NYUMBA YA MAAJABU
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Sehemu Ya 1
Ilikuwa ni siku ya furaha sana walipohamia kwenye hii nyumba nzuri na ya kupendeza, tena iliyovutia katika macho ya watu wengi sana.
Mke alisikika akimuuliza mume wake,
“Ibra, uliwezaje kuwekeza pesa nyingi za kununua nyumba nzuri kama hii?”
“Mke wangu Sophia, kwakweli mambo ya Mungu ni mengi sana, hata mimi sikutegemea kupata nyumba kama hii kwa ile pesa ambayo nilikuwa nayo. Kwakweli tushukuru tu kwa kupata mwanga wa maisha”
“Nadhani sasa mipango yetu itatimia mpenzi”
“Ndio mke wangu kwa hapa lazima mipango itimie”
“Hivi tulipanga kuzaa watoto wangapi vile?”
“Watatu tu wanatosha mke wangu”
“Baby kwa jinsi nyumba ilivyokubwa kwanini tusifanye wanne!”
“Wewe ndio mzaaji mke wangu kwahiyo vyovyote tu inawezekana”
Sophia akakumbatiana na mume wake kwa furaha kwani hii ilikuwa ni moja ya ndoto zake kwenye maisha.
Baada ya wiki moja, Sophia aliamua kwenda kuwatembelea majirani zake wa sehemu aliyokuwa akiishi mwanzoni. Alifika na kuwakuta wakiendelea na shughuli za hapa na pale kama kawaida, moja kwa moja aliamua kwenda kwa rafiki yake wa pekee Siwema ambapo alikaribishwa vizuri sana na rafiki yake huyo.
“Yani Sophia kama usingekuja kunisalimia kwakweli ningekuona ni mtu wa ajabu sana.”
“Hivi Siwema naachaje kuja kukusalimia wewe! Nitakuwa nimerogwa basi, tena nitakuwa ni binadamu asiye na wema wala shukrani”
“Eeh hebu kwanza niambie shoga yangu mmehamia wapi maana si kwa mbwembwe zile za kuondoka hadi vigoda vyako umeacha”
“Shoga mwenzangu, yani wewe ni shoga yangu wa damu kwakweli na kukuficha siwezi. Kwakweli mwenzio nadhani kuna vitu Ibra alikuwa ananificha”
“Kivipi? Na vitu gani hivyo alivyokuwa anakuficha?”
“Hivi unaweza kuamini kwamba Ibra amenunua nyumba na gari!”
“Mmh kwa hela gani? Katoa wapi hiyo pesa ya kununua nyumba na gari?”
“Tena ninavyokwambia nyumba ni nyumba haswa shoga yangu wala sio nyumba uchwara, nitakupeleka na wewe ukajishangalie maajabu ya mume wangu Ibra”
“Mmmh kwahiyo shoga biashara ya mamantilie hufanyi tena?”
“Naanzaje kufanya biashara ya mama ntilie kwenye nyumba ile! Shoga hujaiona na wala sijisifii tu, kwakweli Ibra ana pesa, mpango wangu kwasasa ni kuzaa tu nicheze na wanangu pale maana nikichelewa nitakuta mwana si wangu”
“Shoga tusiandikie mate wakati wino upo, ujue umenitamanisha sana, naomba twende sasa hivi na mimi nikajishuhudie huo mjengo. Ngoja nijiandae fasta twende.”
Sophia akakubaliana na Siwema pale kwahiyo akamsubiri ajiandae ili aweze kwenda nae.
Siwema na Sophia walifika kwenye nyumba husika ambapo nje tu ya nyumba hiyo Siwema alibaki kushangaa na kuduwaa kwani hakutegemea kama ile nyumba ipo vile kama alivyoikuta.
“Khee jamani Sophia mbona umeokota dodo kwenye muharobaini shoga yangu, hebu jibebeshe mimba mapemaa maana hapa utashangaa ushaibiwa shoga yangu”
“Yani hapa ninachotaka ni kuzaa tu, yani toka nimeuona huu mjengo na dawa za uzazi wa mpango nikaziacha pale pale saivi nawaza watoto wa kucheza nae kwenye nyumba hii”
“Hongera sana shoga yangu ila kuwa makini na Ibra maana asije akakuletea mke mwenza bure”
“Thubutuu huyo mke mwenza atapitia mlango gani!! Labda sio Sophia niliyepo humu ndani”
“Nakuaminia Sophia, kama uliweza kumchunga Ibra kule uswahilini ndio ushindwe kumchunga kwenye huu mjengo”
“Hapo sasa, yani hapa Ibra hazungushi amefika hapa Kigoma mwisho wa reli”
Sophia alikuwa akifurahi tu na shoga yake huyu, na leo walipika pamoja na kula pamoja hadi joini ambapo mume wa Sophia aliwasili kutoka kwenye mihangaiko yake ambapo alimkuta Siwema pale kasha Siwema akawapa hongera zao na kuwaaga.
“Hongera sana shemeji yangu Ibra, ila mimi ndio naomdoka shemeji”
“Mmh shemeji jamani ndio haraka haraka hivyo!”
“Shemeji nilikuwepo hapa tangu muda ila nitakuja tena maana ndio nishapapenda tayari ila saizi wacha niende”
Basi Ibra hakuwa na jinsi yoyote zaidi ya kumuaga tu huyu Siwema.
Kisha Sophia akatoka na kwenda kumsindikiza rafiki yake huyu,
“Kwakweli Sophia usizembee, pale ndio umshikirie vizuri Ibra yani umgande kama ruba maana ule mjengo si mchezo shoga yangu. Yani wambea wa mtaa watanikoma nitakavyokuwa najidai kuhusu wewe Sophy.”
Sophia akacheka tu kwani alikuwa akifurahia kile alichokuwa akiambiwa na Siwema.
“Usicheke tu Sophy ila yafanyie kazi maneno yangu”
“Ondoa shaka dada, mambo yataiva tu maana hata mimi nimetamani kuwa na watoto kwasasa”
Wakabadilishana mawazo pale kasha Siwema akapanda daladala na kuagana vyema huku Sophia akisisitiza kuwa awasalimie majirani zao wengine.
Sophy alirudi nyumbani kwake, kwavile giza nalo lilianza kuingia ikabidi aandae chakula cha usiku, na kilipokuwa tayari alikaa na mumewe na kuanza kula huku wakitabasamu.
“Mmmh Sophy muda wote unatabasamu tu mke wangu”
“Hivi naachaje kutabasamu Ibra!! Bahati tuliyoipata ni kubwa sana mume wangu kwakweli sikutegemea kama ipo siku tutaishi kwenye nyumba nzuri na kubwa kama hii, si unajua tulizoea chumba kimoja tu yani jiko hapo hapo, viti, vyombo, kitanda hapo hapo yani shaghalabhagala lakini sasa hivi eti tunaishi maisha ya kitajiri namna hii lazima nitabasamu mume wangu.”
Wakamaliza kula kasha Sophy akatoa vile vyombo na kuvipeleka jikoni huku akitaka kuviosha kwanza ndimbo aende kulala na mumewe, ila Ibra alimfata kule jikoni na kumwambia,
“Sophy mke wangu, vyombo utaviosha kesho bhana hebu twende tukalale”
Sophy akatabasamu kisha akaacha vile vyombo na kuongozana na mumewe hadi chumbani ambako muda mwingi walionekana wakitabasamu.
Kisha wakaenda kuoga pamoja na kurudi kitandani, Ibra alimkumbatia Sophy na kumuuliza tena,
“Hivi ulisema tuzae watoto wangapi vile?”
“Wanne mume wangu au wewe hupendi”
“Mmmh hakuna kitu ambacho unakipenda wewe halafu mimi nisikipende, si unajua jinsi nikupendavyo Sophy! Yani mimi na wewe letu ni moja mke wangu”
“Tena napenda wawili wawe wa kike halafu wawili wa kiume”
“Wow ni mpango mzuri sana hakuna tatizo, tutazaa kadri Mungu atakavyo tujaalia Sophy wangu.”
Wakatabasamu kisha wakalala kama kawaida.
Kulipokucha, kama ilivyoada Ibra aliamka mapema sana kisha akajiandaa kwaajili ya kwenda kwenye kazi zake, Sophy alitaka kujaribu kuinuka ili kumuandalia mambo mbalimbali mumewe ila ibra alimzuia na kumtaka mkewe aendelee kupumzika tu ambapo naye alifanya hivyo kwani alielewa ni jinsi gani Ibra alimpenda.
Kwenye mida ya saa mbili asubuhi, Sophy nae aliamka na kwenda kuoga ili kujiandaa kwa mambo ya hapa na pale.
Akaenda jikoni kwa lengo la kutaka kuosha vyombo vya jana na kujiandalia chakula cha asubuhi, ila alishangaa kuona vyombo vilishaoshwa na vilipangwa vizuri kabatini.
Hali hii ikamfanya Sophia ajiulize kuwa huenda Ibra alimzuia kuamka muda ule ili afanye kile kitu cha kumsahangaza. Kwakweli Sophia alitabasamu kwa jambo hili kwani aliweza kuona ni jinsi gani Ibra anampenda sana.
“Najua Ibra ananipenda sana ila safari hii kazidisha mapenzi jamani mmh yani amefikia hatua hata ya kunitaka mimi nilale halafu yeye akaosha vyombo, haya ni mahaba tena motomoto kwakweli nina kila sababu ya kumzalia watoto Ibra wangu. Kipindi kile nilikuwa najibana kuzaa sababu ya maisha duni ila kwasasa nina kila sababu ya kuzaa kwakweli.”
Kisha akajiandalia chakula pale na kuanza kukila halafu naye akatoka kwa lengo la kwenda kwenye mihangaiko yake mbalimbali.
Wakati yupo nje ya nyumba hiyo kuna mmama alipita na kumsalimia Sophia kisha Yule mama akamuuliza Sophia kama ndiye anayeishi mule ndani,
“Unaishi humo ndani dada?”
“Ndio mama”
Sophia akahisi kuwa huyu mama labda anamuona kuwa haendani na hiyo nyumba, ikabidi amuulize
“Kwani vipi mama yangu! Kuna tatizo?”
“Hapana ila sisi ni majirani kwahiyo ni vyema tukafahamiana, mimi naitwa mama Jane na wewe je?”
“Mimi naitwa Sophia, na hapa naishi na mume wangu yeye anaitwa Ibra”
“Basi ni vizuri, karibu kwangu nyumba ya jirani tu hapo”
“Asante nitakaribia”
“Karibu sana, usiogope kitu sisi ni majirani tu na ni vyema kufahamiana ingawa kufahamu watu waishio humo huwa ni ngumu sana”
“Usijali utatufahamu tu”
Kisha Sophia akaagana na huyu mama halafu yeye kuendelea na safari zake.
Jioni ya siku hiyo Sophia akiwa ndani na mumewe akamsimulia kuhusu huyo mama aliyekutana nae wakati anatoka na vile alivyozungumza nae,
“Kwakweli ni vizuri kufahamiana na majirani ukizingatia tangia tumefika hapa hakuna jirani tuliyemsogelea kumsalimia”
“Basi tutafanya hivyo mume wangu. Ila kitu kingine sasa mmmhh”
Sophy akatabasamu kwanza kabla ya kuongea na kumfanya Ibra amuulize,
“Kitu gani hiki mpaka umeguna Sophy?”
“Mmh naona mapenzi yamenoga mume wangu hadi leo umeosha vyombo!”
Ibra akacheka kisha akasema,
“Mmh acha kunichekesha Sophy yani na uvivu huu mimi nikaoshe vyombo kweli!!”
“Sasa nani kaviosha vile vyombo asubuhi?”
“Nikuulize wewe uliyebaki nyumbani”
Sophia akakaa kimya kwa muda kwanza kwani hakuelewa hapo.
Sophia akakaa kimya kwa muda kwanza kwani hakuelewa hapo, akamuangalia mumewe kanakwamba amwambie kuwa alichokuwa anakisema kilikuwa ni utani tu kisha akamwambia tena,
“Acha masikhara Ibra”
“Wewe ndio uache masikhara, unajua fika kuwa mimi ni mvivu wa kimataifa haya sasa huko kuosha vyombo ningeanzia wapi? Hebu kaandae chakula tule kwanza”
“Lakini Ibra….”
“Lakini nini Sophy? Wewe kaandae chakula tule bhana, mada zingine achana nazo usifikirie ni rahisi hivyo mimi kuosha vyombo”
Sophia akaenda jikoni huku akiwa na mawazo sana ila kuna wakati alihisi kuwa Ibra anatania tu kwani kule ndani walikuwa wao wawili tu kwahiyo akahisi kuwa ni lazima Ibra ndio aliosha hivyo vyombo ila anajigelesha tu, alijiaminisha hivyo huku upande mwingine akiwa na mashaka kiasi.
“Kesho nitampigia simu Da’ Siwema nimsimulie, Yule ni mtu mzima anaelewa vizuri sana”
Kisha akaendelea na uandaaji wake wa chakula cha usiku.
Akapeleka mezani na kuanza kula na mumewe Ibra,
“Yani leo nimechoka Sophy maana nimejikuta nikiwa na kazi nyingi sana”
“Pole mume wangu ila ndio ukubwa huo”
“Kweli kabisa ukubwa jalala maana sio kwa kuchoka huku”
Walipomaliza kula, leo Sophia hakutaka kuacha vyombo vichafu kwahiyo alienda kuviosha na kuvipanga kisha kwenda chumbani kulala na mume wake ambapo alimkuta ameshalala tayari.
“Mmmh kweli leo Ibra kachoka jamani maana yupo hoi kabisa”
Kisha na yeye akatafuta usingizi pale na kulala, alipopitiwa na usingizi tu akajiwa na ndoto.
Kwenye ndoto hii alijiona yeye akiwa mjamzito ila mumewe alionekana kutokuifurahia kabisa ile mimba na alionekana kuongea maneno machafu sana ya kumkaripia,
“Aliyekwambia ubebe mimba nani? Na utaenda kuzalia kwake huyo mtu, sitaki ujinga mimi”
Sophia akashtuka sana kutoka kwenye ule usingizi huku akiilaani ile ndoto na kuona kuwa ni kitu cha ajabu sana kwake kwani haikuwa rahisi kwa Ibra kuikana mimba yake kiasi hicho ila ndoto hiyo ilimfanya asipatwe na usingizi tena hadi panakucha.
Ibra alipoamka tu, Sophy nae alikuwa macho na swali la kwanza ambalo Sophy alimuuliza Ibra ilikuwa ni kuhusu mimba.
“Hivi kwa mfano mimi nikiwa na mimba yako je utafurahi mume wangu?”
“Sophy, ninavyokupenda hivi naachaje kufurahi? Pia nahitaji mtoto Sophy wangu, na mimi napenda niitwe baba. Nakupenda sana mke wangu, najua watoto ndio watakamilisha furaha yetu mpenzi.”
“Asante Ibra”
Kisha Ibra akaanza kujiandaa pale halafu akamuaga Sophy kwa kumbusu kwernye paji la uso.
Ibra alipoondoka tu, Sophy nae akaamka na kwenda kukaa sebleni ili kujipotezea mawazo mbalimbali huku akiona wazi kuwa ile ndoto ni uchizi tu na ni kitu cha kusadikika.
“Ndoto zingine kama zimetumwa loh! Ndoto gani sasa ile? Yani Ibra kabisa akane mimba thubutuu, yani ile ndoto ishindwe na ilegee ujinga ujinga sitaki.”
Muda ulipoenda kidogo akampigia simu Siwema na kuanza kuzungumza naye kuhusu kilichotokea jana na vile ambavyo Ibra alimjibu kuwa hakuosha hivyo vyombo.
“Hayo ndio mahaba mdogo wangu, mwenzako Ibra anakupima tu lakini vyombo kaosha mwenyewe, we unadhani ataosha nani wakati ndani mpo wawili tu?”
“Ndio hapo dada nimeshindwa kuelewa kwakweli maana mimi nimekuta vimeoshwa halafu ni yeye aliyesema nisivioshe halafu anakataa kuwa hajaviosha loh!”
“Anakuchanganya akili tu huyo mdogo wangu, kwani wanaume hujawajua tu, wanapenda kutupima Sophy mdogo wangu. Hata usiwe na shaka mwaya mwenzio saivi anakuonyesha mahaba kimya kimya”
“Kweli dada haya ni mahaba maana ila hapendi kuosha vyombo, hata niumwe ataviacha hadi nipone ila kuona ameosha safari hii tena nikiwa mzima kabisa kweli ni mahaba”
“Ndio mapenzi hayo mdogo wangu hata usistaajabu sana, hapo ndio kupendwa yani wewe jiongeze tu.”
Sophia akafurahia sana ushauri aliopewa na Siwema kwani aliona ushauri huo ukimfaa sana, kisha akaagana nae kwenye simu na kuendelea na mambo mengine.
