LUCIFER ALINIITA KUZIMU
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Sehemu Ya 11
Kabla hajafanya chochote alinieleza kwamba ni lazima apige lamri ili kujua ukubwa wa vita niliyokuwanayo na zindiko atakalonifanyia. Baada ya kufanya hivyo,
alijongea kilingeni palipokuwa na ngozi na matunguri ya uganga, alifanya mambo yake kisha aliniambia nisogee karibu yake.
“Kijana nimeangalia, mbele yako kuna hatari kubwa kwani usingepata ufahamu wa kuja hapa, jua la kesho usingeliona kwani wenzako wamechukia sana kwa kitendo
ulichokifanya,” yule bibi aliniambia na kuongeza: “Ili kuwashinda na wewe uwe salama lazima nikufanyie zindiko la damu… yaani lazima achinjwe mbuzi au
kondoo, je utaweza kulipa gharama?” Yule bibi aliniuliza.
Kwa kuwa fedha haikuwa tatizo, nilimwambia afanye kazi yake nitamlipa ndipo aliwaita wasaidizi wake akawaambia wamchinje mbuzi mweusi aliyekuwepo pale
nyumbani. Baada ya mbuzi kuchinjwa, aliniingiza katika chumba kimoja kilichokuwa na giza, huko niliogeshwa kwa maji ya dawa kisha nilipewa supu iliyokuwa na
dawa, nikachanjwa sehemu kadhaa za mwili wangu na kupakwa dawa. Alipomaliza aliniambia tayari kazi ilikamilika na kwamba hakuna mtu atakayeweza kunidhuru
hata awe mchawi kiasi gani.
Kauli hiyo ya bibi ilinifurahisha, kwa kuwa mfukoni nilikuwa na fedha za kutosha, nilimlipa kisha niliondoka nikafika nyumbani saa tatu usiku. Kwa kuwa njaa
ilikuwa ikiniuma, nilipika ugali kwa samaki na nilipomaliza kula nilikwenda kulala bila kuoga kwani yule mganga alinikataza nisioge hadi kesho yake jioni.
Saa nane usiku nikiwa nimelala, nilisikia kishindo kikubwa juu ya bati, kisha nikawasikia watu wakiongea kwamba nilikuwa nina bahati sikuwepo nyumbani.
Wachawi hao waliokuja kuniangamiza waliongea kwa jazba na mmoja wao alisema kama wangenikuta ilikuwa halali yao kwani mambo niliyowafanyia yaliwachukiza
sana. Wakati wakitoa kauli hiyo sikuwa na wasiwasi kwa sababu tayari nilifanyiwa zindiko, wachawi hao hawakukaa muda mrefu walianza kusonya kisha wakaondoka.
Kulipokucha nilisalimiana na baadhi ya wapangaji waliokuwa wameamka, nilipomaliza kupiga mswaki niliamua kung’oa nyasi zilizokuwa zimeota kuzunguka nyumba
yangu. Kwa kuwa nyasi hazikuwa nyingi nilitumia muda mchache kumaliza kazi hiyo ndipo nilinawa mikono na kuamua kujipumzisha chini ya mti wenye kimvuli.
Kutokana na upepo uliokuwa unavuma nikapitiwa na usingizi hadi niliposhtuliwa na muungurumo wa gari lililofika pale nyumbani. Nilipoamka nilimuona yule
Mwarabu aliyekuwa akihitaji nimuuzie eneo nililokuwa naishi ili ajenge sheli, aliponifikia akanitania kwa kusema; “Wewe unasema unataka kuwa tajiri kama mimi
wakati muda huu wenzako wanafanya kazi wewe umelala chini ya mti kama tajiri?” Aliponieleza hivyo, nilimwambia muda ule nilikuwa napumzika baada ya kutoka
shamba ndipo akasema sawa na kunifahamisha alikuwa na wenzake aliowaacha ndani ya gari. Baada ya kuniambia hivyo aliwafuata, wakateremka garini na kuja
kunisalimia, akawa awanaonyesha eneo la nyumba yangu.
Waarabu hao walizungumza lugha yao ndipo yule mwenyeji akaniambia alikuja kama alivyokuwa ameahidi lakini pale nyumbani hapakuwa mahali pazuri kwa mazungumzo
yetu. Mwarabu huyo ambaye siku hiyo alivaa vizuri zaidi kuliko siku ya awali, aliniomba nipande kwenye gari ili twende sehemu iliyofaa kwa mazungumzo.
Aliponiambia hivyo niliogopa sana na kubaki nikijiuliza kama wakienda kunichinja huko na kunichuna ngozi itakuwaje, kwa ujumla nilipa hofu kwani niliwahi
kusikia baadhi ya matajiri walikuwa na tabia ya kuua watu.
Nikiwa nawaza hivyo, yule Mwarabu aliniomba niingie kwenye gari kwani muda ulikuwa unakwenda ndipo nilimweleza ngoja nikafunge mlango. Nilipoingia ndani
nilitumia kama dakika tatu kufikiria kama niondoke nao au nisiondoke lakini baadaye nikapiga moyo konde na kusema Mungu angenilinda. Baada ya kufunga milango
nilitoka nikaingia kwenye gari, akaliondoa na kuanza kuelekea barabara ya kwenda mjini, kidogo mapigo ya moyo yalipoa. Tulitumia kama dakika kumi tukawasili
kwenye hoteli moja nzuri ya ghorofa, akaegesha gari tukashuka akatuambia tumfuate.
