Mwili wa rafiki yangu uliokotwa kando mwa bahari Kifua chake na tumbo lake likiwa limepasuliwa viungo vikiwa vimetolewa
Chapter 1
Mimi ni single maza nilizalishwa nina watoto wa tatu na wote baba tofauti nisijielezee sana niende na kilichonileta hapa nilikua na rafiki yangu ambae nilimpokea kwenye usingle maza huyu ni rafiki tu ambae tulikutana kwenye bichi nikiwa nimeenda huko kupunga punga upepo kidogo kupoteza mda sasa kuna kwa mbali nilimuona mdada akiwa anauza ukwaju nikamsitua na alikua amembeba mtoto mdogo nikimkadilia kama wa mwaka mmoja na nusu hivi maana mimi pia ni mama nalea so nilijua
Aliniuzia ukwaju chupa moja nikampa elfu 10 hakuwa na chechi akaniambia ananiletea saivi basi nikawa nakunywa mdogo mdogo nilimtazama sana nikajua kabisa huyu tupo njia moja atakuwa kazalishwa bwana kamkimbia aliniletea chechi na hapo sasa ndio ukawa mwanzo wa urafiki kati yangu na yeye tulibadilishana namba pale maisha mengine yaliendelea biashara yangu mimi nilikua nilitafuta pesa kwa kuhangaikia niliweza kujenga genge Ila lakisasa kidogo maana mmezoea kukuta nyanya na vitunguu tu mimi nikali fanya genge kama kaduka hivi nadhani mmeshanielewa hapo sasa
Kwaiyo yule rafiki yangu ambae tulikutana bichi alinitafuta akaniambia dada naomba nionane na wewe Leo nikamuambia Sawa basi nikamuelekeza mpka akafika ofisini kwangu
Nilimpokea pale na alikuja na deli lake la ukwaju akaweka pale nikaona wamechukua chukua pale Mbili tatu huku tukiendelea kupiga stori akasema nimefurahi kufika hapa nikamuambia karibu usiogope maisha na kuhusu mtoto usiwaze Sana dada yako nipo nitasimama na wewe maana sote tushakua single maza tushikane mkono basi pale tulipiga stori tukacheka na kufurahi basi ilifika mida ya kufunga kukawa ni usiku sasa akasema dada mimi leo naomba niwe mgeni wako nitalala kwako japo nakaa na wazazi nitawapigia simu nitawaelewesha Nikamjibu Sawa mdogo wangu kweli mpka nyumban siku ikaisha
Kesho asubuhi alimpigia mama yake nikaongea naye nikamuelezea tulivyo kutana na na tulipo fikia saivi mama yake akaniambia basi kwa sababu mwanangu amelala kwako basi na wewe njoo nyumbani tukuone kweli tulienda mpk kwao mim nitajitambulisha kwao ili hata siku nyingine wasisituke wajue yupo kwangu
Kilichonifanya nisimulie hii story ni hivi rafiki yangu aliamua kuja kukaa kwangu japo siku za jumamosi na Jumapili tulikua tunaenda nyumbani kwao sasa rafiki yangu alipataga mchumba tena kwenye mitandao maana rafiki yangu huyu bado mdogo mdogo kwaiyo mamb ya mitandaoni anapenda sana kujipost post sasa basi alipataga mchumba Instagram wakawa wanazungumza Mala nyingi sana japo mm alinificha baadae alikuja kuniambia sasa walikubaliana wakutane akanishilikisha akaniambia sasa dada huyu mkaka anataka tuonane amesema niende bahari I sasa hivi nikamuambia mmmmh mbona haraka hivo kwa nini msimalize miezi mitatu kwanza umchunguze vizuri ujue kazi yake na pia kwa nini usimwambie aje mkutane hapa kwangu
Ninapo yazungumza haya moyo wangu unaniuma sana Najutia bola ningemuachiaga akakae kwa wazazi wake maybe haya yatokee akiwa kwao na kumbuka ilikua siku ya jumamosi tukiwa tumetoka kwenye ki gege chetu yule mkaka akamtumia elfu 90 akamuambia kanunue chakula basi alinishilikisaha hilo Ila nilimuambia kuwa makini watu wanamna hii wanakuaga na makusudio yao yaani anakupa pesa yote hiii anakujua basi hata nilivyokua namshauli nikama vilikua vinaingia sikio la kushoto vinatokea la kulia pale pale akampigia simu nakuambia mpka tunafika nyumbani ni anaongeaga naye basi nisionekane unaharibu mahusiano ya watu nikatulia Kesho yake sasa asubuhi tu akaniambia dada Nataka nikakutane na mpenzi wangu nikamuuliza yupi akaniambia yule mkaka wa Instagram amenitumia nauli hapa eti kwenda tu apo baharini kanipa elfu50 basi nisindikize dada twende saivi
HUYU mimi nilimchukulia kama mdogo wangu maana nilimuona anateseka na mtoto mgongoni nikamshika mkono sasa kuniambia vile nikamuambia kwanza twende nyumbani kwenu kama tunavofanyaga siku za jumamosi na Jumapili ili mida ya saa 7 umwambie yule kijana aje mpka kwenu sianakupenda atakuja
Hakunielewa kwakweli baadae akaniambia dada unawivu sana au unataka nikuachie nikamuambia tusigombane kwenye kitu ambacho unaweza kwenda mwenyewe basi akanilazimisha San mpka nikamuambia Sawa Ila tusikae sana maana siunajua lazima twende kwenu akaniambia Sawa dada mwenyewe anaruka ruka anafurahia mimi nipo tu namtizama kweli tukaenda baharini mida ya saa 4 hivi kwaiyo kulikuwa hamna watu wengi sana kweli yule mkaka nilimuona wakaanza kusalimiana huku mimi nimembebea mtoto mgongoni nikaona wanaanza kushikanashikana nikaona nisiwahalibie starehe zao nikatoka nikaenda mbali kidogo nikatulia mpk mida ya saa 7 nikaona mbona hanitafuti na tulikubaliana saa 7 hivi twende kwao nikaona niende kuwaangalia kweli sikukuta mtu yoyote piga simu haipatikani nikaona labda wameenda kumalizana so nisiwe na haraka sana ngoja nikaekae mpk mida ya saa 11 nikaona kimya nikazunguka huku na kule si kuwaona nikajisemea huenda wameenda Gesiti
INAENDELEA

