GIFT NISHACHAFUA CHUPI MIMI JAMANIIIII AAAAASSSH
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Episode 16
Sauti ya TV ilikuwa muted, sasa wakati nahangaika na simu kwenye TV nikaona inasomwa taarifa ya habari mara nikaona wameonyeshwa wajeda pale kwenye runinga hah…….😳😳😳kuna nini?!…..niliitupa simu pembeni nikakimbilia remote haraka nikaongeza sauti kisha nikatega sikio🫢🫢 taarifa ya habari ilikuwa inawahusu wanajeshi walioko katika kambi aliyopo Ryan 😳😳😳 ilisemekana kuwa kuna sintofahamu imetokea katika hiyo kambi na imepelekea baadhi ya wanajeshi kuuawa💔💔wengine wako mahututi na wengine hawajulikani walipo😳😳😳 sikuwa na ustahimilivu wa kuendelea kuisikiliza ile habari nilizima TV haraka kisha nikasogea Dirishani machozi mengi yakawa yananitoka😭😭😭 nilikuwa namuwaza Ryan atakuwa salama kweli?!…..
Nilisimama dirishani nikalishika tumbo langu nikamwambia mwanangu nina imani baba yako yuko salama atarudi tu kwa ajili yetu😭😭😭wakati ningali bado naendelea kulia kwa maumivu Brighton alirudi kule chumbani akiwa ameshikilia chakula🥺🥺 alishtuka kunikuta ninalia alikiweka kile chakula mezani akakimbia kuja kuniangalia😳😳😳alifunga dirisha haraka kisha akanivuta nirudi nyuma😔😔 mawazo yake yalimtuma kuwa ninataka kujitupa kutoka juu ghorofani😑😑😑 Brighton aliniuliza Gee kwanini unapenda kulia?!.????.😞😞 una matatizo gani?!…..
Sikumjibu chochote nilimuomba tu aniache niondoke😭😭😭 Brighton aliomba nile angalau chakula alichoniandalia kwa sababu tangu asubuhi sijala chochote…..Sikuwa na hamu ya kula chochote nilimwambia aniache mimi sina njaa nilifungua mlango kwa ajili ya kuondoka lakini Brighton alinishika mkono na kunirudisha kule chumbani kwake 😒😒….. niacheeeeeeeeee 🗣️🗣️🗣️ niliongea kwa nguvu na kucha zangu nikawa nimezizamisha kwenye mkono wa Brighton 🫢🫢 nilimtoboa mpaka damu zikaanza kutoka🫢🫢baada ya kuona damu nilimwachia haraka nikarudi nyuma😟😟alianza kupapuliza sehemu nilipomtoboa nilimuonea huruma et🥹 nilimsogelea na kumwambia sorry😔😔 sikutaka kufanya hivyo ni bahati mbaya😣😣 nilipapuliza sehemu alipoumia nikafungua mkoba wangu nikatoa kitambaa nikamfunga ili kuzuia damu zisiendelee kumtoka😩😩 sasa wakati mimi nahangaika kumfanyia Brighton huduma ya kwanza yeye akawa ananiangalia tu usoni kwangu😌😌😌nilimfunga ile sehemu alipoumia baada ya hapo nikamwambia sorry😞 Brighton siyo muongeaji ila anaonekana mwenye hasira za karibu sana😑😑😑 anaonekana mwenye dharau pia☹️☹️☹️ nilipomaliza kumfanyia huduma ya kwanza niliuchukua mkoba wangu nikatoka kule chumbani kwake nikaanza kushuka chini nyumba yake ni ghorofa pazuri hatari🙌🙌 nimeshuka mbio mbio mwenzenu nilipofika chini nataka kufungua mlango nikashangaa naitwa hello Princess🫢🫢🫢niligeuka haraka nikashangaa kuwaona wazazi wa Brighton wakiwa sitting room alafu wote wakawa wananionyesha smile🫢🫢 ina maana wazazi wake wapo🙈🙈🙈 nilishika break ikabidi niende kuwasalimia🫢🫢🫢
baada ya salamu mara kwa nyuma nikamsikia Brighton anawaambia wazazi wake kuwa nimekataa kula chakula chao😳😳😳wazazi wa Brighton waliomba niwe huru kuwepo pale nyumbani kwa Brighton nisiwe na hofu yoyote walituomba tukale chakula kisha tushuke chini kuna maongezi walitaka tuyaongee kabla sijaondoka…..ilibidi tu nirudi sikuwa na namna😑😑😑 tulirudi mpaka flow ya juu nikagoma kuingia chumbani nikabakia sitting room Brighton alikwenda akahamisha chakula akakileta sebleni😑😑kitendo cha yeye kufungua zile hotpot za chakula😑😑😑 kichefu chefu kikaanza🫢🫢🫢kama nilivyokwisha waambia mimba yangu ilikuwa na ubaguzi wa vyakula haswa chakula kilichotiwa viungo nilikuwa nikisikia tu harufu naanza kutapika😩😩😩 ile harufu ikazidi kunichefua nikawa nashindwa wapi nikatapikie😩😩😩 angalau hata ningekuwa na kitambaa ningejiziba pua na mdomo kupunguza ile harufu isinifikie moja kwa moja😑😑😑 kitambaa changu ndo nilikitumia kumfunga Brighton mkononi kwenye kidonda🥲🥲🥲nilihangaika kwenye kiti pakawa hapakaliki nikasimama juu🤣🤣🤣muda wote huo Brighton akawa amesimama tu ananiangalia
