LUCIFER ALINIITA KUZIMU
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Sehemu Ya 6
Baada ya kufanya uchawi huo, nilitoka na kuendelea kufanya mambo yangu huku nikiwa na hasira kufuatia baba mdogo kunipiga bila sababu. Hata hivyo, nilipanga
kumhamisha pale nyumbani baada ya kupita siku sita, kwa upande wa yule kijana ni kweli hakurudi nyumbani na tulipokutana njiani alinichangamkia kwa furaha
kuliko zamani. Nilipomwuliza kwa nini hakupenda kurudi nyumbani, akaishia kucheka na kunieleza kwamba aliamua tu mwenyewe.
Kumtega nilimwuliza kuhusu kuja kuchukua nguo zake, akaniambia alikuwa na zingine, nikajua uchawi wangu ulifanya kazi. Niliishi na baba mdogo kwa chuki hadi
ilipofika siku ya tano ndipo niliamua kumkimbiza pale nyumbani ili nipamiliki.
Usiku wa manane kukiwa kimya muda ambao wachawi huwa huru kufanya mambo yao, niliamka na kutengeneza ulosi kisha nilinuiza kwamba baba mdogo aondoke na
asirudi tena. Nilipomaliza, nilimfuata kiuchawi chumbani kwake na kumuwekea roho ya kuikimbia nyumba yake kisha nikarudi kulala chumbani kwangu. Kulipokucha
niliamka na kumkuta baba mdogo akiwa anaota jua la asubuhi, aliponiona alinichangamkia sana tofauti na siku nyingine tangu tulipokorofishana.
“Kaloli mwanangu umeamka salama?”
Aliponiuliza hivyo nilimwambia nilikuwa mzima wa afya ndipo alinieleza kwamba alihitaji kuzungumza na mimi, nikamwambia sawa. Baba mdogo aliniambia kwamba
nitakapomaliza kazi zangu ndipo tutaongea, nikamwambia hakukuwa na shida. Kama tulivyokubaliana, baada ya kumaliza kazi nilimfuata baba mdogo ambaye siku
hiyo hakwenda shambani ndipo alinifahamisha kwamba alikuwa anataka kuhamia kwao.
Alipotoa kauli hiyo nilifurahi sana kwani nilijua uchawi wangu ulifanya kazi, nikamwuliza kwa nini aliamua kurudi kwao na pale atapaacha na nani! Baba
aliniambia kwamba nyumba na kila kitu kilichokuwepo pale vitakuwa mali yangu, moyoni nikasema; ‘mimi si nilikuambia utaikimbia nyumba yako ukabisha…mimi
ndiyo Kaloli!’ Kumdhihaki nilimchimba anieleze sababu iliyomfanya aondoke, akaniambia alichoka tu kukaa pale hivyo aliamua kwenda kuishi na wazazi wake.
“Hivyo ndivyo nilivyoamua, nikiondoka sitarudi tena hapa…huu mji nimekuachia na hakuna mtu atakayekusumbua,”
Baada ya baba kuniambia hivyo, nilimuuliza alitarajia kuondoka lini, akasema siku iliyofuata asubuhi na mapema. Kauli hiyo ya baba ilinifurahisha sana kwani
nilijua muda wa kujitawala pale nyumbani uliwadia, jioni ilipofika baba aliniita na kuniambia kwamba ilitokea ghafla tu kupachukia sana pale alipokuwa
akiishi.
Nilipomuuliza sababu za kupachukia alisema sijui anapaonaje ni heri arudi akaishi na wazazi wake, nikamwambia ulikuwa uamuzi wa busara.
Siku iliyofuata baba akiwa na furaha aliniaga ambapo nilimsindikiza akaondoka akiwa na begi la nguo tu, huku nyuma nikajisifu kwa kumkomesha. Kukufafanulia
hapo ni kwamba wachawi huwa hawana huruma wanapoamua kumroga mtu, huwa hawajali kama mtu husika ni mzazi au ndugu yake wa damu. Baba alipoondoka kwa furaha
niliyokuwa nayo, nilimchinja kuku kisha nilimchoma na kumla ikiwa ni kujipongeza kwa kumuondoa pale nyumbani kwa sababu ndiye alikuwa kikwazo.
Kwa kuwa nyumba ilikuwa kubwa, siku ya pili nilimtafuta dalali na kumwambia anitafutie wapangaji wanne, ambapo walipatikana watatu. Wapangaji hao wakiume
walikuwa na wake zao ambao walikuwa wazuri sana, baada ya kupita siku mbili yule dalali alimleta dada mmoja mzuri ambaye hakuwa na mume, nikampangisha chumba
kilichobaki. Nilipoishi na wapangaji hao kwa muda wa miezi minne ndipo niliamua nianze kuwawangia usiku, lengo langu lilikuwa ni kuwadhibiti kwa kila kitu.
Mpangaji wa kwanza kumchezea alikuwa wa chumba cha tatu kushoto kutoka nilichokuwa nalala aliyekuwa na mke mdogomdogo mzuri.
Nakumbuka siku hiyo usiku wa manane, niliamka kichawi yaani nikiwa sina nguo mwilini na kuingia katika chumba cha wapangaji hao. Baada ya kuingia niliwakuta
wakiwa wamelala, nilimtia roho ya usingizi yule mwanaume kisha nikambeba na kumlaza chini akiwa hajitambui. Akiwa amelala fofofo, nilipanda kitandani na
kuanza kufanya mapenzi na mkewe hadi niliporidhika ndipo nilimbeba yule mwanaume na kumlaza kitandani kisha nikamtoa ile roho ya usingizi.
