SAMAIRAH
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Sehemu Ya 1
Aryan aliumia sana na kujikuta anaongea kwa uchungu Mussa nimewakosea nini hadi mfikie hatua ya kutaka kunipa ukilema? Yule jamaa alinyanyua ile sindano ile anataka tu kumchoma sindano machoni alijikuta akiidondosha mwenyewe kisha alishuka chini taratibu na kusema jamani tumbo linaniuma , hakika yule njemba alijaribu kujikaza lakini hakuweza hadi akalala chini huku akihisi mwili wake kukosa nguvu,
Wenzake walivyoona mwenzao kapatwa na homa ya tumbo ghafla ndipo njemba ya tatu alitoa upanga ili amkate Aryan mikono na miguu lakini hata yeye hakufanikiwa alikamatwa na tumbo ,anajikuta anaachia upanga huku akilia kwa maumivu tumboo jamani tumbooo,
Sasa njemba ya tatu ambae alikuwa amemkaba Aryan kwa nyuma nae tumbo likamkamata vile vile wakajikuta wanamwachia Aryan
Walianza kutembea kwa kutambaa na kujiburuza maana waliumwa tumbo kwenye kitovu na walihisi limekaza ,walijiburuza huku Aryan akiwashangaa na kujiuliza hawa watu nini kimewakuta ,”ooh asante Mungu”Aryan alijisemea moyoni.
Aryan hakutaka lile suala alipeleke polisi,wale njemba walijiburuza weee hadi walivyotoka nje walishangaa wanakuwa poa hata matumbo yao hayaumi tena ,
Oya mwamba tumbo langu haliumi tena kwani ilikuwa ni nini? Njemba moja aliuliza huku wakipanda kwenye bajaji ,mmoja aliguna na kusema mmmh kwa leo tuache kumfanyia ubaya yule jamaa maana nilihisi kufa kufa ,waliondoka zao.
Basi siku hiyo Aryan alikaa na bibi wakapakua chakula chao wakaanza kula ,Aryan alimsaidia bibi kumega matonge anampa kwenye mkono halafu anaupeleka mkono wa bibi hadi kwenye chombo cha mboga hakika bibi alijihisi faraja baada ya kufadhiliwa na Aryan walivyomaliza kula bibi alimwita Aryan.
Aryan nae alienda na kukaa karibu yake ,bibi alishika mkono wa Aryan kisha akaanza kuonge”Aryan mjukuu wangu nimekaa hapa japo kwa muda mfupi ila nimegundua kuwa watu wengi wanao kuzunguka hawakupendi wengi wao ,hasa hawa majirani ,jana wakati naenda msalani ,majirani walikuja na kuniambia niondoke huu mtaa “,Aryan alimwangalia bibi ambae goti lake bado halijapona vizuri ,Aryan alisema ” bibi nimesema hakuna kuondoka hapa mimi nitahakikisha nakulinda nakuhudumia kwa kila kitu ,
Kisha bibi akaendelea na maongezi ,”usiku nimeota ndoto mbaya mama mmoja kafukuzwa kazi ambayo alikuwa akifanya ,huyo mama alivyofukuzwa wakati ana mawazo ya kufukuzwa kazi alipita kandokando ya barabara aligongwa na gari ila hakuumia sana ,ila kapelekwa hospitali,
Aryan alitabasamu na kumwambia bibi ndio maana napenda kukaa na wewe story zako bana huwa zinanifurahisha ,sasa hio si ndoto ya kawaida bibi?
Bibi alitabasamu na kumwambia ndio ya kawaida ila nimejisikia kukuambia tu ,yalikuwa maongezi huku Aryan akimsugua bibi miguu na maji ya uvuguvugu,bibi alianza kupendeza na kuonekana safi.
Tukirudi maeno ya mwenge mama yake na Aryan baada ya kufukuzwa kule kwa akina Jesca aliondoka zake akiwa anavuka bara bara hakuangalia gari pande mbili za barabara,
Mama akajikuta anagogwa na gari na kudondoka ,kelele zilisikika watu wakisema ajali ajali ,watu walikimbia hadi kwa yule mama ,bahati nzuri aliyemgonga alikuwa ni mama ,
Yule mama alikuwa na moyo wa kipekee alishuka upesi kwenye gari na kuomba watu wamsaidie kumpakia huyo mama kwenye gari yake ,hakupenda kuchelewesha alimuwahisha hospitali.
Mama alioneka kuchubuka maeneo ya mkono wa kulia na damu nyingi kumtoka sana puani ,
Yule mama baada ya kumpakia yule mama aliyemgonga ,kila akiangalia ile damu inayotoka kwa yule mama anaitamani akitaka kupeleka kidole walau achovye alambe kidogo anasita, mara simu yake ikaita aliipokea na kusema
Haloo ,upande wa pili sauti ilisikika ikisema mama leo sijisikii vizuri nimeenda kwa rafiki yangu Jesca ,nilichokiona kule hata sijapenda Jesca kamfanyia roho mbaya mfanya kazi wao wa ndani
“Samairah mwanangu haya nenda nyumbani nikirudi tutaongea vizuri” kisha mama akakata simu ,kumbe aliyemgonga ni mama yake na Samaira ,ambae samairah alitokea kumpenda huyo mama.
Na tukirudi nyuma ile ndoto ya bibi aliyemsimulia Aryan kuwa ameota mama mmoja kapata ajali ilikuwa ndoto ya ukweli ni mama yake na Aryan kapata ajali.
Tukirudi maeneo ya muhimbili mama aliwahishwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi alipokelewa kisha akaanza kufanyiwa matihabu, lakini mama yake Samairah ambae ndiye alimgonga alirudi kwenye gari na kuanza kulamba ile damu ya mama ambae ilidondoka kwenye siti ya gari.
Mama alilamba ile damu yote ,kisha akasema natamani nirudi katika hali yangu ila binti yangu nitamuachaje? Mama alitikisa kichwa kisha akawasha gari nakuondoka zake
Mama Samairah ni mtu wa aina gani hadi analamba damu za watu na anasema anataka kurudi katika hali yake.
Tukirudi maeneo ya mikocheni zile njemba baada ya kushidwa kumtoboa macho Aryan walirudi kwa akina Kudra na kuwaeleza kila kitu kwamba wameshidwa ile kazi ,Kudra alichukia sana na kuwaambia wakamtafute tena na kuhakikisha wanamtoboa macho Aryan,
Hatimae siku ijayofuata wakiwa darasani Mussa alisimama na kusema jamani nyie wasichana kama mnajipenda nione mtu anamfuata Aryan nitakachomfanyia kitu atajuta ,wasichana wote walitokea kumchukia sana Mussa ,Jesca alisimama na kusema mimi kwa Aryan hunitoi ntamfuata,,, tena pale pale Jesca alichukua kiti na kwenda kukaa karibu yake.
Jesca alimsogelea Aryan na kumnong’oneza “Aryan nakupenda kwanini hutaki kunisikiliza moyo wangu umekuchagua wewe ni samehe hata kwa mabaya yote niliyokufanyia niko tayari kufanya chochote kwa ajili yako”,,hayo ni maneno yake Jesca alitokea kumpenda sana Aryan ,ila tatizo Aryan huwa hawapendi wanawake.
Yale maneno ya Jesca yalimfanya Aryan asimame na kumwambia haya nimekusikia nitakujibu baadae kisha Aryan na akaondoka zake ,siku hio Jesca alijisikia amani baada ya Aryan kumwambia atamjibu baadae.
Tukirudi kwa Samairah alikuwa kajiinamia kwa mara ya kwanza alijikuta anaanza kumuwaza Aryan ,”ivi kwa mfano Aryan akiwa mpenzi wangu si itapendeza ee nikiwa njiani twashikana kikono nikienda kwao kujisomea twacheza” Samairah akajikuta anatabasamu.
Aryan baada ya kurudi tena darasani mwalimu aliingia na kuanza kufundisha basi Samairah aliingiza mkono kwenye dawati na kutoa daftari lake lakini kwenye begi aliweka ile bangili aliyopewa na mama yake Aryan
Ile bangili ilidondoka chini kengereee ,ile sauti ya mshido wa bangili baada ya kudondoka kila mwanafunzi akajikuta anageuza macho aliko Samairah
Hata Aryan aliangalia lakini Aryan alipoiona ile bangili alisimama na kuitazama vizuri,Aryan alijisemea ile bangili ya Samairah mbona inafanana na bangili yangu ninayoipendaga ,daa mama angekuwepo ningeenda kuiangalia sasa hata sijui mama alikoiweka ila inafanana sana.
Aryan alipotezea na kuendelea na masomo huku Samairah aliiokota ile bangili na kuiweka kwenye begi kisha masomo yakaendelea,hatimae walimaliza kipindi na muda wa mapumziko uliwadia
Jesca alikutana na Samairah kisha Jesca alimuuliza hivi Samairah ,”ushaniambiaga kuwa Aryan hana mama?” Samairah aliitikia ndio mama yake hajui aliko Jesca alitulia kidogo kisha akasema “ningejua mama yake aliko ningemfuata nimweleze kuwa nampenda mwanae halafu ningempenda mama yake na Aryan ningemnunulia mazawadi naimani Aryan nae angenipenda,,unaonaje wikiendi hii tuende kwa Aryan kujisomea maana wewe si uliniambia unapajua ,
Samaira alitulia kidogo na kumwambia sawa tutaenda halafu si unajua jumatatu tunaanza mitihani ee ,ila kuhusu mama yake na Aryan hata sijui nikushauri vipi maana we mwenyewe hupendi watu wa hali ya chini maana hata majuzi ulinishangaza ulivyomfanyia yule mama aliyekuwa anafanya kazi za ndani kwenu.
Jesca aliongea ,”aah lile limama silipendi tu halafu nishawahi kuliwekea hadi sumu nusu afe sema baba aliwahi kumpeleka hospitali ki ukweli yule mama mmmm silipendi sijui kwa nini sema baba alikuwa anampenda sababu anajua kupika ,nilikuwa nampiga hata makofi ,basi tu nilitokea kumchukia”.
Yule ndo mama yake halisi na Aryan na anasema halipendi lile limama halafu anamuulizia mama yake na Aryan ili awe anampelekea zawadi mi sijui akija kugundua kuwa yule ni mama yake na Aryan atafanyaje.
Siku hiyo Aryan alivyoona ile bangili alijikuta anakosa raha na kusema mama yangu angekuwepo ningefurahi mno halafu ile bangili yangu nishawahi kumwambia nitamvisha mwanamke ninayempenda,Aryan wakati anawaza alishangaa warembo wawili wanamgusa kichwa.
We Aryan mbona una mawazo ya nini bana jumamosi tunakuja kwako kujisomea alikuwa ni bibie Samairah wakiwa na Jesca ,Aryan alisema poa karibuni.
Hatimae wanafunzi waliruhusiwa na ilikuwa ni ijumaa walitangaziwa kuwa jumatatu wanaanza mitihani ya kufunga mhula wa pili ,wanafunzi walitawanyika lakini Samairah alimkimbilia Aryan na kumpa kibahasha flani ,Aryan alikipokea na kuuliza kina nini?
Samairah alimkabidhi na kusema utaona huko huko nyumbani ,Aryan alifika nyumbani aliangalia alikuta kuna noti mbili za elfu kumi Aryan alifurahi kama kawaida aliwasha jiko akapika kisha akamwamusha bibi wakala.
Usiku uliingia Aryan siku hiyo hakusoma alilala.
Aryan alianza kuota ndoto yupo ufukweni na bibie Samairah na wanafurahi kwa pamoja lakini wakiwa katika pozi la kukumbatiana , Aryan aligeuza macho nyuma aliweza kuona kundi la akina Kudra wamesimama nyuma yao halafu Kudra ameshika bastola na kumnyoshea,,Kudra alicheka kwa nguvu na kusema huyo Samairah ni mpenzi wangu nampenda kwakuwa wewe hunisikii wasalimie kuzimu Kudra aliinyoosha bastola kwa Aryan.
Aryan akajikuta anapiga kelele ,usiku kisha akainuka “aaah kumbe naota” duu ile anainua kichwa baada ya kutoka kwenye ndoto ukweli Aryan alishangaa kuwaona wanaume watatu wamesimama chumbani mwake ,.Aryan kucheki mlangoni
Mlango umevunjwa mara akamulikwa tochi kisha akaoneshwa shoka.
Tulipo ishia jana baada ya Aryan kuzinduka kwenye njozi alikuta njemba zimesimama tena zimeshika silaha za kijadi ,Aryan aliulizwa aseme kazi ya shoka.
Aryan kabla hajajibu jamaa mmoja alisema leo hatuna muda wa kupoteza kata shingo , Aryan alifumba macho yake baada ya yule jamaa kunyanyua shoka juu, kumbe baada ya kunyanyua shoka juu ,kwenye bati kulikuwa na nyoka katega kichwa chake kwenye ubao nyoka alitema mate kwa fujo wakati huo Aryan huyo kafunika uso
Vile vinyunyu vya mate viliwafanya wale watu wabaya waangalie juu,ni kosa kubwa walilofanya yule nyoka ndio aliongeza kasi ya kutema mate ,kila mmoja alijikuta anafumba macho yao na kusema “nyokaaa” lakini tayari macho yao yashaingia mate ya nyoka ,na nyoka mwenyewe ni yule mweusi,,
Kablaa hawajaa kaa sawa nyoka alimrukia mmoja kwenye shavu alimuuma,kawaida nyoka akiuma mtu lazima ajiviringishe ndo aachie meno yake sasa ,
Alivyomng’ata shavuni jamaa aliruka nje kisha wote wakatoka kila mmoja akijitetea uhai wake ,yule jamaa alitoka nae yule nyoka hatimae nyoka aliachia meno shavuni kwake,kwakuwa ulikuwa ni usiku na mbalamwezi ili pamba vyema walianza kumpiga yule nyoka hatimae wakamuua ,yule aliyeumwa sumu ilipokea haraka uso ukabadilika na kuwa na michirizi mieusii wale wengine wakataka waingie ndani wamuue Aryan lakini na wao sumu tayari ishapokea macho yakajaa machozi huku yanauma hata kuona hawawezi.