Tulimfuata hadi sehemu iliyokuwa na lifti tukaingia, akabonyeza kitufe tukapanda hadi ghorofa ya mwisho tukaingia kwenye sehemu iliyokuwa na meza kubwa na
viti zaidi ya sita,Tv na vitu vingine. Tukiwa tumeketi, yule Mwarabu alimwita mhudumu ambaye alifika na kumsikiliza kila mmoja wetu alihitaji kula na kunywa
nini! Licha ya kunywa chai nyumbani, nilimwambia aniletee chai, chapati mbili na mayai mawili ya kukaangwa, wao wakaagiza soda.
Nikiwa nakunywa chai na wao wakiendelea kunywa vinywaji vyao, yule Mwarabu akaniambia kwamba jana nilimuuliza ili niwe tajiri natakiwa kufanya nini,
nikawambia sawa kabisa nilitaka kujua jambo hilo. Baada ya kumweleza hivyo, alicheka na kuniambia kama nilihitaji kuwa tajiri kwanza nipunguze matumizi
yasiyo ya lazima na niache starehe kama kunywa pombe nk. Wakati akinieleza hivyo simu yake ikaita, akapokea na kuanza kuzungumza na mtu aliyempigia ambapo
nilimsikia akimwambia wapande ghorofa ya juu kabisa
Hazikupita dakika tatu walifika vijana wawili, tuliposalimiana nao mmoja wao akasema; “Bosi tumepata viwanja vitatu vizuri nadhani utavipenda kwani vipo
sehemu nzuri.” Baada ya yule Mwarabu kuambiwa hivyo, alifurahi sana na kuwaeleza kuwa waondoke waende wakavione ndipo walimalizia vinywaji na kuniambia
niendelee kunywa chai, wakashuka chini. Hata hivyo, dakika tano baadaye mmoja wa wale vijana alirudi na kuniambia kwamba bosi wao alisema haikuwa vizuri
kuniacha peke yangu hivyo alinifuata.
Tulipofika chini tuliingia kwenye gari tukaondoka kuelekea sehemu iliyokuwa na viwanja hivyo, kwa kweli vilikuwa kwenye maeneo mazuri ya kujenga sheli. Wale
Sehemu Ya 12
Waarabu walifurahi ndipo yule tajiri alisema turudi hotelini, tukaingia tena kwenye gari lake na kuanza safari. Tulipofika tulikwenda kukaa sehemu awali
ndipo alifungua pochi yake akatoa kitita cha noti ambapo alihesababu shilingi laki mbili akanikabidhi. Baada ya kunikabidhi aliniomba msamaha kwa usumbufu
wote kisha akaniambia nirudi nyumbani nikaendelee na kazi zangu.
“Kijana utanisamehe kwa kukusumbua ila kwa kuwa kwako napajua nitakuja kukutembelea siku nyingine,”yule Mwarabu aliniambia.
Kwa kuwa biashara iliingia nuksi, niliwaaga nikateremka chini lakini nikajiwa na mawazo kwamba nisirudi nyumbani badala yake nitafute chumba cha kupanga
kisha nitafute kibarua chochote. Baada ya kufikiria hivyo nilikwenda mtaani ambako nilimuuliza kijana mmoja kama naweza kupata chumba cha kupanga akaniambia
kuna mzee mmoja alikuwa na vyumba, akanipeleka.
Tulipofika tulimkuta mzee huyo aliyekuwa akiishi na familia yake na baada ya salamu yule kijana alimwambia shida yangu, akakubali kunipangisha chumba. Kwa
kuwa nilikuwa nina fedha siku hiyohiyo nilimlipa kodi ya miezi sita, nikanunua kitanda, godoro, blanketi, shuka moja, ndoo ya kuogea na ya kuwekea maji ya
kunywa na vikombe viwili. Siku iliyofuata ilipofika saa tatu asubuhi nilikwenda kwenye ile hoteli aliyonipeleka yule Mwarabu kwani niliamini nisingeweza
kukosa kazi ya kufanya. Nilipofika katika hoteli hiyo nilimfuata meneja na kumweleza shida yangu ambapo alinifahamisha kwamba hapakuwa na nafasi ya kazi.
Aliponipa jibu hilo nilifedheheka sana na kumsihi anipe kazi yoyote ningeifanya kwa bidii, meneja huyo alitulia kwa muda kisha aliniuliza kama naweza kufua
nguo, nikamwambia naweza. Baada ya kumpa jibu hilo aliniambia nitakuwa nasaidiana na kijana mmoja kufua mashuka, nilimshukuru sana kwa msaada wake. Meneja
huyo aliniambia kwa mwezi atakuwa ananilipa shilingi 65,000, kwa kuwa sikuwa na familia nikakubaliana naye.
