SITASAHAU TANGA
Sehemu Ya 1
Nikiwa kwenye mishe zangu za research kwenye mji wa Tanga, ilikuwa ni research ya siku kumi na nne. Jioni ya siku ya pili nikakatisha sehemu flani hivi mjini hapo kuangalia na kutembea tembea, lahaula nikakutana na binti mmoja wa kuvutia sana kwakweli nikajikuta nikivutiwa naye alikuwa mweupe sana na nywele ndefu na umbo kama la mamiss hivi dah nikaona hapa ndio penyewe yani kwani alikuwa na ugonjwa wangu mkubwa unaonivutia kwa wadada nao ni rangi nyeupe.
Sikutaka kupoteza wakati mtoto wa kiume ikanibidi nimsogelee ili niweze kumsabahi, tukasalimiana pale na kujuana majina na tukabadilishana namba. Basi ikawa kila jioni nakutana na yule binti, pesa yote namalizia kwake. Kwakweli nikampenda kwani alikuwa ni binti mzuri sana kama malaika aliyeshushwa hata demu wangu niliyemwacha Dar nikamsahau kabisa kwani hakuwa na mvuto kama huyu dada wa kitanga.
Baada Ya kumaliza ile research ya siku kumi na nne sikutamani kurudi Dar ila ilinibidi nirudi ili nikakabidhi kazi ya watu na nikasake mavumba ya ziada ya kunifaa kumchumbia yule binti wa kitanga.
Niliporudi Dar sasa ndio nilielewa ule wimbo wa “Tanga kunani pale”.
Siku hiyo nikiwa kwenye chumba changu nimetoka kuoga mara simu ikaita kuichek ni yule binti wa kitanga.
MIMI: Hallow mpenzi
BINTI: Ndio mpenzi, mbona hujajisugua vizuri umeacha povu sikioni?
MIMI: (Nikachukua kidole na kugusa sikioni kukitoa kikatoka na povu), haa umejuaje mpenzi?
BINTI: Nimekuona hapo mpenzi wangu.
MIMI: (Nikiangalia kushoto na kulia), umenionaje?
BINTI: Usijari mpenzi, chukulia kawaida tu.
Baada ya simu kukatika, Dah nilikaa nikawaza na kuwazua nikaamua kupotezea tu. Nikavaa fastafasta, halafu nikaenda kununua msosi nikachukua na kilimanjaro moja nikashushia ili nilale vizuri. Mara simu ikaita,
BINTI: Mpenzi si nilikukataza wewe kunywa pombe?
MIMI: (Nikiwaza kichwani, majanga haya) mbona mi sijanywa pombe!
BINTI: Nimekuona mpenzi umekunywa bia moja.
MIMI: (Nikashtuka na kuangalia kushoto na kulia), aaah sijui eeeh kwani umejuaje?
BINTI: Fanya yote ila tambua hakuna utalofanya nisijue.
Halafu akakata simu, nikaanza kuwaza tena amejuaje kama nimekunywa? Au kasikia harufu ya pombe kwenye simu. Mara sms ikaingia kwenye simu yangu, kuangalia ni yule binti, sms iliandikwa “usiwaze sana mpenzi”
Nikiwa chumbani nimejiinamia mara demu wangu wa Dar akanipigia simu na kuniambia kuwa nimempotezea siku hizi kwani tangu nimerudi sijaonana nae, sikutaka kuongea mengi ila nikamwambia asijari nitaonana nae tu. Wakati najiandaa kulala binti wa Kitanga naye akanipigia,
BINTI: Mpenzi ulikuwa unaongea na nani kwenye simu?
MIMI: Ni rafiki yangu wa kawaida tu mpenzi.
BINTI: Niambie ukweli tafadhari.
MIMI: Huo ndio ukweli mpenzi.
BINTI: Sawa ila nitakachofanya usinilaumu badae.
MIMI: Jamani mpenzi unataka kufanya nini tena?
BINTI: Si nilikukataza kuongea na wanawake wewe, na kwanini unanidanganya?
MIMI: Aaah samahani mpenzi, sitarudia.
Akakata simu, nikawaza sana bila ya kupata jibu nikaamua kulala tu.
Asubuhi nikashtushwa na simu yake,
BINTI: Mbona hukushusha chandarua usiku?
