PENZI PENZINI
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Sehemu Ya 5
Dullah alaifurahi kuomuona mpenzi wake akiwa ameshakula maana ilikuwa ni ishara nzuri kuwa anaendelea vizuri. “Vipi dear unaendeleaje? Ndo lilikuwa swali la kwanza la Dullah “Naendelea vizuri dearest usijli” alijibu Alice.“Kwani ilikukwaje maana hujanambia kilichotokea zaidi ya kukaa kimya au dakari alianza mambo yake ya kupima maji maana nasikia anatamaasanaa yule hasa akiona vitu vizuri” alihoji Dullah. “Hamna shida, hofu yako tu mpenzi” Alice alijaribu kumtetea dakatari. “Sema
Kwa upande wa Gaston maisha yaliendelea kama kawaida na alijitahidi sana kupunguza mazoea na Mwajabu kwa sababu alihisi kuwa kitendo cha kuendelea kuwa naye kinaweza kumsababishia kuyumbisha jahazi lake la mapenzi na Jesca mtu ambaye hakuwahi kufikiria kuaachananaye.Akaanzisha shera au utaratibu wake mpya kuwa msichana anayesoma naye darasa moja ni marufuku kabisa kuingia chumbani kwake. Alifanya kila hila na kufanikiwa kuachana na Mwajabu. Alimueleza binti huyu ambaye mahusiano yao yalianzishwa na fumanizi kuwa yeye ana wake na Mwajabu ana wake basi kila mtu abaki na wake.
Gaston kummaliza kabisa akachonga mpango na Alice kuwa Alice ajifanye kuwa yeye ndo demu wake mpya hivyo kumrusha roho mwajabu.Gaston alimuweka wazi shemeji yake huyo kuwa binti huyo anamtaka kimapenzi. Gastona alidai kuwa yeye hayupo tayari kumsaliti mpenzi wake Jesca hivyo hiyo ndo njia sahihi. Alice kwa kuwa alikuwa hajui ukweli wowote baina ya Gaston na Mwajabu hivyo alikubali kutumika kama chambo. Visa vilipozidi Mwajabu akakubali matokeo kuwa hawezi kulazimisha mapenzi. Binti huyu akaamua kuendelea na maisha yeka ambayo alikuwa akiishi kabla hajafumaniwa.Mwajabu aliumia sana maana alimpenda Gaston kutoka moyoni kuacha wale waume za watu ambao alikuwa nao kwa sababu za kimaslahi.
Baaada ya fumanizi alijiweka kwa Gaston akiamini kuwa atakuwa akimsaidia helaya kula maana alikuwa akifanya hivyo kabla hata ya kujuana kimwili kwa sababu walishakuwaga ni marafiki. Mwajabu ikumbukwe hakuwa na mkopo na alitokea familia masikini sana ambayo haikuweza kumudu gharama za chuo hivyo aliamua kufanya mambo yote hayo ilimaradi tua apate elimu ya chuo.Kwa hiyo kuachana kwa Gaston kulimaanisha kuwa hata helaya kula itakuwa ni tatizoo kwake.Kwa hiyo Mwajabu ilibidi amtafute baba Juma mume wa mtu ambaye ndo alikuwa msaada wake.
Baba Juma ambaye alipata msukosuko mingii sana baada ya lile fumanizi ikiwa ni pamoja na kuingia kwenye banda la ngurume alikuwa amepata funzo la mwaka. Ilibidi amueleze ukweli Mwajabu kuwa sasa hivi hawezi kuwa na mchepuko wa aina yeyote.Mwajabu alijaribu kumshawishi kwa njianyingi lakini ilishindikama kwa sababu mzee huyuo aliamua kutulia na mkewe akasema hawezi kurudia kosa lilomwaibisha hivyo kwa kumsaidia tu alimtumia shilingi elfu 50 akamwambia waachanae kwa amani tu. Mwajabu akaendelea kuishi maisha ya upweke lakini bado aliaamii siku moja ataweza kuwa na Gaston kwa sababu licha ya mambo mengine ya kimaisha ila yeye anahisi moyo wake ulimpenda kiukweli ukweli kijana huyo. Gaston alikuwa ni mwanume mkarimu sana kwa sababu alikuwabado akimsaidia kimasomo na siku zingine alikuwa akimpa helaya kula kwa asbabu alikuwa akijua maisha halisi ya bintii huyo. Siku zote Gaston alisisitiza kuwa atamsaidia kwa hali na mali lakini sio kuwa wapenzi. Ukarimu huo ndo ulikuwa ukimfanya Mwajabu aendelee kuamini one day Gaston atakuwa wake. Mwajabu kuonesha kuwa ni kweli anampenda Gaston kutoka moyoni alishafanya uchunguzi na kugundua Alice sio mpenzi wake na Gaston bali ni shemeji yake na pia Alice ana boyfriend wake amabye kila wikienda anakuwa naye tena nje ya maeneno ya chuo ambaye ni Dulah.
Siku zilizidi kwenda na hatimaye wakaingia mwaka mwingine wa kimasomo.Huu ulikuwa ni mwaka mgumu kwa kina Gaston kwa sbabu ndo ulikuwa ni mwaka wao wa mwisho. Gaston alijitahidi kusoma sana kwa bidii ili kuhakikisha wastani wake (GPA) inapanda. Akiwa katika harakati hizo siku moja Beatrice yule msichana wake wa kwanza alikuja Moshi maalumu kwa ajili ya Gaston na hiyo ni kutokana na ahadi yake aliyompa mara ya mwisho walipowasliana.Kama mnakumbuka Beatrice alimwambia Gaston katika maisha yake hajawahi kukutana na mwanaume anayejua mapenzi kama Gaston.Kwa mujibu wa Beatrice yaani pamoja na kwenda Uganda kimasomo lakini bado hakuna mwanaume aliyeweza kumpa furaha ya kweli kama Gaston alivyokuwa akimpa.
Ujio wa binti huyo Moshi ulimchanganya sana Gaston hasijue atafanya nini ili aweze kumkwepa. Akaona njia sahihi ni kumzimia simu siku anayosema anakuja. Lakini kuna wazo moja lilimjia eti kwa nini hasimuone hata jinsi alikvyokuwa je, amezidi kuwa zuri au amechuja?. Gaston kilichokuwa kinamsumbua ni kwamba katika mademu zake wote aliowahi kuwa nao hakuna hata mmoja aliyeweza kufiki uzuri wa Beatrice..Gaston aliamua kumueleza ukweli kuwa yeye ana mtu wake na wapo wote chuoni tena wanakaa chumba kimoja.
Beatrice alyakubali yote hayo lakini alisisitiza kuwa anaomba kuonana na Gaston.Akatoa wazo kuwa yeye atashukia Arusha ili waweze kuonana huko kukwepa usumbufu. Beatrice alisistiiza kuwa Gaston hasiwe na hofu kwa sababu gharama zote ni juu yake. Beatrice kumchnagnya kabisa aliamua kumtumia picha zake zile ambazo zitamtoa udenda Gaston na kuamua kuonana naye.Alimtumia picha za utamu utamu ambazo ni ngumu sana mwanamke kumtumia mwanaume kama hamuamini.Gaston alijikuta akikubali ofa hiyo kwa sharti moja yaani wasubiri wikiendi ifike ili waweze kulala wote na kula bata.Wakati Gastona akitaka kutimiza ule msemo wa awali ni awali hakuna awali mbovu mpenzi wake Jescanaye alipata safari ya kwenda Arusha ambapo alitumwa na baba yake.
Jesca aliamua kumfanyia suprise mpenzi wake Gaston kwa kutomwambia ujio wake ili aafanyie suprise ya kufika gheto kwake.Pia hakuona haja ya kumwambia rafiki yake kipenzi Alice juu ya ujio wake huo. Kwa bahati nzuri au mbaya safari au ujuo wa Jesca na wenyewe ulikuwa ni wikiendi kama ulivyokuwa kwa Beatrice.Basi ijumaa ilifika Gaston akawa anajiandaa vya kutosha kabla ya kwenda Arusha kuonana na Beatrice. Beatrce alimwambia Gaston kuwa apende usafiri mwingine na yeye kwa kuwa anatokea Dar basi wote wakifika Arusha watajua wakutane wapi.
Beatrice hakutaka tabu alipofika Arusha alichukua chumba kwenye moja ya hotel ya kifahari aambayo ilikuwa maeneno ya stendi. Na baada ya kupata room nzuri iliyoendana ana hadhi yake ya kuwa mtoto wa Waziri mstaafu alimwandikia Gaston meseji kumuelekeza mahali alipo.Mda ambao sms inatumwa ndo mda huo huo ambao Gaston alikuwa amefika stend na pia ndo mda huo huo Jesca naye alikuwa akifika stend ya Arusha. Gaston alishuka kwenye gari na kuulizia jengo hilo ambalo alielekezwa. Wakati akaielekezwa mpenzi wake Jesca ambaye alikuwa anashuka kwenye gari alifanikiwa kumouna kupitia dirishani.J
esca alinyanyua simu yake na kumpigia ili kuahkikisha kuwa ni yeye au la. Alifanikiwa kuona Gaston akipokea simu jambo lilomfanya Jesca akate na kuanza kushuka kwenye gari.Hata kabla hajasimama vizuri kuna sms ya Gaston iliingia kwenye simu yake. “Nipo darasani mpenzi nitakupigia baadaye. “Huyu mtu atakuwa si mwema kuna ualifu anaenda kufanya yaani mimi ndo huwa nadanganywa hivi yaani leo atanitambua aliwaza Jesca huku hasira zikizidi kumpanda”.Jesca akaamamua kumfuatilia hatua kwa hatua ili aone mwisho wake.Gastona akenda moja kwa moja kwenye hotel hiyo na alipita reception akauliza chumba namba 116 chumba ambacho alikuwepo Beatrice.
Muhudumu akapiga simu kwenye chumba hicho kuthibitisha kama ni kweli binti huyo alikuwa na mgeni wa kiume yaani Gaston. Beatrice alijibu ndio na aelekezwe aende. Jesca na yeye amabaye alikuwa nyuma nyuma baada ya Gaston kukwea lifti na yeye akasema anaenda chumba namba 116 na hapo muhudumu akashangaa ikabidi apige tena simu..****
Baada ya zoezi la kutoa mimba baina ya Alice na Dullah kukamilika kila mtu alirudi kambini kwake.Wikiendi iliyofuta Dullah alikuwa akikabiliwa na mitihani ya MOCK hivyo hakuweza kushuka mjini. Alice alitumia nafasi hiyo kuenjoy na marafiki zake. Alice alishuka gheto akiwa na marafiki zake wawili yaani Easther na Stela.WikiendI ingine ilifika tena ambapo Dulla alikuwa yupo free baada ya kumaliza mitihani hivyo alikuwa na hamu sana ya kuwa na mpenzi wake Alice.Lakini Alice hakuwa tayari kuwa nae kwa sababu alitakaa mwezi mzima upite bila ya yeye kufanya mapenzi. Hivyo basi alijua kama akikutana naye lazima watachakachuana kwa hiyo alitumia kigezo kuwa na yeye alikuwa na test jumatatu kitu ambacho si kweli. Mbaya zaidi Dullah alikuwa akipata ratiba zote za Alice kuanzia ratiba ya kuingia darasani mpka test na mitihani.
Na alikuwa akipata ratiba hizo kutoka kwa marafiki zake na Alice ambao alijenga nao sana urafiki.Dulah kwa kuwa alikuwa amechoshwa sana na mitihani hakuona hajaya kubisha akaendelea na ratiba zake ikiwa ni pamoja na kuwatafuta marafiki zake ili waweze kubadilishana mawazo.Aliwasilisha hoja ya Alice ili kuomba ushauri kwa marafiki zake ambao aliwaamini sana. Aliwaeleza marafiki zake kuwa mpenzi wake Alice amebadilika sana na amekuwa muongo je afanyaje? “Ujue wasichana wana tabia ya kuchoka kufanya kitu fulani mara kwa mara hivyo cha msingi wewe mpe mda ajitafakari na kama wikiend ijayo hasipoonekana basi utakuwa na hojaya msingi” alifafanua Omary.
Kabla Dulah hajasema kitu Peter rafiki yake mwingine alidakia na kusema hapana “watoto wa kike sio hata wa kuwapa mda, wakishaanza upuuzi wao ni shida ukimpa nafasi tu atakutawala” Dullah akasema anamuunga mkono Peter kwa sababu mwanamke ukimwendeeza atakutawala.Ila kwa namna moja au nyigine hatuwezi kulea ujinga mimi naona tusubiri hiyo wikiendi ijayo hasipokuja ndo tumtafutie adhabu ya kumpa alisema Dulla. Wote kwa pamoja wakakubalina wasubiri wikiendi ijayo ili wajue nini kitaendelea.Waliendelea kupunguza stress za mtihani na baadaye waliamua kwenda club kwa sababu muziki ilikuwa ni moja ya starehe yao.
Kama kawaida waliingia club na kukaa kwenye viti virefu na kuanza kupiga vinywaji.Walikaa sehemuambayo wangeweza kuona kila mtu anayeingia.Watu walizidi kuongezeka kadiri mda ulivyokuwa unaenda. “Ebwana daaaah hao mabint watatu wanaoingia ni shida cheki walivyobomba”alisema Omary ili kuwashitua wenzake. “Wa mbele mbona kama ni shemeji yetu” alishituka Peter mara baada ya kumuona Alice akiwa amevaa kigauni kifupi ambacho kiliacha sehemu kubwa ya mwili wake wazi hasa mapaja na mgongo.Akafuatiwa na Stela ambaye yeye alikuwa amevaa kibukta kifupi kilichombamba pamoja na Easther amabye na yeye alivaa skin mtepweto ambayo ni shida wenyewe waliziita soksi.
Dullah alitumbua mimacho mara baada ya kuwaona mabinti hao wamekwenda kukaa kaunta utazani makahaba wanaotafuta wateja. Omary alimzuia Dullah mara baada ya kuona anataka kunyanyua na kweenda kuwafuata. “Utaharibu movie broh waache kwanza ili tujue wapo wenyewe au la?” Alisema Peter Waliamua kuahama sehemu hiyo wakaamua kwenda sehemu amabyo ni giza zaidi ili wasionekane. Wlivyonyanyuka tu wale mabinti wakenda kukaa kwenye viti walivyoviacha.
Mziki uliendelea na Stella miongoni mwao ndiye aliyeonekana kuwa na mzuka sana wa kucheza muziki.Baadaye wote mizuka iliwapanda wakaingia stegini na kuanza kucheza.Baadaye waliongezeka wanaume watatu wanaosoma nao hivyo kila mmoja akachukua msichanawake na kuanza kucheza naye. Dullah akaenda chuoni ili ampigie shushushu wake ili kupata habari zaidi.Shushushu wake alimwambia kuwa hapo chuoni kulikuwa na shindano la Mr and Mrs University.Kwa hiyo kwa mda huo shindano lilishamalizika na mshindi alishapatikana na watu wakaenda club kumalizia siku.Dulah akaumuuliza kama anamjua mshindi.Shushushu akamjibu kuwa mshindi ni mmoja wa rafiki zake na Alice .
Hapo Dulah akawa amepata picha kamili kuwa mshindi atakuwa ni Easther maana ndo alikuwa na muonekano wa kimisss na pia alikuwa na kipaji cha kuimba. Hata kama ni hivyo kwa nini anidanaganye si angenambia tu ukweli tungekutanaClub aliwaza Dulah mara baada ya kukata simu. Akasema ataanzisha fujo na hawata amini kitakachotokea.Hakutaka kusubiri alienda moja kwa moja kwenye vile viti na kumshika bega Alice.Alice alipogeuka alikutana na sura ya mpenzzi wake Dulah.Alishituka sana na kujikaza kisha akamwambia “karibu mpenzi”. Dulah kwa hasira akamuuliza hapa ndo chuoni? Alice na yeye akajibu kwa dharau na wewe hapa ndo shuleni.
Kauli hiyo ilimkera sana Dulah akajikuta amemnasa kibao bila ya kutarajia.Alice ikabidi aangue kilio bila kutarajia.Kama hiyo haitoshi Dulah alimvuta nywele na kumpa vibao viwili vya nyongeza jambo lilomfanya Alice alie kwa sauti kubwa. Wale vijana waloikuwa kampani na Alice hawakutaka kusubiri walimvamia Dulah na kuanza kupigananaye. Dulah alikuwa ni mtu wa mazoezi sana si unajua tena ndo waziri wa ulinzi shuleni kwao.Peter na Omary nao hawakuwa mbali walikuja kumsaidi rafiki yao. Ilibidi Dj asimamishe mziki ishara kuwa kuna matatizo.Mabausa walikuja kuamua ugomvi huo kablaya kujua nini chanzo.Dulah alikuwa amevua mkanda wake wa kiunoni kwa hiyo yeyote aliyemsogelea alikuwa akimpatia dozi.
Katika purukushani hizo bausa mmoja alifanikiwa kuudaka ule mkanda hivyo Dulah akawa hana jinsi zaidi ya kukimbia.Alipotoka nje anataka kuvuka barabara maana wale mabausa walikuwa wanakuja kwa kasi akasikiamlio wa defender ya polisi akaona isiwe tabu akaingia chini ya gari moja ambayo lilikuwa karibu nalo. Ile defender ikapita kwa nguvu na ikafanikiwa kuwakamata wasichana wachache ambao walikuwa wakijiuza hapo nje.
Wale mabausu wakajua na Dulaha atakuwa amesombwa na defender hiyo iliyokuwa doria.Omary rafiki yake na Dulah akang’ang’niwa na walinzi wakati Deo kijana aliyekuja na kina Alice yeye alikuwa akiomba mabinti hao wamtetee kuwa sio yeye aliyoanzisha ugomvi bali alikuwa anaamulia. Siku ikawa imeingia doa Alice akwatetea wote wawili yaani Omary na Dulah wakachiwa. Hakuna aliyetamani kuendelea kubaki eneo hilo.Rafiki zake na Dulah wakawa kwenye wakati mgumu kwa sababu Dulah ndo alikuwa na ufunguo wa gari.Mbaya zaidi hiyo ilikuwa ni ya kaka yake na Peter. Omary akaamua kumpigia simu Dulah na alipopokea aliwaeleza kuwa yeye tayari amefikagheto.
Walishangaa kwa sababu walitarajiwa kuwa awaambie yupo polisi kwa sababu hata walinzi waliamini hivyo. Ikabidi Peter apande bodaboda akazifuate funguo za gari hilo maana aliona kuacha gari hiyo ya kaka yake kulala hapo ni hatari. Ikabidi amtumie huyo huyo bodaboda kurudi naye lakini Dulah alikataa kulala na kusema waende club ingine wakamalizie starehe zao kwani ndo ilikuwa ni saa 7 usiku.Kwa sababu wote walikuwa wamelewa wakajikuta wanaamua kufanya hivyo. Kumbe mawazo yao hayakutofautina sana na mawazo ya kina Alice.Alice na kampani yake na wao waliaama kutoka club ya mwanzo na kwenda ingine.Kwa bahati mbaya walikwenda club ile ile ambayo walikwenda kina Dullah.
