MWANAFUNZI MCHAWI
Sehemu Ya 6
“Unasemaje wewe?” Dorice aliuvua woga akajikuta ameropoka kwa hasira.
“Sikiliza Dorice.. Kwa muda mrefu sana nilikuwa natafuta mke, sikumpata. Nilitamani sana kuoa binadamu ili niishi nae, na kwakuwa mama yangu ananipenda amenitafutia wewe na ninakupenda. Nataka nikuoe..!”
“Toka hapa.. Usinisogelee… ” Alifoka Dorice na kumsukuma Mansoor.
Mansoor alihuzunika sana kwa kitendo alichofanyiwa na Dorice, akatikisa kichwa na kupiga hatua za taratibu kisha akatoweka ghafla machoni kwa Dorice. Dorice alishtuka sana akabaki ametumbua macho tu.
“Mungu wangu nisaidie niondoke huku, mkosi gani huu? Nitafanywa vibaya na viumbe hawa sijui majini… Bila shaka ni majini! Niolewe na jini? Siwezi Mimi…!” Alizidi kuwaza Dorice huku kijasho chembamba kikimtoka kwa kasi.
Ghafla mlango wa chumba alichokuwamo Dorice ukafunguka ghafla, Dorice alishtuka sana kukutana na sura ya malkia akiwa na hasira kupita maelezo.
“Dorice binadamu! Ungekuwa umeuwawa masaa mengi yaliyopita.. Lakini kutokana na mapenzi ya mwanangu Mansoor kwako ndio maana upo hai mpaka sasa.. Ni kitu gani kinakupa jeuri ya kumtesa mwanangu wa pekee?” Malkia alizungumza kwa sauti Kali iliyoambatana na radi. Alionekana mwenye hasira sana.
Dorice aliogopa sana wala hakuthubutu hata kunyanyua kinywa chake akabaki kimya huku akitetemeka.
“Dorice! Una machaguo mawili tu! Chagua moja… KUOLEWA NA MANSOOR AU KIFO!”
Alisema malkia yule kwa ukali, Hofu ikamzidia Dorice.
********
Doreen alipoathubutu kutumia uchawi wake kumdhuru Nadia Joseph, ghafla akakumbana na kichomi kikali sana ubavuni mwake. Akahisi maumivu makali yaliyomfanya apige kelele sana zilizowashtua darasa zima. Wanafunzi wote wakamgeukia yeye lakini kwa kukwepa aibu akajifanya kujinyoosha akiwa bado anaugulia maumivu yale makali. Baada ya hapo wanafunzi wale wakaendelea na shughuli zao.
“Doreen.. Nakupa onyo, acha kuwachezea wenzio! Unajivunia uchawi lakini Mimi nina MUNGU.. Hunitishi kwa lolote maana niliyenaye ni mkuu kuliko nguvu zote.. Nimemwomba Mungu anioneshe MTU anayevuruga shule nashukuru sasa amenionesha! Achana na Uchawi!” Alisema Nadia kwa ujasiri sana ingawa aliongea kwa sauti ndogo ili asisikike sana.
Doreen aliumbuka sana, akaondoka bila kuaga.
Kengele iligongwa wanafunzi wote walitakiwa waende mstarini. Baada ya mkusanyiko wa wanafunzi wote alisimama mwalimu mmoja kwaajili ya matangazo muhimu.
“Kuuna taarifa za kusikitisha sana! Kiufupi ni kwamba Mwalimu Mkuu msaidizi na mwalimu wa taaluma hatuko nao tena. Wameaga dunia Leo asubuhi.. Pia kuhusu mwalimu John kuna sintofamu imetokea kiufupi ni kwamba hajafa bado yuko hai…” Wanafunzi walisikitishwa sana na taarifa zile ila walipigwa butwaa kuhusu mwalimu John kwani walikwisha tangaziwa kuwa amefariki lakini iweje waambiwe yuko hai? Walishindwa kuelewa.
Baada ya mwalimu kutoa matangazo aliondoka zake pale mstarini. Ndipo Nadia Joseph alipoomba nafasi ya kuzungumza na akapewa.
“Jamani wanafunzi wenzangu, hali hapa shule ni mbaya sana… Acheni masikhara hebu fanyeni maombi ya kweli! Mkisali kwa uaminifu MUNGU atajibu tu… Msichukulie mazoea tafadhali…” Aliposema hivyo kuna wanafunzi waliguna lakini Nadia hakujali hilo akaendelea.
“Sasa hivi wanataka titi la msichana.. Usipokua makini unaweza ukachukuliwa lako..!” Nadia aliposema hivyo, alimwona Doreen kwa mbali akiwa amenuna sana huku akimtazama Nadia utadhani anataka kummeza.
Wanafunzi wote wakataharuki, walianza kuogopa sana.
Nadia akaondoka pale mbele kisha wanafunzi wote wakatawanyishwa.
Doreen alikuwa na hasira za kuua MTU. Alimchukia Nadia kupita kawaida, akaahidi kumfanyia kitu kibaya sana…
MWALIMU John alijishangaa kupita kiasi kwani miguu yake yote miwili ilikuwa imeoza vibaya. Alikuwa hahisi maumivu yoyote hapo kabla lakini pindi alipojitizama tu alianza kuhisi maumivu makali sana. Punde funza wakaanza kutoka mguuni. Akabaki anajiuliza nini kimetokea bila kujua sababu.
Mkewe na baadhi ya ndugu zake walibaki kimya, wakimtazama Mwalimu John kwa woga.
“Mke wangu bado unaniogopa? Hunionei hata huruma mumeo? Ama kweli mapenzi yapo kwenye raha tu!” Alisema Mwalimu John kwa huzuni iliyochochea huruma nyingi machoni mwa mkewe. Taratibu akaanza kumsogelea mumewe lakini kuna ndugu yake mmoja akata kakumzuia.
“Niache! Nampenda mume wangu ingawa yupo kwenye hali hiyo..” Alisema mke wa mwalimu John huku akimsogelea mumewe kisha akamkumbatia kwa mapenzi mazito, bila kujali hali aliyokuwa nayo mumewe.
“Nakupenda mume wangu.. Nashukuru umeurudia uhai ili tuendelee kuwa pamoja” alisema mwanamke yule huku machozi yakimchuruzika.
“Nakupenda sana mke wangu, nilikuwa nakuwazia sana hali ambayo ungeikabili kama ningekufa..”
“Sijui ningemweleza nini mwanao aliyeko tumboni mwangu!” Walizungumza yote hayo wakiwa bado wamekumbatiana. Maneno ya mke wa Mwalimu John yalimfariji sana John, akahisi kwamba kweli amerudi duniani.
Ndugu walibaki wametumbua macho wakiwatazama wawili wale, hawakuwa na la nyongeza zaidi ya kumkaribisha mwalimu John ambaye hakuweza hata kutembea kutokana na maumivu ya miguu. Funza walizidi kuongezeka miguuni.
“Mke wangu naumwa sana hii miguu, sijui kama itapoa!”
“Usijali itapona tu mume wangu.. Ila naomba unieleze kila kitu kilichokutokea..!” Alisema mke wa mwalimu John huku akimwinua taratibu mumewe pale chini alipokuwa ameketi.
Mwalimu John alilalama sana kutokana na maumivu Yale lakini ikabidi ajikaze mpaka walipoingia ndani.
“Mke wangu Leyla.. Kweli nimeamini unanipenda!”
Leyla akatabasamu na kumbusu mumewe kisha akasema
“Nakupenda sana mume wangu hebu nisimulie imekuwaje..!”
“Ni stori ndefu sana mke wangu..lakini ngoja nikusimulie mbele ya hawa ndugu zangu wote..!”
Wote sebuleni pale walitulia kimya kusikiliza kisa cha ajabu kilichompata Mwalimu John. Lakini cha ajabu Mwalimu John alipotaka kusimulia tu..
*******
Wazazi wa Eddy walichanganyikiwa sana wakahisi mtoto wao mpendwa tayari amefariki dunia. Wakazidi kumtikisatikisa huku mama yake akiushusha mchozi kama maji, ndipo wakagundua Eddy hajafa ila amepoteza fahamu. Kofi alilopigwa halikuwa la mchezo, lilikuwa kama radi ingawa wazazi wake hawakujua kitu.
Na hiyo ilikuwa ni kazi ya mzimu unaomsaidia Doreen.
Mr.Alloyce alitumia nguvu zake zote kumpepea Eddy mpaka alipozinduka. Alikuwa amevimba USO mzima jambo lililowashtua wazazi wake. Wakatazamana kwa nyuso zilizojaa viulizo bila kujua majibu ya uhakika.
“Eddy” Mr.Alloyce aliita.
“Naam!” Eddy aliitikia kwa sauti ya chini.
“Vipi?”
“Nimepigwa!”
“Umepigwa? Umepigwa na nani?”
“Sijui!”
Yote yaliyomtokea Eddy yalibaki kuwa viulizo kwa wazazi wake, yaliibua fumbo ambalo lilikuwa gumu sana kulitatua.
“Baba Eddy”
“Sema mke wangu..!”
“Mi naona twende kwa mganga tu!”
“Wapi?”
“Tanga kwa mganga Tembo wa Bahari.. Umewahi kumsikia?”
“Mmh! Hapana..!”
“Nasikia ni kiboko sana kwani hata Mama Zuwena aliwahi kwenda akasaidiwa!”
