SEMA JINA LANGU MPENZI
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Sehemu Ya 5
“sawa bana”nilimsuhudia akabonyeza kitufe chekundu katika rimoti yake aliyoshika kisha nikaanza kutetemesha na shoti kali ya umeme huku nikipata maumivu makali sana.akaniacha na kuchukua na kuchukua bastola kisha akaiweka risasi na kuikoki akarekezea kichwani kwangu na kushababisha mimi nianze kutetemeka kutokana kuanzia nizaliwe sikuwahi kuonyeshewa bastola
“ni kwa mara ya mwisho na kuuliza unamjua huyu Mwanamke???”
“M..m….m…h………..”
“Paaaaaaaaaaaaaaaa”…….
Namjuaaaaaa”nilijikuta nikiropoka kwa nguvu baada ya yule jamaa kupiga risasi karibia kabisa na mguu wangu risasi ambayo haikunipata lakini kutokana na mlio wake niliousikia vizuri kabisa katika masikio nikajikuta nakubali kutaja mwanamke Ambaye nilikuwa namjua lakini sikutaka kumwambia moja kwa moja
“Hahaha sasa unavyoringa ringa kunijibu nitakufumua ubongo mimi haya anaitwa nani..??”
“Moureen”
“oooh kumbe kweli unamjua je ni nani yako huyu”
“aaaa ni rafiki yangu tu”
“anhaaa kumbe rafiki yako basi subiri.”nilimshuhudia akikoki tena bunduki na safari alionekana yupo serias kisha akaelekeza katika kichwa changu kwa lengo la kuniuma
“Subiriiiii sio rafiki yangu ni msichana wangu”
“Aaaa mbona unanisumbua kijana unajua nitakuuuua.”
“Hamna usifanye hivyo”
“Sasa sikia nikwambie huyo moureen ni mwanamke wangu ambaye nasubiri muda tu Amalize kusoma nimuoe nishatoa kiasi kikubwa sana cha pesa kwa baba yake jambo ambalo hata yeye analijua sasa basi kuanzia sasa sitaki kukuona tena na moureen na kama ukikaidi ukawa hata unaongeaa naye mimi nakufutilia sana basi nitakuuua umenisikia Mimi ndio Robertson Mugalula Nakuambia Nitakuuuua” hakika maneno yale yaliniingia kabisa katika nafsi yangu huku majonzi na simanzi yaliukumba moyo wangu ambao tayari ulishazama katika penzi zito la msichana huyo.uoga wa kuuwawa na robertson Mugalula jamaa ambaye mwili wake ulikuwa wa mazoezi sana licha ya kuwa na sura nzuri ambayo ilidhirisha kabisa yeye ni handsome boy na sura yake ya Baby face.Machozi yalianza kunitiririka taratibu jambo ambalo lilimfanya robertson kuniangalia kwa dharau kubwa kisha akamuita kijana wake mmoja ambaye alimnong’oneza kitu kisha jamaa huyo akanisogelea nakunitandika ngumi kali sana ya kichwa iliyopelekea kiza kizito kinitokee macho mwangu na kuzimia.
“Oyaaaaaa Hebu Amka”ni sauti iliyoniamsha ikiambata na kofi zito la mgongo ambalo lilinipa maumivu kidogo.nilijikuta nipo katika gari ambalo vioo vyake vilionekana kama ni tinted ambavyo vilikuwa havionyeshi kabisa nje nilimuona jamaa aliyenipiga kofi akiwa kavaa miwani meusi na suti huku mwili wake ukiwa umejazia sana
“Tokaaa”
“eee…naa..aaam aya…aaa”nilijikuta nikijibu kwa kigugumizi kisha yule jamaa akafungua Mlango wa gari hilo kisha akanisukumiza kwa nguvu na kutoka katika gari hilo huku nikidondoka na kuumia mguu wangu wa kushoto kisha gari hilo haraka likaniacha mimi pale ambako baada ya kusimama nilipagundua mapema palikuwa ni pale pale waliponikamata jana yake ambapo palikuwa karibu kabisa na nyumbani.Nilifika nyumbani huku nikichechemea na kisha nikaingia haraka ndani kwangu bila mtu yoyote kuniona niliangalia saa iliyopo chumbani kwangu na kugundua ilikuwa kama saa kumi na mbili jioni.nilienda kuoga kisha nikajitupa kitandani na kuiwasha simu yangu iliyokuwa nimeiweka chini ya mto katika kitanda changu na kubonyeza kitufe cha kuwasha ambapo nikakuta missed call mia moja na messeji Themanini nikazifungua nakukuta nyingi zikiwa za moureen ambazo kwa utulivu nikaanza kuzisoma “vp baby mbona upoke na mbona ujaja chuo nimekumiss vp wewe”ilikuwa ni miongoni mwa messeji ambazo kabla hata sijaendelea simu tena ikaita na nilipoangalia nikaona jina la moureen mpenzi likitokea katika screen ya kioo cha simu yangu
“Haloo vp pablo jamani”
“Kesho nakuomba tuonane raha resort restaurant”
“lakin……..”Nilikata simu kwa uchungu kisha nikamtumia sms saa ya mimi na yeye kuonana katika hotel hiyo ambayo mara nyingi tulipenda kwenda
*-*-*-*-*-*-*-*-*-*-*-*-*
Saa ziliyoyoma na giza likaachia mwanga uchomoze na kuashiria siku mpya inaanza.bila ya kupoteza muda mida ya saa nne nikiwa nimevaa nguo zangu zilizonipendezesha sana.Nikaiwasha simu yangu iliyokuwa nimeizima kutokana na moureen kunisumbua sana kisha Mdogo mdogo nikatoka na kuchukuwa bajaj ambayo hakuchukuwa hata dakika thelathini nilikuwa nimeshafika katika hotel hiyo raha resort ambayo baada kumlipa mwenye bajaji nikaingia na kuanza kumtafuta moureen ambaye alishanitumia messeji kwamba alishafika.Sura yangu ikagonga kwa mwanamke ambaye ilionyesha uzuni mkubwa katika sura yake huku mavazi aliyovaa yalimpendezesha sana nilienda na kumgusa bega ambapo bila ya hiyana akageuka na kunikombatia huku ajibenua na kupeleka mdomo wake katika mdomo wangu ambapo kwa uchungu na simanzi zito nikamtoa
“whats wrong(tatizo nini) mbona sikuelewi yani siku hizi mbili umetesa sana kwa sababu ya kukuwaza”
“oooh moureen nataka tuachane”
“sijakuelewa unasema???”
“na…taka tuach..anee”nilisema kwa shida baada ya kushuhudia kwa mara ya kwanza moureen akidondosha chozi na kuniangalia mimi hali ambayo ilipelekea na mimi chozi kunidondoka
“kisaaa…nini??”
“Ro..bert Mugalula Ndi…”nilijikuta nikisita huku jina hilo nililolitaja likamshtua kidogo moureen ambaye bado machozi yaliendelea kumtiririka huku akiniangalia
“Can i kiss you now(naweza kukubusu sasa)”moureen aliniuliza swali hilo katika hali ya sauti ya kudeka hali iliyosababisha nishindwe kujizuia na kumkombatia kwa nguvu moureen kisha wote tukaanza kudendeka huku kila moja kutojali watu ambao walionekana kushangazwa na tukio hilo lakini ghafla simu yangu ikaita jambo ambalo lilinishtua na kujikuta nikimtoa moureen ambaye hakuwa tayari kabisa kuniachia niliangalia kioo cha simu yangu na kuangalia namba inayonipigia na kukuta namba ngeni jambo ambalo lilinifanya nipokee simu kwa uoga
“Sali sala zako za Mwisho Bitch(malaya)”
…………….