Kilichofuata walipiga mayowe kuomba msaada ,majirani walitoka upesi na kuja kuwashuhudia wakiwa wameanza kuvimba macho Aryan nae alitoka alishuhudia kuona wakipakiwa kwenye gari na walipoulizwa huku mlikuwa mnatafuta nini ,walisema tulipotea njia na tulivyofika hapa tulimkuta huyu nyoka tukaanza kumuua ndo katutemea mate namna hio ,
Walibebwa na kupelekwa hosipitani,
Lakini kabla ya kufika hospitalini hali zao zilikuwa tete walizidi kuvimba uso na macho kutoa machozi mfululizo ,yule aliyeumwa na nyoka alifika kwenye lango la kuingia hospitali alipoteza maisha,
Kiongozi wa hicho kikundi alimpigia simu Kudra na kumweleza yaliyo wakuta ,lakini aliongea kwa tabu sana kutokana na ulimi kuwa mzito baada ya sumu ya nyoka kuanza kumtawala , Kudra alimpigia Mussa walichukua gari hadi hospitali ya massana maeneo ya mbezi hakika waliwaonea huruma vijana walio wapa kazi ya kumuua Aryan ,aliyekufa sura yake ilibadilika na kuwa nyeusi kama yule nyoka huku wengine macho na midomo kuvimba hakika sura zao zilikuwa za kutisha,
Kudra alimvuta Mussa pembeni na kumwambia hii siri usimwambie mtu yeyote tumesababisha kifo ujue na mpaka dakika hii hawajafanikiwa hata kumgusa Aryan walau kumpa ngeu moja ,kinachonipa mawazo jumatatu tunaanza mitihani Aryan akitupita tena baba yangu hata nielewa ,Kudra aliongea maneno hayo huku akionekana kuchukia,Kussa alisema ,oya nimepata wazo ,hawa jamaaa kwakuwa tushawapa hela tayari na dili wamefeli sasa kinachotakiwa tuwaruke mita mia moja ,tuachane nao kwanza navunja laini tusiwe na mawasiliano nao halafu huyo Aryan mimi nitamuonesha adabu ,
Mussa aliongea hivyo kisha wakaondoka hospitali na kurudi zao majumbani,
Hatimae siku inayofuata , asubuhi na mapema Aryan aliamka akiwa mchovu alisafisha mazingira ya nyumbani maana alikuwa na taarifa za ugeni wa Jesca na Samairah watakuja ili waje kujisomea kwa pamoja ,hatimae Abbas nae alifika kwa Aryan , siku hiyo Aryan alimnunulia bibi vitumbua na uji akampa bibi akala huku Aryan yeye alienda kula mihogo ,
Aryan mjukuu wangu nimechoka kukaa ndani naomba unisaidie kunishika mkono unitoe nje nikaote jua ,bibi alimwita Aryan,
Haya nakuja bibi ,Aryan aliitikia wito aliacha kazi yake kisha aliingia ndani akatoa kiti nje kisha akaingia tena na kumshika bibi mkono alimtoa nje na kumkalisha vyema ,Aryan aliingia ndani akachukua kitenge na kumfunika bibi miguu ,kisha bibi akaendelea kupata kajua cha asubuhi.
Ilitimia mida ya saa nne bado akina Samairah hawajafika oya Aryan twende pale kwa mangi tukachukue maji ya kunywa si unajua leo tutakuwa na ugeni na watoto wakishua ,Abbas alimwambia Aryan ,
Aryan alitabasamu na kumwambia twende mtu wangu ,waliondoka huku wanapiga mastory yao.
Wakati wanakata tu uchochoro kuna jirani yake Aryan alikuwa anafua alipoona Aryan katoka aliwaita majirani zake na kuwaambia ,haka katoto siku hizi kana jifanya kidume ,tunakaambia kamfukuze huyu bibi ni mchawi hataki kuelewa ona jana usiku watu wameua nyoka hapa mlangoni mwao ,tumeishi miaka mingi hatujawahi ona nyoka sasa leo huyo nyoka katoka wapi ,alisema mama mmoja ambae mwili wake ni mnene,,
Kabla hajamaliza mama Ashura alichukua beseni la mapovu alimwagia yule bibi usoni pwaaa ,masikini bibi wawatu bila kosa anakuta analowanishwa na mapovu ,bibi alipangusa mapovu usoni na kuita Aryan mjukuu wangu nani huyo ananimwagia mapovu ,kabla bibi hajakaa sawa kuna mama mmoja alitoka na sufuria lenye maji machafu sijui alikuwa anaosha sufuria la ubwabwa,
Alikuja kumwagia maukoko ugali maharage ambavyo vyote vilikuwa kwenye matope ,bibi akajikuta analowa ,kibaya zaidi maji aliyomwagiwa yalikuwa yanatoa harufu bibi alinuka mbaya,
Mara bajaji iliingia na kufunga breki kwenye mlango wa akina Aryan walishuka watoto wawili wakike wamewaka mbaya sana si wengine ni bibie Samairah na Jesca marashi yao waliyojipuliza yaliwafanya majirani watoke kuja kuangalia ni nani huyo kapita, wale wamama walio mmwagia bibi mapovu walitoka ,na kuwashangaa warembo akina Samairah,
Wakati huo bibi anaita Aryan njoo nishike mkono niingie ndani ,Samairah alishangaa kumwona bibi aliwahi na kumshika mkono ,Samairah hakujali aliita bibi kisha akamshika mkono na kuanza kumwingiza ndani ,japo bibi alikuwa ananuka mbaya maji aliyomwagiwa na wale majirani
Bibi aliuliza wewe nani ? Samairah alijitambulisha mimi naitwa Samairah rafiki yake Aryan,kwani Aryan kaenda wapi na akina nani wamekumwagia mapovu ,Samairah aliuliza pindi alivyomwingiza bibi ndani ,bibi aliinamisha kichwa chini na kusema mjukuu wangu ,hii dunia tu nimemwagiwa mapovu bila kosa ,kwanza nishazeeka baasi tu ni hivyo ,
Mara Jesca alimfuata Aryan akiwa amefumba mdomo ,Jesca aliuliza we Samairah ,,Aryan ndo anakaa nyumba chafu libibi lake libaya hapa mimi sikai wala sisomi bibi lenyewe lichafu mmmmh.
Kama ni hivi narudi nyumbani ,
Ni maneno aliyoongea Jesca na kumfanya bibi agune mmmm kisha akamuuliza uko na nani wewe mjukuu ,Samairah alimwambia bibi niko na rafiki yangu tu ,tumekuja kwa Aryan hapa kwa ajili ya kujisomea ,
Samaira alirudishia mlango ,kisha akamvua bibi zile nguo zilizochafuliwa na mapovu ,alivyomaliza aliangalia pembeni aliona gauni ,Samairah hakujali alimvalisha gauni lingine bibi kisha akachukua zile nguo zilizochafuliwa na kwenda kuzifua
Jesca alivyoona hivyo alimwambia we Samairah unakichaa nini yaani unashika minguo ya huyo mbibi mmmm zinanuka hivyo bibi mwenyewe mbaya nimemchukia bure kwanza hapa hapanifai kwaheri naondoka zangu ,msalimie Aryan akija tu ,ila siwezi kusoma na yule bibi akiwa yupo hapo
Kwanza mazingira ya hapa mabaya yananuka mikojo halafu mie nishazoea majumba ya mageti niwashe feni nisome kwa raha ila hapa mmmmmmm siwezi, Samairah aliuliza kwahiyo waondoka ?
Jesca alijibu ndio na kusema mimi nampenda Aryan tu siwezi kaa mazingira haya kwaheri
Hakika Jesca alijishebedua kisha akapanda bajaji waliokuja nayo kisha akarudi na kumwacha Samairah
Samairah aliendelea kufua zile nguo za bibi ,alivyomwangalia bibi aliona akidondosha machozi taratibu huku ameinamisha kichwa chini,
Tulipo ishia jana baada ya Jesca kuondoka na Jesca aliongea maneno makali mno,alipanda bajaji na kuondoka zake ,Samairah aliendelea kufua nguo za bibi zilizochafuliwa lakini alivyogeuza kichwa kumwangalia bibi ,alishangaa kuona akidondosha machozi.
Samairah aliacha kufua 1na kwenda kwa bibi alisogea karibu wala hakumnyanyapaa alimshika mkono bibi na kumuuliza bibi kulikoni mbona walia?,kabla bibi hajaongea chochote Samairah aliupeleka mkono kwenye shavu la bibi na kumfuta machozi wakati Samairah akiendelea kufuta machozi ya bibi Aryan na Abbas walirejea ,
Samairah umekuja ,? Mambo ,Aryan alisalimia kwa uchangamfu huku akimtupia bibi macho ,Samaira alijibu poa ,kisha akasimama Aryan aliuliza mbona bibi analia amefanyaje?
Samairah alisita kusema ukweli kisha akamwambia hebu muulize wewe Aryan maana mie nimekuja hapa nimekuta amelowanishwa mapovu ,halafu nimekuta majirani zako wanamcheka ,bibi alikuwa anakuita wewe ndipo mimi nikamshika mkono na kumwingiza ndani nikamvua nguo zake na kuanza kuzifua.
Aryan taratibu alimsogelea bibi ,kisha akaita bibi kulikoni mbona walia?bibi taratibu aliinua kichwa na kusema ,nalia kwa uzee wangu ,upofu wangu ,huenda ningekuwa na macho ningeshuhudia mengi ,kuna msichana yupo hapo nje jamani kaongea maneno mazito sijui itakuwaje na yeye akizeeka ,maana uzee kila mtu ataupitia kama Mungu atajaalia maisha marefu.
Abbas aliuliza msichana gani yupo nje ,Samairah alidakia na kusema Aryan naomba unisamehe mimi ,nimekuja na rafiki yangu Jesca hapa alivyomuona bibi katika hali ile alivyolowanishwa mapovu ,basi akaongea maneno makali kisha akasema yeye hawezi kukaa mazingira haya karudi zake nyumbani.
Aryan akauliza kwa kuhamaki kweli Jesca alikuja hapa? Ndio Samairah alijibu ,Aryan alimshika bibi mkono na kumwambia inuka nikupeleke chumbani ,bibi wala hakubisha aliinuka kisha akaingia chumbani ,
Aryan alitoka lakini bibi alimwita Aryan njoo, Aryan akarudi bibi alimuuliza huyo msichana ni wawapi ambae kanisaidia kutoa nguo nilizolowanishwa ,Aryan alikaa kimya kidogo kisha akasema ni rafiki yangu nasoma nae.
Haya kajisomee nakuombea mfaulu wote wajukuu zangu kisha bibi akajilaza kitandani ,Aryan alitoka kisha wakaingia chumba cha Aryan akakuta Samaira na Abbas washaanza kusoma ,ndipo na yeye akajumuika walianza kujadili baadhi ya topiki kwa pamoja.
Lakini siku hio Samairah alikuwa watofauti alikuwa anamwangalia Aryan usoni kichwani kisha akajisemea moyoni we Aryan ni handsome jamani ,ona anavyoongea ,ona mdomo wake ,macho yake mazuri ,yote hayo yalikuwa mawazo ambayo bibie Samaira akiwaza ,
Mara mlango uligongwa ,Aryan alisema ingia sukuma mlango uko wazi ,kaliingia katoto ,kalivyoingia Aryan alisema aaah Gwae nakuona ona mapengo yako mabaya ha ha Aryan alimtania Gwae ,
Gwae alikuwa ni mdogo wake Abbas mwenye umri wa miaka mitano kama si minne alikuwa anapengo meno ya juu yalikuwa yameng’ooka ,basi alivytabasamu Samaira aliona lile pengo alimpiga Aryan kangumi kadogo kwenye bega na kumwambia bana Aryan usimtanie mtoto hilo jina la mapengo sio zuri,
Gwae alisalimia shikamoo aunt,alimsalimu Samaira ,Samaira akaitikia na kumuuliza unaitwa nani ,Gwae alicheka na kusema naitwa Gwae ,”jina zuri kama ulivyo wewe Samaira alisifia ,
Kisha akauliza ehe Gwae unasemaje?
“Mama kanituma nije nimwite Abbas anataka akamtume kunduchi , mara Abbas akadakia daa maza nae sasa anataka kunituma tena ,jamani kwaherini nikirudi ntakuja tuendelee kusoma
Haya Gwae twende mdogo wangu ,Abbas aliongea kisha wakaondoka ,sasa chumbani walibaki wawili Aryan na Samairah wakaendelea kusoma ,Aryan alikuwa anafanya hesabu ,Samairah basi alikuwa hasikilizi hata kidogo yeye mawazo yake yalikuwa yapo mbali ,
Alianza kuwaza kimoyo moyo,Aryan nakupenda si uniguse tu hata mkono nipate joto lako? Sasa wewe uko bize na mahesabu yako ,ona macho jamani natamani hata busu lako
Mara Aryan alimwangalia Samairah usoni , macho yao yakagongana ,basi Samaira ashampenda Aryan vibaya mno ,mtoto alizifumba mboni zake alikuwa kakaa kitandani halafu kajilaza chali ,
Aryan hakuelewa alishituka na kusogea mahali aliko aliita Samairah nini kimekupata? Samairah alikuwa kimya huku moyoni mwake akiwaza Aryan si uniinue walau uniguse tu mwili wangu.