Niliteseka mno kujizuia nisitapike lakini wapi😩😩 mwisho wa siku nikaamua kukifunika kile chakula😑😑 nilichukua mifuniko nikafunika zile hotpot Brighton akanishika kwa nguvu akanivuta karibu yake kisha akarudia swali kama aliloniulizaga siku ile kwenye gari are you pregnant,?!niambie hiyo mimba uliyonayo ni ya nani?!……nilikaa kimya😔😔 niliyakumbuka maneno ya baba alinionya nifanye juu chini Brighton asiugundue ujauzito wangu😞😞😞nifanye nini🥲🥲 nilizidi kukaa kimya nikawa namwangalia tu Brighton bila kumjibu chochote😔😔baada ya kukaa kimya Brighton aliniachilia mkono kisha akaniamuru niketi kwenye kiti😒😒😒anapenda kuninyanyasa huyu mbwa🥺🥺🥺ananivuta vuta mpaka nahisi kizungu zungu😩😩 na vile nilivyo na kilo chache alinigeuza kama kitoto chake🤣🤣🤣niliketi kwenye kiti Brighton akazidi kunikata jicho🥲🙌 alishahisi kwa asilimia zote kabisa kuwa mimi ni mjamzito uhakika tu ndo hakuwa nao……alizifungua tena zile hotpot kisha akaanza kunipakulia chakula aiseee nilijikuta tu nishatapika bila kujizuia🙌🙌🙌kumbuka siku hiyo tangu asubuhi sikuwa nimekula kitu chochote niliishia kutapika manjano tupu😣😣😣😣 Brighton alizidi kunishangaa huyu binti ana matatizo gani?!…..
Episode 17
Nilianza kuhisi kizunguzungu kilichonipelekea kukosa nguvu😑😑😑tumbo lilikuwa linauma mno uzalendo ulinishinda nikajikuta naanza kushuka chini😩😩😩kabla sijatua sakafuni mchizi akanidaka🙈🙈🙈 nilitua kifuani mwake nikawa naona maluwe luwe tu🤣🤣🤣kwa kile kizunguzungu si nikaanza kuona nyumba ni kama vile inazunguka lol🤣🤣 Brighton alinikagua muno maskini ya Mungu alinihurumia mpaka machozi yakamtoka😑😑 alinibeba akanirudisha chumbani kwake akanilaza kitandani🥲🥲🥲 aliniuliza kwa upole Babe nini kinakusumbua niambie basi mimi ni mwanaume I promise you nitakusaidia kupata ufumbuzi wa kile kinachokutatiza🥹🥹🥹can you talk to me please 🙏😢 nilimwangalia sana Brighton kisha nikaanza kulia😭😭😭nilimwambia huwezi kunisaidia we niache tu Dunia iniandame😭😭 Brighton alizidi kunionea huruma aliendelea kuniomba niongee chochote nachojisikia kuongea😭😭😭mi nikawa nalia tu make najua nikimwambia kile anachotaka nimwambie sijui kama yuko tayari kukisikiliza🥲🥲🥲
Alinifuta machozi akanibembeleza mpaka nikanyamaza aliniuliza kipi najisikia kula nikamwambia akaniagizia kilipoletwa chakula nilichoagiza nilikula vizuri bila shida wala kutapika😑😑😑 Brighton alinihoji kwanini unabagua chakula?!….hiyo hali uliyonayo mara nyingi wanakuwaga nayo wajawazito why you?!….Kila alipolizungumzia swala la ujauzito🥲🥲 mie nilibakia kimya tu😔😔mimba ni kweli ninayo sikuona kama kuna umuhimu wa kubishana juu ya hilo😔😔😔muda ulizidi kwenda nilimuomba Brighton twende tukazungumze na wazazi wake haraka ili niweze kuondoka nirudi nyumbani mapema……nilitaka niondoke pale ili niweze kwenda kufuatilia habari juu ya boy Friend wangu Ryan🥺🥺 tuliongozana mimi na Brighton hadi chini kwa wazazi wake tuliwakuta wameketi zao wanabebishana tukajiunga nao…..walipotuona walitusifia na kutuambia kuwa tunapendeza kuwa pamoja na tunaendana sana……niliishia kusmile kinafiki tu😒😒😒ukweli ni kwamba moyo wangu haukuwahi kumridhia mtoto wao hata siku moja na vile alivyo mbabe kila muda kunikunja kunja kwa hasira ndo kabisa najikuta nashindwa kumzoea🥲🥲 niliketi pembezoni mwa Brighton naye kwa mahaba akauhandle mkono wangu ubavuni mwake kisha tukatulizana kuwasikiliza wazazi……
