Mwili wa rafiki yangu uliokotwa kando mwa bahari Kifua chake na tumbo lake likiwa limepasuliwa viungo vikiwa vimetolewa
Chapter 2
Nikarudi zangu nyumbani watoto wangu niwakubwa kwaiyo wanajielewa na sitawazungumzia basi nipo nakale katoto ka mwaka na miezi kazaa kalibia miwili sasa Kesho yake asubuhi nikampigia simu nikaona haipatikani niliwaza nisema kwaiy mpk saivi kakaa anafanya nini huko maana sasa ilinilazimu nisiende kufungua genge langu siku ya 4 nikaona hapana hii sio Hari ya kawaida nikaenda kwao teali walikua wananijua nako pia wakaniambia kuwa hayupo toka jumamosi tulipo kuja hajawahi kuja na tukipiga simu haipatikani basi nikawaelezea mkasa wote familia ilicharuka sana
Baba yake Alienda kulipoti polisi Alabi sasa basi zilipita wiki Mbili mwili wa rafiki yangu uliokotwa kando mwa bahari ukiwa umepasulia kifuani na tumboni na viungo vikiwa vimetolewa familia ile walilia sana hata mimi pia nililia sana nilihuzunika mno
Msiba uliisha na mtoto nilitaka nimlee mimi ili nilipie deni la mama yake Ila familia ilikataa na wakachukua mtoto wao Ila sikujua kuwa baba yake na binti alieuliwa alibaki na kinyongo moyoni alijiapisha kisasi juu yangu mimi basi bhn siku moja nikiwa nimetoka kwenye mihangaiko yangu baba yule alinivizia usiku wakati narudi nyumbani ilinitandika kisu cha tumbo na kuanza kuniambia na wewe ufe huku akilia kwa uchungu umeniulia mwanangu nimemlea kwa shida umeamua uuze viungo vyake umepata faida gani basi sikuongea chochote nilikua chini pale naugulia maumivu makali ni damu zinatililika tu akaniambia nitafurahi Sana na wewe ukionja kifo akaondoka zake mm nililala pale pale nilikuja kusituka nipo hospital niliokotwa na wasamalia wema namshukuru sana MUNGU afya yangu ilitengamaa na baadae nikaja kupona Ila mbak leo tumbo langu linanisumbua sana kipindi cha baridi huwa nasikia maumivu makali na sikuenda police kwasababu nilimuelewa yule baba sikutaka nilipize kisasi na nilijifunza kitu sasa naombeni nisiendelee maana nimelia mpk nashindwa ku type
Lai yangu kama mmekutana mtandaoni akikuahidi mkutane kuwa makini mwambie akufate ulipo wewe na kama utamfata wewe hakikisha ni seemu ambayo hajaikusudia yaani kama kasema ni mbezi basi muambie njoo tegeta walionielewa wataelewa namaanisha nini
MWISHO