Safari hii wote walikutana nje shemu ya kulipia kiingilio.Wakaaanza tena kurushiana maneno ya kashfa jambo lilomfanya Omary hasilipe kiingilio kwa sababu yeye ndo alikuwa ameshika pesa. Walimisihi Dulah waondoke zao kwa sababu mmiliki wa club hiyo ndo yule yule wa club waliyokimbia mara ya kwanza baada ya kuanzisha fujo. “Pia nimeona wale wadada wanaongea na wale mabausa hivyo hawawezi kuturuhusu tuingie” alisisitiza Peter. Dulaha akampkonya ile hela Omary kisha akaelekea sehemu ya kulipa kiingilio. Wakati huo kina Alice na kampani yake walishaingia mda mrefu tu.
Yule bausa wa malangoni alitumia busara na kumwamba Dulah “broh ni vizutri kama ungeenda kupumzika kwa sababuu taarifa zenu za fujo tunazo”. Hapo Dulaha akaona ishakuwa mbaya hivyo hakuwa na haja ya kuendelea kulazimisha.Akawaambia wenzake waingie kwenye gari na kuondoka eneo hilo. Waliamua wote waende kulala kwa Dulah kwa sababu alikuwa amelewa sana hivyo suala la yeye kulala mwenyewe ilikuwa ni ngumu maana ingeweza kuleta mahafa. Walifika gheto salama na Dulah alianza kutapika kutokana na pombe kumzidi na pia alichanganya pombe nyingi sana ikiwemo pombe kali eti kupunguza stress au mawazo kwa kile kilichotokea.
Wakati wao wakirudi nyumbani na kulala wenzao waliendelea kula bata na Deo mwanaume ambaye aikuwa akicheza na Alice.Deo alitumia nafasi hiyo vizuri kumfariji Alice.Pamoja na mambo mengine Deo alikuwa akitaka Alice tangu siku ya kwanza alipoingia tu chuoni.Kwa maana walifahamina wakiwa kwenye foleni ya kufanya registration(uasili).Deo alishatumia kila mbinu bila mafanikio kwa sababu kizuizi kikubwa ilikuwa ni Dulah mwanaume ambaye Alice alikuwa akimpenda sana. Ilifika mahali ikabidi Deo akubaliane na ukweli kwamba hawezi kuwa na bint huyo kimapenzi zaidi ya kuwa marafiki wa kawaida tu.
Kwa hiyo urafiki wao ulikuwa na nguvu sana maana Deo aliamini ipo siku Alice atakuja kuwa mpenzi wake.Alitumia nafasi hiyo vizuri sana kwa kumnywesha pombe Alice ili eti tu amsahau kabisa Dulaha wake.Alice hakufurahishwa kabisa na kitendo alichofanyiwa na mpenzi wake Dulah.Aliona kupigwa mbele za watu ilikuwa ni uzaliishaji mkubwa sana “mbona yeye alikuja club bila kuniambia, mbonamimi sijamuhukumuu aliwaza Alice”. Walicheza mziki na kunywa vileo mpaka asubuhi ambapo waliamua kurudi zao chuoni. Kuanzia siku hiyo marafiki zake wakawa wanamshauri kuwa aachane na Dulah kwa sababu ni mwanaume mkorofi na hasiye na mapenzi ya kweli. “Kwa nini
anataka kukumiliki, kukutawala na kukupangia sheri kwani amekuona”? hayo yalikuwa ni baadhi ya maswali ambayo alikuwa akiulizwa na marafiki zake.Maisha yaliendelea na kwa upande wa Dula yeye alikuwa mjini kwa sababu walikuwa wamefunga likizo ya mda mfupi. Dulaha alikuwa ni kama mtu aliyechanganyikiwa asijue nini cha kufanya ingawa ni yeye ndo alifanya makosa makubwa kutokana na hasira za kudanganywa na Alice.Pamoja na hayo Dulah hakuweza kumtafuta kabisa Alice akiamini kuwa yeye ndo alipaswa kutafutwa.Siku zilizidi kwenda wikiendi ilifika lakini hakuna aliyemtafuta mwenziye.Dulah alairudi shule na kuendelea na masomo.
Wiki hiyo moja tu bila mawasiliano na Alice ilitosha kabisa kumkondesha Dulah.Marafiki zake walilitambua hilo wakaona ipo haja ya watu hao kurudiana.Omary ambaye ndiye alikuwa amezoeana sana na Alice ndio aliotumiwa kuomba msamaha.Omary kwa busara alipanda mpaka chuoni kwa kina Alice na kuongea na shemeji yake huyo. Omary aliamua kujishusha na kumuombea msamhaa rafiki yake. “ Kwa nini huo msamaha hasije kuomba yeye mpaka wewe umuombee?” Hilo ndilo lilikuwa swali la kwanza la Alice kwa Omary. “Unajua shemeji makosa yako ndiyo yaliyopelekea Dula kufanya makosa na kwa sababu wote ni wakosaji basi unapaswa kumsamehe.Kama Mungu aliye mbinu anassamehe wewe ni nani hasa hata ushindwe kumsamehe.Samehee saba mara sabini hata vitabu vya dini vinakwambia. Ila kama unaona huwezi kumsamehe ni kila mtu aaendelee na maisha yeka ni sawa mimii ni mjumbe na mjumbe siku zote hauwawi” alisema Omary na kuondoka mara baada ya kuona Alice hataki kumuelewa na alikuwa na kiburi.
Alice akamjibu jibu la mwisho ambalo lilimkera zaidi Omary yaani alimwambia “Shemeji wewe nenda tu siku nikijisikia kumtafuta Dulah nitamtafuta”. Basi waliachanakwa staili hiyo na Omary akafikisha ujumbe kama alivyoambiwa.Maneno hayo ya Aice yalimkera kila mtu aliyepata kuyasikia wakajua huo ndo ulikuwa uamuzi wa mwisho na lilibaki tamko la Dulah tu kukatisha safari ya uhusiano uliodumu kwa zaidi ya miaka 3.Dulah hakutoa tamko la moja kwa moja kwa sababu historia yao ya mapenzi ilionesha kuwa wamepitia majanga mengi hata na hata kipindi kile Alice yupo form five ilishatokea tukio kama hilo. Ambapo aliwakuta yeye na marafiki zake kwenye hotel yao wakila bata.
Waliachanakwa mda tu ila baadaye walirudiana.Ilikuwa ni kawaida kwa Alice kuomba msamaha hasa linapotokea tukio la namna hiyo. Kwa hiyo Dulah aliamini ipo siku Alice ataomba msamaha. Siku zilizidi kwenda lakini Alice hakujaribu kabisa kumtafuta Dulah.Siku moja wikiendi ilifika na ilikuwa ni siku ya ijumaa ambapo Dulah alishuka mjini na siku hiyo alitoroka asubuhi kwa sababuu hakuonaumuhimu wa yeye kuendelea kuwa shuleni ili hali akiwa katika stress za mapenzi.Alifika gheto kwake na siku hiyo alipanga kuhakikisha anapata muafaka wa suala hilo.Baada ya kufanya usafi aliamua kumtafuta Alice kupitia kwenye simu.
Simu iliita mara ya kwanza lakini haikupokelewa vivyo hivyo akapiga tena lakini haikupokelewa. Baadaye Alice alituma sms nipo darasani nitakutafuta nikitoka. Dulah aliendelea kuwa mvumilivu na baadaye kabisa akiwa ameshakata tamaa simu yake iliita na kuangalia alikuwa ni Alice akimpigia.Alipokea na kumwambia kata nikupigie.Alice naye akajibu wewe ongea shida yako bwana. Kauli ilimkrea Dulaha lakini akajitahii na kusema “Kwa kifupi ni mustakabali wa penzi letu ndo kilichonifanya nikutafute”. Wewe unatakaje alisema Aice mara baada ya Dulah kujieleza.
“Unajua makosa ni sehemu ya maisha ya mwanadamu, na hakuna mwanadamu aiyekamilika na ndio maana pia watu wanaenda shule ili wapate uwezo wa kukabilian ana changamoto za maisha ikiwemo mapungufu ya wanadamu”. Alisema Dulah kwa upole. “Hiyo ni misemo tu ya wanadamu baada ya kufany amakosa, cha msingi wewe nenda moja kwa moja kwenye pointi unataka nini kutoka kwangu” alisema Alice kwa ukali. Kwa kifupi nahitaji vitu viwili kutoka kwako, moja ni mazungumzo ya usuluhishi, mbili kama itashindikana uje uchukue vitu vyako kwangu alifafanua Dulah. “Sidhani kama nitakuwa na nafasi ya mazungumzo kutokana na uzalilishaji ulionifanyia, cha msingi kesho jioni nitakuja kuchukua vitu vyangu alisema Alice na kukata simu. “Last never end the world” alisema Dulah mara baada ya Alice kukata simu kwa dharau.
Dulaha Alisema msemo huo wa kizungu akiwa na maana kuwa huo unaweza kuwa mwisho wa mapenzi yao lakini haimaanishi kuwa ndo mwisho wa dunia bado anaamini maisha yataendelea na atampata mwingine ampendaye.Wakati Dulah akiugulia maumivu mazito ya mapenzi kwa upande wa Alice ilikuwa ni tofauti kidogo kwa sababu yeye alishaanza ku enjoy penzi la Deo kwa njia ya simu na malavidavi mengine. Deo tayari aishamnunuli Alice simu kali, akampa na line mpya ilimradi tu kukatisha mawasiliano baina ya Alice na Dulah.
Walikubaliana kuwa Alice abadilishe laini lakini Alice alisema atafanya hivyo baada ya wiki moja yaani ikifika wikiendi akatoe hela zake zote na kuivunjulia mbali maana hata hivyo ilikuwa ikifanana na namba za Dulah ambye hiyo laini alimchongea yeye. Usiku huo Alice alifikiri sana swalala yeye kuachanana Dulah lakini hakupata jibu kwa sababu alikuwa akimpenda sana na hakuelewa kama ataweza kuishi bila yeye. Ingawa Deo alioneshakumjali lakini kwa upande wake hakutokea kabisa kumpenda mwaanaume huyo basi tu alijikuta akimkubalia kwa sababu ya matukio yaliyotokea.Alice akajikuta akieendelea kubaki njia panda hasijue nini cha kufanya.
Kesho yake ilifika na ilikuwa ni mda wa jioni Alice akajiandaa na kuwaaga rafiki zake kuwa anaenda kwa dada yake sehemu moja inayoitwa Boma. Akampigia Dulaha simu na wakapanga wakutane mjini sehemu moja inayoitwa Uhuru Park. Siku hiyo Dulah alikuwa na rafiki yake Omary na alimuomba yeye ndo awe mwenyekiti wa kikao.Omary alikata kwa madai kuwa binti huyo alikuwa na dharau sana.Dulah alimwabia kuwa siku zote matatizo hayakimbiwi bali ukabiliwa. Kwa hiyo wakakutana hapo na Alice alipomuona tu Omary alisema “kumbe mpo wawili si mngenambi ana mimi nije na rafiki yangu”. Omary akajibu kwa kifupi kuwa hajachelewa bado ana nafasi anaweza kumwambia aje. Alice aliona kikao hicho ni bora na rafiki yake mmoja angekuwepo ili wasije wakamzidi kete na kumpakazia makosa. Alice akaona ni bora akmpigie Stella ambaye siku zote amekuwa upande wake na amekuwa akimkubali sana Dulah.Aliona akimpigia Easther ambaye ndo kowadi wa Deo itakuwa ni majanga tupu. Alimwambia Stela achukue bodaboda fasta aende hiyo sehemu waliyokuwepo.Omary akaenda jikoni akaweka oda ya nyama choma.Aliwaacha makusudi ili waanze kikaao chao wenyewe.
Mpaka anarudi kutoka jikoni hakuna hata mmoja aiyejaribu kuongea neno zaidi ya kujianamia tu kama mabubu. Mara Stella akaingia maana kutoka hapo mpaka chuoni kwao haikuwa mbali. Walianza kuongea mawili matatu jinsi ya uzuri wa sehemu hiyo waliyokaa.Stela kama kawaida yake hakuwa mvivu wa kutoa sifa mara baada ya kufika eneo hilo.Nyama choma ilikuja mezani watu wakaendelea kujichana huku kila mmoja akisindikizwa na kinywaji anachokipenda. Baadaye mzee wa Busara ndugu Omary alifungua kikao. “Alice , Dulah pamoja na mgeni kwanza niwapongeze kwa kukubali kukutana. Hata hivyo nawaheshimu sana ndio maana nikakubali kuharisha mambo yangu yote na kuja hapa.
Ninachotaka kuwaeleza kabla ya maamuzi yeyote hayajafikiwa leo hii labda mkumbuke historia zenu. Mimi mwenyewe binafsi ni mtu pekee niliyebahatika kushuhudia mapenzi yenu tangia mmeanza mpaka mlipofikia.Najua mmepitia mambo mengi sana na kama kuachana mngeshaachana miaka mingi iliyopita.Kwa nilichokionamimi sikuile pale club ni maamizi yaliyotokana na hasira.Ndugu Dulaha ahkufanya kitendo xha uungwana kumpiga makofi shemeji maeneo kama yale na kwa hili inabidi ukiri kosa na umuombe Alice msamaha.Bwana shemeji nawe kuwa upande wako hukufanya uungwana kumjibu shemeji vibaya pale alipokuuliza pale ndo chuoni.
Sehemu Ya 6
Kwa hiyo na wewe pia una makosa mawili ya kudanganya na kumjibu vibaya. Hivyo na wewe itakubidi uombe msamaha yaishe. Kwa kifupi wote mnamakosa na hakuna haja ya kumtafuta mchawi cha msingi kabla kila mtu hajasema chochote Alice na Dulah naomba mkumbatiane na Stella uwapige picha ya ukumbusho. Kila mtu ilibidi acheke maana Omary alikuwa akiendesha kikao kidikteta kama mtu vile mwenye madaraka makubwa sana. Stella alivyokuwa na mbwembwe tayari alaishasimama ikabidi wausika wafanye walivyooagizwa.Basi kabla ya kuwaruhusu kila mmoja aseme ya kwake ya moyoni bado nitaomba kila mtu ajibu maswali yangu alisema omary.
Nitaanza na Alice je ni kweli bado unampenda Dullah muendelee kuishi kama wapenzi?Alice akamwangalia kila mtu usoni kisha akajibu ndio. Je na wewe Dulah bado unampenda Alice muendelee kuwa wapenzi.? Dullaha naye akajibu ndio. Basi kama ni hivyo namuomba Stella aseme yaliyo moyoni mwake. “Asante sana kaka mimi binafsi nafurahi kwa sababu sikuona sababu ya muhimu ya watu hawa kuachanaili hali wanapendana sana na wametoka mbali sana. Labda niseme tu ukweli kwamba Dulah alikosea sana siku ile kwa sababu kitendo cha mwanamke kuwa na mwanaume haimaanishi kuwa ni mpenzi wake. Mazingira siku ile yalitulazimisha kwenda club mara baaada ya rafiki yetu Easther kushinda umisss wa chuo. Yeyeni mtu anayependa kwenda club hivi unafikiri angetuelewaje kama tubgektaa kwenda club. Pia lazima nimtetee Aice maana shem amekuwa akimnyima mara kwa mara fursa ya kushiriki furaha na wenzake.
Si unakumbuka pia ile siku ya sherehe ya kuwakaribishawanafunzi wapya(welcome freshers) ulimnyima ruhusaya kushiriki na sisi aliendelea kufafanua Stella. Kwa hiyohata siku ile ilimbidi akudanganye maana angekuomba ruhusa ungemnyima tu. Kwa kifupi rafiki yangu Alice masamehe Dulaha na mpe nafasi ingine lakini pia Shemu wangu Dulah badilika mpe huru mwanamke kamwe hawezi kukusaliti na atajiheshimu sana alimaliza kusema Stella. Hapo Omary akawa mpole kwa sababu yaliyozungumzwa kwa namna moja ua nyingine yalikuwa na uzito. Omarya akampa nafasi Alice aongee.Alice alisema kwa upande wake yeye hana kinyongo ila Dulah afuate ushauri na Stella.
Yaaani kama anataka penzi lao liendelee kudumu abadilike kwani mwanamke hachungwi kama mbuzi. Kabla Dulah hajapata nafasi ya kuongea aliingia Deo na aliwapa salamu kisha akaenda kukaa sehemu ya juu.Alice alishituka kidogo lakini hakujua nini kilikuwa kinaendelea. Lakini kwa haraka haraka ni kwamba Deo alikuwa akimfuatilia Alice ajue alikuwa akienda wapi?je ni kweli alikuwwa akienda kwa dada yake kama alivyosema au alikuwa akienda sehemu ingine.Deo kwa kuwa alikuwa akimtumia sana Easther kama ndo kowadi ilibidi amtumie meseji ili aje aone kainachoendelea.
Dulah akapewa nafasi ya kuongea na alisema kuwa yeye amekubaliana na maazimio yote yaliyopitishwa ila Alice naye aangalia marafiki kwa sababu wengine wana wivu tu hawataki kuona penzi lao likishamiri.Dulah alisema hivyo kwa sababu alijua kabisa watu waliokuwa wakimwaribu Alice ni marafiki zake ambao walishakuwa ni wazoefu wa mji wakaijaribu kukikimbizana na starehe za hapa na pale. Kikao kikawa kimemalizika hivyo na Alice alitaka kurudi chuo na rafiki yake Stella. Lakini Omary alikataa na kusema “Kama kweli shemeji mmekubaliana kuwa mtaendelea kuishi kama maisha yenu ya kawaida mimi naona hana ya wewew kurudi shuke kwa sababu ndo kwanza jumamosi mimi napendekeza wewe ubaki na Dulah wako na shuleni utaenda kesho.
Alice alisita kidogo na kumuuliza Stella vipi unalionaje wazo hilo. Stella naye alirudisha mpira huo kwa Alice na kumwambia yeye ndo ana uamuzi wa mwisho.Alice akaumuuliza tena kwa hiyo utakuwa tayari kwenda mweneyewe chuoni. Stella alicheka kidogo na kumjibu kwani siilikuja mwenyewe.
Kwa hiyo wakakubaliana kuwa Alice ataondoka na Dulah na kwenda kulala gheto kwao.Waliendelea kuvuta mda mpaka kigiza kikaingia.Waliingia kwenye gari na ikabidi wampeleke kwanza Stella chuoni na Alice alimuonya rafiki yake huyo kwa njia ya meseji kuwa akiulizwa kuwa Alice ameenda wapi ajibu kuwa ni kwa dada yake kwani kikao hakikupata muafaka hivyo wameachana rasmi na Dulah. Alice hakutaka kuachana na Deo kwa shari na pia aliitaka apate mda wa kuongea kwanza na Easther ambaye ameonekana na yeye ni kiwazo kikubwa cha yeye kuendelea na mpenzi wake Dulah.
