KILA NIKILALA NA MWANAUME ANAJINYEA
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Iko hivi, Mimi nimewahi kuwa kwenye mahusiano na mkaka mmoja wa huko njombe, ni mbena, yule kaka tulikuwa tuko vizuri tu kwenye mahusiano mara ghafla akasema tuachane, nilishangaa sana, nilijaribu kubembeleza na kumlilia lakini hakunielewa, niliteseka sana ila baada ya mwaka nikawa nimeanza kuzoea, ikabidi niwaze tena kuhusu mahusiano.
Nilikuja nikampata huyo kaka, Sasa siku tumelala kwake, ilikuwa ni mida ya saa 10 alfajiri usiku nikasikia harufu ya kinyesi nikawa najiuliza hii vipi, mara naye akawa ametoka usingizini, akanikuta nashangaa akaniuliza vipi? Nikasema poa, akasema mbona anasikia harufu, na Mimi nikamwambia hata Mimi, Ile akataka kuinuka ndo nikamuona huku kwenye makalio kote amejaa mavi, yeye mwenyewe akaanza kushangaa, tukajikuta tuna shangaa wote, aliona sana aibu, huwezi amini alinifukuza muda huo huo, stori yangu na huyo ikaishia hapo hata Mimi nilijua ni Yeye mwenye matatizo na inawezekana ndo alivyo.
Nikaja nikampata mkaka mwingine, siku hiyo tuko guest tuna fanya mapenzi Kwa mara ya kwanza naye hapo hapo akajinyea, tukashangaa chumba chote harufu ya kinyesi, akakimbilia bafuni, alivyo rudi Kwa aibu akanipa hela akavaa akaondoka, na huyo tena habari ikaishia hapo,
Nikaja tena nikampata mbaba, siku hiyo akanitoa out Sasa wakati ananirudisha nyumbani akataka tufanye kwenye gari alinibembeleza sana ikabidi nikubali, naye tena tukiwa tuna fanya akajinyea, hapo hapo akaniambia nitoke kwenye gari yake na akawa ameondoka Kwa hofu sana,
Baada ya hapo nikaanza kuwa na hofu inawezekana Mimi ndo mwenye shida mbona haya ni maajabu sana, nilikaa mpaka mwezi mzima baada ya Hilo tukio, nikasema ngoja tena nijaribu, nikampata mkaka ambaye ni jirani alikuwa anafanya kazi benki, siku hiyo akaniita kwake, tukiwa tuna fanya tena akajinyea na ilikuwa sebuleni, naye pia akanifukuza tena,
Nikaona ishakuwa shida upande wangu, nikaanza kuishi Kwa hofu sana, maisha nikaona ni magumu Sina kazi yoyote Sasa nitaishije, siku Moja nikapata wazo nikajiuze tu, siku hiyo nilienda kukaa bar Moja hivi, akaja mkaka hivi tukaelewana na tukawa tumeingia guest, Cha ajabu tulifanya mpaka tuka maliza yeye haikumtokea hiyo Hali, nikasema labda hiyo hali itakuwa imepotea, Kuna kaka alikuwa ananisumbua akitaka mahusiano na Mimi, nikamkubalia, siku tunafanya nae pia akajinyea,
ngoja nifupishe stori, Kwa Sasa Mimi kazi yangu ni kujiuza, nikilala na mwanaume Kwa kujiuza hiyo Hali haitokei ila nikisema nianzishe mahusiano ndo nifanye naye hiyo Hali lazima imtokee,
Natamani na Mimi kuwa na mahusiano na mwanaume mmoja Ili nitulie lakini ndo hivyo, nayachukia sana maisha yangu, Kwa Sasa nina miaka 31 naumia sana, nimesha ombewa sana mwanzoni kabisa lakini sikupata suruhisho kabisa.


1 Comment
Hey