Mama Eddy aliamua kumshauri mumewe waende kwa mganga wa kienyeji anaepatikana Pangani Tanga. Mganga Hugo alifahamika kwa jina la Tembo wa Bahari kwani alisifika kwa kutatua matatizo yaliyoshindikana lakini Mr.Alloyce alisitasita kuhusu suala hilo.
“Waganga siwaamini mke wangu..!”
“We unafikiri tutafanyaje sasa! Kama hutaki niachie kila kitu Mimi nitahangaika na mwanangu..!” Mama Eddy alilivalia njuga suala lile hatimaye Mr.Alloyce akaingia laini na kumkubalia mkewe.
“Sawa tutaenda!”
“Twende kesho!”
“Haina shida”
Walikubaliana kuianza safari yao siku ya kesho yake.
Siku ile hawakumsumbua Eddy kwa swali lolote lile, usiku aliingia kulala akiwa bado hana raha kabisa huku akiisubiri siku ya kesho yake ili waende kwa mganga.
Eddy alipojilaza kitandani tu, usingizi mzito ukampitia. Ghafla akamuona Doreen ndotoni akija na kisu kikali sana kinachowaka moto. Eddy aliogopa sana akatamani kuamka lakini akashindwa.
“Eddy ukithubutu kusema lolote kuhusu Mimi utakiona cha moto… Kubwa zaidi ukithubutu kwenda kwa mganga hiki kisu ni halali hapo kifuani pako.. Utakufa!”
Ilisikika sauti ya Doreen ikiongea kwa msisitizo sana huku ikijirudiarudia.
“Mamaaaa!” Eddy alishtuka usingizini na kumwona mama aliyekuwa amelala chumbani kwake ili kujua maendeleo ya Eddy kila wakati.
“Vipi mwanangu?” Mama Eddy alishuka kitandani na kukisogelea kitanda cha Eddy.
“Ndoto mama.. Naogopa!”
“Pole mwanangu.. Usiogope tupo wote humu..! Alisema mama Eddy lakini Eddy bado aliogopa.
Usiku ule ulikuwa mrefu sana kwa Eddy kwani alikumbana na vitisho Vinci kutoka kwa Doreen. Kulipokucha Eddy aliona ahueni kidogo ili aachane na mauza uza ya usiku.
Majira ya SAA kumi na mbili na nusu asubuhi wazazi wa Eddy walikuwa tayari wamejiaandaa. Wakamwamsha Eddy ili anywe chai kisha waanze safari, cha ajabu Eddy aligoma kuondoka.
“Siwezi kwenda kwa mganga! Siendi!”
“Huendi?” Mama Eddy alishtuka
“Siendi mama! Hata kwa greda!”
“Kwanini?”
“Sitaki!”
Eddy aligoma kabisa kuondoka lakini mama yake alimlazimisha na kumweka kwenye gari akisaidiana na baba yake. Safari ikaanza.
********
Doreen aliamua kusubiri usiku uingie ili amfuate Nadia na kumfanyia uchawi wake ili aondoke na ziwa.
Sehemu Ya 7
Eddy aligoma kabisa kuondoka lakini mama yake alimlazimisha na kumweka kwenye gari akisaidiana na baba yake. Safari ikaanza.
********
Doreen aliamua kusubiri usiku uingie ili amfuate Nadia na kumfanyia uchawi wake ili aondoke na ziwa.
Usiku ulipoingia Doreen alikuwa akijipanga kwa kuita mizimu yake yote ili imwongezee nguvu. Alikuwa amejitenga peke yake kwenye kichaka huku akijpakapaka madawa yake ili aongeze nguvu zake za kichawi. Akainuka akiwa uchi huku akijiaminisha kuwa sasa yù kamili. Akatamka maneno yake ya kichawi akatoweka eneo lile..
Muda huo ilikuwa ni saa name usiku.
Akaenda moja kwa moja mpaka bwenini kwa Nadia na kukifikia kitanda chake, mh! Alichokutana nacho hakuamini.. Moto ilikizingira kitanda kizima na hakumuona Nadia Joseph alipo. Akaamua kukisogele kitanda kile taratibu lakini ghafla akapigwa dhoti Kali na kudondoka chini puuuh! Kama mzigo. Na kila alipojaribu kuinuka alishindwa.. Hofu ikamjia akajua tayari amekamatwa kwenye mtego….
DORICE alikuwa akiyatafakari maneno ya malkia wa himaya aliyokuwepo kwa wakati ule. Alikuwa haelewi afanye nini na achague lipi kati ya kifo au kuolewa na jini. Alijikuta yupo kwenye wakati mgumu sana mpaka akajuta kutoroka shuleni. Alimlaani sana Doreen kwani ndiye chanzo cha matatizo yote. Alijikuta analia bila kujua msaada wake utatoka wapi.
Akiwa katika wimbi la mawazo alishtushwa na harufu Kali ya marashi iliyomfanya azinduke na kumtazama mgeni wake. Alipoinua kichwa chake alikutana tabasamu mwanana kutoka kwenye sura nzuri ya upole ya kijana Mansoor.
“Nakupenda Dorice.. Olewa na Mimi!” Alisema mansoor kwa sauti tamu iliyojaa huba. Lakini sauti na maneno hayo habvikuwa kitu kwa Dorice, aliachia sonyo Kali iliyodhihirisha chuki kuu dhidi ya Mansoor.
“Kama kuniua niueni! Siwezi kuolewa nawewe!” Dorice alisema maneno hayo kwa ujasiri sana bila kujali jambo hilo lingeonekanaje kwa Mansoor.
Mansoor alihuzunika sana, akatikisa kichwa kama ilivyokuwa kawaida yake . Akashindwa kuyazuia machozi ya damu machoni mwake lakini Dorice hakujali hilo.
“Dorice! Kwanini haunipendi? Au kwa sababu Mimi sio binadamu mwenzio?” Aliongea Mansoor kwa huzuni sana lakini Dorice hakujibu kitu.
“Tafadhali niambie Dorice… Nikufanyie nini ili uamini kuwa nakupenda?” Aliuliza mansoor kwa sauti ya upole.
“Utanifanyia?”
“Ndio Dorice!”
“Naomba unirudishe duniani…”
“Nikikurudisha sasa nitakuoaje? Siwezi ishi mbali nawewe!”
“Umesema utanifanyia nikuombacho.. Umeniahidi!”
“Ndio ila hilo suala gumu… Kwanini hunipendi?”
“Nampenda mtu mwingine.. Na ndie aliyenifanya nipate matatizo haya yote..” Dorice alisema maneno hayo huku machozi yakimlengalenga kwani kila alipomkumbuka Eddy alidondosha chozi na hakutaka kuamini kama Kweli Eddy amemwacha na yupo na Doreen.
“Unampenda nani?”
“Nampenda mtu anaitwa Eddy, siko tayari kimkosa nataka nipiganie penzi langu… Samahani sana Mansoor… Wewe ni mzuri ila sins hisia na wewe kabisa!” Dorice alijikuta akiropoka maneno hayo yote ili kufikisha hisia zake kwa Mansoor. Maneno Yale yaliugusa vyema moyo wa Mansoor, alihuzunika sana ila ilibidi akubaliane na ukweli.
“Nashukuru kwa kuwa mkweli Dorice.. Nakupenda sana ila siwezi kukulazimisha unipende… Hakutakuwa na mapenzi hapo.. . Naumia sana ila inabidi nizielewe hisia zako!” Alisema Mansoor kwa sauti iliyojaa masikitiko makubwa sana ila hakuwa na jinsi. Mansoor alikuwa ni mini mstaarabu kupita kiasi ingawa mama take alikuwa katili tena mwenye roho mbaya sana.
“Umenielewa Mansoor?!”
“Ndio.. Nimekuelewa sana! Ila nisimulie ilikuwaje?”
Dorice alifuta machozi na kutabasamu kidogo ingawa bado alikuwa na maumivu ya mapenzi kwa Eddy. Akajua ule ni msaada wa kwanza kwake kwenye eneo lile, akaamua kumsimulia kila kitu kama ilivyokuwa kati ya yeye na Eddy na kisa cha kutoroka.
Mansoor alihuzunika sana, akamwonea huruma sana Dorice.
“Binadamu wabaya sana..!”alisema Mansoor.
“Inaniuma sana! Nampenda sana Eddy..!”!
Mansoor alichukua kitu kama kioo, akakitazama kwa muda kisha kikamletea picha ya Doreen.
“Mh! Huyu Doreen.. Ni mtu mbaya sana .. In mtu hatari kupita kawaida..!”
Alisema Mansoor kwa mshtuko huku akimtazama Dorice. Dorice alikuwa haelewi chochote akabaki akishangaa tu.
“Doreen ni mchawi sana.. Na kuna kitu anatafuta! Amemharibu sana Eddy… Eddy yupo kwenye wakati mbaya na muda wowote anammaliza..!”
Maneno ya Mansoor yalimshtua Dorice
“Amemfanyaje? Nisaidie kumwokoa Eddy tafadhali..!”
“Mama hatanikubalia ila inabidi nikusaidie Dorice.. Yote ni kwasababu nakupenda.. Nitakusaidia usijali!”
Alisema Mansoor.
“Nitafurahi sana ukinisaidia Mansoor!”
“Usijali.. Ila mama ni kikwazo..!”
“Jitahidi Mansoor!”
Dorice alichanganyikiwa sana baada ya kusikia kuwa Eddy atauliwa muda wowote na Doreen, ilibidi azidi kumsihi Mansoor aweze kumsaidia kwa namna yoyote ile kwani alitambua uwezo mkubwa aliokuwa nao jini yule mstaarabu.