Kwa hiyo Stella alipoulizwa alijibu kuwa Alice amekataa kumsamehe Dulah hivyo wamekubaliana kuachana.Hakuna aliyaamini maneno hayo kwa sababu Alice aliamua kuzima simu zake zote mara baada ya kuwaona Easther na Deo plae Uhuru Park.Maana Deo alipowakuta pale alikaa kwa juu na alimpigia simu Easther akaja eneo lile.Basi Dulah walindoka na Alice wake wakaelekea gheto huku kila mmoja akiwa hana imani na mwenzake kwa asilimia zote mia moja kama kweli amesamehewa na mwenziye. Walifika getho na Dulaha aliendelea kusisitiza kuwa kamwe Alice hasikubali kuyumbishwa na marafiki. Alice kuonesha kuwa amemsameha alitoa viwalo vyake vyote kisha akachukua taulo na kumwambia Dulah “Twende tukaoge mapenzi wangu”.
Dulaha hakujivunga naye alivua nguo na yeye alichojoa nguo zake na kubaki mtupu. Waliingia bafuni na kuanza kuogeshana.Alice akachukua lile kufuli lake na kuanza kujisugulia hiyo ni mara baada ya kulifua. “Nilisjhakukutaza hiyo tabia ya kutumia nguo ya ndani kama brashi kwa sababu sio vizuri na wakati mwingne ni hatari kiafya maana dead backteria wanaweza kuingia sehemu zingine za mwili wako na kuleta maambukizo,alisema Dula. Wewe naye hayo mabrash yako ni magumu sana na mimi nishazoea kijisugulia vitu laini alijitetea Alice. Walicheza cheza huko bafuni na baadaye walimaliza na kurudi ndani.
Wakapanda kitandani na walionekana kusahau yote yaliyotokea na kwa sasa kila mmoja alikuwa akiwaza raha ya huba atakayopata usiku huo.Walianza safari hiyo kwa mwendo wa uchokozi na Dulaha alikuwa na papara sana ya kuchota maji ya kisima. Alice akamwambia kuwa “leo sikupi mpaka uvae kinga kwa maana si unakumbuka mara ya mwisho kilichotokea”Hapo Aice alisema hivyo huku akikumbukia maumivu aliyoyapata wakati wa zoezi la utoaji mimba ilie ambayo waliipata biala kukusudia
“Sasa usiku huu mimi nitazipata wapi” aliuliza Dulah. Ndo utajua sasa Alice alimjibu huku akishuka kitandani na kuanza kuvaa taiti kama njia ya ya kusisitiza kuwa hayupo tayari kufanya tendo hilo bila kutumia kondomu. Baada ya kuvaa alizima taa na kupanda kitandani.
Dulah akamuuliza kwa hiyo hiyo ndo kinga yako? Alice akajibu “kabisa kwanza sio lazima kila siku tukiwa wote tufanye mapenzi tunaweza kulala tu kwani ukinioa ndo itakuwa kila siku kuchikuch?”. Dullaha kaangalia simu yake ya mkononi akaona haja ya kwenda maduakni kuchukua hizo kinga maana hasingeweza kuvumilia mpaka asubuhi.
Alivaa nguo zake na kutoka nje na kuelekea dukani.Kwa bahati nzuri alikuta duka ndo linamaliziwa kufungwa. Aliona aibu sana mara baada ya kumkuta mwanamke ambaye waliheshimiana sana. “Una mipira” aliuliza Dulah.Mipira gani aluliza muuzaji akijua kabisa Dulaha alikuwa akitaka kondou.Mipira ya kitandani alijibu Dulah.Ooooh ninayo unatka ya aina gani? Nipe ile ya bei ghali kabisa alisema Dulah. Yule dada akamfungia huku akimwambia “hivi shemeji yupo siajmuona siku nyingi. Dulaha alijibu yupo ndo karudi leo.
Basi akapewa bidhaa zake akarudi eneo la mapambano.Kwa jinsi alivyokuwa na hasira na uchu juu ya Alice alitamani aivalie hiyo kondonu huko huko barabarani.Alifika akakuta Alice ameshapitiwa na usingizi. Mmmmm ameshalala aliguna na kujiuliza Dulah. Hawezi kulala hivi hvi nitapiga hata kimoja cha hamu ndo alale aliwaza Dulah.
Alianza kupitisha mikono yake sehemu zote anazojua mpenzi wake huyo akishikwa basi hupata hamu ya kungonoka. Alizichezea chuchu za mrembo huyo kwa kuzipapasapapsa huku akijisemea moyoni mwake wewe ni wangu huwezi kuondoka na kuniacha niishi peke yangu. “Ila tuache utani huyu mtoto ni mzuri sana yaani nikijichanagnya tu mapesheee hawatamuacha hapa mjni alizidi kuwaza Dulah huku akiamishia zoezi la kumpandisha stimu kwenye mapaja na makalio ya Alice.
Alice akiwa usingizini alianza kuhisi anaota ndoto nzuri ya mahaba akajikuta akaijigeuza kutoka mlalo wa ubavu ubavu na kulalai tumbo.Hapo akawa amempa nafasi Dulaha kuanza kuchojoa ile taiti taratibu huku akiendelea kumpapasapasa sehemu zake za nyuma.
Akawa anayabinyabinya yale makalio kimahaba kama,hiyo haitoshi akaaanza kuyalambalamba kwa kutumia ulimi wake huku akichora viduaara vidogo vidogo kuanzia kwenye mapaja mpaka zile sehemu za goti kwa nyumba ambapo kulikuwa na michirizirmichirizi ambayo kwa Dullah ilikuwa ni kivutio sana.
Alice alikuwa akijigeuza geuza kama ambaye aikuwa hataki kukaangwa akiwa bado mzima. Dula aliendelea na mchezo huo na safari hii alikuwa akifanya double click(akibofya mara mbili).Yaani mdomo ulikuwa ukifanya kazi yake na mikono ilikuwa ikifanya kazi yake.Baadaye samakii alisalimu amri kwa kukubali kuingia kwenye kikaangio ambacho kilikuwa na mafuta ya moto sana.
Alice alishituka kutoka kwenye usingizi na kukuta tayari kisu kipo kwenye ala yake.Hakujua kiliingia saa ngapi kwani yeye mwanzoini alihisi kuwa anaota tena yupo na Deo.Kumbe haikuwa ndoto ilikuwa ni kweli lakini hakuwa Deo alikuwa ni Dulah.
Alice akaanza kujikatisha mauno kama vile feni mbovu.
Alice utamu ulipozidi alijikuta akimkumbatia kwa nguvu Dulaha huku akipiga mayowe ya kimahaba yaani mmmmmmmmh iiiissssssssssssssssss,, aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah,, asaaaanteeeeeeeeeeee,, asanteeeee mpenzi wangu Deo, haaaao haapooooo usitoeeee usitoeeeeeeeee nasikiaa raahaaaaaaaaaa Deo wangu.
Nenoo Deo lilimshitua kabisa Dulaha na kujikuta akipoteza kabisa hamu ya kuendelea na mchezo huo Alihisi mtarimbo wake ukisinyaa tena ukiwa bado upo ndani ya ikulu ya Alice. Alamu za hatari zilipiga kichwani mwake akajua tayari kuna wajanja walishapita barabara hiyo ya lami ya Alice.
Alice yeye aliendelea kumkumbatia kwa nguvu huku akionesha kuwa alikuwa akifurahia sana kumbatio hilo na aliendelea kuzungusha kiuno hivyo hivyo.Kiuno cha chini ambacho Alice alikuwa akizungusaha mara baaada ya Dulaha kutulia kilimrudisha Dulaha mchezoni na kuanza kuhisi raha ya ampenzi iliyopotea ghafla. Dulaha aliendeea kujilazimishana zoezi hilo mpaka pale alipofika kileleni..
Alice alijibwaga kitandani kizembezembe akavuta shuka lake na kuendelea kuuchapa usingizi.Dulaha yeye usingizi ulikataa kabisa kuja akatoka kibarazani na kuanza kuwaza kile alichokisikia. “Hili jina la Deo sio mara ya kwanza kulisikia” aliwaza Dulah. Akaanza kuvuta kumbukumbu zake na akakumbuka kuwa alilisikia siku ile walipokuwa club.Akakumbuka jinsi wale marafiki zake na Alice walivyokuwa wakimsihii aache fujo kwa kumtaja jina lake.
Hasira zikaanza kumpanda kila mda ulivyokuwa ukizidi kwenda,Akaanza kuhisi kuwa Aice amekuja kumsanifu tu kwa sababu ameshaingia kwenye uhusiano na mtu anayeitwa Deo.Akaamua kurudi ndani ili alale na hapo ndipo aliopata wazo la kukaguaa pochi ya Alice Alikutana na vipodozi kibao na kioo na alipojaribu kupekua upande wa pili kakakutana na simu smartphone nzuri kubwa na ya ukweli.Simu hiyo ni ile Alice alikuwa ameongwa na Deo.
Hapo Dulah aalishangaa na kujiuliza ina maana ana simu mbili siku hizi.Ile simu ingne ya Alice ailikuwa hapo juu ya meza ikimaanisha yenyewe haikuwa na majanga na ndo maana haikufichwa. Dulaha akazichukua zote na kwenda nazo nje.Akawasha ile smartphone na akakutana na password. “Ooooops shit” alisema Dulaha mara baada ya kuambiwa enter password.
Bado Dulah hakukubali kushindwa akaanza kujaribu jaribu kwa kuingiza password za kila aiana hasa Alice anazopenda kutumia.Akaanza na mwaka wa kuzaliwa wa Alice bado aliambiwaa ameingiza wrongpassword. Akaingiza namba za siri ambazo Alice anazitumiaga benk lakini bado zilikataa.
Akaingiza jina la Alice bado ilikataa na safari hii alipewa onyo asubiri baada ya dakika tano ndo ajaribu tena.Akasubiri na baada ya dadika kadhaa akaanza kujaribu jaribu sana.Aliposhindwa kabisa aliaamua kuingiza jina la Deo na alishangaa simu imefunguka kiulaini kabisa.
Akakaribishwa na sms za mtu aliyeseviwa beeib.Sms zote zilikuwa za mpenzi na zingine zilikuwa zikiuliza kama Alice alishafika kwa dada yake.Meseji zilionesha wazi kuwa tangia siku ile wamegombana na Alice ndio siku hiyo hiyo Deo aliaanza kupewa nafasi.
Dulaha alibaki njia panda hasijue kwenye mda mfupi huo wa mapenzi yao walishafanikiwa kufanya mapenzi au la?Na kama hawakuwahi kufanya mapenzi kwa nini alitaja jina la mwanaume huyo kipindi alipokuwa akifanya mapenzi.Jasho jembemba lilianza kumtoka Dulah akihisi hatari kubwa juu ya kidudupenzi kuvamia uhusiano wao.
Akachukua namba za Deo akazisevu kwenye simu yake pia akachukua za marafiki zake wa karibu na Alice pia akazisevu. Kisha aakaamua kutuma sms kwa Deo iliyosema “vipi mpenzi, natamani tungekuwa tumelala wote” meseji ikajibiwa mda huo huo “Kwa hiyo ukiwa kwa dada yako ndo unazima simu mpenzi ?. “Hapana simu iliisha chaji alafu umeme ulikatika” alijibu Dulah akijifannya yeye ndo Alice. Deo akaamua kupiga simu mara baada ya kuona sms zake hazijibiwi tena.
“Usipige simu mpenzi usiku huu si unajua nimelala na dada yangu” .Mara baada ya Dulaha kujibu sms hiyo hasira zilimpanda sana hasijue nini cha kufanya.Wanasemaga kuwa kuna zawadi ya uvimilivu na ushindi lakini hii itaukwa ni zawadi ya usaliti.Anasatahiili avune alichokipanda this is too much anda i cant tolerent anya more.
Wakati Dulah akaiendelea kuwa kwenye mawazo mazito na kuonja machungu ya mapenzi usiku huo.Alice alishituka kutoka usingizni na akajikuta yupo mwenyewe kitandani.Akajifunga khanga yake na kutoka nje ambapo alimkuta Dullah akilia kilio ambacho hakikuwa na sauti.Kilio kilichoonesha kuwa alikuwa na uchungu sana ndani ya nafsi yake.
Alice alisogea karibu yake na kuanza kumuuliza “mbona unalia kwani kuna tatizo gani babee.?”.Hapo ndo akawa amemzidishia machungu na kufanya Dulah azidi kulia kama mtoto mdogo.
“Mbona sijakuelewa mpenzi wangu tatizo nini?” alihojii Alice kwa upole.Dullah hakutaka kuongea kwa meneno tu bali vitendo, alimpa ile simu ambayo ndo ilikuwa na ushaidi wote. Alice alianza kutetemeka hasijue nini cha kufanya. Mbona niiificha mbali sana na na ninii kilimfanya apekeue simu yangu aliwaza Alce huku akiendelea kutetemeka?. “Mbona hujibu kitu” aliuliza tena Dulah akwa hasira. “Babee hiyo simu ni ya rafiki yangu alinipa nimsaidie niipeleke kwa fundi alijibu Alice. “Kwa hiyo rafiki yako anaitwa Alice siyo aliuliza tena Dulah kwa ghadhabu. .”Ndio babeee huyo ni wajina wangu aliendelea kudanganya Alice.
“Kwa hiyo wewe unanifanya mimi ni mtoto mdogo sio aliuliza Dulaha na kunyanyua na kuiingia chumbani”. Alice alimfuata huku akimsihi apunguze jazba kwa sababu mambo kama hayo yanazungumzika. “Nilishakwambia nifanyie vitu vyote ila sio usaliti” alisema Dulalah. “Unastahili matunda ya usaliti na leo nitakuonesha” alisema Dulah huku ailifunga mlango na kuongeza sauti yaradio. “Babee punguza sauti ya radio utawaamsha majirani usiku huu” Alice lijaribu kumuelewesha Dulah mara baada ya kuona hiyo sauti ilikuwa ni kubwa sana na ukizingatia ilikuwa ni usiku sana.
Hapo Dulaha hakumjibu kitu zaidi ya kuanza kumshushuia kipondo utazani alikua akipiga mwizi.Alizivuta nywele, akampiga makofi, akachukua mkanda na kuanza kumchpa mapajani. Alimpiga sana mpaka Alice ilimbidi aombe masamaaha kwa kusemaa “babee utaniua niache tu nikuambie ukweli”. “Niaache niachee nitasema ukweli” alilalamika Alice mara baada ya kuona kipigo kimekuwa kikali sana. Alice alilia sana na kujuta kukubali kurudiana na Dulaha ambeye ni mkatili hasiyejua njia sahihi za kujua ukweli kutoka kwa mwanamke. “Haya sema huo ukweli kabla sijakuulia huku ndani” alisema Dulah.
“Kwa kifupi Deoo ni mwanaume aliyekuwa akinisumbua tangia niingie chuoni lakini sikuweza kuwa nae. Siku ile tulipogombana pale club na nikaona umekaa kimya mimi nikajua basi huo ndo mwishoo wa mapenzi yetu, nikaamuaa kumkubalia” alisema Alice huku akijifuta machozi. Hapo Dulaha akashuka kidogo na kuwa mpole na kuuliza “Kwa hiyo ndani ya wikiendi 2 tu ushapata mtu mpya na amekuonga mpaka simu”?. “Babee nisameehe nilifanya maamuizi ya kukurupuka na hata hivyo simpendi ilikuwa ni stresss” tu aliendelea kujitetea Alice. “Kwa hiyo kama humpendi kwa nini ulikubali kuongwa simu tena sim uyagharama kama hii” aliuliza Dulaha kwa hasira.
“Hivi ungenambia kama unataka simu ya kuuzia sura si ningekununulia tu kuliko hivyo unavyofanya kutuchanganya” aliuliza kwa mtindo wa kulalamika kijana Dulah.Waliongea mpka pakakucha lakini hawakufikia muhafaka. Kwa sababu Alice alikaomaa na msimamo kuwa atajua jinsi ya kumalizana na Deo na kwamba ataenda chuo na kumueleza ukweli kuwa amerudiana na mpenzi wake.Dulaha yeye alikomaaa na msimamo kuwa kama kweli anataka kuendelea na yeye ahakikishe kuwa wanampigia simu Deo aje mjini akutane na kuongea ana kwa ana wote watatu. Alice alisema anawajua wanaume wa darasani kwao sio waungwana ni wapenda shari hivyo wakifanya hivyo watamjengea bifu na watu wengi na pia Deo anaweza kumchafuadarasani.
Msimamo wa Alice ndo ulikuwa ni huo hawezi mpigia simu Deo, wala hawezi kumwambia kuwa aende mjini. Muafaka ukashindwa kupatikana ikabidi Omary mzee wa usuluhishi mwenye busara nyingi japo ni kijana mdogo apigiwe simu. Alice alichukua simu yake na kumpigia omary. Omary alipopokea akakutana na sauti ya kike na mara baada ya salamu fupi akamuuliza kulikoni asubuhi yote hiyo?. “Shem naomba uje mara mojakuna tatizo limetokea” chukua bodaboda mimi nitalipi alisema Alice na kukakata simu. Omary hakurizika na maelezo hayo ya Alice akaamua kupiga simu kwa Dullah lakini bado ilipokelewa na Alice an akuulizwa vipi tayari umefika. Hapo ikabdi Dulah awe mpole na kumwabia ndo kwanza yupo njiani anaenda.
Omary akachukua bodaboda na kuelekae eneo a tukio haraka haraka maana alihisi labda Dullah amepatwa na tatizo kubwa na ndio maana hata simu yake ilikuwa ikipokelewa na Alice. Omary alibisha hodi na alipokaribishwa aliingia na kuwakuta wapendanao hao wakiwa wamekaa kihuzuni kama vile kulikuwa na msiba. Alipomwangalia Dullah aligundua kuwa alikuwa na macho mekendu na alipomwangia Alice aligundua kuwa alikuwa amevimba usoni. Dulah aalimpa ishara kuwa aketi sofani.
“Shem basi tumekuita hapa kuna tatizo limetokea usiku” alifungua mazunguzmo Alice kwa staili hiyo. “Baada ya kile kikao kama ulivyoshauri sisi tulikuja hapa huku tukiwa wenye furaha. Ila usiku furaha iliingia doa kwani rafiki yako aliamka na kupekeua pochi yangu na kakuta kuna simu aliyoifungua na kukuta sms za mapeni ambazo nilikuwa nikichati na Deo.Sasa ndo najaribu kumuelewesha Dulaha haelewi na amenipiga sana usiku wa leo” aliongea Alive bla kuweka nukta.
Omrry akauliza “huyo Deo ni nani wako mpaka mnachati sms za ampenzi?”. “Ujue shemu siku ile club Dullaha aliniuzi sana na siku zilizofuata hakunitafuta na uyu Deo mimi alikuwa akinisumbua sana kwa mda mrefu akinitaka kimapenzi ikabidi nimkubalie tu kwani niliamini Dulaha hawezi kuwa na mimi tena” alifafanua Alice.Kauli hiyo ilimchanganya Omary kwa sababu haingii akilini unagombana na mpenzi wako leo alafu kesho yake unakuwa tayari umemkubali mwingine. Alice anasisitiza kuwa alifanya maamuzi akiwa na stress ila bado hajafanya lolote na mwanaume huyo hapa alimaanaisha kufanya mapenzi. Kauli hiyo ilimfanya Dulah hashindwe kuendelea kukaa kimya na kusema “Haingii akilini kwa sababu mimi na wewe hakuna aliyemtamkia mwenzeke kuwa mapenzi yameisha na na ndani ya wiki hiyo hiyo umemkubalia mwanaume mwingine na amekuonga mpaka simu. Mimi naomba utamke mbel aya Omary kuwa upo tayari kuendelea na mimi au Huyo Deo wako”.
