ungesema ni ya mtoto mdogo, kifuani alijaliwa matiti makubwa kiasi, ambayo yenye sifa ya kuwa na chuchu, ambazo zinge kuwa miiba, basi ange pata hasara ya kununua nguo mala kwa mala, sababu zingekuwa zina toboka kila mala, kwa sjinsi zilivyo simama na kuchongoka, tumbo lake lilikuwa jembamba, ungesema ananjaa ya mwenzi mzima, ila hatari ni ni kuanzia kiunoni, kushuka chini, kwenye makalio na mapaja, yani Hips, Jakline alikuwa amejazia kweli kweli, na kufanya wazazi wake wamwamishie shule ya sekodari ya waschana ya Chipole, ambayo hipo chini ya wamissional wa kikatoliki.
Mwonekano wake ulimpa shida kweli kweli, huku akisumbua wazai wake kumwamisha shule mala kwa mala, kuepuka usumbufu toka kwa walimu na wanafunzi wa kiume, huku mtaani nako akukupoa, kiasi kwamba ilimlazimu Jakline kushinda nyumbani pindi akiwa likizo, maana kila alipotoka kwenda sehemu yoyote, ange tongozwa na wanaume wengi kweli kweli, asinge weza kutoka nyumbani mpaka kituo cha daladala, kabla ajasimamishwa au kuandamishwa na mwanaume, ambae ange kubari kuwa amekataliwa pale Jackline, angepanda dala dala, na humo ndani ya dala dala, lazima ange jitokeza mwanaume wakujaribu bahati yake, labda ange bahatika kukaa seat moja na mwanamke mwenzie, nahuko anakoenda ndio inge kuwa balaha Zaidi, kila bada ya hatua kadhaa ange jitokeza mwanaume wakujaribu bahati yake, japo wapo walio ishia kutazama kwa macho, kwamana walihisi kuwa awakuwa na hadhi ya kusemesha mschana yule ambae kipindi hicho alikuwa na mwonekano wa Maisha bora, japo siyo sababu kuu, kama ile ya uzuri wa mschana huyu, mwenye umbo matata, ambae ata wakati wa kurudi, inge kuwa hivyo hivyo, na mwaume wamwiho ange mwachia kwenye mlango wa jumba kubwa la kifahari ambali mzee Mbilinyi alikuwa amepangisha, mtaa wa mahenge A.
Mambo yalibadirika miaka miwili iliyopita, kibao kiligeuka na Jackline kuanza kuitaji msaada wa kaka zake, ni mala baada ya bwana Mbilinyi baba yao, kumtelekeza Jackline na mama yake, akiwaacha kwenye nyumba ile kubwa ya kupanga, wakiwa awana ata shilingi moja, kisha yeye kupata kutokomea na mschana mwingine mwenye umri sawa na binti yake Jackline, ambae kipindi hicho alikuwa na miaka ishilini na moja, ana soma kidato cha sita, na alikuwa anakaribia kufanya mitihani yake ya mwisho, kipindi hichi Mzee Mbilinyi, alikuwa amesha stahafu kazi na kulipwa fedha nyingi kama kiinua mgongo chake, Hakuna kaka yake ata mmoja alie mjari Jackline, kama yeye alivyo wajali kipindi wanasoma, ukweli walianzisha chuki kubwa zidi ya Jackline, ungesema baba yao amewatelekeza siku za hivi karibu, mana walimshutumu kuwa yeye na mama yake ndio walio sababisha baba yao awatelekeze, walisha sahau misaada ambayo Jackiline aliwasaidia, awakukumbuka siku ambayo mama yao aliwamwa ghafla na kukimbizwa hospital, ambako paliitajika elfu ishilini za matibabu, wakina God wakaamua kwenda kumwona baba yao, ambae aliwanyima, na kwa bahati nzuri Jackline ndie alie wapatia fedha hizo, akizipunguza katika fedha zake, za matumizi ya shuleni, alikuwa tayari kukosa matumizi yake ya shuleni, na kumsaidia mama yake mkubwa.