Wakati akifanya shughuli zake za hapa na pale mule ndani, akasikia hodi na kwenda kufungua mlango ambapo alimkuta Yule mama ambaye walikutana siku ya nyuma huku akiwa ameambatana na binti aliyeonekana kufanana nae sana, Sophia akawakaribisha vizuri sana watu hao ndani kwako huku akitabasamu,
“Karibuni sana jamani”
“Asante tumekaribia Sophy”
Wakaingia ndani huku Yule mama akianza utambulisho kwa binti aliyeongozana nae,
“Huyu ni binti yangu anaitwa Jane”
“Wow ndiomana umefanana nae sana mama, hongera kwa kuwa na binti mzuri”
Huyu mama akatabasamu kidogo kisha akaendelea,
“Nimeona ni vyema akufahamu jirani yetu ili hata siku akiwa mbweke nyumbani basi aje akutembelee, unajua huyu mtoto ametoka kumaliza kidato cha nne kwahiyo tunangoja matokeo tu kwasasa. Mara nyingi anashinda nyumbani kwahiyo akija kuongea ongea hapa si vibaya.”
“Umefanya jambo jema mama maana hata mimi huwa na upweke sana maana huwa nashinda mwenyewe mahali hapa, pia hongera sana Jane kwa kuhitimu kidato cha nne.”
“Unampa hongera ya bure tu huyu, akili yake yenyewe sijui kama atafaulu huo mtihani, na akifeli ndio atakaa nyumbani atafute mume aolewe tu”
“Jamani mama usiseme hivyo inakuwa kama unamuombea mabaya mtoto”
“Mabaya kajiombea mwenyewe hata sio mimi, mtu gani alikuwa anajijua kabisa kuwa ana mitihani ila ndio tamthilia sijui michezo kila kitu anakijua yeye na hatma yake inakuja kwakweli naona kabisa zero ikimuangalia.”
Jane alionekana kuwa kimya kabisa kwani ilionyesha wazi hakupendezewa na maneno ya mama yake, ili kuondoa ule mzozo ilibidi Sophia abadilishe mada kisha akaenda jikoni na kuwaletea wageni juisi huku wakizungumza mawili matatu.
Muda kidogo Ibra alirudi hata kumshangaza Sophia kwani alionekana kuwahi sana siku hiyo na alionekana kuwa na uchovu.
Sophia akamkaribisha mumewe na kumtambulisha kwa wale wageni ambao walifahamiana na kusalimiana, ingawa Ibra alikuwa amechoka ila alivunga kidogo kwenda chumbani ili wale wageni wasijihisi vibaya, ila huyu mama nae aliaga muda ule ule kwahiyo Sophia akatoa zile glass na kupeleka jikoni kisha akamuaga mumewe na kwenda kuwasindikiza wale wageni, ambapo Sophia alienda nao hadi nyumbani kwao ili kuweza kupafahamu wanapoishi watu hao.
Sophia aliweza kuona mazingira ya uswahili anayoishi huyu mama ila hakushangaa sana kwavile ndio mazingira ambayo hata yeye amekulia na ameyaishi kwa kipindi kirefu sana.
“Sophia, ukiwa na tatizo usisiste kuja, hapa ni kama nyumabani kwenu tu kwahiyo usiogope chochote”
“Usijali mama tupo pamoja”
Sophia hakukawia sana kwani aliaga na kuondoka.
Aliporudi nyumbani kwake hakumkuta Ibra pale sebleni na moja kwa moja akahisi kuwa Ibra atakuwa ameenda chumbani kupumzika tu, kisha nae akaenda chumbani alipo Ibra kwani alipenda kujua ni kwanini mumewe amechoka kiasi kile.
Alimkuta Ibra amejilaza kitandani, akamfata na kumsogelea karibu mumewe kisha akakaa pembeni yake na kumuuliza kuwa tatizo ni nini,
“Vipi tena Ibra mume wangu, nini kimekukumba baba?”
“Kwakweli hata sielewi ila nimechoka mwili na viungo vyote”
“Pole sana mume wangu, ngoja nikuandalie chakula ule kwanza ndipo ulale”
“Usijali kuhusu hilo, nilishaenda jikoni nimepakua chakula na nimekula tayari”
“Dah nisamehe mume wangu jamani”
“Usijali kitu mke wangu, wale ni wageni wetu sote kwahiyo hata usijali na ndiomana hata mimi sikuona tataizo kwenda jikoni na kujipakulia chakula”
“Pole sana mume wangu, basi ngoja nikakuandalie maji uoge”
“Kwakweli sijisikii kuoga kwasasa subiri nipumzike kwanza ndio nitaoga”
Sophia alitulia kwa muda akiitafakari hali ya mume wake kwani haikuwa kawaida kabisa kwa Ibra kuwa vile alivyokuwa.
Alienda sebleni huku akihisi kuwa huenda Ibra akawa na malaria ila ndio hivyo anajikaza kwavile ni mwanaume, kisha akaelekea jikoni na kufunua sofuria alilopikia chakula na kukuta kweli kilipakuliwa kwamaana hiyo ni kweli Ibra amekula kile chakula kisha akaangalia Ibra alipoweka sahani aliyotoka kula nayo ila hakuona sahani wala nini hapo ndipo aliposhangaa na kwenda tena sebleni kuwa huenda ameiacha huko ila hakuona sahani yoyote chafu, wazo likamjia kuwa aangalie na zile glasi ambazo wageni wamenywea juisi ila hakuziona pale zaidi aliziona zimeshawekwa kabatini tena zikiwa safi kabisa,
“Mmh huyu Ibra si anaumwa huyu sasa iweje ameosha vyombo vyake alivyolia na zile sahani jamani wakati mtu ni mgonjwa? Haya ni maajabu mapya kwangu, sasa nitamuulizaje na anaumwa? Ila lazima nimuulize?”
Sophia akatoka jikoni na kuelekea chumbani tena alipo Ibra kwa lengo la kumuuliza kulikoni maana hakuelewa kabisa.
Alimkuta Ibra akiwa bado anagalagala tu kitandani kwani hata usingizi haukumjia, kisha akamuuliza,
“Mume wangu leo umechoka sana ila kwanini umeosha vyombo ulivyolia chakula?”
“Sophy, toka lini hunijui mimi jamani! Mimi naoshaje vyombo mke wangu, kwanza naumwa halafu wewe unaniletea habari zingine kwanini unakuwa hivyo Sophy?”
“Samahani mume wangu ila ningependa twende hospitali”
“Sijisikii kwenda hospitali kwakweli, tafadhali niache nipumzike”
Sophia hakumuelewa Ibra kabisa na akahisi huenda Ibra ana malaria ambayo imempanda kichwani na ndiomana amekuwa vile alivyokuwa.
Sophia aliamua kuinuka tena ili atoke mule chumbani ila kabla hajafika malngoni alijihisi kichefuchefu na kumfanya aanze kukimbilia chooni ili atapike ila kabla hajafika chooni alijikuta kashatapika tayari kwahiyo chooni alienda kama kumalizia tu na alitoka akiwa amechoka sana ila hakuweza kuvumilia kuangalia yale matapishi yake yaliyotapakaa chumbani kwao karibia na mlanngo wa chooni, hivyobasi Sophia akaenda jikoni kuchukua tambala na maji kwa lengo la kufuta matapishi yale.
Ila aliporudi chumbani ili afute alikuta yale matapishi yalishafutwa na pale palishakaushwa kabisa, kwakweli Sophia alichoka gafla, akamuangalia Ibra pale kitandani ila Ibra alionyesha kutokuwa na habari yoyote kwani alikuwa amejilaza vile vile.
Ila aliporudi chumbani ili afute alikuta yale matapishi yalishafutwa na pale palishakaushwa kabisa, kwakweli Sophia alichoka gafla, akamuangalia Ibra pale kitandani ila Ibra alionyesha kutokuwa na habari yoyote kwani alikuwa amejilaza vile vile.
Sophia hakuelewa kwakweli yani hakuelewa kabisa, akaenda tena pale kitandani alipokuwa amejilaza Ibra na kumshtua, ambapo Ibra aliongea kwa kulalamika,
“Sophia jamani mbona hivyo mke wangu? Kwanini unanifanyia hivi lakini si nimekwambia kuwa najisikia vibaya! Sasa kwanini hutaki mwenzio nipumzike jamani unanifanyia mambo ya ajabu, kwanini kunishtua shtua kila muda?”
“Samahani Ibra lakini nani kazoa matapishi yangu?”
“Matapishi?”
“Ndio, kwani hukunisikia wakati natapika?”
“Sijakusikia bhana, unanisumbua tu Sophy hebu acha nipumzike”
Ibra akageuka tena na kulala, kwakweli Sophia hakuelewa chochote alijikuta akijishika tama tu kwa mawazo kwani aliona kama vile Ibra anamchanganyia mada huku nayeye akizidi kujiuliza kuwa kama sio Ibra anayefanya hayo je yatakuwa yanafanywa na nani? Hapo ndio ilikuwa ngumu kabisa kwa yeye kuelewa.
Akajikuta akikaa pale kitandani huku akitafakari kwa muda mrefu sana bila ya kupata majibu hadi akapata wazo la kumpigia simu tena Siwema ili amuulize ila aliona kamavile ni kumsumbua tu huyo Siwema, kwahiyo akatulia kimya kwa muda mrefu kidogo kisha akainuka pale na kuelekea jikoni kwa lengo la kuandaa vizuri mlo wa usiku.
Akiwa jikoni alijiuliza sana kitu kilichopelekea yeye kutapika ni nini,
“Hivi ni kwanini nimetapika ikiwa siumwi wala nini? Ni kitu gani kimepelekea mimi kutapika?”
Alijiuliza bila ya kupata jibu la aina yoyote ile kwahiyo akaamua kuandaa chakula tu.
Alipomaliza kuandaa chakula alitoka jikoni na kuelekea sebleni ambapo alimkuta mumewe amekaa na kwakweli alionekana kuwa sawa kabisa kwasasa tofauti na mwanzo,
“Khee Ibra kumbe umeamka tayari!”
“Ndio nimeshaamka”
“Eeh unajisikiaje na hali!”
“Nipo salama kabisa mke wangu”
“Basi ngoja nikakuandalie maji ya kuoga”
“Hata usijali mke wangu nimeshaoga labda ulete chakula tule”
Basi Sophia hakutaka kuhoji zaidi kwahiyo akaenda kuleta chakula kisha yeye na mumewe wakaanza kula chakula hicho huku wakizungumza mambo mawili matatu,
“Kwahiyo Ibra saivi unajiona umepona kabisa!”
“Ndio nimepona kwani nilikuwa naumwa sana eehh!”
“Yani hadi mimi ulinitia mashaka mume wangu mpaka hofu ilinitawala kabisa”
“Hata usiwe na mashaka mke wangu maana mimi ni mzima kabisa kabisa”
“Basi vizuri mume wangu kama ndio hivyo”
“Ila nakushukuru sana Sophy kwa mapenzi yako unayonionyesha na jinsi unavyonijali”
Sophia akatabasamu huku wakiendelea kula kile chakula, walipomaliza kama kawaida Sophia alitoa vyombo na kutaka kwenda kuviosha ila Ibra alimuita na kumfanya Sophia asioshe vyombo vile.
“Sophy mke wangu napenda nikae na wewe tupumzike pamoja”
“Naelewa mume wangu ila huwa sipendi kulala na vyombo vichafu ndani ndiomana huwa napenda kuviosha pindi tunapomaliza kula”
“Ngoja nikuulize swali, kwani kesho unaenda wapi?”
“Nipo tu siendi popote”
“Sasa tatizo liko wapi hapo? Utaosha hata kesho, mi napenda tukae tuzungumze na tupumzike pamoja”
Ikabidi Sophia atumie nafasi hii kumuuliza Ibra kuhusu matapishi yake,
“Hivi Ibra hukunisikia wakati natapika?”
“Kwani unaumwa?”
“Hapana ila nilitapika”
“Mmmh sijakusikia kwakweli”
“Mmmh kwahiyo nani alizoa matapishi yangu?”
“Mmmmmh Sophy acha habari hizo bhana tumetoka kula, hebu tubadilishe mada”
Sophia hakuwa na jinsi zaidi tu ya kufata matakwa ya Ibra na kisha wakaamua kwenda kulala, Ibra alipopitiwa na usingizi Sophia akakumbuka vile vyombo akaona ni vyema akavioshe ili asipate tena maswali ya kujiuliza kuwa vyombo vimeoshwa na nani, kwahiyo akatoka mule chumbani na kwenda jikoni kwa lengo la kuosha vyombo.
Alivikuta vyombo vipo pale pale jikoni na kisha akaanza kuviosha, muda kidogo alikuja Ibra kutoka chumbani huku akitikisa kichwa baada ya kumkuta Sophia akiosha vyombo,
“Ona sasa mke wangu halafu unakazana kuuliza nani kaosha vyombo wakati unaamkaga mwenyewe usiku wa manane kuviosha jamani unakuwa kama mwanga, majukumu gani hayo ya usiku wa manane?”
“Unajua nini Ibra sikupenda nipate tena shida ya kudadisi juu ya mtu aliyeosha vyombo ndiomana nimeamua kuviosha mwenyewe”
“Kwakweli umenishangaza Sophy yani nashtuka kitandani sikuoni kumbe upo jikoni unaosha vyombo, jamani mke wangu kwanini unakuwa hivyo jamani? Nadhani mtu yeyote atakayesikia hili lazima ashangae, kwani kuna umuhimu gani wa kuosha vyombo usiku kamavile hapatakucha?”
Ibra alionekana kutokupendezwa kabisa nah ii tabia aliyoiona leo kwa Sophy kwani yeye alipenda anapogeuka kitandani basi amkute mkewe akiwa pembeni,
“Basi nisamehe mume wangu, nakuahidi hii hali haitajirudia tena kama nikishindwa kuosha muda ambao tumemaliza kula basi nitakuwa nasubiria hadi kesho yake. Nisamehe tafadhari”
Basi akavimalizia na kuviacha pale juu huku akipanga kuviweka kabatini kesho yake kwani hakutaka kumkwaza mume wake zaidi.
Wakaongozana pamoja kuelekea chumbani ambapo Ibra alionekana kutokuwa na usingizi sana kwani yote ilitokana na vile alivyolala jioni ya siku hiyo, kwahiyo walivyofika tu kitandani Ibra akaanzisha maongezi tena.
“Hivi ulisema kuwa leo umetapika eeh”
“Ndio nimetapika”
“Basi kama hiyo hali itaendelea itabidi twende hospitali”
“Kama ikijirudia tutaenda mume wangu, asante kwa kunijali”
“Unajua Sophy mi nakupenda sana na kwakweli sipendi kuona ukisumbuka wala kuhangaika mke wangu ndiomana unaniona mara nyingine nafoka”
Kisha akamsogelea karibu na kumkumbatia ili waweze kulala, na kweli usingizi ukawapitia hadi palipokucha ambapo kama kawaida Ibra aliamka na kujiandaa kisha kumuaga mkewe na kwenda zake kazini.
Sophia nae kama kawaida yake alipoamka alienda moja kwa moja jikoni ambapo alikuta vile vyombo alivyoviosha usiku vikiwa tayari vimepangwa kabatini,
“Yani huyu Ibra ananikatazaga mimi ili afanye yeye ila ni sawa tu maana yupo kwenye harakati za kunionyesha upendo”
Alipofikilia hayo akaenda kuandaa chai na kunywa halafu akaenda kuloweka nguo ili afue, baada ya kuziloweka alirudi sebleni ili akae angalau kidogo halafu ndio akafue ila alivyokaa pale sebleni akapatwa na usingizi wa gafla uliomfanya alale hadi kujisahau kuwa alipanga kwenda kufua nguo zake.
Ibra alirudi nyumbani na kugonga sana ila kwa bahati nzuri tu alikumbuka kuwa anafunguo za ziada kwenye gari lake kisha akaenda kuchukua funguo zile na kufungua milango ambapo alimkuta Sophia akiwa amelala tena hajitambui kabisa, ikabidi Ibra ndio amshtue Sophia kutoka kwenye ule usingizi aliokuwa amelala ambapo Sophia alionekana kushtuka sana.
“Kheee Sophia ndio kulala gani huko hadi umejisahau yani nimegonga na kugonga ila wapi”
Ila Sophia alionekana kuchoka sana hata akajikuta anashindwa kumjibu mumewe kwa wakati, hadi alipotulia kidogo kama kurudisha akili yake vile ndio akaweza kumjibu mume wake,
“Yani hata sijielewi ila nimechoka balaa”
“Mmh hata kupika umepika kweli wewe?”
“Kwakweli sijapika wala sijafanya chochote kile yani hata sijielewi”
“Pole sana mke wangu basi twende tukajimwagie upate nguvu kisha twende tukale hotelini maana hamna namna tena”
Sophia akakubali na kuzidi kuuona upendo wa Ibra juu yake kuwa Ibra anampenda na kumuhurumia sana kwani ile iliweza kuonyesha ni kwa kiasi gani alipendwa na Ibra.
Walipomaliza kujiandaa wakatoka na kuelekea hotelini kama ambavyo Ibra alisema ili kuweza kula, waliagiza chakula na kuanza kula ila gafla Sophia akapatwa na kichefuchefu na kujikuta akikimbilia nje kutapika, Ibra alivyoona vile akamuomba muhudumu awafungie kile chakula kisha akaenda kumuangalia mke wake,
“Kwani unajisikiaje Sophy”
“Najisikia vizuri tu”
“Vizuri wakati umetapika jamani! Itabidi kesho twende hospitali tukaangalie afya yako”
Sophia akakubali kisha akaja Yule muhudumu na kuwapa chakula chao ambapo Ibra alilipia na kuondoka na mke wake.