“Mimi nipo tayari kuendelea na wewe na ndio maana nimempigia Omary aje tuyamalize.Omary akasema sasa kama ni hivyo mimi naona swala hapo ni dogo sana mpigie huyo Deo mwambie aje mjini mkutane alafu sisi tutajua cha kufanya. Tutakuja sehemu hiyo na kufanya ambushi ya kumuonya aache kutembea na wake za watu.Nazani hiyo ndo itakuwa njia sahihi ya kumfanya akate tamaa na wewe na kukuogoa alisema Omary . “Exacly yaani kama ulikuwa kichwani mwangu alipigilia msumari bwana Dullaha.
“Sio sawa shemu mimi nilikuwa naomba mnipe mda mimi nitamalizana na huyu mtu kwa njia zangu mwenyewe ambazo hazitanichafulia jina hapo chuoni” alisema Alice. “Shem kama kweli umeniita hapa kwa ajili ya usuluhishi basi naomba umpigie simu au niwaache mimi niendelee na shughuli zangu maana tunachojadili hapa ni upuuzi alisema Omary huku akinyanyuka ishara kuwa alikuwa akitaka kuondoka. Alice kuona hivyo akasema “Shemu kaa chini nampgia sasa hivi.Alice akachukua simu lakini hakupiga zaidi ya kubofya bofya kama mtualiyekuwa akichati.Omary akampa ishara Dullah kuwa aikwapue simu.Dullah akafanya kama alivyoambiwa kwa ishara ya kichwa na mikono kisha akafungua mlango na kuondoka zake na kuwaaacha Alice na Omary ndani.
Kitendo cha Dulaha kumpokonywa simu Alice kilimkera sana binti huyo kwa sababu alikuwa kwenye mchakato wa kumtuma sms ya uwongo Deo.Kwa kifupi Alice alikuwa hataki kuachna na Deo kwa ghafla na wakati huo huo alikuwa yupo tayari aendelee na Dulah.Dulah yeye mara baada ya kuipokonya ile simu alitoka nje na kufunga mlango kisha kuondoka na ufunguo.Kwa mantiki hiyo ndani alibaki Omary na shemeji yake.
Alice kwa hasira alianza kupaki nguo zake kwenye mabegi. Dulaha alivyofika getini akamtumia sms Omary kuwa wafanyaje?Omary akamwambia “njoo tufungulie mlango kisha wewe uondoke na hiyo simu mimi nitamalizana naye taratibu kisha nitamwomba tukutane mjini tuyamalize”. Kwa hiyo Dulah alirudi akafungua mlango kisha akondoka zake kama alivyopewa maagizo na mzee wa usuluhishi wa mgogoo wa mapenzi. Omary alifanikiwa kumbembeleza Alice mpaka akakubali kuacha kupanga nguo na kwenda mjini kuongea na Dullah. Basi waliondoka pamoja na wakiwa wanaenda stend ya hice Alice alibadili mawazo na kumwambia Omary “ Shemu mimi sipo sawa hivyo sitaki tena mazungumzo ngoja niende tu kwa mama yangu mkubwa.”
Omary kwa kuwa na yeye alikuwa amechoka kumbembeleza Alice alimkubalia na kumwambia vyovyote atakavyoona yeye ni sawa. Alice akamwambia basi anaomba funguo akachukue pochi yake maana ndo ilikuwa na hela. Ilibidi Omary ampigie simu kwanza Dulah na kumwambia kuwa Alice hataki tena mazungumzo na je ampe funguao maana anadai anataka kwenda kuchukua pochi yake anayodai ina hela.Dulah akajibu kwa kifupi mpe tu hizo funguo. Ingawa Omary alisita kumpa funguo ila kwa sababu mwenye nyumba alisema apewe alimpa. Alice akaita bodaboda na kuondoka zake. “Huyu mwanamke atakuwa na matatizo mengi sana” alisema Omary mara baada ya Alice kuondoka.
Omary akampigia simu rafiki yake Dulah na alimwelekeza sehemu aliyopo.Omary alifika sehemu aliyoelekezwa na alishangaa kumkuta Dulah akiwa anakunywa pombe asubuhi hiyo. “Stress is fertilizer of creativity” Dulah alaimkaribisha kwa kauli hiyo.Ingawa Omary aligundua kuwa rafiki yake anautumia msemo huo vibaya na yeye badala ya kuagiza pombe yeye aliagiza supu. “Kwa hiyo amesema hataki tena aliuliza Dulah wakati Omary akiendelea kusubiri oda yake. Omary alicheka kidogo na kumwambia “ If cant and imposible no way out leave them baried”. “Haina haja ya kung’anga’nia huenda sio fungu lako” aliongeza bwana Omary.Kweli kabisa alidakia Dulaha na kuongeza kuwa yeye anaamini bahati ya mtu ipo mbele kwa mbele.
Waliendela kupiga stori na Dulah alikuwa tayari ameshampigia simu Deo na kumueleza kuwa Alice ni mke wa mtu hivyo awe makini kwa sababu mke wa mtu ni sumu hisiyotibiwa kwa maziwa. “Huyu mwanaume anaoekana kuwa na kiburi sana lakini mimi nitamuonesha mimi ni nani?” aliendelea kusema Dulah. Huu mji ni wa kwetu tumezaliwa humu tumekulia humu hivyo nitatumia gharama zangu zote kuwashikisha adabu aliongeza Dulah. Omary alimwambia haina haja ya kupoteza mda kuaangaika na wajinga kwa sababu kufanya hivyo ni kuwapa changamoto na misukosuko itakayosababisha wao kupendana.
Omary aliendelea kumsihi bwana Dulah hasiangaike na watu hao kwa sababu kufanya hivyo ni swa na kulazimisha mapenzi.
Dulaha alimwambia Omary anamuelewa sana kwa falsafa zake nzuri ila sasa revange is a reason he should get up each day(kisasi ndo sababu inayomfanya amke kila siku). “Ndo maana nakwambia njia hizo hazitakusaidia labda ungebadilisha mikakati kutoka kwenye kisasi mpaka kwenye “Forgiveness is the greatest revange”(msamaha ni kisasi tosha).Kwa upande wa Alice yeye alirudi gheto akapanga vitu vyake kisha akaita tax na kundoka zake. Alichukua vtu vilivyoweza kubebeka na muhimu kwake. Aliwaza kuhusu simu ya Deo aliyoongwa lakini bado hakupata jibu.
Kwa kuwa Dulah alimpokonya simu na kuondoka kibabe na yeye aliamua kuondoka kibabe kwa kundoka na funguo. Aliamini kitendo chake cha kuondoka na funguo kitamfanya Dulah aamtafute na hiyo ndo itakuwa njia rahisi ya yeye kupata simu ya watu aliyoongwa. Aliamini pia bila kurudisha simu hiyo itamlazimu yeye kuendelea na mapenzi na DEO wakati yeye fikra zake zilimtuma kuwa aacahane nao wote na kubaki single.Alice alitaka kabisa kuachana na kitu kinachoitwa mapenzi na badala yake aliweka dhamira ya kusoma kwa bidiii na kufanya mambo yaliyompeleka chuo. Alirudi shuleni na kuendelea na mambo yake.************
Jesca baada ya kumfuatilia mpenzi wake Gastoni mpaka kwenye ile hotel akitaka kujua nini Gaston anakwenda kufanya humo aliwekewa kizuizi mlangoni.Aliulizwa uunakwenda chumba namba ngapi akasema 166 namba aliyoisiki Gaston akiitaja.Muhudumu alimzuia kwa sababu chumba hicho tayari kilikuwa na watu wawili yaani Gaston na Beatrice. Na kwa sheria za hapo hotelini idadi ya wanaotakiwa kulala kwenye chumba kimoja wanatakiwa wasizidi wawili.Jesca wa watu mpenzi wa Gaston ujanja ukawa umemuishia akatamani na yeye achukue chumba sehemu hiyo lakini gharama yake ilikuwa ni kubwa sana.
Akaondoka zake na kuamua kurudi stendi.Alichukua simu yake na kumuandikia sms Gaston iliyosema “najua haupo darasani,upo Arusha kwenye hotel fulani. Gaston mpenzi wangu unavyonifanyia ni usaliti mkubwa ila poa tambua kuna matunda ya Usaliti mara baada ya penzi penzini”. Meseji hiyo ya malalamiko haikuweza kusomewa na Gaston kwa sababu simu yake aliwek asilence mara baada ya kuingia kwenye chumba alicokuwepo Beatrice. Jesca alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa hasaamini kilichotokea.Au nimemfafanisha alijiuiza Jesca lakini hapana sijamfananisha kwa sababu pale stend nilipopiga simu aliitoa na kunitumia sms eti yupo darasani.
Jesca akaamua kumpiga rafiki yake Alice simu kumpa habari hizo. Waliongea mengi na alimueleza kuwa yupo Arusha aliapewa majukumu na baba yake.Alice alimuuliza mbona amekuja kimya kimya bila taarifa.Jesca akamjibu kuwa alitaka kumfanyia suprise Gaston hivyo anakuja Moshi.
Jesca akamuuliza Alice kuwa si anajua chumba anachokaa shemeji yake Gastoni na Alice akamjibu ndio.Badi nakuja ili tuje tumfanyie suprise ya nguvu.Yaani mpka hapo alikuwa hajamwambia ukweli kuwa amemeuona Gaston Arusha alitaka kufika Moshi kwanza ili akakikisha macho yake hasije kuwa anamfananisha.Jesca aliamua kupanda magari ya Dar yanayorudi Moshi kuanzia safari zake hapo.Mida ya saa 3 kasoro alikuwa tayari ameingia mji wa Mmoshi na moja kwa moja alienda mpka chuoni wa kina Alice. Alienda mpaka hostel wanayokaa na alipokelewa vizuri sana.
Baadaye alimueleaza ukweli rafiki yake kuwaa pamoja kuwa amekuja na alitaka amfanyie Gaston suprise lakini mwaanume huyo yupo Arusha na kimwana mwingine. “Gaston huyo shemeji yangu ninayemjua mimi? aliuliza Alice kwa mshangao. Ndio huyo huyo shosti, wakati nashuka stend ya Arusha nilimuon kwa macho yangu mawili nikamigia simu akatoa kisha akakata na kunitumia sms kuwa yupo darasani alizidi kufafanua Jesca. “Wewe utakuwa na wenge la macho, ebu kwanza twende gheto kwake tukamwangalie maana hanaga mambo hayo kabisa na mda mwingi anakuwa gheto kwake akiangalia movie” alisema Alice. Wakaanza safari kuelea kwa kwa Gastoni.
Kwa sababu ilikuwa bado ni mapema waliamua kutembea kwa miguu na walipofika walikaribishwa na kufuli kubwa liloandikwa Top security. “Si nilikwambia ebu jaribu kumpigia simu wewe alipendekeza Jesca mara baada ya kuona kufuli hilo.Alice akachukua simu na kumpigia Gaston.Simu iliita lakini haikupokelewa.Akamtumia sms na kumuuliza “shemu uko wapi mini nipo hapa kwako lakini bado haikujibiwa. Huenda maneno uyasemayo yakawa kweli kwa sababu simu yangu na mimi hapokei alisema Alice mara baada ya kupiga zaidi ya mara moja.
Wakati akisema hayo simu yake iiliita na alikuwa ni Deo akipiga simu.Alice aliiangalia ile simu lakini alishindwa kuipokea. Jesca akamwambia kama ni Gaston anapiga pokea simu tu. “Hapana bora ata angekuwa Gastonn huyu anayepiga simu ni zaidi ya majanga alisema Alice. Baada ya simu kupigwa pigwa mara nyingi ilibidi Alice haipokee na swali la kwanza aliloulizwa ni upo wapi akajibu hostel. “Mbona sikuoni na mimi nimekuja hapa alhoji Deo. “Nipo na rafiki yangu nimemsindikiza kwa boyfriend wake” alijibu Alice.
“Nimekuja kuchukua simu yangu kwa sababu nimechoka kutishiwa maiasha na kutukanwa na bwana wako Dulah. Alice akajibu kwa kifupi kuwa “ataipata kesho kwa leo haiwezekani” kisha akakata simu.
Akavuta pumzi ndefu kisha akaiiachia na kusema “yaani wanaume si jui wapoje wote ni wale wale siku zote”. “Vipi best nani tena anakuvuruga?” ilibidi aulize Jesca. “Wacha tu shosti yale majanga ya Dulaha niliyokwambia yanazidi kuwa makubwa hapa sijui hata nifanyaje maaan huyu aliyenipigia sa hivi alinionga simu yake na huyu ni yule mwanaume aliyekuwa akinisumbua sana sasa mara baada ya kugombana na Dulaha nikajikuta namkubalia yaaani najuta najuta kuwafahamu wanaume” alilalamika Alice huku akipga piga miguu.
“Pole sana rafiki yangu sasa si umrudishie tu simu yake maana huyo hana mapenzi ya kweli” alipendekeza Jesca. “Ujue juzi Dulha alinipigia simu na kunimba tuyamalize tukaenda mimi na rafiki yangu na yeye akawa na rafiki yake, tukafanya kikao na kumaliza na tukaenda kulala gheto. Usiku kumbe mwenzangu akaamkana kuanza kupekua pochi yangu ndo akaikuta hiyo simu ya huyo Deo. Sijui hata aliyejuaje password akaifungua na kukutana na sms za mahaba ambazo nilikuwa nachati na huyo mwanaume” alijaribu kufafanua Alice.
“Sasa sijui kwa nini Dulaha ameshindwa kunielewa maana huyu Deo mimi sijawahi kumvulia chupi zaidi ya kuchati naye utumbo tu.Ebu nishauri nifanyaje maana nimechanganyikiwa mwenzio” alisema Alice. “Sio nikushauri bali tushauriane maana hata mimi sipo sawa” alisema Jesca. Ikabidi waanze safari ya kurudi hostel kwa kina Alice. “Ujue shosti wewe umefanya makosa kwa sababu ni mda mchache sana ukaruhusu moyo wako kumpenda mtu mwingine ambaye pengine hata hakupendi kiukweli alikutamani tu na kutaka kupita nawe.Maana ni kawaida ya wanaume kupenda ngono hata kama ameoa na ana watoto “alifafanua Jesca.
Alice akamjibu kwa kumwambia “hayo yote unayoyasema ni kweli lakini maji yakishamwagika hayazoleki na kwa jinsi Dulah alivyonipiga na kunigeuza gunia la mazoezi siwezi kurudi tena nyuma nitaaishii mwenyewe” alisistiza Alice.Jesca akamwambia “mapenzi ni upofu usiseme hivyo kwa sababu mbele huoni”. Waliendelea kuongea mpaka wakafika hostel ambapo walimkuta Stella na Easther. “Yaanii bora umekuja matusi ninayotukwanwa kwa ajili yako ni makubwa” Stella alimkaribisha Alice kwa staili hiyo. “Nani amekutukana best?” aliuliza Alice kwa upole. “Yaani Deo amekuja hapa kama mbogo amesema eti siku ile tulivyoenda mjini alikuwa anakufuatilia mpaka tulipokuwa pale Uhuru Park na anajua kila kitu kinachoennndelea na bwana wako amempigia simu na kumtishia maisha kama eti ataendelea kukushika masikio” alisema Stela akinukuuu maneno ya Deo.
“Wote ni wapuuuzi tu wasitake kunichanganya” alisema Alice kwa hasira. “Sio wapuuuzi wewe umeshindwa kuzichanga karata zako vizuri huna msimamo hujui ushike wapi na uache wapi” alidakia Easther. “We naye usitake kunivuruga niache kila mtu afuate mambo yake alimjibu” Alice kwa hasira. Alice akamwambia Jesca waondoke eneo hilo wakatafute chakula. Wakenda kuchukua chipsi take away huku Alice akionekana kuchanganyikiwa kabisa. Wakiwa njiani Alice alikuwa akilalamika juu ya Easther “Yaani huyu Easther kushindwa miss university anajiona yeye ndo kila kitu anaweza kuniendesha atakavyo wewe muache tu aaendelee nitamvuruga hasiamini”.
“Achana naye bwana wala usipaniki mambo ya kawaida sana alisema Jesca. Wakachukua chakula na kurudi hostel wakaanza kula huku Alice akiendelea kuzama kwenye dimbwi la mawazo mazito sana hasijue nini cha kufanya. Hapa cha msingi ni kumpigiaa simu Dulah na kumwambia mwenyewe anataka simu yake aliwaza Alice.Alice akanyanyua simu na kumpigia Dulaha ambaye wakati huo alikuwa bar akinywa pombe kama mtu aliyechanganyikiwa. Dulah hakuweza kufanya jambo lolote zaidi ya kumwaaza Alice huku akijiuliza maswali mengi ambayo yalikosa majibu. Aliingalia ile simu ya Alice akaaiacha ikaaita mpaka ikakata kisha akapiga yeye a baada ya salamu Alice alimwambia mwenyewe anataka simu yake.
Dulah kwa akili za pombe akacheka sana na kumwambia “mimi nikajua unaniletea funguo ila kama ni ishu ya simu sahau mimi siwezi kulea ujinga nishaivunjilia mbali”. Alice kwa hasira akakata simu na kusema “huyu hanijui mimi ngoja kukuche nitamuaoneshea”.Akamwangalia rafiki yake Easther aliyekuwepo pembeni na kumwambia haya toa ushauri ila sio lawama. “Mimi naona hapo kwa kuwa una ufunguo kesho tufike eneo la tukio tuchukue kila kitu kinachobebeka alafu tuone nani atakuwa amefaidi kati yako na yeye” alipendekeza Easther. Kwanza vile vitu si mlinunua wote? aliuliza Easther ambaye alionekana ni mjanja kuliko wote kwenye grup lao. Alice akasema “vitu vyote ni vyake sema kwenye hela ya kodi nilimsaidia”.
“Hata kama kwani si alikuwa anaishi na wewe kama amekuoa vile sasa mbona sheria ipo wazi wewe kubali tu ushauri wangu niandae kikosi kazi” alisema Easther. Kila mtu alibaki akimuangalia mwenzake wasijue ujasiri huo mtoto wa kike Easther anaupata wapi. “Mnachoshangaa nini na kunitumbulia mimacho hivi umesahau ile simu ya Deo ni iphone latest thamani yake ni zaidi ya laki tano sasa unafikiri hiyo hela utaipata wapi kama simu imeshavunjwa vunjwa” alihoji Easther.