MIMI: Umejuaje mpenzi? Nilisahau bhana.
BINTI: Usijari mpenzi.
Basi nikaamka na kwenda zangu kuoga, nikarudi na kuvaa ili nijiandae kwenda kwenye mishe zangu. Mara simu ikaita.
BINTI: Mpenzi hiyo tisheti uliyovaa siipendi.
MIMI: (Nikiangalia ile tishirt yangu), umejuaje kama nimevaa tishirt usiyoipenda?
BINTI: Nimejua tu mpenzi, unajua mi nakupenda kwahiyo mambo mengi unayofanya yanakuja kwangu kwa hisia.
MIMI: Asante kwa upendo wako mpenzi basi nitaibadili usijari.
Nikakata simu na kwenda kwenye mishe zangu. Ila nikawaza sana kama yale mambo ni upendo kweli au kuna vitu vya ziada katikati hapa, nikaamua kupotezea na kufanya mambo mengine.
Nikarudi home nikiwa nimejichokea hata nikaona uvivu kwenda kutafuta msosi. Nilipofika nikajilaza kitandani na kujikuta nikipitiwa na usingizi hapo hapo.
Nikaanza kuota nipo sehemu nzuri sana na mchumba angu huyo wa kitanga, tukienjoy na kula raha tu.
Kulivyokucha nikaamka na kwenda kuoga kama kawaida, nakumbuka jana jioni nilikuwa na elfu themanini kwenye wallet, nikaichukua na kuicheki ile pesa nakuta imebaki elfu thelathini nikaanza kujiuliza elfu hamsini imekwenda wapi. Mara yule binti akawa anapiga simu,
BINTI: Mpenzi jana tulienjoy eeh!!
MIMI: Aaaah, eeeh wapi tena?
BINTI: Si ndotoni mpenzi!!
MIMI: Kivipi mpenzi?
BINTI: Yani ndoto uliyoota wewe usiku na mimi nimeota hivyo hivyo.
Akakata simu bado nikawa najiuliza juu ya upotevu wa pesa yangu. Mara akanitumia sms “usijari mpenzi, hiyo pesa tumeitumia ndotoni”
Nikawaza sana juu ya upotevu wa pesa yangu, nikajiuliza inakuwaje mtu ufanye matumizi ya pesa ndotoni? Likanijia wazo kuwa yule binti si mtu wa kawaida. Nikajishauri kwenda kupata ushauri kwa rafiki yangu wa karibu. Wakati natoka kwenye chumba changu kuna sms ikaingia kwenye simu yangu ila nikaipotezea sikuisoma wala nini.
Nikaenda kwenye shughuli zangu, badae nikaenda kwa mshikaji wangu kumweleza kama nilivyowaza. Nikamkuta na tukapiga story mbili tatu badae nikamweleza mambo yote.
MIMI: Ndio hivyo bhana.
RAFIKI: Aaah pole sana mshikaji wangu ila nilikwambia kuwa makini na Tanga, hata hivy usipende kuwatongoza mademu hovyohovyo sehemu yoyote ile.
MIMI: Sasa nishauri ndugu cha kufanya.
RAFIKI: Cha msingi tumtafute mtaalam twende, haya mambo ya kishirikina kaka.
MIMI: Dah umenitisha kaka hata kurudi kwangu naogopa.
RAFIKI: Usiogope wangu, wee nenda tu ukiogopa atakushtukia mapema.
MIMI: Dah sijui kama nitalala leo kaka.
RAFIKI: Usijari kaka, cha msingi potezea kama hujui kitu vile halafu kesho twende kwa mtaalam kaka.
MIMI: Poa kaka nashukuru maana nishapagawa hapa.
Tukaagana pale halafu nikarudi kwangu.
Nikiwa chumbani nikachukua simu yangu kuikaguakagua nikakuta missed call kibao na sms moja nikashangaa hata ilikuwaje sikusikia wakati inaita, kumchek aliyekuwa anapiga ni demu wangu wa Dar na ile sms ni kutoka kwa binti wa kitanga, iliandikwa “usijaribu kumweleza yoyote juu ya habari zangu” nikashtuka sana, ni hii sms niliyoipotezea wakati naondoka asubuhi. Mara simu ikaanza kuita, kuangalia ni dada yangu anapiga
MIMI: Hallow dada,
DADA: Mbona umekuwa na akili fupi sana wewe? Unajua matatizo aliyoyapata mchumba ako huku?