Siku hiyohiyo nilianza kufanya kazi ya kufua mashuka huku nikishirikiana na yule kijana mwenyeji wangu, kwa ujumla nilifurahi mno kupata kazi hiyo. Siku ya
tatu nikiwa nimejipumzisha baada ya kumaliza kufua mashuka, nilimuona mzee mmoja aliyekuwa amebeba shati jeupe la mikono mirefu na suruali ya kaki akitokea
ndani ya ile hoteli. Aliponifikia alinisalimia kwa kusema; “Hujambo kijana?” Nikamwambia sijambo kisha nikamuamkia! Baada ya kuitikia salamu yangu alinipatia
zile nguo na kuomba nimfulie ambapo alitoa noti ya shilingi 2,000 akanikabidhi na kuniambia nikanywe soda, nikamshukuru. Yule mzee alisema nisijali ndipo
alikwenda sehemu aliyokuwa ameegesha gari akapanda na kuondoka, nilifua zile nguo na kuzihifadhi vizuri ofisini nikitumaini angerejea lakini hakurudi. Siku
iliyofuata nikiwa bize kufua mashuka, nilimuona yule mzee ambaye alionekana ni tajiri akitoka mle hotelini na kunifuata, baada ya salamu aliomba nimpatie
nguo zake. Kwa kuwa nilikuwa nimezihifadhi ofisini nilimwambia asubiri nikamchukulie, ambapo nilizichukua nikamkabidhi, akanishukuru. Yule mzee akiwa
anaelekea lilipokuwa gari lake ili aondoke, nilimuomba kama hatajali nizungumze naye jambo flani, akasema niwe huru kumwambia chochote.
“Unasemaje kijana wangu?” yule mzee aliniuliza. Kabla sijamweleza shida yangu nilirudia tena kumuomba msamaha kwa kumsumbua akasema hakuna shida ndipo
nilimwambia nilikuwa natamani sana kuishi maisha kama yake. Kufuatia kauli hiyo, yule mzee alicheka sana na kusema: “ Maliza kwanza kazi zako zote kisha
ukiniona nimerudi njoo chumba namba nane nitakuambia siri za utajiri wangu.” Baada ya kunieleza hivyo, nikawa nina hamu ya kujua alikuwa akifanya nini mpaka
aweze kumiliki gari zuri namna ile ndipo nilimuuliza alikuwa akifanya biashara gani! Yule mzee alicheka na kusisitiza atakaporejea nimfuate chumba namba nane
ili anieleze kila kitu kisha aliniaga, akaingia kwenye gari lake na kuondoka.
Kufuatia yule mzee kukubali kunipa siri ya utajiri wake, nilifurahi sana nikawa namsubiri kwa hamu ili nijue alikuwa akifanya shughuli gani iliyomuwezesha
kupata fedha nyingi. Siku hiyo yule mzee hakuchelewa kurudi na alinikuta nikiwa napiga stori mapokezi ambapo nilimpokea mfuko nikaongozana naye kwenda
chumbani kwake. Tulipofika huko aliniambia nimuache alale kidogo akiamka ataniita, nikasema sawa lakini kabla sijaondoka aliniuliza kama nilikuwa nimekula,
nikamwambia bado akanipatia shilingi 5,000.
Kufuatia kunipatia fedha hizo, nilikwenda kula ugali kwa sato kwenye kibanda cha mama lishe mmoja kisha nilirejea pale mapokezi kusubiria kuitwa na yule
tajiri. Tukiwa tunaangalia runinga, ndipo simu ya mapokezi iliita mhudumu akapokea akaanza kuongea na mpigaji. Alipomaliza aliniambia naitwa na yule mzee,
nilikwenda fasta ambapo nilimkuta akinywa mvinyo huku kavaa bukta akiwa kifua wazi.
“Hivi kijana wangu unaitwa nani?” aliniuliza. “Kaloli,” nilimjibu. Baada ya kumtajia jina langu aliniuliza kabila langu nikamwambia Msukuma ndipo akaniambia
kwamba muda ule ulikuwa muafaka kuniambia siri ya utajiri wake. “Kijana, unaonekana unapenda sana uwe tajiri si ndiyo?” akaniuliza. “Ndiyo,” nikamjibu. Baada
ya kumjibu hivyo, alinifahamisha kwamba alikwisha wasaidia watu wengi sana kisha akaniuliza kama nitaweza masharti… yaani kumtumikia shetani!
Aliponiambia hivyo, nilimuuliza kumtumikiaje shetani ndipo mzee huyo alicheka na kuniambia kufanya mambo yake kama alivyokuwa akifanya yeye. “Kwani wewe
unafanya mambo gani?” Nilimuuliza. Kufuatia swali hilo aliniambia kwamba yeye alikuwa na uwezo wa kumwita jini yeyote mwenye nguvu akaja kumsikiliza.
Aliongeza kuwa, jini akifika alikuwa na uwezo wa kumuomba kitu chochote na kuletewa muda huohuo.