Wakati wakiendelea na mashauriano juu ya ukatili wanaotaka kufanya simu ya Alice iliita na kuangalia alikuwa ni Omary rafiki yake na Dulah. “Niambie shemu” alisema Alice mara baada ya kupokea simu. “Naomba unisaidie kitu kimoja” alisema Omary.Kitu gani aliuliza Alice? Ni kuhusu hizo funguo maana mule ndani pia kuna vitu vyangu alisema Omary . “Utanisamehe shemu wangu fanya mambo yako hayo mengine tuachie mimi na Dulah” alisema Alice na kukuta simu. Baada ya kukata simu akamwambia Easther sasa unaweza kuandaa kikosi cha kazi akikisha hicho kikosi kuna wanaume wa nguvu maana kishanuka hapa ni kuwindana na kulipa visasi maana huyo aliyepiga simu ndo mbaya zaidi anaweza kumpa ushauri Dulah ukawa na madhara makubwa sana kwetu.
“Sasa hayo ndo maamuzi ya kiume alisema easther huku akinyanua simu na kuwapigia simu wanafunzi wa mwaka wa tatu ambao aliwaamini kuhusu mambo ya fujo. Akaja kijana mmoja na kuanza kupanga mikakati ya kwenda kukomba vitu vyote kwenye gheto la Dulah. “Kama ni hivyo tutaingia na Noah tutasomba kila kitu isipokuwa soffa na kitanda yaani mpaka godoro tutabeba” alisema kijana huyo huku akitafuna mirungi ambayo ilikuwa imejaa mdomoni mwake.
Kwa upande wa Dulah na Omary mara baada ya kupewa majibu hayo mabaya na wao walishauriana juu ya nini kifanyike.Omary alisema huyu mwanamke sio mzuri tukiendelea kumchekea atakuja kubeba vile vitu pale chumbani.Cha msingi ni kuongea na mwenye nyumba tuvunje mlango tubadilishe na kuweka kitasa kingine. Dulah alicheka mno na kumwambia rafiki yake huyo aache mawazo ya uwoga maana Alice hana ujasiri huo kwa sababu vitu vytoe pale ndani ni vya kwake na Alice alichangaia kodi tu. Usijiaminishe ndugu na cha msingi ni bora tukachukua angaliazo aliendelea kusistiza bwana Omary.Na siku zote “usimwamini mbwa anayechechemea au mwanamke anayelia”.
Pia ni vigumu sana kwa sheteani kuwa malaika ila ni rahisi sana kwa malaika kuwa shetani. Wewe unafikiri kwa nini aondoke na funguo zote mbili kama sio ana lake la moyoni alihoji bwana Omary. “Aaaaaahhha hacha uwoga mtoto wa kiume yule demu ni malaya tu hana lolote na hii simu ndo inamchanganya na kwa ushenzi si mrudishii ili nione atafanyaje” alisema Duulha huku akipiga pafu la pombe. Yaani alikuwa ameleewa chakari na Omary alikuwa anaogopa hata kumuacha mwenyewe maaana mda wowote angeweza kufanya kitu kibaya.*
Sehemu Ya 7
Hali ilikuwa ni ya hatari kwa sababu Dulah kabla ya tukio hilo alikuwa akinywa pombe kidogo tu analewa lakini sa hivi akinywa pombe nyingi halewi. Dulaha akasema kesho nitampigia baba mwenye nyumba maana lazima atakuw ana funguo za ziada. “Alafu lakini kwa nini tusipange mbinu ingine rahisi zaidi ya kumfanya Alice ashuke mjini na kuchukua vitu vyake maana lazima afuate vitu vyake mule kuna mpka ATM card yake na ninavyomjua mimi kwa uwoga wake hawezi kushuka mpka hajue sipo mjini”. “Kwa hiyo unafikiri ni mbinu gan?”i aliuliza Omary kwa shaku ya kutaka kujua mawazo yake. “Mimi naona kesho wewe umpigie na kumwabia kuwa nimelzwa KCMC naumwa sana au nimekunywa sumu kwa ajili yake.
Najua atataka kuja hospitali kuniona au kama ulivyosema anaweza kutumia mwanya huo kwenda kuchuka vitu. Hiyo ni idea nzuri sana kamanda nimeipenda hapo lazima tutamshika na tutajua nini muafaka wake akija hospitali inamaanisha bado anakupenda na akikimbilia gheto kuchuukua vitu ujue mapenzi yameisha hivyo.Kwa hiyo pande zote mbili walishaweka mikakati Alice na marafiki zake waliweka mikakata na pia Dula na rafiki yake waliweka mikakati****
Kwa upande wa Gston mara baada ya kuingia hotel ile ya kifahari na kuelekezwa chumba namba 166 ambapo ex girlfriend wake Beatrice alikuwa akimsubiri. Gaston aliaanza kupandisha ngazi taratibu huku akiangaia uzuri wa hotek hiyo. Alifika kwenye hicho chumba kapiga hodi na Beatric akafungua malango huku akiwa amejifunga khanga moja kuanzia kifuani mpaka chini. Beatrice alipanua mikono ishara ya kutaka kumbatio. “Waooooooh my love one and only nilikumiss sana” alisema Beatrice mara baada ya kumkumbatia Gaston na kumpiga mabusu. Waliingia ndani na mlango kufungwa.
“Daaaah umekuwa mtamu zaidi ya mcharo” alichombeza Gaston mara baada ya kuona michirizimichirizi ya nguo ya ndani amabayo ilizibwa na khanga laini.Macho ya Gaston yakaganda kwenye mapaja ambayo kwa sehemu kubwa yalikuwa wazi na kuonesha mpaka vitu vilivyokuwa havistahili kuoekana machana. Beatrice alionekana kuwa mrembo zaidi mara mia zaidi ya alivyokuwa zamani.
“Nimefurahi sana kukuona G wangu yaani atakama ungekuwa umeoa lazima tu ningekutafuta maana wewe ndo furah yangu iliyopotea mda mrefu. Yaani wewe ni zaidi ya alamasi mchangani”aliendelea kumwamga sifa binti huyo. Gaston alibaki akitabassam tu na kushangaa uzuri wa chumba hicho na vitu vilivoymo. “Alafu kuna mtu amepiga simu anaitwa Jesca yupo reception anasema anataka kuja chumba hichi au wewe unamjua alihoji Beatrice?” Hapo Gaston alishituka kidogo mara baada ya kusikia jina lile. “Hilo jina ni la mpenzi wangu au alikuwa akinifuatilia nin?” aliuiliza Gaston na kutoa simu yake mfukoni. Hapo ndo akaziona zile sms zilizotumwa na Jesca “Najua haupo darasani upo Arusha kwenye hotel moja ila fanya yote lakini jua kuna malipo ya usaliti” meseji hii ndo ilimchosha kabisa Gaston. Beatrice kuona Gaston amachanganyikiwa ghafla akajua kabisa kitumbua chake kinaweza kuingia mchanga dili likageuka dirisha.
Beatrice akamsogelea zaidi Gaston na safari hii akaamua kuvua kabisa ile khanga na kubaki na kibikini tu huku matiti yake yaliyochongoka vizuri yakibaki wazi dhahiri bila kificho.Beatrice akaamua kumpagawisha mwanaume uyo kwa haraka maana anaweza kubadili mawazo na kuondoka zake mara baaada ya kugundua alikuwa akimpenda sana huyo mtu aliyeitwa Jesca. Gaston akamuuliza Beatrice “tufanyaje mara baada ya kugundua kuwa tayari mambo yalishaahribika?”. “Cha msingi wewe zima hiyo simu au weka silent kisha tufanye yetu kwanza maana maji yakishamwagika hayazoleki”.
“Na leo nitakupa vitu hadimu ambavyo hujawahi kupewa na huyo Jesca wako” alisema Beatrice kwa sauti ya mahaba. Akamsogelea zaidi na kuanza kumpapasa kifuani kwa kutumia mikono yake laini. “Naomba maji ya kunywa” alisema Gastonn mara baada ya kushikwa kidevu na kuchezewa chezewa vimzuzu vyake alivyokuwa ameviachia kama beberu. Beatrice kwa mbwembwe huku akiwa ndani ya kibikini tu akaanza kutembe kwa mwendo wa kimiss huku akifuata simu ya mezani. “ Helow chumba namba 116 nikusaidie nini aliuliza yule dada wa reception. Naomba niletee chupa ya Amalura na maji ya Kilimanjaro .
Gaston akashituka kidogo mara baaada ya akusikia chupa ya Amalura wakati yeye amezoea kuona watu wakipimiwa kwenye glass tu. Mlango ukagongwa na muhudumu akaleta vitu alivyoaagizwa.Beatrice akachukua glass akamiminia maji kisha akaanza kunywa yeye na kumpa Gastoni ambaye bado alikuwa dilema hasijue nini cha kufanya juu ya Jesca wake.
Baada ya kunywa maji alimiminiwa glass ya amalura akapiga pafu moja na kujihisi yupo sawa. Beatrice hakutaka kumpa nafasii ya kumuwaza Jesca wake alimsogelea na kumkalia mapajani huku akiongea naye kwa sauti ya mahabaaa. “Yaaani leo babee nimekuandalia vitu vizuri sana na hautojutia kuwa na mimi” alisema Beatrice huku akijisugua sugua kimtindo mara baada ya kuishi mtarimbo wa Gaston ushaanza kupiga piga pushapu kama zile za Magufuli kwenye makalio yake.
“Ujue Gaston wangu mapenzi yapo kama dunia na yanakuwaga na mzunguko hivyo lazima uweze kuacha vitu vibaya ili uweze kupata vitu vizuri” alisema Beatrice. Wakati wako ni sasa naamini hautahuzunika tena kuhusu mapenzi maana mimi furaha yako nimerudi kwa ajili yako alaiendelea kutamba Beatrice.Pamoja na maneno yote mazuri hayo bado Gaston akili zake hazikuwepo hapo. Alihisi amepoteza dhahabu kwa kuangaika kukusanya mchanga.
“Kwa jinsi ninavyomjua Jesca this love is over” aliendelea kuwaza Gaston huku akijaribu kupitisha mikono yake kwenye kifua cha Beatrice sehemu za matiti.Akakaribishwa na joto zuri la huba ambalo lilikuwa limejiifadhi kwenye kifua cha binti huyo.Binti huyo akajikalisha vizuri kwenye mapaja ya Gaston huku akianza kuhema kwa nguvu kutokana na mikono ya Gaston kubarizi na kutalii kwa spidi kubwa kwenye mwili wake.
Kitendo kile cha Beatrice kukaa vizuri kwenye mapaja ya Gaston kilimfanya mtarimbo wa Gaston uanze kuumuka na kuvimba utazani umewekewa amira. Gaston mawazo ya Jesca yakatoweka uchu na tamaa ya kutaka kuupanda mlima wa Beatrice vikamtawala.Alitumia nafasi hiyo kumgeuza kichwa binti huyo na kukutanishi ndimi zao na kuanza kupeana denda la huba lenye ladha ya ile amalura.
Hapo sasa ndimi kwa ndimi mdomo kwa mdomo vilizungumza. Gaston alaijikuta akinyonya ndimi za Beatrice na kuhisi ladha tamu na adimu ambayo alipotezana nayo kwa mda wa miaka miwili. Mambo hayo yalimfanya asahau yote yaliyotokea na kukumbuka mbali sana enzi akiwa na binti huyo aliyemfundisha mapenzi. Beatrice alizidi kutoa mihemo ya huba huku akaiamini siku hiyo itakuwa ya furaha sana kwake.Beatrice akaona anapata tabu sana kunyonya ndimi kwa kuzungusha shingo yake akaaamua kugeuka na kumkalia Gastoni kwa mbele wakawa wanaangaliana mbele kwa mbele jambo ambalo liliongeza msisiko zaidi.
Vifua vyote viwili vikawa vinasuguana na kila mmoja wao akapitisha mikono yake kwenye mgongo wa mwenzake na kuanza kumpasapapasa kimahaba. Spidi na hashki hashki za mapenzi ziliongezeka na Gaston akambebea juju juju Beatrice na kumwaga kitandani. Akuataka kuchelewa zaidi aliamua kumchojoa kile kibikini kilichobakia.Hakutaka papara bali alikivua kwa madaha utazani anamvua mtoto mdogo. Alipopitisha mikono yake kwenye ikulu ya binti huyo alikaribishwa na unyevu nyevu na ute ambao tayari ulishalowanisha sehemu hizo kutokana na romance waliyopeana.
Hali hiyo pia ilimtokea Gaston maana na yeye sehemu ya mbele ya kirungu chake kulikuwa na kamasi jembembe linalovutika kuashiria kuwa yupo fiti kimaumbile.Staili ya mnyoo wa nywele za sehemu za siri za Beatrice ulimvutia sana GastOn kuendelea kuzichezea sehemu hizo. Akamkumbuka Mwajabu yule classmet wake alivyomfundisha jinsi ya kuchezea maungo ya mwanamke hasa zile sehemu zenye msisimko na kuleta raha ya huba. Staili za kizungu ambazo Gaston alishazizoea kuziona kwenye mikanda ile inayokatazwa zilitosha kabisa kumfanya na yeye apitishe ulimi kwenye tundu la sindano.
Na kwa kuwa macho yake yana matatizo ya kuona mbali ikawa ni kazi sana kwake kuingiza uzi kwenye tundu la sindano hivyo akawa anaingia na kutoka mpka pale aliopofanikiwa kulilenga lile tundu ambalo linauwazi linaloruhusu uzi kuingia.Baada ya kugundua kuwa amepata sehemu inayostahili aliendelea kunyonya kiulaini kama ubuyu vile. Beatrce alitoa sauti zote za mahaba ambazo hakuwahi kulia kabla.Mmmmmmmmh isssssssssssss ooooooooooy kwiiiiiiiiiiiii kwii wiiiiiiiiiiiiii haaaaaapoooooooooo hapoooooooooo.Kelele hizo zilihashiria pia kuna kitu alikuwa anakimiss hivyo aliamua kukitafuta kwa kutumia mikono yake.
Na alipofanikiwa kuushika mtarimbo wa Gaston aliuelekeza kwenye kinu chake tayari kwa shughuli ya kutwanga na kupepeta.Kwa kuwa ndo kwanza kinu kilikuwa na unyenvu nyevu, kilimfanya mtwangaji kutwanga kwa nguvu bila kupata ugumu wowote.Zoezi hilo liliendelea huku kila mmoja akijaribu kucheza na hisia za mwenzake ili wamalize pamoja.Baada ya dakika kadhaa walikuwa juu ya kilele wakibarizi upepo mwanana na kupiga picha za ukubusho.
Kila mmoja a likuwa kimya akivuta pumzi ndefu na kuhema kwa nguvu kutokna na nguvuu nyingi walizotumia kuhakikisha wanafika hapo. Na kwa kuwa mlima kilianjaro una vilele viwili yaani Kibo na Mawezni waliingiwa na tamaaa ya kupanda vilele vyotev iwili kwa mda mfupi.Safari ya kuelekea kilele kingine ikaanza na ufundi mdogo tu ulitumika kwa sababau kila mtu alishajua njia ya mwenzake. Hivyo wakaazna raundi ya pili na sehemu ya kukimbia walikimbia na sehemu ya kutembea polepole walietembea pole[ole.
Baada ya mda wakawa wanaweza kushuka kutoka kilele kimoja na kupanda kilele kingine. Kila mtu alikuwa amerizika na dozi waliyopeana huku wakiaamini wanaweza kufanya hivyo tena usiku wa manane kwa kupanda vilele vya milima mingine kama safu ya milima ya himalya ya mlima Everrist. Waliweka camp wakapumzika na baadaye walienda kuoga kisha kwenda kupata chakula sehemu ya juu ya hotel hiyo ambayo ilikuwa wazi.
Sehemu hiyo ilimfurahisha sana Gaston maana ilimwezesa kuliona jiji la Arusha kwa uzuri zaidi.Waliendelea kufurahia chakula kilichopikwa kwa utaalamu wa hali ya juu. Beatrice hakuacha kumsifia Gaston kwa raha nzuri alaizompatia. Akaamini kuwa kile alichokuwa akikitafuta kwa miaka mingi sasa amekipata. “Hivi haya maufundi ya kuchezea maungo ya mwanamke ulijifunzia wapi”? aliuliza Beatrice maana siku hiyo Gaston alimfikisha kileleni mara nyingi tofauti na siku nyingine. “Wewe unafikiri nitakuwa nimejifunzia wapi kama sio Kwa Jesca” alijibu Gaston kuonesha kuwa binti huyo bado alikuwa akilini na moyoni mwake.
“Ukiwa na mimi naomba usilitaje hilo jina tafadhali” alisema Beatrice kuonesha kuwa amekereka. Gaston ahakujibu kitu zaidi ya kuendelea kufakamia chakula amabcho kilikuwa mbele yake. “Asante kwa chakula alisema Gaston mara baada ya kumaliza kula. “Yaani wewe unanichekesha sana asante kwa chakula kwa ni mimi ndo nimepika?” aluliza Beatrice. Mama yangu alinifunza kushukuru kabla na baada ya kula na kama chakula hiki umelipia wewe basi inanipasa kushukuru alisema Gaston. “Dah inaelekea siku hizi una busara” sana alisema Beatrice mara baada ya kufurahiswa na maneno ya Gaston.
Waliendelea kupiga stori za hapa na pale huku kila mmoja akimuuliza mwenzake maisha yaliendaje mara baada ya kuachana.Kila mtu alaieleza raha na karaha alizozipitia. Baadaye waliamua kuingia ndani mara baada ya kuona hali ya hewa imebadilika na kuwa ya baridi.Kibaridi cha Arusha kilianza kupuliza na kufanya sehemu hiyo ya juu kushindwa kukalika. Waliingia ndani na kulala. Usiku wa manane Beatrice aaimwamsha Gaston ambaye alikuwa akifurahia usingizi mwanana kwenye kitanda hicho chenye raha za ajabu.
Beatrice hakuona aibu ya kumuamsha kwa nguvu mara baada ya kuona juhudi zake za kumchezea na kumshikashika kunako haziizai matunda. Gaston kwa kuwa alikuwa na uchovu wa masomo alijigeuza na kumpa ishara kuwa Beatrice ajipakulie mwenyewe.Beatrice akapanda juu na kuanza kuongoza safari hiyo inayoaaminika kuwa na raha sana raha za huba. Beatrice akajipakulia saizi yake na alisahau tu kuweka matunda ambayo yangefanya umlo huo kuwa mlo kamili. Gaston kwa kuligundua hilo aliamua kumuwekea matunda kwenye sahani yake kwa kumsalidia kumpakulia vitu hadimu. Sio matunda tu bali alimwekea chachamdu kali ya mapenzi na kumfanya Beatrice kutoa machozi na kujuta kuomba kupakuliwa chakula hicho usiku huo.
