HAINA MABEGA
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
SEHEMU YA KUMI NA ISHIRINI
“Ahsante” niliitikia kinyonge sana kama mtu aliemwagiwa maji ya baridi niliweka chakula na kutaka kutoka nje.
“Wala usiwahi kuondoka nataka tuzungumze kidogo kaa kwenye kiti hapo” nilisita kidogo kukaa mwisho nikaamua kukubali nikakaa kwenye kiti.
“Pole kwa msiba uliokukuta, nilikuona namna ulivyokua unalia msibani ulinipa huzuni sana, sio kwasababu ya wewe kulia ni kwasababu niliona ulionesha mapenzi ya wazi kwa mtu aliepoteza maisha tena ulimpenda zaidi yangu mimi niliohai”
“Nenda kwenye pointi hayo mambo yameshapita sitaki kukumbushwa tena” niliongea kwa sauti ya juu, sikutaka atumie mwanya huo kunikumbusha maumivu ambayo yalishaanza kupona kwenye moyo wangu.
“Oooh sawa, sikia Gasper hongera kwa kupata ajira, limenifurahisha sana lakini ujue kwenye dunia ya sasa kutegemea ajira peke ake kama chanzo cha mapato utaishi kwenye umaskini kwa muda mrefu, kazi itakutesa na siku utakayostaafu hutokua na pesa ya maana utakufa na manung’uniko kibao, sasa nakusogezea ule mpango wa kufungua duka la nguo asilimia sabini zako na thelathini zangu, ukipata kipato huku na kule angalau utakua na kipato kikubwa cha kufanya mambo yako” Dr Furaha alinirudishia mpango wa kufungua duka, mpango ule ule aliokua nao kabla sijaenda mafunzoni.
“Ni hilo tu au kuna mengine” nilimuuliza
“Mengine yapo ila ni muhimu yote kuyazingatia”
‘Sawa hilo la kufanya biashara kwa ushirikiano na mtu mwingine siko tayari, ahsante kwa ushauri wa kuwa na chanzo kingine cha mapato nitalifanyia kazi enhe lingine nataka kuwahi mgahawani kuendelea na kazi”
“Mmmh sawa, jambo lingine ni hili nataka nikukumbushe ni wapi tumetoka, ni mangapi nimeyafanya kwenye maisha yako, siongei hayo kwakua nataka unilipe pesa zangu hapana kwakua pesa ni kitu cha kupita tu, nataka tumalizane kwa mioyo safi kabisa, ili mimi nisiwe na kinyongo na wewe usiwe na kinyongo na mimi” Dr Furaha aliongea vitu vya maana ambavyo vilivuta usikivu wangu na kunipunguzia hali ya kukunja uso niliyokua nayo.
“Kumalizana kwa amani ni jambo la msingi sana au kuna kitu unataka kukazia katika hilo?”
“Ndio lipo, nataka tucheze mechi ya mwisho ya kuagana, nataka kiungo chako kinipe raha kwa mara ya mwisho nikuahidi baada ya leo sitokusumbua tena kwenye maisha yako nitakua nimetosheka, nitakufungulia roho kabisa na kila mtu atafanya maisha yake” Dr Furaha alisogeza mezani pendekezo lake, nilikaa kimya kwa muda nikiwaza jambo, kisha nilifungua kinywa changu kuzungumza.
“Umesema mara ya mwisho sindio?”
“Ndio mara ya mwisho”
“Sawa iwe ya mwisho kweli, location”
“Kwangu pale pale tulipoanzia tukafungie pale pale”
“Mmmh hiyo hapana kubwa siwezi kuja kwako, kama sehemu nyingine sawa” nilitumia mbinu ya kijasusi ya kutokumuanini mtu, tangu nitoke mafunzoni nilijua mechi zote za uwanja wa ugenini si salama siwezi kuzicheza kwa usalama wangu.
“Poa saa kumi na mbili tutaenda hotel moja nzuri tukulane weee mpaka tutosheke”
“Poa badae bhasi” niliaga kuondoka kabla sijaondoka Dr Furaha alinipiga busu la upepo, sikumjibu na kuondoka zangu niliendelea na kazi ilipofika saa kumi na nusu niliwaaga wafanyakazi wenzangy nikarudi nyumbani nikajiandaa ilipofika saa kumi na moja na nusu nilikua juu ya pikipiki kuifuata hotel niliyoelekezwa, nilifika chumbani alipokua nilipiga show fresh kama kawaida sikuangusha ukoo wangu, baada ya show aliniomba tuzungumze kidogo kabla ya kuagana.
“Sikia Gasper leo ndio siku ya mwisho mimi kukutafuta tena, mimi ni mtu mzima najua ni ngumu lakini nitajitahidi mpaka kuliweza jambo hilo, kabla ya kuagana naomba nikupe zawadi ndogo hivi itakufaa wewe na vizazi vyako vijavyo” Dr Furaha aliongea na kuivuta pochi yake muda wote huo nilikua kimya nikimtazama tu.