Baada ya yule mzee kuniambia hivyo nilimuuliza kama nami naweza kumuomba fedha akaniletea akasema siyo pesa tu kitu chochote nitakachokitaka. Aliponieleza
hivyo aliniuliza kama nipo tayari kumtumikia shetani nikakubali ndipo aliniambia tusubiri usiku uingie ili twende sehemu ambayo kazi hiyo itafanyika. Kabla
sijaondoka mle chumbani, alichukua karatasi na kuniandikia vitu vifuatavyo ambavyo alisema nikavinunue kwani vitatutumika katika zoezi hilo.
Kuku mweusi, udi ishirini, ubani maka na majani ya mtende, baada ya kunikabidhi ile karatasi aliniambia nikimaliza kazi zangu niende nikavinunue.
Kwa kuwa sikufahamu ningevinunua wapi, nilimuuliza akaniambia vinapatikana kwenye maduka ya dawa za asili. Siku hiyo nilifanya kazi yangu nikiwa mwenye
furaha kwani nilijua muda mfupi nami nitakuwa tajiri kama yule mzee ambaye alikuwa akiishi maisha mazuri sana. Nilipomaliza kazi, nilimuaga yule kijana
Sehemu Ya 13
niliyekuwa nikifanyanaye kazi kwamba natoka kidogo, aliponiuliza nilikuwa nakwenda wapi nikamwambia nyumbani.
Licha ya yule kijana kuwa mtu wangu wa karibu, sikutaka kumshirikisha kabisa kwenye mpango wangu wa kumtumikia shetani. Sikutaka kufanya hivyo kuhofia siri
hiyo kuvuja na kusababisha watu kujua mambo aliyokuwa akiyafanya yule mzee tajiri aliyekuwa akiheshimiwa sana.
Baada ya kumuaga yule kijana nilikwenda kwenye duka moja la dawa asili, bahati nzuri vitu vyote nilivyovihitaji nilivipata kisha nilikwenda sokoni nikanunua
kuku mweusi na kumpeleka nyumbani. Ingawa nilipomaliza kazi nilipenda kushinda pale hotelini ambapo kuna wakati wateja walikuwa wakinituma na kujipatia fedha
za ziada, siku hiyo sikurudi hadi ilipofika saa mbili usiku muda tulioahidiana kukutana na yule mzee.
Nilipofika pale hotelini niligonga mlango wa chumba cha yule mzee, akanifungulia nikaingia ndani na kuketi kwenye kochi. Mzee huyo aliniuliza kama kila kitu
alichoniagiza nilikipata nikamwambia ndiyo, akasema safi sana na kunisifia kwamba nilikuwa kijana shapu! Baada ya kuniambia hivyo aliniuliza nikikutana na
jini sitatimua mbio, kwa kuwa nilihitaji kuwa tajiri kama yeye nilimweleza sitakimbia, akacheka. “Haya nisubiri kidogo nami nijiandae,” yule mzee aliniambia.
Baada ya kusema nimsubiri, aliingia bafuni akaoga kisha alitoka akachukua nguo na kuingia tena bafuni ambapo alibadilisha na kutoka.
“Kijana wangu ukikutana na jini utamuomba kitu gani?” aliniuliza. Kufuatia swali hilo nilimwambia nitamuomba anipe umaarufu ili nifahamike duniani kote,
akaniuliza kwa nini nisiombe fedha, magari, nyumba na vitu vingine! Aliponiuliza hivyo nilisisitiza kwamba nahitaji kuwa maarufu kama walivyo marais ambao
wanaheshimika kila wanakokwenda, akacheka. Katika kichwa changu nilijua kama nitakuwa mtu maarufu, fedha, magari na vitu vingine ningevipata kirahisi ndipo
yule mzee aliniambia tuondoke.
Tulipotoka mle chumbani tulikwenda sehemu aliyoegesha gari lake tukapanda, kabla hajaliondoa aliniambia tunakwenda msituni ambako kazi hiyo ingefanyika,
nikasema sawa. Tukiwa tumeanza safari, mzee huyo aliniambia tulikokuwa tukienda ni mbali sana na tungefika kati ya saa nne, saa tano au saa tano na nusu na
kwamba lazima zoezi hilo lifanyike saa sita.
Mzee huyo aliendesha gari kwa kasi ambapo tulipita kwenye pori na hatimaye tulifika kwenye msitu huo, akasimama na kuegesha gari. Baada ya kushuka
aliniongoza hadi sehemu iliyokuwa na njia panda akasema nimsubiri kisha alirudi kwenye gari lake akachukua kisu na fimbo nyeusi. Akiwa na vitu hivyo alirejea
alipokuwa ameniacha na kuniambia muda ule ulikuwa muafaka kuanza kazi yetu. Hata hivyo, alinifahamisha kwamba atanielekeza namna ya kufanya kisha ataondoka
na kuniacha peke yangu kwani wakati wa zoezi hilo hakutakiwa kuwepo.
Mzee huyo alinifahamisha kwamba, kama jini angefika na kumkuta pale angemuua na kunywa damu yake kwa sababu angekuwa amekiuka masharti. Aliongeza kuwa,
wakati namuita jini huyo natakiwa kuwa peke yangu kwa sababu mimi ndiyo nakuwa mlengwa hivyo eneo lile hatakiwi kuwepo mtu mwingine. Baada ya kunieleza
hivyo, alinikabidhi kile kisu na fimbo na kuniambia nimfuate, nikafanya hivyo. Tukiwa tumesimama njia panda aliniambia kwa kutumia ile fimbo nichore duara,
nilipofanya hivyo akaniambia nimpe zile udi na ubani maka.