Walimaliza na kupitiwa na usingizi.Alfajiri na mapema kibaridi kilizidi na kumfanya Gaston ashituke na kutaka kutafuta joto kwenye mwili wa Beatrice. Kwa kuwa Gaston ndo alikuwa dereva mzoefu basi hakutaka kumsubiri sana abiria wake yeye aliwasha gari na kupiga honi kuashiria safari inataka kuanza. Abiria Beatrice alikuwa anasuasua kuamka hivyo Gaston aliamua kuupanda mchuma hivyo hivyo. Beatrice kuja kushituka usingizini anakuta tayari ndege ishaanza safari ikabido na yeya afunge mikanda vizuri ili hasije kupatwa na majanga.Safari hii Beatrice alikuwa chini akizungusha zungusha ki kwetu kwetu kile kiuno laini alichojaliwa na Mungu. Alizungusha kisawasawa na ikumbukwe Beatrice alijua kutofautisha mauno ya sebene na mauno ya mahaba niue nilegeze na kunigaragaza kabisa.
Zoezi liliendelea mpaka wote wakafikia safari yao ya mda mrefu ambayo walikuwa wameianza tangia jana na kuweka vituo mbali mbali kwa ajili ya kupumzika.Walikaa hapo mpaka mida ya kurudisha chumba na kwa sababu Gaston alisisitiza kuwa anataka kurudi chuoni basi ziara yao iiishia hapo. Beatrice naye akasema anaenda Moshi kumsalimia bibi yake hivyo wote safari yao ikawa ya kuelekea Moshi. Walipofika stend ya Moshi Gaston ilibidi amsindikize Beatrice kwenye stend ndogo ambapo angepata magari ya kuelekea huko Marangu Mtoni.
Kumbe wakati huo na kina Jesca na Alice walikuwa stend.Jesca alikuwa akirudi zake Arusha kukamilisha kazi aliyotumwa na baba yake. Walifanikiwa kumuona Gaston akiwa na kimwana huyo ambaye pamoja na mambo mengine aliwafunika Jesca na Alice kwa uzuri. Mbaya zaidi Jesca alifanikiwa kumtambua Beatrice kwa sababu licha ya kusikia historia yake pia Gaston aliwahi kumuonesha picha zake na kumueleza kuwa huyo ndiye alikuwa girlfriend wa kwanza.
Roho ilimuuma sana Jesca na kuamua kumfuta Gaston na kabla hata Beatrice hajapanda gari alitokea mbele yao.Ilikuwa ni zaidi ya shoti ya umeme kwa Gaston kumwona Jesca akiwa mbele yake na sio Jesca tu bali na shemeji yake Alice. Jesca alimsogelea huku machozi yakimtoka na kumwambia “ Gaton asante kwa zawadi ya usalit lakini tambua ipo siku utanikumbuka na wewe utaonja machungu ya usaliti”. Beatrice naye kwa mbwembwe aliuliza huyu ndo nani babee? Gaston hakuwa na jibu la swali hilo zaidi ya kuendelea kukaa kimya na kutetemeka utazani kulikuwa na baridi kali ya kutisha.
Gari likuja na Beatrice akambusu Gaston akaanda gari na kuondoka zake. Jesca akazidi kupandwa na hasira na yeye akavuka barabara na kuondoka zake.Alice alishika kichwa kwa jinsi rafiki yake alivyovuka barabara kizemba bila kuangalia pembeni. Mlio wa honi ulipoigwa na gari ndo ndo ulimshitua kila mtu na kuthibitisha kuwa Jesca alikuwa amechanganyikiwa kwa kile alichokiona.
“Take care of her, we will talk later on”(muangalie tutaongea baadaye) alisema Gaston mara baada ya kuhisi kuwa Jesca hakuwa sawa na anaweza kupatwa na matatizo makubwa mda wowote. Alice naye alivuka barabara kumkimbilia rafiki yake.Gaston alifikiria haraharaka cha kufanya akaona bora awafuate kwa nyuma Aliwakuta ndo wanaagana hili Jescaa ingie kwenye gari tayari kwa kuondoka na kurudi zake Arusha. “Please baby, naomba tuongee” alisema Gaston kwa upole. “Sina mda wa kuongea na msaliti, nimekuona jana Arusha kwa macho yangu na leo pia”alisema Jesca kwa hasira. “Ndio lakini hujui yule ni nani yangu nahitaji kukuelewesha” alijaribu kujitetea Gaston.
“Usipoteze mda wako huo ndo mwisho wa mapenzi yetu wewe endelea tu na Beatrice wako sihitaji kuwa na wewe tena endelea na ex wakoo maana naona penzi limefufuka upya” ,alisema Jesca na kupanda gari.Wakati huo huo Dulaha naye alikuwa ghoofani hapo stend akiwaangalia watu hao waliokuwa chini.Ingawa alikuwa juu lakini aliweza kuliona tukio hilo na akajua kabisa kulikuwa na kutokuelewana. Alibahatika kumtambua Jesca na Alice lakini Gaston hakaumfahamu.Jesca alimtambua kwa sababu kipindi kile alipokuwa akimfuta Alice Dodoma huyo ndo alikuwa kampani kubwa ya mpenzi wake Alice.
Ili kujua nini kinaendelea alimwambia rafiki yake Peter aliyekuwa naye amfuatilie Alice na Gaston ajaue wanaenda wapi alafu yeye atamfuatilia Jesca kujua nini kimetokea mbona kama walikuwa hawaelewani.Kwa bahati mbaya Dulaha hakubahatika kumjua Gaston hivyo hakujua nini kilikuwa kinaendeea na alihisi labda ni mpenzi mpya wa Alice.Dulaha akaingia kwenye gari alilopanda Jesca na alimfuta. “Vipi shemu alimgusa begani mara baada ya kumuana Jesca akiwa amejiinamia kwenye siti ya gari.
Jesca alinyanyuka kwa nguvu akizani labda ni Gaston aliamua kumfuata tena huko ndani. Alivuta pumzi ndefu mara baada ya kugundua kuwa sura hiyo haikuwa ya Gaston bali shemeji yake Dulah.Jesca alikuwa akimkubali sana Dulaha na aliaamini kuwa ni miongoni mwa wanaume waliojua kupenda, kujali na kutunza msichana. “Mambo shem alisema Jesca mara baada ya kumwangalia Dulah machoni. “Salama tu shemu za kwako , alafu umekuja hata kunitafuta? Alilalamiaka Dulah. “Yaani wewe acha tu niipanga kukutafuta ila kwa majanga yaliyotokea nimechanganyikiwa mwenzio” alijibu Dulah.
“Yaani hapa na majeraha ya moyo sina hata chembe ya amani moyoni mwangu” alisema Jesca. Kwa bahati mbaya gari lilianza kuondoka hivyo ilimpasa Dulah kushuka ikabidi kondakta wa gari hilo kumuuliza vipi kamanda unaenda Arusha?.Hapana nashuka ila huyu ni abiria wangu msimtoze nauli aliwambia konda kisha na yeye akashuka. Jesca aliendelea kujiuliza maswali mengi sana kuhusu wanaume.Hivi ni kweli huyu naye ni mkorofi au rafiki yangu Alice ndo mkorofi alijiuliza jesca mara baada ya Dulah kushuka kwenye gari. Jesca roho ilikuwa inamuuma sana kuona anampoteza Gaston mwanaume ambaye alikuwa akimpenda sana. Au sijui nimsamehe tu tuendeeee na mapenz yetu ila no, kuna makosa ya kusamehewa lakini sio usaliti aliendelea kujisemea Jesca. Aliendelea kuwaza kuhus mapenzi huku akilinganisha pia na mapenzi baina ya Alice na Dulaha ambao na wao walifikia mwisho.
Aliendele kumtafakari Gaston na kujikuta akijisema kweli awali ni awali na hakunaawali mbovu. Yaani Gaston na ujanja wale wote amekwama kwa Beatrice mtu aliyemwacha na kumtupa kama kifaranga cha kuku ndipo mimi nikamuokota?Kweli mapenzi yanarani dunia aliendela kujiuliza maswali mengi Jesca yasiyo na majibu.Dulha alishuka kwenye gari alimpigia simu rafiki yake Peter na kumuuliza yupo wapi. Peter yeye baada ya kupewa kazi ya kuwafuta Alice na Gaston aliwashuhudia wakienda stend ya KCMC.Hivyo kwa mantiki hiyo ni kwamba walikuwa wanaenda chuoni na wala Alice hakushitushwa na habari kuwa Dulha alikuwa amelazwa hospitalini.
Walifikiri cha kufanya haraka harakawasijue cha kufanya na kwa sababu Omary hakuwepo waliamua kuingia mahali wakaendelea kupata kinywaji huku wakimsubiri mwenzao Omary maarufu kama mzee wa plan B.Alice alifika chuoni na rafiki yake Stela na Easther walikuwa wakimsubiri tayari kwa ajili ya kwenda kukamilisha lile zoezi la kuchukua vitu kwenye gheto la Dulah. Waliingia kwenye Noah na kulikuwa pia na wanaume wawili ambao walikuwa wakiwamini kwa ajili ya usalama wao. Walifika sehemu ambayo gheto lilkuwepo wakafungua na kuingia ndani.Wakaanza kukomba vitu vyote vilivyokuwa vikibebeka.
Alice alikuwa akijiamini kwa sababu walikuwa na wanaume ambao waliaminika sana kwa mambo ya vurugu pale chuoni kwao.Baada ya kuhakisah kuwa wamebeba vitu vyote vya thamani isipokuwa kitanda na sofa waliingia kwenye Noah na safari ya kurudi chuoni ikaanza. Jirani ambaye alishuhudi vitu vikibebwa aliingia hofu kwa sababu Dulha alishamueleza kuwa walikuwa na ugomvi na Alice. Pia Dulah alishampa kazi mama huyo ambaye mda mwingi alikuwa akishinda nyumbani kuwa atakapo muona tu Alice ampe taarifa.
Hivyo alimpa taarifa na Dulaha na kikosi chake na wao wakawa wanakuja kwa kasi ili kuzuia uharamia huo uliokuwa ukitendwa na mabinti hao pamoja na wanaume wa kukodi. Yaani wanafika tu wanakutana na Noah ikitoka na kuondoka ikabidi wageuke na kuanza kuwafukuzia kwani na wao walikuwa kwenye gari ainaya spacio.
Ile Noah ilienda mpaka stend kisha Alice na mwanaume mmaja wakashuka wakawa wanaelekea kwenye jengo la ghorofa ambalo lipo hapo stendi. Dulah naye akashuka kwa kasi ya ajabu huku mkononi akiwa ameshika chupa kubwa ya konyagi wenyewe wanaita Mzinga bapa tayari kwa kwenda kufanya fujo. Omary ilimbidi apaki gari na kujaribu kumfuata Dulha kwa sababu alijua kabisa kwa jinsi Peter alivyokuwa na umbo dogo ni lazima atashindwa kummudu. Omary alimkimbilia Dulah na kujaribu kumsihi hasifanye tukio lolote baya ambalo litachafua jina lake na jina ya kampuni yao hapo stendi. “Nasema niacheni niipasue sura yake ambayo ndo anaringia alisema Duhal kwa ghadhabu. Peter yeye alimfuatilia Alice ili ajue alikuwa akielekea wapi.
Kumbe Alice alikuwa ameshatafuta mteja wa baadhi ya vitu ama flat screen na sabufa. Baada ya Peter kusikia watu hao wakipatana bei alishuka ngazi tayari kwa ajili ya kwenda kutoa taarifa. “Jamani tusifanye makosa hivi vitu vinataka kuuzwa”alisema Peter.Tufanyaje aliuliza Dulha huku akionesha kuwa ni mtu aliyechanganyikiwa kutokana na tukio hilo. “Sasa sikia hapa tutumie sheri na tuwakamate kama wezi” alipendekeza Omary huku akianza kutembea na kuelekea kituo cha polisi ambacho kipo hatua chache kutoka hapo stendi. Peter wewe baki hapo angalia wasije wakatoroka, lipendekza Dulah.
Wakati wanaelekea kituoni Dulah alimuona polisi anayemfahamu hivyo kamuuelezea suala lake haraka haraka sana. “Sasa siku hizi huwezi kumkamata mtu bila kuchukua RB kwa hiyo nendeni mkachukue Rb kwanza kisha ndo tumkamate alipendekeza afande huyo.Dulaha hakutaka kuongea mengi aliingiza mkono mfukoni akatoa noti ya shiling elfu 10 akamkabidhi kisha akamwambia “ naomba tusaidiane tumkamate kwanza then tutafuata hizo taratibu zingine” alisema Dulah. Yule polisi hakujivunga siunajua tena mambo ya mama bandika ugali mboga nitaleta.
Sasa kama mtu mwenyewe ni wa kike mimi siruhusiwi kumkamata njooni huku tuchukue askari wa kike alipendekeza huyo afande. Fasta fasta askari wa kike alipataikana na Alice alifuatwa na kuwekea chini ya ulizni. “Upo chini ya ulinzi kwa kosa la uwizi alisema askari huyo wa kike. “Naomba utii sheria bila shuruti twende kituoni na utaambiwa umeiba nini na nini alijibbiwa Alice mara baada ya kujitetea kuwa yeye sio mwizi. Alice hakuwa na ujanja zaidi ya kukubali kwenda polisi.Yule kaka aliyekuwa na Alice akawafuta wenzake kwenye gari na kuwaeleza kuwa mambo yameshaharibika dili limegeka dirisha. Alice alipelekwa rumande na kinyume na sheria RB ikakatwa baada ya yeye kukamatwa.
Baadaye wote wawili yaani Dulah na Alice walitakiwa kuandika maelezo. Alice alisisitiza kuwa yeye hajamuibia bali alichukua vitu alivyonunua yeye. Kwa mujibu wa maelezo aliyayaandika Alice, ni kwamba katika chumba hicho kila mtu alikuwa na mchangoo wake.Kwa hiyo yeye alinunua vitu vya ndani na Dulah ndo alilipa kodi.
Maelezo ya Dulaha yalitofautiana maana yeye alisema binti huyo hakuwa na kitu hata kimoja na vyote alivinunua kwa pesa yake.Yaani kwa kifupi wote walikuwa wakiongopa na kudanaganya polisi. Ukweli ni kwamba Alice alikuwa na mchango kidogo katika kodi na vitu vyote alinunua Dulah.Ikabidi polisi waende mpaka gheto kuangalia chumba hicho na vitu vilivyochukuliwa.Wakakuta kweli chumba kimekombwa na cheupe peee kama mtu ndo alikuwa anaanza maisha. Polisi walienndelea kubaki dilema wasijue mkweli ni nani, ikabidii watumie diplomasia.
Waliwasii wapenzi hao wayamalize mambo hayo na warudiane na waendelee na maisha yao kama kawaida.Lakini Alice alikiri na kutamka mbele ya polisi na Dulaha kuwa hayupo tayari kurudiana na mwanaume huyo na wala hampendi hata kidogo.Kauli hiyo ilikuwa ni zaidi ya mkuki moyoni aua mwiba kidoleni kwa Dulah. Dulah alikuwa yupo tayari wayamalize na waendeeaa na mapenzi yao lakini Alice alitamka kwa kinywa chake kuwa hampendi na anamchukia kuliko maelezo. Ikabidi Alice aendeeelee kukaa rumande na Dulaha alisistiza kuwa Alice afunguliwe kesi ya wizi. Dulaha alikuwa yupo tayari kutumia gaharamm yoyote ilimradi tu amshikishe Alice adabu.
Huko nje ya kituo chao polisi idadi ya wanachuo ilizidi kuongezeka na kila mmja alitaka kuonesha mchango wake wa kumtoa Alice kituoni. Juhudi zao zilikuwa zikigonga mwamba kwa sababu Dulah alikuwa ni mtu maarufu akitumia jina la baba yake na kuna baadhi ya polis alishawapa pesa ilimradi tu binti huyo alale polisi. Baadaye taarifa zilimfikia Gastonn kuwa shemeji yake yupo kituoni hivyo na yeye akashawishika kwenda ili aone atamsaidiaje. Gaston alivyofika eneo hilo akakuta mambo ni magumu na wanachuo wenzake walishakata tamaa ya kumtoa Alice maana inaonesha dhairi sheria zilikuwa zinapindishwa mara baada ya nguvu ya pesa kutumika.
Sehemu Ya 8
Gaston akafikiria haraka haraka akaona njia sahihi ni kutafuta msaada wa kisheria kutoka kwa mtu aliye na uelewa mkubwa wa sheria. Wazo lake likadondokea kwa binamu yake ambaye alikuwa ni wakili wa kampuni moja hapo mjni Moshi.Alimpigia na kumuelezea kwa kifupi kilichotokea.Mwanasheria huyo akamwambia hakuna sababu yoyote itakayomnyima Alice dhamana na kumfanya alale rumande zaidi ya kumsumbua tu.Kosa kama hilo ni dhairi kuwa anatakiwa apewe dhamana na kisha kama kuna ushadi wa kueleweka kesi ipelekwe mahakamani na huyo mwanaume anatakiwa atambue kama aliishi na huyo binti zaidi ya miezi sita kama mke na mume basi hivyo vitu watagawana aljaribu kufafanua mwanasheria huyo mara baada ya kupigiwa simu. Basi Gaston alimuomba mwanasheria huyo aje polisi kuwasaidia kumtoa huyo binti maana wao wamegonga ukuta. Basi wakili huyo akakubali na wakakutana polisi.
Mda ulikuwa umeenda sana na kina Dulah walikuwa wameshaondoka huku wakiwa na imani kuwa binti huyo atalala rumande kutokana na hongo waliyokuwa wametoa. Alice naye alishakata tamaa kwa sababu watu wote walishaondoka akawa amebaki mwenyewe huko ndani ya kituo. Hakuona msaada wa kina Deo, Easther , Stela na wapambe wengine waliomshauri kufanya upuuzi huo wa kuchukua vitu vyote vya Dulah. Alice hakuamini kuwa kosa hilo ambalo llikuwa halina kichwa wala miguu ni kweli llikuwa likimfanya alale polisi.Roho ilimuuma sana na kuamini kuwa Dulaha alikuwa ni mwanaume mwenye roho mbaya pengine kulo wanaume wote huku duniani.
Mida kama ya saa sita usiku Alice alishangaa kuitwa na polisi kaunta na alishangaa kuona anatolewa sehemu hiyo iliyokuwa na sifa mbaya. Alikabiziwa vitu vyake na kuambiwa kuwa ahakikishe kuwa kesho saa mbili anafika kituoni hapo. Gaston alimtambulisha Alice kwa mwanasheria huyo na baada ya utambulisho walikuwa wapo huru kuondoka zao. Alice hakuaamini kuwa eti Gaston ndo alikuja kumpa msaada mara baada ya rafiki zake wote kushindwa kumsaidia.
Hakujua ni zawadi gani Gaston anastaili kwa mchango wake huo wa kuepusha historia mbaya ambayo ilikuwa itokee historia ya kualala polisi.Kwa sababu wakili huyo alikuw ana gari na yeye alikuwa akikaa Soweto na mda ulikuwa umeenda sana aliamua kuwalipia tax iwapleke huko maeneo ya chuoni na yeye kuwahi nyumbani kwa sababu hata hivyoo kwenye gari alikwa na mkwe amabaye alikataaa kuachwa mwenyewe nyumbani usiku huo.