******
Doreen alibaki pale chini kwa muda mrefu sana akishindwa kutoka mle ndani.
Alihangaika sana mpaka kijasho kikaanza kumtoka kwani aliziona kabisa dalili za kufamwa, aliwaza aibu ambayo ingemkuta hakujua afanyaje.
Akiwa katika harakati hizo za kutaka kuondoka akahisi moto mkali ukimpitia, akapiga kelele za maumivu huku akigalagala pale chini. Chumba kizima kilikuwa kimya sana kwani wanafunzi wote walikuwa wamelala fofofo na hakuna aliyeweza kusikia kilio kile.
Doreen aliteseka sana na tangy aanze uchawi hakuwahi kukumbana na hali ile.
Aliona uchawi sasa ni wa mateso, kwani maumivu aliyokuwa anayapata hayana mfano.
Doreen alijitahidi kufanya kila awezalo ili aweze kutoka ndani ya bweni lile lakini halo ikazidi kuwa mbaya. Ghafla akasikia mtu akikohoa akajua mwisho wake umefika. Akaanza kuropoka maneno yake ya uchawi ili aweze kutoka hatimaye akafanikiwa. Ikawa ahueni yake ingawa mwili wote ulikuwa unamuuma vibaya sana.
Alifika kwenye kichaka ambacho aliacha vitu vyake, akajibwaga kama mzigo huku akiugulia maumivu. Aligalagala pale chini kwa muda wa SAA zima hatimaye maumivu yakapungua. Akaamua kurudi bwenini kulala.
Alinyatanyata mpaka alipokifika kitanda chake. Alilala huku akimfikiria Nadia.
“Mh! Huyu mtu si wa mchezo dah!” Alijisemea Doreen kimoyomoyo, kwa maumivu aliyoyapata hakuweza hata kuinuka kitandani.
” Nitafanyaje Mimi? Siku zimeisha sana sasa lakini bado kitu kimoja tu, titi la msichana mzuri! Nitapataje sasa?” Alijiuliza Doreen bila kupata majibu.
“Enhe! Inabidi nifanye kitu.. Nimtumie MTU..!” Doreen alipata wazo kuwa inabidi amtumie mtu ili kupata titi hilo ili akamilishe mambo aliyoyahitaji. Lakini asingeweza kufanya kwa usiku ule kwani alikuwa hoi bin taabani.
Usingizi ukampitia kidogo na kwakuwa ilikuwa SAA kumi na nusu hakulala sana kengele ya kuamka ikamshtua.
Kulikuwa tayari kumekucha. Doreen alikuwa hana nguvu kabisa mwilini na mwili wake ulikuwa bado unamuuma hivyo akashindwa kwenda darasani kwa madai kuwa alikuwa mgonjwa. Ila moyoni alimwogopa sana Nadia na hakutamani hata kumwona kwani alimuonea aibu.
Wanafunzi wote walienda darasani isipokuwa Dorice, alibaki bwenini na alitaka kuitumia nafasi ile vizuri ili amtumie mtu kutafuta titi la msichana mzuri wa kuvutia.
******
Wazazi wa Eddy walishika njia kutokea mkoani Iringa kuelekea pangani Tanga.
Walikuwa na matumaini mazito ya kumpata mganga mashuhuri aitwaye Tembo wa Bahari.
Hawakua na wasiwasi wowote juu ya mganga huyo kwani tayari walikuwa wamezisikia sifa zake kuwa yupo vizuri sana katika suala la matibabu.
Eddy alikuwa ametulia kimya ndani ya gari lile ambalo dereva alikuwa ni Mr.Alloyce.
Kila Mara aliyakumbuka maneno ya Doreen kuwa endapo watafika kwa mganga basi uhai wake utakuwa umefikia kikomo. Kuna wakati aliyapuuzia mawazo hayo lakini wakati mwingine alihisi yana ukweli ndani yake, kama Doreen aliweza kumtoa sehemu zake nyeti atashindwa kumuua? Alijiuliza Eddy.
Ukimya ulitawala ndani ya gari lakini kelele nyingi zilitawala kichwani mwa Eddy kwani mawazo yalikuwa hayakauki kichwani mwake
“Mama!” eddy aliita.
“Sema mwanangu..!”
“Nina njaa!”
“Ngoja nikupe chakula..!”
Mama Eddy alichukua hotpot na kumtolea mapaja ya kuku yaliyokaushwa vizuri pamoja na chipsi mayai zilizoshikana vizuri.
“Chukua ule..”
“Sawa! Ila nipe chakula!”
“Mh! Chakula hicho!”
“Hicho siwezi kula maana kina uchafu..!”
Alisema Eddy maneno yaliyomchanganya sana mama yake kwani kila alipotazama chakula kilikuwa kizuri tu.
“Hakuna uchafu..!”
“Upo!”
Eddy alisisitiza na Mara hiyo akaanza kuhisi kichefuchefu.
“Mama simamisheni gari nataka nikatapike nje..”alisema Eddy. Kwa haraka Mr.Alloyce alisimamisha gari wakamtoa nje Eddy ili akatapike.
Eneo like lilikuwa na miti mingi kwani lilikuwa pori. Eddy aliwatazama wazazi wake, kisha akasogea kando kidogo.
Akawatazama tena kwa jicho la wizi , akajiweka sawa kisha bila wazazi wake kutarajia akatimua mbio Kali kuelekea porini.
Wazazi wake wakapigwa butwaa sana wakashindwa wafanye nini wakabaki wamezubaa huku wakitazama kwa mshangao. Eddy alikuwa tayari amewapotea machoni mwao kwani mbio alizokuwa akikimbia zilikuwa za MWENDOKASI…..
..DOREEN alikuwa bado hana hali nzuri kiafya, mwili wake ulikuwa hauna nguvu kabisa kwani ile adhabu aliyoipata usiku ilimwadhibu haswa. Alijikuta anamwogopa Nadia kupita kiasi, moyoni mwake alikiri kuwa kweli Nadia Joseph alikuwa Mchamungu kweli.
Wakati huo akiwa bado yupo kitandani akiugulia maumivu, Doreen alifikiria jinsi ya kuweza kupata titi la msichana mrembo ili akamilishe kazi yake aliyotumwa kuifanya. Siku zilikuwa zimeisha sana lakini alijipa moyo kuwa ameshamaliza kazi kwani kupata titi aliona kama kazi rahisi tu ingawa ilishaanza kupata vikwazo.
Doreen alishuka kitandani kwake. Akavua nguo zote kisha akasogelea begi lake na kuchukua shanga nyeusi akaivaa shingoni mwake.
Na kwakuwa alikuwa peke take chumbani mle Doreen alifanya mambo yake bila woga. Akachukua kichupa kimoja kidogo kwenye begi lake halafu akamimina kidogo unga unga uliokuwamo mle na kujipaka usoni kisha akapiga magoti chini na kuinamisha kichwa chake huku akitamka maneno Fulani.
Ghafla karatasi ambayo ilifanya mauaji ya walimu ofisini ikamjia mkononi make.Ikumbukwe kuwa karatasi ile ilichukuliwa na mwalimu Jason ambapo kulikuwa na maandishi yaliyomuonya kuwa asimpe mtu mwingine, hivyo Mwalimu Jason aliamua kukimbia nayo na alikuwa akikaa Nayo kwa siku zote zile.
Doreen alitabasamu baada ya kuitazama karatasi ile, akaishika vizuri kwa mikono miwili kisha akasema “NENDA KWA MWALIMU JASON! MWAMBIE ANILETEE TITI LA MSICHANA MREMBO! NAKUAMINI!” alisema Doreen kisha akaiachia karatasi ile, ikapaa hewani na ikapotea.
Doreen alifurahi sana akajua tayari amekwisha maliza kazi yake. Akiwa bado ameketi pale chini akiendelea na mambo yake mengine ghafla mlango wa bweni lake ukagongwa halafu akakumbuka kuwa hakuubana mlango ule vizuri kwa komeo Doreen alishtuka sana kwani alikuwa mtupu na alikuwa na maunga unga usoni. Akahisi fumanizi la uchawi tayari limemfikia.
********
Mansoor alikubali kumsaidia Dorice ili kumwokoa Eddy lakini bado moyo wake ulimuuma sana. Hakuwa radhi kumwacha binti yule kirahisi pasina kumuoa ilhali moyo wake ulizimia kwa mapenzi kwa mrembo yule. Mansoor alimpenda sana Dorice hivyo akajiona bwege sana kumwacha msichana yule aondoke kwenye himaya yao wakati moyo unamhitaji.
“Mwanamke anahitaji kubembelezwa! Nikimbembeleza sana anaweza kunikubali…. Yawezekana anamuogopa mama yangu kutokana na vitisho alivyompa… Mhh nitajaribu tena bahati yangu kwani moyo wangu hautakuwa na amani kabisa nikimuacha Dorice!” Aliwaza Mansoor akiwa ametulia peke yake kando ya Maua mazuri yanayotoa harufu ya kuvutia. Aliwaza sana juu ya kumpata Dorice lakini bado hakuona njia sahihi ambayo ingekubalika haraka zaidi ya kumshawishi tu huba na kumbembeleza kwa mahaba.
Akiwa katika wingu hilo zito la mawazo Mansoor alishtushwa na upepo mkali. Akajua moja kwa moja mama yake alikuwa njiani kwani upepo ule zilikuwa in hatua za Malkia. Punde si punde malkia akatia timu na kuketi kando ya Mansoor.