MIMI: Kwani kafanyeje tena dada?
DADA: Muda wote amekupigia simu hupokei, mwenzio yupo hoi huku ule ujauzito umetoka.
MIMI: (Hata nilisahau kama demu wangu wa Dar alikuwa na mimba yangu) nini dada mbona sikuelewi?
DADA: Huwezi kunielewa kwa simu, kama unaweza njoo hospitali au njoo nyumbani.
MIMI: Poa dada ngoja nijiandae.
Nikakata simu, nikaenda kuoga na kuvaa fastafasta niondoke, wakati nataka kutoka simu yangu ikaanza kuita, kuitoa na kuiangalia ni yule binti wa kitanga.
BINTI: Unataka kwenda wapi?
MIMI: Aaah hapana siendi popote.
BINTI: (Akacheka kidogo), unataka kwenda wapi?
MIMI: Eeeh aaah nataka kwenda kutafuta chakula.
BINTI: Haya rudi kakae, chakula nitakuletea leo.
MIMI: (Huku nikiwa na hofu moyoni), utaniletea kivipi?
BINTI: Kwani shida yako ni chakula au ni nini? Kama ni chakula sasa mashaka ya nini si nimekwambia nitakuletea au?
MIMI: (nikaamua kujigeresha kidogo), aaah Acha utani bhana mpenzi wangu, unajua wazi upo mbali sasa chakula utakiletaje?
BINTI: Nitakileta kwa hisia na utashiba kabisa kwahiyo usitoke.
Akakata simu, nikaanza kuwaza itakuwaje sasa na vipi kuhusu kwenda hospitali nikawaza cha kufanya, au niende halafu akipiga nimwambie sijaenda? Bado nikawa na utata moyoni. Nikainuka pale nilipokaa na kujipa moyo kuwa naenda tu hata iweje. Nikaenda mpaka mlangoni ile nataka kufungua mlango tu sms ikaingia kwenye simu yangu, kuangalia ni demu wa kitanga “nimekwambia usitoke”
Nikakosa raha kabisa, nikarudi na kukaa kitandani nikaamua kujilaza nikitafakari, mara sms ikaingia kwenye simu yangu kuangalia ni yule binti wa kitanga “angalia mezani nimekuletea chakula”
Loh nikainuka kama nimepigwa shoti vile, kuangalia naona juisi ya Azam mango na biskuti, nikawaza kuwa ameletaje vitu vile nikaanza kupata mashaka, mara sms nyingine ikaingia
“usiogope mpenzi, kula tu”
Nilikosa amani kwakweli, nikasogelea ile juisi na kuiangalia kama ni juisi kweli ndio ilikuwa Azam mango kabisa na ndio juisi niipendayo, mmh nikaziangalia na zile biskuti zilikuwa biskuti za ukweli kabisa zile zenye mchanganyiko wa chokleti, kutokana na njaa yangu nikaanza kuvifakamia huku bado niliwaza ameletajeletaje.
Nilipomaliza tu, akapiga simu.
BINTI: Vipi mpenzi umeshiba?
MIMI: Ndio nimeshiba, kwani umeviletaje?
BINTI: Hata kushukuru hujui?
MIMI: Samahani mpenzi nilijisahau.
Akakata simu, nikakaa na mawazo pale kitandani. Mara simu ikaita kuangalia ni dada anapiga tena.
DADA: Vipi wewe yani huna hata hofu na mwenzio?
MIMI: Aaah dada samahani.
DADA: Kwahiyo unakuja au huji?
MIMI: Aaah sijui dada.
DADA: Hujui nini? Nipe jibu moja, unakuja au huji?
MIMI: Sitaweza kuja kwa leo dada, nitakuja kesho.
DADA: Nilijua tu, mxyuuuu (akanisonya na kukata simu).
Nikawa pale kitandani nimejiinamia tu huku kichwani mawazo mengi yamenitawala, mara sms ikaingia kwenye simu yangu
“si ulale mpenzi wangu jamani”
Nikaamua kujilaza huku nikijiona bonge la boya maana nipo kama vile mtu anayeongozwa na rimote.