Baada ya kufanya hivyo, nilirudi chumbani kwangu nikajilaza kitandani nikiwa mwenye furaha kufuatia kitendo nilichomfanyia yule mke wa mtu. Kwa kuwa usiku
huo nilikuwa na hamu sana ya kula nyama, sikuweza kupata usingizi kabisa, nikaamua kuiita ndege ya kichawi (ungo). Baada ya kufanya hivyo, hazikupita dakika
nyingi nikasikia kitu kimetua sakafuni tii, nilipoangalia niliuona ungo. Usafiri huo ulikuwa na zana zote za kichawi yaani hirizi ya kinga, mafuta, tunguri
na vitu vingine ambavyo wachawi huvitumia kufanya ulosi.
Nikiwa mtupu nilipanda kwenye ndege yangu na kunuiza inipeleke mochwari ya Hospitali ya Rufaa ya Bugando ya jijini Mwanza. Niliuambia ungo huo kwamba
nilihitaji sana kitoweo hivyo uondoke haraka kuelekea Bugando, ndipo ulitokea upepo mkali sana. Ingawa mle ndani tulikuwa watu wengi hakuna aliyesikia upepo
huo ukivuma isipokuwa mimi tu, upepo huo ulifunua paa kwenye kona ungo ukapaa. Kwa kuwa ndege ya kichawi inakwenda kwa kasi ya ajabu, kufumba na kufumbua
ilitua nje ya mochwari ya Bugando.
Baada ya kuteremka niliingia ndani ambapo niliwakuta wachawi wenzangu waliofika pale kwa lengo kama langu, yaani kutafuta kitoweo. Kwa kuwa hatukufahamiana,
tulisalimiana kwa kugonganisha makalio yetu kisha niliwauliza walitokea wapi, mmoja wao akanijibu kwamba katika Kisiwa cha Ukerewe. Mchawi huyo
aliponifahamisha hivyo, nilishukuru ndipo kila mmoja wetu akaanza kuchagua ni maiti gani ilifaa kwa kitoweo.
Sehemu Ya 7
Katika chumba hicho cha kuhifadhia maiti, kulikuwa na maiti za watu wazima, watoto na vikongwe, lakini binafsi nilihitaji maiti ya mwanamke mwenye mimba
ambao nyama yao huwa tamu sana.
Tukiwa bize kutafuta maiti, wahudumu wa chumba hicho walifungua mlango wakaileta maiti ya mwanaume mmoja na kuilaza sakafuni. Wakati wakiilaza maiti hiyo,
hawakuweza kutuona na walipomaliza waliondoka bila kujua kama mle mochwari mlikuwa na wachawi. Baada ya kuondoka, wachawi wawili waliichukua ile maiti na
kuisogeza pembeni kabisa, wakaanza kucheka. Kufuatia kukosa maiti ya mwanamke mwenye mimba, niliamua kupiga darubini yangu wodini kujua kama kulikuwa na
wagonjwa wenye ujauzito waliokuwa maututi.
Baada ya kuangalia wodi ya wazazi nikamuona dada mmoja aliyekuwa hoi, nikamfuata na kusimama mbele yake ambapo nilimtia roho ya mauti, hazikupita dakika tatu
akaaga dunia. Nilichokifanya niliichukua ile maiti kichawi na kuipeleka mochwari kwa wenzangu ambako nilikuta wameondoka na ile maiti ya yule jamaa mnene
aliyekuwa ameletwa punde.
Kwa kuwa nilikuwa nimewasiliana na yule dogo kiongozi wetu ambaye wakati huo alikuwa kwenye kikao na wachawi wengine, alifurahi sana nilipomwambia nimepata
kitoweo akaniambia nikipeleke haraka sana. Baada ya kuniambia hivyo nilizipakiza maiti mbili kwenye ungo yaani ya yule mama mjamzito na ya kijana mmoja kisha
nilinuiza kwamba ungo upae, ukatii. Wachawi wenzangu waliponiona natua walifurahi sana, baada ya kutua niliibeba ile maiti ya mama mwenye mimba na kwenda
kuiweka pembeni kidogo.
Wakati wachawi wenzangu wakiendelea kushangilia kwa kuwapelekea nyama, niliibeba maiti ya yule kijana na kuiweka kando. Kwa kuwa nilikuwa na roho ya kichawi
isiyo na huruma, nilichukua panga na kujongea ilipokuwa maiti ya mama mjauzito nikaichinja shingo yake kama kuku na kuilaza kwenye sufuria. Wachawi wenzangu
walipoona jinsi damu ilivyokuwa ikitiririka kama bomba walishangilia, ilipojaa nilibeba ile sufuria na kumpelekea yule dogo kiongozi wetu.
Kwa kuwa ilikuwa lazima aanze kunywa yeye, alipokea ile sufuria na kuipeleka mdomoni ambapo alikunywa kiasi na kunirudishia. Baada ya kunirudishia, nami
nilikunywa kisha nikawapatia wenzangu ambao nao walikunywa kwa zamu mpaka mchawi wa mwisho. Tulipomaliza kunywa ile damu ambayo ilikuwa tamu sana, tulianza
kushirikiana kukata nyama za zile maiti huku wengine wakiongeza kuni kwenye moto tukaziinjika.