Nilijikuta nikianza kutetemeka baada ya Namba hiyo kukata simu kabla hata sijaongea chochote.Macho yangu yalikuwa yamenitoka huku majasho yakianza kunitoka mwilini mwangu hali iliyosababisha Moureen aanze kunishangaa
“Whats wrong pablo??(tatizo nini)”moureen aliniuliza lakini sikumjibu nikaanza kurudi nyuma nyuma hali ambayo moureen bado alikuwa haelewi
“unaenda wapi sasa??”nilijikuta kama nimechanganyika na kuanza kukimbia na kuelekea nje jambo ambalo lilimfanya nae moureen naye kunikimbilia lakini kabla hata sijaufikia mlango wa kutokea Nje milio ya risasi ikanipitia karibu kabisa katika masikio yangu na kunikosa na kwenda kuwapata waliokuwa mbele yangu ambao papo hapo wakadondoka na kufa hapo hapo jambo ambalo lilishtua watu wote katika hotel na kusababisha watu kuanza kupiga makelele na kuanza kukimbia hovyo ndani ya hoteli bila ya kutojua risasi imetokea wapi.kukimbia hovyo hovyo kwa watu kulisaidia kwa kiasi kikubwa mimi kutoka nje lakini Nje ndipo kulikuwa Na magari mengi meusi ambayo baada ya kuyaona Nikajikuta nikirudi ndani na kupotezana kabisa na moureen aliyekuwa akinikimbilia lakini hakufanikiwa kunipa kutokana na hata yeye kuchanganyikiwa na milio ya risasi.niliingia ndani kabisa ya hoteli na kuelekea moja kwao moja katika Miongoni mwa meza kubwa na kujificha chini ya Meza hiyo.macho yangu yalishuhudia watu wote wakiambatana na Wafanyakazi wa hoteli hiyo wakikimbia na kuacha hoteli yote ikiwa tupu ni mimi tu ndio niliyebaki huku nikiwa nimejificha katika meza kubwa ambayo iliniwezesha kutoonekana na kuona yaliyokuwa yanaendelea.nikiwa katika hali ya kukodoa macho ghafla watu waliovaa suti kama kumi wakiongozana na Robertson mugalula wakiwa wameshika bunduki wakaingia katika hotel hiyo na kuanza kunitafuta kila pande na kilichozidi kuniogopesha walipoanza kuangalia pia chini ya meza zilizokuwa zimedondoka na kunipa hofu kubwa.nikiwa natetemeka huku Bado majasho yakiendelea kunitoka nikaanza kuomba dua ili Mungu aweze kufanya miujiza kutokana na hali kuwa Mbaya.kwa macho yangu niliona kiatu kikali aina ya foengo kikiwa kinakuja kabisa katika mezi niliyokuwa na kushababisha mimi nitulie na kujikunja tuli kama Nyoka na kuendelea kumuomba Mungu afanye miujiza yake.Alifika pale na kuianza kuishika meza hiyo ambayo mimi nikiwa chini ya meza hiyo akiwa na lengo la kuinyanyua.Akiwa katika harakati ya kuinyanyua ghafla king’ora cha mlio wa gari la polisi ulisikika kwa nguvu hali iliyomfanya aichie meza kisha kwa mwendo wa speed akanzaa kukimbia kwa kutoka nje akiambatana na wenzake.hapo ndipo na mimi nilipopata nafasi ya kutoka na kufanikiwa kuwachenga mapolisi ambao baada ya mimi kutoka ndipo walipoingia wakiwa wamejiandaa vya kutosha.hakika mihemo ya kunusurika ndio ilichukuwa nafasi yake katika mwili wangu huku nguo zangu nilizovaa zikiloa zote kutokana na majasho mengi yaliokuwa yakinitiririka.hakika ilikuwa ni jambo jipya kabisa katika maisha yangu kwa sababu sikuwahi kutokewa na msukosuko kama huu wakataka kabisa kuuliwa niliendelea kujilaumu sana kutokana na kukaidi onyo nililopewa lakini nguvu ya mapenzi ndio yalinifanya nishindwe kabisa kujihimili mwenyewe.hakika hata kwa muda huo kwenda nyumbani nilianza kupaogopa kwa sababu nilihisi kama watakuwa wanapajua.mawazo ya kwenda kwa shangazi yangu ndio yalichukua nafasi yake na kukata shauri ya kwenda kwa kuchukua bajaj ambayo nilitegemea kwa vyovyote itaweza kunifikisha haraka.nilienda kuchukua bajaj ambayo kwa haraka ikaanza kwenda huku nikiwa bado nawaza.nikiwa katika dibwi la mawazo ghalfa simu yangu ikaita nikajikuta nikiipokea bila hata ya kuangalia nani aliyekuwa anapiga.
“haloow baby vp upo salama??,upo wapi??” ilikuwa sauti ya moureen niliyosikia hakika nilivyochoka nilijikuta nikiikata simu hiyo kutokana na ukweli kwamba nilishajichokea na maisha lakini ile naikata tu messeji ikaingia kwa uvivu nikaiangalia na kukuta ni ile namba iliyonambia nisali sala zangu za mwisho na kunifanya moyo wangu tena uanze kudunda kwa kasi ya ajabu na kuchoka kabisa.kwa simanzi zito nikajikuta nikiifungua huku nikiwa na uoga kabisa wa kuisoma hiyo messeji iliyosomeka
“PABLO PABLO,UNAVYOFIKIRIA UNAWEZA UKANIZIDI AKILI HATA MIMI SASA BASI NATAKA UCHAGUE MOJA KUUA WEWE AU SHANGAZI YAKO NA FAMILIA WASIO NA HATIA HAHAHAHA CHAGUO NI LAKO
” hakika macho yangu hayakuweza kuamini messeji ile iliyotumwa niliendelea kuisoma kwa kuirudia kama mara kumi hivi huku akili yangu haukataka kuamini kabisa kwamba mtego uliobaki nilikuwa siponi kabisa.Kwa haraka haraka nikamlipa mwenye bajaj na kushuka kutokana na kufikia karibu na maeneo ya nyumbani kwa shangazi nilitembea kwa tahadhari kwa kujifificha mpaka pembezoni kabisa karibia na nyumba ya shangazi.
“Eee Mungu wangu!!!!”nilijikuta nikilalamika baada ya macho yangu kutua kabisa katika nyumba ya shangazi huku njee magari kumi meusi yakiwa yamepaki nje ya nyumba yake.nilijikuta nikikata shauri ya kwenda lakini kabla hata sijanyanyua kwato zangu Nilimshuhudia robertson Mugalula akitoka ndani ya nyumba ya shangazi akiwa anasindikizwa na bodyguard zake wakiwa wamemkamata shangazi na mumewe aliambatana na mtoto wake wa kiume na kuingizwa ndani ya moja kati ya magari yale kumi meusi kisha nikaona vumbi tu likitumika baada ya magari hayo kuondoka kwa kasi ya ajabu…………
Hakika nilijikuta nikiganda kama mtu aliyepigwa shoti kali sana mwili wangu uliokuwa umelowa jasho ndio ulizidi kumiminika majasho ambayo licha yakuwa hali ya hewa ni ya kawaida isiyoleta joto lakini mimi nililowa mwili mzima.Hali ya kukamatwa kwa shangazi yangu na familia yake ilileta gumzo mtaani hapo ambapo hakuchukua hata nusu saa Majirani walijaa na kila mtu akiwa anasema lake.Akili katika kichwa changu haikuweza kusoma chochote kila njia nilikuwa nikiifikiria ya kuweza kujikwamua katika hili nilikuwa sipati jibu.Siku sita kutoa machozi aliyokuwa yakinitiririka katika mashavu yangu huku nikiwa siamini kabisa kama Mapenzi ndio yalikuwa tatizo.Nikiwa katika dimbwi zito la mawazo simu yangu ya mkononi ikaita tena na kuingalia nakukuta Jina la moureen likitokea katika screen ya simu yangu nilijitutumua na kuiweka sikioni kwa hali ya unyonge
“Hey upo wapi moureen”
“baby ulitoka salama ba..”
“upo wapi??”