Mara usingizi ukanipitia pale kitandani, nililala hadi nikajisahau nikaja kushtushwa na mlio wa simu.
RAFIKI: Vipi kaka mbona leo hujatokea maeneo?
MIMI: Kivipi ndugu wakati ndo kumekucha!
RAFIKI: (huku akinicheka), kumekucha wakati saa kumi na moja jioni hii?
MIMI: (nikafungua pazia na kuchungulia dirishani, kumbe kijua cha jioni ndio kipo ukingoni), acha masikhara bhana saa mbili hii (huku nikiangalia saa yangu ya ukutani).
RAFIKI: (Akinicheka tena), wee boya saa kumi na moja hii labda kama leo una kazi ya ulinzi ndio mida ya kujiandaa hii (akinicheka tena).
MIMI: (Nikiangalia vizuri ile saa ya ukutani, iliyoonyesha mshale mdogo kwenye tano na mkubwa kwenye nane), daah nilichanganya mida kaka.
Nikakata simu na kuanza kuwaza imekuwaje nimelala hadi kujisahau vile, ni usingizi wa namna gani ulinipata dah!! Mara rafiki yangu akaanza kupiga tena.
RAFIKI: Kaka, vipi ule mpango wa kwenda kwa mtaalam au umepotezea?
MIMI: Hapana sijapotezea kaka, nataka sana unipeleke itakuwaje sasa?
RAFIKI: Wewe tu, nilitaka nikupeleke leo au unaona yale majanga yako ya kawaida kaka?
Kabla sijamjibu simu ikakatika, na kuanza kuita tena kuangalia ni binti wa kitanga.
BINTI: Ulikuwa unaongea na nani?
MIMI: Rafiki tu mpenzi wangu.
BINTI: Ulikuwa unaongea nae kuhusu nini?
MIMI: Hamna kitu ni salamu tu.
BINTI: Unanificha sio?
MIMI: Hapana sijakuficha huo ndio ukweli.
BINTI: Wee ni muongo eeh!! Haya njia ya muongo fupi na mi naijua.
Akakata simu, nikabaki kwenye maswali na viulizo vya kila aina. Kwanza nikawaza juu ya usingizi niliolala hadi kusahau kuamka kwenda popote pia kusahau kula. Nikajiuliza inamaana sijala chochote tangu nilipokula juisi na biskuti usiku. Mara sms ikaingia,
“usijari mpenzi kula na kuoga na vyote vya muhimu umefanya ndotoni”
Aaah majanga haya!!
Sehemu Ya 2
Nikabaki nimeduwaa tu na macho yamenitoka hata nisijue cha kufanya kwa wakati ule. Nikaamua kuinuka pale kitandani na kujinyoosha nyoosha ila cha kunishangaza sikuwa na njaa kabisa.
Nikawa nimesimama huku nikitafakari yale majanga, mara simu yangu ikaita,
RAFIKI: Vipi wewe mbona umenikatia simu bhana?
MIMI: Hapana sijakata, imejikata yenyewe.
RAFIKI: Halafu wewe naona akili yako imepinda. Haya vipi itakuwaje, nikupitie kesho asubuhi?
MIMI: (nikiwa bado sijiamini amini kama siku imeisha kweli), aaah eeh haya poa basi.
RAFIKI: Mbona hueleweki unajiumauma tu, au hutaki? Niambie bhana.
MIMI: Hapana sio kama sitaki.
RAFIKI: Ila nini sasa? Ongea bhana mtoto wa kiume acha kujiumauma hapo.
MIMI: Aah sijui bhana
Nikajikuta nimekata ile simu, hata nilikuwa sijielewi kabisa. Mara dada akawa anapiga
DADA: Yani mdogo wangu siku hizi kweli umekuwa shetani, toka asubuhi hadi muda huu unashindwa hata kutujulia hali? Yaonyesha umefurahishwa sana na yaliyo mpata mwenzio.
MIMI: Samahani dada, naomba mnisamehe sana sio kusudio langu.
DADA: Ila ni kusudio la nani?
MIMI: Sijui dada.
DADA: Hivi wewe una kichaa au?
Nikakata simu kwani naona wananichanganya tu na wakati sijielewi kabisa.