Mienzi mitatu mbele kodi ya nyumba iliisha, na Jackline na mama yake walifukuzwa kwenye ile nyumba ya kupanga, ambapo walienda kutafuta nyumba nafuu ya kupanga, ambayo waliipata mtaa wa kanisani kule bimbambili, karibu na kiwanda cha M mills, ata Jackline alipo maliza mitihani yake ya kidato cha sita, na kupata alama zisizo mpa nafasi ya kujiunga na chuo moja kwa moja, na alikosa uwezo wa kiunga na chou cha ualimu, na kuamua kutafuta ajira ya muda, ili aweze kumsaidia mama yake ambae alikuwa ana jiusisha na biashara ndogo ndogo, pia angeweza kupata fedha ambazi zunge msaidia kujinga nachuo.
Jackiline Peter Mbilinyi, alibahatika kupata kazi ya kufundisha katika shule moja ya secondary mshanganyiko ya Namtumbo, ambayo hipo chini ya umoja wawazazi wa mkoa wa Ruvuma, japo shule ilikuwa inatoa Elimu ya kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha sita lakini yeye alipewa nafasi ya kufundisha kidato cha kwanza na pili, masomo ya English na history. ******
Naam ilikuwa ni mwaka 1997 mwezi wa saba siku ya juma mosi, mida ya saa kumi za jioni, mida ya saa kumi za jioni, nje kidogo ya mji mdogo wa Namtumbo, (wilaya kwa sasa) kwenye miinuko ya Nandungutu, kama siyo vilima, sehemu ilipo shule ya sekondari mchanganyiko ya Namtumbo inayomilikiwa na jumuhiya ya wazazi wa mkoa wa Ruvuma, jino hii ya kipekee ambayo mwalimu Jackline, atoweza kuisahau, walionekana wanafunzi na walimu walikuwa wamejaa kwenye uwanja wa michezo, wa shule hii, pamoja na raia wa maeneo ya karibu, waliokuja kushuhudia mchezo wa kirafiki wa mpira wamiguu, kati ya timu ya shule na timu kubwa na kongwe ya Maji Maji sc, ya mjini Songea, kipindi hicho ikiwa ligi daraja la kwanza, (ndiyo ligi kuu kwa sasa) ikiwa ni maazimisho ya siku ya kuwakaribisha kidato cha sita, (well come form six) ni utaratibu wa shule hii kufanya hivyo, kila wanapo adhimisha makaribisho ya kidato cha kwanza na kidato cha sita, au mahafari ya kidato cha nne na cha sita, ambapo wange itimisha kwa kucheza music mida ya usiku.
Ili kuwa ni week moja tangu tu! mwalimu Jackline aliport kazini kwa mala ya kwanza, pale namtumbo secondary, sambamba na wanafunzi wapya wa kidato cha tano, hali iliyo sababisha baadhi ya wanafunzi kumfanaisha na wanafunzi wenzao, ni kutokana na mwonekano wake na umri wake kulingana na baadhi ya wanafunzi, ambao kwa kiasi kikubwa aliwazidi uzuri wa umbo na sura.
Hakika siku hii uwa ni ya kipekee sana, maana uambatana na shamla shamla za wanafunzi na raia wa jirani, bila kusahau walimu wao, nisiku ambayo raia waliichukulia kama siku ya kuja kutathmini wascha wazuri waliofika pale shuleni, na wenye bahati walianza kuwekanao mihadi ya kukutana nao siku za jumapili ambazo wanafunzi uachiwa kwenda kuabudu, wakijuwa njia rahisi za kuwa nasa wanafunzi hao, ambao shida kubwa ilikuwa ni kwenye vyakura (kwa wakati huo) ukiachilia mbali, uji ambao akukuwa na kitafunwa walasukari, pia chakura chao kikubwa kilikuwa ni ugari wa dona na maharage, chakula kama wali, kwao ilikuwa ni dhahabu katika mazingira ya pale shule, ambapo wangepata toka kwa mpishi ambae mpaka leo sikuwai kulifahamu jina lake harisi, zaidi ya lile la utani babu chenga, alilopewa kwa ajiri ya kuwauzia wanafunzi bidhaa hiyo adimu na pendwa, ambayo alikuwa anawauzia kwa wizi na kificho, au pengine wage enda kula chakura hicho, siku ya jumapili, pale wanapoenda kutembea namtumbo mjini, huku wafadhiri wao wakubwa wakiwa ni, raia wenye uchu, hiyo ilisababisha washana wengi kupoteza bikira zao kwa maandazi na wali, kama ilivyo sasa kwa chips kuku.