“nipo njiani naelekea home”
“basi njoo mitaa ya nyumbani mara moja sasa hivi”
“mm lakini…”
“lakini nini do you love me..njoo mara moja”
“love you baby nakuja”nilijikuta nikihema baada ya kumaliza na moureen ambaye nilimuambie aje nyumbani.Akili yangu ilishavurugika nakukubali liwalo na liwe kichwa changu kilikuwa kishapata usumbuzi wa tatizo hilo huku mawazo ya kuwapata shangazi na familia yake ndio ilichukua nafasi yake.niliamini sitaweza kumpata shangazi yangu bila moureen.Haraka haraka nikaenda duka la madawa na kununua dawa ya usingizi kisha haraka haraka nikachukua bodaboda ambayo kwa haraka ikaweza kunifikisha Mtani kwetu ambapo sikuweza kwenda katika nyumba yangu niliyopanga kutokana na kuogopa kupatikana kirahisi na robert mugalula.nikaenda dukani na kununua maji ambayo nikaweka ile dawa ya usingizi kisha nikaenda sehemu ambayo nilimwambia moureen aje hapo.Macho yangu yakatua katika gari kali jeusi la moureen ambalo mara ya kwanza nilitaka kukimbia kwa kuangalia vibaya labda linaweza likawa la kundi la akina robert lakini kutokana na kumjua vizuri niliweza kumtambua kupitia kioo cha gari yake.bila ya kuchelewa moureen akafunga breki na kufungua mlango wa gari yake na kuniruhusu mimi kupanda nikaingia na ukaribisho wa mabusu mazito na moureen ambaye aliyeonekana kuumisi sana mchezo huo ambayo kwa wakati huo sikuwa na hamu nao.mkononi mwangu nilikuwa nimeshika chupa yangu ya maji ambayo kwa taratibu nikapa maji hayo moureen
“moureen unaonekana una kiu hebu kunywa maji haya kidogo”
“jamani umejuaje nipe”sikutaka kuchelewa nikayafungua yale maji yenye dawa ya usingizi nakumpa moureen ambaye kwa taratibu akaanza kunywa pole pole na kuyanywa mpaka nusu huku akiniangilia kwa macho ya kurembua.
“hivi pablo nataka uniambie kwani kule hotelini ilikua…..” kabla hata hajamalizia sentensi moureen akashika kichwa chake na kuanza kulalamika na hakuchukua hata muda usingizi mzito ukampitia.bila ya kupoteza muda nikaliwasha gari lake na kuanza kuliendesha huku mkononi nikichukua simu yangu nakuanza kutafuta namba ya robert Mugalula kisha nakuipiga ambayo kwa muda kidogo ikaita kisha ikapokelewa
“kijana pablo kumbuka una masaa ishirini na nne tu ya kuchagua kujisalimisha ili familia yako isiendelee kuteseka au unaweza ukaacha na tutakuleta maiti.”
“Na mimi nakuambia hivi ugomvi ni mimi na wewe na kama utaiachia familia yangu basi na mimi nitamuua moureen ambaye nipo naye kwa mikono yangu.”
“unasemaje kijana??”.hakika nikakata simu kwa kujiamini na huku macho yangu nikimuangalia moureen ambaye wakati huo alikuwa yupo katika usingizi mzito kabisa.nilianza kuliendesha gari hilo kwa uangalifu na kwenda kulipaki sehemu ya kujificha huku na mimi nikilala humo humo ndani ya gari.hakika hali ya hofu ikaanza kunitanda baada ya kushika simu ya moureen na kukuta messeji nyingi za mapenzi baina yake na robert jambo ambalo liliniumiza sana moyo wangu.simu katika simu yake zilikuwa zikiingia kwa wingi na kunifanya niingiwe na hofu ikifuatiwa na simu yangu ambayo katika mida ya saa nne ikaingia messeji iliyozidi kuninyong’onyesha
“KIJANA KUMBUKA KWAMBA UTAPOINGIA KATIKA MIKONO YETU KICHWA CHAKO MALI YETU
“maneno hayo yalinitia hofu huku nikibaki kujiamini tu na kuzidi kumuomba mungu aniwezeshe kuipata familia yangu.usiku mzima mimi na moureen ambaye kwa wakati huo alikuwa bado yupo katika usingizi tulila na katika mida ya saa mbili asubuhi nikaamka na kuanza kuelekea chuo kwa kutumia usafiri wa wake.lakini kabla hata sijafika moureen akashtuka na kujishangaa akachukua simu na kuangalia saa zilizoambata na missed call na messeji na kunifanya niwe na hofu baada ya kuniangalia kwa hasira.akachukua chupa ya maji aliyokunywa na kuinusa kisha kwa hasira akanipiga nayo.
“Pablo ndio umefanya nini sasa??”
“moureen sikia nikwambie…ya..”
“yani wewe wa kunifanyia mimi hivi Pablo unaninyesha dawa ya usingizi ili nilale na wewe mpaka…aaa sasa mbona umenitafutia matatizo nitaenda kusemaje nyumbani eee pablo nijibu..aaaa nakuomba shuka kwenye gari yangu.”moureen alisema maneno yale kwa uchungu huku akinikunja shati langu kwa hasira kubwa kisha akafungua mlango la gari lake na kuanza kunifukuza hakika nilijaribu kumuelewesha lakini bado alikuwa mkali na hakutaka kusikiliza chochote.
“Nakuambia toka masikini wewe”maneno yale yaliotoka katika kinywa cha moureen yaliniumiza na kunifanya nitoke huku nikiwa na mawazo.lakini ile naangalia tu gari la moureen likiondoka kwa kasi ghafla macho yangu yakakutana na robert ambaye sura yake ilikuwa imekunjamana kwa hasira kali.nikiwa katika harakati za kuanza kukimbia nilisikia mlio wa pikipiki ambapo baada ya kugeuka nikaona pikipiki ikija kwa kasi karibu yangu na kufanya niikwepe lakini ile naikwepa tu nikapigwa rungu kubwa la kichwa na dereva huyo wa pikipiki na kuachia mlio mkali wa maumivu kisha mdogomdogo nikaenda chini na kiza kinne kikachukua nafasi yake katika mboni ya macho yangu.
*-*-*-*-*-*-*-*-*-*-*
“oooh aaaaaaaaaaaaa” fahamu zilizirudi na huku maumivu ya kichwa kuchukua nafasi yake nakufanya nitoe ukelele wa miguno.macho yangu yalitua katika mataa taa yaliokuwepo ndani ya jumba hilo lililonipa shauku kubwa la kunyanyuka kwa sababu mpaka muda sikujua nipo wapi.nikiwa katika harakati za kurudisha kumbukumbu zangu zilizopotea wakati huo ghafla maji ya baridi yaliokuwa na barafu barafu yakatua kabisa katika mwili wangu na kunifanya nipige ukelele kutoka na baridi kali nililoanza kulisikia huku kumbukumbu ya yaliotokea nyuma yakija kabisa katika kumbukumbu zangu.nikanyanyuka haraka haraka lakini nikajikuta nikirudishwa chini na kamba ambayo ilioanza kufungwa na kuzunguka kiuoni changu.nikiwa katika tahamaki Macho yangu yakatua kwa robert ambaye wakati huo alikuwa amekombatia na moureen ambaye wakati huo alikuwa katika nyuso za uzuni.baba yake moureen alikuwepo naye akiambata na mama yake moureen aliyekuwa ananiangalia kwa dharau.
“Pablo kama umeshavua nguo hauna budi kuyaoga hahaha…….
Sehemu Ya 6
Maneno hayo aliyesema robert akiwa kamshika kiuno moureen jambo ambalo liliniumiza kiasi fulani jambo ambalo lilionekana katika furaha ya wazazi wa moureen ambao wote walikuwepo wakiwa wananiangalia kwa dharau
“sasa kama nilivyokuambia nataka tucheze kamchezo kidogo hebu James walete haooo” hakikupita hata dakika robert akamuita james ambaye alikuwa na mwili mkubwa wenye mazoezi na kumfanya aonekane kama mcheza mieleka.james akaenda mpaka kwenye mlango ambao ulikuwepo mbali kidogo na mimi na kuingia kisha akatoka na mashine kubwa iliyokuwa nzito kutokana na jinsi alivyokuwa akiiburuta.Macho yangu sawa sawa yakatua katika shangazi yangu akiongozana na mjomba na mwanae ambao walikuwa wamefungwa kamba shingoni kwa kila mmoja ambao wote walikuwa wanaugulia kwa chini chini kutokana na kufungwa vitu vigumu mdomoni.hakika niliumia sana baada ya kumuona hata mtoto mdogo wa miaka nane mtoto wa shangazi naye akiwa anaburuzwa kama ng’ombe huku naye akiwa anatokwa na machozi ambayo yalisababisha na kufungwa kwa kamba hiyo shingoni.