“Hii ni cheque ya millioni kumi, naomba upokee hii pesa itakufaa zaidi kwenye harakati zako za kimaisha ujue wewe ndio kwanza unaanza maisha”
“Mmmh usijali haina haja, pesa ulizowahi kunipa zinanitosha kabisa hii itakufaa na wewe kwenye maisha yako”
“Heee kwa huo mshahara wa laki saba, mimi hizi millioni kumi ni pesa za kawaida kwangu kama wewe unavyoshika laki moja ndivyo mimi nashika hii millioni kumi, weww pokea na hutoona nikikutaja mahali kwamba nimekupa pesa wala sitokufuatilia kwa chochote pokea tafadhali” Dr Furaha alizidi kubisisitiza. Pesa ilitamanisha kwelikweli ilikua pesa nyingi ambayo sikuwahi kuishika mara moja hata nikikusanya mshahara wangu kuifikia pesa hiyo ingenichukua miezi kumi na tano, sasa kuiacha pesa ya bure bure namna ile ilihitaji moyo sana, nilikaza mwishoni niliamua kuipokea pesa hiyo, baada ya kutoka hapo nilipitia benki niliitoa pesa yote millioni kumi, nikapitiliza mpaka nyumbani kwa wazazi wangu, walinipokea kwa furaha sana japokua ilikua usiku ilipofika asubuhi ya jumapili, tulikwenda kanisani kama familia tuliporudi niliomba kuongea na wazazi wangu wote.
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA
“Wazazi wangu tangu zamani nilikua na ndoto ya kuwafanyia kitu kikubwa sana mpaka ninyi mfurahi hiyo siku haijafika ila leo nina hiki kidogo ambacho mimi nimekipata nimeona niwaletee ili na ninyi mpate kula matunda ya kunizaa, kunilea mpaka kunifikisha katika umri huu. Nina millioni kumi hapa nataka niwape kama mtaamua kujenga vyumba vya kupangisha ni ninyi yaani fanyeni chochote ambacho mtakipanga na kukiamua”
“Alililililili luulululululu” mama alisimama na kupiga vigelegele vya kushangilia kile nilichokiongea. Niliziweka millioni kumi mezani, pesa ambayo haikuwahi kuwepo ndani ya nyumba yetu, mimi nilikua nimeziweka mezani.
“Kweli nimezaa, kweli nina jembe, Mungu nakushukuru kwaajili ya huyu mtoto, mbariki na kumfunika aingiapo na atokapo, maisha yake yaendelee kuwa nuru, giza lisimuweze kamwe, nambariki hakuna hila wala kibaya kitakachosimama juu yake” Baba alinishika kichwani na kunibariki. Niliamua kuzipeleka pesa zote nilizopewa na Dr Furaha kwa wazazi wangu ili kama kuna maneno au kibaya alikinenea kwenye hizo pesa bhasi kiyeyushwe na baraka za wazazi wangu, unaona akili hiyo, nipigie makofi tafadhali. Wazazi waliamua pesa zile zitatumika kwenye ujenzi wa vyumba vya kupangisha kwakua tulikua na eneo kubwa ambalo lilibaki wazi, nililala nyumbani na siku iliyofuata nilirudi nyumbani kwakua nilikua naingia kazini mchana, baba alianza maandalizi ya ujenzi pesa si ipo ujenzi ulienda haraka haraka ndani ya mwezi tu vyumba vinne vilikua tayari mpaka kupauliwa waliweka milango ya na madirisha, nilijibana bana nikaongezea millioni moja kwaajili ya kufanya finishing ya mambo madogo ya ndani, vyumba vilipata wapangaji wa haraka na fedha iliyopatikana ilikua inaingia kwa wazazi moja kwa moja na kywasaidia kwenye mambo ya kiuchumi, miezi mitatu ya kurudi rudi nyumbani nilifanya hivyo kila weekend nilizokua off nilifanya hivyo ili kutojirudi kwenye tabia yangu ya kupenda wanawake, katika kipindi hiko nilikua karibu na mwanamke mmoja tu ambae ni Zai, yule mpenzi wangu ambae nilianza nae mapenzi tangu akiwa shuleni, alishamaliza shule hivyo alikua mtaani tu, tulikua tunawasiliana sana nilimchunguza kwa miezi mitatu mingine mwishoni kaona ni kheri nimuoe tu, nikapeleka barua kwao, ikakubaliwa si unajua nilikua na kazi tayari,
hakukua na ugumu wowote ule, nililipa mahali yao, nikafunga nae ndoa, kingine kilichonivutia kwa Zai mpaka kuamua kumweka ndani ni kwamba msichana hakua na tamaa, pili alikua ananisikiliza na kunipenda, tatu kalikua kadogo kwa umri hivyo ilikua rahisi kumwongoza, nne nilikafungua mwenyewe maganda yaani mimi ndio mwanaume wa kwanza kumtoa bikra hivyo nilikua na amani nae.