Mechi yaleo ilikuwa ni kivutio kikubwa sana kwa raia na wanafunzi, kutokana na mambo mawili makubwa, moja ikiwa ni kuitazama timu kubwa, ya maji maji, iliyokuwa inawika kwa kipindi hicho, (kabla aijanza kuporomoka mwaka mmoja baadae) pili ilikuwa ni kushihudia kama timu ya shule itaweza kubadiri matokeo, tofauti nay ale ya miaka mwili iliyopita, katika siku ya welcome form one, ambapo timu ya shule ilifungwa magori kumi na moja, gori kipa wa timu ya shule alikuwa jamaa mmoja ambae kumtaja itakuwa ni fedhea, ila kwa sasa yupo mkoa wa pwani.
Mwalimu Jackline peter ambae akuwa mpenzi au shabiki wa mpira huu wamiguu, alikuwa amekaa kwenye bechi la timu ya shule, pamoja na walimu wenzake wanne, wawili wa kiume, pia yeye na mwalimu Nyoni, alie mzidi miaka kama saba hivi, ambae ndie mwalimu msimamizi wa wanafunzi wakike (matron), ambae alikuwa amekaa kulia kwa mwalimu Jackline, ikiwa ni upande wakushoto wa mwalimu Mbele, mmoja kati ya wale walimu wa kiume, alie kuwa anatembea nae, huku yeye mwalimu Jackline, alie kaa mwanzoni mwa bechi, akiwa kama mtowa huduma ya kwanza wa timu ya shule, kama alivyo chaguliwa na uongozi wa shule, unge litambua ilo kutokana na box dogo jeupe la plastic lenye msalaba mwekundu, ambalo lilikuwa mbele yake usawa wa miguu yake iliyofunikwa na gauni refu, na kubakiza nyayo pekee, ambazo zilikuwa nime veshwa viatu vizuri vya mikanda, na kuacha vidole vyake virefu vyenye kucha nzuri zilizo pakwa rangi nzuri zionekane, huku mbele yao wakionekana wachezaji sita wahakiba, huku walimu wa timu hiyo ya shule akiwa amesimama na kuamasisha wachachezi akiwarekebisha na kuwakumbusha mambo madogo madogo, “sasa mwalimu Nyoni, dakika ya kumi na tano tayari magori mawili mpaka mpira unaisha si tutafungwa mengi?” aliuliza mwalimu Jackline, huku wakiendelea kutazama mpira, “kwa hakiri yako, timu yetu ndio yakucheza na maji maji?” aliuliza mwalimu Nyoni, huku wenzake wakicheka kidogo, hapo Jackline alishangaa kidogo, “kumbe wanajuwa utafungwa, kwanini sasa tunacheza nayo?” alijiuliza mwalimu Jackline, huku anageuka kutazama wanafunzi jinsi walivyo kuwa wanashangilia bila kukata tamaa, ndio wakati alioweza kuona jinsi baadhi ya macho ya midume ilivyo kuwa inamkodolea macho, ungesema ajavaa nguo, “kweli utoto kazi, ebu ona wanafunzi wanavyo shangilia, utazani wao ndio walioshinda” alisema mwalimu Jackline huku anarudisha macho yake mbele, kutazama mpira, akaona mchezaji wa maji maji anaelekea gorini huku anawakata chenga wachezaji wa timu ya shule, “unazani wanashangilia mpira hao, wenzako wanashangilia disco baadae” alisema mwalimu Mbele, huku shangwe toka kwa mashabiki wa timu ya maji maji, ambao wengi wao walikuwa ni raia toka namtumbo mjini, “tayari wameingiza jingine” alisema mwalimu Jackline, na wakati huo akashtuka kuna mtu amesimama karibu, yani pembeni ya benchi, akainuwa uso na kumtazama, alikuwa ni mwalimu Haule, mwalimu nidhamu, ni mtu wa makamo, wanafunzi walipenda kumwita njwanga, nimsemo ambao, alipenda sana kuutumia, asa anapomsema mwanafunzi mkorofi, au alie kosa nidhamu, (njwanga tafsiri yake ni kitu cha ovyo), “karibu ukae Mwalimu” alisema mwalimu Jackline huku anasimama, akiluusu makalio yake ambayo ungesema yalikuwa yame banwa, kujiachia na kuonekana ukubwa wake, “hapana mwalimu, kaa tu, mimi siyo mtazamaji wa mpira” alisema Njwanga, ambae kwa ujanja wa hali ya juu sana, aliukikamata kiganja cha mkono wa mwalimu Jackline na kumwachia mala moja, kiasha kuanza kuondoka, akimwacha mwalimu huyu mrembo kuliko ata wanafunzi, akishangaa na kutazama kiganja chake, ambacho kilikuwa kime kumbatia kipande cha karatasi, hakuna alie ona tukio lile la kukabidhiwa kipande kile cha karatasi, maana watu wote walikuwa busy…