Aryan alimsogelea na kumshika mashavu alimtikisa huku anaita Samairah,,Aryan nae alipanda kitandani kisha akamwinua na kumlaza mapajani mwake ,huku akiita Samairah ,
Samairah alitabasamu kimoyo moyo akajisemea mambo si ndo hayo alikuwa kavalia sketi fupi sana alivyoipandisha miguu kitandani basi mapaja yake yalionekana meupe pale pale Aryan alivyopiga jicho ,aliona mapaja nae hisia flani zilianza kumwingia
Alimgusa tumbo na kutikisa huku akiita Samairah.
Samairah aliyafumbua macho yake na kucheka na kusema Aryan nilikuwa nakupima je mfano nikipata tatizo utanisaidia? Aryan alitabasamu na kusema kwanini nisikusaidie ,basi mtoto wa kike alirembua na kujisemea kimoyo moyo ulivyonigusa kwenye mashavu nilisikia raha.
Mara simu ikaita kwenye begi la Samairah ,nani huyo ananipigia tena Samairah aliinuka ,kitendo cha kuinuka na kushuka kitandani Aryan aliangalia kiuno cha bibie kilivyokaa vizuri kisha akasemaa aaah wanawake bana.
Samairah alitoa simu kwenye begi kisha akapokea haloo Jesca unasemaje ,upande wa pili simu ilisikika mtu akilia Jesca alisema ,huku sauti yake ikiambatana na kilio ,Samairah nipo huku maeneo ya kunduchi nimetekwa na yule bajaji aliyetupeleka kwa Aryan hivyo nakuomba uje unisaidie maana nampigia mama yangu na baba simu zao hazipatikani.
Kabla Samairah hajajibu bangili ile ambayo Samairah alidondosha darasani ,leo tena ikadondoka na Aryan akaiona Samairah alikata simu na kusema haya nakuja , Samairah akaiokota ile bangili kisha akarudisha kwenye begi.
Aryan akauliza Samairah hio bangili hebu nione? Samaira aliitoa kisha akampa Aryan akaiangalia ,Aryan alianza kuwaza hii bangili mbona inafanana na yangu ambayo nilishawai kuiokota baharini na nilisema nikitokea kumpenda mwanamke nitamvalisha hii bangili ,
Aryan alimrudishia na kusema hii bangili inafanana na bangili ambayo mama yake anayo ,
Kisha Aryan akauliza kwani hii bangili yako umeipatia wapi? Samairah alitabasamu na kusema nimepewa zawadi hivyo naipenda na naitunza.
Sasa Aryan naomba unisindikize maeneo ya kunduchi Jesca kanipigia simu kasema katekwa na dareva wa bajaji ,Aryan aliuliza Jesca huyu ninae mjua ama , ndio Samairah alijibu ,
Kwanini waenda kumsaidia ,Samairah alishusha pumzi kisha akaongea” Aryan yule Jesca ni rafiki yangu halafu mimi ndio nimemchukua kwao na kumleta huku sasa unafikiri akipata matatizo wazazi wake watanielewaje si watasema mimi ndio nimeshirikiana na hao watu”
Okay sawa haya twende ,walitoka na kuacha begi ,walichukua bajaji safari ya kuelekea kunduchi, Aryan alimuuliza Samairah swali ,”hivi yule anae kujaga kukuchukua na gari shuleni ni baba yako?
Samairah alitabasamu na kusema Aryan we nawe huyo si baba yangu ,huyo ni dereva wangu ,mama ka mwajiri kwa ajili ya kunipeleka shule na kunirudisha ,
Ooh mi najuaga ni baba yako ,Aryan aliongea ,na kumfanya Samairah akae kimya kwa muda kisha akaongea.
Aryan mimi sina baba nina mama tu , baba yangu waligombanaga na mama ,hivyo baba yangu ameendaga mbali , na hatoweza kurudi ,maneno ya Samairah yalimfanya Aryan akumbuke hata yeye baba yake ashafariki sasa Samairah nae kasema baba yake kaenda mbali Aryan alisema huenda hata baba yake kafariki.
Hatimae walifika kunduchi mahali waliko elekezwa walifika na kukuta geti jeusi waligonga wakiwa wanasubiria kufunguliwa Aryan aliuliza lakini Samairah unakurupuka kwanini tusingeenda kutoa taarifa polisi sasa unahisi sisi tutaweza kutoa msaada?
Samairah alitabasamu na kusema Aryan mie najua kupiga ngumi tofauti na unavyonifikiria wewe ,nyumbani huwa nina mwalimu ananifundisha masho art hivyo naweza kupiga ngumi mbaya ,Samairah aliongea huku anacheka maana yeye muda wote huwa anacheka.
Baada ya muda geti lilifunguliwa na kijana mmoja mweusi mwenye sura yakikauzu ,aliongea mnatafuta nini? Samairah aliongea rafiki yangu kaletwa huku niambie yuko wapi ,
Yule jamaa alicheka kisha akamshika Samairah mkono na kumvuta akaingia ndani halafu Aryan akampiga teke , Aryan alidondoka chini ,
Kosa moja alilofanya yule jamaa alimpiga Aryan teke maeneo ya kifuani ambako ana ugonjwa wa kupoteza kumbu kumbu,
Aryan aliinuka huku akisikia maumivu makali
Aryan alijikongonja na kukaa kwenye kivuli cha mti huku akiugulia maumivu makali kifuani
Aryan alijiuliza hapa kwani nipo wapi ,masikini tayari kumbu kumbu zake zimepotea.
Tukija ndani baada ya Samairah kuchukuliwa na yule jamaa alimkunja mikono kwa nyuma na kumfunga kamba hatimae alimwingiza ndani ya ile nyumba ,
Ilikuwa nyumba ambayo imeezekwa bati lakini kuta zilikuwa bado hazijasakafiwa.
Ndani kulikuwa na sauti ya kilio cha bibie Jesca ,hatimae Samairah nae aliingizwa ndani kisha akasukumizwa kama mzigo, Samaira alienda kudondoka na mdomo na kufanya damu ianze kumtoka mdomoni ,
Kisha yule jamaa alimwinua na kusema sasa wewe umejileta mwenyewe ,wewe nitakufaidi peke yangu halafu huyu mwenzako atabakwa na hawa jamaa watatu ,
Samairah aliinua kichwa akawaangalia wale vijana kisha akamwangalia Jesca ambae kapigwa uso umevimba na nguo yake kuchanwa alimwonea huruma.
Samairah alicheka kisha akawaambia hivi nyie watu mnajipenda ? Ama hamjipendi.
Yale maneno ya Samairah yaliwakera wale vijana ndipo mmoja aliinuka na kusema we demu unatupima eee sisi alimtandika Samairah ngumi ya usoni Samairah alidondoka chini
Puuuuh!
Samairah alianza kuwaza kimoyo moyo ,”mama ulisema nisitumie nguvu zangu vibaya lakini nitajikomboa vipi hapa pasina kutumia uwezo wangu mama utanisamehe leo navunja masharti uliyoniwekea nimechoka kuona watu wakionewa.
Pale pale Samaira alijikaza kamba alizofugwa mkononi zikakatika akainuka taratibu ,macho yake kwenye kile kiduara cheusi kilionesha alama ndogo nyekundu.
Samairah alisema mwachieni rafiki yangu ,yule jamaa aliyempiga ngumi Samairah hadi akadondoka alikunja ngumi tena na kusema wewe demu hujafunzwa adabu na wahuni mnajifanya watoto wakishua ee sasa ngoja ucheki shoo
Alirusha ngumi Samairah alikuwa mwepesi aliikwepa taratibu jamaa alienda mzima mzima kupiga ukuta.
Uwiiii sauti ya kilio ndio ilisikika mkono wake ulivunjika mara tatu kibaya zaidi hadi mfupa ukatokeza kwa nje
Halafu Samairah alimshika Jesca mkono na kuanza kumfungulia kamba.
Ndipo vijana wengine wawili wakazuia mlangoni
Tulipo ishia jana baada ya Samairah kukwepa ngumi ya yule kijana na kumfanya yule kijana aende moja kwa moja hadi ukutani na kuupiga ngumi ukuta ,ni sauti ya maumivu makali ndio aliyoitoa akilia baada ya mkono wake kuvunjika mara tatu,
Samairah alimwendea Jesca alianza kumfungulia kamba, lakini vijana wengine wawili walizuia mlangoni na kusema we demu hapa hutoki ,yaani unasababisha jamaa yetu anavunjika mkono ehee hapa leo utajijua ,
Jamaa mmoja alitoa bomba la sindano na kumwambia we demu unaona hii ,nakuchoma halafu nakutia dawa ambayo itakulegeza mwili ndani ya dakika moja na utakuwa kama huyo rafiki yako,
Samairah alimtizama Jesca ambae kalegea mwili mzima akiwa amejilaza kwenye kiti huku mikono yake imefugwa ,Samairah aligundua kuwa hawa watu sio wazuri ni wabaya kupita maelezo ,alizidi kuangalia mazingira ya pale aliweza kuona begi la Jesca likiwa pale chini ,
Tayari alifanikiwa kumfungua Jesca lakini Jesca hakuwa na nguvu mwili wake wote ulikuwa umelegea na macho yake aliyafumba ,tukirudi nje ya ile nyumba Aryan alikuwa bado akiugulia maumivu makali kwenye kifua huku kumbukumbu zake zimepotea ,Aryan kila akijitahidi asimame ili aondoke akajikuta anayumba na kujisikia kizungu zungu kikali ,
Kwa mbali kulikuwa na watoto sita wasio zidi umri wa miaka sita ama saba walikuwa wakicheza mpira wakipita eneo ambalo Aryan aliko ,
Katoto kamoja kaliongea we Jimmy kasimame kwenye ule mti karibu na yule kaka halafu nikupigie pasi ndefu tuwe tunarudishiana tuone nani atapoteza nafasi ,
Jimmy alikubali na kusema sawa Dani ila usipige pasi kubwa sana maana wewe unabutuaga mpira ukija kuingia kwa nyumba za watu itakuwa sio poa,
Wakati huo Aryan anajikakamua kuinuka mara Dani akapiga mpira shuti kali ili kumpasia mwenzake Jimmy,,ule mpira ulienda kwa kasi sana na kupita juu juu ,Jimmy alijaribu kuruka ili audake hakufanikiwa ule mpira ulienda moja kwa moja na kutua kifuani kwa Aryan paaah
Aryan alidondoka na povu likaanza kutoka ,tambua Aryan ugonjwa wake wa kupoteza kumbu kumbu ukimpiga kifua anapoteza kumbu kumbu ili uzirudishe lazima umpige tena kifua ,ki undani bado hatujajua yale maradhi kayapataje ila tunavyozidi kusonga mbele tutaelewa ,
Aryan alidondoka chini na kupoteza fahamu kabisa ,alianza kukoroma huku povu jeupe likitoka mdomoni ,wale watoto walivyoona vile ,
Jimmy alisema Dani ,umeua mkaka wawatu ,wale watoto waliwahi na kwenda kumwangalia Aryan walikuta akikoroma huku povu likitoka mdomoni ,rafiki zake Dani walianza kukwambia Dani umeua Dani umeua ,
Dani aliwaambia hapa tukimbie tuondoke lasivyo tukikamatwa ujue tutapelekwa gerezani wale watoto walichukua mpira wao na kuondoka walikimbia ,
baada ya dakika tatu alirudi katika hali yake ndipo kumbu kumbu zake zikarejea
Alianza kukumbuka nilikuja na Samairah hapa sasa kaenda wapi ,mmmh hebu ngoja nikagonge lile geti sijui ndo aliingia hapo ,wakati Aryan anaenda kugonga lile geti ndani yake ya hiyo nyumba.