Walipofika nyumbani waliweka kile chakula na kuanza kula tena ila Sophia alionekana kula kwa kujivuta vuta sana,
“Lazima unaumwa Sophy ingawa wewe mwenyewe unajiona kuwa mzima”
“Ni kweli kabisa najiona kuwa mzima mimi”
“Hata kama unajiona ni mzima lazima kesho twende hospitali maana hii hali ni mbaya mke wangu”
“Sawa nimekuelewa kwa hilo”
Walipomaliza kula, Ibra alibeba vile vyombo na kuvipeleka jikoni kisha akamtaka mke wake kuwa waende kulala,
“Ila sina usingizi Ibra”
“Hata kama, ila mi nakuomba twende tu chumbani”
Kisha wakaelekea chumbani na moja kwa moja wakaenda kitandani ambapo ibra alikuwa akimuangalia sana mke wake kwani aliona wazi kuwa lazima atakuwa anaumwa tu ila anajikaza.
Kulipokucha, asubuhi na mapema Ibra akamuamsha mke wake ili aweze kujiandaa na waweze kwenda hospitali ambapo Sophia alifanya hivyo ila alipomaliza kujiandaa akamwambia mume wake,
“Lakini unajua Ibra mi siumwi kabisa na wala hata sijisikii vibaya”
“Unaweza ukajiona kuwa huumwi kumbe ugonjwa upo ndani kwa ndani, usifikiri ni kitu rahisi kutapika vile Sophia usiwe mbishi kwani mi nakuona kabisa kuwa unaumwa”
“Na hospitali tutaenda kujielezaje sasa?”
“Tutajieleza kama hali halisi ilivyo”
“Ila bado mimi sidhani kama naumwa kwani nahisi ni uchovu wa jana tu”
“Uchovu wa jana umefanya kazi gani?”
Sophia akafikiria kidogo na kukumbuka kuwa aliloweka nguo,
“Mmmh jana nililoweka nguo ila sikuzifua mmh si zitanuka jamani maana nilisahau kabisa”
“Basi usijali tutafua pamoja tukirudi”
Sophia akatabasamu kisha akatoka na mume wake kwa lengo la kwenda huko hospitali, ila alipofika malangoni akakumbuka kitu kwenye zile nguo alizokuwa ameloweka jana yake ikabidi amwambie mumewe amsubiri akachukue.
Alipofika uwani ambako aliloweka zile nguo alikuta zote zikiwa kwenye kamba tena zilionekana kukauka kabisa, kwakweli Sophia akashangaa sana na kumita Ibra kwa nguvu ili kumuonyesha kile anachokiona.
Ibra nae alifika kwa haraka sana kama alivyoitwa na Sophia, kisha Sophia akamuonyesha nguo kwenye kamba ambapo Ibra aliuliza kwa mshangao
“Kwani vipi Sophy?”
“Nguo kafua nani?”
“Nguo kafua nani kivipi?”
“Kwani wewe huoni nguo kwenye kamba?”
“Naziona ndio kwani tatizo nini?”
“Nani kazifua sasa wakati mimi niliziloweka tu!”
Ibra alikuwa akimshangaa tu mkewe ambapo kabla hata hajasema chochote, Sophia alianguka chini na kuzimia.
Ibra alikuwa akimshangaa tu mkewe ambapo kabla hata hajasema chochote, Sophia alianguka chini na kuzimia.
Ikabidi Ibra ambebe mke wake na kwenda kumpakia kwenye gari kisha kumpeleka moja kwa moja hospitali huku akihisi kuwa pengine mkewe ana maralia imempanda kichwani ndiomana anaongea mambo yasiyoeleweka.
Walifika hospitali na moja kwa moja kupokelewa na wahudumu wa hospitali ile ambapo muda kidogo tu Sophia alionekana kuzinduka na kuwa sawa kiasi ambapo Ibra aliingia na mkewe kwa daktari na kuelezea kwa kifupi matatizo ya mke wake ambapo daktari aliwatajia vipimo vya kupima.
Walimaliza kufanya vipimo na wakaa mapokezi wakisubiri majibu na kuitwa na daktari. Muda wote Ibra alikuwa akimtazama mkewe kwani alimuona kama mtu mwenye matatizo sana kwa kipindi hicho, Sophia alimuuliza mumewe,
“Mbona unaniangalia sana bila ya kusema chochote?”
“Kwakweli sina usemi mke wangu ingawa kuna mambo mengi sana najiuliza kuhusu wewe”
“Kama mambo gani?”
“Nadhani tutaongea zaidi tukirudi nyumbani, ngoja kwanza daktari atupe majibu ya vipimo ulivyofanyiwa”
Muda kidogo daktari aliwaita na walipoingia ofisini tu daktari alianza kwa kumpongeza Ibra,
“Hongera sana bwana Ibra, mkeo ni mjamzito”
Ibra akatabasamu kiasi kisha akamuuliza daktari,
“Kwahiyo tatizo lake ni mimba tu au kuna lingine?”
“Hakuna lingine lolote, ni mimba tu. Tena itakuwa vyema kama mkiwahi kuja kuanza na kliniki ili kujua maendeleo ya mtoto aliyeko tumboni”
“Sawa daktari, kwahiyo hakuna tiba yoyote anayoweza kupatiwa?”
“Mr. Ibra, mimba si ugonjwa wa kutibiwa huwa ni hali tu inatokea kwa mwanamke kutokana na kile kitu tofauti kinachojitengeneza kwenye mwili wake. Cha muhimu kujua kuwa mkeo ana mimba na unatakiwa kuwa nae karibu sana ili uweze kumsaidia baadhi ya mambo. Mkianza kliniki mtajifunza mengi zaidi kwahiyo mzingatie hilo.”
“Sawa basi tumekuelewa daktari, tutafanyia kazi ushauri wako”
Kisha daktari akampatia Sophia dawa za vitamin ambazo zingemsaidia kiasi kwa hali aliyokuwa nayo kwa kipindi hicho halafu wakaanza safari ya kurudi nyumbani kwao.
Walipokuwa njiani kurudi wanapoishi, wakamuona mtoto mdogo barabarani kwa makadirio anaweza akawa kwenye miaka mitatu, alionekana kusimamisha gari yao kanakwamba anaomba msaada ila Ibra alipita bila kusimama ambapo mbele Sophia alimshika mkono na kuonyesha kutokufurahishwa na kitendo cha Ibra cha kumpita mtoto Yule aliyeonekana kutaka msaada.
“Hivi Ibra inamaana Yule mtoto hukumuona?”
“Aaah Sophy, mtoto mdogo kama yule anawezaje kusimama barabarani na kusimamisha gari jamani!! Mambo mengine tutumie akili ya ziada tu mke wangu”
“Sijapenda Ibra yani sijapenda kabisa kabisa”
“Kwahiyo unatakaje?”
“Turudi ili tujue ana tatizo gani”
“Hivi unajua kama hata majambazi wanawatumiaga watoto wadogo mke wangu! Tusije tukajitafutia matatizo bure jamani”
“Hata kama turudi tu kwakweli, hivi wewe huna hata huruma jamani! Mtoto mdogo vile unaanza kumuwekea imani za majambazi mmh! Turudi tafadhari.”
Ibra hakutaka kumkwaza mke wake tena ukizingatia kwa ile hali yake ya ujauzito aliyoambiwa na daktari, hivyobasi akarudisha gari nyuma kwa lengo la kumfata Yule mtoto.
Walifika pale ambapo Yule mtoto aliwasimamaisha na walimkuta pale pale ambapo Ibra alisimamisha gari kisha Sophia akashuka na kumchukua Yule mtoto kisha akapanda nae kwenye gari na kujaribu kumuuliza anapoelekea ambapo Yule mtoto aliwaonyesha kwa kidole tu anapoelekea kisha Ibra akaondoa gari na kuanza kwenda alipoonyesha Yule mtoto.
Walifika mahali kisha Yule mtoto akasema,
“Simama hapa hapa”
Ibra alisimamisha gari ila kwa hofu kiasi kwani hakutegemea kama Yule mtoto anaweza kuonngea ukizingatia mwanzo aliwaonyesha kwa mkono tu.
Kisha Sophia akafungua mlango kwa vile alikuwa amempakata mtoto huyo na kumshusha akizani labda kuna maelekezo mengine Yule mtoto atayatoa, ila Yule mtoto alivyoshuka tu aliwatazama na kuwaambia,
“Asanteni kwa kunikaribisha rasmi kwenye maisha yenu”
Akapunga mkono kisha akaondoka kwa kukimbia ambapo kwa sekunde chache tu alipotea kwenye macho yao.
Ibra na Sophia wakatazamana kisha Ibra akamuuliza mkewe,
“Hivi umemuelewa huyu mtoto?”
“Mmmh hata sijamuelewa”
Ibra nae akaguna kisha akaondoa gari mahali pale na kuendelea na safari yao ya kurudi nyumbani.
Walipofika nyumbani ilionyesha wazi kuwa Ibra alichoshwa kabisa na Yule mtoto ambaye walikutana nae njiani kwani ilikuwa ngumu sana kwake kuelewa msaada ambao Yule mtoto aliuhitaji kutoka kwao, kisha akamuuliza tena mke wake
“Hivi Yule mtoto ulimuelewa?”
“Hapana hata sikumuelewa”
“Safari ijayo usiwe na roho ya huruma kiasi kile itatuponza, huruma muda mwingine sio nzuri”
“Lakini tumepungukiwa na nini mume wangu kumsaidia Yule mtoto jamani? Hata Mungu atatuongezea thawabu”
“Thawabu zipo ila si kwa staili ile ya Yule mtoto, natumaini hakuwa na nia mbaya juu yetu”
“Mtoto Yule bhana hawezi kuwa na nia mbaya kwakweli”
“Sawa”
Kisha Ibra akabadilisha mada na kumpongeza mke wake kwa mimba aliyobeba,
“Hongera sana mke wangu, sasa furaha yetu itaenda kukamilika”
Sophia akatabasamu kisha akamsogelewa mumewe na kumkumbatia kwani aliona mawazo yake yakianza kutimia juu ya wao kuwa na watoto wa kutosha mule ndani.
“Hongera na wewe pia mume wangu maana hii ni furaha yetu wote”
“Yani sipati picha kumshika mwanangu akizaliwa maana nitafurahi sana kumuona kwakweli, itakuwa furaha kubwa sana ya maisha yangu”
“Mimi je! Nitafurahi sana sana maana sasa nitakuwa nimepata mtu wa karibu, siku ya kwanza kumshika na kumnyonyesha nitafurahi sana”
Walionekana kutabasamu na kufurahia ambapo muda huu ibra alionekana kumuuliza mkewe kuwa atapendelea kula chakula gani maana alitaka kujitolea siku hiyo kupika kwaajili ya mke wake, Sophia akatabasamu na kumjibu mumewe kuwa atakula chakula chochote tu.
“Leo nitakupikia mwenyewe Sophy, tafadhali wewe pumzika tu hapo nipike fasta fasta tule”
Sophia akatabasamu na kukaa kwenye kochi huku akihisi kuwa mumewe anafanya mbwembwe tu kwani alijua muda wowote atamshtua kuwa akapike mwenyewe, Ibra alienda jikoni na kumuacha Sophia pale sebleni ambapo kwa muda mfupi kabisa Sophia alipitiwa na usingizi pale pale kwenye kochi.
Sehemu Ya 2
Wakati Sophia amelala pale kwenye kochi akajiwa na ndoto ambapo kwenye ndoto hiyo akamuona Yule mtoto waliyemkuta kule njiani, alionekana akitabasamu huku akimuangalia Sophia na kumwambia,
“Nitakuwa nakusaidia kazi zote ngumu na hata zile nyepesi zikiwa nyingi nitafanya mimi, napenda ukarimu wako ila huyo mtoto ajaye atakuwa ni ndugu yangu mimi sababu yeye nitampenda zaidi”
Sophia alijikuta akimuuliza huyu mtoto,
“Kivipi?”
Huyu mtoto alionekana akicheka tu bila kuongeza neon la ziada na kumfanya Sophia ashtuke sana kwenye ile ndoto na kujikuta kama akipiga kelele hivi ambapo Ibra alimfata mbio na kumuuliza kuwa kuna tatizo gani.
“Vipi Sophy mke wangu ni nini tatizo?”
“Mmh nimeota ndoto hata siielewi”
“Ndoto gani hiyo?”
“Nimemuota Yule mtoto tuliyemkuta njiani”
“Sophy mke wangu nakuomba uachane na habari za Yule mtoto kwani naona wazi zitakuchanganya tu, yani fanya hivi kwenye akili yako kuwa hatujawahi kukutana na Yule mtoto maana bila ya hivyo sidhani kama itakuwa rahisi kumsahau. Bora ujiwekee kuwa hatujawahi kukutana nae kabisa, Yule mtoto hafai kumuweka akilini kwani hakuwa mtoto wa kawaida kabisa”
“Kwanini unasema hakuwa mtoto wa kawaida?”
“Wewe fikiria hata alipoingia tu kwenye gari alionyesha kuziendesha akili zetu na kujikuta tukifanya anavyotaka yeye kamavile kumpeleka pale alipopataka tena kwa maelekezo ya kidole tu, kwakweli Yule mtoto si wa kawaida hatutakiwi kumuweka akilini mke wangu.”
“Sawa nimekuelewa mume wangu”
“Twende basi tukale”
“Mmh hata nina hamu ya kula basi!!”
“Njoo tule hivyo hivyo mdogo mdogo”
Ikabidi Sophia asogee na mumewe mezani na kuanza kula, kwakweli alimpa hongera mumewe kwa chakula kile maana kilikuwa kitamu sana,
“Asante ingawa nimekipika kawaida tu yani hata mimi mwenyewe nashangaa kuwa kitamu hivi”
Sophia akatabasamu kwani mumewe alimshangaza sana kusema kuwa hata yeye anashangaa utamu wa chakula wakati kakipika mwenyewe.
Walipomaliza kula, Sophia alitoa vile vyombo na kuvipeleka jikoni kisha akaviosha ambapo muda huo Ibra alikuwa sebleni.
Sophia alipomaliza kuosha vile vyombo, iakamjia kumbukumbu ya zile nguo chafu ambazo aliziloweka pia ikamjia kumbukumbu ya vile alivyozikuta kwenye kamba kuwa zilishafuliwa na kuanikwa, ni hapo hapo akakumbuka kuwa hiyo ndio sababu iliyomfanya azimie hapo kabla.
Kwahiyo alipotoka jikoni tu, moja kwa moja akaelekea uwani ambako huwa anafua nguo zake, alipofika uwani safari hii hakuona nguo yoyote cahafu wala za kwenye kamba hakuziona. Akapata wazo la kwenda chumbani kuangalia, ambapo alifika chumbani na kufungua kabati alikuta zile nguo zote zilishakunjwa na kupangwa kabatini, kwakweli Sophia akaguna na kujiuliza kidogo.
“Inamaana Ibra ndio kafanya haya mambo? Ndio lazima tu atakuwa yeye tu maana hakuna mwingine wa kufanya haya.”
Kisha Sophia akatoka chumbani na kurudi sebleni na kwenda kukaa karibu na Ibra kisha akamwambia,
“Asante mume wangu kwa kunisaidia udobi”
“Udobi? Udobi gani tena?”
“Si zile nguo chafu umezifua zote na kuzianua kisha umezipanga kabatini”
“Mmh mbona kama sikuelewi!”
“Hunielewi kivipi wakati zile nguo umeshaanuwa na kupanga kabatini”
Ilionyesha Ibra alikuwa haelewi kitu kwakweli, ikabidi Sophia amshike mkono na kumpeleka mpaka uwani pa kufulia ambapo hapakuwa na nguo yeyote kwenye kamba, kisha akampeleka chumbani na kufungua kabati ambapo ilionyesha nguo zikiwa zimepangwa vizuri kabatini, Ibra akamtazama Sophia na kumuuliza
“Nani kafanya yote haya?”
“Unaniuliza mimi tena! Si wewe hapo”
“Sijafanya hiki kitu mimi”
Wakajikuta wakitazamana kwa muda kidogo, huku wakiwa na hofu kwa mbali.
Ilionyesha Ibra alikuwa haelewi kitu kwakweli, ikabidi Sophia amshike mkono na kumpeleka mpaka uwani pa kufulia ambapo hapakuwa na nguo yeyote kwenye kamba, kisha akampeleka chumbani na kufungua kabati ambapo ilionyesha nguo zikiwa zimepangwa vizuri kabatini, Ibra akamtazama Sophia na kumuuliza
“Nani kafanya yote haya?”
“Unaniuliza mimi tena! Si wewe hapo”
“Sijafanya hiki kitu mimi”
Wakajikuta wakitazamana kwa muda kidogo, huku wakiwa na hofu kwa mbali. Kila mmoja alihisi kuwa mwenzake kuna kitu anamficha hivyo wakajikuta wakiwa kimya kwa muda.