Sehemu Ya 4
Wanatazama shangwe za wapinzani wao, “siunaona ata dakika ya ishilini bado gori la tatu, yani leo tubandikwa zaidi ya kumi na moja” alisemamwalimu Nyoni, ambae wanafunzi walipenda kumwita charanga, ikiwa ni aina ya mauni aliyopenda kuyavaa, (yalikuwa ndio ya kisasa kwa pindi hicho) “lakini hii timu ni kubwa sana, si inachezaga nazile za simba na yanga?” aliuliza mwalimu Jackline akijitaidi kuficha mhangao na viulizi alivyokuwanayo, juu ya kile alichopewa na njwanga, ambacho moja moja alijuwa ni ujumbe (ndio njia ya mawasilino kwa kipindi hicho) “tena wachezaji awa siyo wale wanaochezaga kwenye mechi za ligi” alifafanua mwalimu Mbele, alie onekana kuchukizwa na mwenendo wamechi ile.
Naam! huku shamla shamlazikiwa zinaendeleea, na mpira ukienda kuwekwa kati, Jackline akiwa ameshikilia kijikaratasi mkononi, anatafakari juu ya kitu ambacho kitakuwa kimeandikwa ndani ya karatasi lile, ambacho moja kwa moja alihisi kuwa itakuwa ni ujumbe wa kimapenzi, wakashuhudia mpira ukianzishwa na tumi ya shule, ambapo walipasiana watu wawili tu! Kabla mpira auja naswa na wachezaji wa maji maji, ambao walipeana pass ndefu ndefu, mipira miwili tu! Walisha lifikia gori, na kufunga tena gori jingine, shangwe zililipuka pale uwanjani, huku baashi ya walimu na wanafunzi wenye kuipenda timu yao wakionyesha wazi kuumizwa na matokeo yale, “haaaa! Sasa hii si rede jamani!” alisema mwalimu Jackline ambae alijikuta anaumia moyoni kwa kuona timu ya shule inazidi kubugizwa magori, “mbona bado, utaona jinsi tunavyo fungwa mengi mengi” alisema mwalimu Charanga, yani Nyoni, kwa sauti iliyo jaa hasira.
Wakati mpira unaenda kuwekwa kati, mala akaonekana mwanafunzi mmoja akielekea nje ya uwanja, akipitia upande wa pili, wa uwanja huu, “mbona Side anatoka?” aliuliza mwalimu Mbele kwa sauti ya mshangao, huku wote wakimtazama yule mwanafunzi wa kidato cha nne, ambae alikuwa anacheza namba nane, “mh! Kwajinsi navyo mfahamu yule, atakuwa amesha chukia” alisema mmoja wa wachezaji wa timu ya shule wa akiba, waliokuwa wamekaa mbele ya benchi ili, “kweli ameshukia, ebu mwone alivyo kunja sura” alisema mwalimu Nyoni, huku wakiendelea kumtazama mwanafunzi yule ambae ndie aliekuwa anaonyesha uhai katika uchezaji wake mle ndani, akitoka nje kabisa ya uwanja, “tunaomba mchezaji mwingine”alisikika refa akisema huku anamtazama kocha alie kuwa ameduwaa akimshangaa Side, nae akawatazama wachezaji wake, “nani ataenda kucheza nane?” aliuliza mwalimu Charle au Kambuzi kama wengi walivyo penda kumwita kutokana na ufupi wake, na mtindo wa ndefu aliopenda kuufuga, ambae ndie mwalimu wa timu pia, hapo akawaona wachezaji wanatazamana, kila mmoja akitarajia mwenzie ataingia, lakini akuna alie kuwa tayari, “Dass vipi utacheza nane?” aliuliza mwalimu Cherle, ambae miaka ya nyuma aliwai kuchezea timu ya Zimani moto ikishiliki, ligi daraja la pili, na kuipandisha daraja la kwanza, ikishiliki msimu mmoja tu, na kushindwa kujiendesha hivyo kushuka mazima daraja, “labda inge kuwa namba nyingine mwalimu hiyo siiwezi” alijibu Dastan, na ilo ndilo lilikuwa jibu la kila mwanafunzi, alie ulizwa kuhusu kuingia, ikionyesha wazi kuwa walikuwa wanaogopa.