Yule jamaa alieshikilia bomba la sindano yenye sumu ya kulegeza alimsogelea Samairah “we demu tokea tumeanza kazi za kuteka watu kama ninyi watoto wakishua tuna miaka zaidi ya mitatu sasa wewe leo ndo umenishangaza hebu mwangalie rafiki yetu amevunjika mkono hadi mfupa kuchomoza kisa wewe hakia nani kitu ambacho tunakufanyia utaenda kusimulia ,halafu sisi tuna kambi zaidi ya mia ,tukiteka mtu tunampeleka sehemu mbali mbali usifikirie ni rahisi kutukamata
Sana wacha nikudunge hii sindano kwanza ulegee halafu tukufanyie kitendo cha kinyama
Samairah alimwangalia yule kijana kisha akasema we kijana ungejua mimi ni nani walahi usingejisumbua na ungeomba msamaha mara dufu ,yote hayo bibie Samairah alijisemea kimoyo moyo ,kisha Samaira akasema
Mimi sitaki kupigwa wala kufanyweje nasimama mimi mwenyewe nidunge hio sindano yako ,yule jamaa alisema oya Rama huyu demu analeta ushua kwenye anga za wahuni mkabe , Rama alimrukia Samairah na kumkaba mikono Samairah wala hakuhangaika kujitoa alitulia tuli ,yule mwanaharamu aliishika sindano yake na kumdunga Samairah maeneo ya shingo sindano aliizamisha cha ajabu Samairah hakushtuka alitulia tuli ,yule jamaa alibinya lile bomba na kusukuma sumu ambayo itamlegeza Samairah
Samairah baada ya dakika moja aliachiwa na kudondoka chini ,wakati huo Jesca hali yake bado iko vile vile hajitambui ,yule jamaa aliyevunjika mkono alitoka nje ,sijui aliita bajaji na kuwahishwa hospitali ili akapate matibabu kwanza ,
Wale wenzake waliobaki Rama alitoa mkanda wa suruali na kufungua zifu alivua suruali na kubaki na boxer
Oya shedi hapa hatuna muda wa kupoteza nishikie miguu mie nijilie vitu ,kabla hajakata moto maana ile sumu ni kali halafu mtoto mkali hapa nitapata joto safi ,Rama aliongea huku akipanua miguu ya Jesca ,
Shedi alimuinamia Samairah na kutaka kuanza kumvua nguo huku wakijua tayari sumu ishaanza kufanya kazi
Samairah alianza kuwaza kimoyo moyo ,hawa watu leo ndio itakuwa mwisho wao kufanya upuuzi huu wakati anajifanya kalegea na dawa aliangalia pembeni aliona chupa ya soda ,alijivuta upesi akaishika wakati huo shedi kainama anahangaika kumvua nguo ,alichokifanya Samairah alimpiga nayo kwenye usoo paaa
Ile chupa ilipasukia usoni paaa vipande vya chupa vilipasua uso wa shedi Samairah alikuwa mwepesi mno aliserereka chini huku mkononi kashika vipande viwili vya chupa baada ya ile chupa kupasuka ,alimkita maeneo ya siri Rama kwa nguvu
,Rama alipiga ukunga wa nguvu huku mikono yake kaibana kwenye sehemu za siri alidondoka kama gunia
Samairah alishika tena kipande kingine cha chupa kisha aliruka akadanki kwenye ukuta akakikita kile kipande cha chupa kwenye shingo ya shedi
Halafu akamkonyeza vipi maumivu yake unayasikiaje ,maana wewe umenidunga sindano na haijanidhuru sasa wewe hapo sikilizia usipo wahishwa hospitali unakufa nimekata mshipa wa fahamu ,
Samairah alimwangalia na Rama ambae kadondoka chali damu zinamtoka kwenye sehemu za siri
Samairah alishika shingo mahali alikodungwa sindano alibinya ,
Sumu ilitoka nyeusi kisha akatabasamu na kusema hakika binadamu wanapenda kujiingiza kwenye matatizo
Samairah alimnyanyua Jesca ambae kalegea na wala hajitambui ,Samairah alianza kuwaza hivi Jesca atakuwa kaona kitu kilichotokea na je Aryan akigundua kuwa mimi si binadamu wa kawaida atanielewaje ? Na sielewi ameanza kuingia kwenye moyo wangu ,yote mawazo yalikwa kichwani mwa Samairah alimkokota Jesca hadi walivyotoka nje ya geti walimkuta Aryan amekaa baada ya kugonga geti kwa muda mrefu hakupata msaada aliamua kukaa
Aryan aliita Samairah umemuokoa Jesca aaah umefanyeje? Halafu mbona Samairah yupo katika hali hii,Samairah alitabasamu na kusema amedugwa sindano yenye sumu hivyo tumuwahishe hospitali , Aryan alimsaidia Samairah kumbeba Jesca hadi barabarani walichukua bajaji na kumpeleka Jesca hospitalini ,
Lakini walivyofika maeno ya mbezi afrikana Jesca alizinduka na kurudi katika hali yake . Aliyafumbua macho na kujikuta ameegemea kwenye bega la Aryan ,tena Aryan alimshika maeneo ya tumbo ili asidondoke maana alikuwa kazidiwa na dawa
Jesca kuona amelala kwenye bega la Aryan alianza kuwaza kumbe mimi mzuri ee ona Aryan amekubali kunilaza kwenye bega lake jamani raha ,huyu mkaka mzuri nampenda,,
Si apandishe mkono anishike na kifuani yale yote ni mawazo ya Jesca baada ya kuzinduka ,
Alifanya makusudi akajilaza kabisa kifuani mwa Aryan wakati huo wapo kwenye bajaji ,mara Samairah alimwangalia Jesca alikuta ametabasamu na amejilaza kwenye kifua cha Aryan ,sijui wivu umeanza kili ,Samaira alimwinua jesca na kumuegemeza kwenye siti ,jesca alivyo na makusudi akajilaza kabisa kwenye mapaja ya Aryan.
We Jesca si umeshazinduka hebu kaa vizuri ,Samairah alimwinua ,Jesca alipikicha macho yake akasema nikijilaza kwenye miguu ya Aryan nasikia raha ,Samairah alimwambia hebu acha zako ,
Hapo ndipo Aryan akagundua kuwa Jesca ameshazinduka ,alimshika mkono na kumwambia “unajisikiaje? Kitendo cha kumshika mkono Jesca ndo anasikia raha alitabasamu na kujisemea najisikia vizuri huku anaupeleka mkono wa Aryan kifuani mwake
Aryan alitoa mkono upesi na kumwambia dereva wa bajaji apaki bajaji kuwa yeye anataka kurudi nyumbani ,
Samaira wataka kurudi nyumbani? Aryan alitikisa kichwa na kusema ndio nataka kurudi nyumbani nimechezwa na machale nahisi bibi nyumbani hayuko sawa
Aryan alishushwa na bajaji kisha akachukua pikipiki ili arudi.
Nyumbani ,sasa tukirudi maeneo ya tegeta mahali anako ishi Aryan leo akina Mussa na Kudra waliwasili maeneo haya huku wakiongozana na mtu ,
Kudra “huyo Aryan unae msemea wewe anaishi katika nyumba hii na mlango umefugwa yawezekana ametoka ,Kudra aliangalia nyumba kisha akasema kama tulivyozungumza pitisha hio petroli kwenye hio nyumba halafu tupige njiti nyumba nzima iwake , akikosa mahali pakukaa hata weza kwenda kufanya mtihani na atafanya sisi turudi katika nafasi zetu
Akina Kudra walikuja na mtu walimpa kazi amwagie nyumba anayoishi Aryan petroli halafu waichome lengo lao Aryan asiweze kwenda kufanya mtihani ,
Yule jamaa aliangalia huku na kule hapakuwa na watu alimwaga petroli upesi walivyomaliza walichukua kiberiti waliwasha njiti kisha wakaitupia mlangoni waliwasha piki piki na kuondoka upesi ,
Mussa alijisemea hapa hatakuwa na ujanja tena nguo za shule zikiungua moto na madaftari hata weza kwenda tena shule waliondoka zao
Moto uliwaka maana petroli na moto ni vitu vinavyoshabihiana, nyumba ilianza kuwaka kumbe ndani ya nyumba bibi alikuwa amelala
Baada ya ule moshi kuingia ndani bibi alianza kukohoa ,kibaya zaidi bibi ni kipofu na Aryan hayupo ,, watu walijaaa na kusema moto jamani moto wenyewe wako wapi ,
Majirani wala hawakuhangaika kuuzima moto ndo kwanza wamesimama na simu zao wanarekodi video jinsi nyumba inavyo waka
Bibi alihisi kifua kina mmbana baada ya moshi kutanda ndani
Tulipoishia jana baada ya kundi la wenye roho mbaya akina Mussa na mwenzake Kudra waliweza kuichoma nyumba ya akina Aryan,kisha waliwasha piki piki na kukimbia ,walijisifu kwa kufanikiwa kuwasha ule moto,bibi ndani alipata moshi mzito alianza kukohoa kwa fuju ,lakini sauti yake haikusikika kutokana na moto kuzidi kuwaka ,akina mama Asharua na mama bonge ambae ni majirani zake na Aryan wao ndio walikuwa wakwanza kusema moto jamani moto,
Walisimama na kushika viuno hamna aliyesema waingie wajaribu walau kuokoa mali za Aryan ,
Mama Ashura alisema jamani yule bibi ambae simpendi mungu kasikia kilio changu sijui huu moto umetokea wapi leo huyu bibi ataungua ngoja nikae kabisa nisikie kichwa chake kitakapopasuka paaa aliongea kisha wakacheka na rafiki yake mama kibonge ,watu walizidi kujaa ,wengi wakisema jamani nyumba ndo inateketea hivyo ,mjumbe wa nyumba kumi nae alifika na kusema nini chanzo cha moto ,kila mmoja alisema hatujui ,
Mjumbe aliuliza sasa yule kijana yuko wapi? Mama Ashura alijibu katoka zake siku hizi anajifanya kakua ameenda kutafuta mademu ,ha ha ha ,watu walicheka huku wakiangalia nyumba ikiungua.
Masikini hali ya bibi ndani ilizidi kuwa tete alishindwa kuhema na kujikuta akitapa tapa ,bibi alijaribu kupaza sauti walau kuomba msaada lakini sauti yake haikufanikiwa kusikika maana alikuwa anashidwa kuita sababu ya moshi kutanda ,
Bibi alijikongonja lakini hata mlangoni hakufanikiwa kufika bibi alipoteza fahamu akadondoka
Moto nje na ndani ukazidi kupamba moto ,yaani baada ya bibi kutoka kwenye kile chumba tu kuna kuti lenye moto lilidondokea kitandani kagodoro kalishika moto na kuanza kuwaka
Mlio wa piki piki ulisikika hatimae Aryan alifika nyumbani alikuta mlangoni moto umepamba moto ,masikini Aryan aliita kwa nguvu bibiiiiiiii bibiiii nani kayatenda haya Aryan aliuliza kwa sauti ya juu lakini kila mtu alimcheka mama Ashura alidakia Aryan mimi nipo hapa nasubiri kichwa cha bibi kilipuke ,
Daaah Aryan alitazama mazingira ya hapo nje aliona ndoo ya maji alichukua akajimwagia kisha akaingia ndani huku akiita bibi ,bibiii watu walimkataza asiingie ataweza kufia huko lakini Aryan alizama ndani alimkuta bibi kadondoka chini ,
Wakati Aryan kazama ndani huku nje akina Samairah na Jesca nao wanaingia na bajaji sijui nini wanakitafuta lakini walivyokuta moto umewaka waliuliza Aryan yu wapi
Mama Ashura alitabasamu na kusema Aryan anakitafuta kifo kaingia ndani kutoa msukule wake ule mjibibi , Jesca alisimama mbali na kusema aka na uzuri wangu huu niungue aku ,sitaki mwenzangu,
Samairah nae aliangalia pembeni aliweza kuona kibeseni chenye mapovu ambacho mchana wake alifua nguo za bibi alivyomwagiwa maukoko ,Samairah mtoto mrembo hakujali uzuri wake alijimwagia yale mapovu kisha akazama ndani ,huku akiita Aryan Aryan ,
Alimkuta Aryan yuko sebuleni anahangaika kumnyanyua bibi ili amtoe nje lakini kwakuwa alikuwa peke yake basi alijikuta anakosa namna ya kufanya ,Aryan aliingia chumbani kwake alichukua begi la Samairah ambalo aliliacha mchana ,kisha akaenda kwa bibi ,bibi alifumba macho na kukata tamaa.
Aryan nae moshi ulimzidi kisha akakosa pumzi Aryan alimkumbatia bibi na kusema tutakufa wote,akiwa kapoteza tumaini alishangaa kumwona mtoto wa kike Samairah kanyoosha mkono ,Samairah alimshika Aryan kisha akamwinua alivyofika mlangoni alimsukumiza kwa nje Aryan alidondoka nje na kupoteza fahamu akiwa kakumbatia begi la Samairah
Samaira akiwa kafunika uso wake kaziba kitambaa kwenye pua na mdomo aliingia kwenye chumba cha Aryan alichukua madaftari na nguo za shule baadhi na nguo za Aryan alirusha nje kupitia dirishani
Samairah alimwendea bibi alimnyanyua japo mzito alianza kutoka mdogo mdogo nae alianza kukosa pumzi Samaira moshi ulizidi kumlewesha akajikuta anaanza kuyumba kabla hajadondoka mtaalamu Abbas nae alikuwa ashatia timu ,Abbas alimshika bibi akamtia mgongoni huku mkono mmoja kamshika Samairah mkono,Abbas alijikuta anawatoa wote kwa pamoja
Ile wanatoka tu nyumba ilianguka mabati yakiwa yamewaka moto,yakaangukia mahali bibi alikuwa amelala ,Abbas alivyowatoa Samairah na bibi ,ndipo bibie Jesca alikuja na kumwangalia Aryan ambae anahema juu juu ,alimtizama usoni na kujisemea
Asante mungu handsome wangu hajafa yuko hai lakini kwanini Samairah kamuokoa yule mbibi angemwokoa tu Aryan wangu ninaempenda ,alitoa kitambaa na kuanza kumpepea Aryan
Mama Ashura alikunja sura baada ya kuona ,bibi katoka salama ,
Nyooo ule mbibi umetolewa naona sijui umekufa sijui umezimia kwanza washanikera ngoja nikaepue maharage yangu
Mama Ashura alichukia mno aliondoka na kusema sasa hivi tuone wataishi vipi nyumba hawana imeungua ,mama Ashura ile anaingia kwake tu alipokelewa na kofi zito
Paaaa we mwanamke mshenzi yaani unaacha maharage yanaungua unaenda kushangaa nyumba inaungua hata msaada hamkutoa unapiga tu porojo ,ni maneno ya mume wake ,
Hivi unajua hela zinavyotafutwa? Nakuuliza kwanini umeunguza maharage ,baba Ashura nisamehe ,kabla hajamaliza baba Ashura alivua mkanda alianza kumpiga kama punda uwiiii nakufaaa ,jamani mume wangu nisamehe alianza kupiga kelele za kuomba msamaha lakini hadi watu wanafika walikuta ngeu usoni zimesimama na dera limechwanwa paja moja la kulia lipo nje ,
Mama bonge alimshika mume wake mama ashura na kumbananisha kwenye ukuta na kumwambia
Wewe jiangalie ukirudia tena ntakunyonga lini mwanamke akapigwa kama punda ,alimwachia baba Ashura,ndipo baba Ashura hakukaa tena nyumbani akaondoka zake na kumwacha mkewe akilia
Tukirudi upande wa pili Samairah alikuwa wakwanza kuzinduka alivyofumbua macho alikuta Abbas anamwagia maji kichwani Samairah alitikisa kichwa alivyoyatupa macho kwa Aryan aliweza kumwona akipepewa na bibie Jesca ,yaani Jesca anajikuta anajisahau kupepea na kuanza kuwaza ,Aryan ngoja nikuguse kifua nikupepee lakini Samairah aliweza kufika na kumwekea maji kichwani Aryan alizinduka
Ndipo walikaa kwa muda wa nusu saa ndipo bibi nae alizinduka wote walinusurika ,bibi alijikuta amekumbatiwa mkono ,bibi aliita Aryan mjukuu wangu ,”naam bibi niko hapa ,bibi alitikisa kichwa na kusema watu wabaya dunia haina kosa hata kidogo ,Aryan alimwangalia bibi ambae nywele zake zimekuwa nyupe baada ya kupitishwa kwenye moto, ,Aryan alimwangalia Samairah ambae alikuwa tayari ashavaa lile bangili ambalo alipewa na mama yake Aryan,ila yeye hajui kama ndio mama yake na Aryan ,
Watu waliondoka na kuwaacha akina Aryan baada ya kuona wametoka salama hawakuwapa hata msaada wa mawazo walitawanyika ,Aryan aliangalia madaftari yake aliangalia na nguo zake za shule ,
Aryan aliwaambia Samairah, Abbas na Jesca mimi shule basi tena naacha sina mahali pa kuishii sina hata hela ya kurudishia nyumba ya mama yangu ,Aryan alianza kulia na kuita mama ,mama mwanao nateseka alilia kwa uchungu mno.