Wazazi wa Brighton walikuwa wanatutaarifu juu ya ndoa yetu ambayo walipendelea ifanyike haraka kabla ya wao kurudi makazini kwao huko nchini China🥲🥲🥲habari za ndoa zilinishtua mno🥺🥺 sikuwa tayari hata kidogo🥲🥲😑 nilijikuta nimeropoka mbona mmeiwahisha sana hii ndoa???!!!! Wote wakashikwa na mshituko😳😳😳ina maana hamko tayari?!.????? Walihoji wazazi wa Brighton…..Brighton alinigeukia akanitizama na kuniuliza are you ready?!….. nilitikisa kichwa bila kusema chochote😞😞 wazazi muda wote waliokuwa pale sebleni kumbe walikuwa busy kupanga mipango ya harusi yetu😳😳😳tayari walishaweka oda ya ukumbi na tayari walikuwa wameshawatafuta wana mitindo wa kudizaini nguo zetu za harusi tutakazozichagua😳😳😳ndoa yetu ilipangwa kuhudhuriwa na watu wachache tu, wanafamilia, ndugu jamaa na marafiki😩😩…..ilipangwa kufanyika classic wedding yenye watu wasiozidi 50☹️☹️…..mama yake Brighton alitusogelea akiwa na laptop yake mkononi muda wote alikuwa busy kuandaa harusi ya kijana wake walitaka iwe harusi ya kifahari mno kumbuka Brighton ndo mtoto pekee kwa wazazi wake…… mama Brighton alituonyesha ukumbi wa kifahari ambako itafanyika sherehe ya ndoa yetu akatuonyesha na dizaini mbalimbali za mavazi mazuri yatayofaa kuvaliwa kwenye harusi yetu……
Nilizidi kushangaa na kujiuliza what can I do???? Tulipatiwa tarehe zilizopendekezwa pia ili tuweze kuchagua moja tuitakayo sisi🥺🥺🥺baada ya mambo yote hayo kuwekwa wazi mezani Brighton aliwaomba wazazi wake watupatie muda wa kuchagua vile tutakavyovipenda then tutawapa majibu……..sikuwa na la ziada pale nyumbani kwa Brighton niliwaaga wazazi wake tukatoka…..tulipofika nje Brighton aliniomba nipande kwenye gari anirudishe nyumbani nikamwambia siendi nyumbani🥺🥺🥺niache tu niondoke peke yangu kuna sehemu nataka kwenda peke yangu🥹🥹 wakati naongea hivyo na machozi yakawa yananilenga kilichokuwa kinanitesa ni zile habari za fujo zilizotokea kwenye kambi ya kijeshi aliyopo mchumba wangu Ryan 😭 Brighton aliniambia popote unapotaka kwenda nitakupeleka! Panda kwenye gari tuondoke🗣️…… nilikuwa mbishi kupanda kwenye gari Brighton alinibeba kwa nguvu akaniingiza kwenye gari kisha akalock milango akaondoa gari🥺🥺aliuliza wapi napotaka kwenda nikamwambia ninataka kwenda kanisani😔😔😔 kanisa gani nikamtajia akaondoa gari……
Wakati tulipokuwa njiani kuelekea kanisani simu yangu ilianza kuita alinipigia rafiki yangu Brinnah nilipokea haraka na kuiweka sikioni kisha nikaita helloo bestie 😔😔 sauti ya Brinnah ilinishtua alikuwa anaongea kama mtu anayelia😳😳😳 aliuliza niko wapi alihitaji kuniona yeye bado alikuwa yuko kazini alikuwa hajaondoka bado ilibidi nimuombe Brighton ageuze gari tuelekee kazini kwanza nikamuone Brinnah…..tulipofika jirani na pale kazini kwangu Brighton alizuiliwa kuingia akabaki nje nikaingia ndani peke yangu niliwakuta wajeda wengi sana pale kambini kila mmoja niliyekutana alikuwa katawaliwa na sura ya simanzi😭😭😭 kabla ya yote nami nikajikuta tu naanza kulia😭😭mwili wangu ulikuwa unapata msisimko wa kutisha sana….. niliienda hadi sehemu aliponielekeza Brinnah nikamkuta kajikunyata peke yake anaangua kilio kisichoelezeka😭😭😭aliponiona alinikimbilia akanihug kwa nguvu🥺🥺kisha akaiwasha simu yake na kunionyesha zile taarifa za kuhusiana na wale wajeda waliofariki huko katika kambi ya kina Ryan kabla sijaishika ile simu nilihisi ni kama miguu inaishiwa nguvu nikakaa chini pressure ikaanza kupanda na kushuka machozi mengi mno yakawa yananishuka bila kipimo🙌🙌 niliipokea ile simu nilipoicheki nikayaona yameorodheshwa majina ya wanajeshi waliouwawa🥲🥲 nilianza kuyasoma yale majina haraka haraka huku moyoni nikiwa naomba jina la Ryan lisiwemo🥹🥹🥹
Je Ryan yuko hai au naye kaishatangulia mbele za haki,!?????