“jamani ee mnaugomvi na mimi kwanini mnawaoneea watu wasiohusika sasaaaaaaaa”nilijikuta nikisema kwa uchungu hali iliyosababisha james aje pale na kunipa ngumi kali sana ya mdomo na kunifanya nitapike damu kutokana na uzito wa ngumi hiyo iliyonipelekea maumivu makali yalionifanya nidondoshe chozi.hakukawa mtu wa kupoteza muda james akaninyanyua kisha akanifunga kamba kiuoni ambayo ilionganishwa mpaka katika mashine ya kuzunguka ambayo pia kamba hiyo iliwafikia shangazi,mjomba na mtoto wa shangazi.kisha mimi nikasogezwa umbali mrefu sana baina ya mimi na familia yangu kisha james akachukua bunduki na kuanza kupiga risasi taa kubwa za humu na kufanya vyupa vingi vikubwa kudondoka kisha na kuwashwa taa zingine kutokana na zile kupasuka na kusababisha kiza kwa sekunde kama kumi hivi.james akapiga makofi ambapo vijana wawili ambao sikujua wametokea wapi pia nao wakaja na mapipa mawili ambayo wakayafungua na kumwanga vyupa vingi vyenye ncha kali katika sakafu kutoka nilipo mimi mpaka kwa familia ya shangazi.hakika kwa muda huo sikuwa naelewa nini nilikuwa namuangalia shangazi yangu na mjomba akiambatana na mtoto wao kwa huruma kutokana na kuwasababishia matatizo ambayo hata siku moja sikuwai kurifikilia katika maisha yangu.akiwa na kipaza sauti ambacho kilishikwa na robert ambaye alianza na haloo haloo ambayo ilinifanya nimuangalie kisha kwa hali ya tabasamu aliyonionyeshea akiambata na wazazi wake ni moureen tu ambaye kwa kiasi kikubwa alionyesha uso wa huzuni wenye simanzi nzito huku akikwepesha macho yake wakati nilipogeuka kumuangalia robert na kisha nikamuangalia yeye.
“Sasa Basi umeona vyupa hivyo Pablo kama unataka Kuikoa Familia yako Unatakiwa upite hapa katikati ya vyupa hivyi kwa dakika kumi lakini tena haraka haraka kama ukichelewa kumbuka na mashine ile itajinyonga nyonga kama unakwenda kwa mwendo mdogo utasababisha familia yako akianzia Shangazi yako atanyongwa na kamba hiyo akiambata na wanaofuta sirudiii” hakika hali ya kuchanganyikwa ikachukua nafasi yake huku kutoelewa maana ndio ilikuja kabisa katika kichwa changu na kunifanya nishangae kwa kuangalia urefu wa sehemu na vyupa vingi vilivyokuwepo hapo.nikiwa katika hali ya kupigwa butwaa nikashtulia na kofi zito la uso na kunifanya nitoe miguno ya maumivu kutokana na uzito wa kofi hilo kutoka kwa james
“Simamaaaaaaaa”sauti ya kukoroma yenye ukali kutoka kwa james ndio kilikuwa kishawishi cha mimi kusimama na kwa kufumba macho haraka haraka nikwangalia akina shangazi na kwa kujiamini nikaanza kutembea katika vyupa hivyo haraka haraka.
“aaaaaaaaaaaaaaaaa uuuuuuu mamaaaaaa”hakika nilipata maumivu makali sana kutokana na kukanyanga vyupa kimoja chenye ncha kali sana na kutokeza kwa njee katika mguu wangu wa kulia na kunifanya niiiname kwa kuugulia jambo ambalo lilinigharimu kwa sababu kuniama kwangu mimi kulisababisha shangazi yangu akabwe sana na kamba mpaka kusababisha kuchana plasta alizibwa nayo mdomoni na kutokana na maumivu ya kamba hiyo iliyosababisha kuanza kutoa ulimi njee huku akitoa macho kwa sana.na kunifanya nisikwe na uoga uliosababisha nisimame na kutaka kutembea lakini kutokana na maumivu makali nikajikuta nikidondoka.
“Noooooooooooooooo….
Nilimshuhudia shangazi akitoaa macho ukiambatana na ulimi alioutoaa nje kisha nakuianama huku akiwa amesamama kutokana na mnyororo ule aliofungwa ambao ulinifikia mpaka mimi kiunoni.Hakika sikuwa nala kufanya nguvu za kusimama ziliniishia kabisa huku nikiwa nimepiga magoti nilisikia kelele za Mume wake shangazi akiambatana na mwanaye mdogo wakitapatapa kutokana na kukabwa sana na mnyororo nilijitahidi kutaka kunyanyuka kwa sababu hatima yao ipi mikononi mwangu lakini Miguu yangu ilikataa kata kata niliendelea kulia kwa uchungu kutokana sikuwa na uwezo wa kuwaokoa tena.
“Dady Noooo stop it dadyyy!!!(baba hapa basi baba) sauti ya moureen nikaisikia ikichanganyika na kilio cha nguvu kilichonisababisha nitake kugeuka lakini nilishindwa.kelele za vibao vikali nilivyofikia vilidhihirisha kabisa alikuwa anapigwa Moureen ambaye baada ya vibao hivyo sikumsikia tena moureen akipiga kelele.Nilipo rudi kuwaangalia Mume wako shangazi na mwanae walikuwa washamfuata shangazi wote walikufa kifo kilichosababisha na mimi huku nikishuhudia kwa macho yangu.mwili wangu ukaanza kutetemeka kwa hasira kali za hali ya juu machozi yalizidi kunitiririka na kuogesha mwili wangu huku majasho nayo yakichukua nafasi katika mwili wangu huku nikiwa nimekang’ata meno yangu kwa hasira iliyonifanya nikunje ngumi.Nguvu za ghafla zikaingia katika mwili wangu nakujikuta nikinyanyuka ghafla na kuanza kuwageukia baba yake moureen aliyekuwepo na mke wake,robert akiwa kamkumbatia moureen ambaye wakati huo alikuwa analia kimyakimya wakiambata na mabody guard wake wanne.Kwa mwendo wa kukimbia nikaanza kuwafuata jambo ambalo liliwastua wote huku mabody guard wale nne wakianza kujiandaa vyema.mikononi nilikuwa sijafungwa kitu mnyororo niliofungwa ulikuwa kiuoni lakini haukunipa shida kukimbia huku nikiwa nawafuata na huku nikikanyaga vyupa bila hata ya kusikia maumivu.nikajikuta nikimrukia body guard yule alinipiga vibao vya kuniamsha na kumng’ata katika shingi yake kwa nguvu huku yeye akinisambulia kwa ngumi nzito ambazo maumivu yake sikuyasikia.body guard yule alijitahidi sana kufurukuta lakini nilimzidi nguvu kwa kumng’ata sana mpaka kuanza kumtoa damu shingoni kwake na kumfanya adondoke na kuaga dunia.Nikaanza kumsogolea robert ambaye wakati huo alikuwa hana la kufanya wakati huo alibaki akiwa anashangaa Baada ya kuniona nikiwa katika hali ile hakika nilikuwa kama nimechanganyikiwa huku nikiwa na damu mdomo baada ya kumng’ata mmoja katika ya mabody guard wa robert
“Hebu mdhibitini huyo..”robert aliwaamrisha mabody guard wake ambao wakati huo walikuwa wanatetemeka kwa uoga kutokana na hali ambayo ilisababisha mama yake moureen akiambatana na baba yake kukimbia.sikuwa na muda wa kupoteza nikaanza kuwatandika mabody guard wale kwa ujuzi ambao mpaka sasa nikikumbuka uga natabasamu mpaka kupelekea wote kuwazimisha.kisha nikaanza kumsogelea robert ambaye baada ya kuona wafanyakazi wake washashindwa akachomoa bunduki kwa lengo la kunipiga jambo ambalo nililiona nakuanza kumvamia nakuanza kuigombea bunduki aliyoshika huku kila mtu akitumia nguvu zake.tukiwa katika harakati za kugombania ghafla mlio wa risasi ukasikika na nilipoangalia ilikuwa ni risasi iliyonipata mimi sawa sawa katika tumbo hali ambayo ilinifanya nitulie na kuanza kuangalia damu zilizokuwa zikinibubujika katika tumbo langu
“Hahaha sasa niwakati wakusali sala za mwisho kwa sababu ni muda wa kukumaliza”robert alisema Maneno yale huku akiwa ameniwekea bunduki kichwani baada ya mimi kupiga magoti na kuanza kushikilia sehemu niliyopigwa risasi hiyo.