Wakati nyama zikiendelea kuiva, yule dogo kiongozi wetu wa uchawi akatuambia kwamba alihisi ile nyama isingetosha kulinganisha na uwingi wa wachawi
tuliokuwepo. “Jamani hii nyama itakuwa haitutoshi kwani leo tupo wengi sana,” yule dogo alituambia. Baada ya kusema hivyo aliagiza ikatafutwe nyingine haraka
sana, alipotoa kauli hiyo kutaka sifa nilimwambia nitaenda mimi. Wachawi wengine wakiwa wananishangilia, nilipanda kwenye ungo wangu nikanuiza unipeleke
mochwari ya Bugando, kufumba na kufumbua ukapaa.
Sikuchukua muda mrefu nikatua nje ya mochwari hiyo ambapo niliingia ndani kichawi, nikabeba maiti mbili na kuzitoa nje. Baada ya kuzipakiza kwenye ndege
yangu, nikaondoka kurudi kwa wenzangu, kama ilivyokuwa awali, walipoona ungo unatua walishangilia sana. Baada ya kuzishusha zile maiti, dogo kiongozi wetu
aliagiza zichomwe kama mishikaki kwa sababu zile za awali zilipikwa.
Alipotoa kauli hiyo alipaza sauti na kusema wote tumsikilize kwani kulikuwa na jambo muhimu alitaka kuongea nasi. Tukiwa tumetulia kimya aliniita na
kuniambia nisogee karibu yake, nikafanya hivyo. “Naomba mnisikilize kwa makini, mnamuona huyu kijana hapa!” Yule dogo mchawi aliwaonesha mimi akiwa kainua
mkono wangu wa kushoto juu. Kufuatia kuulizwa hivyo, wachawi wote walisema walijibu waliniona ndipo alisema kuanzia siku ile amenipandisha cheo nitakuwa
msaidizi wake.
Aliendelea kusema ameamua kufanya hivyo kwa sababu nilikuwa najituma na nilikuwa nina busara ambazo zinatakiwa sehemu yoyote. Aliposema hivyo, wachawi
wenzangu walishangilia mno, mimi nikabaki ninatabasamu kwani sikutegemea kupewa madaraka makubwa kiasi kile. Baada ya kunitambulisha, kazi ya kuchoma nyama
na kupika iliendelea na zilipoiva mtu wa kwanza kupelekewa kitoweo hicho alikuwa yule kiongozi wetu.
Alipoonja alituruhusu tuendelee kupata kitoweo na kunywa damu iliyobakia na waliopenda kucheza ngoma wafanye hivyo. Tulipomaliza kula nyama, yule dogo
alituamuru tukusanyike pamoja kwani kuna mwenzetu mmoja alihitaji kuongea nasi. Tukiwa tumefanya hivyo, alimwita yule mwenzetu na kumwambia aeleze shida yake
ndipo alianza kwa kusema; “Ndugu zangu, mimi naishi na mjomba wangu ambaye ni mlokole, kwa kweli amekuwa akiharibu sana mambo yangu hasa usiku.
“Kutokana na ulokole wake, kila siku usiku anaamka na kuanza kuomba kitendo hicho kinaharibu nguvu zangu za kichawi hivyo naomba mnisaidie kupambana naye.”
Baada ya mwenzetu kutueleza hivyo, mkuu wetu alicheka sana na kutuambia kwamba ilikuwa kazi ndogo sana kupambana na huyo mjomba wake. “Mtu mmoja hawezi
kukukosesha raha, usiku huu atakiona cha moto,”
yule dogo mkuu wetu alituambia na kuangua kicheko. Alipomaliza kucheka alimwambia yule mwenzetu aliyeomba asaidiwe kwamba awachague wachawi watano aliopenda
waongozane naye kwenda kumkabili huyo mjomba wake. Nataka mkifika mkamtie roho ya uchizi aanze kuongea maneno yasiyoeleweka na kufanya mambo ya ajabu ili
atambue kwamba sisi ndiyo wakuu wa ulimwengu wa giza.
Baada ya mwenzetu kuambiwa hivyo, mtu wa kwanza kumchagua nilikuwa mimi kisha aliwachagua wengine watatu pamoja na yeye tukawa watano. Yule dogo kiongozi
wetu alituambia niite ungo utakaotupeleka kwa yule mlokole, nikafanya hivyo ambapo hazikupita sekunde kumi ungo ukatua. Baada ya ungo kutua, tuliingia wote
kisha niliuamuru upae ndipo tukaanza safari ya kwenda nyumbani kwa mlokole.
Jambo la kushangaza tulipofika eneo ambalo nyumba ya yule mlokole ilikuwepo, nilipojaribu kuelekeza ungo utue haukutua badala yake ulielekea upande wa
kushoto. Kukufafanulia hapo ni kwamba, inapotokea wachawi wanakwenda sehemu kwa kutumia ndege ya kichawi (ungo) halafu kila wakitaka utue unagoma elewa hapo
si mahali salama. Kwa kuwa tulipania sana kumkomesha yule mlokole, licha ya ungo kugoma kutua tuliulazimisha na kuurejesha hadi juu ya anga ilipokuwepo
nyumba ya mlokole.
Tukiwa hapo, tuliulazimisha utue ndipo uligeuka juu chini na kutumwaga kando ya nyumba hiyo na chombo hicho kuangukia upande mwingine. Kilichosababisha ndege
yetu ianguke ni maombi yaliyokuwa yakifanywa na mlokole huyo usiku ule kwani yalikuwa makali sana. Tukiwa tumeanguka, yule mlokole alifungua mlango na
kutoka, akatuona wachawi wanne kasoro yule ndugu yake aliyekuwa kaangukia upande mwingine.