Ibra akaona ni vyema kupotezea hayo mambo ili asije akalumbana na mke wake bure, kwahiyo alichokifanya ni kumshika mkono na kurudi nae sebleni kisha kuanza kuongea nae mambo mbalimbali kuhusiana na mipango yake.
“Sophy mke wangu, inatakiwa katika akili zetu sasa tuanze kupanga mipango kuhusu mtoto wetu ajaye, kwanza kabisa nakushukuru sana mke wangu kwa hiyo zawadi uliyoibeba tumboni mwako kwaajili yangu”
Sophia akatabasamu kwani maneno ya mume wake yalimpa faraja sana, kisha nae akamwambia mumewe,
“Hata mimi nina furaha sana kwani ile ndoto yetu ya kuwa na watoto wane naiona ikitimia kabisa.”
“Kwahiyo umepanga mdogo wake huyu aje baada ya muda gani?”
“Yani huyu akifikisha miaka miwili tu namletea mdogo wake”
“Lakini nasikia kwenye uzazi wa mpango huwa wanasema angalau watoto wapishane miaka mitano mitano ili kila mmoja apate yale malezi ya kutosha ya kitoto”
Sophia akacheka kidogo na kumwambia mumewe,
“Achana na hayo mambo ya wataalamu na hao wa uzazi wa mpango mume wangu, katika maisha kila mtu huwa anajipangia mambo yake mwenyewe, kwetu tumezaliwa tisa tena mama alituachanisha kidogo sana, mwingine kampita mwenzie miaka miwili, mwingine mmoja, mmoja na nusu lakini wote tumekuwa vizuri tu hatuna kasoro wala dosari yoyote kama unavyotuona.”
“Kasoro ipo Sophy”
“Kasoro gani?”
“Kwanza kabisa kwenu mmezaliwa wengi kushinda uwezo wa wazazi wenu, pili mlipishana karibu sana. Angalia mlivyo ni nani aliyebahatika kusoma kwenu hata aweze kuitwa msomi labda”
Sophia akanuna kiasi kisha akamuuliza Ibra,
“Kwahiyo kusoma ndio kasoro? Mbona nyie mpo wachache kwenu na hata hamjasoma kivile!”
“Ni kweli kwetu tupo wachache na hatujasoma hivyo ni kutokana na uwezo wa wazazi wetu ila uchache tuliokuwa nao umefanya tuweze kupambana na ugumu wa maisha. Kwakweli kwa upande wangu kaka zangu wote wamejikwamua kimaisha, kumbuka tupo watano nyumbani kwetu. Kaka zangu watatu walishajikwamua kimaisha, dada nae alijitahidi kujikwamua na sasa kaolewa huku akiendeleza gurudumu la maisha yani nilibaki mimi tu nyuma ambapo nami nimekomboka kwa sasa tena nimewapita wote kimaisha. Haya kwa upande wa kwenu yani mwenye afadhari ni wewe tu, angalia akili za dada zako zilivyo na Yule mdogo wako wa mwisho ni nini anafanya. Kaka zako je, bangi bangi na wao hapo kuna maendeleo gani ya kuwa wengi ambao hamueleweki? Kwa walivyo wazazi wenu wangewazaa wachache na uhakika wasingeshindwa kuwasomesha”
Sophia akanuna zaidi na kumuuliza tena Ibra tena kwa kupaniki,
“Tungekuwa wachache mimi ningekuwepo? Nakuuliza wewe ningekuwepo? Maana mimi kuzaliwa kwetu ni mtoto wa nane ndio akazaliwa Yule mdogo wangu, mara nyingine ujifikiriage kabla ya kuongea mambo ya kijinga jinga.”
Kisha akainuka kwa hasira na kuelekea chumbani.
Ikabidi Ibra ainuke na kumfata mkewe chumbani ili aweze kumbembeleza ambapo akamkuta akilia,
“Jamani mke wangu usichukulie hasira yale yalikuwa ni maongezi tu wala sikuwa na nia mbaya”
“Hukuwa na nia mbaya wapi wakati unaisema familia yangu!”
“Nisamehe mke wangu tafadhali, nakupenda sana Sophy”
“Yani mi kusema watoto wapishane miaka miwili miwili umeona ndio ishu, kuna watu wanahangaika na wake zao huko sababu hawataki kuzaa zaa watazeeka ila mimi niliyejitolea kwako unaniona mjinga poa bwana.”
“Tafadhali mke wangu nisamehe, nakuomba nisamehe sana”
Ibra akapiga na magoti kumuonyesha mkewe kuwa anajutia kitu alichoongea, kitendo cha Ibra kupiga magoti kikampa Sophia faraja na kujikuta akitabasamu na kufanya afurahi na mume wake.
Kwavile ilikuwa ni jioni, Ibra akamuomba mkewe watoke kidogo wazunguke zunguke maeneo ya karibu kama kufanya zoezi la kutembea tu ambapo Sophy alikubali kisha akabadili nguo na kuwafanya watoke sasa.
Walipokuwa nje ya nyumba yao, Ibra aliona kuna upande ambao hajawahi kutembelea toka walipohamia kwenye nyumba ile na kumuomba mkewe waelekee upande ule kidogo, kisha wakatoka pale na kuanza kuelekea ule upande.
“Ila tusiende mbali sana nitachoka mwenzio”
“Usijali Sophy, tunatembea kwa stepu hakuna haja ya kwenda mbali sana.”
Wakiwa njiani wakaonana na Jane ambapo Sophia alisimama kwa tabasamu na kusalimiana na huyo Jane,
“Shikamooni”
“Marahaba, mbona hukuja tena nyumbani wakati uliniahidi kuwa utakuwa unakuja”
Jane akatabasamu kidogo kisha akasema,
“Kesho nitakuja dada hata usijali”
Waliongea kidogo pale na kuagana nae.
Alipoondoka, Sophia akamuuliza mumewe kama anamkumbuka Yule Jane,
“Mmh hata simkumbuki”
“Ndio Yule binti wa Yule mama jirani yetu ambaye mwanzoni kabisa nilikutana nae pale getini kwetu, na siku amekuja na binti yake hata wewe uliporudi uliwakuta”
“Aaah nishawakumbuka, si unajua tena kichwa hiki kina mambo mengi”
“Loh naona kweli mambo mengi maana hata hili ulikuwa hukumbuki kweli mambo yanakutinga”
Kisha wakaendelea na matembezi yao ya hapa na pale, kuna mahali palikuwa na kimlima kidogo ambapo Ibra akashauri warudi tu kwani alihisi kupanda kile kimlima kutamfanya mkewe achoke sana,
“Turudi nyumbani Sophy”
“Aah jamani, tusogee sogee kidogo yani mi ndio ushanitamanisha na kutembea, twende tukaishie pale kwenye kimlima”
“Ila si unaona giza nalo limeanza kuingia”
“Ndio naona ila tuishie hapo kwenye kimlima”
Ibra hakumpinga kwavile aliyekuwa akimuonea huruma ni yeye mwenyewe, kwahiyo wakaendelea mbele kidogo na kuanza kupandisha kale kamlima.
Walipofika juu kidogo kulikuwa tena na kamteremko kakushuka chini ila kuna kitu kilimshtua Sophy kwa kule chini na kumfanya amkumbatie mumewe kwa nguvu,
“Nini tena Sophy?”
“Ona kule chini”
Ibra alipoangalia akamuona tena Yule mtoto wa mchana akiwatazama kamavile anaomba msaada, Ibra akamshika mkewe mkono na kurudi nae nyuma kisha kugeuza na kuanza kurudi nyumbani huku akiongea,
“Yani mimi nikikataa kitu ujue lazima kuna tatizo ona sasa bora hata tungerudi pale pale nilipokataa”
Sophia hakujibu chochote zaidi ya kukokotana na kurudi nyumbani.
Walifika nyumbani, ila Sophia alidai kuchoka sana na kuelekea chumbani kulala ambapo ibra nae alielekea chumabani na kulala pembeni ya Sophia kwa kumkumbatia ili aweze kuwa na amani.
Wakati usingizi umemkolea kabisa Sophia akajiwa na ndoto, akamuona tena Yule mtoto akiwa pale pale chini kidogo ya kile kilima ambapo kwenye ndoto hii Sophia alijiona akimfata Yule mtoto alipo na kumuuliza kuwa tatizo ni nini, kisha Yule mtoto akamwambia,
“Sina ubaya na wewe Sophia, una moyo wa kujali halafu una upendo sana ila tatizo ni huyu mume wako hana huruma kabisa. Je ungependa nimfanye nini?”
Sophia akawa kama anamshangaa huyu mtoto na kumuuliza,
“Umfanye nini kivipi na kwanini?”
“Mumeo ana roho mbaya sana Sophia, sipendi watu wasio na huruma wakati mimi huwa nakusaidia mambo mengi sana. Niambie basi nimfanye nini?”
“Hapana usimfanye chochote mume wangu”
“Usiwe na huruma hivyo Sophia kwa mtu asiye na huruma, yani mimi hata ukiniambia nimuue sasa hivi huyu mumeo namuua”
Sophia akashtuka kutoka kwenye ile ndoto na kupiga kelele huku jasho jingi likimtoka na kufanya Ibra nae ashtuke na kumuuliza mkewe kuwa tatizo ni nini,
“Vipi Sophy?”
Sophia alikuwa akihema juu juu na kumjibu mumewe,
“Nimeota ndoto mbaya sana”
“Mmmh pole mke wangu, hiyo ndoto inahusu nini?”
“Nimemuota tena Yule mtoto eti alitaka kukuua wewe”
Ibra akatabasamu kwavile hakuwa mtu wa hofu kwa mambo kama hayo haswa ya kuhusu ndoto, kisha akamwambia Sophia,
“Mke wangu, usiwe na wasiwasi juu yangu halafu ndoto za namna hiyo zisikutishe sana. Mimi ni mwanaume jasiri siwezi kuteketea kirahisi hivyo. Pia naomba Yule mtoto umtoe mawzzoni mwako mke wangu tafadhali”
Kisha Ibra akainuka na mkewe na kwenda kuoga ili angalau kupata nguvu mpya na kuondoa uchovu uliopita hata iwasaidie kuanza upya usingizi.
Walimaliza kuoga na kurudi tena kulala.
Kulipokucha, Ibra aliamka na kujiandaa kwenda kwenye mahangaiko yake kisha akamuaga mke wake na kumwambia kuwa endapo kutatokea tatizo lolote basi asisite kumpigia simu.
“Usijali nitakujulisha mume wangu”
Kisha Ibra akmbusu mkewe kwenye paji la uso na kumuaga.
Sophia hakuweza kuendelea kulala kwani muda ule ule aliamka na kwenda sebleni akiwa amejikalia tu kisha muda kidogo akafanya kazi zake za hapa na pale kisha kupumzika tena.
Akiwa pale sebleni alisikia hodi na kwenda kufungua ambapo aliyeingia alikuwa ni Jane hivyo kumfanya Sophia afurahi sana kwa kupata kampani ya muda ule.
“Bora Jane umekuja maana nilikuwa mpweke sana”
“Ndiomana nikaamua kutimiza ahadi yangu”
Sophia alimkaribisha vizuri sana Jane na kukaa pamoja sebleni huku wakizungumza mambo mbalimbali, ambapo Sophia alimuuliza Jane,
“Hivi huwa unafanya nini ukiwa nyumbani mwenyewe, ukiachana na kazi za nyumbani”
“Kwakweli dada mi napenda sana kusoma stori haswa stori za kutisha”
“Kheee wa ajabu wewe sasa stori za kutisha unazipendea nini?”
“Yani mi huwa napenda tu halafu huwa naona kama kweli vile”
“Basi mimi katika vitu ambavyo sipendi ni kusoma stori haswaa za kutisha sababu huwa naona ni uongo mtupu. Waandishi wanaandika vitu vya kidhahania yani havina ukweli wowote.”
“Mmh ila vingine vina ukweli dada, mfano mamabo ya misukule”
Sophia akacheka sana,
“Yani Jane na usomi wako wote bado unaamini kuhusu misukule! Hakuna kitu kama hicho duniani, tatizo lako hizo stori zimekukaa kichwani, ushawahi kuona msukule wewe? Zaidi ya kuona kwenye sinema na kusoma kwenye stori, hakuna kitu kama hicho”
“Lakini dada mara nyingi wanaoandika stori huwa ni mambo ambayo yapo kwenye jamii ndiomana yameandikwa”
“Aaah ni propaganda tu hizo ili wapate wasomaji wengi hakuna ukweli wowote”
“Ila kuna mambo ni mazuri na yanatufundisha kwakweli, mimi toka nianze kusoma hizi stori nimejifunza mambo mengi sana. Kwanza siwezi kulala bila kumuomba Mungu maana usiku wetu umezingirwa na mambo mengi, na pia nikiamka lazima nimshukuru Mungu na kuomba aniongoze siku hiyo ingawa mara nyingine nasahau kuomba nikiamka kwakweli”
Hapo hapo akajicheka tena na kusema,
“Aah hata leo yenyewe nimeshau kusali, kwakweli Mungu anisamehe tu”
Sophia nae akacheka na kumwambia,
“Hebu acha masikhara yako Jane, yani mi mtu haniambii kitu kuhusu mastori ya uongo yani siwezi kupoteza muda wangu nifatilie.”
Kisha wakabadili mada na kuanza kuongelea mambo mengine.
Mchana ulipofika Sophia alijisikia uchovu sana na kumuomba Jane akamsaidie kupika,
“Mdogo wangu Jane naomba msaada tafadhali”
“Sema chochote dada nitafanya”
“Jikoni kuna ndizi nilizimenya na nyama ipo kwenye friji, unaweza kwenda kupika ili tule”
“Aah usijali dada, jikoni ndio wapi?”
Sophia akamuonyesha Jane mlango wa jikoni ambapo Jane aliinuka na kuelekea jikoni.
Alipoingia alienda moja kwa moja na kufungua friji ambapo hakuona nyama yoyote ila alipoangalia kwenye jiko aliona sufuria imefunikwa vizuri kabisa akaamua kusogea na kufunua, kwanza akasikia harufu nzuri sana ya chakula na alipoangalia aliona ni ndizi zikiwa zimepikwa vizuri kabisa tena zikiwa na nyama na bado zilikuwa za moto. Kwakweli Jane alishangaa kiasi na kujiuliza,
“Hivi kaniambia nije nipike au nimsaidie kupakua jamani! Mbona chakula alishapika tayari! Nadhani kaniambia nije nipakue.”
Kisha akachukua bakuri kubwa na kupakua halafu akapeleka mezani na kuweka sahani halafu akamfata Sophia na kumwambia tayari.
Sophia akamuangalia kwa makini na kumuuliza,
“Tayari nini?”
“Tayari chakula kipo mezani”
“Mmh usinitanie Jane, haiwezekani zile ndizi ziwe zimeiva! Hebua acha utani”
Akaelekea na Jane mezani ila bado Sophia hakuamini na kumuangalia vizuri Jane kisha akamuuliza,
“Je wewe ni binadamu wa kawaida?”
Jane akamshangaa Sophia kwa swali lile.
Sophia akamuangalia kwa makini na kumuuliza,
“Tayari nini?”
“Tayari chakula kipo mezani”
“Mmh usinitanie Jane, haiwezekani zile ndizi ziwe zimeiva! Hebu acha utani”
Akaelekea na Jane mezani ila bado Sophia hakuamini na kumuangalia vizuri Jane kisha akamuuliza,
“Je wewe ni binadamu wa kawaida?”
Jane akamshangaa Sophia kwa swali lile.
Kwakweli Jane hakuweza kumjibu Sophia kwani lile swali pia halikuwa la kawaida na hata hivyo Sophia hakuonekana kawaida kabisa kwani alionekana ni mtu mwenye mashaka na Yule Jane.
Wakiwa bado wanatazamana, wakashtushwa na hodi na kufanya Sophia aende kufungua ambapo aliyeingia alikuwa ni mumewe Ibra ila muda huo huo Jane nae hakuweza kukaa kwani aliaga juu juu na kuondoka zake hata Ibra aliweza kuelewa kuwa lazima kuna tatizo kwavile hakuuelewa ule uagaji wa Jane na kuondoka.
Ibra akamuangalia mkewe na kumuuliza kuwa ni nini tatizo, Sophia akaamua kumueleza mumewe jinsi ilivyokuwa hadi kupelekea hali ile, Ibra akasikitika na kumuangalia mkewe kisha akamwambia,
“Unajua mke wangu kila siku napenda kukwambia kuwa uwe unafikiria kwanza kabla ya kuongea jambo lolote maana maneno yako huwa katika hali ya ukali sana. Nilivyokuzoea mimi ni tofauti na mwingine alivyokuzoea.”
“Hivi unafikiri ningemuulizaje jamani? Tatizo Ibra hukuwepo, yani mtu nimemwambia muda huo huo kuwa akapike halafu muda huo huo anaenda jikoni na kuniambia chakula tayari! Inakuingia akilini kweli? Nakwenda mezani nakuta kweli ameshaandaa chakula mmh! Kwakweli kwa upande wangu imekuwa ngumu sana kujizuia kwa hiyo hali jamani maana haiwezekani tena haiwezekani kabisa.”