“One!!!,twoo!!!three”huku akihesabu robert ile anataka kufyatua risasi tu kitu kizito mfano wa chuma ukasikika ukilia katika kichwa chake na kumfanya atoe ukelele wa maumivu makali na kumfanya adondoke chini kwa maumivu huku akiidondosha bunduki ile na kuanza kuugulia.niliangalia na kumuona moureen akiwa kashika chuma lile akiashiria kuwa ndiye yeye aliyempiga na kuanza kunisogelea kisha akanikombatia akiwa analia.nikiwa nimekombatiwa ukungu mweusi ulitanda katika macho yangu uliosababisha nizimie na kutojua kinachoendelea.
*-*-*-*-*-*-*-*-*-*-*
Hali ya baridi iliyosababishwa na kiyoyozi ndio iliniamsha na kunifanya nianze kuangalia huko na huku Nilijikuta nikiwa ndani ya gari ambalo pembeni mwangu alikuwepo moureen ambaye alikuwa ameshalala katika gari hilo.Kumbuku ya yaliotokea yalinijia katika kichwa changu na kunifanya nishike sehenu niliyopigwa risasi na kukuta bandeji kubwa iliyofungwa kiustadi na kiujuzi wa hali ya juu.kukuru kakara zangu zilisababisha nijitoneshe vidonda vya miguuni nilivyojikata na vyupa vile na kunifanya nianze kupiga kuugulia kwa kunung’unika kutoka na maumivu makali ya vidonda hivyo.Kumbukumbu ya yaliotokea kwa familia yangu ikibainisha kifo cha shangazi na familia yake ilinijia kichwani kwangu na kunifanya nianze kulia kilio kikubwa kilichomshtua sana moureen Niliyemshtua kutoka usingizi kutokana na kilio kikubwa nilichokuwa natoa
“Am sorry sana Pablo halikuwa kusudio Langu ni familia yangu mimi nakupenda sana”hakika siku na jibu la kumjibu moureen nilibaki tu nikilia Mapenzi bana sikuwahi hata siku moja kuja kutarajiwa kuwa yatakuja kunitesa kiasi hicho na kusababisha vifo vya familia yangu wakiwa hawana hata hatia.sikuhitaji kumchikia moureen lakini familia yake Niliichukia na huku kimoyomoyo mawazo ya kulipiza kisasi ndio ilikuwa fikra mpya katika kichwa changu.
“pablo haina haja ya kulia sasa inabidi tuanze kupambana na familia yangu ambayo inatutafuta kwa lengo la kutuuua kumbuka nafanya hivi kwa ajili yako nawageuka familia yangu na kuwa upande nafanya hivi sababu Nakupenda Pablo Nakupenda”maneno hayo aliyasema moureen akiwa machozi yanamdondoka katika mashavu yake.Nilimsogelea na kumkombatia huku na mimi Nikiwa nalia kisha wote tukajikuta tukianza kunyonyana denda zito lenye majonzi ya furaha ndani yake.ghafla simu ya moureen ikaita na alipoangalia Akaona namba ya Baba yake akaipokea na kuweka loudspeaker ili tusikie wote.
“WEWE NI MWANANGU NA KAMWE HAUWEZI KUNIKIMBIA MIMI NAPENDA KUKWAMBIA NIKUKAMATA WEWE NA HUYO MBWA WAKO VICHWA VYENU HALALI YANGU”…….
Sehemu Ya 7
Baada ya kusema maneno hayo yaliokuwa yakitoka kinywani kwa baba moureen kupitia kwenye simu wote tukajikuta kwa hofu tukiangaliana huku kila mmoja akiwa ana waza lake tukiwa ndani gari hilo huku mimi nikiendelea kukiangalia kidonda changu ya sehemu niliyopigwa risasi.tukiwa katika hali hiyo ghafla simu ya moureen ikaita tena na kwa shauku kubwa wote tukajikuta tukiweka mkazo wa umakini kuangalia simu hiyo iliyokuwa ikiita.
“Moureen unaendeleaje huko.”
“Baba amenipigia simu na kuongea maneno ya kutisha huku akisisitizia akitukamata basi vichwa vyetu halali yake”
“Dooo vp Pablo anaendeleaje hapo.”
“Kidogo anaendelea vizuri.”
“Pouwa basi ondokeni haraka sana kutokana sasa hivi wameichukua simu yako na kuanza kuingiza katika computer kwa lengo la kujua upo wapi.”
“sasa tuelekee wapi doctor”
“Bagamoyo nendeni mpaka makumbusho ya taifa kisha kachukueni vile vyumba vya kule ufukweni muutulie kisha tupa hiyo laini na sajili nyingine halafu nicheki hakika unampa dawa pablo anywe.” simu ilikatika na kumfanya moureen ashushe Pumzi ndefu na kuniangalia mimi niliyekuwa namuangalia kwa makini moureen.hakusita kunisimulia habari ya doctor aliyekuwa akiongea naye huku akisema kwamba ndiye yeye alinisaidia kunitoa risasi niliyopigwa na kunitibia vidonda vyangu vya mguu nilivyojichoma na vyupa na tena akiendelea kunisisitizia kwamba kwa sasa ni yeye tu ndiye mkombozi wetu kutokana na kutupa kile kinachojiri kutokana na yeye kuwa daktari akina moureen nyumbani kwao.Bila ya kupoteza muda moureen akawasha gari kwa mwendo wa haraka na kuliingiza katika barabarani kutoka katika msitu mnene niliokuwa siufahamu kwa muda huo kutokana na kutotaka kuuliza.kwa mwendo wenye spidi ya hali ya juu moureen akafanikiwa kufika mwenge mapema tu na kukuta foleni katika mataa ya pale mwenge kuelekea lugalo foleni ambayo ukubwa wake ulitufanya tuingie hofu.tukiwa katika hali ya foleni katika barabara hiyo la mwenge ghafla kundi kubwa la watu waliokuwa katika pikipiki huku wakivaa suti nyeusi wakiambatana na miwani wakaanza kuzunguka katika foleni hiyo huku wakikagua kila gari watu waliokuwepo humo.hali ya hofu ikatanda dhidi yetu huku na kuanza kuomba mungu.Lakini kabla hata ya kufika kwetu taa za kuruhusu magari ya upande wetu ikawaka na moja kwa moja moureen akachomoza gari haraka na kuwapita baadhi ya magari kwa kuovertake haraka haraka jambo ambalo halikuonekana na matraffic na wale watu waliovaa suti na kuwaacha wakibaki wakikagua magari mengine.Hakika baada ya kupita pale hatukupata vizingiti vingine huku kwa saa kama saa tatu usiku tukafanikiwa kufika bagamoyo Na kutokana na moureen kuwa na pesa akachukua chumba ambacho kwa usiku huo tukalala wote kwa mara ya kwanza na kutofanya chochote na kulala mzungu wa nne katika kitanda kimoja.hakika siku zilizidi kuchomoka huku moureen akizidi kuwasiliana na doctor huku akizidi kutupa habari zilizozidi kunichanganya kwa sababu aliniambie wanataka kupandika picha za wanted kuwa mimi nimteka moureen.tulikaa siku kama Nne katika chumba hicho huku hali yangu vidonda vyangu vikiendelea vizuri na kunifanya nijisikie mzima huku vidonda vyangu vikipona kabisa.ilipofika siku ya tano usiku tukiwa ndani ya chumba cha hoteli ambayo tumepanga Tukiwa tunaangalia Movie iliyokuwa ikionyesha kwenye dstv ndani ya television iliyokuwepo chumbani humo ghafla scene ya mapenzi ikaanza kuonyesha kwenye movie hiyo na kusababisha moureen aniangalie kwa macho maregevu kisha akanisogelea
“Baby tangia uwe na mimi hatujawahi kusex niliku….”kabla hata moureen hajamaliza akaanza kunishika koki yangu iliyokua ina hamasika kidogo kidogo kwa kuangalia movie hiyo iliyokuwa inanisisimua.hakika sikumjubi chochote nikapeleka mdomo wangu katika mdomo wake na kuanza kunyonyana naye denda huku mkono wangu ukianza kuchezea matiti yake na mwingine nikipapasa ikulu yake hali iliyomfanya moureen akiruka ruka huku akihema kwa kutuo miguno ya raha iliyokuwa inanisisimua kwa hali ya juu.hakika ilipita kitambo sana sijafanya mapenzi kwa hiyo chance ile aliyonipa moureen niliona kama lulu huku nikijikuta nikipania mechi na kuanza kumvua nguo moja moja moureen aliyekuwa analegea pole pole.lakini baada ya kumvua nguo kabla hata hatujaendelea simu yake ikaita na kunifanya nisite kuendelea kumchezea moureen huku moureen mwenyewe akitaka kuipuuzia simu hiyo.nilijikukota kiuvivu na kuangalia ni nani aliyekuwa akipiga.si mwingine bali alikuwa ni dokta nikaipokea kwa tahadhari kubwa na kuanza kumsikiliza.