Nilipompatia alivichukua na kuviweka katikati ya lile duara kisha akaniambia nimpe yale majani ya mtende. Baada ya kumkabidhi alijongea nayo hadi kwenye lile
duara akayatandaza kisha alinipatia kiberiti, kisu, ile fimbo nyeusi pamoja na saa. Aliniambia kwamba ile fimbo niishike mkononi wakati wote au niiweke
mfukoni na ile saa alinipatia kwa ajili ya kuangalia muda. Mzee huyo aliongeza kuwa, ikifika saa sita kamili niviwashe moto vile vitu yaani udi, ubani maka
pamoja na majani ya mtende.
Aidha, aliniambia nikishavichoma moto nimchukue yule kuku mweusi niingie naye kwenye duara nimchinje na kumgawanya sehemu mbili zinazolingana.
Tukiwa safarini maongezi yetu yalihusiana na mambo ya kupata utajiri, kwani nilitamani sana kuwa kama yule mzee. “Siku nitakayokuwa tajiri kama wewe
nitafurahi sana kwani najua nitaheshimiwa na kila mtu,” nilimwambia yule mzee aliyeishia kucheka. Kwa kuwa Mwanza hadi Dar ni mbali, tuliwasili saa mbili
usiku ambapo yule mzee alikodi teksi iliyotupeleka katika hoteli moja iliyopo Kariakoo. Kulipokucha yule mzee aliniambia kwamba siku hiyo ndiyo ilikuwa ya
mwisho kunipatia msaada, kauli yake ilinishtua nikamuuliza kwa sababu gani.
Mzee huyo alicheka na kuniambia hatua iliyokuwa imebaki ilinihusu mwenyewe na kwamba baada ya kukamilisha kila kitu tutaachana. Mzee huyo aliniambia huenda
tutaonana nitakapofanikiwa mambo yangu, yaani nitakapokuwa tajiri kama yeye. Baada ya kuniambia hivyo, alisema kazi iliyokuwa mbele yetu ni kwenda katika
maduka ya dawa asili kununua vitu vitakavyoniwezesha kwenda kwa lusifa, nikamwambia sawa.
Tulipomaliza kunywa chai aliniambia kwamba vitu tunavyokwenda kuvinunua haikuwa rahisi kuvipata, nikamuuliza ni vitu gani akaniambia mayai viza mawili ya
bundi na paka mweusi ambaye hajawahi kupandwa. Aliponiambia hivyo, sikutaka kumuuliza vitu hivyo vilikuwa vya nini badala yake nilimpa moyo kwamba
tungevipata, akafurahi sana. Kama alivyokuwa amenieleza, tulitembea karibu maduka yote ya Kariakoo hatukupata ndipo tulikwenda Manzese tukabahatika kupata mayai viza ya bundi.
Alimpomuuliza jamaa aliyemuuzia mayai hayo ni wapi tungempata paka mweusi asiyepandwa akatuelekeza Buguruni kwa mzee mmoja, tukaenda huko. Saa kumi na moja
jioni baada ya kupata vitu hivyo, tulielekea ufukweni ambapo yule mzee alimchinja yule paka na kutoa jicho lake moja. Zoezi hilo lilipokamilika aliniambia;
“Sasa kila kitu kipo tayari turudi hotelini tukasubiri muda ufike ili twende Daraja la Salenda kwenye lango la kuendea kuzimu.”
Ilipotimu saa sita usiku tulitoka pale hotelini na begi dogo lililokuwa na mayai viza ya bundi na jicho la paka mweusi ambaye hakuwahi kupandwa ambapo yule
mzee alimwita dereva teksi mmoja. Dereva huyo alipokuja kutusikiliza alimwambia atupeleke katika Daraja la Salenda, baada ya kukubaliana kiasi cha fedha
alichohitaji tuliingia kwenye teksi yake tukaanza safari. Kwa kuwa kutoka Kariakoo kwenda Daraja la Salenda hapakuwa mbali, tulitumia muda mfupi kufika ndipo
yule mzee alimwambia dereva aegeshe gari mbali kidogo na daraja kisha amsubiri.
Baada ya dereva kufanya kama alivyoagizwa, tuliteremka na kwenda darajani ndipo yule mzee akaniambia kwamba siku hiyo ilikuwa ya mwisho kunipa msaada na
kwamba sijui kama tutaonana tena. Aliongeza kuwa, ikitokea bahati nzuri tutaonana nikiwa nimefanikiwa kama yeye kisha akasema nimpatie lile begi lililokuwa
na mayai viza ya bundi na jicho la paka. Baada ya kumpatia alilifungua akatoa jicho la paka akanikabidhi na kuniambia niliweke mfukoni, nikafanya hivyo.
Yule mzee hakuishia hapo, alitoa yale mayai mawili akanikabidhi na kusema moja ya yai hilo litanipeleka kuzimu kwa lusifa na lingine litanirudisha duniani.