Ibra akaongozana na mkewe mpaka mezani na kuangalia zile ndizi pale mezani kisha akachukua kijiko na kuzionja, halafu akakaa kimya kwa muda na kusema
“Mmmh ndizi tamu sana hizi sijapata kuona yani na njaa yangu hii hebu kaa hapo tuanze kula”
“Ila upikaji wake ni wa kustaajabisha mume wangu”
“Achana na mambo ya upikaji, mi nakujua Sophy mke wangu usikute ulimuagiza binti wa watu akapike halafu ukapitiwa na usingizi, mtu anakwambia chakula kimeiva unashtuka na kuona ni muda huo huo kwavile ulipitiwa na usingizi, hebu kaa tule”
Ibra akaweka chakula kwenye sahani na kuanza kula vizuri kabisa huku akimsisitiza Sophia nae aweze kula ambapo Sophia aliamua kula kutokana na vile ambavyo mumewe alimsisitiza.
Kwakweli chakula kilikuwa kitamu sana na kufanya waifurahie ladha ya kile chakula lakini bado Sophia alikuwa na mashaka sana juu ya upikaji wa kile chakula hata imani yake juu ya Jane ikapungua kabisa.
Walipomaliza kula, Ibra akamshauri mkewe kuwa waende wakamuombe msamaha Jane,
“Mmmh sijui atanifikiriaje sasa!”
“Usijali twende kisha mi nitazungumza nae maana mi ndio nakufahamu vizuri wewe”
Basi wakakubaliana na kuinuka wakielekea kwakina Jane.
Walipofika walimkuta mama Jane akiwa nje akichambua mboga, ikabidi Sophia ajichekeleshe kidogo na kuulizia kama Jane yupo,
“Jane karudi ila kapitiliza moja kwa moja chumbani, ngoja nimuite”
Mama Jane akamuita Jane kisha Sophia akakaa karibu na huyu mama akimsaidia kuchambua ile mboga, Jane alipotoka moja kwa moja Ibra akamuomba pembeni ili azungumze nae ambapo alisogea na Ibra kwaajili ya mazungumzo,
“Jane samahani kilichotokea kati yako na mke wangu naomba umzoee tu”
“Mimi sina tatizo nae ila sikumuelewa tu alivyokuwa akifoka na kuonyesha kunishangaa”
“Pole sana mdogo wangu, unajua nini huyu Sophy huwa ana matatizo ya kusahau anaweza fanya jambo kisha akasahau halafu muda mwingine anasahau muda sababu ya kusinzia naomba umsamehe sana”
“Mmh mi sikujua hilo, ila kama ana tatizo la kusahau basi sasa naweza kuelewa kwanini alikuwa akifoka vile. Nimemsamehe na wala sina mashaka nae”
“Kama umemsamehe ni vizuri, na usisite kuja kuendelea kututembelea tafadhali maana pale nyumbani huwa anabaki mwenyewe na upweke.”
“Ilimradi nimeshagundua tatizo lake basi haitanisumbua tena”
Kisha Ibra akamuita mkewe na kuwapatanisha ambapo Sophia na Ibra wakaaga baada ya lile tukio na kuondoka, huku Sophia akimsisitiza Jane aende kumtembelea tena kesho yake.
Walipoondoka tu, mama Jane akamuita binti yake ili kujua kilichoendelea kwani haikuwa kawaida kwa Jane kufatwa vile nyumbani kwao.
Jane hakumficha mama yake, akamueleza kila kitu ambacho kimetokea siku hiyo.
“Mmh kwahiyo chakula alishapika akasahau na kukwambia wewe ukapike?”
“Ndio hivyo mama, maana alinipa maelekezo sijui nyama ipo kwenye friji niitoe kisha niipike na ndizi, kuingia jikoni hakuna nyama kwenye friji ila nilipofunua sufuria nakuta ndizi zilishapikwa tayari tena zimenona balaa dah kafanya nimeondoka bila hata ya kula hata kidogo.”
“Kama ndio hivyo basi kusahau kwake ni babkubwa maana mmh! Mtu unasahau kabisa kama ulishapika, ila ni bora mumewe anajua tatizo la mke wake.”
“Ndio, kaniambia nimchukulie kama alivyo sababu ni tatizo lake la kusahau”
“Mmh haya mwanangu ila siku nyingine uwe makini na maneno yake”
Jane akakubaliana pale na mama yake kisha akarudi zake ndani huku akiamini kuwa Sophia alipika zile ndizi ila amesahau kutokana na tatizo lake la kusahau.
Ibra na Sophia walipofika nyumbani moja kwa moja Ibra akakumbuka kitu,
“Aaah! Hata nimesahau kumshukuru Yule binti kwa chakula kitamu, kwakweli anajua sana kupika”
Sophia akamuangalia mumewe na kumuuliza,
“Inamaana anajua kupika kushinda mimi?”
“Mmh mke wangu jamani huo sasa ni wivu, mimi nimemsifia tu wala sijasema kama amekupita wewe. Hata hivyo hakuna anayekufikia wewe mke wangu kwa chochote wala lolote”
Sophia akatabasamu kwani hizi sifa alizopewa na mumewe zilimfanya ajisikie vizuri sana, kisha Sophia akainuka na kuelekea meza ya chakula halafu akamuuliza mumewe,
“Wakati tunaondoka hivi tulitoa vyombo mezani kweli?”
“Mmh mi sikumbuki ila mezani nilikuacha wewe halafu niakenda kukaa kwenye kochi kwani vipi?”
“Kwa kumbukumbu zangu sikumbuki kama nilitoa vyombo kwakweli ila naona vimeshatolewa je nani kavitoa?”
“Aah Sophia jamani unakoelekea mke wangu siko kabisa yani mmh wewe kila kitu kwako kipo nyuma mbele. Kuna mtu aliniambia kuwa wanawake wajawazito huwa na tabia ya kusahau kwakweli leo naamini maneno yake. Hebu njoo kwanza mke wangu tujadili mambo ya msingi. Leo nimerudi mapema hata huniulizi kwanini mapema ila kila muda unazuka na jipya sijui ndio maisha gani haya mke wangu.”
Sophia akaamua kusogea pale sebleni na kukaa na mumewe ingawa katika kichwa chake kilikuwa na maswali mengi sana ila aliamua kuyapuuzia kwa muda, kisha akamuuliza mumewe kuhusu kuwahi kurudi kwake,
“Eeh mbona leo umewahi kurudi sana?”
“Kwanza kabisa leo nilipokuwa kazini mawazo yangu yote yalikuwa juu yako kwani nilikuwa nikiwaza juu ya upweke ambao utakuwa nao. Ndiomana nimewahi kurudi ili nikuliwaze mke wangu.”
Sophia akatabasamu kwavile aliyapenda sana maneno ya mumewe ya kumbembeleza, kisha Ibra akaendelea kuongea,
“Halafu nimepata wazo mke wangu, kwanini tusiwe na msichana wa kazi humu akusaidie saidie”
“Msichana wa kazi! Wa nini mimi? Kwakweli huwa sina imani na hao wasichana wa kazi mume wangu jamani nisije nikaibiwa bure bora ufikirie jambo lingine”
“Uibiwe nini mke wangu?”
“Nitaibiwa wewe”
“Mmh yani huo wivu wako majanga loh! Basi itabidi ukamshawishi mdogo wako Tausi aje hapa au unaonaje?”
“Hapo sawa, basi tutapanga ili nikaongee na mama nije nae hapa huyo Tausi anisaidie saidie ukizingatia hasomi wala nini”
Wakakubaliana pale kisha Ibra akaamua kwenda kuoga kwanza kuondoa uchovu wa siku hiyo ambapo alipomaliza kuoga akamwambia na mke wake nae akaoge, Sophia akainika na kwenda kuoga ila alikuwa na mawazo mengi sana mule bafuni haswa kwa mambo ambayo yanamtokea halafu hayaelewi elewi, alikuwa akijiuliza vitu vingi sana bila ya kupata majibu.
Alipotoka bafuni alimkuta Ibra akiwa kitandani amejilaza ambapo Ibra alimuita mke wake huyu ili aende pale kitandani na wajumuike nae.
Sophia alisogea karibu na alipo mumewe ila alimuangalia tu na kufanya Ibra amuulize,
“Sophy mke wangu mbona wanitazama tu kama hujui nilichokuitia? Unajua nimekumiss sana mke wangu”
Kisha Ibra akamsogelea kwa karibu Sophia na kumkumbatia huku akimpapasa, iala Sophy alionekana kutofurahishwa kabisa na kumfanya Ibra amuulize kwa kumshangaa,
“Vipi Sophy mke wangu nini tatizo?”
“Sijisikii”
“Hujisikii kivipi?”
“Kwani mtu akisema hajisikii huelewi au?”
Halafu Sophia akainuka pale kitandani na kuelekea sebleni, kitendo hicho kilimfanya Ibra amshangae sana mke wake na moja kwa moja akafikiria kuwa ni mimba iliyomfanya awe katika hali ya namna ile kwani katika maisha yao ya kawaida haijawahi kutokea hata mara moja Sophia kuongea maneno ya vile wala kumbishia mume wake katika tendo lile.
Ibra alitulia tu pale chumbani akitafakari na kujiuliza kuwa imekuwaje kuwaje maana ilikuwa ngumu kwake kuelewa.
Sophia alienda sebleni na kukaa kwenye kochi ila alijikuta akijifikiria sana kwa alichomjibu mumewe na moja kwa moja kujiona kuwa ana makosa, kwanza alijishangaa pia kuweza kumjibu mumewe vile wakati hajawahi hata siku moja kumkatalia hata kama akiwa hajisikii kweli.
“Mmh hivi Ibra atakuwa ananifikiriaje jamani loh! Kwanini nimefikia hatua ya kumjibu vile wakati ni mume wangu? Nina kila sababu za kwenda kumuomba msamaha maana jambo nililofanya si la kawaida kwakweli.”
Hivyobasi akainuka na kurudi tena chumbani ila alipoingia chumbani na kumuangalia Ibra pale kitandani hakumuona na kufanya ajiulize kuwa Ibra ameelekea wapi maana kama angetoka basi lazima angepita pale sebleni na yeye angemuona ila hakumuona kutoka, akajaribu kuita ila hakuitikiwa na Ibra. Moja kwa moja akahisi kuwa huenda Ibra yupo chooni hivyo akaamua kwenda chooni kumuangalia, ila alipofungua mlango wa choo hapakuwa na mtu yoyote na kumfanya Sophia apatwe na hofu moyoni.
Akaamua kwenda kukaa tena kitandani, alifika na kukaa huku akiwa na mawazo mengi sana alijiinamia kwa muda kisha akaamua kujitupa kitandani huku akiwaza alipokwenda Ibra. Ila alipojitupa tu alishtuka sana kwani alihisi kuwa kuna mtu amemlalia, kitendo hicho kilimfanya Sophia ageuke kuangalia ni nini akamuona ibra akiwa amelala tena hana habari kabisa.
Kwakweli Sophia alishtuka zaidi kwani mwanzoni hakumuona huyu Ibra hapo kitandani, akashangaa imekuwaje kuwaje.
Akaamua kwenda kukaa tena kitandani, alifika na kukaa huku akiwa na mawazo mengi sana alijiinamia kwa muda kisha akaamua kujitupa kitandani huku akiwaza alipokwenda Ibra. Ila alipojitupa tu alishtuka sana kwani alihisi kuwa kuna mtu amemlalia, kitendo hicho kilimfanya Sophia ageuke kuangalia ni nini akamuona ibra akiwa amelala tena hana habari kabisa.
Kwakweli Sophia alishtuka zaidi kwani mwanzoni hakumuona huyu Ibra hapo kitandani, akashangaa imekuwaje kuwaje.
Aliamua kumtingisha Ibra na kumuamsha ambapo Ibra aliamka huku akimshangaa Sophia kwa kumuamsha kwa nguvu vile,
“Yani kwa muda mfupi tu Ibra ndio umelala usingizi wa kiasi hicho? Kwanza niambie ulienda wapi?”
“Kwenda wapi kivipi?”
Ibra alikuwa akimshangaa mkewe, kisha Sophia akamueleza vile ambavyo yeye alikwenda sebleni na alivyorudi chumbani bila ya kumkuta pale kitandani na alipojaribu kumuita na kumuangalia sehemu mbalimbali bila ya kumuona na vile alivyofika pale kitandani na kushtukia kuwa amelala.
Kwakweli Ibra alijikuta akicheka tu huku akimuangalia mkewe mpaka Sophia akapata hasira na kumuuliza Ibra kwa ukali,
“Sasa kinachokuchekesha?”
“Jamani Sophia mke wangu kwakweli naona sasa hiyo mimba imeanza kukuendea kombo maana si kwa mambo unayoyafanya mmh!! Hivi inakuingia akilini kweli eti mimi usinikute hapa kitandani halafu urudi tena unikute, jamani aah! Mi nilikuwa nimelala hapa maana siwezi kubishana na wewe ukizingatia ushakataa ninachokitaka, ila uzuri ni kuwa natambua hali yako na ndiomana nikaamua kulala tu ila hilo swala lako la kutokuniona na kuniona ndio linanichekesha kwakweli”
Ingawa Ibra aliongea hayo ila ilikuwa ngumu sana kumuingia akilini Sophia ukizingatia ni jambo ambalo anajua wazi limetokea hata kama ikiwa ni kupoteza kumbukumbu basi si kwa staili ile.
“Sogea tulale mke wangu”
Ibra akamkumbatia Sophia na kumsogeza karibu yake ili wapate kulala kwani aliweza kuona kuwa mawazo ya Sophia hayakuwa sawa kwa muda huo.
Kulipokucha kama kawaida Ibra aliamka na kujiandaa kwaajili ya kwenda kwenye shughuli zake, kma kawaida yake akamuaga Sophia kuwa anatoka ila kabla hajatoka Sophia akamzuia kutoka na kufanya Ibra amshangae na kumuuliza,
“Mbona unanizuia Sophy?”
“Usiende kazini leo sitaki kubaki peke yangu”
“Jamani Sophy mke wangu kwa staili hii tutaendelea kweli? Tutapata wapi pesa kwa ajili yetu na mwanetu mke wangu? Kwanini uwe hivyo jamani!”
“Nisamehe Ibra ila sijisikii kubaki mwenyewe”
“Basi inuka twende kwakina Jane tumuombe urudi nae hapa na ushinde nae, tafadhali tufanye hivyo mke wangu maana kazi nayo ni muhimu pia kwenye maisha yetu haya”
Sophia akakubali juu ya hilo, kisha akainuka pale kitandani na kutoka pamoja na mumewe wakielekea kwakina Jane.
Walifika na kuwagongea hata mama Jane alishangaa kuwaona asubuhi yote ile pale nyumbani kwake, ikabidi watumia Kiswahili cha kumvutia ili aweze kum,ruhusu Jane kwenda muda huo na Sophia nyumbani kwake. Mama Jane alielewa na kwenda kumuamsha Jane kisha kumwambia kuhusu ujio wa wakina Sophia.
“Mmh mama asubuhi yote hii jmani?”
“Naelewa kama ni asubuhi mwanangu ila hawa ni majirani zetu inapaswa kuwa nao karibu.”
Jane akaamka na kutoka nje kisha kuwasalimia Sophia na Ibra halafu akawaambia akaoge kwanza ajiandae ndio aende, ila Sophia aksamuomba Jane,
“Beba tu nguo, twende ukaoge nyumbani Jane”
Jane akafikiria kidogo na kukubali, kisha akaenda kuchukua nguo na kutoka halafu wakaingia kwenye gari ya Ibra ambapo aliwaacha pale nyumbani kwake kisha yeye kuelekea kwenye shughuli zake.
Sophia na Jane waliingia ndani ambapo kabla ya yote Jane aliomba kuonyeshwa uwani ili aweze kuoga na kujisafisha, Sophia alifanya hivyo kisha nay eye akaenda kuoga maana hata yeye alikuwa bado hajaoga kisha walipomaliza wakaandaa chai na kunywa halafu wakaanza stori za hapa na pale ambapo kwanza kabisa Sophia alimuomba msamaha Jane kwa kile ambacho kilitokea.
“Usijali dada nimeshakusamehe”
Sophia akatabasamu ingawa kiukweli bado alikuwa na maswali mengi sana moyoni mwake kuhusu hali halisi ya maisha yaliyopo pasle.
Muda kidogo Jane alianza na stori zake,
“Basi bhana jana usiku nimesoma stori hiyo inatisha hadi nikaogopa kulala, yani usingizi ukachelewa kuja balaa ndiomana mpaka saizi nina usingizi”
“Yani wewe kwa stori zinazotisha hujambo, hivi unazipendea nini jamani? Mwenzenu stori ambazo hazina uhalisia wala huwa sizifagilii”
“Uhalisia upo dada, unajua mara nyingine mtu unaweza ukalala halafu ukaota ndoto mbaya sana na usipokuwa makini ile ndoto inakutokea kwenye maisha halisi”
“Sasa kuhusu ndoto mbaya unakuwaje makini hapo?”