Hapo mpira ulikuwa umesimama kabisa, wanasubiri maamuzi ya timu, maana ilikuwa ni mechi ya kirafiki, kama ingekuwa ligi, basi Side angepewa kadi nyekundu na mpira ungeendelea, “nyie mnaogopa nini, hii si mechi ya kirafiki tu!” alilalamika mwalimu Charle, huku akiwatazama wachezaji wake, ambao ata awakushtuka kwa maneno ya mwalimu wao, ambae kwakuona vile akageuka kwa lengo la kumweleza refa aendeleze mpira, lakini kabla ajasema lolote, akasikia sauti toka nyuma ya bechi, “mwalimu naomba niingie” ilikuwa ni sauti tulivu yakiume, siyo yeye tu! alie geuka kwa mshangao, ila ata wachezaji, na walimu waliokaa kwenye benchi, nao waligeuka kutazama nyuma yao.
Naam waliweza kumwona kijana mmoja mwenye mwili mpana wa wastani, uliojengeka kimazoezi, kifua kipana kilichofichwa na nguo nyepesi ya kubana, nakusababisha kufua chake cha mazoezi kionekanane vyema, uso wake wenye uzuri wa kiume, ukiwa umetawaliwa na tabasamu, akiwa amesimama nyuma kidogo ya bechi lile, “we ni mwanafunzi mgeni?” aliuliza mwalimu Nyoni, yani charanga, huku mwalimu Jackline akimtazama mwanafunzi yule kwa macho ya mshangao wakipekee, sijuwi kwanini, maana alikuwa anaanzia miguuni ambako alivalia viatu vya mpra yani njumu za puma, pia amevalia truck suit ya kijani yenye fito nyeusi mapajani, kile kijishati cheupe cha kubana, “nimgeni huyo, ameamia form six” alijibu mmoja wawachezaji waliokuwa wamekaa chini, huku mwalimu mbuzi akimwonyesha ishala ya kuwa asogee karibu yake, “yani mgeni tu uingie humu si utatufungisha nyingi?” aliuliza mwalimu Nyoni, lakini mwanafunzi yule mgeni akujibu kitu zaidi ya kutabasamu huku anamsogelea mwalimu mbuzi, akipita pembeni ya mwalimu Jackline, ambae ata yeye akujuwa ni kwanini anamtazama sana yule mwanafunzi, “utaweza namba nane?” aliuliza mwalimu Mbuzi, huku wanatu karibu wote pale uwanjani wakimtazama mchezaji huyu, ambae angeingia baada ya kiungo mshambulia Side, “ndiyo mwalimu, japo na week kama mbili sija fanya mazoezi” alijibu mwanafunzi yule kwa kujiamini, huku anatabasamu, nazani ni moja ya tabia yake, “ok! Unabukta ndani?” aliuliza mwalimu Mbuzi, “ndiyo mwalimu” alijibu mwanafunzi yule na pale mwalimu Charle, akatoa amri apatiwe jezi ya juu.