Episode 18
Nilisoma kwa mtiririko kuanzia mwanzo bila kuliona jina la baby dady wangu Ryan🥹🥹🥹nilijipa moyo na matumaini ya kwamba huenda jina lake likawa halipo katika idadi ya wanajeshi waliouwawa💔💔 niliendelea kuyasoma majina machache yaliyobakia jina la pili kutokea mwisho lilikuwa ni jina la mwanaume wangu Ryan 😭😭😭 nilipoliona jina la Ryan niliitupa ile simu chini kisha nikaanza kulia kwa sauti na kuita Ryaaaaaaaaaaaaaaaaaan💔💔💔💔💔💔💔💔💔💔 watu waliokuwa jirani walikimbia kuja kunishika na kuniinua kutoka chini😭😭😭😭😭sikutaka kushikwa na mtu yoyote kila aliyenisogelea nilikuwa namsukuma na kuomba wakae mbali na mimi😭😭nilichanganyikiwa💔💔siku hiyo nilitamani hata kujiua sikuona kama kuna umuhimu wowote wa mimi kuishi bila Ryan😭😭😭nililia mno niliumia mno💔💔rafiki yangu Brinnah alinikumbatia kwa mara nyingine kisha akaniambia haya ni majina tu mimi nina imani Ryan hawezi kuondoka akakuacha peke yako cha kufanya let’s go and pray for him🙏🙏🙏 Brinnah alinishika mkono hadi lilipo gari lake tukapanda kwenye gari tukaondoka kwenda kanisani😩😩😩 tulifika kanisani usiku mida ya saa mbili tukaweka sadaka zetu madhabahuni kisha tukasujudu na kuanza kusali😭😭😭😭tulimlilia mno Mungu🙏🙏🙏tulisali bila kuchoka kwa masaa yasiyopungua mawili baada ya hapo tulitoka kanisani tukarudi kwenye gari…….
Brinnah aliniomba tuondoke wote kwenda nyumbani kwao nikishakaa sawa nitarudi nyumbani kwetu…… niliona ni sawa tu kwa sababu nyumbani kwetu napo baba yangu alishaanza kuniletea noma….wakati tulipokuwa njiani kuelekea nyumbani kwao na Brinnah si ndo nikamkumbuka Brighton nilipomuacha😩😩😩nilichukua simu haraka ili niweze kumtaarifu aondoke asinisubilia coz tyr nishatoka……nilipoishika simu nilikuta missed call zaidi ya 50🤣🤣🤣zote za Brighton🥲🥲🥲nilimtumia msg nikamwambia I have already left, don’t wait for me😌😌 aliuliza uko wapi?! Umeondoka na nani? Kwanini uondoke bila kunitaarifu🥺🥺🥺 this time nilitaka tupange mipango juu ya ndoa yetu but I see like kuna kitu unanificha Gee☺️☺️☺️ Brighton alianza kunilalamikia na kuniamrisha nimwambie sehemu nilipo aje kunichukua sikumjibu kitu nilizima simu nikatunza kwenye mkoba😞😞😞 tulienda hadi nyumbani kwa rafiki yangu Brinnah sikutoa taarifa nyumbani kwetu juu ya sehemu nilipo…….usiku huo mimi na Brinnah tulianza kuipiga ile namba ya Ryan lakini bado ikawa haipatikani😭😭😭😭nilizidi kupoteza matumaini juu ya kuonana naye tena🥲 nilihisi ndo nishampoteza💔💔 Brinnah alinishauri tuwatafute ndugu wa Ryan huenda wao wakawa na taarifa zaidi juu ya Ryan…..
Ryan hakubahatikaga kunitambulisha kwa wazazi wake….. wakati aliopanga kunipeleka kwao ndio wakati aliohamishwa na kupelekwa mbali💔💔 taarifa juu ya mahusiano yetu familia yake inajua kila kitu🙏🙏 kilichokuwa kimebakia ni kutambulishwa tu picha zangu walishaonyeshwa wazazi wake na ndugu zake wa karibu na tayari walishayabariki mahusiano yetu🙏🙏🙏kipindi nilipomwambiaga Ryan habari juu ya ujauzito wake aliniunganishaga na mama yake tukawa tunawasiliana na tulikuwa tuko kwenye mipango ya kuonana😔😔 ule usiku nilimpigia mama Ryan simu ikawa inaita tu na kukata bila kupokelewa😭😭😭 alikuja akanipigia ndugu yake Ryan akaniambia mama yao tangu alipopata habari juu ya kifo cha Ryan alipoteza fahamu💔💔💔nilizidi kuchanganyikiwa na kujiuliza ina maana ni kweli Ryan kafariki🥹🥹🥹nilianza kuunganisha matukio ya tangu usiku wa jana baba alipoondoka kwa hasira kwa lengo la kwenda kumuadhibu Ryan au yeye ndo kapanga yote yatokee?!…..sikuweza kuendelea kubakia pale nyumbani kwao na Brinnah nilimuomba anisindikize kwanza nyumbani nikaongee na baba yangu…..usiku mida ya saa sita tuliianza safari kwenda nyumbani kwetu nilimkuta baba yangu na bibi yangu wakiwa wamejawa na wasiwasi sana waliponiona walinikimbilia kuja kuniwow na kuniuliza ni wapi nilikotoka☺️☺️☺️niliwapita nikatangulia ndani na rafiki yangu Brinnah…..