Kama ilivyo kawaida ya walokole wanapoona hali ya hatari huamua kuomba, alianza kukemea huku akilitaja jina la Bwana Yesu. Kabla hajaanza maombi mimi na
wenzangu tulikuwa tumegandiana lakini kadiri alivyokuwa akiomba tulijinasua na kuwa huru na kuweza kusimama. Tukiwa tumesimama, yule mlokole aliendelea
kukemea kwa jina la Yesu ndipo tulipata nguvu tukafanikiwa kutoweka kila mmoja kwa njia yake. Mimi nilikwenda nyumbani na kufikia kitandani, nikajilaza na
kuanza kutafakari lile tukio, sikuchukua muda mrefu nilipitiwa na usingizi hadi nilipozinduka asubuhi.
Kutokana na uchovu wa safari ya kichawi na mkasa uliotukuta usiku, siku hiyo niliamua kukaa nyumbani bila kwenda kokote. Baada ya kunawa uso nilitoa kiti na
kwenda kukaa chini ya mti wenye kivuli uliokuwa kando ya nyumba yangu. Nikiwa hapo nilisikia kelele za watu wakilia kutoka nyumba jirani, nikawa najiuliza
kulikuwa na nini bila kupata majibu. Wakati kelele hizo zinaendelea, nilimuona yule dada mpangaji wangu ambaye hakuwa na mke akirejea kutoka zilikokuwa
zikisikika kelele hizo.
Alipofika tulisalimiana na kumwuliza kwa nini hakwenda kazini, akaniambia aliamua kumpumzika kwani alichoka sana. Kwa kuwa dada huyo alitokea upande ambao
vilio vilisikika nilimwuliza vilikuwa vya nini akaniambia hakuelewa chochote kisha akaingia ndani. Nikiwa najiuliza kilichokuwa kikiwaliza watu hao, mara
nilimuona jamaa mmoja ambaye alikuwa mwanajeshi akija huku mkononi kashika fimbo nne kubwa.
Sikuwa na shaka naye kwani nilijua alikuwa akipita kuelekea mtaa wa nyuma lakini jambo la kushangaza aliponifikia alianza kunitandika mwilini. Nilipomwuliza
sababu za kunilamba bakora, akaniambia mimi na vijana wengine tulimwibia antena yake hivyo tutamtambua.
Licha ya kumwambia ilitakiwa afanye uchunguzi ambao ungemwezesha kumpata mwizi wa antena yake kisha kumpeleka polisi, hakunielewa. Mwanajeshi huyo aliyekuwa
na cheo kazini kwake alinijibu kwamba yeye mwenyewe alikuwa polisi, hivyo lazima tungerudisha antena yake. Kwa kweli kitendo hicho kilinikera sana ndipo
nilimwambia atanitambua kwa sababu aliingia sehemu isiyoingilika lakini mwanajeshi huyo alinibeza na kuendelea kunitandika. “Eti nimeingia sehemu
isiyoingilika, yaani kidudu mtu kama wewe unaweza kuniambia maneno hayo, lazima utasema antena yangu mmeiuza wapi!”
yule mwanajeshi aliniambia huku akiendelea kunicharaza bakora. Licha ya kutoa maneno hayo, nilimwambia alikuwa amechezea sehemu mbaya kwani siyo kila mtu
alikuwa akistahili kupigwa ovyo kama alivyofanya. Nilipomwambia hivyo, alinilamba kiboko cha mgongoni na kuniita mshenzi mkubwa, akaondoka huku akitukana matusi ya nguoni.
Sehemu Ya 8
KWA kuwa sehemu tuliyokuwa tukikutana na kufanya mikutano yetu ilikuwa mbali, niliuita ungo wangu, ulipofika nilipanda na kunuiza unipeleke kwa wenzangu.
Jambo la kushangaza nikiwa angani ghafla ungo ulianza kuyumba huku na huko nami nikaanza kuishiwa nguvu, moja kwa moja nilibaini safari yangu haikuwa ya
heri. Nilikumbuka niliambiwa na viongozi wangu kwamba inapotokea hali hiyo nilipaswa kumuita malkia anisaidie, nikaanza kumwita na kumuomba aninusuru na
hatari iliyokuwa mbele yangu.
Licha ya kumuita mara tatu lakini sikuweza kupata msaada ndipo niliuamuru ungo unirudishe nyumbani haraka sana. Nilishukuru sana kwani baada ya kutoa kauli
hiyo ungo yaani ndege yangu ya kichawi, ilikata kona na kuanza kurudi nyumbani kwa kasi ya ajabu na haukutumia muda mrefu ukatua nje ya nyumba yangu. Baada
ya kutua, niliumuru uondoke kisha nikaingia ndani na kuanza kutafakari kilichosababisha hali ile ya hatari.
Moja kwa moja niligundua njia niliyopita haikuwa salama yaani chini palikuwa na nyumba ya walokole wenye roho mtakatifu waliokuwa wakiomba na kukemea nguvu
za giza. Kukufafanulia hapo ni kwamba wachawi hawafurukuti mbele ya watu wa Mungu ambao wanaishi kitakatifu yaani wale waliojazwa roho mtakatifu wa ukweli.
Mchawi anapokumbana na maombi ya watu hao huungua hata kama alikuwa anasafiri kwa kupita juu ya anga zilizopo nyumba au makanisa yao huweza kuanguka au
kuungua kwa moto.