Kwa hiyo wakaachiana hapo kituo cha polisi. Gaston na Alice wakaingia kwenye gari(tax) tayari kwa kuelekea maeneo ya chuoni. Wakafika kwenye geti la chuo ambapo Alice alitakiwa kushuka kwa sababu alikuwa anakaa hostel za ndani ili amuache Gaston aendelee na safari mpka ghetoni kwake mita chache kutoka hapo getini. Mlizi wa kwenye geti la chuo alimtaka Alice aoneshe kitambulisho kuthibitisha kuwa yeye ni mwanachuo. Kwa bahati mbaya Alice siku hiyo hakutembea na kitambulisho.Mlizi akaweka ngumu kuwa hawezi kuingia bila kitambulisho.
Alice akabidi amuulize Gaston kuwa wafanyaje? Gaston akajibu hakuna jinsi ingine usiku huyo waende tu gheto kwake yeye atalala hata kwa jirani. Mmmmh haugopi? aliuliza Alice.Niogpe nini sasa kwani wewe ni si ni shemeji yangu aliibu Gaton.Shemeji yako kwa nani sasa wakati rafiki yangu Jesca ushamzingua aliseme Alice huku akipanda gari. “Yaani huwezi amini kilichotokea sio hata usaliti bali tu rafiki yako sio muelewa ila nitakueleza kila kitu hope utaelewa alijaribu kujitetea Gaston.
Walifika gheto kwa Dulah wakaingia ndani na Gaston alitoka ili aweze kwenda kumgongea rafiki yake ili aone kama wanaweza kulala wote usiku huo.Jirani yake huyo ambaye pia ni mwanachuo alifungua na kuuliza kulioni usiku huo. “Daaah kuna majanga yametokea vipi naweza kulala hapo kwako nina mgeni alafu wa kike nataka nimpishe”. Jamaa akacheka kidogo na kusema sasa kama ni wa kike si alale naye tu au ni nani yake?.Gaston akajibu kuwa alikuwa ni shemji yake.
Jirani yake huyo akaendelea kucheka na kumwambia leo nina kicheche au mchepuko kwa jina rahisi hivyo haitowezekana kukupa hifadhi. “Wewe lala naye tu jiarani tena ikiwezekana kula mzigo kabisa shemeji kitu gani kwani alifikaje machinjioni usiku huu” alishauri jirani huyo wa Gaston amabaye pia alisifika kwa sifa mbaya wa kuwa na mademu wengi.Yaani alikuwa akibadilisha mademu kama nguo.
Wakati Gaston anatoka na kuenda kuomba sehemu ya kulala, Alice alijisogeza mlangoni na alikuwa akifuatilia maongezi yao.Alirudi kwa kunyata na kukaa kwenye sofa mara baada ya kuona Gaston anarudi. “Sasa shemu leo tutashea umasiki wewe utalala kitandani , mimi nitalala kwenye sofa ila usiwe na wasiwasi kuwa huru alisema Gaston mara baada ya kuingia ndani.Alice alitabasamu akasema usiwe na hofu mimi nitalala kwenye sofa na wewe ulale kitandani.. “Hapana shemu naomba ulale kitandani najua leo umechoka sana kimwili na kiakili”. Basi tutalala wote ila mzungu wa nne alipendekeza Alice. Vipi nikuekee maji ya moto au utaoga ya baridi Gaston alimuuliza Alice mara baada ya kuhisi kuwa atakuwa na uchovu.
Naomba nipashie tu shemu wangu alijibu Alice. Gaston akaweka maji kwenye jiko la gasi huku akimlalamikia mzee mwenye nyumba kuwa amempa taarifa kuwa heater ya bafuni kwake imeharibika na hajatuma fundi mpaka wakati huo.Gaston baada ya kubandika maji alifungulia radio yake na kwa kuwa ilikuwa ni usiku sana aliweka ile miziki laini ya kuchombeza na kubembeleza. Maji yalichemka kisha Alice aliingia bafuni na kuoga. Wakati Alice ameingia bafuni kuoga Gaston alianza kuwaza ujinga. “Hivi patakucha kweli au ndio kama siku ile mambo ya Mwajabu. Alafu mimi ninakuwaga na bahati ya mtende yaaini mipira ya kona nishindwe tu kumalizia alijisemea Gaston huku akoiongeza maji jikoni ili na yeye akaoge pindi tu Alice atakapotoka bafuni.*
Haikuchuka mda mtoto mzuri Alice alitoka bafuni na kumpa nafasi Gaston aingie kuoga.Gastona naye aliingia kuoga na kumpa nafasi ya Alice na yeye kumuwaza kidogo “Huyu mwanaume ni mkarimu sana na siku zote amekuwa akinipigania kwenye shida zangu lakini sasa kwa nini amemfanya vile rafiki yangu Jesca na kuamua kumsaliti kisa girlfriend wake wa kwanza.Ila jamani yule Beatrice naye ni mrembo mwanaume yeyeote ni ngumu sana kuruka mtego wa ulimbo wake alijiuliza na kujijibu mwenyewe”.
Lakini Gastona alinambia ana utetezi ebu ngoja akitoka bafuni nisikilize utetezi wake. Gaston alirudui kutoka bafuni na akashangaa kumkuta Alice yupo kwenye sofa na amewasha Tv na kuweka moviee amabyo walishawahi kuiangali kipidi kile walipokuja na rafiki yake Stela. Ngoja nikuwekee season two hii si ulishaiangalia alisema Gaston mara baada ya kuona Alice anarudia kitu ambacho alishawahi kukiangalia. “Nitafurahi pia shemu wangu” alisema Alice huku akinyanyuka na kwenda kwenye friji kaungalia kama angeweza kupata kitu cha kunywa. Alifanikiwa kupata kinywaji ambacho kilikuwa na kilevi na hakuuliza kuwa kilikuwa ni kinywaji gani yeye alichukau glass na kujimiminia.
Lengo lake kubwa lilikuwa ni kupunguza stress. Gaston naye akamimina kinywaji na kuendelea kumpa kampani shemeji wake huyo ambaye alionekana kabisa kuwa alikuwa hana mpangao wa kulala. Kwa kuwa Alice alikuwa amejilaza kwenye sofa na Gaston naye aliamua kujilaza kwenyekitanda wakawa wanapiga stori za hapa na pale. “Haya niambie siku ile ilikuwaje tena mpaka ukaamua kumsaliti rafiki yangu Jesca?” aliuliza Alice. Tena nafuu umeniuliza alidakia Gaston kwa kujiamini. Ujue rafiki yako alipaniki tu bilakujua nini kilikuwa kinaendeea baina yangu mimi na yule binti.
Yule binti kweli alikuwa ni ex girlfrend wangu.Lakini tulishaachana ila kipidi tunaachana na yule binti kuna kitu kilikuwa kinanitatiza maana alikuwa ni majamzito na alisisiza kuwa ile mimba ilikuwa ni yangu jambo ambalo mimi sikuliamini. Baadaye tulipoteza mawasilano na kila mtu akaendeleana maisha yake lakini baadaye nilikuja kusikia alijifungua kabla ya kwenda chuoni. Kila mtu alaiyefanikiwa kumuona mtoto huyo alisema lazima mimi nitakuwa ni baba wa mtoo huyo kwa jinsi nilivyofafnana naye. Kwa hiyo Beatrice hakunitafuta ili turudainae la hasha bali tukapineDNA kwa sababu hata yeye hakuwa nauhakika kuwa yule mtoto alikuwa niwa nani kwa sababu alizini na wanaume wawili ndani ya wiki moja alijaribu kudanganya Gston uwongo uliofanana na ukweli. Alice ilibidi acheke kidogo na kusema kweli huyo ni kiboko kama hajui hata mimba ni ya nani basi ni shida shidani.
Ukweli ndo huo ambao Jesca hakunipa nafasi ya kuueleza ila ni kweli nilienda Arusha ila si kwa ajili ya kumsaliti ila ni kwa ajli ya kuthibitisha kama kweli ile ni damu yangu. Kwa hiyo matokeo yalikuwaje aliuliza Alice kwa shaukuu. Shemu naye una haraka majibu yakitoka nitakwambia alijibu Gaston. “Kwa hiyo baada ya kupima ndo mkaamua kwenda hotelini kukumbushia enzi zenu?”aliuliza Alice huku akicheka. Wala hata pale nilimsindikiza tu na mimi nilienda kulala sehemu ingine na asubuhi tukakutana stend na yeye alikuwa anakuja Moshi alizidi kujitetea Gaston kwa uwongo uliofanana na ukweli. “Sasa mbona pale stendi Moshi alikuita babee na pia alikuaga kwa kukukumbatia jambo lilomuumiza sana Jesca?. Alihoji Alice.
“Aaaaaah hiyo kawaida sana kwa Beatrice kwani ana mambo ya kizuungu.Kwani kuitwa babeee ni kosa jamani si ana kumbushia enzo tu, alafu pale alikuwa anamrusha roho Jesca maana nlishamuonesha picha zake na kumuambia huyo ndo my everything” alijibu Gaston. “Sasa shemu lakini kwa nini ulikuwa hupokei simu kama hayo unayoyasema yana ukweli?” aliendelea kuulza maswali Alice kuonesha badoo alkuwa na mashaka.“Yaani siku ile nilikuwa nimevurugwa sana hasa mara baada ya Jesca kunitumia meseji na kunieeza kuwa ameniona Arusha.Nikaamua kutokupokea simu ya mtu wowote na kwa kuwa nilikuwa sijafanya makosa niliamini siku nikitoa utetezi wangu Jesca anatanielewa” alisema Gaston.
“Ujue tukio langu halitofautiani sana na la kwako siku ile tulioenda club mara baaada ya rafiki yenu kushinda taji la miss University aliendelea kujitetea Gaston. Ila kweli kinachotuponza watu tuliopendana ni wivu ulipitiliza”. “Yaani mtu unaweza hata kujinyonga kwa sababu ya mapenzi kumbe hata sio ishu kubwa kihivyo” alisapoti Alice. Lakini majanga yenu sio makubwa sana mnaweza kuyamaliza na kurudiana alisema Alice tofauti na ya kwetu. “Yaani mimi na Dulaha siwezi kurudiana naye kwa namna yeyoeta ile kutokana na ukatili alionitendea. Yaani kweli amediriki kuniita mwizi na kuwaonga hela mapolisi nilale ndani. Unafikiri kama sio wewew kuja na wakili maarufu mimi si ningelala ndani leo?” aliendelea kuhoji Alice
Wakati wakipiga stori Alice alikuwa pia akichati na rafiki yake Sstella na kumueleza kuwa Gaston amekuja kumtoa na kwa sasa yupo kwake anaangalia muendelezo wa ile moviee ya siku ile. Stela akamwambia huyo ndo mwanaume na kama vipi ajiweke tu maana rafiki yake Jesca ndo kashajitoa tu. “Yaani hapo usijivunge best wewe mpagawishe usiku wa leo na hiyo ndo zawadi ya ukarimu wake kwako alisistiza Stela kwenye maeseji.Mesji hizo za Stella zilimfanya Alice acheke kwa nguvu jambo lilimfanya Gaston kumuuliza alikuwa akicheka nini? “Si ni hawa marafiki zangu nimewaambia umekuja kunitoa kituoni na nipo kwao hawaamini. Eti mwingine ananambia nimpindue Jesca alisema Alice na kumshirikisha burudani Gaston aliyokuwa akiipata kwenye mesji. Ingawa walichukulia kama utani lakini wa namna moja au nyingine maneno hayo yalimwingia sana Alice na kutamani kama ingekuwa kweli.
Alice aliendeleakuangalia movie lakini Gaston alipandisha miguuu yake vzuri kitandani kuashiria kuwa usingizi ulikuwa umemzidia. Akiwa kwenye hali hiyo alijkaza na kushusha neti.Alice yeye akaamua kukomaa pale pale kwenye sofa huku akiomba kurushiwa shuka ili ajifunike miguu ambayo ilikuwa imeanza kusumbuliwa na mbu. Dakika 5 baadaye Gaston alianza kukoroma kuashria kuwa usingizi ulimkolea napia alikuwa amechoka sana.Baadaye Alice naye alipitiwa na usingizi pale pale kwenye sofa. Baadaye simu ya Gaston iliita mlio wa alamu ambayo ulikuwa umetegwa.
Ilikuwa ni kawaida kwa Gaston kila ifikapo saa 9 usiku anaamka na kusoma au kama sio kusoma basi atatumia hata dakika kumi kutafakari maisha yake. Na hiyo ni kutokana na ushauri aliopewa na marehamu baba yake kuwa siku zote akilala asilale kama mwanamke, bali yeye alalapo ahakikishe kuwa usiku wa manane anashtuka na kutafakari mustakabali wa maisha yake.Kwa mujibu wa baba yake ni kwamba kama mtu ataweza kuamka usiku kuna uwezekano mkubwa wa yeye kupata majibu ya maswali magumu ya kimaisha kama ni kwa jinsi gani anawea kuwa tajiri au kupata njia itakayomuwezesha kufanikiwakwa jambo lolote analotaka kulifanya.
Alamu hiyo haikumshitua tu Gaston bali hata Alice ambaye mbu wapenda damu walishamtafuna kwa mda mrefu. Gaston aliizima ile simu kabisa kisha akaamka na kwenda chooni. Alipotoka alizima Tv akamnyanyua Alice na kumpeleka kitandani.Kisha akamfunika shuka vizuri.Alice alijkausha kama vile alikuwa kwenye usingizi mzito na nia yake alitaka kujua Gaston anataka kufanya nini.Gaston alizima taa kisha akapanda kitandani.Kila mtu alikuwa akihema kwa nguvu hasijue nini kingetokea mda mfupi baadaye. Kwa upande wa Gaston usingizi ulikata kabisa akiwaza itawezekanaje kulaal na binti marembo kama Alice mpaka asubuh bila kusababisha madhara. Lakini ngoja leo nioneshe ujasiri kama ni bahati yangu basi nitamla siku nyingine aliwaza Gaston.
Yaani hapa akinichokoza tu nampa potelea mbali alijsemea Alice ambaye na yeye usingizi ulimkata.
Gaston alijitahidi kuondoa mawazo ya ngono jambo lilomfanya apate usingizi na hii ni kutokana na usingizi wa uchovu aliokuwa nao siku hiyo. Kwa upande wa Alice na yeye alipata usingizi na hii ni kutokana na uchovu aliokuwa nao kutokana na mikimkiki aliyokutana nayo mchana wa siku hiyo. Alihisi raha ya usingizi maana mwanzo hakufaidi usingizi kutokana na tabu ya mbu wasumbufu waliokuwa wakimsumbua pale kwenye sofa.Alipitiwa na usingizi akaota ndoto nzuri ya mapenzi, mapenzi ambayo alikuwa akipewa na shemeji yake huyo. Ndoto ilikuwa tamu mpaka akawa anatoa sauti za miguno ya kimahaba ambazo zilimfanya Gaston ashituke kutoka usingizi.Iiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiisssssssssssssssssss,, mmmmmmmmmmmmmmmmmmmh,, sheeeeeeeeeeem sheeeeeeeeeeeeem waaaaanguu aaaaaasanteeeeeeeee,, asanteeeeeeeee Gaston.
Gastonn alishangaa sana na kwa mara ya kwanza maishani mwake alishuhudia mtu akiweweseka kwa mahaba ya ndotoni. Alishindwa kueleawa nini kinaendeea na alitamani ampe dawa. Aliamka na kwenda haja ndogo huku akimwacha Alice akijibiringita biringita hapo kitandani huku miguu ikicheza cheza kama mwanamke aliyekuwa akipewa huduma ya mautamu. Gaston mtarimbo wake ulisimama na akaona njia sahihi ni kukimbilia kwanza chooni. Tayari palikuwa pamekucha na kwa kuwa waliambiwa warudi polisi saa mbili asubuhi Gaston aliamua kufungua maji na kuoga. Ndoto ya Alice iliendeleea huku akitoa maneno ya shukuranai, asaaaanteeee, aaasanteeeeeeeeeeee my shemu kweli wayajua mapenzi.
Baaada ya maneno hayo Alice naye alishituka kutoka usingizni na kujikuta yupo peke yake kitandani. Hakutaka kuamini kama kweli ile ni ndoto, akaamua kupitisha mikono yake sehemu zake za siri na kujikagua.Akakuta kuna unyevunyevu wa ute ute ishara kuwa huenda kuna mvua ya manyunyu ilinyesha mda mfupi uliopita. Akajipapasa papasa pia matiti yake akayakuta yamesimama vizuri utafikiri ametoka kufanya mapenzi. “Mmmmmh usikute Gaston ameshafanya yake ndo maana amekimbilia bafuni aliendelea kuwaza Alice huku akivuta taswaira ya raha alizozipata kutokana na ndoto hiyo. “Daaah ndoto zingine bhana yaaani full mautamu alisema Alice na kuvuta shuka na kujifunika vizuri”.
Alice alijitumainisha kuwa ni ndoto kwa sababu alikuw ana nguo alizovaa tena zennye ulinzi mkali kuanzia getini mpaka ndani. Aliendelea kukumbatia mto kwa nguvu akitamani usiku uanze upya ili yeye aendelee kulala. Gaston alitoka bafuni akampashia maji huku yeye akiendelea kujiandaa kwa kunyoosha nguo ambazo alitarajia kuzivaa siku hiyo. Maji yalichemka na Gaston alimwamsha Alice ili aaende kuoga. Alice naye kwa kutambua saa mbili waliyoambiwa aliamka na kwenda kuoga. Alioga fasta fasta akatoka akaajiandaa na kurudia kuvaa nguo zake zile zile kitu ambaccho ni nadra sana kwa Alice kurudia nguo. “Itabidi tupitie chuoni ili nikabadilishe hizi nguo” alisema Alice alipokuwa akivaa suruali yake. Waliondoka na kupitia chuo ambapo Alice aliingia hostel na kubadilisha nguo huku Gaston akimsubiri hapo nje. “Mbona hatokei tena yaani wanawake bhana siku zote hawajui kuzingatia mda ona sasa saa mbili inatukutia hapa aliendelea kulalamika Gaston.Alice ikabidi awasubiri na marafiki zake wajiandae ili waondoke wote.
Alice ikabidi ampigie simu tu Gaston na kumwambia aingie tu ndani.Gastona aliingia lakini tayari alishapandwa na hasira. “Kwa hiyo mnajipara kwani mnaenda kwenye harusi” alipiga madongo Gaston mara baada ya kuona Easther yupo kwenye dresing table akijiremba.“Eeeeeeh babu weweeee sisi ni watoto wa kike hati, na mwanamke urembo babuuu” alijibu Easther kwa shombo shombo ya maneno.Mara Stela akaingia ndo kwanza alikuwa ametoka bafuni huku akitetemeka kutokana na ubaridii wa maji aliyoga. “Yaani maji ni ya baridi haraka haraka hizi zinatuletea” majanga alisema Stela ambaye alikuwa ndani ya khanga moja huku mkononi akiwa ameshika kufuli lake ishara kuwa alilifua mara baada ya kuoga.