“Vipi mwanangu? Mbona unasononeka sana kiasi cha kuondoa amani ya moyo wangu?”
“Hakuna tatizo mama!” Alijibu Mansoor huku akijaribu kuachia tabasamu.
“Unanificha Mansoor.. Au yule binadamu asiyejaa hata kiganjani bado anakusumbua?”
“Hapana mama.. Hana tatizo lolote na anaonesha moyo wa kunipenda!” Ilibidi Mansoor amdanganye mama yake kwani alijua madhara ambayo angemfanyia Dorice kama angemweleza ukweli.
“Kweli?” Malkia alifurahi.
“Kweli mama yangu.. Malkia mtukufu..!” Alitabasamu Mansoor ingawa moyoni aliumia.
“Vizuri sana… Nadhani furaha yako itarejea sasa!”
“Ndio mama wala usiwe na wasiwasi!”
Malkia aliondoka zake akiwa ameghairi lengo lake la kumwangamiza Dorice. Kwani alipanga kuondosha uhai wake endapo angekataa kumpenda Mansoor.
Sehemu Ya 8
Malkia aliondoka zake akiwa ameghairi lengo lake la kumwangamiza Dorice. Kwani alipanga kuondosha uhai wake endapo angekataa kumpenda Mansoor.
Mansoor alimfuata Dorice kwenye chumba alichokuwa anaishi. Aliingia chumbani mle akiwa amemletea zawadi ya maua mazuri yanayonukia vizuri sana. Alipoingia tu, akasikia sauti ya kilio kutoka kwa Dorice. Mansoor akashtuka kidogo kisha akamsogelea taratibu Dorice.
“Unalia mini Dori?”
“Nataka nirudi nyumbani… Wazazi wangu watakuwa wananitafuta sana..!”
“Usilie Dorice…!”
“Siwezi kuzuia maumivu yangu juu ya wazazi wangu Mansoor… Pia namfikiria mpenzi wangu..!”
“Nyamaza Dorice.. Nitakusaidia kwa yote hayo… Hebu nitazame!” Mansoor alimkazia macho Dorice kisha akamkabidhi Maua aliyokuwa ameyashika.
“Yanini..?”
“Usijali.. We pokea tu..”
Dorice aliyapokea maua Yale huku akisitasita sana. Baada ya kuyapokea mansoor alitabasamu sana.
“Asante kwa kupokea zawadi yangu Dorice… Nakupenda sana!” Dorice hakujibu kitu zaidi ya kumshangaa Mansoor.
“Nataka nikusaidie… Upo tayari..?”
“Nipo tayari Mansoor tafadhali..”
“Sawa Dorice.. Kabla sijakusaidia nahitaji unisaidie kitu..”
“Kitu gani!?” Dorice alishtuka sana.
“Nataka uolewe na Mimi.. Tafadhali Dorice… Nitakusaidia kwa lolote utakalo ukikubali kuolewa na Mimi..!”
“Mansoor! Nilishakwambia nampenda Eddy…”
“Ukikubali kuolewa na Mimi nitakusaidia kumpata Huyo Eddy na nitakuruhusu uendelee Naye… Nakuomba Dorice! Ilidhishe nafsi yangu!” Alisema Mansoor huku akipiga magoti.
*******
Mwalimu Jason alikuwa akisumbuliwa sana na karatasi lile alilolichukua ofisini baada ya kifo cha Mwalimu Mbeshi. Halikutakiwa kuonekana na MTU yeyote wala kuguswa na maji.
Lilikuwa likimchanganya sana kichwa kwani kila siku lilikuwa likibadili ujumbe na kuandika masharti mapya.Siku hiyo asubuhi mwalimu Jason kutokana na kutokwenda kazini aliamka asubuhi na mapema ili afue nguo zake.
Alikusanya nguo chafu zote na kuziweka kwenye beseni la kufulia lenye maji na sabuni. Na alikuwa na uhakika kabisa kuwa karatasi halikuwa kwenye nguo zile. Akaanza kufua nguo zake kwa umakini ili azitakatishe ndipo alipogundua kuwa suruali yenye karatasi lile la maajabu ipo ndani ya beseni la maji.
Kengele ya hatari ikagonga kwa kasi moyoni mwake, akaipoa suruali ile huku mapigo yake ya moyo yakimpiga kwa kasi.
Akaanza kutafuta karatasi lile kwenye mifuko ya suruali ile. Hofu ikamzidia maradufu baada ya kutafuta kila mfuko na kulikosa karatasi lile.
Mwalimu Jason alichanganyikiwa sana, ikambidi aanze kupekua suruali zake zote na kutafuta vizuri karatasi lile alikuwa akiliita karatasi la kifo kwani kila mara lilikuwa likimuonya kuwa akikosea sharti basi lazima afe.
Mwalimu Jason alipekuwa kila suruali aliyokuwa ameiloweka kwenye maji lakini bado hakuona karatasi akazidi kuchanganyikiwa.
Alizitupa chini nguo zote kisha akaingia ndani na kuanza kupekua kwenye kila suruali lakini bado hakuona karatasi lile. Mwalimu Jason alipigwa na butwaa. Kijasho chembamba kikaanza kumtoka kila kona ya mwili wake. Akajitupa kitandani na kuanza kulia kwa woga. Alijua tayari kifo kiko mbele yake si muda mrefu.
Ghafla simu yake ikaita na kwakuwa alikuwa kwenye kilio hakuweza kupokea simu. Akaicha tu bila hata kuingalia.
Lakini kwa bahati njema aliona karatasi ikiwa pembeni ya mto wake wa kulalalia. Mwalimu Jason alifurahi kisha akaichukua karatasi ile na kusoma ujumbe mpya ulioandikwa hivi “MSICHANA YEYOTE ATAKAYELALIA KITANDA HIKI.. UNATAKIWA UMKATE TITI LAKE LA KUSHOTO HARAKA IWEZEKANAVYO. LASIVYO UHAI WAKO UTAFIKIA KIKOMO!”
Mwalimu Jason akatumbua macho kwa mshangao. Akarudia kusoma ujumbe ule mara mbilimbili lakini hakuna kilichobadilika. Akahisi mwili wake unaishiwa nguvu kabisa kwani Siku ile alikuwa na miadi na mpenzi wake. Alijiuliza atafanya nini hakuwa na la kufanya.Simu take ikaita tena akaitazama ilikuwa ni namba ya mpenzi wake. Akapokea.
“Baby mbona hukupokea simu?”
“Ulipiga?” Jason alijifanya kama hajui lolote kama simu ilipigwa.
“Kwani hukuona? Ok.. Nipo njiani nakuja!”
“Eeeh!” Jason alishtuka sana.
“Vipi mbona unashtuka?”
“Ah..una.. Naomba usije home Leo.. Kama vipi tukutane Hotelini..”
“Hivi Jason una akili timamu wewe? Hapo kwako kuna nini? Au una MTU mwingine?”
“Sina MTU mwingine baby.. Ila..” Jason alitamani kujitetea ila hakuweza kufanya hivyo.
“Nitoke Dar kuja Iringa kwaajili yako halafu uniletee hizo habari zako.. Kwani tulikubaliana nini?” Msichana yule alimjia juu mwalimu Jason
“Usipaniki baby basi.. Hotelini ni kuzuri pia..!”
“Kama una michepuko yako basi tutajua..!”
Msichana yule akakata simu.
Mwalimu Jason alijiona ana mtihani mkubwa sana. Aliwaza na kuwazua lakini bado hakupata jibu. Majira ya SAA Kumi na nusu jioni mlango uligongwa. Mwalimu Jason alienda kufungua akakutana USO kwa uso na sura ya Judith ambaye ni mpenzi wake akiwa amenuna sana.
Mwalimu Jason hakuwa na la kufanya zaidi ya kumkaribisha Judith ndani.Waliposalimiana tu Judith akaingia chumbani kwa mwalimu Jason ili akaweke mizigo yake.Lakini kila alipomtazama Mwalimu Jason, hakuwa na furaha hata kidogo.
“Mbona hujanifurahia?”
Aliuliza Judith
“Nipo kawaida.. !” Alijibu mwalimu Jason.
“Ok basi ngoja nikapumzike kidogo maana nimechoka kweli..!” Alisema Judith huku akipiga hatua kuelekea kitandani…
. MANSOOR alimtazama Dorice kwa jicho la kiulizo lililomtaka azungumze chochote lakini Dorice hakusema neno zaidi ya kuangua kilio cha huzuni baada ya kukosa msaada kwa Mansoor. Dorice alilia sana kwani alijua kurudi tena duniani sasa ni ndoto.
“Mansoor naomba unisaidie!” Dorice alipiga magoti akamsihi Mansoor aweze kumsaidia ili arudi kwao pia amsaidie kumwokoa Eddy ili furaha ya penzi lake irudi.
“Dorice! Naweza kukusaidia kwa yote hayo… Ila inabidi ukubali kuolewa na Mimi maana bila hivyo mama yangu hatonielewa…!” Mansoor alisisitiza.
“Siwezi kuolewa na wewe..!”
“Kwanini? Au kwa vile Mimi sio binadamu mwenzio? Jua nakupenda na nitakuruhusu kuendelea na Eddy.. Nielewe Dorice!” Mansoor alizidi kumweka Dorice katika wakati mgumu sana. Kwani kiukweli Dorice aliuhitaji msaada wa Mansoor ila masharti yake yalikuwa kikwazo sana. Dorice alishindwa kung’amua juu ya mtihani ule mzito. Alijua fika wazazi wake wataumia sana endapo wakijua kuwa Hayupo duniani, aliyafikiria maumivu ambayo mama yake angeyapata kama yeye angepotelea kule kwenye ulimwengu wa majini.