Nikiwa namsikiliza kwa makini, aliniambia ikifika saa saba usiku nisimame kisha niangalie baharini na kusema maneno haya;
“Enyi mizimu ya baba na mama yangu, naombeni mnifungulie mlango wa kuingia kuzimu.”
Aliongeza kuniambia kuwa baada ya kutoa kauli hiyo nilitupe lile yai baharini nitaona lango kubwa la dhahabu likifunguka. Baadaye aliniambia kwamba panapo
majaliwa tungeonana, akaondoka kuelekea tulikomuacha yule dereva teksi na kuniacha peke yangu. Ingawa sehemu hiyo inatisha sana usiku, sikuogopa kitu nikawa
naangalia saa yangu ili itakapofika saa saba kamili usiku nifanye kama alivyoniagiza.
Muda huo ulipofika niliinuka kwenye jiwe nililokuwa nimekaa nikatazama baharini na kusema yale maneno kisha nikalitupia lile yai baharini, kufumba na
kufumbua niliona lango kubwa la dhahabu likifunguka mbele yangu, nikastaajabu. Baada ya kufunguka nililifuata nikaingia kisha lilijifunga ndipo nilisikia
sauti ya mtu ambaye sikumuona ikinikaribisha kwa kusema: “Kijana wangu, karibu sana katika ufalme wangu na kitu nilichokuahidi kukupatia utakipata huku
kuzimu, karibu sana!”
Baada ya mtu huyo asiyeonekana kunikaribisha, aliniambia nisonge mbele kisha nikate kushoto ili anionyeshe mambo yaliyokuwa yakijiri katika makazi yake ya
kifalme. Nilipofanya hivyo nilishangaa kuwaona watu waliokuwa wapo kwenye mateso makali wakilia kwa maumivu waliyokuwa wakiyapata. Mtu huyo ambaye
hakuonekana aliniuliza kama nimeweza kumtambua japo mtu mmoja kati ya wale waliokuwa wakiteswa na kulia, nikamwambia sikumtambua yeyote.
Nilipomwambia sikumtambua yeyote aliniambi niwasogelee karibu kisha niwaangalie kwa makini, nilipofanya hivyo nilipigwa butwaa kumuona kijana mmoja aliyekuwa
msanii maarufu wa muziki wa Bongo Fleva hapa nchini. Mtu huyo aliniuliza kama nilikuwa namfahamu kwa jina nikamwambia nilikuwa namfahamu sana ndipo
aliniambia walifanya naye mkataba ili awe mtu maarufu na tajiri lakini alikiuka masharti akaamua kumuua kwa ajali.
Sehemu Ya 14
Msanii huyo alikuwa akilia kwa mateso aliyokuwa akiyapata na baada ya Lusifa kumwambia nilikuwa nimetoka duniani na nilikuwa namfahamu, akaniomba nimuombe
ampunguzie adhabu. Baada ya msanii huyo (nalihifadhi jina lake) ambaye kufikia leo angekuwa mbali sana kimafanikio kuniambia hivyo, nilipata huzuni ikabidi
nimuombee msamaha kwa Lusifa.
“Mtukufu Lusifa, naomba umpunguzie adhabu huyu ndugu yangu kwani anajutia sana makosa aliyoyafanya nitashukuru kama ombi langu utalipokea,” nilimwambia
Lusifa ambaye hakuonekana. Nilipomaliza Lusifa aliniambia kwamba hatamsamehe yule msanii kwani alifanya makosa makubwa na kwamba adhabu aliyopewa alistahili
kuitumikia.
Licha ya kumbembeleza sana ampunguzie adhabu alikataa na kusisitiza kwamba asingemsamehe ndipo aliniambia hata mimi nikishindwa kufuata masharti
atakayonipatia yatanipata kama yaliyompata yule msanii na watu wengine niliowakuta kule kuzimu. Baada ya kuniambia hivyo, Lusifa alinifahamisha kwamba pale
kwenye himaya yake na duniani kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakimuabudu na kufuata masharti yake. Alipotoa kauli hiyo aliniambia kwamba lengo lake anataka
kuitawala dunia kupitia dini yake aliyoianzisha muda mrefu ambayo ina wafuasi wenye uwezo mkubwa sana kifedha na madaraka.