“Unajua inatakiwa ukiota ndoto mbaya ukishtuka tu Sali ili Mungu akuepushe nay ale mabaya uliyoyaota”
“Mmmh ila Jane wewe unanifurahishaga sana, hayo mastori yako ya kutisha ndio yamekufundisha hivyo? Kitu kama kipo kipo tu hata mtu ufanye nini”
“Ila na wewe dada kwa kupinga sikuwezi mmh. Ila kwakweli nina usingizi sana, nataka nilale tu hapa hapa kwenye kochi.”
“Hakuna shida wewe lala tu”
Sophia alitulia akiangalia runinga huku Jane akiwa amejilaza kwenye kochi.
Wakati jane akiwa amelala hoi kabisa, Sophia akasikia kama vyombo vikilia jikoni na kumfanya ashtuke sana huku akisikilizia kwa makini, kadri alivyozidi kusikiliza ndivyo mlio wa vyombo ulivyozidi kwakweli uoga ukamshika na kumfanya amshtue Jane kutoka usingizini ambapo Jane alishtuka sana huku akimuangalia Sophia kwa mshangao.
Sophia akamuuliza Jane kwa uoga flani hivi,
“Umesikia hiko?”
Ila muda huo ile sauti ya vyombo haikusikika tena na kumfanya Jane azidi kumshangaa Sophia kwavile yeye hakusikia kitu chochote kile.
“Sisikii chochote”
Sophia akakaa kimya kwa muda na kupumua kwa nguvu kanakwamba kitu ambacho kilikuwa kimetokea kilikuwa kikubwa sana, kisha Jane akamuuliza
“Kwani kulikuwa na kitu gani kikilia?”
Sophia alijikuta akishindwa kumjibu Jane kwani mdomo wake ulijawa na uzoito gafla.
Walikaa pale wakitazamana ambapo Jane aliamua tena kujilaza kwenye kochi ila Sophia aliogopa hata kwenda chooni kwa muda huo.
Mida ya mchana Jane alishtuka na kudai kuwa kwasasa usingizi umeisha na anaweza akafanya vitu vingine, kwavile Sophia aliogopa kwenda jikoni kutokana na mlio wa vyombo akaamua kumuomba Jane akapike chakula ili waweze kula.
“Mmh dada usije ukanifanyia kama mambo ya jana!”
“Hapana siwezi kufanya hivyo”
“Haya ngoja niende huko jikoni, ila unataka nipike nini?”
“Kuna maini kwenye friji, uyachukue halafu upike na wali”
“Hakuna tatizo”
Jane akainuka na kuelekea jikoni ili aweze kuandaa hiko chakula, ila alipofika jikoni kama alivyoona jana ndivyo alivyoona leo kuwa sufurua zimefunikiwa jikoni, akasogea na kufunua akaona maini yakiwa yameungwa vizuri sana tena yakiwa bado yamoto, kisha akafunua sufuria lingine ambapo napo akaona wali ukiwa umepikwa vizuri sana.
Jane akatabasamu na kujiuliza zaidi kuhusu tatizo la Sophia,
“Yani anapika mwenyewe halafu anasahau, basi hapo nikienda kumwambia mbona umeshapika atashtuka sana bora leo nisimwambie. Ngoja nirudi nimwambie vinachemkia nione kama anaweza kukumbuka kuwa ni yeye mwenyewe ndio alipika”
Kisha Jane akatoka jikoni na kwenda sebleni ambapo alimwambia Sophia kuwa ameacha vinachemkia, akamuona Sophia akipumua kidogo kwavile aliona kuwa siku hiyo hakuna maajabu yaliyotokea halafu wakaendelea kupiga stori mbili tatu ambapo Jane alimuuliza Sophia kuhusu swala lake la kupoteza kumbukumbu,
“Hivi tatizo lako la kupoteza kumbukumbu lilianza lini dada?”
“Tatizo la kupoteza kumbukumbu! Mi sina tatizo la kupoteza kumbukumbu”
Jane akacheka kisha akasema,
“Ama kweli mgonjwa huwa hajijui, yani dada hujui kabisa kama una tatizo la kupoteza kumbukumbu?”
“Sina hilo tatizo Jane, niamini jamani hilo tatizo sina kabisa”
“Haya basi ngoja nikusimulie kitu, kuna stori moja nilisoma kuhusu misukule yani unaweza ukaishi na misukule ndani bile kugundua”
Sophia akashtuka kidogo na kumuuliza Jane,
“Kuishi nayo kivipi”
“Unaweza ukashangaa unakaa kwenye nyumba labda umepanga kumbe mwenye nyumba ana misukule yake basi ukikaa unashangaa kama mtu kapita halafu humuoni huyo mtu kumbe ndio hiyo misukule”
“Uwiii mbona yanatisha hayo mambo!”
“Pole dada nilisahau kama hizi stori huzipendi”
“Kweli sizipendi ila ngoja kwanza, mtu unawezaje kugundua kama misukule ipo ndani na unawezaje kuiepuka?”
“Ila dada wewe si ulisema kuwa haya mambo ni ya kufikirika halafu hupendi stori za kufikirika, naomba niishie hapo, au umesahau kama ulisema kuwa hakuna misukule duniani ni stori tu wanazitunga”
Kisha Jane akainuka na kuelekea tena jikoni huku akiwa amemuacha Sophia akiwa na maswali mengi sana. Cha kwanza aliwaza uwepo wa misukule na matukio ambayo huwa anayaona kwenye ile nyumba kwani kwa kifupi yalikuwa yakimstaajabisha.
Jane akarudi tena na kumwambia kuwa ameshaandaa chakula mezani ila Sophia alijikuta akitaka kufahamu mengi sana kuhusu hiyo misukule na kujikuta akimuuliza maswali Jane ambapo jane akamuomba wakaulizane maswali hayo wakati wanakula.
Sophia alielekea mezani na kujiwekea chakula huku Jane nae akiwa amejiwekea cha kwake kisha Sophia akamuuliza tena Jane ila Jane bado alimpa masharti.
“Si vyema kuongea wakati wa kula dada, inatakiwa tumalize kwanza kula halafu ndio tutaendelea na maongezi”
Walikuwa wakila pale ila kichwa cha Sophia kilijawa na maswali mengi sana.
Walipomaliza kula jane alipeleka vile vyombo vyote jikoni kisha wakarudi kukaa sebleni ambapo Sophia akaanzisha tena maswali yake,
“Tafadhali Jane naomba unijibu maswali yangu”
“Haya niulize sasa nikujibu”
“Je misukule inaweza kufua nguo?”
“Kufua nguo! Mmmh! Sijui labda mwenye ile misukule akiiongoza”
“Sasa misukule inaweza kufanya vitu gani?”
“Mi ninachojua misukule inaweza ikala chakula chako ndani, huwa inapelekwa kulima nadhani hata mwenye misukule akiamua kuwa iwe inafua inaweza kufanya kazi hizo maana wale ni binadamu wa kawaida ila tu huwa wanaondolewa ufahamu”
“Basi niambie mtu unawezaje kujua kuwa unaishi na misukule na vipi unaweza kuiepuka?”
“Kuhusu kuishi nayo unaweza kugundua kama kukuta vitu vimefanyika ndani ndivyo sivyo ila kuiepuka sijui maana mi mwenyewe ile stori sijaimalizia”
“Mmh je misukule inaweza ikamdhuru mtu?”
“Misukule haina ufahamu dada, sidhani kama inaweza ikamdhuru mtu”
Sophia akawa kimya kwa muda ambapo Jane akaendelea kuongea,
“Kweli leo nimeamini kuwa kumbukumbu zako huwa zinapotea maana nakumbuka ulivyonikanusha kuhusu hizi stori halafu leo wewe ndio umekuwa wa kwanza kutaka kujua undani wake mmh kweli dada unasahau sana”
“Unajua nini Jane, kiukweli hizo stori mimi huwa siziamini ila kuna mambo flani hivi yananichanganya ndiomana nikakuuliza ila siku moja utayajua tu”
Wakiwa wanazungumza pale, Ibra nae akawa amerudi kutoka kwenye mihangaiko yake ambapo Sophia alimkaribisha mumewe na moja kwa moja akaenda kumpakulia chakula kwanza huku Ibra akimshukuru sana jane kwa kuweza kushinda na mkewe kwa muda wote toka ameondoka,
“Usijali kaka, mi nipo pamoja nanyi”
Sophia akamkaribisha mumewe mezani ambapo Ibra alikula chakula kile huku akikisifia sana kuwa ni kitamu, kisha akauliza
“Nani kapika?”
“Jane huyo”
“Khee huyu mtoto anajua kupika sana”
Sophia akatabasamua tu, baada ya Ibra kumaliza kula Sophia akatoa vile vyombo na kwenda kuviweka na vingine vichafu pale jikoni kisha akarudi sebleni ambapo Jane nae hakutaka kukaa zaidi kwani aliaga na kufanya Sophia na mume wake kuinuka na kumsindikiza ila hawakumfikisha hadi kwao, kisha Ibra akamuomba Jane uwepo wake kesho yake tena.
“Tafadhali Jane naomba kesho tuje tukufate tena ushinde na mke wangu”
“Hakuna tatizo kaka”
Kisha wakarudi na kumuacha Jane nae akielekea kwao.
Walirudi ndani huku Sophia akifurahia uwepo wa mume wake,
“Kwakweli nafurahi siku hizi unawahi sana kurudi”
“Lazima niwahi kurudi mke wangu maana siwezi kukuacha na hali yako hiyo”
Sophia akamuacha mumewe akaoge kisha yeye akaelekea jikoni ili aoshe vyombo na aweze kukaa na mumewe kuzungumza mawili matatu.
Alipoingoia jikoni alishangaa sana kuona vyombo vyote vimeoshwa na vimeshapangwa kabatini kwakweli alijikuta akipiga kelele na kumfanya Ibra amfate kwa haraka sana,
“Vipi Sophia nini tena mke wangu?”
“Misukule”
“Misukule! Misukule imefanyaje?”
Ibra alikuwa akimshangaa mkewe na kuangaza macho yake huku na kule kuangalia kama kuna chochote.
Alipoingoia jikoni alishangaa sana kuona vyombo vyote vimeoshwa na vimeshapangwa kabatini kwakweli alijikuta akipiga kelele na kumfanya Ibra amfate kwa haraka sana,
“Vipi Sophia nini tena mke wangu?”
“Misukule”
“Misukule! Misukule imefanyaje?”
Ibra alikuwa akimshangaa mkewe na kuangaza macho yake huku na kule kuangalia kama kuna chochote.
Ila Ibra hakuona chochote mule jikoni na kumuuliza tena mke wake,
“Sophy, misukule kivipi?”
“Misukule imeosha vyombo na kuvipanga”
“Misukule imeosha vyombo na kuvipanga? Wee Sophy akili yako iko sawa kweli? Unajua misukule wewe?”
Ibra alikuwa akimshangaa mke wake na kumuona kama ni mtu aliyekuwa akichanganyikiwa maana mambo aliyokuwa akiongea hayakuwa na mantiki yoyote ile.
Aliamua kumuinua mkewe pale chini na kuelekea nae chumbani kwani alikuwa kama kapigwa na bumbuwazi.
Walipokuwa chumbani sasa, Ibra aliamua kumuacha kwa muda kitandani kisha yeye kwenda kuelekea kuoga kama alivyokuwa amepanga.
Kwakweli Sophia hakujielewa kabisa na kuhisi hadithi za Jane za kuhusu misukule zikianza kumuingia akilini vilivyo na kuona ni kweli ile nyumba yao ina misukule maana kila akiangalia yale matukio kengele ya hatari ndivyo ilivyozidi kulia katika ubongo wake.
Wakati akiwaza hayo akasikia kama mlango wa sebleni ukifunguliwa na kufungwa kanakwamba kuna mtu kaingia au katoka ila akajiuliza kuwa itawezekanaje ikiwa alishafunga mlango huo wakati wanaingia ndani, kwakweli uoga ulimshika mpaka pale Ibra alipotoka bafuni kuoga na kumkuta mkewe akiwa amejikunyata.
Ibra alimfata mkewe na kukaa naye karibu kisha akamkumbatia na kumuuliza kwa ukaribu zaidi,
“Kwani nini tatizo mke wangu? Unajua Napata shida sana kukuelewa!”
“Ibra hata mimi sielewi kwakweli yani sielewi kabisa kabisa”
“Unajua kwangu inakuwa ngumu sana kwasababu sijawahi kuishi na mwanamke mjamzito maana inawezekana haya ni mambo ya kawaida kwa wajawazito ila mimi sielewei kwakweli. Inabidi unifafanulie mke wangu kuwa ni mambo gani yanakusibu au ni vitu gani unaviona ili nijue tunaanzia wapi kupata ufumbuzi”
“Tatizo Ibra nikisema huniamini, hebu sikia tulitoka hapa tumeenda kumsindikiza Jane ila kulikuwa na vyombo vichafu jikoni, tumerudi ili nikavioshe nakuta vyote vimeoshwa wakati humu ndani tupo mimi na wewe tu. Nimekaa hapa nasikia mlango wa sebleni ukilia sasa hayo mambo yanamaana gani mume wangu?”
“Mmh kama hayo mambo ni ya kweli basi kuna makubwa”
“Mi nahisi kuna misukule humu ndani”
“Hebu Sophia tusiongelee hizo habari maana usiku huo unakuja tutashindwa kulala”
Kisha Ibra akamuomba mkewe ajiandae ili angalau watoke waende mahali wapate kubadilisha hali ya hewa.
Sophia alipomaliza kujiandaa, yeye na mumewe wakatoka mule ndani na kufunga milango vizuri kabisa kisha wakapanda kwenye gari yao na moja kwa moja Ibra akaelekea na mkewe hotelini ili kutimiza lengo lake la kubadilisha hali ya hewa ila kichwani alikuwa na maswali mengi sana ambayo hayakuwa na majibu kwa wakati ule.
Kikubwa alichowaza ilikuwa ni kama Sophia anaongea ukweli kuhusu yale matukio basi lazima kuna kitu kinaendelea kwenye ile nyumba yao, pia akawaza kuwa kama ni kweli basi huenda majirani zao ni wachawi.
Sehemu Ya 3
Kulipokucha kama kawaida Ibra alijiandaa na kwenda kwenye shughuli zake, kisha Sophia nae akaamka na kujiandaa kisha akelekea kwakina Jane kwani alishajipanga kutimiza anachokitaka kwa siku hiyo.
Kama alivyoambiwa na Yule mganga yani alipokaribia tu kwakina Jane akatafuna kile kijani kisha akafika na kumuulizia Jane ambapo walienda kumuitia, Jane alitoka na kushangaa aliyemfata pale kwao kisha akamsikiliza lengo lake ambapo Sophia alimwambia kuwa anamuomba nyumbani kwake. Jane alitaka kukataa ila akakumbuka maneno ya Ibra kuwa yeye ndio faraja ya huyu Sophy mke wa Ibra kwahiyo Jane akakubali na kumwambia kuwa akioga tu ataenda.
Akaagana nae pale, kisha Sophia akawa anarudi nyumbani kwake huku akifurahia kuhusu Yule mganga kuwa ni kiboko kwani hakutegemea kama Jane angekubsali kirahisi namna ile.
Sophia alipofika tu kwake, akachukua ile dawa na kuinyunyuzia mlangoni kisha akaenda jikoni na kuweka juisi kwenye glasi kisha kuweka na ile dawa ili Jane akija tu ampe juisi hiyo.
Muda kidogo Jane nae aliwasili ambapo cha kwanza kabisa alipofika mlangoni alishangaa kuona kama unga unga na kumuuliza Sophia,
“Dada ni nini hiki mlangoni?”
“Wewe pita tu kuna vitu vilianguka”
KwakweliSophia hakupendezwa kabisa na hili swali la Jane kwani alizidi kujidhihirisha kuwa ni mchawi, Jane aliingia ndani na kukaa pale sebleni kisha Sophia akaenda jikoni kumletea ile juisi.
Wakati Sophia akitoka jikoni na ile juisi akamshangaa Jane akiwa ametulia kabisa akiangalia Tv ambayo yeye hakuiwasha kwavile alikuwa akimsubiri fundi atakayeletwa na mumewe, kwahiyo Sophia alimuuliza Jane kwa mshangao,
“Kwanini umeiwasha hiyo Tv Jane ni mbovu”
“Sijaiwasha dada, nimeshangaa imewaka tu”
Sophia alimuangalia Jane kwa jazba sana tena kwa mshangao mkubwa.
Muda kidogo Jane nae aliwasili ambapo cha kwanza kabisa alipofika mlangoni alishangaa kuona kama unga unga na kumuuliza Sophia,
“Dada ni nini hiki mlangoni?”
“Wewe pita tu kuna vitu vilianguka”
KwakweliSophia hakupendezwa kabisa na hili swali la Jane kwani alizidi kujidhihirisha kuwa ni mchawi, Jane aliingia ndani na kukaa pale sebleni kisha Sophia akaenda jikoni kumletea ile juisi.