Baba yangu alinifuata nyuma nyuma huku akinihoji maswali mengi…..kuna nini mwanangu umetoka wapi usiku huu?!……Nilimgeukia babangu huku nikiwa nalia😭😭😭kabla sijaongea chochote nilijishikilia🙌🙌🙌 unajua kuna vitu vingine hata watu wako wa karibu hawafai kuvisikia😩😩😩kuna mambo mengine ni ya siri hata Brinnah hakufaa kuyasikia ilibidi nimpeleke Brinnah chumbani kwangu kwanza baada ya hapo nikarudi kuongea na baba…..nilimuuliza baba yangu Daddy why??😭😭 kwanini umeamua kuukatili moyo wangu baba kwaniniiiiiiiiii???😭😭😭 baba wewe ndo umehusika na kifo cha Ryan eh..??? Kipi alichokukosea hadi ukaamua kumlipa ubaya kiasi hiki🧎🏾♀️🧎🏾♀️🧎🏾♀️😭😭 nililia mno mpaka baba yangu akashindwa kunitizama😭😭😭😭 alinigeuzia mgongo kisha akayafuta machozi yake💔 alipoona naendelea kumlaumu alinigeukia akaniambia Gee nilikuonya mapema🥹🥹🥹na ukaniahidi kuwa you will do as we promised each other sikuwa na budi kufanya hiki nilichokifanya☺️☺️☺️kwa hiyo kweli wewe ndo umefanya eeh😭😭💔💔 I hate you Dady💔💔💔nakuchukia😭😭😭hufai kuwa binadamu baba wewe ni mnyamaaaa😭😭😭umemuulia mwanangu baba nani atamlea mtoto wangu💔💔💔 nilimlaumu mno baba yangu hakuonekana kujutia alichoniambia ni mimi nijiandae na ndoa yangu na Brighton…..huo ujauzito kuanzia sasa ni wa Brighton fanya juu chini Brighton asigundue chochote kuhusiana na huo ujauzito kuwa ni wa Ryan😡😡na kuanzia leo sitaki kukuona ukienda kazini wala sehemu yoyote ile mpaka ndoa yako na Ryan ipite😑😑😑😑
Baba alizidi kunionyesha uhalisia wake😳😳😳🙌 niliumia mno lakini sikuwa na cha kumfanya niliishia kulia kwa maumivu makali yasiyoelezeka😭😭😭kila linaponitokea jambo la kuniumiza huwa najifungia chumbani kwangu na picha za mama yangu nalia weeee mpaka nasinzia🥹🥹🥹 angalau siku hiyo nilikuwa na watu wa kunifariji bibi na Brinnah walikesha na mimi mpaka asubuhi…….kulivyokucha tuliongozana nao mpaka makaburini nikaenda kuongea na marehemu mama yangu😭😭😭ilipofika jioni Baba yangu aliniomba nijiandae haraka tutoke sikujua tunakoenda ni wapi nilijiandaa nikamaliza tukaondoka tulienda katika hotel moja huko tukawakuta kina Brighton na wazazi wake😒😒 walikutana kupanga tarehe ya harusi🥹🥹🥹🥹baba yangu alipendekeza harusi ifanyike haraka lengo ilikuwa niolewe kabla ya mimba haijawa kubwa……harusi ilipangwa kufanyika ndani ya hiyo hiyo week😳😳😳bado sikuwa tayari kufunga ndoa na Brighton🥹🥹🥹nilijiuliza kipi nifanye ili kuzuia yote haya?! Nafsi yangu bado ilikuwa inanituma kuwa Ryan wangu yuko hai hajafa 🥹🥹🥹🥹wakati bado naendelea kuwaza namna ya kuizuia ndoa na Brighton niliikumbuka ahadi aliyoniahidi rafiki yangu Brinnah aliniambiaga kuwa kama nisipokuwa tayari kufunga ndoa na Brighton yeye atafanya hivyo kwa ajili yangu😔😔……
Episode 19
Siku moja jioni Brinnah alipotoka kazini alipitia nyumbani kwetu kuja kuniona….. aliniletea na taarifa juu ya mazishi ya wale wanajeshi waliouwawa mojawapo akiwa ni Ryan💔💔….. sasa cha kusikitisha tarehe ya mazishi ya Ryan iliambatana na tarehe ya ndoa yangu na Brighton😳😳……Brinnah alitaka kujua uamuzi juu ya ndoa yangu na Brighton bado sikuwa tayari nilimuomba tuendelee na mipango yetu tuliyokwisha ipanga🥺🥺 alistaajabu akauliza ina maana bado una imani juu ya Ryan?!…. nilimwambia ndiyo bestie mimi nina imani Ryan yuko hai na lazima arudi kwa ajili yangu na mtoto wetu🥹🥹🥹nampenda😭😭😭sizani kama kuna mwanaume mwingine nitakayempenda kama nilivyompenda yeye😔😔 siwezi kumsaliti Ryan……imani yangu ilizidi kunituma kuwa Ryan yuko hai🥹🥹🥹kila nilipoyafunga macho yangu nilimuona yeye tu🧎🏾♀️😔😔 kila niliposinzia nilimuota yeye tu😔😔😔sauti yake ya kuniomba nisije mtenda ilizidi kupenya masikioni mwangu😔😔…..Brinnah bado aliniambia muda na wakati wowote nitakao muhitaji yeye yupo kwa ajili yangu🙏🙏……siku hiyo hiyo ilibidi tuanze kumtafuta dactari wa kumfanyia Brinnah sajali nyieeee😩😩😩