Lusifa aliniambia kwamba katika dini hiyo ana wafuasi ambao ni watumishi wa Mungu, wafanyakazi, wasanii na wafanyabiashara. Kwa kuwa nilitamani sana kumuona,
nilimuuliza kwa nini aliongea na mimi akiwa haonekani na kumuomba ajitokeze, akacheka na kusema: “Kijana wangu hapo ulipo hauna damu ya kuweza kunipatia ili
unione.” Alipotoa kauli hiyo nilimuuliza kwa nini alikuwa akipenda damu, akaniambia ndiyo kilikuwa chakula chao kikuu yeye na wafuasi wake. Baada ya
kuniambia hivyo alisema nitoke pale nilipokuwa nimesimama nianze kutembea huku na huko ili niweze kuwaona watu waliokuwa wakimtumikia. Wakati nikifanya
hivyo, niliwaona viumbe wa ajabu na wa kuogopesha, baadhi walikuwa binadamu kama mimi, waliponiona walinikimbia. Watu hao walikuwa na maumbo tofauti, baadhi
walikuwa na macho matatu makubwa kwenye paji la uso wao, wengine walikuwa na miguu mitano na mikia mirefu. Aidha, wengine walikuwa na miguu yenye kwato kama
za ng’ombe na vichwa vyao vilifanana na vya paka, vifua vyao vilikuwa sawa na vya binadamu na kulikuwa na wanawake wazuri sana. Nikiwa naendelea kutembea
bila kumuona Lusifa niliyekuwa nikiongea naye, nilimuuliza kwa nini aliwadanganya Adam na Eva wakala lile tunda la mti wa katikati?. “Niliwadanga kwa sababu
siku zote napenda binadamu wawe chini yangu kama nami ninavyotakiwa kuwa chini ya aliyeumba dunia hii ambaye tayari amenihukumu,” Lusifa aliniambia. Baada ya
Sehemu Ya 15
kuniambia hivyo, nilimwambia anipatie magonjwa niliyomuomba pamoja na dawa za kuyatibu ili nirudi duniani, akaniambia atanipatia kwa sababu aliniahidi.
Lusifa aliniambia nigeuke nyuma nimuone nyoka aliyewadanganya Adam na Eva, nilipogeuka niliona joka kubwa sana, nikashtuka! Joka hilo lilikuwa na miiba mwili
mzima na kichwani lilikuwa na pembe mbili fupi ambazo zilivalishwa pete zilizokuwa zinang’aa. Lusifa ambaye hakutaka kujitokeza aliniuliza niliona nini
kichwani kwa joka hilo, nikamwambia pembe zilizovishwa pete, akacheka. “Haya lifuate joka hilo kisha kwa kutumia mkono wako wa kuume chukua pete moja kisha
uivae katika kidole chako cha mkono wa kulia.” Kwa kuwa nilikuwa naliogopa joka hilo, nilimwambia nisingeweza akaniambia nisiogope halitanidhuru ndipo
nililifuata na kuvua pete moja ya dhahabu na kuivaa kidoleni, mwili ukanisisimka. Pete hiyo ilikuwa inang’aa kama kioo na nilipojitazama niliweza kuiona sura
yangu, nikamwambia Lusifa tayari nilikuwa nimevaa. Lusifa alinieleza kwamba ile pete ilikuwa na kila kitu, kwa kuwa sikuelewa alimaanisha nini nikamuuliza
ndipo alisema; “Hiyo pete ina mambo mengi sana na itakusaidia kwa kila unachotaka kufanya, unachotakiwa kufanya ni kuiomba kitu chochote utapata.”
Nilipoingia mle chumbani kichawi nilimrushia pepo mchafu ili amvuruge akili ndipo mchungaji huyo aliyekuwa ametoka Kongo na alikuja jijini Dar es Salaam
kufanya mikutano ya Injili, akashtuka na kuamka.
Alipoamka akaanza kunikemea kwa lugha ya Kikongo ambayo sikuielewa, wakati akifanya hivyo alikuwa akilia na machozi kumtiririka mashavuni.
Jambo lingine lililonishangaza, alikuwa akitokwa na jasho jingi mwilini licha ya kwamba kile chumba kilikuwa na kiyoyozi.
Wakati akinikemea, yule mwenyeji wake naye aliamka akaungana naye kunikemea ambapo alitamka maneno yafuatayo:
“Katika jina la Yesu Shetani toka rudi kuzimu, hauna mamlaka yoyote juu ya watoto wa Mungu, rudi katika makazi yako nyiye pepo wachafu toka!
“Nawaamuru nyiye pepo wachafu toka rudini mlikotoka…hamna mamlaka katika hii dunia kwa jina la Yesu toka!”
Wakati wakinishambulia kwa maombi sikukubali kuondoka nikawa nawasogelea ili niliwarushie moto lakini nilishindwa.
Kutokana na maombi yao mazito, walifanikiwa kunimaliza nguvu zangu lakini nami nilifanikiwa kumdhibiti yule mchungaji mwenyeji ambaye alianguka chini na
kupoteza fahamu.
Yule mchungaji wa Kongo alipomuona mwenzake amelala chini, alichukua begi dogo lililokuwa pembeni ya kitanda, akalifungua na kutoa kichupa.
Wakati akifanya hivyo nilikuwa ninamwangalia kwa makini ndipo alichukua Biblia na kuishika pamoja na ile chupa, ghafla nikiwa kama pepo niliondoka na kuuacha
mwili wangu wa asili.
Kukufafanulia hapo ni kwamba, mchawi anapokutana na nguvu za Mungu, nguvu za giza au mapepo yaliyomo mwilini mwake huondoka na kurudi yalikotoka na kuuacha
mwili ukiwa huru.
Nikiwa katika nafsi hiyo ya kichawi, nilipofika kuzimu nikaanza kumuita Lusifa kwa kusema: “Baba, baba, baba!”
Lusifa aliitika na kunipa pole na kuniambia kwamba alikuwa akiniona jinsi nilivyokuwa katika vita kubwa na binadamu wenzangu.