Wakati Sophia akitoka jikoni na ile juisi akamshangaa Jane akiwa ametulia kabisa akiangalia Tv ambayo yeye hakuiwasha kwavile alikuwa akimsubiri fundi atakayeletwa na mumewe, kwahiyo Sophia alimuuliza Jane kwa mshangao,
“Kwanini umeiwasha hiyo Tv Jane ni mbovu”
“Sijaiwasha dada, nimeshangaa imewaka tu”
Sophia alimuangalia Jane kwa jazba sana tena kwa mshangao mkubwa sana kwani aliona akimtungia maneno tu muda ule, akamuuliza tena
“Inamaana imejiwasha?”
“Mi sijui, nilihisi labda umeme ulikatika na ukasahau kuizima sasa ndio umerudi na kuwaka moja kwa moja”
“Haiwezekani yani ni haiwezekani kabisa, hata hivyo karibu juisi”
Sophia akampatia Jane ile glasi ya juisi, ambapo Jane nae aliipokea na kushukuru.
Sophia alikaa kwenye kochi huku akimsubiria Jane anywe ile juisi ila Jane alikuwa kimya kidogo huku kaishikilia ile juisi na kumfanya Sophia amuulize,
“Mbona hunywi sasa!”
“Nakunywa dada, nilikuwa naiombea kidogo”
“Kheee inamaana huniamini?”
“Hapana dada, nakuamini sana tu ila mama jana alinifundisha vitu vingi sana na ndiomana saivi nataka kuanza tena kumrudia Mungu”
“Kwahiyo amekufundisha kutokuamini watu na kuombea kila wanachokupa?”
“Usinifikirie vibaya dada ila jana kuna makala nilisoma ilinifundisha vitu vingi sana ndipo nilipomuuliza mama nae akanielezea mambo mengi, tunatakiwa kukabidhi kwa Mungu kila kitu tunachofanya. Kama ile juzi ningemuomba Mungu aniongoze basi yasingenitokea yote yale yaliyonitokea ila kwavile nilitumia akili zangu za kibinadamu ndiomana ikawa vile. Natakiwa kukabidhi kwa Mungu kitu chochote kile hata nilichokitengeneza mwenyewe”
Kisha Jane akanywa kidogo ile juisi ila alishusha glasi na kutoka nje na kuitema, kwakweli Sophia alimshangaa sana hata gadhabu yake ikazidi maradufu na kumfuata nje na kumuuliza kwa ukali,
“Yani unatema juisi niliyokupa! Kama ulikuwa hutaki si ungesema tu kwani ningekulazimisha jamani?”
“Dada jamani hebu shika na wewe uionje, hii juisi ni chungu wala sijaitema kwa kutaka”
Sophia alichukua ile juisi ila alishindwa kuionja kwavile alijua wazi kitu ambacho ameweka kwenye ile juisi, kisha akarudi sebleni na ile glasi ya juisi ambapo Jane nae alirudi pale sebleni ambapo ile Tv iliendelea kuonyesha kama kawaida.
Walipokuwa wamekaa Sophia akamuangalia tena Jane na kumuuliza,
“Inamaana hii juisi kweli ni chungu?”
“Hata wewe ionje dada ni chungu kweli labda ni kikombe”
“Toka lini juisi ya embe ikawa chungu?”
“Mi sijui dada ndiomana nimesema labda ni kikombe”
“Mmmh una mambo yako tu wewe na hata sio kwamba juisi ni chungu”
“Kama unabisha dada ionje na wewe uhakikishe nisemayo”
“Nionje ili nife!”
Jane akamshangaa sana Sophia maana juisi kaileta mwenyewe halafu yeye huyohuyo anakataa kuionja, moja kwa moja Jane akahisi kuna uwalakini kwenye ile juisi na kisha akamuuliza Sophia,
“Kwani dada umeweka nini kwenye hiyo juisi?”
“Unahisi nimeweka nini?”
“Mi sijui maana uliyetengeneza ni wewe”
“Sijaweka chochote”
“Basi labda maembe uliyotengenezea yalikuwa mabovu”
“Unayajua maembe mabovu wewe au unaongea tu”
“Dada usipaniki tafadhali”
Mara Tv ikajizima tena na kufanya watazamane ambapo moja kwa moja Jane alihisi kuwa umeme umekatika,
“Mmmh umeme umekatika nini?”
“Umeme ungekatika friji lingeendelea kuunguruma?”
“Khee dada mbona unaongea kwa hasira hivyo jamani! Mi nimeuliza tu”
“Si nilishakwambia kuwa hii Tv ni mbovu sasa maswali gani unauliza hayo”
“Basi yaishe dada”
Mara mlango ukagongwa na aliyeingia alikuwa ni Ibra, ila alishangaa uwepo wa Jane mahali pale kuwa imekuwaje kuwaje hata ikawa rahisi sana kwake kusahau kilichotokea juzi. Ila alimkaribisha vizuri tu,
“Oooh Jane nafurahi sana kukuona upo hapa na mke wangu, kwakweli karibu sana”
“Asante ila mimi ndio napaswa kukukaribisha wewe sababu ndio umenikuta”
“Ni kweli nimekukuta ila hapa ni kwangu na nina haki ya kukukaribisha”
Ibra akakaa kwenye kiti ila macho yake yalienda mezani moja kwa moja ambapo aliona glasi ya juisi, ila alishangaa kitu na kuuliza kwa mshangao,
“Kheee hii juisi nyekundi ni juisi gani?”
Sophia na Jane kwa pamoja walijikuta wakiiangalia ile juisi ambapo Jane nae aliuliza kwa mshangao,
“Mmh hii juisi si ilikuwa na rangi ya njano hapa, imekuwaje imebadilika?”
Sophia alizidi kushangaa tu bila kusema neon lolote kwani alihisi huenda ile dawa aliyoweka kwenye ile juisi ndio imeibadilisha baada ya kukaa kwa muda.
Ibra akachukua ile glasi ya juisi na kuiangalia kwa karibu ila alishtuka sana kuona kama vitu vikicheza cheza ndani ya glasi ile, ambapo aliiacha chini na kumwambia Sophia,
“Hebu angalia ndani ya hiyo glasi, hivi ni juisi kweli hiyo?”
Jane akadakia kujibu,
“Ndio ilikuwa ni juisi sema ilikuwa chungu”
Kisha na yeye Jane akachukua ile glasi kuangalia ila alichokiona kilimshtua zaidi na kumfanya aiachie ile glasi ambapo ilianguka chini na kupasuka, ila kilichotapakaa baada ya ile glasi kupasuka kiliwashtua wote kwani ilikuwa kama damu ya mtu imemwagika.
Ibra alikuwa wa kwanza kuuliza,
“Ni mambo gani haya jamani?”
Huku akiamini kuwa huenda maneno ya mke wake kuwa Jane ni mchawi ni ya kweli, alimuangalia Jsne na kumuuliza,
“Ni wewe uliyetengeneza hii juisi?”
“Hapana, mi mwenyewe nililetewa na dada ili ninywe”
Ibra akamuangalia kwa makini mkewe ila Sophia hakuweza kusema chochote kwani alikuwa akitetemeka tu na ukizingatia alikuwa anajua kinachoendelea, Ibra aliamua kumuuliza mkewe sasa
“Unaweza kuniambia hii juisi imekuwaje?”
“Sijui imekuwaje ila nitakueleza ninavyojua mimi ila naomba Jane aondoke na tuongee kifamilia”
Jane hata hakutaka kuangaliwa na kuambiwa ondoka kwani pale pale aliaga na kuondoka zake.
Ndani ya nyumba alibaki Sophia na mumewe Ibra sasa ambapo Ibra alihisi kuna kitu mkewe anakijua na kumfanya amkazanie ili amueleze kuwa ilikuwaje,
“Naomba unisamehe mme wangu, nimefanya yote haya ili kuiokoa familia yetu”
“Kuiokoa familia yetu kivipi?”
“Kwanza niahidi kuwa utanisamehe”
“Sasa Sophy nisipokusamehe wewe nitamsamehe nani? Wewe ndio mke wangu, mama wa watoto wangu na hapo ulipo umebeba mwanetu tumboni mwako hivi naanzaje kutokukusamehe kwa mfano”
“Ngoja nikueleze basi ilivyokuwa”
“Wewe nieleze tu hata usiwe na wasiwasi”
Ikabidi Sophia amueleze Ibra mlolongo mzima wa yeye na Siwema kwenda kwa mganga wa kienyeji hadi yeye kupatiwa dawa ya kumdhuru Jane ambapo ndio aliiweka kwenye hiyo juisi.
“Mmmh kama ndio hivyo basi hiyo dawa ni kiboko mke wangu, ila siku nyingine usirudie tafadhali. Kwanza nikuulize una ushahidi gani kuwa Jane ni mchawi?”
“Mume wangu ni kutokana na mambo yanayotokea humu ndani, na mganga kasema kuwa yote yanasababishwa na huyo Jane”
“Najua wewe habari za waganga huzijui vizuri mke wangu ila kwavile umeamua kujihusisha nao basi utazijua mwanzo mwisho, ila siklu nyingine usijaribu hiki kitu. Hivi mfano Jane angekufa humu ndani tungempelekaje kwao mke wangu? Tena ushukuru Mungu huyo Jane ana imani zake na Mungu wake maana angekunywa tu hiyo juisi iliyogeuka kuwa damu basi kungekuwa na habari nyingine muda huu. Tafadhali mke wangu kuwa makini sana, Siwema atakupoteza wewe”
Kisha Ibra akaenda kuchukua tambara ili kuweza kufuta pale chini ila alikuta ile damu imeganda kamavile iliwekwa kwenye barafu kwahiyo alifanya kazi ya kuigandua na kwenda kuitupa nje kisha akapasafisha kabisa pale na kutulia huku akimuangalia mkewe ambaye alikuwa kimya tu kwa muda huo. Ibra aliamua kumuuliza tena,
“Je hiyo dawa bado unayo?”
“Hapana, niliitoa yote kama nilivyoelekezwa na Yule mganga”
“Ninachokuomba mke wangu usije ukarudia tena tafadhali, saivi kuwa makini na hiyo mimba. Kwanza vipi kuhusu kuanza kliniki?”
“Nitaanza tu mume wangu hata usijali”
“Basi ukiona imefika kipindi muafaka cha kuanza useme ili niwe nakupeleka”
“Sawa hakuna tatizo”
Wakati wakiendelea kuongea, mara kidogo Tv ikajiwasha kama kawaida na kumfanya Ibra ashtuke na kumuuliza mkewe kwa mshangao,
“Si nilisema hii Tv isiwashwe jamani Sophy na jana nikaizima hadi kwenye soketi imekuwaje tena?”
“Huyo Jane wako unayemtetea ndio aliyeleta tena mauza uza ya hiyo Tv maana hata mimi nilimshangaa akajitetea kuwa imejiwasha”
Ibra akapata hasira na kuinuka kisha akaenda kuchomoa nyaya zote za Tv ili kusiwe na muunganiko wowote kati ya umeme na Tv kisha akamuomba mkewe kuwa waende chumbani.
Sophia akainuka huku akiambatana na mumewe na kuelekea pamoja chumbani, ila walipofika tu cha kwanza kabisa Ibra alimuuliza mkewe
“Eeeh leo tunakula nini”
“Hata sijui maana sijapika”
“Kwahiyo mawazo yako leo ilikuwa ni juu ya kumuangamiza Jane tu hata ukasahau lishe dah! Basi jiandae twende hotelini tukale”
Sophia alijiandaa kisha wakatoka pamoja na mumewe kuelekea hotelini kula.
Walifika hotelini na kuagiza chakula, kisha kilipoletwa walianza kula na kumaliza ambapo Ibra alifurahi kwakweli maana mkewe siku hizi alikuwa na matatizo kiasi kwahiyo alihisi labda atatapika au atakataa kula hapo hotelini, kisha akamuuliza Sophia,
“Vipi leo hujajisikia voibaya mke wangu maana umeweza kula hapa hotelini hadi nimeshangaa”
“Kwasababu tumebadilisha hoteli ndiomana nimeweza kula, lile li hoteli lako silitaki kabiosa”
“Ila si nilishasema kuwa ile hoteli hatutaenda tena kutokana nay ale wanayotutegeshea njiani, kwakweli hata mimi ile hoteli siitaki tena na kama nilivyoahidi haitokuja kutokea tena niende kwenye ile hoteli”
“Hapo sawa mume wangu maana hoteli zingine zimekaa kiushirikina tu”
“Vipi tubebe chakula kingine twende nacho nyumbani?”
“Mmh hapana jamani maana kama mimi hapa nimeshiba balaa, kesho nitapika tu”
“Basi turudi nyumbani sasa”
“Labda tununue juisi maana si unajua hata usiku haujaanza kuingia vizuri”
“Lakini si ulitengeneza juisi wewe mpaka ukampa Jane!”
“Aaah achana na ile juisi bhana, kwanza tukirudi naimwaga yote”
Ibra akacheka tu kisha wakamuita muhudumu na kumuagiza juisi ya boksi na alipoleta walibeba na kuelekea kwenye gari yao kwa lengo la kurudi nyumbani.
Wakiwa njiani ndani ya gari, wakakatisha kwenye moja ya kituo cha daladala ila gafla wakasikia sauti ikiita kwa nguvu jina la Sophia na moja kwa moja wakahisi kuwa huenda kuna mtu kwenye kituo cha daladala anayemfahamu Sophia kwahiyo Ibra akasimamisha gari yao ili kumuangalia mtu huyo. Ila gafla mlango wa nyuma wa gari yao ukafunguliwa na akaingia mtu, ambapo kwa pamoja waligeuka na kumuangalia mtu huyo, wakamuona ni Yule mtoto ambaye huwa wanamkuta njiani akiwafanyia vituko cha kwanza walishangaa sana.
Kwakweli Ibra alipatwa na hasira ya gafla kisha akashuka kwenye gari na kwenda ule mlango wa nyuma na kuufungua ambapo alimtoa mtoto huyo kwa ghadhabu kubwa sana kisha akamrusha nje ila Yule mtoto hakuanguka wala nini kanakwamba Ibra alimuondoa na kwenda kumsimamisha ila bado Ibra hakushangazwa na lile swala bali alirudi kwenye gari na kuondoa gari yao kwenye lile eneo huku akiwa amechukia sana kwani chanzo cha wao kubadilisha hoteli na njia ni huyo huyo mtoto.
Walipofika nyumbani, kabla hata ya kushuka kwenye gari ili afungue geti, wakaona kitu kama nyoka kikimalizikia kuingia ndani kwao kwa kupitia chini ya geti ila waliona mkia tu ambapo Sophia ndio alikuwa wa kwanza klushtuka na kumwambia mumewe,
“Mmh sio nyoka Yule?”
“Hata mimi nimeona kama nyoka vile”
“Duh mbona makubwa!”
Ikabidi washuke wote na kuingia kwa tahadhari ili kama ni nyoka basi wajue cha kufanya kabla ya kuingiza gari ndani, ila walipoingia tu getini waliona nyoka mkubwa akiwa amejiviringisha pembezoni mwa mlango wao wa kuingia ndani kanakwamba anawasubiria kuwa waingie nae.
Ikabidi washuke wote na kuingia kwa tahadhari ili kama ni nyoka basi wajue cha kufanya kabla ya kuingiza gari ndani, ila walipoingia tu getini waliona nyoka mkubwa akiwa amejiviringisha pembezoni mwa mlango wao wa kuingia ndani kanakwamba anawasubiria kuwa waingie nae.
Kwakweli hapakuwa na mwenye ujasiri kati yao wa kuweza kuendelea mbele, Ibra alimuangalia mkewe na kumuuliza,
“Tutafanyaje sasa?”
“Wewe ni mwanaume unatakiwa ujue cha kufanya”
“Yani uanaume kwa joka lote lile, mbona hunitakii mema mke wangu!”
“Sasa tutafanyaje?”
“Nadhani tuondoke tukatafute hoteli ya kulala kwa leo, lile joka tushughulike nalo kesho maana giza nalo hilo limeshaingia, hakuna namna hapa. Tutampata nani muda huu wa kutusaidia kulimaliza joka kubwa vile?”
Ikabidi wakubaliane kufanya hivyo maana haikuwa kitu rahisi kwa wao kupambana na lile joka, na kwa jinsi giza lilivyoingia haikuwa rahisi kusema utatafuta watu ili waweze kulimaliza joka lile.
Wakarudi nje na kupanda kwenye gari yao kisha kuondoka na kuelekea hoteli nyingine ya karibu ili kuangalia ustaarabu wa kupata chumba na kulala, kwa bahati nzuri walipata chumba kwenye hoteli ambayo walienda kwa muda huo.
Ila mpaka wanaingia ndani kila mmoja alikuwa na mawazo yake kuhusu lile joka waliloliacha nje ya nyumba yao, Sophia alimuuliza mumewe,
“Hivi joka kubwa kama lile linaweza kutokea wapi mjini hapa?”
“Kwakweli hata mimi sielewi Sophy maana sio hali ya kawaida kabisa ile, tena mjini hapa jamani kukutana na nyoka kama Yule mmmh!”
“Mi nahisi ametumwa Yule mume wangu”
“Inawezekana kabisa unayoyasema maaana si kitu rahisi kwa mjini hapa kukutana na nyoka mkubwa kiasi kile”
“Sasa unahisi tufanyeje?”