Nikakaa chini na kujiinamia huku nikipanga mipango kuwa niondoke mahali hapo hata nikalale nje ili nisipitilize tena. Mara simu ikaita,
BINTI: Mambo mpenzi, nimekumiss.
MIMI: (hapo natamani hata kumtukana), poa tu hata nami nimekumiss pia.
BINTI: Unaonaje leo twende tukatembee mpenzi?
MIMI: (huku nimejawa na hasira), unajua usinichanganye wewe! Tukatembee vipi wakati tuko mbali mbali?
BINTI: Ndio unanikaripia eeh!
MIMI: (Nikawa mpole tena), hapana mpenzi nisamehe.
BINTI: Sijazoea kukaripiwa, umeniudhi sana.
Akakata simu, dah nikapagawa zaidi. Nikainuka tena na kwenda hadi mlangoni ili nifungue mlango nitoke. Mara simu ikaita,
BINTI: Unaenda wapi?
MIMI: Aaaah eeeh mmh!
BINTI: Unakwenda wapi?
MIMI: Aah maswali gani tena hayo?
BINTI: Wewe kiburi eeh!
MIMI: (nikiwa na hasira na mimi), niache bhana nikapunge upepo nje.
BINTI: Kumbe wewe ni kiburi na jeuri!!
MIMI: Ndio mambo gani hayo jamani mpenzi?
Akakata simu, nikiwa bado nimesimama pale mlangoni akanitumia sms
“huendi popote”
Nikajikuta nikiwaza mambo mengi, mara dada akaanza kupiga tena.
DADA: Vipi na leo unakuja au huji?
MIMI: Aaah daah sijui bhana.
DADA: Hivi mdogo wangu una nini wewe?
MIMI: Sielewi kitu dada.
DADA: Uko wapi sasa hivi?
Ile nataka kumjibu simu ikakatika, kuichek eti imeisha chaji nikaamua kwenda kuichomeka kwenye chaji, huku mawazo mengi kichwani yakiwa yamenitawala. Nilipokaa kidogo nikaiwasha tena na hapo nikakutana na sms kutoka kwa binti wa kitanga,
“nimekwambia leo huendi popote, utakula jeuri yako”
Nilikosa raha kwakweli nikatamani hata nipae niondokane na hayo majanga. Nikajiuliza kuwa huyu binti ana mamlaka gani ya kunizuia mimi nisitoke? Nikajipa moyo na kujipigapiga kifuani huku nikisema, mimi kidume bhana nitatoka tu. Mara akanipigia simu tena, nikaitoa pale kwenye chaji na kupokea.
BINTI: Unasemaje mpenzi?
MIMI: Mbona sijasema chochote.
BINTI: (Akacheka sana halafu akakata simu).
Nikaamua kuirudisha simu kwenye chaji, huku kichwa changu kikiwa kama kimevurugika.
Nikainuka na kwenda kufungua mlango ila ukawa mgumu kufunguka, nikasikia mlio wa sms nikarudi kuisoma,
“hivi nilivyokwambia kuwa leo huendi popote ulijua masikhara?”
Nikaiangalia ile sms mara tatu tatu, nikaona huyu mwanamke anacheza na akili yangu sasa. Nikiwa nimejawa hasira nikachukua simu na kumpigia ila haikupokelewa, nikapiga tena haikupokelewa na tangu nimerudi Dar huyu binti amekuwa na kawaida ya kutokupokea simu zangu. Nikachukia sana, hasira zikanizidi. Nikainuka tena kwa hasira nikaenda mlangoni na kuusukuma mlango lakini haukufunguka. Nikawa nimepatwa na joto la hasira huku jasho jingi likinitoka, nikarudi na kukaa kitandani mara sms ikaingia kwenye simu,
“pole kwa joto mpenzi”
Nikazidi kupandwa na hasira hata nisijue cha kufanya, nikachukua tena simu ili nimpigie rafiki yangu kabla sijapiga simu yangu ikaanza kuita.
BINTI: Unataka kumpigia nani?
MIMI: Nimekupigia simu hujapokea ila nikitaka kumpigia mtu ndio unajua?
BINTI: Nijibu kwanza unataka kumpigia nani?
MIMI: Rafiki yangu tu.
BINTI: Ulitaka kumwambia nini?