Tulitaka mtu mwenye siri kidogo ambaye hatoweza kuivujisha siri yetu🫢🫢🫢 tulimpata dactari mmoja kutokea nchini uturuki tulipanga kikao naye ila aliomba pesa nyingi sana……alitaka alipiwe nauli ya kutoka uturuki mpaka Sweden akodishiwe hotel malipo ya muda na malipo ya kazi😩😩😩pesa ilikuwa nyingi ilizidi hadi pesa nilizokuwa nazo bank😔😔 Brinnah aliniongezea kiasi kikubwa cha pesa lakini bado hazikutosha….. niliwaza kutoa pesa kwenye account ya Ryan maana card yake ya bank aliniachiaga mimi ili nisipate shida yoyote kipesa🥵🥵…….account ya Ryan ilikuwa na pesa nyingi sana kabla sijaitumia ile pesa nikawaza tumboni nina mtoto ambaye anatarajia kuja Duniani na anahitaji matunzo😔😔sina kazi na baba hajulikani alipo sijui kama kweli yupo hai au ndo kaishatuacha peke yetu😭😭 nafsi iligoma kuitumia ile pesa niliwaza maisha yangu ya mbeleni yanayokuja yanahitaji pesa nyingi maana sijui hata hatma ya maisha yajayo ni ipi😔😔😔 niliwaza kuuza gari aliyoninunuliaga Brighton nikaona nitashitukiwa😩😩😩 cha kufanya ni kumuomba pesa huyo huyo Brighton☹️☹️
Nilimpigia simu Brighton nikamwambia babe I have something I wanna talk to you😔😔😔ile sauti yangu ya upole na huzuni vilimchanganya Brighton hajawahi kunisikia nikimuongeresha kwa kutulia kiasi kile mara zote huwa namsemesha kwa kujilazimisha tu😌😌😌 Brighton alilegea akaniambia anything you want baby just talk to me……nikaanza kufunguka🙈🙈🙈nikamwambia mshikaji baby i need money for some things😔😔 Brighton hakuhoji ah wala be🤣🤣🤣🤣hakuuliza pesa ni za nini wala wataka kupeleka wapi alichoniuliza ni how much do you need darling💋💋💋 nikawa naogopa kumtajia kiasi cha pesa maana ni kiasi kikubwa na nimemshitukiza🤣🤣🤣 ikabidi nianze kuzunguka mbaaaaali mara oh babe but I know nimekushtukiza but kweli nina shida and I need more money to fix😔😔 Brighton akarudia kuniuliza how much you need darling?!
Nikataja kwa sauti ya chini maskini sijawahi kumchuna mtoto wa mtu😩😩 ila sasa nimetaitiwa sina cha kufanya zaidi ya kuchuna baada ya kumtajia akaniuliza wahitaji cash💸 au nikuwekee bank nikamwambia cash itapendeza zaidi……Brighton alimwagiza dreva wake akaniletea hizo pesa😌😌 ni nyingii zilijaa kwenye briefcase😌😌🙌🙌 baada ya kuzipokea sikukumbuka hata kumwambia asante🤣 yani mtu kama humpendi ni humpendi tu🤣🤣🙌 hata akupe nini utachukulia kawaida tu😩😩😩unayempenda akikupa hata pipi tu unajiona wewe ndo unapendwa kuzidi wote😩 ilipopita kama nusu saa hivi Brighton ikabidi anipigie mwenyewe make kaishasubilia hata kimeseji cha asante hajakiona🤣🤣 alipopiga nikapokea yani sikuwa hata nawaza mambo ya kumshukuru😝😝😝nimepokea simu nikaiweka sikioni nikamuuliza vipi😝😝una shida gani😒😒😒 mtoto wa watu akabaki kushangaa hivi huyu ndo nimetoka kumtumia mamillion ya pesa sasa hivi😳😳😳 alf ananiongeresha namna hii hata kiasante cha kujilazimisha hamna🤣🤣 nahisi aliwaza tu hivyo japo hakuongea🤣🤣🤣 alikaa kimya kama sekunde chache akakata simu akaniandikia msg sorry nilitaka kuuliza kama umepokea ulichokihitaji😩😩😩si ndo nikakumbuka kumbe natakiwa kushukuru🤣🤣🤣🙌ikabidi sasa nijiandikishe kimeseji cha kinafiki nikamwambia thanks baby I have received it 😝😝😝😝akanijibu okay baby ukihitaji zaidi nijulishe I love you💘💘💘nikamjibu ok😝😝😝
Baada ya kupata pesa tukaanza kupanga taratibu za sajali😌😌😌 tulituma nauli ya ndege kwa Doctor na nusu ya pesa alizozihitaji akawa amekata tkt ya kuja Sweden 😩😩😩 tulikodi hotel kali ya five star akafikia huko pesa si ipo🤣🤣ilibidi tumuonyeshe Doctor makeke ili asije tudharau akafikiri hatuna pesa akajafanya sajali ya ovyo🤣🤣🤣ila pesa ambayo hujaihangaikia jamani haiumi🤣🤣🙌 baada ya Doctor kuwasili usiku wa manane ikabidi nitoroke tukamwangalie kumbuka siruhusiwi kutoka ninachungwa kama dhahabu😕😕 yote hayo ilimradi nisijetoroka kabla ya ndoa🥵🥵……Tulienda mimi na Brinnah tukafanya kikao na dactari akatushauri kwa siku tulizonazo hazituruhusu kufanya sajali ya kubadili sura 😭😭😭 sajali ya sura inahitaji muda mrefu kidogo mpaka mgonjwa apone vizuri nasisi tulikuwa na siku tano tu😩😩😩kipi tufanye yarab🥹🥹🥹inamaana ndo nimefeli kweli😭😭😭niliangua kilio cha ela yote😩😩😩 dactari aliwaza kitu akatuambia ipo mbinu mbadala ya kuwasaidia lakini inahitaji mkwanja mrefu kidogo…..