Bila aibu akitundika nguo hiyo ya ndani kwa juu sehemu maalumu iliyoandaliwa kwa ajlii hiyo.Shemu tuvumiliane mimi nabadilisha nguo hapa hapa alisema Stela huku akivaa nguo alizokuwa ameziandaaa . “Mmmmmh sia haba anakijungu” alijsemea Gaston mara baada ya kubahatika kuona baadhi ya maungo ya binti huyo. Ndo maisha ya chuo kama ni mgeni unaweza kushangaa na kufikiri labda hawanazo. Baadaye waliondoka huku wakiwa nyuma ya mda.Wakiwa njiani Gaston alipokea simu kutoka kwa yule wakili ambaye walikuwa naye jana. “Vipi mbona hamjafika mpaka sa hivi aliuliza wakili huyo”. “Tusameehe tu kiongozi tupo njiani tunakuja siunajua tena mambo ya watoto wa kike” alijittetea Gaston. Vipi ni yule wakili aliuliza Alice mara baada ya simu kukatika. “Yap” alijibu Gaston kwa kifupi.***
Kwa upande wa Dulah na marafiki zake wao waliondoka pale kituoni mapema mara baada ya kuhakikisha kuwa Alice atatala polisi mpaka asubuhi.Kuondoka kwao haikumaanisha kuwa walienda kulala la hasha walienda mahali na kutafuta msaada wa kisheria wa jambo hilo ili kesho wanapokuja wajue kama wafute kesi au waipeleke mahakamani. Dulah alifanikiwa kwenda kwa mwanasheria mmoja ambaye pia ni Lecture na wakili wa kujitegemea anayefundisha kwenye moja ya vyuo vilivyopo Moshi. Mwanasheria huyo ambaye ni rafiki mkubwa wa baba yake mdogo na Dulah aliwashuri wafute tu kesi hiyo na kuomba binti huyo arudishe vitu vilivyochukuliwa. Aliwashauri hivyo kutona na ukweli kwamba sheria siku hizi inawalinda sana watoto wa kike na kwa kuwa walishakaa wote zaidi ya mwaka mmoja hivyo basi uwezekano kuwa mahakama ingeamuru vitu hivyo vigawane sawa kwa sawa ulikuwa ni mkubwa.
Kwa hiyo na wenyewe walikwenda kulala wakiwa na wazo moja tu kuwa pakikucha watakwenda kufuta kesi. Na hili mambo yawe rahisi Dulah alikubalii kurudisha ile simu ya Deo ambayo ndo ilikuwa chanzo cha ugomvi. Asubuhui palikucha na wao waliwahi kituo cha polisi saa mbili kama walivyoambiwa.Walishangaa sana mara baabda ya kugundua kuwa Alice hakulala kituoni. Wale maaskari ambao aliwaonga walijitetea kwa kusema kuwa mkuu wa kituo alipita usiku na kuongea na watu wote waliokuwepo ndani. Hivyoo akaamuru wote ambao kesi zao ni nyepesi sana waachiwe huru kwa dhamana. Waliendelea kuwa subiri kina Alice mpaka saa mbili na nusu ndo waliingia na kama kawaida yao walikuwa kikundi.
Hata kama alikuja kutoka usiku sana lakini adabuu nimshamshikisha alisema Dulaha mara baada ya kumuona Alice akiwa mbele kama kiongozi wa msafara vile.Yaani haoni hata aibu kuvaa nguo nilizonunulia mimi alizidi kuwaza Dulah. Alikwenda kuripoti na wote waliitwa na Alice alikwenda na yule wakili aliyetafutiwa na Gaston. Dulah kumuona yule wakili alicheka kwa sababu alikuwa akimfahamu na alikuwa pia akihusika na kusaidia kampuni yao kisheria.Mashauriano yaliendelea huku kila upande ukieleza matakwa yake. Alice alikuwa akitaka arudishiwe simu na pia apewe baadahi ya vitu kwa sababu alishiriki kupatikana kwake kwa namna moja ua nyingne.
Lakini kwa upande wa Dulah ailikuwa ni tofauti na yeye alikuwa akitaka kurudisha simu kisha wasahameane na kurudiana.Dulha alisisitiza kuwa bado anampenda binti huyo na yupo tayari kuendelea kuishi naye. Ingawa Dulah alitoa msimamo huo lakini si kwa sababu eti alikuwa bado akimpenda kiukweli bali ni kwa sababu alihofiia kugawana hivyo vitu ambavyo vilikuwa na thamani kubwa sana.Baada ya Alice kukomaa na msimamo wake kuwa hayupo tayari kurudiana na Dulha , Ilimbidi Dulah kutoa msimamo mwingine kuwa atamrudishia Alice hela aliyochangia kwenye kodi na kwa kuwa Alice alitoa laki moja yeye atampa laki mbili wamalizane.
Alisema hivyo akijua kuwa vitu vyote vya ndani pamoja na jiko la gesi alinunua Alice hivyo hatakuwa amepotza sana. Alice kwa kuwa alikuwa amechoshwa na majadilanao hayo ambayo yalichuku mda merfu.Hakuona haja ya kuendeea kupoteza mda kwa kuendelea kubishana kuhusu vitu vidogo kama jiko na vyombo maana hata akiviichukua hakuwana na pa kuvipleka. Akakubali kupata hasara maana anakumbuka hela alizotoa ili kukipamba na kukifanya chumba hicho kiwe na muonekano mzuri ulifikai laki nne. Utaratibu wa kurudisha vitu ulikamilika huku ukisimamiwa na askari polisi. Kila mtu alipata haki yake n huo ndo ukawa mwisho wa safari yao ya mapenzi amabyo ilianza miaka 4 iliyopita
Alice baada ya kupata ile simu alimrudishia Deo mwanaume ambaye kwa namna moja au nyngine alishiriki kuvuruga penzi lake na Dulah.Deo alitaka kuikataa hiyo simu ili eti uhusaiano wao uendelee kwa sababu alishakuwa na uhakika kuwa Alice hawezi kurudiana na Dula tena kwa namna yoyote na hiyo ni kutokana na matukio yaliyotokea. Alice moyo wake ulishaingia kinyongo na alimchuki Deo na alimuona kama limbukeni wa mapenzi.Alimpa simu yake na kumwambia ukweli kuwa hampendi na hawezi kuwa naye kwa namna yoyote ile. Huo nao ukawa mwisho wa Deo na Alice. Alice alichafukwa na alikuwa akitumia ile falsafa ya naomna bora niwe peke yangu.***
Maisha ya upweke yalianza pande zote mbli yaani kwa Alice na kwa Dulah, kwa Jesca na kwa Gaston.Alice alipanga kuendelea kuishi single mpaka hapo atakapo pata mwanaume ampendaye.Mda mwingi alipokuwa hana vipindi alikuwa akienda kwa Gaston mtu ambaye kwa sasa alikuwa zaidi ya shemeji yake. Wakati mwingine walikuwa wakiangalia moviee mpaka usku wa manane na pia wakati mwingine walikuwa wakisoma wote mpaka usiku wa manane. Alice alimsihi sana rafiki yake Jesca amsamehe Gastoni na waendeleee na mapenzi yao lakini binti huyo alikataa katu katu na kudai kuwa hayo ndo matunda ya usaliti. Gaston naye alijitahidi kwa kila njia kurudiana na Jesca lakini ilishindikana akajikuta akijutia sana kumkubalia Beatrice siku ile kwa sababu kwa sasa hamfai kwa lolote kwa sababu yupo mbali na yeye na wala hawawezi kuonana kwa urahisi mpka miezi 6 ipite.
Maisha ya Alice yakaanza kubadilika siku hadi siku akawa ni mtu wa kutafuta faraja sehemu mbali mbali za starehe. Kila wikiendi yeye na kampani yake walikuwa wakienda club kujirusha na kufurahia anasa za dunia hii. Wakawa wanakunywa pombe kupita kiasi na siku ambayo walikuwa hawana pesa walianza kunywa pombe mtaani tena pombe kali zile za bei rahisi. Walikuwa wakienda kule kwenye bwaloo la polisi kwenye chuo cha Polisi cha CCP ambacho kilikuwa mkabada na chuo chao. Kama mnavyojua kwenye kambi za polisi na jeshi pombe na vinywaji vingine huwa ni bei rahisi. Siku ingine kwa sababu ya kampani na kumkubali Gston walikuwa wapo tayari kumlipia hata kiingilio ilimradi tu waende wote club. Katika harakati hizo za kutafuta faraja Alice na Gaston walijikuta wakizama kwenye penzi zito penzi la shemeji. Waliamua kujipa raha wenyewe kwa sababu walikuwa wakipendana na kulikuwa hakuna kuzuizi chochote ambacho kiliwazuia kutofanya hivyo.Siku ya ufunguzi wa ukurasa wao wa mapenzi walienda club na baada ya kupombeka vya kutosha Alice alianza makeke yake.Wakiwa club na hata mda ulikuwa bado haujaenda sana Alice alianza kusema “Shemejii twende tukalale na jisikia vibaya”.Gaston akawaambia wenzake kwa Alice amezidiwa hivyo waondoke. Wenzake walikataa kwa sababu ndo kwanza walikuwa wameingia club. “Mzigo wako huo alisema Easther mara baada ya kushiriishwa swala hilo”.
Gaston hakuawa na jinsi zaidi ya kumbeba Alice na kumtoa nje ambapo walikchukua tax na kuondoka zao.Na sio kwamba Alice alikuwa amelewa na kuzidiwa kiasi hicho la hasha bali ilikuwa ni mbinu ya kwenda kulala na Gaston kwa sababu mbinu zote za kike ambazo alishawahi kuzitumia zilikuwa zikigonga mwamba.Akaona isiwe tabu kwa sababu siku hiyo ndo alikuwa amemaliza period na alikuwa na kiraru kilichopitiliza.Hamu kubwa ya kufanya mapenzi aliyokuwa nayo binti huyo ilimfanya atumie mbinu hiyo ya kujifanya amelewa. Walifika geti la chuo na Alice alikataaa kushuka kwa madai kuwa anaogopa kulala mwenyewe.
Baada ya Gaston kumshauri ashuke Alice alikataa na kumuuliza kwani aliogopa nini mbona walishalala wote mara kibao na hakuna lolote lililotokea au siku hiyo alikuwa na mwanamke. “Hamna wewe ni shemeji yangu unajua kwa hiyo mimi nikilala na wewe unanipa wakati mgumu” alisema Gaston.Na pia eti watu wanamfikiria vibaya kwa sababu wanamuona yeye ni mshika dau kumbe ni mshika oembe.Alice akacheka sana na kumwambia dereva “ebu washa gari tuende mpaka madukani leo nataka nikamuoneshe huyu mwanaume kuwa yeye si mshika pembe bali ni mshika dau”. “Alafu Gaston sijui upoje kusoma hujui hata kuangaia picha na yenyewe hujui”aliendelea kupiga madongo binti huyo huku akijifanya kuwa maelewa sana.Gaston aliukuwa ameshaelewa ni nini mtoto huyo wa kike alikuwa anataka.
Kabla hajamjibu kitu Alice alimsogelea karibu na kuanza kumpapasa papasa huku akimsogezea midomo yake kumaanisha kuwa alikuwa akitaka frech kiss. “Taratibu shemu utasababisha ajali alisema Gaston mara baada ya kuona binti huyo alikuwa na papara ya malavidavi. “Alafu nilishakwambia sitaki uniite shemu, ushemej wetu si ulishaisha mara baada ya wewe kuachana na Jesca” alismea Alice bila aibu. Gastoni ikabidi acheke tu na kumwambia dereva akunje kulia sehemu ambayo nyumba aliyokuwa akiishi ilikuwepo. Walishuka na kumlipa dereva ambaye aliomba kuongezewa pesa kwa madai kuwa walikubaliana wataishia chuoni lakini wamepitiliza. Gaston hakuwa mbishi alimuongezea hela na kuachana naye .Wakati huo huo Alice alikuwa pembeni yake huku mkono yake akiwa ameizungusha kiunoni mwa Gaston.
Walitembea kwa stahili hiyo ya kukumbatiana mpaka wakaingia ndani na Alice hakutaka hata mlango ufungwe, alimsukuma Gaston kitandani na kuanza kufungua vifungo vya shati ambavyo alikuwa amevaa siku hiyo. “Funga mlango basi mbona una haraka hivyo alisema Gaston. “Alice alinyanyuka kama mtu aliyechanganyikiwa akafunga mlango kisha akarudi kwa haraka pale kitandani.Hakutaka kumpa upenyo Gaston aondoke pale kitandani. Alimpandia kwa juu na moja kwa moja tayari aliashaupeleka ulimi wake kwenye kinywa cha Gaston. Mtoto wa kike huyo alikuwa na papara kwani tayari mikono yake wakati huo ilikuwa inafungua zipu za Gaston na kutaka kumtoa nyoka pangoni.
Gaston alishindwa kuelewa mizuka hiyo Alice aliipata wapi. Bila kutegemea Alice alipeleka kinywa chake sehemu hizo za mapajani na kuanza kujinyonyea lol pop. Alice alikuwa kama vile anapiga mswaki.Alice alianzia kufurahia raha za dunia ukilinganisha na akili za pombe alizokuwa nazo na yeye alitamani kutoa huduma hiyo ambayo kwa wengine huwa ni kinyaa.Aliamua kumsaidia binti huyo mara baada ya kuona binti huyo akitoa ishara kuwa na yeye anataka huduma hiyo.Gaston naye hakufanya makosa aliamua kuanza makeke yake hata kabla ya kuchojoa nguo za binti huyo. Alianza makeke hayo juu ya kufuli ambalo lilikuwa limelowana kwa utete ute uliokuwa ukimtoka bintii huyo kwenye shemu za ikulu. Alianza kuzisuagua sehemu hizo za juu ya kufuli mara baada tu ya kufungua zipu ya suruali ya kike aliyokuwa amevaa Alice.
Alisugua pampuchi ya Alice kisawaswa kwa kutumia mikono yake huku ulimi ukiendelea kumlamba lamba maeneno ya kitovuni. Huduma hiyo ilimfanya Alice kuanza kutupa tupa miguu huku akigugumia kwa milio ya raha ya huba aliyokuwa akiisikia. Kutupa tupa huko miguu kwa Alice kama kuku anayetaka kuchinjwa kulimrahisishia Gastoni akajikuta amachojoa ile suruali na taili nzuri aliyokuwa amevaa binti huyo. Gaston kwa utaratibu akazishusha nguo hizo mpaka chini na kubakisha kufuli tu.Akamgeuza kama samaki tayari kwa kumkaanga.Alikisogeza kile kikufuli pembeni kidogo na kuanza kupitisha ulimi kwa nyuma sehemu ya makalio. Ilibidi Alice ajibinue zaidi ili kufanya zile sehemu zilizokusudiwa kuonekana kwa urahisi.Kichwa cha Gastoni kilizama kwenye makalio ya Alice akijaribu kutafuta madini ya chumvi chumvi ambayo yanasemekana kuwa ndo huwa yanampa mwanamke raha kama yatanyonywa vizuri na kupunguzwa kutoka kwenye kisima hicho.
Baada ya mda mfupi waliamua kuchojoa kabisa wakabaki kama walivyozaliwa jambo lilohashiria kuwa wapo tayari kwa ajili ya mechi hiyo. Alice alikaa kwenye sofa huku akijisugua sugua sehemu za pampuchi yake mara baada ya kuona Gaston alikuwa akichelewa kumshusha nyege alizompandisha mda mfupi uliopita. Gaston alielewa lugha ya picha aliyokuwa akituia Alice hivyo alimsogelea Alice akapiga magoti kisha kuingiza mtwango kwenye kinu.
Hapo alikutana na joto la huba ambalo alihisi lilikuwa la kipekee zaidi akachomoa haraka haraka baada ya kukumbuka kuwa alikuwa hajavaa kondomu. “ Ooooooops, jamani wewe mbona unanikata stimu mwenzio” aliuliza Alice kwa huzuni. “Usijali ngoja nivaae kinga alisema Gaston huku akivuta droo ya meza yake.Siunajua tena gheto la ukweli haliwezi kukosa dhana za kazi kama hizo. “Wewe nayeee, ebu acha uwoga wako alisema Alice huku akimfuata na kumzuia asivae kinga. “Leo nipo safe day bhana hatuwezi kula pipi na maganda yake siku special kama hii” alisema Alice huku akimsukumia Gaston kitandani.Alice hakutaka kuchewewa bali alianzisha mpira bila hata ya refa kupiga kipenda. Alice alianza kupeleka mashambulizi ya haraka haraka ili aweze kupata golii la mapema.
Spidi yake ilimfanya Gaston ambinue na kumweka chini ili yeye ndo awe dereva maana ilionekana Alice alikuwa ni lena hivyo alishindwa kuendesha gari vizuri.Staili hiyo ikawa imempa nafasi Alice kuendelea kujisugua sugua sehemu za juu za ikulu yake kwa kutumia vidole vyake huku mtwangio wa Gaston ukiwa ndani ya chungu chake ukitwanga na kupepeta. Kuna vitu vilikuwa vikitoka shemu hizo kama uji uji mweupe kwenye koki ya bomba ilozibwa kwa lailoni kisha lile lailoni likatoboka kitundu kidogo. Gastoni ilimbidi achomoe kwa nguvu ili aone ni nini kilikuwa kikitoka.Kumbe mtoto wa watu alikuwa akifunga magoli kila mara baada ya sekeunde kadhaa.
Alice hakukubali kitendo hicho cha Gston kuchomoa wakati yeye ndo alikuwa akimfurahia raha ya mapenzi.Ilibidi autafute huo mtwangio haraka haraka na kuurudisha kwenye kinu chake.Akampa ishara kuwa aongeze spidi kwa kuwa yeye alikuwa akifurahia.Sijui ujuzii huo wa kujipa raha kwa vidole huku mtwangio ukiwa ndani aliupata wapi.Kuongezekaa kwa spidi ya Gason kulimfanya Alice afunge goli tena na kumfanya binti huyo avute pumzi ndefu sana. Gaston alishangaaa sana kwani ilikuwa ndo mra yake ya kwanza kuona mwanamke akifurahia mapenzi kiasi hicho. Yaani ndani ya mda mfupi tu Alice alishapanda na kushuka kileleni mara 3 na hiyo ilimaanisha alishamfunga Gaston mabao matatu bila. Iilibidi Gaston abadilishe staili ya ushambuliaji kwa kuamua kuwapandisha mabeki wakasaidie kufunga mipira ya kona ambayo washambuliaji wake walikuwa wanashindwa kufunga kwa kutumia kichwa.
Alimvuruga vuruga binti huyo mpaka akajikuta amehama kitandani wapo sakafuni huku Alice alikwa ameinama kama vile alikuwa akichuma tembele bustanini. Hapo ikawa ni nafasi ya Gaston kufunga goli la nguvu na kuwafanya wote waanguke chini kutokana na mpira huo wa kona waliokuwa wakigombania. Sio tu Gaston ndo alikuwa amefikia mshindo bali hata Alice alikuwa juu ya kileele tena kwa staili yake ile ya kujipanua mapaja na kuruhusu bao kutoka kwa nguvu na kulowanisha mashuka.
INAENDELEA