Samairah alimwambia Aryan usiseme hivyo nitajaribu kwenda kuongea na mama kama ataweza akusaidie walau hela ukapangishe chumba tumalizie mitihani baada ya muda kidogo kuna piki piki ilikuja wakashuka watu watatu ,
Wakiwa wanacheka ha ha ha wewe si ulijifanya mjanja unapendwa na wanafunzi sasa basi tuone itakuweje
Kumbe walikuwa ni akina Mussa na Kudra walimcheka sana Aryan ndipo Samaira aliwaambia Kudra nyie ndo mmehusika na kuchoma nyumba ya akina Aryan ,Kudra alicheka kwa dharau na kumwambia Samaira tumeanza na Aryan tutamalizia na kwako si unajifanya unaringa na huo uzuri sisi ndo wababe .
Waliwasha piki piki wakaondoka ,Aryan alimwangalia Abbas akamwangalia Samairah pamoja na Jesca Aryan alisimama na kusema shule siachi hata kama ntalala mtaroni ntaenda tu ,
Yale maneno yalimfanya Jesca amkumbatie Aryan kisha akataka kuupeleka ulimi kwenye lips za Aryan ,Samairah alifumba macho ili asione kinachoendelea maana hata yeye anampenda Aryan mbaya ,
Ila Aryan alikwepesha na kumwambia Jesca hapana,Jesca alimkaba Aryan shati na kumwambia Aryan naomba unipe jibu langu toka majuzi hujanijibu swali langu nambie kama unanipenda kama hunipendi niungane na akina Mussa.
Daah Jesca alivombana Aryan namna hio ,Aryan alikuwa na hasira sana alitabasamu na kumwambia usijali bado nafikiria ,Jesca alimwambia juma tatu unipe jibu kama hutaki kuwa na mimi nijue cha kufanya ,lakini Aryan ningependa unieleze mama yako yuko wapi ,maana nikimpata mama yako ataweza kunisaidia kukueleza ili unipende kama mimi ninavyokupenda ,au huyu bibi ni mama yako ,
Aryan alikaa kimya na kumwambia mama yangu sijui aliko ,Jesca alisema pole ntakusaidia kumtafuta ,mama aliyekuzaa handsome wangu ,maneno ya Jesca yalimfanya Samairah kukosa raha maana hata yeye anampenda Aryan
Mara bibi akadakia ,” we binti muongeaji sijui waitwa nani ,yaani katika hii dunia hamna mwanaume atakae kupenda kwa mdomo wako wenye maneno machafu ,afadhali huyu binti hata mimi nimempenda toka moyoni ,bibi alimtaja Samairah amempenda na si yeye.
Sehemu Ya 2
Jesca aliamka na hasira we mbibi ushajizeekea unaniambiaje alitaka kumpiga kofi lakini Samairah aliudaka mkono wa Jesca wakati huo Aryan anashuhudia
Mara gari aina ya prado ikaingia ilipaki pale mahali akina Samairah waliko wakati huo Aryan alitoka kidogo kwenda msalani
Alishuka mama mmoja aliita Jesca ,
Jesca aligeuka nani huyo anamwita alishangaa kumwona yule mama ambae alikuwa anafanya kazi za ndani kwao ambae ndiye mama halisi wa Aryan,
Mara mama yake na Aryan alimwona Samairah alimkimbilia na kumkumbatia ,mama akiwa na furaha aliuliza wewe binti nimetokea kukupenda ulisema unaitwa nani vile ,
Kabla Samairah hajajibu
Sauti nyingine ilisikika ikiita mwanangu Samairah unatafuta nini huku?
Alikuwa ni mama yake na Samairah ambae ndiye alimgonga na gari mama yake na Aryan
Samairah aliita mama niko kwa rafiki yangu,Abbas nae aliita Aryan kwa nguvu ,njoo uone maajabu ya leo.
Aryan anafika pale anamwona mama yake amekumbatiana na Samairah ,Aryan nae alikimbia na kumkumbatia mama yake huku analia
Pale pale Jesca alisema Mungu wangu kumbe huyu mama nilikuwa namtesa ni mama yake na Aryan uwiiiii
*****
Tulipo ishia jana baada ya mama yake na Aryan kukutana na mwanae ,Jesca aliwaza haaa kumbe huyu mama nilimtesa alivyokuwa anafanya kazi za ndani nyumbani ni mama yake na Aryan,uwiii ,mungu wangu je akimwambia Aryan yale mateso ambayo nilikuwa namfanyia Aryan atanielewaje ,
Pale pale alisogea pembeni alimpigia simu baba yake kisha mazungumzo yakaanza
” baba naomba umrudishe yule mama ambae alikuwa anafanya kazi hapo nyumbani na mshahara mlipe hata laki tano baba naomba ufanye hivyo lasivyo mwanao ntakuwa kichaa ,we Jesca una nini leo yule mama si ashaondokana sijui aliko ,Jesca alijibu niko nae huku tegeta au ile nyumba ya mbezi naomba umpe huyo mama lasivyo mwanao ntakuwa chizi ,baba yake Jesca alishindwa kuelewa mwanae ana nini.
Jesca hebu rudi nyumbani uje unieleze vizuri ,Jesca alitoroka pale pale hakumwaga hata Samairah wala Aryan alitafuta piki piki na safari ya kwenda sinza ilianza.
Aryan baada ya kumkumbatia mama yake na kumweleza majanga waliyopata nyumba imeteketea ,mama Aryan alimwambia Aryan nimekuja na mgeni huyu hapa ndio alinigongaga na gari bahati mbaya namshukuru Mungu sikuumia sana akanihangaikia matibabu hatimae nikapona ndipo akanileta na gari hadi nyumbani ,
Aryan anageuza macho amwangalie huyo mama ni nani ndipo nyuso zao zilipogongana na kugundua ndio yule mama ambae alishawahi kununua karanga maeneo ya mwenge ,pia alimnunulia na chakula ,leo hii wamekutana tena ,Aryan alishidwa kujizuia na kumkumbatia yule mama huku akitoa shukrani zake za dhati ,,yule mama alivyomwangalia binti yake aliweza kuona ile bangili na ile bangili anaijua.
Mama aliita Samairah hio bangili umetoa wapi hebu niione ,Samairah kabla hajajibu mtu ambae alimpaga aliitoa na kumwonesha mama yake mama yake na Samairah kosa moja alilofanya ile bangili aliishika na mkono ambao ulikuwa umevalia pete inayofanana na hio bangili.
Unaambiwa miale mikali ilitokea na kuingia machoni mwa Aryan ,Aryan alidondoka chini puuuu,huku akilia kwa uchungu ,kumbe ile bangili haikuwa ya kawaida na mama Samairah na mwanae sio binadamu wa kawida.
Miale ikizidi kubadilika miekundu bluu njano na iliingia kwenye macho ya Aryan ,mama yake na Aryan alikimbilia mahali aliko mwanae lakini kila akijaribu kusogea alishidwa anajikuta anarudishwa kulizidi kutokea nguvu za ajabu ,
tukirudi nyuma kidogo kwenye vipande vya story vilivyopita baada ya mama yake Samairah alivyomgonga mama yake na Aryan na alivyompeleka alirudi kwenye gari ,alilamba ile damu ambae ilidondokea kwenye siti
Leo tutajua mama Samairaha na mwanae ni akina nani na hio bangili ina kazi gani.
Mama Aryan alizidi kulia huku akiita mwanangu mwanangu wakati huo Abbas na Jesca washaondoka,wamebaki wanne tu na ilikuwa tayari ishatimia saa moja usiku.
Mama Samairah kila akijaribu kuitupa ile bangili iling’ang’ania pale ilivyogusana na pete ,mionzi mikali iliingia kwa Aryan,
Pale pale Aryan alipoteza fahamu
Radi zilizidi kupiga kwenye pande kuu za dunia ,mashariki magharibi ,kaskazini na kusini ,
Upepo mkali ulivuma
Mama Samairah alimwambia mwane mfunike mama yake na Aryan macho upesi
Samairah alimfunika mama yake na Aryan macho ,ndipo mama Samairah alianza kubadilika na kuwa kiumbe wa ajabu mama Samairah alizidi kutoka pembe moja ndefu kwenye paji la uso huku akifuka moshi mzito kwenye mdomo wake.
Mama Samairah ule moshi ulianza kupaa hewani na kutengeneza mistari ya rangi mbili ,bluu na kijani ambayo sawa na ile bangili mama Samairah alisema asante mwanangu umefanikisha kunirudisha niliko toka nakuacha mwanangu baki kwenye hii dunia lakini bado niko na wewe leo hii naenda kukutana na baba yako nimepata njia ya kurudi nilikozaliwa.
Mama Samairah alipotea alifuata ule moshi ambao ulitengeneza mistari miwili pale ndipo bibi alifunguka macho yake na kuweza kuona vizuri, bibi alisimama na kuuliza naota ama ni kweli ivi kweli naona ee
Wewe binti mbona umemkumbatia huyo mama macho ,Samairah baada ya kuambiwa vile na bibi alimwachia mama yake na Aryan ,mama hakuelewa chochote aliuliza yule mama yako ameenda wapi,?
Samairah alitabasamu na kusema kaondoka hivyo naomba tumbebe Aryan tumwingize kwenye gari kisha niwapeleke kwenye nyumba mpya kuanzia leo mateso yenu yameisha ,
Samairah alivyoangalia chini aliona ile bangili aliichukua na kuivaa ,
Samairah baada ya kumpakia Aryan alimpandisha na bibi kisha na mama yake na Aryan ,Samairah aliwasha gari ,ndipo alisikia sauti ikimpa maelezo na ile sauti ilikuwa ya mama yake ,
“Samairah najuwa wewe ni binadamu ambae una asili ya kijini naomba uhakikishe hao watu wanaishi maisha mazuri ,naomba uwapeleke mbezi kwenye ile nyumba yetu mpya,
Samairah aliwasha gari hadi maeneo ya mbezi alifika alipiga honi mlinzi alifungua geti kisha gari ikaingia ilikuwa ni nyumba ya kisasa mlango ulifunguliwa na mdada wa kazi kisha Aryan aliingizwa hadi kitandani akiwa hajitambui , Samairah alionekana si mgeni wa hiyo nyumba alienda chumba flani alitoa chupa ambayo ilikuwa na maji meupe alimimina machoni mwa Aryan na kifuani.
Ndipo pale Aryan alianza kuota ndoto “ilikuwa siku ya juma mosi Aryan akiwa na baba yake ,baba alimwambia mwanangu twende leo bahari inatoa utajiri nimeoteshwa ndoto ,Aryan alimuuliza baba ,sasa baba bahari itatoaje utajiri?
Baba alicheka na kusema mwanangu hii story ya bahari kutoa utajiri ni yatoka enzi na enzi ni pale inapotokea mwezi kuvutana na jua na leo imetokea hivyo tukienda baharini tutapata utajiri ,
Aryan alikubali aliondoka na baba yake walifika baharini ndipo walikuta watu wengi wapo baharini wanasubiri kupata utajiri ,siku hio ilikuwa ya tofauti kabisa tofauti na miaka ya nyuma.
Miaka ya nyuma ikitokea kupatwa kwa mwezi basi ukienda baharini utakutana na vito vya thamani lakini leo hii tumekuta na bahari ikiwa na mawimbi makubwa ,
Watu wengi wakiwa wamejaa baharini ,Aryan akamuuliza eti baba hawa watu nao wanasubiri utajiri? Ha ha ha baba alicheka na kusema ndio mwanangu hawa wote wanasubiri utajiri maana leo bahari inatoa utajiri ,lakini baba mbona watu wote wapo wakubwa huku na hakuna watoto wadogo kama mimi kwanini umenileta?
Aryan aliuliza , baba alikaa kimya na kusema mwanangu huu utajiri unaweza ukawa wakweli ama wauongo maana bahari huwa na tabia ya kumeza watu hivyo ikitokea hivyo basi mwanangu naomba uhakikishe unamtunza mama yako na ukikua na wewe usije ukafuata hizi mila ,
Basi siku hio mida ya saa tano mwezi ulianza kupigana na jua ,ila wanasayansi wanasema kupatwa kwa mwezi ,jua lilianza kumeza mwezi ndipo giza lilianza kutanda baba alimkalisha mwanae mbali kabisa na bahari ndipo yeye alisogea kwenye kingo za bahari ili kuangalia kama bahari itarusha madini ama vito vyenye thamani.
Aryan akiwa anamwangalia baba yake akiungana na watu wengine baharini ,Aryan aliwaza ina maana hawa watu wote wakiwa matajiri dunia itakuweje ,lakini wakati anawaza.
