MREMBO JASUSI ALIYEMNASA RAISI KIMAPENZI, NA RAISI AKAMATWA
Chapter 1
Ilikuwa ni miaka ya 90 kuelekea 2000. Pale Liberia kulikuwa na Rais mmoja mbabe sana, anaitwa Charles Taylor. Huyu jamaa alikuwa haambiliki, alikuwa anafadhili vita vya Sierra Leone wapigane wenyewe kwa wenyewe..
CIA walikuwa wanamtamani sana, lakini walikosa njia ya kuingia Ikulu kwake.
Sasa, CIA wakapiga hesabu Huyu mwanaume anapenda sana warembo. Hapo ndipo wakamvuta binti mmoja fundi, mrembo balaa na kichwa chake nihatari, anaitwa Alicia Macy.
Alicia aliingia nchini kama mfanyakazi wa kutoa misaada . Alijua kuvaa, alijua kuongea, na alijua namna ya kumfanya mwanaume yeyote ageuke shingo.
Haikuchukua muda, akajisogeza kwenye duru za karibu na Rais. Siku moja kwenye bonge la party, Charles Taylor akatupa jicho kwa Alicia. Binti akacheza kama yeye, akatupa tabasamu moja la gharama. Taylor akaingia kingi, hakujua kuwa huyo mwanamke ni “sumu” iliyotumwa na Washington.
Alicia akawa mpenzi wa Rais. Alikuwa anakaa naye Ikulu, wanalala kitanda kimoja, na wanakula meza moja. Wakati Taylor anadhani amepata “tunda” la roho yake, Alicia alikuwa anapiga kazi.
INAENDELEA