Je ni mbinu gani hiyo?!….. unahisi Gift atafanikiwa juu ya hiyo mipango yake?! Zimebaki siku tano tu ndoa yake na Brighton kufungwa dactari kasema sajali haiwezekani ndani ya hizo siku ipi njia mbadala ya kumsaidia Gift?!……
Episode 20
Dactari alituambia ya kwamba uwezekano uliopo wa kunisaidia ni kutengeneza fake skin yenye sura yangu kisha mhusika ataivaa na itaonekana kama ngozi yake na ni ngumu sana kushtukiwa🫢🫢🫢 alitusaidia kututafutia mtaalamu atakayeweza kudizaini hicho kitu tukampata na tukapanga kuonana naye usiku wa siku inayofuata🥲🥲🥲 mnamo majira ya saa 10 za usiku ndiyo mida tuliyomaliza kikao cha siri na dactari tukarudi nyumbani kwa siri bila kushtukiwa🙌🙌🙌 tulijiegesha kitandani asubuhi kama kawaida Brinnah alidamka akajiandaa kwenda kazini mimi nikabaki tu nyumbani nishazuiliwa kwenda kazini hadi ndoa ipite😔😔…..siku hiyo nilifunga kwa ajili ya maombi😔😔😔nilimuomba mwenyezi Mungu anisaidie kile ninachokipanga kiende vile nilivyopanga🙏🙏🙏 niliomba pia maombi maalumu kwa ajili ya mwanaume wangu Ryan😭😭nilimwambia mungu wangu ni wewe ninayekutumainia na imani yangu inanituma kuwa Ryan yuko hai🥹🥹🥹nilimuomba amuweke hai kwa ajili yangu na mtoto😭😭😭 niliomba mno bila kuchoka ilipofika jioni saa moja Brinnah akawasili kutoka kazini tukafungua naye alinisaidia kufunga pamoja na bibi🙏🙏🙏 tulifungua kisha tukaanza kuandaa mazingira ya kuchomoka usiku kwenda kumuona huyo mtu wa kututengenezea hiyo skin fake ya sura yangu kwa ajili ya Brinnah😌😌😌🙌 ilipofika usiku saa nne tulikula Dinner kisha tukapanda chumbani kulala ilipofika saa sita za usiku mida yetu ya kutoroka nyumbani tukaamka tukaanza kujiandaa…..
Baada ya kujiandaa niliufungua mlango wa chumbani kwangu taratibu kwa ajili ya kuchunguza kama baba na bibi wameshalala🫢🫢🫢 nilienda mlangoni kwa bibi nikasikilizia nikaona pako kimyaa nikaanza kupiga hatua kuelekea chumbani kwa baba🚶🏼♀️🚶🏼♀️🚶🏼♀️mara nikaisikia sauti ya tv chini sitting room 😳😳😳ina maana daddy bado yuko sitting room 😳😳😳😳 nilinyata taratibu kwenda kuchungulia nikamuona kweli yupo busy kuandaa card za mwaliko wa harusi😳😳😳😳tunatokaje yarabiii🥹🥹🥹🥹nilirudi chumbani taratibu nikamwambia Brinnah mzee bado hajalala tunafanyaje🙌🙌 tukajadiliana tupitie dirishani mmhhh kuchungulia kutoka juu tulipo mpaka chini ni parefuuuuuu😝😝😝🙌 what should we do😑😑
Tulizidi kupoteza poteza muda mzee naye akawa hatoki kule sebleni🥹🥹 tulifikia muafaka wa kushuka chini kwa kutumia kamba🤣🤣🤣uzuri ni kuwa kila chumba kina kamba kwa ajili ya emergency 🤣🤣🤣 tulifunga ile kamba kwa umakini kisha tukaitupia kwa nje akaanza kushuka Brinnah🙌🙌🙌 alipofika chini nami nikashuka alhamdulilah tuliweza bila kushtukiwa🙏🙏🙏tuliitisha usafiri mpaka hotel walipo wataalam tukaweka kikao tukakubaliana pesa na vile ndo tulikuwa na haraka tulipigwa pesa nyingi sana sikuwa na budi nilichokitaka tu ni kazi yangu itengenezwe kiweredi…..nilifanya malipo nikachukuliwa picha yangu pure itakayotumika kutengenezea hiyo fake skin😌😌😌baada ya hapo tukaambiwa baada ya siku tatu kazi yetu itakuwa tayari….. tulisubilia baada ya siku tatu tukaenda kuaangalia kama tayari tukakuta kweli imetengenezwa fake skin yenye sura yangu piwa🤣🤣 na alipoijaribisha kuivaa Brinnah alionekana kama mimi na vile mwili figure tulikuwa tunalingana sura tu ndo ilikuwa tufauti alivyovaa ile fake skin yenye sura yangu alionekana kama mimi😝😝😝 haikuwa rahisi mtu kugundua hata kwa kushika lbda akichana na kiwembe ndo inaweza kuharibika vinginevyo ni ngumu mno mtu kusanuka ile kitu ilikuwa na mwonekano kama wa ngozi ya binadamu😩😩😩tulimshukuru mungu angalau kawezesha hilo kutimia🙏🙏🙏 tulirudi home na hiyo sura yangu ya mchongo tukaifungia kabatini isubilie siku ya ndoa😔😔😔😔