Yalitokea mawimbi makubwa ambayo yaliruka hewani na kwenda kuwakumba watu wote ambao walikuwa wamesimama pembezoni mwa bahari wakisubiri utajiri
Ila siku hio ilikuwa ya tofauti watu wote walimezwa na bahari kisha wakazamishwa ndani,
Aryan alisubiri kwa muda huenda atamwona baba yake lakini hakutokea ndipo alipo tokea ndege mzuri mwenye rangi ya blue pamoja na kijani alikuja na kukaa mbele ya Aryan akiwa mdomoni na bangili aliiacha ile bangili kisha akaruka na kutokomea mbali ya upeo wa macho ,
Aryan aliinuka na kuokota ile pete aliipenda kisha alitokea kumpenda yule ndege
Aryan alichukua ile pete na kuiweka mfukoni cha ajabu baharini hapakuwa na njia baada ya wale watu kumezwa na bahari alitokea mama mmoja alionekana akiwa makini akitafuta kitu alipita mahali aliko Aryan lakini hakumwona Aryan,,,,,ila Aryan yeye alimwona alitizama na kusema yule ndege alitua hapa sasa hio bangili iko wapi ,aliitafuta hakuiona ,Aryan alitaka kusema bangili hii hapa lakini kinywa kilikuwa kizito
Hatimae taarifa zilisambaa watu kumezwa na bahari wakiwa wanasubiria kuona utajiri ,Aryan alilia sana baada ya baba yake kutotokea alirudi nyumbani na kumkuta mama yake anaumwa akiwa hoi
,,,Mama mama amka nini tatizo Aryan alimwita mama yake lakini alitoa ile bangili alivyoiweka kitanda cha mama ,Aryan alishuhudia kitanda kikivunjika changa paaa
Mama alidondoka Aryan kwa kuwa alikuwa mdogo alihangaika kumwinua mama yake ,hata hivyo mama nae alijaribu kujikakamua alisema anahisi kifua kimebana
Aryan alimwangalia mama yake kisha akasema mama pole ila nimeokota hii bangili nimeipenda aliiweka kifuani mwa mama yake ndipo mama
Alikohoa kwa nguvu alitoa mwanga mdomoni wa rangi ya bluu na kijani kama rangi ya ile bangili
Ule mwanga uliingia kifuani mwa Aryan na ndipo toka hiyo siku alipata huo ugonjwa wa kupoteza fahamu,”
Turudi upande wa pili kwa Jesca alivyofika nyumbani alikuwa akilia akisema mama baba leo nakuwa chizi Aryan wangu ,namtaka yule mama mmupe hata nyumba Aryan hana nyumba.
Yale maneno yaliwachanganya wazazi wake na Jesca ndipo baba aliuliza unanini? Jesca alipita hadi sebuleni kufika sebuleni
Alibaki mdomo wazi baada ya kuwakuta Kudra na Mussa wamekaa kwenye masofa wameshika visu
Tulipo ishia jana baada ya Jesca kufika nyumbani aliongea na kuonekana kama amechanganyikiwa lakini alivyo tupa macho kwenye masofa aliwaona Kudra pamoja na Mussa wakiwa wamekaa kwenye mikono yao wameshika visu,
Jesca alishituka kidogo kisha akajisogeza hadi waliko akina Kudra na kuuliza kwa upole ,Kudra na Mussa ehe nambie mmefuata nini?
Kudra aliachia kisu kwa dharau kisha akasema “Jesca haiwezekani uaibishe familia yako elewa baba yako na baba yangu ni marafiki inawezekana vipi umpende yule choko ,kinachoniuma eti Mussa humtaki ,halafu baba yangu kasema msimu huu wa mitihani ataenda kuhonga walimu ili sisi watatu tufaulu kwenye mtihani”
Jesca aliwaangalia kwa umakini na kuwauliza kwa nini mmechoma moto nyumba ya akina Aryan ,Mussa alidakia na kusema aaah sisi tuchome moto ili tufaidike nini ,sisi hatuja choma moto ,tulipata taarifa kwenye mitandao kisha tukafika na kuja kushuhudia ,Jesca alikaa kwenye kiti na kusema nikweli baba yako atatoa hela ili tufaulu au mnanidanganya,Kudra alisema sasa tukudanganye ili iweje ,ndio hivyo kama upo tayari useme halafu tupange misheni nyingine,
Jesca alitulia na kusema yaa nakubali ila wakitoa hela waambie waniweke mimi niwe wa kwanza halafu wewe Kudra wapili halafu Mussa watatu vipi hapo si itakuwa poa
Wote waliitikia na kusema ndio itakuwa poa ,”lakini mwalimu Farida jioni nilipita kwake kanambia wanafunzi watatu wa shule ya makongo wamehamia kwetu halafu wote wakike na inasemekana wana akili mbaya,
Jesca kwa mshituko alisema haa wale wadada wamehamia sijui akina Nanaa ,Lusi na nani mwingine , Mudra alisema na Joyce
Okay tutawakalisha msijali sisi tunatumia pesa halafu wao wanatumia akili ,Mussa alisema ,unajua kale kaboya Kiaryan kinajiona kina akili,, baada ya kuanza urafiki na Aryan sasa tunataka tuunde misheni tutakula dawa ya unga utapaka kwenye kitambaa kabla ya kuingia kwenye mtihani utamziba mdomoni akishavuta ule unga , akiingia darasani atasinzia tu ,hivyo akijibu swali moja atalala ,na akilala sisi ndo tunapata nafasi ya kufaulu ,
Jesca alishangilia na kupiga makofi akasema hapo bomba ,kisha akina Kudra waliaga na kuondoka zao ,walimwacha Jesca na mama yake ,Jesca alianza kumuhadithia mama yake “mama yule mmama ambae alikuwa anafanya kazi hapa kumbe alikuwa mama yake na Aryan kijana ninayempenda kuliko kitu chochote ,mama kama kuna uwezekano tumrudishe hapa ili aje afanye kazi halafu mmlipe mshahara mkubwa ,hapo ndipo atamshauri mwanae awe mpenzi wangu ,
Au tuwanunulie nyumba ,maana hawana nyumba ya kuishi,mama Jesca aliwaza ,mmmh mwanangu sikufichi yule kijana sidhani kama ataweza kuwa mpenzi wako maana kwa unyama uliomfanyia yule mama sidhani ,
Yale maneno ya mama yake Jesca yalimfanya Jesca akose amani basi Jesca aliondoka na kuingia ndani chumbani kwake
,tukirudi maeneo ya mbezi kwenye jumba la kifahari baada ya kukumbuka matukio ya nyuma jinsi alivyookotaga ile bangili alizinduka huku akiita mama mama’
Alikurupuka alivyogeuka alimkuta mama yake amejiinamia ,mama alisogea na kuushika mkono wa mwanae kisha akamwinua
Aliita Aryan uko salama? Aryan akiwa anahema alijibu ndio mama lakini nimeota ndoto mbaya sana ,
Mama alimwambia pole mwanangu
Aryan aliuliza hapa tuko wapi? Mama alitabasamu na kusema mwanangu hapa tuko mbezi na hii ni nyumba mpya ambayo tumepewa na mama yake Samairah ,lakini huyo mama kasafiri Samaira alinambia , Aryan aliuliza na bibi yuko wapi ,
“Bibi yuko sebuleni anaangalia tv ,mama alisema na kufanya Aryan acheke ha ha haaaaa mama sasa kipofu anaangaliaga tv ama anasikiliza ,mama alisema anaangalia nenda utamwona,
Aryan aliinuka na kuelekea sebuleni alimkuta bibi kakodolea tv anaangalia move ya kilio changu ,
Aryan alijua labla bibi haoni ,alisimama mbele yake ,bibi alisema Aryan umeamka mjukuu wangu kaa pembeni usinikinge naangalia tv ,pale Aryan alichoka ndipo alipouliza bibi sasa hivi kwani unaona?
Bibi alitabasamu na kusema sijui nimejikuta naona macho yangu yalifunguka sijui baada ya kupata moshi mwingi ndo yakaamua yaone ,Aryan alicheka na kusema kweli haya maajabu.
Ki ukweli Aryan ,bibi na mama yake hawajui kitu chochote kilichotokea ila ukweli kamili Samairah anaujua na mpaka sasa Aryan hajagundua kama Samairah si binadamu wa kawaida ,
Aryan alishangaa kukuta nyumba ina mfanyakazi wa ndani getini mlinzi yupo ,ilibidi aulize ,mama sasa hii nyumba tumepewa kivipi maana sijaelewa ,mama alisema hata mimi sijui ila Samairah ameondoka kasema kesho ndio atatueleza vizuri.
Basi Aryan alirudi kwenye chumba chake aliwasha taa na kujisemea leo hii taa inawaka ntasoma hadi kieleweke na sasa sina mawazo tena nimempata mama yangu sasa ivi ni mwendo wa kusoma ,
Aryan alishika kitabu cha jografia lakini kila akifungua topiki anajikuta anaijua ,yote sasa hadi akawa anajishangaa na kusema kumbe watu wanao soma kwenye umeme wanakuwa na akili ivi Aryan aligairi kusoma na kusema kesho kitaeleweka huko huko ,
Asubuhi yake alizivaa nguo zake za shule kisha akatoka getini alianza kutembea mdogo mdogo ,ile anafika geti la shuleni ,Aryan alishangaa mabinti watatu warembo kupitiliza na walikuwa ni wageni machoni mwake ,
Walimkimbilia na kwenda kumkumbatia huku wakitaja jina Aryan Aryan Aryan ilibidi aogope inawezekana vipi wanafunzi wageni wajue jina lake.
Mimi naitwa Joyce nimehamia hapa shuleni kwenu toka shule ya makongo kiukweli hongera siku ile uliimba wimbo mzuri niliupenda ” Joyce aliongea huku akimgusa gusa mikono Aryan
Mara mwingine akadakia mimi naitwa Nanaa ,naomba nikupokee hicho kitabu halafu leo si ndo tunafanya mitihani ee ,Aryan alisema yaa tunafanya mitihani kisha aliondoka hakutaka kuweka nao ukaribu
Lakini wakati anapiga hatua mbili tatu Aryan alishangaa anashikwa mkono alivutwa kidogo kugeuka alishangaa kumwona Jesca mtoto kaweka lipstick kapendeza mbaya ,Aryan alimkazia jicho na kumwambia nini unataka ,Jesca aliyakwepesha macho yake na kujisemea “Aryan toka mwanzo nakupenda ila wewe hutaki kunielewa halafu leo ninazawadi ya mama yako ,baadae ntakupa” ,
Aryan alimwambia sawa baadae kisha akaondoka ,ile anataka kuingia darasani alikutana na kundi la akina Mussa wamesimama kati kati mlangoni , Aryan alisalimia mambo zenu ,akina Mussa walikausha Mussa alitoa bisi bisi kisha akamwambia oya we boya unaona hii leo lazima izame mwilini mwako kisha akarusha ngumi nzito ambayo ilimpata Aryan maeneo ya kwenye paji la uso.
Uwiiii jamani mkono wangu ni kelele za maumivu Mussa alipiga baada ya kumpiga Aryan aliteguka vidole vyote lakini Aryan wala hakuumia aliondoka zake na kwenda nje ,
Hatimae muda wa kuingia darasani uliwadia Aryan kila akiangalia hamuoni Samairah ,mara Abbas akaja ,”vipi ndugu yangu umemuona Samairah” Aryan aliuliza
Abbas alitabasamu ndio Samairah nimemuona yupo zake kidato cha kwanza amekaa zake kimya , kengele iligogwa wanafunzi walikusanyika mstarini mwalimu alisimama na kuwatambulisha akina Joyce,Nanaa na Lusi na kuwaambia kuwa ni wanafunzi wapya wamehamia kwenye shule yetu.
Wakati wanafunzi wote wapo mstarini Kudra aliwasili akiwa na baba yake waliingia ofisi ya mkuu wa shule.
Baba yake akawa anamaongezi ya siri na mkuu wa shule ,mzee alitoa bahasha tatu zikiwa zimejaa hela ndipo mzee akaongea ,mkuu wa shule nina vijana watatu nataka mhula huu waongoze majina yao yapo kwenye hizo bahasha na bahasha zipo na pesa za kutosha milion moja.
Mkuu wa shule baada ya kusikia kiwango cha pesa kwanza alitabasamu na kusema hilo ondoa shaka wataongoza wala usijali
Baba yake Kudra aliaga na kuondoka ,
Mkuu wa shule aliziangalia zile pesa akajisemea moyoni matajiri mnahangaika sana kama mtoto hana akili si ukubali tu ,kisha akaziweka zile pesa kwenye droo.
Wanafunzi walianza kuingia kwenye madarasa Jesca alitoa kitambaa cheupe ambacho kilikuwa na sumu ya unga alimfunika Samairah kwa sekunde tatu kisha akakitoa
Akina Mussa na Kudra waliona kisha wakamkonyeza Jesca yess kazi nzuri.
Kudra alisema sasa hapa ndio msimu wangu kule mzee ashamaliza kwa mkuu wa shule na haka ka Samairah kanajifanya kana akili leo katalala tu darasani.
Samairah alielewa mchezo alivyoingia darasani aligawiwa karatasi ya maswali na majibu ,alimwangalia Aryan mahali aliko aliona Aryan yuko bize anajibu.
Samairah alijibu mtihani ndani ya dakika kumi ashamaliza maswali yote,tambua Samairah anauwezo wa ajabu ,alivyomaliza alilala
Sasa akina Mussa na Kudra walianza kukonyezana na kusema yeees tumemuweza ,Samairah alijifanyisha anaushingizi lakini ile sumu haikumdhuru hata kidogo.
Hatimae walipo maliza mtihani walitoka nje ,Jesca kwa mbwembwe alimuuliza Samairah mbona ulikuwa umelala? Samairah alimwambia hata sikuelewa nilijikuta na usingizi
Vipi umemaliza mtihani ,Jesca aliuliza ,Samairah alikaa kimia kwa muda kisha alianza kuwaza.
Jesca huna wema nilikuokoa ulivyotaka kubakwa halafu unataka kunifanyia hivyo ila kwangu umechemsha alimjibu hata sijui kama nimemaliza.