MIMI: (Nikiwa na hasira), unajua nimechoshwa na maswali yako?
BINTI: Umechoshwa na maswali sasa ulipokuwa unanipigia ulitaka nini?
Akakata simu, dah huyu binti nilitamani hata kumtukana matusi yote ya dunia.
Njaa ikanianza, nikawa nawaza sasa nitatoka vipi kwenda kununua chakula. Simu ikaita,
BINTI: Vipi una njaa eeh!!
MIMI: (Hapo natamani kumtukana), unauliza majibu?
BINTI: Kwahiyo unatakaje?
MIMI: Nataka kwenda nje kununua chakula.
BINTI: Leo hutoki ila chakula nitakuletea.
MIMI: Dah!! Kwanini unanifanyia hivyo lakini?
Akakata simu, nikawa ni mtu mwenye mawazo. Nikainuka tena na kwenda kufungua mlango bado ulikuwa mgumu, mara dada nae akaanza kupiga simu
DADA: Uko wapi lakini? Si ulisema utakuja leo yani huwezi amini mwenzio kazidiwa vibaya sana huku.
MIMI: (nikajikuta naropoka tu), Sasa jamani dada, kwani mi ndio daktari?
DADA: Unasemaje wewe?
MIMI: Aah samahani dada ulimi umeteleza.
DADA: Endelea na hiyo tabia yako tu.
Akakata simu. Nikawaza sana kuwa imekuwaje hadi nimemjibu dada vile. Mara sms ikaingia
“umemjibu vizuri sasa dada yako, hongera mpenzi”
Aah nikazidi kupatwa na hasira, mara akanipigia simu
BINTI: Nikuletee chakula gani leo mpenzi wangu?
MIMI: Niletee chakula kizuri cha kushiba.
BINTI: Haya usijari, nitakuletea mpenzi.
Akakata simu nikashangaa imekuwaje hata nikamjibu vizuri vile wakati nina hasira nae.
Nikawa bado na mawazo nikaona sms kwenye simu,
“angalia mezani mpenzi”
kuangalia, dah kaniwekea vyakula vya kila aina, kutokana na njaa yangu uroho ukanijaa. Nikasogea pale mezani na kuanza kula, nilipomaliza akanipigia simu.
BINTI: Hata kunikaribisha mpenzi?
MIMI: Aah mmh nilisahau mpenzi, samahani.
BINTI: Usijari sana, vipi umeridhika nacho lakini?
MIMI: Ndio nimeridhika mpenzi, ila umekiletaje?
BINTI: Nimekileta kwa hisia mpenzi, vipi unataka kuoga?
MIMI: Ndio nataka kuoga mpenzi.
BINTI: Haya ngoja kidogo mpenzi.
Akakata simu, Nikawa kama mtu aliyepigwa bumbuwazi nilikuwa nikingoja huko kuoga kwa hisia nako kutakuwaje.
Nikawaza pale ndani huku nikingoja huko kuoga kwa hisia.
Mara akanipigia simu,
BINTI: Mpenzi upo tayari kuoga?
MIMI: Ndio mpenzi nipo tayari.
BINTI: Haya vua nguo zako zote.
Akakata simu, hofu kubwa ikanitanda moyoni nikawaza kama nivue kweli nguo au la, nikiwa bado naendelea kuwaza akanitumia sms “vua basi ukaoge mpenzi”
Bado nikawa nawaza tu, akanipigia simu
BINTI: Kwani unaogopa nini mpenzi?
MIMI: Hapana siogopi kitu ila naomba kesho ndio nioge kwa hisia mpenzi.
BINTI: (Akacheka sana), kwanini umeghairi mpenzi?
MIMI: Hapana mpenzi ila sijajisikia kuoga usiku huu.
BINTI: Haya usijari mpenzi.
Akakata simu, nikawa nimekaa huku nikipanga mipango ya kesho tu kwenye kichwa changu.
Nikiwa ndani ya mawazo rafiki yangu akinipigia tena simu,
RAFIKI: Kesho nitakuja kukufata hapo kaka twende ile sehemu.
MIMI: Poa kaka.
Alipokata tu simu nyingine ikaingia
BINTI: Mwambie huyo rafiki yako aache kabisa kujihusisha na mambo haya atapotea.