Hata hivyo, siyo watu wote wanaojiita walokole wana nguvu za Mungu kuna baadhi hawana nguvu hizo kwa sababu hawaishi kitakatifu hao huchezewa na wachawi kama
watu wengine. Walokole wa aina hiyo ambao baadhi pia ni wachawi, hushirikiana na wachawi kuwaroga watu lakini ukiwakuta wanavyojinyenyekeza kanisani siyo
rahisi kuwajua. Kwa kuwa bado ilikuwa usiku niliamua kwenda nyumbani kwa yule mwanajeshi kufuatilia kama alikumbana na uchawi nilioutega.
Nilipofika nilikuta mambo yamekwenda sawa kwani mguu wake mmoja ulianza kumuuma na kuanza kuvimba, nikafurahi sana. Baada ya kuhakikisha jambo hilo, nilirudi
nyumbani nikiwa mwenye furaha kwani nilijua mwisho wake wa kuringa na kusumbua watu uliwadia. Yule mwanajeshi alihangaika sana kutafuta tiba hospitalini bila
mafanikio na alipopimwa ugonjwa haukuonekana lakini aliendelea kulia kwa maumivu aliyokuwa akiyapata. Kama nilivyokuwa nimenuiza, alitumia fedha nyingi
kutafuta matibabu bila mafanikio mpaka akaanza kufilisika kwani kila fedha aliyopata iliishia kwenye matibabu ya kawaida na asili.
kwenye matibabu ya kawaida na asili. Kwa kuwa alikuwa anapata maumivu makali kiasi cha usiku na mchana kushinda akilia, madaktari wakamshauri akatwe mguu huo
uliokuwa ukiendelea kuvimba. Kama ujuavyo maradhi yanapofikia hatua mbaya na ya kukatisha tamaa, yule mwanajeshi ambaye alikuwa haendi hata kazini akakubali
mguu ukatwe. Matukio hayo yalinifurahisha kwani alikuwa ameingia kwenye maji ya kina kirefu na nilijisemea moyoni nitamkomesha hadi dakika ya mwisho.
Kwa kuwa nilidhamiria kumkomesha yeye na familia yake niliamua kuwapa roho ya kupenda ngono mabinti zake wawili ambao walikuwa wazuri waliokuwa wanasoma
chuo. Ukiacha kuwatia roho hiyo, nilipanga kuwavuruga akili zao washindwe kuzingatia waliyofundishwa chuoni na kuwaelewa walimu wao……
UKIACHA kuwatia roho hiyo, nilipanga kuwavuruga akili zao washindwe kuzingatia waliyofundishwa chuoni wawe wanawaza mambo ya wanaume. Kukufafanulia hapo ni
kwamba wachawi wana uwezo wa kuwavuruga watu akili zao mfano wanafunzi wenye akili na kuwa na tabia mbaya, wasiopenda shule na kujiingiza kwenye mambo ya
uasherati. Mambo hayo yanafanyika sana majumbani mwetu, ukimuona mtoto aliyekuwa na akili na nidhamu nzuri kabadilika tabia ujue tayari wachawi wamefanya
kazi yao.
Kujiepusha na uchawi huo ni watu kuwa wacha Mungu na ikitokea mwanao aliyekuwa katulia kabadilika tabia, usimuadhibu bali washirikishe watu wa Mungu
wamuombee kwani wachawi wanakuwa wameuchukua ufahamu wake. Kama nilivyopanga, niliwafuata kichawi wale mabinti zake nikawatia roho ya kuwavuruga akili, wawe
wanasinzia darasani, hata wakifundishwa wasielewe na kupenda ngono.
Baada ya kutimiza hilo, hazikupita siku tatu mabinti wa mwanajeshi huyo wakaanza kulala darasani na kadiri siku zilivyokuwa zikienda wakawa wanapenda ngono.
Kwa kuwa walikuwa wanasoma chuo, wakawa wanatembea na wanafunzi wenzao, walimu jambo hilo liliwashangaza sana walimu na wanafunzi kwani awali walikuwa mfano
kwa tabia nzuri. Kutokana na tabia hiyo, walikuwa wakipewa adhabu na mama yao kuitwa mara kwa mara chuoni kuhusu tabia za wanawe lakini hawakuweza
kubadilika.