Aryan wakati anatoka kwenye mtihani ,alitoka na kwenda kukaa nyuma ya madarasa alishangaa kumwona mrembo Joyce anakuja na kukaa karibu yake ,Aryan vipi mtihani umeuonaje ,Aryan alisema mbona wakawaida.
Joyce macho yake yalikuwa kwenye uso wa Aryan alimwangalia na kusema hakika wewe ndiye mwanaume wakipekee nani kakupa huu mvuto? Mtoto alianza kuwaza mwenyewe mara Jesca nae alitia timu bila hata kuuliza alimpiga mtoto wa watu na jiwe kichwani kisha akaongea nyie wapuuzi mmehamia kwenye shule ili mnichukulie mpenzi wangu hapa hapati mtu,
Masikini Joyce alianza kujihisi kizungu zungu huku damu zinamtoka kichwani alijaribu kuinuka akajikuta anayumba ile anataka kudondoka mtaalamu Aryan aliwahi na kumdaka ,
Ile anamdaka Joyce ,Mussa nae alitia timu ,aliitoa bisi bisi na kutaka kumchoma Aryan
Masikini bisi bisi ilienda moja kwa moja na kuikita kwenye paja la bibie Joyce ,
Joyce alipiga kelele za maumivu jamani nakufaaaaa.
Tulipoishia jana baada ya Mussa kutaka kumchoma bisibisi Aryan,ila kwa bahati mbaya ilimkuta bibie Joyce kwenye paja lake ,Joyce alipiga makele ya uchungu ,huku akiomba msaada jamani nakufa ,nakufaa mie ,walimu na wanafunzi walikimbia na kuwahi nyuma ya shule ,ndipo walishangaa kumwona msichana aliyehamia shule ndo kwanza anasiku moja tayari kaumizwa damu zimeenea mwili mzima ,Mussa wala hakukimbia alisimama pale pale ,ndipo Aryan alitoa maelezo kwa mkuu wa shule ,
Mkuu washule alitoa kauli moja ,we Mussa nifuate ofisini ,kisha akaanza kupiga hatua kuelekea ofisini ,huku,mwalimu wa biology akimchukua Joyce na kwenda kumpatia huduma ya kwanza.
Mussa wewe ni mtoto wa mzee Obote yule tajiri? ,mkuu wa shule aliuliza hilo ,swali ,Mussa kwa kujiamini alijibu ndio ,huku akionesha kiburi ,mkuu wa shule alitabasamu ,aliongea ngoja nimpigie baba yako simu,mkuu wa shule alibonyeza vitufe kadhaa vya simu yake baada ya muda kidogo simu ilipokelewa na mazungumzo yalianza ,
Haloo Mr Obote ,ni mimi hapa mkuu wa shule anaposoma kijana wako Mussa ,upande wa pili sauti nzito ilijibu ,ehe kuna tatizo gani,”mkuu wa shule aliendelea kuongea ,mtoto wako kapiga mwanafunzi mwenzake ki sheria hilo ni kosa kubwa hivyo mtoto wako tunamfukuza shule,
Mr Obote alikohoa kidogo kisha akasema mkuu kwanini unataka kufanya hivyo naomba tufanye yaishe hapo hapo shuleni haina haja ya mimi kuja ,nakutumia laki sita sasa ivi kijana wangu aendelee kusoma ,
Ha ha ha ,mkuu wa shule alicheka huku mkono wa kushoto anagusa gusa kitambi chake alisema ongeza laki moja iwe laki saba ,Mr Obote nae hakubisha alisema sawa ,
Baada ya muda kidogo simu ya mkuu wa shuke iliingia sms ,mkuu wa shule aliitizama simu yake na kuona m-pessa ,alitabasamu alivyohakikisha kuwa pesa imetumwa alimruhusu Mussa akatoka na kwenda darasani kuendelea na mitihani .
Zilipita siku kadhaa baada ya tukio la kuumia kwa Joyce ,huku Aryan kila akimtafuta Samairah waongee ,Samairah alikataa na kusema hajisikii vizuri,ukaribu wa Samairah ulimfanya Aryan kujiona na yeye ni mtu kati ya watu lakini alijikuta anakosa furaha baada ya Samairah kukataa kata kata kuongea nae.
Hatimae walimaliza mitihani Aryan alimfuta Samairah na kumshika mkono,Aryan alimuuliza Samairah kwanini hutaki kuongea na mimi ni kitu gani nimekukosea? ,Samairah hakujibu chochote zaidi ya kudondosha machozi ,kisha akamwambia Aryan niache niende ila ipo siku nitakuambia yanayo nisibu,Aryan hakuwa na la kufanya alimwachia Samairah akaondoka,
Samairah alianza kuwaza ,”Aryan nakupenda lakini kila siku unakuwa kwenye matatizo najaribu kukaa mbali nawe ili nisione ukionewa ,maana nahofia kutumia hasira zangu na kuwadhuru wengine ,.Aryan najua nakupa wakati mgumu ila nitakueleza kwa undani zaidi ,pia ninachohofia muda sio mrefu utapoteza mtu ambae unaukaribu nae na hupendi apotee ila atapotea,”
Samairah alifuta machozi yake kisha akabeba begi lake na kuondoka zake moja kwa moja hadi nyumbani.
Tukija maeneo ya tegeta tunamuona mdogo wake na Abbas ambae anaitwa gwae , alivyotoka shuleni na wenzake moja kwa moja alirudi nyumbani mida ya saa nane ,lakini siku hiyo hakumkuta mtu yeyote nyumbani,
Gwae mwenye umri wa miaka mitano alilitizama kufuli mlangoni ,kisha akashika tumbo lake,alishangaa utumbo wake ukiunguruma kwa fujo yote hayo chanzo ni njaa alikuwa kakabiliwa na njaa mno ,
Mtoto mdogo alikaa pale uani hadi ilivyofika saa kumi jioni alihisi mwili kulegea na njaa
Gwae alianza kuwaza sasa mama kaenda wapi halafu leo hajanipa hela ya kula shuleni nimerudi nyumbani hayupo ,,gwae alibidi aondoke hapo nyumbani hadi kwa mama Ashura akiwa na rafiki yake Rashidi ambae walikuwa wanasoma darasa moja ,
Rashidi ,”mimi nimeenda nyumbani sijamkuta mama yangu sijui kaenda wapi halafu nasikia njaa ,gwae aliongea huku midomo yake kuonekana kukauka yote sababu ya njaa,Rashidi alimuuliza kwani kaka yako Abbas anarudi lini “gwae alitizama jua na kusema huyo hadi jua lizame ,
Gwae alitizama kwa mama yake na Rashidi mama ambae anajulikana kwa jina mama Ashura aliona akipakua wali ,gwae alijikuta akimeza mate na kutamani walau autie kinywani,
Hazikupita dakika mbili ,
Mama Ashura alimwita mwanae ,Rashidi ,njoo ule mwanangu ,Rashidi aliitika naam mama nakuja ,Rashidi alimwambia rafiki yake gwae twende tukale mama yangu tayari ashapakua ,
Gwae alitabasamu maana alikuwa amebanwa mno na njaa halafu kwa umri wake mdogo alikuwa kachoka ,gwae alianza kumwelezea Rashidi ,mimi sijui mama yangu kapatwa na matatizo gani ,jana usiku hata hajatupikia yaani kaja kapika uji bila sukari halafu akasema kunyweni kama hamtaki acheni ,
Mama aliondoka usiku huo huo ,hata sijui wapi kalala natamani hata baba yangu angekuwepo najua angeninunulia maandazi na kachori ,ki ukweli gwae alikuwa mdogo lakini alikuwa na akili sana.
Wakati huo Rashidi na gwae waliingia kwa mama Ashura walikuta kapakua sahani moja ,
Kisha aliweka chini kwenye mkeka ,Rashidi alichukua maji akanawa mikono kisha akampa na gwae anawe ,ile gwae anaanza kunawa mama Ashura alishika bakuli la kunawia mikono kisha kwa sauti ya juu akaongea.
We we we mtoto koma hapa hamna kula ,nasema kale kwenu ,we mtoto inuka kale kwenu ,mama Ashura alimtimua gwae ,Rashidi alidakia na kusema mama mwache ale amesema anasikia njaa halafu mama yake hayupo ,
Rashidi kabla hajamaliza alipigwa kofi zito na mama yake ,masikini Rashidi alilia ,,kitendo cha kulia ndio alizidi kumchokoza mama yake ,
Mama Ashura alishika mpini wa jembe na kusema Rashidi nakupasua kimyaa kaa hapa na ule upesi ,nitakupasua nyau wewe ,”mama Ashura aliongea kwa ukali mno tena kwa sauti ya juu na kumfanya mwanae atulie na kuanza kula huku analia
Wakati huo gwae kasimama anaangalia rafiki yake anakula ,huku tumbo lake likinguruma na njaa ,mama Ashura alimshika gwae masikio alimvuta kwa nguvu hadi gwae akalia kisha akamrusha nje ,
Gwae alikaa hapo njee huku analia maana alivutwa sana masikio ,mama Ashura kaanza kuongea tena “tena wewe mtoto hizi hasira nilizonazo zitakuishia juzi nilimwomba mama yako wigi niende kwenye kitchen party alininyima ,nilimwomba aniazime gauni lake na mkoba lakini mama yako alikataa kata kata ,
Na mimi nasema hapa chakula huli kama mama yako hayupo utakula udongo upo ,hebu toka hapo usinitie kichefu chefu , ” mama Ashura aliongea ndipo mama bonge alidakia na kusema hata mimi haka katoto sikapendi ,kalinigombanisha na mme wangu , juzi nilikuwa ile baa ya pale bondeni si nilipata kabuzi flani tukiwa kwenye korido moja kwenye uchochoro wa pale kwa mama pita ,si kale kabuzi changu kalinikumbatia na kuanza kunibusu , haka katoto sijui kalitokea wapi kaliniona ,kakakimbia na kuja kumwambia mme wangu ameniona niko na mwanamme tumekumbatiana ,nakuambia shoga yangu mme wangu aliwaka
Hadi nimetokea kukachukia haka katoto ,kaende zake huo ,gwae aliinuka chini ndipo aliangalia sebuleni kwa rafiki yake alimwona anakula ,gwae alizidi kujisikia vibaya
Mara kuna muuzaji wa mitumba alipita jirani na kwamama ashura ,mama Ashura huwa hapitwi na kitu alimsimamisha na kuanza kuchagua mitumba alichukua gauni mbili kisha alimnong’oneza muuza mitumba ,kaka hapa sina hela halafu hizi nguo nimezipenda baadae uje mme wangu atakuwa hayupo anaenda kazini maana analinda hivyo tutamalizana
Muuza mitumba alijikuta anajilamba midomo baada ya kuona maziwa ya mama Ashura alivyoyapiga jeki na brazia kisha yakajaa vyema huku kavalia dera lake na alivyojaaliwa nyuma ,basi muuza mitumba alijikuta anaitikia sawa nitakuja ,
Mama Ashura aliondoka akiwa ametabasamu ,tukirudi kwa gwae baada ya mama Ashura kwenda kuchagua mitumba ,rafiki yake alimwita walau apate vijiko viwili vya ubwabwa kisha akipata na kikombe cha maji tumbo litatulia,
Rashidi alikuwa anampenda sana rafiki yake gwae maana hata kwenye masomo huwa akishidwa hesabu gwae anamsaidia .
Gwae njoo kula upesi mama kaondoka Rashidi alisema ,japo gwae alikataa ila rafiki yake alimlazimisha akale hakupenda amwone akishinda na njaa
Gwae kutokana na njaa kuwa kali alijikuta anakubali waliingia sebuleni haraka na kukaa kwenye kamkeka kadogo ,gwae alipeleka matonge mawili
Ile anapeleka mkono achukue tonge la pili,mama ashura tayari alikuwa ashaingia
Mama Ashura hakuwa na huruma hata kidogo aliruka na kusema wewe mtoto wa malaya mama yako kaenda kutembea na mabwana zake alimuua mmeo ili apate uhuru wa kutembea na wanaume wawatu ,,wakati huo gwae ndio mkono unafika kwenye sahani alivyoshituka baada ya kumwona mama Ashura alibaki vile mkono ukiwa kwenye sahani.
Mama Ashura aliukanyaga mkono wa gwae na kuukandamiza chini kwa nguvu ,ni sauti ya mfupa ilisikika koooooooh! Huku sambamba na kilio cha gwae
Mama nakufaa mkono wangu ,ndipo mama Ashura aliutoa mguu wake kisha akaangalia mkono wa Gwae tayari ushavunjika
Ha ha ha ha ha ha
Alicheka na kusema hiyo ndo dawa ambayo ulikuwa unaitaka
Masikini Gwae mkono umevunjwa kisa chakula jmn
SONGA NAYO
Episod ya 19
Tulipoishia jana baaada ya mama Ashura kuukanyaga mkono wa Gwae na kuvunjika ,masikini mtoto alianza kulia huku akiita mama mama ,Gwae alipata maumivu makali mno ,njaa yake na rafiki yake kumjali ndo ilomfanya kufikia kuvunjwa mkono ,Gwae kila akiangalia mkono wake ndipo alizidi kulia kwa nguvu ,
” mama Ashura wala hakujali kama kamvunja mkono ,ndo kwanza kainama na kuichukua ile sahani ya ubwabwa na kupeleka chumbani kwake ,,Rashidi alimwangalia Gwae akilia na yeye akajikuta machozi yanamtoka ,” mama Ashura alitoka na kumkuta mwanae akilia ,aliita Rashidi kisha akampiga kibao kizito ,kelele ,unalialia nini si nishakukataza kutembea na haka katoto kwanza mama yake anasifa mbaya hapa mtaani,ashaua mume wake ,isitoshe ni ……mama Ashura hakumalizia alisita na kuacha ,kisha alimshika mwanae mkono na kumpeleka chumbani kisha akamfungia.