“Sijui nimkubali halafu akinirudisha duniani nimkatae?” Dorice Alizidi kuwa na utitiri wa mawazo kichwani mwake. Ghafla akashtushwa na sauti nzuri ya mahaba ya Mansoor akizidi kumshawishi kuwa amkubalie ili aweze kumsaidia kutatua matatizo yake.
“Dorice! Nifanye nifurahi tafadhali.. Nilipendwa na wengi ambao si chaguo langu.. Nasikitika chaguo langu linakuwa mwiba moyoni mwangu! Kwanini lakini?”
Dorice alivuta pumzi ndefu na kuishusha taratibu, huku akiwa ameinamisha kichwa chake. Taratibu akanyanyua kichwa chake na kumtazama Mansoor. Macho yake yalistaajabu uzuri wa asili aliokuwa nao kijana yule. Hata kama majini ni wazuri lakini Mansoor alizidi kipimo, kuanzia macho yake, pua yake na midomo mizuri ya kupendeza sana.
“Nimekubali Mansoor! Ila kabla ya yote naomba uniahidi kama utanisaidia!” Alisema Dorice kwa sauti iliyotulia sana. Maneno hayo yalifungua ukurasa mpya moyoni kwa Mansoor, alifurahi kupita kiasi akamkumbatia kwa nguvu Dorice.
“Nakuahidi kukusaidia Dorice!” Alisema Mansoor akiwa amemkumbatia Dorice.
Walikumbatiana kwa muda kisha wakaachiana. Mansoor akamtazama Dorice huku akitabasamu.
“Nataka uvae vizuri nikupeleke kwa mama yangu muda huu!”
“Nitavaa nini? Sina nguo!”
Alisema Dorice kwa woga huku moyo wake ukimsuta kwa kumsaliti Eddy kwani alikwisha muahidi kuwa hatokuwa na mwanaume mwingine yeyote zaidi yake.”lakini ni kwa sababu yake..!” Alijipa Jibu Dorice.
“Unapenda nguo gani?” Aliuliza Mansoor.
“Nguo yoyote itakayonifaa!” Alijibu Dorice.
Mansoor alinyoosha mkono juu ghafla ukatokea mfuko mmoja wenye ukubwa kiasi kisha akamkabidhi Dorice. Dorice aliogopa sana, akasita kupokea.
“Usiogope.. Chukua!”Dorice akapokea mfuko ule japo kwa woga kisha akaufungua ili atazame kilichomo. Akapigwa na bumbuwazi.
*****
Eddy aliwaacha wazazi wake barabarani pale wakiwa hawaelewi la kufanya. Walibaki wanatazamana kwa muda wa dakika tano nzima bila kusema neno lolote. Kila mmoja alionekana kutoelewa kilichotokea.
Sehemu Ya 9
“Usiogope.. Chukua!”Dorice akapokea mfuko ule japo kwa woga kisha akaufungua ili atazame kilichomo. Akapigwa na bumbuwazi.
*****
Eddy aliwaacha wazazi wake barabarani pale wakiwa hawaelewi la kufanya. Walibaki wanatazamana kwa muda wa dakika tano nzima bila kusema neno lolote. Kila mmoja alionekana kutoelewa kilichotokea.
“Mr. Alloyce.. Tutakuwa wazembe tena wajinga… Mtoto ameondoka tumesimama tu kama milingoti hapa!” Alisema mama Eddy.
“Tufanyeje mke wangu?”
“Tumfuate!”
“Tutamfuata wapi sasa?”
“Kokote, kwani we hujaona alikokimbilia?”
“Dah! Tuna mtihani mzito!”
Ilibidi waingie msituni na kuanza kumsaka Eddy. Walimtafuta kila kichaka lakini hawakuona hata dalili za uwepo wa kijana wao. Jua liliwawakia huku wakizidi kumtafuta Eddy lakini bado hawakuona hata dalili za kumpata.
“Hili tatizo la kimwendokasi dah!” Alisema baba Eddy.
“Inabidi tulitatue kimwendokasi!”alijibu mama Eddy akiwa ameshika mkono kiunoni. Anahema kupita kiasi kutokana na uchovu aliokuwa nao.
“Mke wangu!”
“Abee..”
“Mimi naona turudi tu nyumbani hapa tutafanya kazi bure!” Alishauri Mr.Alloyce
“Nilishasema wewe humpendi mwanangu.. Turudi nyumbani halafu?”
Mama Eddy alimjia juu mumewe, akaona kama hana mapenzi wala uchungu kwa mwanae lakini baba Eddy alikuwa sahihi kabisa kwani mpaka pale walipofikia wasingeweza kumpata Eddy. Walikuwa wamechoka sana, pia wasingeweza kusonga mbele zaidi kutokana na ukubwa wa msitu waliokuwamo.
“Sikiliza mke wangu.. Nataka turudi tutafute njia sahihi ya kumtafuta mtoto hapa tunazidi kupoteza muda!” Kwa shingo upande mama Eddy aliamua kusikiliza ushauri wa mumewe. Wakatembea umbali mrefu sana mpaka walipolifikia gari lao.
Walipofika kwenye ile gari, kengele ya hatari iligonga mioyoni mwao wakatazamana kwa mshangao lakini hawakuwa na la kufanya kwani gari yao ilikuwa ikiteketea kwa moto mkali utadhani imemwagiwa petroli.
“Nini hiki?” Walijiuliza kwa pamoja bila kupata jibu la haraka. Ilibidi wasogee kwa ukaribu ili wahakikishe wakionacho. Ni kweli gari yao ilikuwa ikiwaka moto, na alikuwa hatua za mwisho kiasi kwamba hata wangezima moto ule bado gari yao isingesalimika.
“Haya maajabu!”
“Tena maajabu haswaaa ya ulimwengu..!”
Wakiwa bado wanaendelea kushangaa ajali ile ya moto kwenye gari ile, ghafla moto ukazima kama vile umezimwa kwa maji halafu gari ikatoweka machoni mwao.
Waliogopa kupita kiasi wakajikuta wanatimua mbio bila kutazamana.
Walikimbia sana wakiifuata barabara, kwa bahati mbaya mama Eddy alijikwaa na kuanguka chini kama gunia. Damu nyingi zikaanza kumtoka mguuni. Akapiga kelele Kali za maumivu, zilizokatisha mbio za Mr.Alloyce. akageuka nyuma na kumwona mkewe akivuja damu nyingi sana. Akarudi haraka.
“Vipi mke wangu?”
“Nime..nimeumia Mme..wangu..!” Mama Eddy aliongea kwa shida sana kwani alipata maumivu makali sana.
Walikuwa hawana hata mia mbovu mifukoni mwao kwani pesa zote waliziacha kwenye gari ambalo limepotea kimaajabu.
“Mke wangu” aliita baba Eddy baada ya kuona mkewe anakoroma isivyokawaida.
“Mama Eddy..!!!!!!”
*****
Mwalimu John alikuwa bado anatokwa na funza mguuni, alitaka kuieleza familia take juu ya kile kilichompata lakini pindi alipotaka kuiambia familia yake juu ya mkasa ule mzito ghafla akapigwa Kofi zito lililomrusha kama shoti ya umeme kutoka juu ya kiti mpaka chini. Alipiga yowe Kali lililowashangaza watu wote sebuleni pale. Waliogopa sana.
Leyla mke wa Mwalimu John alimsogelea mumewe na kumwangalia kama yupo salama ghafla akapigwa na mshangao ulioambatana na furaha kwani miguu ya mwalimu John ilirudi katika hali ya kawaida na haikuwa na funza tena.
“Mume wangu!” Aliita Leyla kwa Furaha, lakini John aliendelea kulalamika pale chini kwani Kofi alilopigwa lilikuwa zito kuzidi uzito wa mwili wake lakini hakujua limetoka wapi.
“Jamani.. Njoo muone maajabu..!”
Alisema Leyla akiwaambia ndugu wengine wa mumewe.Wote walimsogelea na kushangaa kilichotokea, wakakiri kwamba kweli dunia ina maajabu tena yanayotisha na kuogopesha.
Mwalimu John aligalagala pale chini kwa muda wa kama robo saa kisha taratibu akainuka. Alipotazama miguu yake aliifurahia sana kwani ilikuwa imerudi kwenye hali yake ya kawaida. Akainuka pale chini na kumkumbatia kwa furaha. Lakini cha ajabu kila alipotaka kuzungumza chochote..
*****
Doreen alibaki ametulia kimya pindi mlango unagongwa. Aliona anachofanya ni ujinga ni heri ainuke avae nguo kabla hajafumwa. Alipoinuka tu mlango ulifunguliwa. Doreen alishtuka sana kwani alikuwa yupo uchi wa mnyama na alikuwa amevaa shanga huku usoni amejipaka maungaunga na kumfanya awe na mwonekano wa kutisha.
Madamu Amina akiwa ameambatana na nesi wa shule walishtuka sana kukmkuta Doreen akiwa vile. Walitazamana kwa mshangao kisha wakamtazama Doreen kwa hofu.
“Doreen unafanya nini?” Aliuliza Madam Amina kwa woga ingawa alikikaza tu. Doreen alibaki kimya tu bila kujibu chochote. Macho ya Madam Amina yalitua moja kwa moja kwenye kile kichupa cha dawa kilichokuwa pale chini tena kilikuwa kimefungwa kijitambaa kidogo cha kaniki kwa juu. Kiliwatisha sana.