“Hakikisheni mnaondoka Haraka Washafika b……….” simu ile ikanichanganya baada ya kukatika na kumuambia moureen ambaye baada ya kusikia taarifa hilo alikurupuka kwa haraka na kuanza kuvaa kisha wote tukatoka na kwenda kulipia haraka haraka na kwenda kuchukua gari letu lakini ile tunaingia barabarani kwa lengo la kuondoka baada ya kuingia Katika gari.
“Paaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa”Mlio wa kupasuka katika kioo cha gari yetu ukasikika ukifuatiwa na ukelele mkali kutoka moureen aliyeokena kudhurika kwa kiasi kikubwa kutokana na kioo kuvunjikia karibu yake kutokana na yeye kuwa dereva..
Baada ya kutoa ukelele huo moureen akazimia na kushababisha gari ianze kuyamba yumba jambo lililonifanya nianze kwenda kukaa sehemu hiyo ya udereva kwa shida ili niendeshe mimi kutokana na gari hiyo kutaka kupoteza uelekeo kutokana na mshtuko alioupata moureen aliyekuwa akiendesha gari na kumfanya azimie baada ya risasi kuvunja kioo hicho.kabla hata sijaanza kukanyaga breki ili kupata uelekeo mzuri wa gari hiyo lilokuwa likiyumba yumba ghafla gari letu likapigwa kikumbo kikali na gari nyingine na kushababisha gari letu kuvamia genge la vitu vya sokoni lililokuwa limefungwa usiku huo na kufanya nipate maumivu makali kutokana na kugongwa gongwa na mbao zilizoambata na mabati ambayo hayakusita kunikata pale yalipogusa mwili wangu.Ila licha ya kuingia katika mkumbo huo wa kuvamia genge lakini gari letu halikuzimika huku mimi nikiwa bado naliendesha na kukanyaga gia namba sita ambayo ilikuwa inasaidia gari letu kwenda kwa kasi ya ajabu.Nyuma yetu tulikuwa tunafatwa na magari kama sita ambayo kila gari lilikuwa linatugonga pale yanapotufikia huku wakitumiminia risasi ambazo ziliendelea kutoboa vioo vya gari katika upande wa nyuma huku kioo cha mbele kikiwa kimetoka kabisa.moureen alikuwa kazimia jambo lililomfanya ayumbe yumbe ndani ya gari lililokuwa nikiliendesha mimi kwa kasi kwa lengo la kuwakimbia wanaotufukuza ambao walikuwa si wengine bali ni kundi la robert mugalula.kutokana na speed yangu kuwa kali nikajikuta nikiingia katika korongo la msitu ambao hata nilikuwa sipajui ni sehemu gani lakini ilikuwa maeneo ya bagamoyo.nilijitahidi sana kukanyaga breki ili lisimame lakini lilikataa kutokana na mteremko mkali ambao ulinifanya nikate shauri yakutoka huku nikimshikilia moureen aliyekuwa ajitambua na kuangaika kuufungua mlango kwa lengo la kutoka nje kutokana na mteremko huo kuonekana mbele yake kuwa na miti mikubwa ambayo kama gari hilo likigonga na sisi kuwepo katika gari hilo lingetusababishia maafa.nikiwa katika kufanikiwa kuufungua mlango huo wa gari nikaanza kusogea haraka haraka huku nikiwa nimemshikilia moureen ambaye sikutaka kumuacha licha ya kuwa katika hatari kubwa ambayo kama ningelitoka mimi basi ningekuwa tayari nishatoka.kwa hali ya kujiandaa kabisa baada ya kuufika mlango ile nataka kutoka tu gari lisilojulikana lilipotokea likaja kugonga mlango huo ambao ukajibamiza na kunibana mimi kwenye maeneo ya mbavu na kunifanya nitoe ukelele mkali sana wa maumivu huku damu nyingi zikianza kunitoka kutoka na mlango huo kunibana sawa sawa.nikiwa katika hali ya kuugulia sehemu hiyo niliojibana macho yangu yakagonga katika mti mkubwa uliokuwa mbele yetu ambapo gari letu lilikuwa likielekea palepale.Nikajikuta nikifumba macho na kuanza kumuomba Mungu aniokoe katika balaa lile na kwa hofu kubwa nikajikuta nikizimia kwa hofu kabla hata ya gari letu kugonga mti huo na kunifanya nisielewe kilichokuwa kinaendelea…
*-*-*-*-*-*-*-*-*-*-*-*
“Mmmm..ooooh..aaaa mama..nakufa..naumia yalaaa.oooh”ilikuwa ni miguno ya kulalamika niliyoitoa baada ya kuamka na kujikuta nikiwa nimefungwa kichwa chini miguu juu katika mti mkubwa ambao ni kamba tu ndio ilikuwa imefungwa katika miguu yangu na kupitia katika mti na kunifanya nibembee kichwa chini miguu juu.maumivu nilikuwa nayasikia kila sehemu huku damu nyingi zikiwa zinanitoka katika sehemu mbalimbali za mwili zilikuwa zikichuruzika chini huku nikishuhudia mwenyewe katika macho.maumivu niliokuwa nayapata nahisi ilikuwa bora nife kutokana na majeraha hayo kuuma.nikiwa na hali ya kushangaa shanga nikamuona mtu mwingine akiwa amepigishwa magoti huku akiwa uchi na mwili wake mzima ukiwa umetapakaa damu ambaye alikuwa kafungwa kamba mikononi na miguuni.niliangalia sura yake kwa makini kutokana na yeye kuniangalia mimi kwa huruma jambo lililonifanya nimtambue kuwa alikuwa ni dokta ambaye alitusaidia katika mikasa iliyopita.nikiwa katika hali ya kumuangalia kwa huruma ghafla mlio wa risasi uliopenya katika kichwa cha yule dokta ukasikika na kupasua kichwa chake na kufa papo hapo na kunifanya nitoe macho kama nimebanwa na mlango.Ghafla nikamuona robert mugalula aliyekuwa amefungwa bandeji kichwani kwake akasogea huku akipuliza bunduki ambayo alionekana ndio yeye alimlipua dokta kisha mkono wake mwingine akiwa ameshika mkia ambao baada ya kuuangalia kwa makini ulikuwa ni mkia wa taa.akanisogelea kidogo na bila ya kunisemesha akaanza kurusha rusha mkia huo na kuweka sawa kwa lengo la kunitandika nao mimi ambao kabla hata sijapigwa nikahisi mkojo kutokana na sifa kubwa ya mkia wa taa ambao niliusikia tu kwa juu juu ni jinsi gani unavyoumiza.
“YAAAALAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA…
Nilijikuta nikipiga ukelele wa nguvu wenye maumivu makali ambayo hayakuweza kuvumilika hii ni baada ya Robert kufyatua mkia ule wataa aliokuwa ameushika na kunichapa nao kwenye kidonda changu nilichokua kinaniuma hii ni baada ya kujibana na mlango wa gari na baada ya kuchapwa na mkia ule wa taa maumivu yalianza kurudi upya huku nikiishuhudia mvumuko wa damu nyingi zilizokuwa zikimwagika kama maji katika kidonda changu hicho.sikuweza hata kushika kidonda changu kutokana na kushindwa kukifikia kwa sababu nilikuwa nabembea baada ya kufungwa kichwa chini miguu juu.Baada ya kunichapa mkia ule robertson alitulia kwa muda huku akiniangalia kwa hali ya kukunja sura yake.Akiwa katika hali ya kuniangalia ujio mwingine ukaja walikuwa ni baba yake moureen aliyeambatana na wafuasi wake ambapo bila hata ya kumuongelesha robertson kwa ishara tu akaomba mkia wa taa baada ya kupewa akanisogea kisha akaimaliza kuichana shati yangu iliyokuwa imeshachanika na kuimalizia kabisa na kunibakisha tumbo wazi kabisa.akaanza kunitemea mate yasiokuwa na idadi kisha bila ya kunionea huruma akaanza kunikojelea huku akinishindilia matusi yasiokuwa nampangilio baada ya kumalizia kunitukana na kunitemea mate akarudi nyuma kidogo na kuaanza kuuzungusha mkia wa taa na bila ya kukosa na yeye akanilenga pale pale na kunifanya nipige kelele mpaka sauti ikakauka na kutoa machozi ambayo kwa mara ya kwanza nililia mpaka machozi kukauka.baba yake moureen akaishia hapo aliendelea kunitandika baadhi ya sehemu huku kila sehemu mkia huo ulikuwa unanichana na kuniweka Alama kubwa kutokana na mkia huo kuwa na mibamiba.