Mama Ashura alimwendea Gwae na kushika fimbo ,haya geuka ulikotoka nenda kwenu usitupigie makelele kwanza mie nina miahadi na muuza mtumba nijiandae kunengua viuno nimfilisi mtaji wa mitumba si kapenda mwenyewe ha ha .
Hakika mama Ashura aliongea hivyo huku akimwangalia Gwae akiondoka huku analia mkono wake umevunjika ,mamaa mkono wanguu mamaaaaa! Naumiaa !! ,mama panauma
Hakika Gwae alilia kwa uchungu huku akielekea kwao.
“Aryan hebu tulia mbona nasikia sauti kama ya mdogo wangu Gwae akilia ” Abbas aliuliza wakiwa maeneo ya kwa akina Abbas ,Aryan nae alisikiliza kweli kama vile sauti ya Gwae itakuwa jino lingine limeng’oka nini maana sasa hivi ndo umri wake wakung’ooka meno, Aryan aliuliza wakati huo tayari kagiza kashaanza kuingia ,
Abbas alisema “hebu twende tumfuate ,” walianza kutembea taratibu kuelekea mahali inakotoka hio sauti ya kilio ,
Walikatiza uchochoro mmoja ndipo wakakutana uso kwa uso na Gwae akiwa analia kwa uchungu.
Abbas alivyomuona mdogo wake mkono ulivyolegea alijua huyu tayari amevunjika ,we Gwae umefanyaje mkono wako ,maana wewe kwa utundu haujambo,
Gwae kwa sauti ya kilio alisema kaka mkono umeumia ,hiii hiii “Abbas aliuliza tena umefanyaje wakati huo tayari ameushika mkono ,pale pale Abbas alijikuta akichuchumaa na kusema ulikuwa unacheza mchezo gani hadi ukavunjika mkono ,
Gwae alijibu mama yake na Rashidi kanikanyaga.
Aryan alidakia mama yake Rashidi !,Gwae ilibidi aeleze kilichomkuta,kaka mama Rashidi amenikanyaga alivyonikuta nakula chakula na mwanae ,na kunambia kuwa hataki nile kwako,
Abbas siko zote huwa anahasira mbaya kulikuwa na kibanda flani cha fundi seremala kwa juu alikuwa kaweka miti miti ili kuzuia upepo using’oe bati
Abbas alivuta limti likubwa na kulitia begani alisema mama Ashura kwangu umechokoza nyuki ,leo utaiona kuzimu , basi Abbas akiwa amepandwa na hasira Aryan alimzuia na kumwambia Abbas hapana usifanye hivyo ,
Abbas alimsukuma Aryan na kumwambia niache ,ila Aryan aliinuka upesi na kujikaka mua ,alimzuia Abbas kwa nguvu na kumwambia maneno ambayo yalimfanya Abbas akaelewa,
“Abbas tafadhali nakuomba usifanye hivyo chamsingi tumpeleke Gwae hospitali akapatiwe matibabu ili asiendelee kuuumia sasa ukifanikiwa kumuua mama Ashura na ukapelekwa jela je Gwae nani atamhangaikia kama ujuavyo mama yako siku hizi kabadilika hatulii nyumbani,”
Sawa Aryan nimekuelewa nimeacha twende tumpeleke kwanza dogo hospitalini, Abbas alielewa na kutupa ule mti walimpeleka hadi hospitalini ,maeneo ya tegeta kibaoni njia ya kuelekea madale kuna hospitali moja inaitwa P.K
Walifanikiwa kupokelewa vizuri kisha Gwae akapelekwa kwenye chumba cha kufungiwa p.o.p, yaani lile gamba gumu,watu wengi wanapenda kuita hogo.
Abbas akiwa amejiinamia alimuuliza Aryan ,sasa tumemleta Gwae na matibabu ashaanza kupatiwa hiyo hela tutaipata vipi laki tatu yote hiyo, Aryan alishusha pumzi kisha akasema kuna hela Samairah alinipa laki mbili tutaongea na madaktari wataelewa bana usihofu ,Abbas kidogo akashusha pumzi
” lakini Aryanmama yangu kazidi halafu unasema nimvumilie hadi lini ,ona hadi sasa hivi tumerudi shule hatujamkuta na usiku katulaza na uji daah mama simwelewi hata kidogo”,
Aryan alijibu” Abbas elewa huyo ni mama yako hata awe na sifa mbaya kiasi gani atabaki kuwa mama yako hivyo ninachokushauri usisikilize maneno ya watu,”
Sawa Aryan nimekuelewa, Abbas aliingiza mkono mfukoni alitoa karatasi kisha akasema
Oya Aryan kuna karatasi hii hapa nimekuta pale home sijui mama atakuwa ameacha ujumbe.
Abbas alifungua lile karatasi na kukutana na ujumbe aliouacha mama yake ” Abbas hakikisha unamtunza vizuri mdogo wako Gwae mimi nipo maeneo ya hapa hapa nyumbani ila nyumbani nitakuwa siji mara kwa mara.
Abbas ule ujumbe ulimfanya achoke ,Aryan alimshika bega Abbas na kumwambia haya mapito tu ,hebu fikiria mimi niliishi mwenyewe hadi nikaachaga na shule lakini sikukata tamaa ninachokuomba kaza moyo.
Akina Abbas walimsubiri Gwae hadi muda wa saa sita usiku ndipo alifanikiwa kufungwa mkono wake kisha Aryan akaingia kwenye chumba cha daktari mkuu kwa ajili ya malipo,
Aryan alimwangalia daktari kwa umakini ,kuna miale midogo ilitoka kwenye macho ya Aryan na kuingia kwa daktari ,
Daktari alijikuna kichwa ,wakati huo Aryan anawaza atamweleza vipi daktari ili akubali kupokea laki mbili ,!
Mara daktari alimwangalia Aryan na kumwambia haya mgonjwa wako tayari kama tulivyokubaliana nipe hio laki moja. Aryan hakuamini ikabidi aulize umesema shilingi ngapi?
Daktari aliseti miwani yake na kusema sina muda wa kuzungumza sana kuna wagonjwa wengi wananisubiria nimesema unipe laki moja,
Aryan upesi alitoa laki moja kisha wakaruhusiwa kuondoka na kupewa dawa za kupunguza maumivu ,walichukua bajaji na kuanza kurudi nyumbani.
Njiani wote walikuwa kimya kila mmoja akiwaza vitu vyake
Walifika kwenye baa flani maeneo ya karibu na nyumbani ,bajaji iliharibika ,ndipo ikabidi washuke dereva achunguze tatizo ni nini,
Walishuka ndipo Aryan alisema Abbas twende pale baa tukachukue walau chipsi za kula maana si unajua nyumbani kuna kufuli tu na mama hayupo.
Walifika baa na kwenda moja kwa moja kwenye jiko la chipsi walimkuta muuzaji kisha Aryan alisema naomba ututengenezee chipsi mayai tatu ,halafu ufunge,
Walikaa kwenye viti vya pale baa huku mziki ukiendelea kurindima kwenye hio baa taratiiibu.
Abbas alimuuliza mdogo wake ,Gwae vipi kwenye mkono bado wasikia maumivu,Gwae alitikisa kichwa na kusema ndio nasikia maumivu
Wakati huo Aryan akiangalia angalia mazingira ya pale baa wakati anaangalia alijikuta anabaki mdomo wazi,
Aliweza kumshuhudia mama yake na Abbas akiwa amepakatwa na kijana mdogo ,kibaya zaidi mama yake na Abbas alikuwa kavalia nguo za utupu naweza sema nguo zinazotumiwa na makahaba, kwa umri alionao mama yake na Abbas haipendezi kwa vitu anavyovifanya
Mapaja yote yalikuwa wazi huku akishikwa shikwa na walevi ,kijana ambae alikuwa amemkalia aliupeleka mdomo na kuanza kunyonya mate huku wengine wakimshika shika makalio yake, mama yake na Abbas mkononi akiwa ameshikilia chupa ya bia huku mkono mwingine kashikilia sigara,
Aryan aliinuka na kutaka kumwambia Abbas ili waondoke asiweze kushuhudia mambo anayoyafanya mama yake baa,
Ile anamwita Abbas,,hebu tuondoke mazingira haya si mazuri
Kumbe tayari Gwae ashamwona mama yake
,Gwae aliita mamaa
Tulipo ishia jana baada ya Aryan kumshuhudia mama yake na Abbas akiwa baa huku kazungukwa na walevi wakiume wakimshika shika kila mahali,Aryan hakupenda Abbas ashuhudie kitu anachokifanya mama yake pale baa.
/////////////////////////////////
Aryan aliinuka upesi kwenye kiti ,na kumwambia Abbas tuondoke lakini kabla hajamalizia kumbe Gwae alishamuona mama yake,Gwae aliita kwa nguvu mamaaa
Aryan alitamani angekuwa karibu na Gwae huenda angemziba mdomo asiite mama lakini ndio hivyo aliita huku akatoka mikononi mwa kaka yake na kukimbia kueleka kwa mama yake huku analia.
Aryan kidogo alisikia aibu maana kitendo anachokifanya mama yake na Abbas si kizuri hata kidogo ,Abbas aligeuka na kumwangalia mdogo wake anaenda wapi ndipo alidondosha machozi taratibu bila kutarajia,
Aryan kwakuwa anajua hasira za Abbas anajua anaweza akatenda kitu chochote kibaya pale baa na angezua matatizo mengine,Aryan alimsogelea na kuita Abbas nakuomba ulichokiona fanya kama hujaona kitu,naomba usichukulie hasira naomba utangulie kwenye bajaji halafu mimi naenda kumchukua Gwae tuondoke nyumbani
Kaka chipsi tayari hizi hapa ,muuza chipsi alikabidhi chips kwa Abbas kisha Aryan alianza kumfuata Gwae ,hatimae alifika kwa mama yake na kumkuta kakumbatiwa na kijana mdogo tena kapakatwa mama anafanya kupiga funda moja la bia kisha akamunywesha yule kijana kisha mama kwa sauti ya kilevi anasema mahaba niueee jamani ,
Kuna mlevi mmoja alisema wewe mtoto unafanya nini baa halafu umeumia mkono,yule mlevi aliongea kwa dharau huku akimshika mama yake Abbas maeneo ya mgongoni ,ndipo mama yake na Abbas aligeuka na kumwona mtoto wake Gwae.
Mama wala hakujali alisema we mbwa umefuata nini huku halafu huna adabu ,pale mama alifusha kofi na kumpiga Gwae maeneo ya mgongoni ,wala hakuangalia kama mwanae kavunjika mkono,masikini Gwae alipepesuka na kwenda kudondoka chini bahati nzuri hakuutanguliza ule mkono uliovunjika ,alitanguliza mkono wa kushoto na kudondoka ,kibaya zaidi alidondokea mahali kulikuwa na walevi wakicheza mziki ,
Mama mmoja bonge alicheza kama anarudi nyuma aliukanyaga mkono wa kushoto wa Gwae,ni sauti kama ya mtu anavunja ukuni ilisikika kooooh! Mamaaa uwiii jamani mkono wangu ndipo yule mama bonge baada ya kusikia sauti ya mtoto akilia ndipo alitoa mguu wake.
Gwae akajikuta tena anavunjwa mkono mwingine , alilia kilio kisicho elezeka wakati huo Aryan kafika na kumwinua Gwae , hapo ndipo mama yake na Abbas aliinuka na kushusha kimini chake maana kilikuwa kimepanda kwa juu na kufanya sehemu kubwa za mwili wake kuonekana wazi wazi
Wewe mtoto nani kakuambia utembee na mwanangu baa mama wala hakujali alirusha chupa ya bia na kumpiga nayo Aryan usoni paaah! Aryan alihisi kama anaona nyota nyota ,alishika kichwa chake na kuyumba
Ndipo mziki wa baa ulizimwa ,Abbas alivyosikia kishindo cha chupa alikimbia kuelekea mahali yuko mama yake ,ile anafika alishangaa kumwona rafiki yake Aryan ameshikilia kichwa huku damu zinamchuruzika.
Abbas kwa hasira alimkaba mama yake kiblauzi alicho vaa na kuuliza kwa uchungu nini unafanya mama ,mama nambie nini hiki unakifanya? Wakati Abbas kamshika mama yake kwa hasira alivyogeuza macho baada ya kusika kilio cha mdogo wake aligeuza macho pale pale alijikuta anamwachia mama yake na kuelekea mahaki Gwae aliko,
Masikini Gwae alikuwa analia baada ya kuvunjwa mkono kwa mwingine ,kilio cha Gwae kilimfanya na Abbas kulia ,
Yule kijana mdogo naweza sema rika sawa na mwanae Abbas ambae ndiye alikuwa amempakata mama Abbas,
Aliuzungusha mkono kiunoni mwa mama yake na Abbas kisha akaita baby huyu ni nani hadi anakushika blauzi anajua bei yake?,mama Abbas alisema hata mimi nashangaa simjui mimi
,yule kijana baada ya kuambiwa na baby wake kuwa hawa watu hawajui alichokifanya nae alishika chupa ya bia alimtwaga Abbas kichwani na kumwambia wewe boya jiangalia huyu manzi wangu.
Mjinga nini ,kisha akampiga teke shavuni Abbas akajikuta taratibu analala chini na kuwa kimya” mama yake alimfuta yule kijana na kusema baby pole kwa kazi nzito tuondoke kwanza hii baa ishatia gundu”.
Waliondoka hamna hata mtu aliyewagusa na kuwaacha wanae wakiwa katika hali mbaya,Abbas ndio kazimika kabisa huku Gwae akipiga ukunga na kulia kilio cha uchungu, kuna jamaa mmoja aliinuka na kusema jamani watu wote hapa tuna akili timamu hawa watoto tuwapeleke hospitalini wakapate matibabu maana yule maza sio yaani anabadilisha vijiwanaume kila dakika ,
INAENDELEA