Mwanafunzi yule alirudi pale kwa wenzake, akavua truck yake ya chini, bila kuvua viatu, kisha akavalia jezi ya juu, juu ya ile nguo yake ya kubana ya mikono mirefu, aliacha inachungulia, ikiwa ni mitindo ya wakina JJ okocha, kisha akaingia ndani ya uwanja, huku mwalimu Jackline akimsindikiza kwa macho, na kuangalia umbo la kijana huyu, lililopendeza kiume, wakati huo zikisikika sauti za wanafunzi wengine wakimsimanga mzhezahuyu mgeni, “atawezaje huyoooo! Wakati bado anakamba mguuni” kama ujuwavyo vituko vya shuleni, asa ukizingatia tayari walisha kata tamaa ya kupata ata gori la kufutia machozi, maana walisha fungwa nne ndani ya dakika ishilini za mwazo.
Naam mpira ulianza tena, huku wengi wakiwa awalijuwi jina la mchezaji huyu mpya watimu ya shule, japo dakika tano mbele walikuja kulijuwa jina la mchezaji huyu, nibaada ya kupigwa mpira mmoja mrefu toka kwa walinzi wa timu ya shule, ambao aliunasa mchezaji yule na kuutuliza kama vile unge mgonga na kuondoka, kisha aka tishia kama ana taka kuupiga kwa nguvu kuelekea gorini alafu akatoa pass ndogo kwa mchezaji mwenzie namba tisa, akimwacha namba sita wa timu ya maji maji, akiyumba pasipo mwelekeo, kitendo ambacho kilileta radha flani na kuibua shangwe ya ghafla, kwa washabiki wa tinu ya shule, namba tisa ambae akuitegemea ile pass akabutuwa mpira kuelekea gorini, nao ukapaa juu kabisa, “safi Michael tulia sasa” alikika mwalimu Mbuzi, ambae nikama alipata uhai mpya, hapo ndipo zilipoanza kukika kelele za Michel Michael toka kwa mwanafunzi wakike, “anaonekana yupo vizuri” alisema mwalimu Mbele, kwasauti ya matumaini mapya, dakika mbili mbele Michael aliunasa mpira ambao ulikuwa ni wakurusha, uliokuwa umetolewa na mchezaji wa timu maji maji, ambao aliupokelea kifuani na kuuweka chini, huku akisongwa songwa na mchezaji wa timu ya maji maji, kwa ufundi Michael akaugusa kidogo kwa kisigino, mpira uka pita katikati ya miguu ya mchezaji yule wamaji maji, wenyewe wanaita tobo, kisha akawai upande wapili, ikalipuka shwangwe kubwa pale uwanjani, huku mwalimu Jackline akihisi kitu kama msisimko ukiutawala mwili wake, na kushukia akipiga makofi pongezi, huku akimtazama kijana yule wa kidato cha sita, akikokota mpira kwa kasi kuelekea gorini, na wakati anakaribia box kubwa la mita kumi na nane, tayari beck namba tano wa maji maji, kipindi hicho anaitwa Mbopa Luoga, alisha msogelea tayari kumkabiri, hapo Michael akanyoosha mguu nakuupiga ule mpira Mbopa akarusha mguu wake kuuzuwia mpira, lakini kilichotokea tofauti na alivyo tegemea, kumbe mpira aukupigwa shuti, ila ulibetuliwa kidogo sana, na kupita juu kidogo ya kichwa cha Mbopa, ambae ambae alitamani kutumia mikono yake kuudaka mpira ule, lakini akuweza, hivyo akabakia anamtazama Michael akiuwai mpira na kuzidi kulifwata gori, huku kelele za shangwe ziki lipuka kwa pande zote mbili, maana ata mashabiki wa timu ya maji maji nao walijikuta wanashangilia.
Kijana Michael akusubiri kuikuta kumi na mbili aka aachia shuti moja kali sana, ambalo lilimsinda gori kipa ambae licha ya kuambaa mbaa kuufwata lakini akaziona wavu zinacheza, hapo zililipuka shangwe za hali ya juu, siyo tu wanafunzi peke yao, ata walimu nao waliinuka toka kwenye bechi na kushangilia, gori lile, ata mwali Jackiline nae akiwa ameshikilia kijikaratasi chake, alijikuta anainuka na kushangilia, tena kwa sauti ya juu kabisa, huku akirusha rusha mikono yale na kusababisha kifua chek kilicho beba maziwa mazuri na magumu yenye chuchu mchongoko yatikisike kwafujo sambamba na makalio yake makubwa.
INAENDELEA