Mabinti hao walizidi kuchanganyikiwa na kufikia hatua ya kuitwa malaya kwani walikuwa wakitembea na waume za watu ndipo walifukuzwa chuoni. Binafsi jambo
hilo lilinifurahisha sana kwani nilichokita kilikuwa kimetimia, kwa kweli ndugu zangu uchawi ni kitu kibaya sana kwani watu wanaojihusisha na mambo hayo
hawana huruma. Wakati wasichana hao wamechanganyikiwa na umalaya, baba yao hali ilizidi kuwa mbaya na kufikia hatua ya kuuza gari lake pamoja na mali zingine
ili kujitibia. Kwa upande wangu ilikuwa furaha kwani kitendo cha jamaa huyo kunitandika bila kosa kiliniumiza sana na nilijisemea moyoni kwamba alikuwa
ameingia sehemu mbaya. Siyo mimi tu, hata baadhi ya watu wengine waliofanyiwa vibaya na mzee huyo walifurahi sana alipokumbwa na matatizo na kumshukuru Mungu
kwa kuwalipia bila kujua kama mimi ndiyo nilimroga. Wale wasichana waliendelea kufanya umalaya hadi kwenye mabaa ndipo baba yao alishindwa kuvumilia
akawatimua nyumbani ambapo mpaka leo wamekuwa wahudumu wa baa na baba yao kachananyikiwa akili. Siku moja nikiwa nimelala baada ya kuivuruga familia ya yule
mwanajeshi, nilishtuka kutoka usingizini nilipoangalia pembeni ya kitanda nikamuona yule dogo kiongozi wa wachawi. Yule dogo ambaye alikuwa akiheshimiwa sana
alinisalimu nami nikamsalimu ndipo aliniuliza ilikuwaje siku ile nilishindwa kutua na ungo wangu ukawa unayumbayumba! Nilimjibu kwamba hata mimi
nilishangazwa na hali hiyo ndipo akacheka sana na kuniambia bado nilikuwa sina nguvu nyingi za kichwai. Dogo huyo alinifahamisha kwamba siku ile aliona kila
kitu na kwamba eneo nililokuwepo lilikuwa ni Gamboshi makazi ya wachawi ambalo mtu mwepesi hawezi kukatiza kirahisi. Akaongeza kuniambia kwamba, kwa kuwa
aligundua sikuwa na nguvu alinifuata ili twende Gamboshi kwa ajili ya kuongezewa nguvu na kujifunza mambo mengine ya kichawi. Kiongozi huyo alinifahamisha
kwamba wenzetu walikuwa wametangulia huko hivyo tutoke ndani tukapande ungo wake tayari kwa safari. Tulipotoka tulipanda ndege yaani ungo kisha alimuomba
malkia atuongoze tufike salama ndipo kilitokea kimbunga kikausomba ungo na kuupaisha juu. Ungo ulipokaa sawa, aliuendesha kwa kasi ya ajabu tukawasili kwenye
anga la kisiwa cha Gamboshi, tukatua na kupokelewa na wenzetu. Miongoni mwa wachawi niliowaona ni pamoja na wale niliokwendanao kumroga mjomba wangu na
Sehemu Ya 10
Nilipotoka kwangu kila mtu niliyekutana naye alikuwa akinikata jicho na baadhi niliwasikia wakisema; “Jamani huyu kaka kumbe mchawi mkubwa!” Kauli hizo
ziliniumiza sana na kunizidishia hasira dhidi ya yule mpangaji wangu, hata hivyo kujisafisha na kashfa hiyo niliamua kuigiza kama nimeokoka. Jambo la kwanza
kulifanya siku iliyofuata nilinunua Biblia na kila ilipofika Jumapili nilikuwa nakwenda kusali, lakini siyo kwenye makanisa ya kilokole ambayo wanakemea
nguvu za giza. Nilijua nikienda huko nitaumbuliwa na maombi nikawa nahudhuria ibada kwenye makanisa ya kawaida.
Baada ya kununua Biblia kila Jumapili nilikuwa nakwenda kusali lakini siyo kwenye makanisa ya kilokole ambayo wanakemea nguvu za giza. Nilijua nikienda huko
nitaumbuliwa na maombi, nikawa nakwenda kusali kwenye makanisa ya kawaida. Kufuatia kila siku kwenda kanisani, majirani zangu waliamini kwamba sikuwa mchawi
na yule dada alinisingizia tu. Kwa kuwa nilipanga kumuua yule mpangaji wangu, niliamua kumpa roho ya mauti ndipo siku moja niliporejea nyumbani kutoka
shambani nilitengeneza uchawi kisha nilinuiza afe ghafla.
Hata hivyo, nilihisi rafiki yake mmoja aliyekuwa akiishi naye ndiye aliyemshawishi aende kupiga ramli kwa mganga wa kienyeji ili kumjua mtu aliyekuwa
akiwawangia. Awali nilitaka naye nimtie roho ya mauti lakini niliamua kuachana naye na ‘kudili’ na aliyenidhalilisha hadharani. Baada ya kuandaa uchawi
wangu, siku iliyofuata saa mbili usiku ndipo niliiamuru ile roho ya mauti ikamuingie yule dada na akifa maiti yake ipelekwe hospitali na si kwa mganga wa
kienyeji.
Kukufafanulia hapo ni kwamba, mtu aliyekufa ghafla kwa kurogwa, ndugu zake wakimshtukia kwamba karogwa wakimpeleka kwa mganga wa kienyehi huzinduka lakini
akipelekwa hospitali anakufa moja kwa moja. Kulitambua hilo, wakati nanuiza ile roho ya mauti kwenda kwa yule dada sikusahau kuiambia ndugu zake wasipate
ufahamu wa kumpeleka kwa mganga ila hospitali. Baada ya kunuiza nilijifanya naumwa nikalala chumbani kwangu kwani nilijua muda si mrefu yule dada angefariki
dunia.
Nikiwa chumbani kwangu nilisikia yule dada akilia na kusema kwamba rafiki yake alianguka ghafla na kufariki dunia, kilio cha dada huyo kiliwashtua wapangaji
wengine. Kutohisiwa mimi ndiye nilimuua yule dada, niliamka huku nikijikongoja na kujifanya naumwa nikatoka na kuanza kuhoji kimetokea nini, wakaniambia yule
dada kafariki. Nilijifanya nimehuzunishwa sana na kifo hicho ndipo nilishangaa kumuona yule rafiki wa marehemu ametoka mbio.
Hakutumia muda mrefu huko alikokwenda akarejea na gari akiwa na mganga ambaye nilibaini ndiye waliyekwenda kupiga ramli na kuambiwa mimi nilikuwa nawaroga.
Jamaa huyo nilikuwa namfahamu kwani tulikuwa tukiishi eneo moja na alisifika sana kwamba alikuwa mganga mahiri. Baada ya kufika waliingia ndani, kwa kuwa
chumba hakikuwa na silingibodi juu nilimsikia mganga huyo akisema yule dada alirogwa na alikuwa na uwezo wa kumzindua kwa sababu hakufa.