“Doreen! Unafanya nini? Mbona hujibu?” Alisema nesi kwani walikuwa wamefikishiwa taarifa kuwa Doreen ni mgonjwa ndio maana amebaki bwenini.
MAMA Eddy aliendelea kukoroma kwa nguvu pale chini na kuzidi kumchanganya sana mumewe Mr.Alloyce. Mwanaume yule alichanganyikiwa haswa na kujikuta akiangusha chozi lake kwa uchungu kwani alishindwa kuielewa hali ya mkewe. Alimuita Mara kadhaa lakini Mama Eddy aliendelea kukoroma tu bila kujibu neno.
Mr.Alloyce akazidi kuchanganyikiwa sana bila kuelewa afanye nini na kwa wakati ule hakukuwa na msaada wowote katika eneo lile. Akachukua simu yake na kuitafuta namba ya rafiki yake haraka kisha akapiga lakini alipopiga tu akakutana na maandishi haya ” Emergency call only” ndipo akagundua kuwa sehemu aliyokuwapo haikuwa na mtandao, akazidi kuogopa huku huzuni ya kupotelewa na mkewe ikimvaa kwa kasi ya ajabu. Kwa muda wote huo hakuna gari yoyote ilipita eneo lile.
“Na..na..nakufa..nakufa mume ..wangu..” Ilisikika sauti ya mama Eddy.Sauti ile ya mama Eddy ilikuwa kama mwiba mchongoma uliopenya katikati ya moyo wa Baba Eddy. Hakuamini kile alichokisikia kwa mkewe akahisi ilikuwa ndoto tu isiyokuwa na ukweli wowote.
“Usife mke wangu.. Usife mpenzi wangu!” Aliropoka Mr.Alloyce lakini tayari alikuwa amechelewa sana kwani mkewe alikuwa tayari amekata roho.
“Mke wangu! Mke wangu!” Baba Eddy alijaribu kumuita mkewe lakini tayari alikuwa ameaga dunia. Simanzi ilimjaa Mr. Alloyce alijkuta Analia kama mtoto mdogo huku akijigaragaza chini kama mwendawazimu. Alilia kwa uchungu sana kwani alimpenda mkewe kwa dhati na hakuwa tayari kumpoteza. Alikuwa ndiye ndugu yake pekee aliyesalia kwani Mr.Alloyce hakuwa na kaka, Dada wala wazazi.
Wakati akiwa ameushikilia mwili wa mkewe ghafla akajikuta hajashika chochote mkononi mwake zaidi ya gauni alilokuwa amevaa mkewe, ndilo pekee lililombakia mkononi. Akashtuka sana, akajaribu kupepesapepesa macho huku na kule ili aone mkewe ameenda wapi lakini hakumuona. Mr. Alloyce akainuka pale chini haraka na kuanza kutimua mbio kwani alishaona hali si shwari.
Alikimbia kwa muda mrefu bila kujijua anakimbiaje mpaka pale fahamu zake halisi zilipomrudia ndipo akasimama kidogo na kupumzika. Alihema kwa nguvu huku akiwa amejibwaga chini ghafla akasikia mlio mkali ukimjia nyuma yake. Mr.Alloyce akainuka chini na kuanza kukimbia tena lakini akiwa katika mbio hizo akapata ufahamu tens akasikiliza tena ule mlio akagundua ni mlio wa honi ya gari.
Akaamua kusimama ili aombe msaada. Baada ya muda ya sekunde kadhaa basis la abiria likitokea Dar es salaam lilikaribia mahali alipo Mr.Alloyce ndipo alipoanza kupunga mkono ili aombe msaada.
Dereva wa basi lile alikuwa mwelewa sana, akasimamisha gari na kumsaidia Mr. Alloyce aliyekuwa akihema sana. Mr.Alloyce alishukuru sana akaingia ndani ya basi.
“Vipi mbona umeshika gauni hilo mkononi?” Aliuliza kondakta baada ya kumkagua kwa macho Mr.Alloyce
“We acha tu..” Alijibu Mr. Alloyce huku akihema sana.
“Isije ikawa umeua huko halafu sisi tumekusaidia hapa…!” Alisema kondakta.
Mr. Alloyce alikataa kwa kichwa tu kwani hakuweza hata kujibu kutokana na maswahibu yaliyomkuta.
“Haya.. Unashuka wapi?”
“Naenda Ipogoro Iringa!” Alisema Alloyce na kuinamisha kichwa huku akilia.
******
Doreen alishindwa la kufanya mbele ya mwalimu wake pamoja na Matron alibaki ameduwaa tu lakini cha ajabu hakuonesha aibu yoyote. Alijikausha kimya tu akiwatazama.Mwalimu Amina na Matron walomsogelea Doreen kwa woga.
“Unaumwa nini?” Aliuliza Matron
“Kichwa!”
“Pole! Nakuletea dawa!” Alisema matron kwa sauti ya upole sana.
“Asante” alijibu Doree kwa sauti ya chini kidogo ila kwa kujiamini sana.
Matron na Madam Amina walitoka. Doreen aliinuka pale chini na kuvaa nguo zake kisha akajifuta madawa yake usoni.
“Huku ni kudhalilika sana ingawa nimejikaza kisabuni, duh!” Aliwaza Doreen huku akirudisha vitu kwenye sanduku lake.
Matron na madame walibaki na maswali mengi sana vichwani mwao. Kila mmoja alijiuliza kivyake lakini uvumilivu ukawashinda. Wakajikuta wameanza kuulizana ili wasaidiane kupata majibu wakati huo wakielekea kwenye dispensari ya shule kuchukua dawa.
“Hivi we umemuelewa yule mtoto?” Aliuliza matron kwa sauti ya chini.
“Mh! Nikajua we umemwelewa.. Sijamwelewa! Lakini nimepata jibu la kitu kimoja…” Alisema madam Amina huku akipunguza sauti na kumsogelea vizuri matron.
“Nini tena?”
“Nilisikia kuwa huyu binti ni mchawi na ndiye aliyesababisha majanga yote haya hapa shule na niliongea na afisa elimu kuhusu hilo..”
“Mh! Afisa elimu hataelewa maana kama ujuavyo serikali haiamini uchawi!”Alisema matron.
“Nilizongea nae kiutu tu.. Na Leo nimpata picha ya huyu mtoto kwenye simu..!”alisema madam Amina huku akifungua picha kwenye simu na kumuonesha Matron. Ilikuwa ni picha iliyomwonesha Doreen jinsi alivokuwa kule chumbani. Matron alishtuka kidogo kwa ujasiri aliokuwa nao madam Amina mpaka akampiga picha Doreen.
“Nimeamua nimpige hii picha kama uthibitisho… Nimempiga kwa uangalifu sana … ” alisema madam Amina huku akimpigia simu Afisa elimu ili afike shuleni pale na waweze kumfukuza shule Doreen kama walivyokubaliana na Afisa Elimu.
“Sasa mna vithibitisho?”
“Hapa hakuna kutumia serikali la sivyo tutaisha… Huyu afisa elimu tumeongea mengi ambayo huwezi kuelewa..!”
Alisema Madam Amina kwa kujiamini sana kisha matron akachukua dawa za kutuliza maumivu na kuelekea bwenini kwa Doreen. Njiani alikuwa akimpigia simu Afisa elimu lakini hakupatikana.
Walifika bwenini ili wamkabidhi Doreen dawa. Lakini walichokikuta wakabaki wanatazama kwa mshangao wa hali ya juu.
*****
Mwalimu Jason alitamani amzuie mpenzi wake Judith asilale kitandani kwake lakini hakuweza. Judith alikuwa tayari amejilaza kitandani kwa Jason.
“Judith ndo tabia gani?”
“Ipi? “
“Umefika hata hajaongea chochote unalala? Kwanini?”
“Kama huna muda na Mimi nifanyaje?”
“Uvofanya sio bhana! Inuka basi njoo sebuleni..”
“Sitaki!”
Sijui ni shetani gani aliyempitia Judith siku ile maana alikuwa king’ang’anizi wa mambo kuliko kawaida. Licha ya mwalimu Jason kumkatalia kulala kitandani pale lakini Judith hakumwelewa hata kidogo.
Mwalimu Jason alibaki kimya huku malumbanoakali yakiendelea kichwani mwake. Alikuwa haelewi aamue nini kati ya kifo chake au kukata titi la Judith. Alikuwa na mapenzi ya dhati sana kwa mwanamke yule lakini Leo hii shetani alitaka aingilie kati kuvuruga penzi lao. Mwalimu Jason alikaa chini machozi yakimbubujika. Judith aligundua kuwa mpenzi wake alikuwa Analia moyo wake ukashtuka kwani daima hakupenda kuona mpenzi wake akiwa katika halo ya huzuni.
Akainuka kitandani na kumfuata Jason pale alipokuwa ameketi.
“Baby! Mbona unalia?” Aliuliza Judith kwa sauti ya mahaba yenye kubembeleza. Lakini Jason hakujibu kitu zaidi ya kuendelea kulia.
“Nisamehr mpenzi nilikuwa nakutania tu.. Kwani hujazoea utani wangu baby?” Masikini Judith alianza kujitetea akidhani amemkosea mpenzi wake bila kujua kuwa uhai wake ulikuwa hatarini sana. Jason hakujibu kitu, akaendelea kulia tu na kumfanya Judith ajisikie vibaya sana na kuhisi kuwa alimkosea mno Jason. Judith akaendelea kuomba msamaha lakini ilikuwa kazi bure.