Usiku wa siku hiyo tulipotoka kuichukua hiyo fake skin sikuweza kulala nilikaa macho mpaka kukakucha😭😭 nilikuwa na mawazo sana kuhusiana na msiba, siku iliyokuwa inafuata ndo ilikuwa siku ya kuwapumzisha hao wajeda waliofariki💔💔💔 swali ambalo bado lilikuwa linaikoroga akili yangu ni kuhusiana na Ryan💔💔hivi ni kweli kabisa naye yumo miongoni mwa hao waliofariki au laa?! Mimi bado sikuwa naamini kuwa Ryan kafariki hadi nitakapomshuhudia kwenye jeneza😭😭😭nilitawaliwa na huzuni usiku kucha kulivyopambazuka siku hiyo ilikuwa weekend Brinnah hakwenda kazini tulitegea hadi pale alipoondoka baba yangu nasi tukajiandaa tukavaa mavazi yaliyofunika sura zetu kisha tukawa tumeondoka kwenda msibani😔😔…..miili yote iliagiwa katika ile kambi nilipokuwa nafanya kazi baada ya kuaga ndo kila familia waliruhusiwa kubeba miili ya wapendwa wao kwenda kuwapumzisha💔💔💔💔 mimi na Brinnah tulipofika kule kambini kwa bahati mbaya tulikuta zoezi la kuaga miili ya marehemu limeshakamilika💔💔hatukubahatika kuziona sura za watu waliofariki…..majeneza yalikuwa mengi sana kila jeneza liliwekewa picha ya mhusika kwa mbele…….
Kati ya yale majeneza yaliyokuwepo pale jeneza moja lilikuwa la mchumba wangu Ryan 😭😭😭nilipoiona picha yake nilishindwa kujizuia nikaanza kulia Brinnah alinivuta mkono tukasogea pembezoni sehemu ambapo hakuna watu akaanza kunifariji kumbuka msibani tumeenda kwa kujiiba tu sikuruhusiwa kupeleka miguu yangu huko….. ilifika hatua ya ndugu kubeba miili ya wapendwa wao nikashuhudia ndugu wa Ryan wakiwa wanasaidiana na wanajeshi wengine kulibeba jeneza la Ryan kuliingiza kwenye gari😭😭😭😭tulielekea haraka sehemu tulipopaki gari tukapanda na kuanza kuifuatilia ile gari iliyoubeba mwili wa Ryan sikuwa napajua kwao tuliwafuata nyuma ili tuweze kupafahamu nyumbani kwao mimi nilikuwa napajua nyumbani kwa Ryan kwao ndo sijawahi kwenda…..gari tuliyotumia ni ya Brinnah haikuwa inajulikana kwa baba wala Brighton……. tulizifuata gari za msafara hadi nyumbani kwao na Ryan 😭😭😭😭 tulibakia kwenye gari tukawa tunafuatilia taratibu zote za ibada baada ya ibada tukatelemka kwenye gari kwa ajili ya kwenda kuupumzisha mwili wa marehemu💔💔💔 sasa wakati watu wakiwa busy kuushusha mwili wa Ryan kaburini mimi nilikuwa kwa mbali nalia na kuyaangaza macho yangu kila sehemu nikawa siamini kile ninachokishuhudia😭😭 kichwani nikawa najihoji maswali sasa kama Ryan kafariki si bora hiyo kesho nije nifunge tu ndoa na Brighton 😭😭😭sa nitafanyaje wakati mwenzangu kaishaniacha💔💔💔wakati bado nikiwa nalia kwa uchungu na maumivu ghafla nilianza kuhisi msisimko wa uwepo wa Ryan kwenye yale maeneo😳😳😳😳nikaanza kuangaza kila kona simuoni nilipogeuka nyuma yangu kwa mbali nikamuona jamaa kama Ryan 😳😳😳 kukaza macho vizuri bwana ni yeye😳😳😳si nikaanza kupiga hatua kumfuata naye ndo akawa anaondoka pale alikuwa kavaa nguo nyeusi na kofia ya kuficha sura😳😳😳😳Ryan😳😳niliita taratibu kisha nikaanza kumkimbilia na kumfuata kwa nyuma🥺
Je itakuwaje?!……
INAENDELEA