Hakuishia hapo, alisema inatakiwa wamtoe pale na kumpeleka nyumbani kwake ambako atamfanyia dawa. Niliposikia kauli hiyo, moyo ulinipiga paa! Kwa kuwa
sikutaka kabisa dada huyo azinduke niliwafuata na kuwaambia wampeleke hospitali kwa sababu alipoteza fahamu kwa tatizo la kuishiwa damu. Jambo la kushangaza
ni kwamba licha ya kusisitiza sana wampeleke hospitali na kuwaambia huko nyuma niliwahi kuwa daktari lakini yule mganga alipinga.
Alichokifanya aliwasihi watu waliofika pale nyumbani wakiwemo ndugu wa yule dada kwamba, wasihuzunike kwani hakufa bali alirogwa na atamzindua kisha
akaondoka naye. Kitendo hicho kiliniumiza sana kwani yule mganga alikuwa na nguvu nyingi hivyo nisingeweza kupambana naye ili aniachie mtu wangu niliyetaka
kumfanya msukule. Baada ya kutafakari sana, ilipofika saa sita usiku niliuita ungo wangu nikaamua kumfuata yule dogo mchawi ili akanisaidie.
Nilipofika nilimsimulia kila kitu kuhusu yule dada na mganga na kumuomba anisaidie ili asimzindue kwani nilitaka kumfanya msukule. Yule dogo akashauri kesi
hiyo tuipeleke kwa malkia ndipo tulipanda ungo na kumfuata malkia ambaye ndiye alikuwa mkuu wetu katika ulimwengu wa kichawi. Baada ya kunishauri hivyo
tuliondoka hadi kwa malkia, tukiwa kwenye makazi ya mkuu wetu huyo tulimuona akiwa ameketi nje ndipo dogo akaniambia nimfuate kwa unyenyekevu nikamwambie tatizo langu.
Nilipomfikia nilimsujudia mara kumi na sita kisha nikamweleza shida yangu ndipo malkia akatikisa kichwa na kusema; “Huyo mganga anataka kumfufua mtu wako si
ndiyo?” Nikamwambia ndiyo. Baada ya kumweleza hivyo, akaniuliza nilikuwa nataka msaada gani, nikamwambia aniongezee nguvu ili nikamshinde mganga na kumgomboa
mtu wangu, akasema sawa. Malkia alipotoa kauli hiyo alininyoshea kidole cha shahada ghafla mwili wote ulinisisimka ndipo aliniambia kazi yangu ilikwisha
hivyo tuondoke.
Kwa kuwa katika safari hiyo kila mmoja wetu alisafiri na ndege yake ‘ungo,’ tuliondoka, tulikwenda sambamba hadi sehemu flani tuliachana na dogo. Dogo
akaeleka kwake nami nikaelekea kwa yule mganga kwani baada ya kuongezewa nguvu nilijiamini sana na nilipanga kwenda kumkomboa yule dada.
Nilipofika karibu na nyumba yake, nilitua na kuiacha ndege yangu kisha nikamfuata mganga na kumuuliza yule dada alikuwa wapi akasema alimponya na tayari
alirudi kwao. Kitendo hicho kilinikera sana nikamuuliza kwa nini aliingilia mambo yangu, akaniambia nisimbabaishe na uchawi wangu. Kwa kuwa nilikuwa
nimeongezewa nguvu nilimwambia aliingia sehemu ya hatari hivyo nitazichukua nguvu zake zote ili abaki kama mtu wa kawaida. Baada ya kusema hivyo nilimnyoshea
kidole nguvu zake za kiganga zikamtoka kisha nilimuwekea roho ya kichaa, tangu siku hiyo akawa chizi mpaka leo. Nilipotoka kwa mganga nilirudi nyumbani na
kumkuta yule mpangaji wangu akiwa mzima, nikamtia roho ya mauti akafa na hakuna mtu aliyeshtukia kama mimi nilihusika na kifo chake.
Baada ya yule dada kufariki, ndugu zake walifika wakaichukua maiti na kuipeleka nyumbani kwao kwa ajili ya maandalizi ya mazishi siku iliyofuata. Wakati wa
pilika hizo, nami nilijumuika nao na kuonesha huzuni juu ya kifo cha mpangaji wangu lakini moyoni nilifurahi sana. Kufuatia msiba huo, watu waliongea mengi
kwani wapo waliodai marehemu alikumbwa na jini na kama siyo jini alikuwa kafanyiwa mambo ya Kiswahili.
Wengine walioshika dini walisema ahadi yake ya kuondoka duniani iliwadia hivyo wamshukuru Mungu na kuacha kufikiria kwamba alikuwa karogwa au kukumbwa na
jini. Binafsi nilipendezwa sana na kauli za watu hao kwani walisaidia kuwafanya wanandugu kutofikiria kwenda kupiga lamri ili kujua ndugu yao alikufa kifo
cha kurogwa au kawaida. Kama inavyofahamika kwamba mtu akifa ndiyo inakuwa mwisho wake na kinachofuatia ni maziko, siku iliyofuata jioni yule mpangaji wangu
alipelekwa makaburini kwa ajili ya kuzikwa. Baada ya taratibu zote za kukamilika, alizikwa kisha waombolezaji walirudi majumbani mwao na ndugu waliendelea na
matanga.