“Hujanikosea!” Jason aliamua kimjibu Judith. Na wakati huo kuna sauti aliyoisikia masikioni mwake ikimwambia”Chukua titi haraka!” Jason akaongeza kilio.
Sauti ile ilizidi kumsisitiza mpaka akajikuta anainuka na kutoka chumbani mle. Judith alibaki kajiinamia akijiuliza mini kimemkumba mpenzi wake. Ghafla akainua kichwa ns kumuons Jason akimjia huku ameshika kisu kikali sana.
Sehemu Ya 10
“Hujanikosea!” Jason aliamua kimjibu Judith. Na wakati huo kuna sauti aliyoisikia masikioni mwake ikimwambia”Chukua titi haraka!” Jason akaongeza kilio.
Sauti ile ilizidi kumsisitiza mpaka akajikuta anainuka na kutoka chumbani mle. Judith alibaki kajiinamia akijiuliza mini kimemkumba mpenzi wake. Ghafla akainua kichwa ns kumuons Jason akimjia huku ameshika kisu kikali sana.
“Vipi baby?” Aliuliza Judith kwa mshangao.
“Nakupenda sana.. Ila…inanilazimu!’ Alisema mwalimu Jason huku akimsogelea Judith. Judith alitoa macho kwa hofu..
..DORICE alipozitazama zile nguo zilikuwa ni nguo nzuri sana za kuvutia. Kulikuwa na gauni moja refu linaloacha wazi mikono lenye rangi ya dhahabu inayong’aa sana. Kulikuwa na viatu virefu vinavyoelekeana na rangi ya gauni kidogo, ushungi wenye rangi ya gauni, mkufu wa dhahabu pamoja na hereni.
Dorice alivishangaa vitu vile kwa mshangao wakati huo Mansoor alikuwa akiachia tabasamu mwanana pembeni yake.
“Vaa Dorice!” Ilisikika sauti ya Mansoor ndipo Dorice alipopata nafasi ya kumtazama tena Mansoor. Akapigwa na bumbuwazi baada ya kuona mansoor amevalia nguo tofauti na alizokuwa amevaa mwanzo, alionekana kama mwanaume wa kihindi pale anapofunga ndoa kwa mavazi yake. Dorice alimshangaa sana Mansoor, woga kiasi ukamvaa moyoni mwake kisha akaanza kuzivaa nguo zile alizopewa na Mansoor.
Pindi anapozivaa nguo zile Mansoor alikuwa tayari ameshatoweka eneo lile.Doricealipovaa nguo zile, alibadilika sana. Alionekana mrembo mno kwa jinsi alivyopendeza. Ukimtazama kwa haraka utadhani msichana kutoka India kumbe ni mnyaturu wa Singida.
Alijitazama kupitia kioo kilichokuwa mbele yake, akajikiri kwamba kweli Mungu hakumkosea katika uumbaji ila alitumia ufundi wa hali ya juu katika kukamilisha sura na umbile lake.
Bada ya kumaliza kuvaa, Mansoor alitokea tena palepale alipokuwa amesimama mwanzo. Alimshtua sana Dorice lakini tayari alikuwa ameshaanza kumzoea Mansoor hivyo hakuogopa sana.
“Umependeza sana Malkia wangu.. Kwa jinsi ulivyositamani hata uende Duniani.. Nahisi wivu sana..” Alisema mansoor huku akimtazama mrembo yule kama waridi likiwa bustanini wakati wa jua la asubuhi.
“Uliniahidi nini?” Aliuliza Dorice kwa hamaki.”Usijali… Nitakupeleka duniani kama nilivokuahidi ila nimekuambia tu hisia zangu… Kama unanipenda kweli ni heri ubaki na mimi huku huku kwetu!” Alisema Mansoor kwa sauti ya upole sana. Dorice hakijibu kitu. Wakaondoka pale na kwenda moja kwa moja kwa malkia.
Malkia alifurahi sana kuona kijana wake ameambatana na mtu ampendae. Radi tatu mfululizo zilipigwa ili kudhihirisha furaha aliyokuwa nayo malkia. Mansoor alitabasam akiwa amemshika mkono mkewe mtarajiwa.
“Harusi ya mwanangu Mansoor… Iwe ya furaha sana kwani amepata kile alichokuwa anahitaji..” Alisena malkia kwa sauti kali. Dorice alimtazama Mansoor kwa woga.
“Usiogope malkia wangu.. Na kuanzia Leo nitakuita Aisha..!”
“Aisha! Kwanini?” Alihamaki Dorice.
“Ukiwa mke wangu huwezi kuitwa Dorice..” Alisema Mansoor.
Wakati Dorice akiendelea kushangaa ghafla upepo mkali ukapigwa, halafu kwa muda huohuo walijikuta wapo eneo lingine lililojaa watu wengi ambao Dorice hakuwaelewa elewa kwa jinsi walivyokuwa.
********
Majira ya SAA moja jioni Mr. Alloyce alikuwa amewasili nyumbani kwake. Kichwa kilijaa mawazo tele ambayo hakujua yataisha vipi kwani matatizo aliyokuwa nayo yalikuwa nimazito kuzidi kilo mia za Mawe. Njia nzima aliwaza na kuwazua lakini bado alijiona yupo kwenye msitu mkubwa wa matatizo ambao hakujua atapenya vipi ili kuepukana nao.
Kila Mara sura ya mkewe mpenzi ilimjia kichwani mwake hakuamini kama kweli amempoteza katika mazingira ambayo ilikuwa vigumu kuyaelewa. Alimfikiria mwanawe Eddy ambaye mpaka Dakika ile hakujua angeanzia wapi kumtafuta ilhali hajui alikoelekea!. Kichwa kilimgonga sana kwa mawazo.
Alifika getini kwake na kumkuta mlinzi wake ambaye alimfungulia. Bila hata ya salamu Mr.Alloyce alipita getini pale na kuelekea ndani lakini alishtushwa sana kuona taa zinawaka ndani pia alisikia sauti kubwa ya muziki. Mr.Alloyce alisitisha mwendo wake kidogo. Akamgeukia mlinzi.
“We Seba nani yupo ndani?”
“Atakuwa Eddy Huyo..”
“Eddy! Eddy gani?” Mr. Alloyce alishtuka sana.
“Kwani kuna Eddy wangapi hapa Mzee..!” Alijibu Mlinzi Seba kwa masihara kwani alikuwa niMTU wa masihara sana.
“Sipo kwenye utani ujue Seba.. Nani yupo ndani?..” Aliuliza kwa hasira mr. Alloyce kwani alihisi Seba anamtania.
“Eddy Mzee..” Alijibu mlinzi.
Mr.Alloyce alihisi kama nguvu zikimpungua mwilini mwake kwani alikuwa haamini yanayotokea kwenye maisha yake. Alijkuta anapatwa na woga ghafla.
“We Seba hebu twende wote ndani..!” Seba hakusita aliamua kumsindikiza bosi wake. Lakini moyoni mwake alikuwa na maswali mengi kwa nini bosi iweje arudi peke yake tena kwa mguu bila gari?. Alijiuliza ila hakuthubutu kunyanyua mdomo wake kuuliza chochote kwani alishaona hali ya bosi wake siku ile haikuwa nzuri.
Walifika mlangoni na kukuta mlango ukiwa wazi ilhali waliondoka na funguo. Suala like lilizidi kumchanganya Mr.Alloyce.
“Hebu niitie Huyo Eddy kwanza!” Alisema Mr.Alloyce kwani alikuwa anaogopa kuingia ndani ila hakujionesha kwa Seba kuwa alikuwa na hofu.
“Eddy!” Aliita Seba.
“Naaam!” Sauti kutoka ndani ilisikika.
“Muite aje nje.. Haiwezekani afungue mziki kama disco humu..” Alisema Mr Alloyce kwa kujivungisha tu kwani bado alikuwa haamini kama Kweli Eddy yupo nyumbani.
“Njoo huku we bwana mdogo..” Alisema Seba. Punde tu, Eddy alitoka nje na kumkuta baba yake. Mr.Alloyce alishtuka sana akahisi yupo ndotoni lakini ilokuwa sio ndoto Bali kweli. Machozi ya furaha yalimtoka, kwani hakutaraji kama angemkuta mwanaye akiwa yuko hai.
“Daddy! Karibu ndani!” Alisema Eddy kwa uchangamfu sana.
“Asante! Seba waweza kwenda..!” Alisema Mr.Alloyce huku wakiingia ndani na mwanae. Mr.Alloyce alishindwa kuizuia furaha yake, alijikuta anamkumbatia mwanaye kwa nguvu huku chozi likimdondoka.
“Eddy mwanangu umefika SAA ngapi?”
“Nilikuja toka mchana..!”
“Kwanini ulitutoroka?”
“Niliwatoroka wapi?” Aliuliza Eddy kwa mshangao, swali hilo lilimshangaza sana Mr.Alloyce. Ila hakutaka kuendekeza zaidi mada ile akijua kuwa inaweza sababisha mambo mengine.
“Umekula nini?” Aliamua kubadilisha mada Mr.Alloyce.
“Nilipika ugali na samaki zilizokuwemo kwenye jokofu.”
“Ulikula ee..?”
“Ndio”
Mr.Alloyce alishangaa sana kusikia vile kwani hakutegemea kama Eddy angekula chakula kwani siku zote alikuwa akikataa chakula akidai ni kichafu. “Leo amekula?” Alijiuliza Mr.Alloyce ama kweli Mungu ametenda.