“Niuweeeniiiii tuuuu jamani mnasubiri nini niuweeniiii ooooooo aaaaaaaaaaaaaaaaaaa nasema niuweeeeniii”Nilijikuta nikiropoka maneno hayo yalimfanya robert asogee na kumsukumiza kidogo baba yake moureen kisha akanisogelea na kunisika kichwa na kunitandika ngumi kali ya pua nakusababisha damu ziliendelee kunibubujika.
“Leo ni siku ya kukutoa roho umfuate mbwa wako moureen kuzimu na wazazi kwa sababu huna hadhi ya kustahili”robert alinambia huku akiwa katika hali ya kujiamini na kunifanya nichanganyike baada ya kuniambia nimfuate moureen kuzimu hali iliyonifanya niaanze kupata picha ya kuwa Moureen alikuwa kashauliwa.sikutaka hata kuamini huku kwa muda mfupi nikijikuta nikikubwa na msongamano wa mawazo yalioanza kunishambulia katika kichwa changu.kamba niliyofungwa katika mti ikakatwa nakunifanya nidondoke chini sikufungwa kitu chochote lakini nilikuwa sina uwezo wa kukimbia kutokana na vidonda vingi vilivyoninyong’onyesha na kunifanya nibaki namuangalia robert ambaye akanipigisha magoti kisha akatoa bastola yake na kuiweka risasi kisha akaisogeza katika kichwa changu.
“Ee Mungu mimi mja wako ambaye kwa sasa niko hatarini kupoteza uhai wangu bila ya sababu yoyote ya msingi hivi Kwa nini usinisaidie kwa hili.Eebaba Muumba mimi mja wako ambaye nimeuliwa familia yangu ambayo nilikuwa naitegemea na mimi unataka na mimi niondoke katika tumbo la Ardhi hii Aaa fanya miujiza sina wakumtegemea isipokuwa wewe sina ni wewe ndio mwenye mamlaka yakuamua na kama nikifa hapa basi ndio wewe utakaokuwa umepanga na hakuna anayeweza kupangua.Naomba unisamehe madhambi yangu yote niliokukusea najua sijawai kutubu baada ya kufanya madhambi yote lakini leo nakuomba msamaha kwa kuamini uwepo wako Asante.” hakika sikuwa na budi ya kusali sala zangu za mwisho kimoyomoyo tena kwa uchungu huku nikakaza macho yangu katika mkono wa bwana robert ambaye nilishuhudi kidole chake kikinyonga taratibu katika kidude cha kufyatulia risasi na kunifanya nizidi kutoa macho.ile anataka kufyatua tuu ghafla kitu kama mshale kikatua katika kidole cha robertson aliyekuwa anakaribia kufyatua risasi katika bastola aliyeshika na kumfanya aiachie bastola ile huku akipiga ukelele kutokana na maumivu ya mshale aliopigwa na kusababisha wote wapigwe na butwaa na kuanza kuangalia mshale huo ulipotekea.wakiwa katika hali ya mshangao ambao hata mimi nilikuwa katika hali hiyo.Mshale mwingine ukatua kichwani kwa mfuasi wa baba yake moureen aliyekuwa pembeni yake na kufa papo hapo hali iliyosababisha………..
Sehemu Ya 8
Wafuasi wengine waanze kumkimbiza baba yake moureen aliyekuwa kaganda baada ya kupata na kama mshangao baada ya kuona mfuasi wake wa pembeni kupigwa mshale wa kichwa na kudondoka wakamfuata na kumnyanyua robertson ambaye alikuwa bado anaguliwa maumivu ya kupigwa mshale wa mkono lakini kabla hata hawajaondoka naye mishale miwili ilitua katika miguu ya wale wafuasi wa robertson ambao walishafanikiwa kukimbia nakujikuta wakimuacha robertson ambaye baada ya kusikia wafuasi wake akilalamika akajikuta mwenyewe akikaza mwendo na kutaka kukunja lakini mshale mwingine wa bega mkampata na kumfanya atoe ukelele mwingine lakini hakuweza kusimama.niliendeleaa kushangaa huku nikiendeleaa kuwaangalia wafuasi wa robertson waliopigwa mishale miguuni ambao wote kwa pamoja wakati huo walikuwa wanaugulia kwa kutoa kelele za maumivu huku wote wawili wakiangaika kuichomoa mishale hiyo iliyopenya katika miguu ya kila mmoja huku kila mmoja akipigwa mguu wa kulia.nikiwa bado natafuta ni nani aliyekuwa akirusha mishale hiyo kwa kugeuka nyuma lakini kabla hata sijageuka upande mwingine mishale miwili tena ikapita tena juu ya kichwa changu na kuwapata wale wafuasi waliokuwa wakiugulia maumivu
mishale ya kichwa kila mmoja na kusababisha wote wafe hapo hapo.ghafla nikaguswa bega kwa nyuma na mkono ulionekana mgumu kutokana na kuniumiza pale aliponigusa kisha nikageuka na kumuangalia aliyenigusa ambaye macho yangu yakagonga katika jamaa aliyeonekana mzungu kabisa kwa macho huku akiwa kavaa kofia kubwa iliyofunika sura yake.nilimuangalia sana huku naye akiwa ananiangalia mimi pia mdomo wangu ulikuwa mzito sana kunyanyua mdomo kuongea na kujikuta nikiendelea kumuangalia mzungu huyo ambaye akanishika shika maeneo ya bega na kupandisha kwenye shingo yangu nakunibonyeza sehemu katika shingo ambapo baada ya kunibonyeza giza nene likatanda katika macho yangu na kuzimia hapo hapo.Nilishtuka na kujikuta nikiwa nimelala katika chumba chenye mwanga hafifu huku ni kibatali tu ndio nilikiona kikiwaka.jitahada zangu za kuamka ziligonga mwamba baada ya kujitonesha mwenyewe vidonda vyangu mgongoni na kunifanya nitoe ukelele wa nguvu na kuhema juu juu.nikamshuhudia mzungu huyu aliyekuwa mzee akija pale pale kwangu nakuniangalia kisha akachukua maji maji yaliokuwepo kwenye chupa na kuanza kunimwagia katika vidonda vyangu vilivyokuwepo nyuma ya mgongo na kunifanya nianze kuugulia tena kwa maumivu hali iliyomfanya hata yeye awe ananiangalia kwa kunikazia macho..
“Kijana unaitwa nani??”
“naitwa pa..blo”
“nyanyuka hebu jitahidi kunyanyuka”nilijikuta nikiingia msangao baada ya mzungu huyo mzee kuongea kiswahili fasaha kabisa huku nikifuata ushauri wake wakunyanyula kwa shida huku nikimuangalia mzee huyo ambaye naye alikuwa bize akaniangalia kwa ujasiri.
“Pablo mimi naitwa Gardner thomas ni mtalii ambaye nilikuja huku bagamoyo kutoka kwetu switzland sikufanikiwa kurudi baada ya ndugu zangu niliokuja nao kuuawa na sisi kuporwa dhahabu ambazo tulizinunua kwa kiasi kikubwa sana Mimi ni mzee licha sio mzee sana ni mimi ambaye niliweza kukimbia nakuanzisha maisha yangu hapa porini vp kwani wewe una tatizo gani.”. nilimuangalia mzee gardner kwa muda kisha bila ya kuficha nikaanza kumueleza hali iliyonikuta mwanzo mwisho na kumshukuru kwa kuniokoa maisha yangu ambayo nilihisi yalikuwa hatarani kukatika.