Maisha yetu ya ndoa yalianza vizuri nilijitahidi kumpa kila kitu mke wangu Zai kwa wakati huo alikua anaitwa Cecilia kwani alibadili dini na kuwa mkristo kiufupi alinifuata kwenye dini yangu ndio ikawa rahisi kwetu kufunga ndoa.
Ndoa yetu ilikua ya furaha sana, nilimwomba tukae mwaka mmoja bila kupata mtoto kipindi chote hiko tule maisha na kufurahia ndoa yetu, kweli siku zile za hatari hatukua tukishiriki tendo la ndoa, miezi mitatu ya kwenye ndoa siku moja jioni tulikua tunatoka mlimani City kununua vitu vitu pamoja na kutazama Cinema wakati tunatoka nikakutana na jamaa mmoja ambae tulijuana miaka ya zamani kidogo kwani tuliishi wote mtaani, wakati tunaongea nilimwambia mke wangu atangulie kwenye gari, sikutaka mke wangu awepo wakati naongea na jamaa, mara nikasikia kelele upande alipoelekea mke wangu kutazama vizuri nilimwona mke wangu analazimishwa kuingia ndani ya gari na jamaa fulani hivi.
“Mke wangu anatekwa” nilihamaki kwa sauti nilichomoka ili kwenda kunsaidia mke wangu nilipofika kuna jamaa alichomoa bastola na kuninyooshea walimsukuma mke wangu na kuanguka chini, walinikamata mimi na kuniingiza kwenye gari, nikiwa ndani ya gari nilizimishwa, walinzi wa getini walipotaka kuzuia gari ilipigwa risasi moja hewani walipisha wenyewe, gari iliondoka mahali hapo kwa kasi ile ile. Mke wangu alibaki na yule jamaa wakishauriana nini cha kufanya mwisho wakakubaliana waende kutoa taarifa kituo cha polisi kilichopo ndani ya chuo kikuu UDSM juu ya kutekwa kwangu.
SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI
Nilizinduka nikiwa na uchovu kidogo, nilifikicha macho yangu na kuweza kuona vizuri, nilikua nimelala juu ya sofa nilipotazama mazingira vizuri hayakuwa mageni kabisa machoni mwangu ilikua nyumba ya Dr Furaha, nikaamua kukaa, sebuleni pale nilikua peke angu tu, niliwaza kidogo kwamba Dr Furaha ameamua kuniteka ili kunifanyisha mapenzi kwa nguvu au, nikapandisha hasira yangu jikajiambiza kwamba akitokeza mbele ya macho yangu tu nitamuwakia na kumhoji kwanini kaamua kwenda kinyume na maagizo yangu, nilisubiri kwa dakika tano ili niwe sawa kwanza.
“Oooh kumbe umeamka kijana wangu, karibu sana naomba mleteeni kifungua kinywa kijana ameamka” Mwanaume mmoja mzee aliongea baada ya kuingia sebuleni, sura yake ilikua ngeni sana machoni mwangu sikuelewa kwanini alikuwa pale tena nyumbani kwa Dr Furaha, hakua peke ake alikua na njemba watatu, wawili ndio wale walionikamata na kuniingiza kwenye gari na watatu ni yule rafiki angu wa utotoni ambae alikua ananiongelesha wakati mke wangu anashikwa, hapo nikaelewa mchezo mzima kwamba hata kukutana na yule rafiki angu wa utotoni yote ilikua sehemu ya mpango wa kuniteka, swali liliendelea kusokota akilini mwangu iweje anilete nyumbani kwa Dr Furaha.
“Mke wangu naomba mletee mgeni angalau kikombe cha chai apate kidogo” mwanaume alikazia zaidi, mara alifika Dr Furaha akiwa na kikombe cha chai. Kufikia hapo nilijua kwisha habari yangu, nimejaa kwenye mfumo wa mume wa Dr Furaha.
“Mpe chai kijana mke wangu mbona unasita”
“Sawa mume wangu nampa” Dr Furaha alinipa kile kikombe japo hakuweza kunitazama kabisa usoni yaani alikwepesha macho yake vibaya mno.
Nilikipokea kile kikombe nikiwa natetemeka, hofu ya kufanyiziwa kitu kibaya ilikua inajirudia akilini mwangu.
Sikunywa kile kikombe cha chai kuhofia huenda ile chai ina sumu.