Mr. Alloyce pia alimshangaa sana mwanaye kwa uchangamfu aliokuwa nao siku ile, alikuwa na furaha ambayo Hakuwahi kumwona akiwa nayo tangu apate matatizo yake. Mr.Alloyce alifurahi ingawa alijiuliza sana imekuwaje?. Baada ya wote kuketi kwenye viti kwa ukimya mzito, ndipo Eddy alipoamua kuvunja ukimya kwa kumtupia swali baba yake. Swali lililoibua simanzi moyoni mwa Mr.Alloyce.
“Mama yuko wapi?”
Swali hilo liliibua machozi kwa Mr. Alloyce, alishindwa amwambie nini mwanaye.
“Daddy mbona unalia kulikoni?” Aliuliza Eddy kwa mshangao.
“Eddy… Mama yako amefariki… Sielewi ntafanyaje… Sielewi ntawaambianini ndugu zake mpaka wanielewee.. Sielewi..!”
“Amefariki? Kivipi?” Eddy alishtuka sana.
“Amefariki baada ya wewe kutoroka..!”
“Kwani Mimi nimewatoroka wapi?”
“Eddy umesahau au..? “
*********
Mwalimu Amina na Matron walibaki wakishangaana tu kwani walipoingia bwenini alikokuwa amelala Doreen. Hawakumkuta mtu yeyote ila walikaribishwa na harufu kali ya haja kubwa.
Walipotazama chini kulikuwa na hali mbaya sana kwani kinyesi kilikuwa kimetandazwa chini kwa mafungu kama matano. Walikunja sura zao kwa kinyaa hawakutaka hata kuingia bwenini mle.
“Doreen!” Aliita Madam Amina kwa sauti lakini hakujibiwa. Alienda hadi chooni kumwangalia lakini hakuwepo.Madam Amina aliamua kwenda madarasani kumtafuta lakini ilikuwa kazi Bure kwani huko pia hakuwepo.
“Dunia ina mambo..!” Alisema Madam Amina. Matron alibaki anashangaa tu huku anatikisa kichwa kwa masikitiko.
“Ila tusije tukauliwa na sisi…!” Alisema Matron.
“Hakuna kitu kama hicho..!”
” mbona unajiamini sana? Una nini mwenzetu?”
“Mungu tu ndo nilienae ananifanya nijiamini sana..!”
“Mh Haya.. Nimeamini kweli huyu mtoto nimchawi haswa.. Kweli amejisaidia bwenini namna ile?.. Sasa sijui ameenda wapi..”Alisema matron.
“Bora tu aondoke ili shule ibaki na Amani tu..!” Alisema Madam Amina.
Kiukweli aliwashangaza sana. Ila bado hawakujua binti yule ameenda wapi.
*********
Mwalimu Jason alikuwa ameshikilia kisu kile chenye makaliili atimizesharti alilopewa kwenye karatasi lile la ajabu. Machozu yalimchuruzika sana, alilia kwa uchungu ulioje.
“Judith… Nakupenda… Ila sina budi kufanya hili…!” Alisema mwalimu Jason huku akitamani kusitisha jambo analotaka kufanya lakini alishindwa kutokana na nguvu za Giza zilizokuwa zikimshinikisha kufanya vile. Alimuonea huruma sana Judith, msichana ambaye alimpenda kwa dhati na kuahidi kufunga naye ndoa. Alimtazama Judith kwa simanzi, judith alikuwa akilia sana huku haja ndogo ikimshuka taratibu miguuni mwake. Alitetemeka kwa hofu sana akijuta kwanini alienda kumtembelea Jason.
“Nataka titi lako..”
“Jason kweli we umekuwa katili namna hiyo.. Kwanin lakini Jason.. Nimekosa nini ..” Alilalamika Judith machozi yakimchuruzika mashavuni mwake alikuwa mwekundu kama pilipili iliyoiva.
“Kwa sababu hiyo.. Bora nife Mimi Judith.. Maana nina mawili tu ya kuchagua. .” Jason aliposema hivyo tu akakiinua kisu na kukishusha kwa kasi mpaka kifuani kwake. Kikazama taratibu huku Judith akimshuhudia jinsi Jason anavyojiua..Akataka kupiga kelele lakini akajiziba mdomo kwa hofu na mshangao…
.EDDY aliumia sana kwa taarifa zile za kifo cha mama yake. Hakutaka kuamini kama kweli mama yake hatakuwa pamoja nao tena. Machozi yalimbubujika kwa kasi huku akimwita mama take kana kwamba alikuwa karibu yake.
Mr.Alloyce alishindwa kuvumilia, alijikuta akiungana na mwanaye kulia. Walilia sana mpaka machozi yaliwakauka, Mr Alloyce alichukua leso yake na kujifuta machozi yake kisha akachukua simu ili awajulishe ndugu na marafiki kuhusu kifo cha mkewe.
Moyo wake ulisita sita sana kwani aliwaza ni jinsi gani ndugu wangeupokea msiba ule wa ghafla bila hata maiti.
“Eddy watanielewaje shemeji zangu? Umesababisha yote haya mwanangu, lakini siwezi kukulaumu!” Alisema Mr Alloyce huku machozi yakimlengalenga.
“Nisamehe dady kwa kuwa chanzo cha matatizo yote!” Alisema Eddy na kuendelea kulia.
Lakini hawakuwa na jinsi ya kufanya kwani tayari maji yalikwisha mwagika na ilikuwa vigumu sana kuzoleka. Ilibidi wakubaliane na kilichotokea ingawa kishingo upande sana.
Mr Alloyce alitafuta namba kwenye simu yake, MTU wa kwanza kumpata alikuwa shemeji yake aishiye jijini Dar ( Dada wa mama Eddy). Simu iliita kisha ikapokelewa, kwa kutetemeka na woga Mr Alloyce akaanzisha mazungumzo.
“Halloo Shem”
“Niambie Shem wake mie.. Kwema huko?” Alisema shemeji take Alloyce kwa uchangamfu sana kama ilivyokuwa kawaida yake. Hakuijua msiba mzito uliokuwa moyoni mwa Mr.Alloyce.
“Huku sio kwema Shem..!” Aliens Mr Alloyce.
“Sio kwema kuna nini?” Alishtuka.
“Sio kwema naomba kesho mfike nyumbani kwangu tafadhali..”
“Kuna nini shemeji? Naomba niambie tu.. Nini kimetokea?”
“Utajua kila kitu kesho..!”
“Hapana..niambie Leo.. Au MPE mama Eddy simu niongee nae..!” Maneno hayo yalimkata maini Baba Eddy hakuelewa ajibu nini akabaki kimya kwa sekunde chache akitafakari cha kujibu lakini ghafla akasikia sauti Kali ya Eddy ikimwita.”Daaaaaaaaady!”
Mr Alloyce alishtuka sana kwani Eddy alikuwa ametoka sebuleni pale dakika chache zilizopita wakati yeye akiongea na simu. Hofu ikamkamata ghafla na kumfanya Mr Alloyce atupe simu sofani na kuelekea sauti ya Eddy inakotokea. Eddy aliita tena “Daaaaaaaady!” Mara hii sauti ile iliambatana na mwangwi mkali uliozidi kumtisha Mr Alloyce.
Alitoka sebuleni na kwenda koridoni lakini hakumuona Eddy. Akasikia sauti ikitokea chooni, alikimbia haraka na kwenda chooni lakini hakumuona, ghafla sauti ya Eddy ikasikika tena ikitokea chumbani kwa Eddy ilibidi amfuate haraka lakini cha kusikitisha Mr Alloyce hakumkuta Eddy ila alikuta damu nyingi zikiwa sakafuni. Alishtuka sana.
*****
Doreen aliamua kuondoka katika shule ya mabango kwani mambo yake yalikwishaanza kuharibika hivyo aliona heri aondoke zake kabla mambo makubwa hayajampata. Na yote hiyo ilitokana na maombi makali aliyokuwa akiyafanya Nadia Joseph ili kuinusuru shule yake kwa majanga yanayoikumba kila kukicha. Aliamua kujitesa kwa kufunga kila siku ili mradi tu shule yao ikomboke na irudi katika mstari ulionyooka.
Hakika Sikio la Mungu si zito ili lisisikie, Mungu alisikia maombi ya Nadia ndio maana alianza kuharibu mambo ya Doreen taratibu.Doreen alimchukia sana Nadia, akaahidi kumfanyia kitu kibaya sana ili alipize kisasi
“Ipo siku yake… Nitamwadhibu huyu mshe** kwa alichonifanyia… Nimeondoka kwasababu yake… Ila hata ipite miaka kumi ntampata tu!” Alijisemea Doreen na kusonya. Wakati huo akiwa njiani kuelekea nyumbani kwa mwalimu Jason kwani alipajua vizuri sana.
Alitembea kwa haraka kwa mwendo wa nusu SAA nzima hatimaye akawasili ndani ya nyumba ya Mwalimu Jason ili akatazame kinachoendelea.
Aliongia mdani na kukutana na ukimya mzito. Kwa ujasiri na kujiamini sana Doreen aliingia chumbani kwa Mwalimu Jason na kukuta harufu Kali ya damu na mwili wa mwalimu Jason.
Kwa wakati huo Judith alikuwa tayari amechapa lapa ili kuiepuka kesi ya mauaji ambayo ingemkabili. Na kama angekuwepo ndani mle basi ingekuwa nyama ya Doreen kwani angetumia vizuri nafasi ile kupata titi la Judith.
INAENDELEA