Lusifa alirudia kunipa pole ndipo aliniuliza kama nilikuwa napenda kuendelea kumtumikia, nikamwambia nitaendelea.
Baada ya kumwambia hivyo, alinishukuru na kuniambia kitu alichokuwa akikihitaji ilikuwa sadaka ya damu ya wazazi na ndugu zangu wote.
Tofauti na siku nyingine zote alizokuwa akizungumza nami, alikuwa akitoa kauli hiyo kwa ukali sana mpaka nikaogopa!
“Kijana sasa unatakiwa kutoa sadaka ya damu ya wazazi na ndugu zako wote ndipo utakuwa tajiri mkubwa, nasisitiza kwamba muda wako wa kutoa damu umefika,
umenielewa?” David anasema Lusifa alimwambia kwa ukali.
Baada ya kuniambia hivyo, nilisita kumjibu akaniuliza kwa nini nilikaa kimya, nikamwambia sitaweza kufanya hivyo, akacheka sana.
Alipomaliza kucheka akasema au anibadilishie masharti, nikamwambia sawa ndipo alisema nitafanyanaye mkataba mwingine wa kuwa tajiri kwa miaka 36.
Lusifa aliponiambia hivyo bila kujua ningepewa masharti gani nilifurahi sana na kumwambia nilikuwa tayari kutimiza masharti hayo lakini siyo kuwaua wazazi na
ndugu zangu.
Baada ya kumweleza hivyo, aliniambia kuwa atanipa utajiri wa miaka 36, muda huo ukiisha nitatakiwa kuondoka kwenye sura ya dunia na kwenda kuishi kuzimu.
Alisema huo utakuwa mkataba wetu mimi na yeye lakini kama siku zangu za kuishi duniani zitafika mwisho kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu aliyeniumba, nitakufa
muda wowote.
Kwa kuwa nilichokuwa nikihitaji ni utajiri, sikufikiria suala la kifo, nikamwambia tuwekeane mkataba huo ili nianze kufurahia maisha.
Baada ya kumwambia hivyo, Lusifa ambaye sikubahatika kumuona, alicheka sana na kuniambia nigeuke nyuma.
Nilipogeuka nililiona lile joka la kutisha ndipo aliniambia nikaichukue ile pete iliyokuwa imebaki juu ya pembe yake kisha niivae na kurudi nilipokuwa
nimesimama.
Kwa kuwa sikuwa muoga, nilijongea mpaka lilipokuwa lile joka, nikatoa ile pete ya dhahabu iliyokuwa iking’aa sana na kuivaa katika kidole changu.
Niliporejea sehemu niliyokuwepo, Lusifa aliniambia kitendo cha kuivaa pete hiyo, tayari tuliwekeana mkataba na kwamba niiombe kitu chochote nitapata.
Alipomaliza kuniambia hivyo aliniaga na kunitakia safari njema ya kurudi duniani, nilimshukuru kwa kunipatia utajiri niliokuwa nautaka.
Lusifa alipoondoka nilirudi duniani nikiwa katika hali ya pepo na kutokea katika daraja la Salenda.
Kwa kuwa sikuwa na mwili wa kawaida baada mwili wangu halisi kuuacha pale hotelini, nilipokutana na wale wachungaji walionikemea na kuharibu nguvu zangu,
niliamua kuufuata.
Mpenzi msomaji, kukufafanulia hapo ni kwamba mtu anapokuwa na mapepo anaweza kuuacha mwili wake halisi sehemu yoyote bila mtu ambaye hana nguvu za kichawi au
Mungu kutambua.
Mwili halisi wa mtu anayeishi na mapepo, huweza kutenganishwa na mapepo kwa njia ya maombi au mchawi husika kuuacha sehemu anayoitaka mwenyewe.
Kwa upande wangu mwili wangu ulibaki pale hoteilini kufuatia kukemewa kwa jina la Yesu na wale wachungaji ndipo kabla ya kuanza kufanya kitu chochote
niliamua kuufuata.
Nilipofika pale hotelini sikuukuta, kwa kuwa nilikuwa nina mapepo waliokuwa wakiniongoza nilibaini mwili wangu ulikuwa ukiombewa kanisani.
Hapo tena ngoja nifafanue, mtu mwenye mapepo anapoombewa yale mapepo huweza kuondoka na kuuacha mwili ambao watu wa kawaida wanaweza kufikiri ni binadamu
halisi.
Hivyo ndivyo ilivyotokea kwangu, wale wachungaji waliponizidi nguvu nilibaki pale hotelini ambapo walinichukua na kunipeleka kunifanyia maombi kanisani kwao.
Sasa nilipogundua nilikuwa nimepelekwa kanisani, niliondoka nikiwa na nafsi ya kimapepo kuufuata mwili wangu.
Nilipofika kanisani, mapepo yangu yalifanikiwa kuingia kwenye mwili wangu lakini kabla sijafanikiwa kutoka nilisikia nimepigwa na kitu kizito kichwani.
Baada ya kupigwa na kitu hicho, kichwa kikawa kizito, nikaanza kuona maghorofa yote yaliyopo Posta yanazunguka kisha mwili wote ukaanza kuwaka moto.
INAENDELEA