“Wakati unapata chai japo ni kavu, nataka tuwe tunatazama movie kidogo naamini kila mmoja ataipenda” Mwanaume huyo aliongea na kubofya rimoti, Tv iliwaka hapo hapo, kilichoonekana kwenye Tv kilinimaliza nguvu zote, kulikua na rekodi kamili tangu siku ya kwanza niliyoingia kwenye nyumba ile, vitu vyote nilivyofanya na Dr Furaha vilionekana kwa uwazi kabisa, nilipomtazama Dr Furaha alikua amepiga magoti huku akilia ameishika miguu ya mumewe akiomba msamaha, kwa upande wa mumewe nae alikua analia kwa kuona usaliti mkubwa aliokua anafanyiwa na mkewe wa ndoa. Nilijiona mimi ni mfu mtarajiwa yaani kama mwanaume analia vile mimi atanifanya nini, nilimwomba Mungu aipokee roho yangu, nilikua najua kuhusu jehanum kwa dhambi nilizozifanya sikutaka kutupwa kwenye ziwa na moto nilichoona hapo ni kifo tu ili niwe salama ni mimi kutubu.
“Nikiwa huko nchi za watu nilikua nafuatilia kila kitu kilichokua kinaendelea ndani ya nyumba yangu kwakua kabla sijaondoka nchini nilitega camera kwa siri sana, mke wangu hakuligundua hilo ndio maana aliamua kunisaliti na wewe kijana mdogo nikikutazama ninaweza kukuzaa kabisa lakini ukaona nilipochovya mimi na wewe ukachovye hapo hapo, ukabembea kwenye matiti ya mwanamke mkubwa sawa na mama ako, unajua iliniumiza kiasi gani aiiiiiiiiiii aaaaaaaaaaaaaah” mwanaume huyo alielezea ilivyokua hakuweza kuendelea kuongea alikamatwa na kilio kizito, alilia sana nilijihisi hatia, nilijua kosa kubwa nililotenda nilijiona mimi ni mtu mbaya kumuumiza baba wa watu mpaka analia kama mtoto.
“Sasa wewe si unapenda kuona tupu za wakubwa zako, wewe si kidume sana sawa ngoja uone na tupu yangu” mwanaume alitoa mkanda kisha akashusha suruali mkewe alipotaka kumzuia alimsukuma akimwambia akae pembeni kabla ya kushusha boksa aliwaambia vijana wake.
“Tokeni nje huyu nammudu peke angu, sitaki ninyi mshuhudie hiki ninachotaka kukifanya hapa”
Akilini mwangu nilijua nimeisha leo natendewa kitendo ambacho nilimtenda Dr Furaha, nilitamani kufa kuliko kufanywa hiko kitu nilijiambiza hata kama nina makosa atakaponisogelea kunishika nitamuua, hata kama na mimi nitakufa ni sawa ila sikutaka kupoteza ubingwa wangu, vijana walitoka nje, mzee alishusha boksa chini na kutamka maneno mazito.
“Nakulaani wewe na vizazi vyako vyote, kamwe hutopata furaha katika maisha yako yote, uliyonitenda mimi yakurudie wewe mara saba, pesa na dhahabu zikikuona zikukimbie, ulaaniwe kwa majina yote ya mwenyezi Mungu” mzee alitoa laana zote kisha alipandisha boksa na kuvaa suruali yake, tayari alishatoa laana yake, aliniruhusu niondoke pasipo mchubuko wowote mwilini mwangu yalikua maajabu sana kitendo alichokifanya yule mwanume. Tukio lile lilipita miaka miwili kazini nilifukuzwa kazi kwasababu zisizokua za msingi, mke wangu Zai alipoteza maisha akiwa wodi ya kujifungulia, nilipoteza mke na mtoto, nilirudi kwa mama Shirima kuomba kazi akanipa cheo cha umeneja nlifanya kazi kwa mwaka mmoja nilisababisha hasara ya millioni moja, mama shirima alinifukuza kazi sikua na uwezo hata wa kulipia chumba cha kupanga nilirudi nyumbani kwa wazazi, nilianza kupata magonjwa hovyo hovyo wazazi wangu walipotembea kwa watumishi wa kuniombea waliambiwa kwamba nimelaaniwa kutokana na makosa niliyoyafanya, wazazi walinibana sana nikawaeleza ukweli wote kwa yale wasiyoyajua walihuzunika sana tukaamua kwenda kwa Dr Furaha ili kuomba msamaha kwa mumewe, mlinzi alituambia kwamba Dr Furaha na mumewe wamehamia uingereza na hata nyumba ilishauzwa kwa mmiliki mwingi, sikupata njia yoyote ya kumpata mume wa Dr Furaha ili aweze kuondoa laana kwenye maisha yangu, haikuwezekana tena niliendelea kuwa na maisha magumu, laana inashika sio lazima upewe na wazazi tu, laana inatesa tujitahidi kuwa watu wema sana.
MWISHO..


1 Comment
It had good conclution bro and educetable