MIMI: Mbona sikuelewi?
Akakata simu, nikazidi kupagawa kwa mawazo hata nisijue cha kufanya kwa wakati huo. Mara taa ya chumbani kwangu ikazimwa kukawa na giza na utulivu uliopitiliza, nikaanza kuogopa huku nikitamani kupiga kelele lakini nikashindwa kufanya hivyo nilikiona chumba kikiwa kikubwa sana, jasho la uwoga likaanza kunitoka nililowa mwili mzima kama nimemwagiwa maji. Mara taa ikawashwa tena na simu ikaanza kuita,
BINTI: Kumbe wewe ni muoga sana eeh!
MIMI: Aaah mmh kiasi tu sio sana.
BINTI: Kukuzimia taa tu jasho limekutoka kama unakimbizwa, nikikufanyia mengine je?
MIMI: hapana usinifanyie vibaya mpenzi.
Akakata simu na kupiga tena,
BINTI: Ooh mpenzi nimesahau, je utapenda tukatembee leo?
MIMI: Aah hapana mpenzi, tutaenda siku nyingine.
BINTI: Kwanini jamani mpenzi?
MIMI: Hamna sababu mpenzi ila tutaenda siku nyingine. Naomba kesho uniamshe mpenzi.
BINTI: Sawa usijari, umekuwa muelewa sasa mpenzi nimefurahi. Ila nakuomba tukatembee.
Akakata simu ilinibidi niwe mpole na nijifanye kuwa nafurahia vyote anavyonifanyia huku akili yangu kichwani ikiwaza mambo mbali mbali ikiwemo namna ya kumuepuka binti huyo.
Nilikuwa nikijigeuza geuza tu pale kitandani huku mawazo mengi yakinitawala.
Mara simu yangu ikaita,
BINTI: Mpenzi leo hulali?
MIMI: Nitalala tu mpenzi si utanishushia neti?
BINTI: Dah nafurahi umenikubali mpenzi, nitakushushia usijari.
Akakata simu, nami nikajilaza pale kitandani. Nikaota ndoto kuwa nipo sehemu nzuri sana na yule binti.
Asubuhi kulipokucha, yeye akawa wa kwanza kunipigia simu. Nikaamka na kwenda kuoga nikarudi na kujiandaa ili nitoke, mara dada akaanza kunipigia,
DADA: Mdogo wangu tafadhari tunahitaji pesa kidogo kwaajili ya kuongezea kulipia hospital na vitu vingine.
MIMI: Hakuna shida dada, kwani mnataka kiasi gani?
DADA: Ungetuma kama elfu thelathini hivi.
MIMI: Sawa natuma sasa hivi kwa njia ya simu.
Nikakata simu na kuanza kutuma pesa, nikafata muamala mzima ila badae naletewa sms kuwa salio halitoshi kuhamisha kiasi cha pesa ninachotaka.
Nikaamua kuangalia salio duh nikakuta eti imebaki mia tano. Nikajisemea ‘hata sikubali hawa wendawazimu washaniibia hela yangu kwenye simu yani laki mbili na nusu imebaki mia tano sikubali lazima niwafatie huko makao makuu
nilikuwa naongea kwa jazba huku nikiangalia lile salio mara mbili mbili bila hata ya kuamini kama hela yangu imekatwa na mtandao kama kawaida ya wizi wao au ni vipi.
Nikaanza kutoka ndani nikiwa na jazba za mtandao ule, mara akanipigia simu
BINTI: Mbona una hasira sana mpenzi?
MIMI: Si hawa wapumbavu wa mtandao wameniibia pesa yangu.
BINTI: Hawajakuibia bhana.
MIMI: Kama hawajaniibia pesa yangu yote imekwenda wapi?
BINTI: Ngoja nitakwambia.
Akakata simu, nikiwa bado nimesimama pale mlangoni huku nina uchungu na hasira ya pesa yangu, mara akanitumia sms
“mpenzi, ulivyoshinda ndani jana na juzi ulifikiri unahudumiwa kwa pesa ya nani? Na tulipoenda kutembea usiku je? Pesa yako imetumika kwenye kukuhudumia kwahiyo usilaumu mtandao, hiyo pesa umeitumia mwenyewe”
INAENDELEA