“Usijali utakaa hapa mpaka utakapo pona kisha nitakusaidia kuweza kulipiza kisasi kwa wale wote waliokutendea ubaya.” hakika baada ya gardner kunambia vile nilifarijika sana huku nikiendelea kummiminia shukrani za dhati kabisa mzee huyo.siku sita kudondosha chozi kila nilipokuwa namkumbuka moureen kutokana na kauli yake aliyoitoa robert kuwa moureen alishakufa niliendelea kuombeleza mwenyewe huku mzee gardner kuendeleza kunifariji kwa kunipa moyo huku akiendelea kunipa tiba mbadala ya vidonda vyangu.hakika siku zilichomoka na kufika mwezi ambapo kwa kutumia dawa za mitishamba vidonda vyangu vilipona kabisa tuliishi maisha ndani ya pori tukitegemea vyakula vya wanyama kama sungura na ndege kama njiwa waliokuwa wapo wengi katika pori hilo.hali yangu iliendelea kumridhisha gardner ambaye akaanza kunipa mazoezi yakurainisha viungo kwa lengo la kujiweka sawa kisha nakuniahidi kunifundisha kupambana na watu kwa lengo la kwenda kulipiza kisasi kwa wale wote walionikosea.roho ya chuki ikazidi kuniingia huku kila nikikumbuka yaliotokea nilijikuta nikishikwa na hasira za ajabu…………
Mazoezi ya kukimbia umbali mrefu msituni na kuruka ruka baadhi ya mawe yaliowekwa na mzee gardner yalizidi kuniweka katika hali nyingine tofauti ya ukomavu wa mwili wangu kwa muda mchache nikajikuta nikiingiza vitu vingi katika mwili wangu zilivyonisaidia kuniweka sawa kupita kiasi.kuendelea vizuri kwangu vizuri katika mazoezi kulizidi kumfurahisha sana gardner ambaye alianza kidogo kidogo kunifundisha jinsi ya kukabiliana na adui.
“Kila kitu unachotaka kukifanya lazima uwe na nia nacho je mpaka sasa ushawai kupigana na mtu yoyote pablo.”
“No mzee sijawai sikumbuki labda utotoni kwangu ila ukumba huu sijawai ooo nilishawai baada ya kushuhudia tukio la shangazi yangu kufa kama nilivyokuambia kwamba nilipata hasira iliyozidi kipimo na kujikuta nikiwazamia baadhi ya wafuasi wake robert na kuwauwa laki…”
“Ooo basi nikuambie kitu hebu attack me(nivamie mimi)”
“Eeeee unasema??
“Nivamie kijana anza kunishambulia kama unapigana na adui” mzee gardner aliniambia na mimi bila ya kusita nikajikuta nikimvamia mzee huyo na kuaanza kurusha ngumi nzito nzito zilizopanguliwa vikali kwa ustadi wa juu kisha mzee huyo akanipiga mtama na uliosababisha nidondoke.
“Simama attack me haraka kumbuka familia yako iliyouwawa kikatili kumbuka ulivyotaka kuuwawa kumbuka kwa ushampoteza mchumba wako uliyempenda kupitiliza.” hakika maneno hayo ya mzee gardner yalinipandisha mori na kujikuta tena na simama na kuanza kumvamia lakini nilikuwa narudisha chini kwa mtama kila ninapojaribu kumvamia mzee huyo.alionekana kama mzee sana lakini alikuwa vizuri sana na kusababisha mimi kumvamia karibia mara hamsini lakini sikufanikiwa hata kumpata hata kidogo na kujikuta nikirusha ngumi kibao zilizokwepa kwa ufundi kisha nakudondosha.
“Nahisi utakuwa utumii akili unajua kupigana na mtu unatakiwa utumie akili huyu anakujaje anaendaje umenielewa”
“Yes nimekuelewa”
“Na kitu kingine angalia balance yako ya mwili kisha msome adui yako anakufuata vipi kamwe katika miongoni mwa sheria za kumpiga adui yako wewe unatakiwa umfuate sio yeye akufuate wewe hivi ushawai kuangalia ngumi alizokuwa anapiga tyson”
“ndio”
“sasa ngoje niaanze kukufundisha” hakika maneno ya gardner yalinijenga sana kisaikolojia na kujikuta nikienda naye sawa sawa katika kila zoezi alilokuwa akinipa.Ndani ya siku saba tu nilijikuta nikiwa nimeivaa na kuanza kupamba naye mzee gardner ambaye alifurahishwa sana na kiwango changu cha upiganaji.hakika hali ya kutaka kulipiza kisasi ilizidi kuniingia katika kichwa changu huku maneno ya mzee gardner yalizidi kunishawishi kulipa kisasi.hakika mzee huyo hakuishia hapo pia alinifundisha jinsi ya kutumia mishale kulenga shabaha zoezi ambalo niliweza kuliweka kichwani kwa muda mfupi sana na kunifanya na mimi niweze kulenga shabaha kali.Siku moja mimi nikiwa nyumbani mzee gardner siku hiyo alienda porini zaidi sehemu aliniokoa mimi kwenda kuchukua dawa zake za mitishamba ambazo mara nyingi alikuwa anapendeleaa kuzitumia.nikiwa peke yangu mimi niliendelea kufanya mazoezi yakujiweka sawa kama nilivyozoea kisha nakuamia upande wa mishale na kuanza kulenga lenga vitu vilivyokuwepo hapo nje kama miti huku nikijitahidi kulengesha sehemu ambayo nilikuwa najisikia kulengesha.ghafla nikiwa katika zoezi hilo nikaanza kusikia majani yakianza kuchakarika huku na huko na kuashiria kuwa kuna kitu kibaya kinakuja bila ya kulaza damu nikaanza kujiandaa kwa kuweka mishale yangu sawa huku mwingine nikiuweka sawa kwenye upinde na kuvuta kabisa na kusubiri kinachotokea ili nifyatue.Macho yangu kakuta na mzee gardner aliyekuwa akikimbia kwa kasi na kunifanya mimi nizidi kuwa na hofu kubwa iliyosababisha nipigwa na butwaa la nguvu.
“Pablo kimbiaaaaaaa” maamrisho ya kukimbia hakuniingia kabisa nikajikuta miguu yangu ikifa ganzi na kujikuta nikiendeleaa kusimama pale pale na kuangalia nini kilichomfanya mzee gardner kukimbia.nikiwa katika mshangao ghafla gari kubwa likatokeza na kufungwa breki umbali kidogo na nyumba yetu pale kisha watu wapatao ishirini wenye kuvaa miwani meusi na suti nyeusi wakashuka huku wakiwa na silaha ambapo baada ya kushuka tu wakaanza kunimiminia mimi risasi ambazo zote hazikunipata kisha na mimi pia nikaanza kukimbia kwa kasi.nilianza kukimbia na kuanza kuita jina la gardner bila mafanikio huku kila nilipokuwa naangalia nyumba nilikuwa nafuatwa na watu wale ambao nilishawajua walikuwa ni wafuasi wa robertson.sikutaka kumpambana nao peke yangu kwa kuhofia kwamba wapo wengi.mbio zangu ziliishia katika kichaka chenye majani mengi ambayo yalinisaidia kujificha na kuanza kuangalia nini kinachofuata hakika nilipotezana na mzee gardner alitangulia kukimbia nikiwa katika hali ya kujificha bahati nzuri nilikuwa sijasahau upinde wangu na mshale ambayo nilianza kuiweka sawa baada ya kumuona jamaa mmoja ambaye alikuwa kashikilia risasi vizuri huku sura yake akiwa ameikunja kuasiria kwamba yupo kazini.ghafla mzee gardner akatokea pasipo julikana na kwenda kumkaba jamaa huyo ambaye baada ya kukabwa akatoa roba ya mzee huyo na kuanza kumtembezea kichapo kikali kilichoniogopesha sana na kujikuta nikishindwa hata kuingilia kutokana na nguvu nyingi alizokuwa nazo jamaa huyo.baada ya kuhakikisha kuwa kamdhibiti jamaa huyo akaokota bunduki aliyoidondosha wakati akipigana na mzee gardner kisha bila hata ya kuremba akafyatua risasi iliyompata sasa mzee gardner ya kichwa na kufa hapo hapo.hakika macho yangu yakanitoka ghafla nikajikuta nikipiga kelele na kutoka kichakani na kwenda kumvamia jamaa huyo kisha………….
INAENDELEA