Kwa kuwa mimi ndiye niliyemuua yule dada kwa lengo la kumfanya msukule, ilipofika saa saba usiku niliondoka kichawi na kuelekea makaburini kwa ajili ya
kuuchukua msukule wangu. Kukufafanulia hapo ni kwamba mtu aliyeuawa kichawi kwa lengo la kufanywa msukule, akishakufa wachawi husika humchukua na kumuweka
sehemu ambayo atakuwa anawaona ndugu na watu wengine lakini huwa hana uwezo wa kuwaita. Wakati huo, kwa watu ambao siyo wachawi au walokole wenye nguvu za
Mungu, wanapoiangalia ile maiti wanaiona ya kawaida lakini inakuwa imegeuzwa mgomba au gogo la mti.
Jambo lingine ni kwamba mtu aliyechukuliwa msukule akizikwa, ukienda kuangalia kaburi lake baada ya siku mbili au tatu utakuta limetitia kwani tayari wachawi
wanakuwa wamemchukua mtu wao. Baada ya kufika makaburini, nilifanya ndumba zangu ndipo yule dada alitoka kaburini nikampeleka kumuuza kwa wachawi wenzangu.
Kulipokucha niliamka nikiwa mchovu sana kwa sababu ya mzunguko wa kichawi nilioufanya usiku, niliandaa chai nikanywa kisha nilijipumzisha kitandani hadi saa
tatu na robo nikaamka.
Kwa kuwa kijua kilianza kuwa kikali nilitoka ndani na kwenda kuketi chini ya mti wenye kimvuli uliokuwa pale nyumbani sehemu ambayo nilipenda sana
kujipumzisha. Nilikaa hapo hadi saa nne ndipo niliona gari aina ya Range Lover likija pale nyumbani na kusimama, mara akashuka Muarabu aliyekuwa kavaa
kinadhifu sana.
Alipofika alinisalimia kwa kusema; “Hujambo kijana?” Nikaitikia sijambo, shikamoo? Akasema marahaba. Baada ya salamu yule Muarabu aliniambia kwamba yeye
alikuwa ni mfanyabiashara aliyekuwa akimiliki visima vya mafuta kwao Uarabuni. Akaendelea kuniambia kwamba alihitaji tufanye biashara…yaani nimuuzie lile
eneo langu ili ajenge sheli kisha aliniuliza nilihitaji anipe shilingi ngapi ili twende tukaandikishane kwenye ofisi za serikali za mitaa. Kabla sijampa jibu
niliomba nimuulize swali na kama angenijibu nilivyotaka nisingemuuzia uwanja badala yake ningempatia bure pamoja na nyumba yangu.
Nilipotoa kauli hiyo, yule Muarabu akasema; “Niulize ili nikujibu.” Alipokubali, nilimuuliza nifanyeje ili nami niwe tajiri kama yeye, yule Muarabu alicheka
sana. Alipomaliza aliniambia kwamba hapa duniani kila kitu kinawezekana hata mimi naweza kuwa tajiri tena hata kumpita yeye. Baada ya kuniambia hivyo, simu
yake ikaanza kuita ndipo alipokea na kuanza kuzungumza na mtu aliyempigia ambapo nilimsikia akimwambia; “Sawa, naondoka sasa hivi itabidi nirudi tena siku
nyingine au nitawaeleza wenzangu.” Alipomaliza kuzungumza na mtu huyo, aliniambia kwamba anatakiwa kuondoka haraka kuelekea Zanzibar kwa ndege na kuahidi
kurudi siku iliyofuata muda kama aliofika kisha akafungua pochi yake akatoa kibunda cha noti na kunipatia.
Baada ya kunikabidhi fedha hizo, aliniaga akaingia kwenye gari lake na kuondoka ndipo niliingia ndani nikahesabu zile fedha nikakuta ni shilingi laki mbili.
Kitendo cha kupewa fedha nyingi kiasi kile na yule Mwarabu, nilijikuta naumia na kujiuliza kwa nini mimi sikuwa tajiri na uchawi niliokuwa nautumikia na kuua
watu ulinipa faida gani?
Nilijutia sana uovu wangu wa kuwatesa watu wasio na hati na kujikuta nimeanza kulia na kuongea peke yangu na kujiuliza; “Hivi huu uchawi ungekuwa utajiri
tangu nilipoanza kuwatesa watu hivi sasa si ningekuwa tajiri mkubwa na kila mtu angeniheshimu?” Baada ya kuwaza sana, nikaamua kuacha mambo hayo ndipo
nilikusanya matunguri ya kichawi na ule mkoba wa kichawi wa bibi nikauingiza kwenye kile chumba cha yule dada niliyemuua nikaenda dukani.
Niliporejea nilikuwa nina chupa ya mafuta ya taa ambayo niliyamimina kwenye ndumba zangu na kuzichoma moto, nikaanza kusikia zile roho za uchawi nilizokuwa
nazitumikia zikilia. Hazikuishia kulia tu bali zilikuwa zikilalamika na kuhoji kwa nini niliamua kuwatesa namna ile na kuomba niwasaidie lakini sikujali
mpaka matunguri yangu yalipoteketea kabisa.
Kwa kuwa nilielewa wachawi wenzangu wasingefurahishwa na kitendo nilichokifanya na lazima wangeniangamiza, niliamua kwenda kumuona bibi mmoja ambaye
alisifika sana kwa uganga ili anifanyie zindiko. Kabla sijaondoka nilifunga kwa kufuli mlango wa kile chumba nilichokitumia kuteketeza matunguri yangu kisha
nilielekea kwa yule bibi mganga. Bahati nzuri nilipofika nilimkuta ndipo nilimueleza shida yangu, akaniuliza nilitaka zindiko hilo anifanyie lini!. “Muda huu
kwani nikichelewa tu nitauawa na wachawi wenzangu kwani nimewakorofisha sana,” nilimuambia yule mganga.
INAENDELEA