“Kwakweli hata sijui, nahisi kuchanganyikiwa tu”
“Mmmh mi nahisi kesho twende kwa da Siwema atupeleke kwa yule mganga ili aweze kutusaidia kwa hili, yani Yule nyoka ni wa kutumwa kabisa kabisa si jambo la kawaida mume wangu”
“Unafikiri nitabisha? Hata siwezi kubisha mke wangu, yani sibishi chochote kwakweli katika maisha yangu sijawahi kuona nyoka mkubwa kama Yule zaidi ya kuona kwenye sinema tu. Kwakweli haya ni makubwa, na kama ni uchawi basi ni uchawi wa wazi wazi kabisa yani”
Sophia alilidhika na kauli ya mumewe ya kukubali kwenda kwa mganga ili pia aweze kuwaeleza zaidi kuhusu Jane kwani alipenda mumewe nae aelewe kwa kina ubaya wa Jane anayemtetea kila siku.
Ibra aliona ni vyema wakapumzisha mawazo hivyobasi akamuomba mkewe walale tu ili kesho yake waamkie huko kwa Siwema, Ibra alimsogelea mkewe pale kitandani na kumkumbatia ili wapate kulala kwa pamoja. Na haikuchukua muda wote wawili wakajikuta wakipitiwa na usingizi.
Sophia alianza kupatwa na ndoto ambapo katika ndoto hiyo aliona lile tukio ambalo liliwapata wakati wakitoka hotelini kula ambapo aliona tukio zima la Yule mtoto alivyopanda kwenye gari yao na jinsi Ibra alivyomshusha kwa ghadhabu, ila kwenye hii ndotro alimuona huyu mtoto akiwaambia kuwa,
“Nitawakomesha”
Sophia alijikuta akishtuka kutoka usingizini huku jasho jingi likimtoka ambapo Ibra nae alishtuka huku akimshangaa mkewe na kumuuliza kuwa imekuwaje tena,
“Ndoto mume wangu”
“Ndoto! Ndoto gani?”
Gaf;la wakasikia mtu akiita jina la Sophia kwa nguvu toka nje ya hoteli hiyo ambapo Sophia alitaka kuitika ila Ibra alimziba mdomo na kumkataza.
“Usipende kuitika unapoitwa usiku, je unajua anayekuita ni nani na ana lengo gani na wewe?”
Sophia akahema kwa nguvu sana na kumuuliza mumewe,
“Hivi kwanza kuna mtu anayenifahamu huku?”
“Ndio ushangae sasa, hakuna anayekufahamu je utakuwa unamuitikia nani? Hata kama ukiwa mahali kwa watu wanaokufahamu tafadhali mke wangu usipende kuitika usiku, yani wewe chukulia kwamba anayeitwa sio Sophia wewe, chukulia kwamba kuna Sophia wengi sana ulimwenguni huenda kuna mmoja ndiye anayeitwa lakini sio wewe.Usiitike kabisa mke wangu”
Ile sauti ya kumuita Sophia nayo ilikazana na kumfanya Sophia kuingiwa na uoga ila mumewe alijaribu kuongea nae na kujitahidi kumtoa ile hali ya uoga ili awe katika hali ya kawaida kabisa na ahisi kuwa anayeitwa sio yeye.
Sauti ile iliita na kuita ila mwishowe ikafifia kabisa na kuwa kimya ila bado Sophia hakulala na kumfanya Ibra nae asiweze kulala kwani alikuwa akimpa maneno ya kumfanya mkewe asijisikie vibaya hata kidogo.
Kwavile hawakuwa na usingizi, ikabidi Ibra amuulize Sophia kuhusu kile alichokiota ambapo Sophia alimueleza lile tukio aliloliota na jinsi mwishoni alivyoambiwa na Yule mtoto, kidogo Ibra akapata wazo jipya na kumwambia Sophia,
“Unaona sasa, unakumbuka ule mchana ilikuwa sauti kama ile tuliyosikia ikikuita na tuliposimamisha gari ndio akapanda yule mtoto wa maajabu halafu saizi unaota tena na sauti inaanza kukuita tena, je huwezi kuona kuwa matukio yanawiana hayo!”
“Mmh halafu kweli mume wangu, bora umenikataza kuitika”
“Ndio hivyo, nadhani alitaka uitike ili awe na uhakika na chumba tulicholala. Ondoa mashaka mke wangu, tulale kwa amani sasa maana hawajui tumelala chumba kipi”
“Kwahiyo kama ni watu wabaya basi wamechemka”
“Tena wamechemka haswaaa”
Ibra akamkumbatia mkewe kisha wakaanza kuutafuta usingii na hatimaye wakalala tena.
Kulipokucha, waliamka mapema sana na kwenda kuoga ili kujiandaa kutoka pale hotelini, ambapo walitumia muda mfupi tu kujiandaa kwani hawakuwa na mengi ya kufanya.
Wakati wanatoka pale hotelini walishangaa kuna mahali watu wengi sana wamejaa na kufanya washuke kwenye gari yao na kwenda kushuhudia kuwa ni kitu gani kimetokea, waliposogea walishangaa kumuona binti mmoja pale chini akiwa ameuwawa kikatili sana ila muda mfupi tu walifika maaskari ambao ilionyesha walipewa taarifa kuhusu Yule mtu aliyeuwawa mbapo walimfunika na kumpakiza kwenye gari yao na kuondoka na baadhi ya watu kwa maelezo zaidi.
Ibra alikuwa akishangaa sana na kufanya nae aulize kwa kina kama sehemu hiyo huwa kuna matukio yoyote ya ajabu,
“Eti kaka, kwani hapa huwa kuna matukio ya hivi?”
“Kwakweli kaka haijawahi kutokea yani ndio mara ya kwanza na kila mmoja anashangaa maana hatujawahi kupatwa na matukio ya hivi halafu ubaya zaidi ni kuwa haijulikani ameuliwa na kitu gani”
“Mmh ndugu zake wamepatikana?”
“Kwakweli ilikuwa ngumu kumtambua ila kuna binti mwingine alipita hapa na ameweza kumtambua, hivyo amekimbia kwao kuwaita ndugu zake nadhani wakifika hapa itabidi waelekee moja kwa moja polisi au hospitali maana polisi wamewawahi kufika”
Muda kidogo walifika watu kama wamechanganyikiwa kabisa huku wakitaka kuonyeshwa huyo marehemu ambapo watu waliwapa maelekezo juu ya polisi waliofika na kuchukua ule mwili wa marehemu, kati ya wale watu alisikika mama mmoja akilia sana huku akionge,
“Mungu wangu jamani, naomba unisaidie asiwe binti yangu kweli jamani, yani Sophia wangu mimi hapana haiwezekani kabisa”
Wengine walimuita dereva wa bajaji aliyewapakiza wale na kuelekea nao kwenye kituo cha polisi ili waweze kuwahi kumuona huyo marehemu kabla hajapelekwa monchwari.
Sophia alimuangalia mumewe na kumuomba kuwa waondoke eneo lile kwani tayari alihisi kuchanganyikiwa baada ya kusikia kuwa Yule binti aliyeuwawa aliitwa Sophia pia, Ibra alimsikiliza mkewe na kisha wakaelekea kwenye gari ambapo moja kwa moja safari yao ilikuwa ni kwenda kwa Siwema na hakuna aliyeongea kwa muda huo.
Walipofika nyumbani kwa Siwema walimkuta akijiandaa kwaajili ya majukumu yake mengine, hata na yeye alishangaa ujio wao ila kwa haraka haraka akahisi kuwa huenda Yule binti ameshakufa kwahiyo ndio wamekuja kumpa habari, kwahiyo aliacha alichokuwa anafanya na kwa shauku kubwa alitulia kuwasikiliza kilichowapeleka mahali pale.
Sophia hakutaka kupoteza muda na moja kwa moja akaanza kumueleza yaliyotokea nyumbani kwao mpaka kuwafanya wao kuamua kuja kwake ili awapeleke huko kwa huyo mganga.
“Kheee mbona makubwa jamani! Je nah ii asubuhi huyo joka mmemuacha hapo mlangoni?”
“Hata nyumbani hatujaenda tena, usiku tumelala hotelini kwakweli hali ni mbaya, twende tu kwa huyo babu akatusaidie jamani”
“Basi ngoja nijiandae fasta fasta twende jamani maana haya mambo ni makubwa sana”
Siwema akaingia ndani, muda kidogo akapita tena Yule bibi ambaye alimwambia Sophia kuwa nyumba yake ni ya maajabu ila huyu bibi hakuwasalimia wala nini zaidi ya kumsemesha Sophia kwa kumwambia,
“Una bahati sana, ushukuru mumeo ana upeo mkubwa”
Sophia akamshangaa huyu bibi na kumuuliza kwa jazba,
“Kivipi”
“Usiku ule ungeitika wakati unaitwa basi sidhani kama muda huu ungekuwa hapa, ingawa umemuingiza pabaya mtu ambaye hakustahili kabisa”
“Sikuelewi ujue”
“Ni ngumu kunielewa kwasababu huwa naongea ukweli mtupu, mnatakiwa muwe karibu sana na Mungu lasivyo ile nyumba itawashinda”
“Nyumba na kuitwa usiku vina uhusiano gani?”
Kabla huyu bibi hajajibu, Siwema alikuwa kashatoka ndani na hapo hapo akaanza kumfokea Yule bibi kwa kumfukuza.
“Hivi wewe bibi una mpango gani na familia yangu? Si nilishakwambia usipite hapa nyumbani kwangu tafadhali ondoka mchawi mkubwa wewe tena ukome kukatisha hapa”
Yule bibi aliondoka bila ya kuongea chochote za ziada ingawa alionekana kuondoka akiwa amenyong’onyea, ikabidi Ibra nae amuulize Siwema kwa ukaribu kuwa Yule bibi ni vipi
“Yani Yule bibi ni mchawi hakuna mfano nawaamnbia halafu huwa anajifanya kila kitu anakijua, Sophia nilikwambia lakini usipende kumsikiliza huyu bibi hata nashangaa unavyomsikiliza jamani. Haya twendeni tusije tukachelewa foleni huko kwa babu”
Ikabidi Ibra afungue gari na wakapanda wakielekea kwa mganga wa kienyeji sasa.
Walipofika kwa mganga kama kawaida walikuta foleni kubwa tu maana mahali hapo palikuwa hapakosi watu hata mara moja.
Ila waliamua kuvumilia kwenye foleni hadi pale ilipofika zamu yao na kuingia ambapo mganga alikuwa amekaa na matunguli yake ila alikuwa kimya kabisa mpaka pale wao walipoanza kumueleza ambapo Siwema alianza kwa kumuomba msamaha kwanza,
“Babu tusamehe, nadhani tumekosea masharti na yametupata makubwa. Nje ya nyumba kuna nyoka mkubwa amefanya tushindwe kuingia ndani”
Huyu babu alianza kuongea kwa jazba,
“Mnajua nyie ni wajinga sana, tena wajinga haswaa yani mlishindwa kujiuliza kuwa kwanini ile dawa iliganda? Na nani aliwatuma muende kuitupa nje?”
Sophia nae akaanza kujitetea,
“Tusamehe babu, kwakweli hatukujua cha kufanya. Tusamehe tafadhari, tunaomba msaada wako”
“Ile dawa ni kali sana, mara nyingi mimi huitoa kwa lengo la kummaliza mchawi kwamaana ile dawa mtu akiinywa hawezi kuepuka kifo hata afanye kitu gani. Ile dawa ilitakiwa inywewe na muhusika ambapo angeinywa tu angeona habari yake kwanza wadudu wa tumboni wote wangekuwa wakubwa maradufu na hao ndio wangemuua kisha kuanza kumtoka hovyo hovyo yani kila sehemu ya uwazi kwenye mwili wake ingetoa wadudu ambao wangekuwa wakubwa sana na hakuna ambaye angeweza kukaa karibu na mwili wa marehemu huyo kisha wangeenda kumzika mapema sana. Sasa nyie mmeitupa pale nje kwenu tena ikiwa imekauka vile, ubaya wa ile dawa ikikauka tu harufu yake huwavutia viumbe jamii ya nyoka. Pale kwenu palikuwa na nyoka mdogo ambaye amekunywa ile dawa na mwisho wa siku ndio kawa vile. Hata mkirudi tena kumuona mtakuta amekuwa mkubwa zaidi ya mwanzo na huwa ni vigumu sana kuwaua nyoka waliokula ile dawa kwani ukiwasogelea tu hukimbilia kukudhuru kwanza”
Ibra alihisi kuchoka kabisa kwa maelezo haya, kisha akamuuliza Yule mganga,
“Sasa tutafanyaje babu?”
“Hapo dawa ni moja tu, tunatakiwa tutoe kafara ya ng’ombe mzima”
“Ng’ombe mzima?”
“Ndio ng’ombe mzima tutamchinja kisha damu yake tutaiweka dawa ambapo huyo nyoka ataifata hiyo damu kisha atajifia mwenyewe halafu tutachinja kondoo na mbuzi kwa lengo la kumfanya huyo nyoka atoweke kabisa”
Ibra alijikuta akiwa na mawazo lukuki maana hakujiandaa kwa hayo maswaibu ya kununua ng’ombe mzima wa kafara kisha kondoo na mbuzi. Yule mganga akawasisitizia kabisa,
“Hiyo kazi inatakiwa ifanyike leo, yani leo maana kadri huyo nyoka atakavyozidi kukaa ndio itakavyokuwa ngumu kumtoa”
“Basi babu ngoja tulete pesa kwaajili ya kununua huyo ng’ombe, mbuzi na kondoo”
Kisha wakatoka nje ambapo Ibra alikuwa na mawazo tu muda wote, alichukua simu yake na kuwapigia rafiki zake akiwaomba wamkopeshe pesa maana aliona akiitoa kwenye biazshara yake atafanya iyumbe mapema sana.
Kwa bahati nzuri aliowapigia na kuwakopa walimtumia pesa bila hata kukawia na kufanya ashukuru sana ili akakamilishe hilo zoezi na waweze kurudi kwao.
Ila Ibra alijikuta akimlaumu sana mkewe na kumuona kuwa ni mwanamke mpumbavu maana yote hayo kayasababisha yeye kwa kutaka kummaliza Jane na mwisho wa siku wamejikuta wakiingia kwenye gharama zisizo na maana.
Walienda kumtaarifu mganga kuhusu upatikanaji wa fedha kisha vile vitu vikaenda kutafutwa ili kujiandaa kwa hiyo shughuli ya kumtoa Yule nyoka nyumbani kwa Ibra.
Walipofanikiwa kupata vitu vyote, kwanza kabisa Yule ng’ombe alichinjwa pale pale nyumbani kwa mganga ambapo mganga aliweka damu ya Yule ng’ombe kwenye chupa na kuiweka na dawa.
“Yani hapa nataka tukifika tu kitu cha kwanza iwe ni kuimwaga hii damu maana haitakuwa vyema kwenda kumchinja ng’ombe mbele ya Yule nyoka.”
Kisha mbuzi na kondoo nao wakachinjwa ambapo damu yao iliwekwa kwenye chupa moja na kuchanganywa.
“Sasa akisha kunywa hii ya ng’ombe, atakufa kisha tutammwagia hii ya kondoo na mbuzi ili atoweke.”
Kisha wakaenda kupanda kwenye gari, Ibra, mganga, msaidizi wa mganga, Siwema na Sophia. Safari ilikuwa ni kwenda nyumbani kwa Ibra.
Walipofika nyumbani kwa Ibra, walishuka wote kwani Ibra alisimamisha gari yake nje kisha wakasogelea geti na kufungua kwa tahadhari, cha kushangaza sasa pale ambapo walimuacha nyoka jana walimkuta Jane amekaa tena akiwa hana habari yoyote.
Walipofika nyumbani kwa Ibra, walishuka wote kwani Ibra alisimamisha gari yake nje kisha wakasogelea geti na kufungua kwa tahadhari, cha kushangaza sasa pale ambapo walimuacha nyoka jana walimkuta Jane amekaa tena akiwa hana habari yoyote.
Kila mmoja alikuwa na mshangao juu ya lile, ambapo Ibra alimuita Jane kwa uoga flani kuona kama ni mtu au ni lile joka limejigeuza kuwa ni mtu, Jane nae alipoitwa aliitika na kuinuka pale kisha akaanza kuwasogelea ambapo Sophia akamwambia Jane kwa ukali
“Tafadhali Jane usitusogelee ila tuambie umeingiaje humu ndani?”
“Kuingiaje kivipi? Mi nimekuja nikakuta geti liko wazi nikaingia”
“Nyoka yuko wapi?”
“Nyoka? Nyoka gani?”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Unatuuliza sisi tena wakati palikuwa na nyoka hapo mlangoni”
“Sijaona nyoka kwakweli na nipo hapa kama saa moja iliyopita”
“Na ni nani aliyekwambia uje leo?”
“Sijaambiwa na mtu yeyote ila kuna vitu niliviota usiku ndiomana leo nikaja ili nikuulize”
Yule mganga nae aliwatazama Ibra na Sophia na kuwauliza kuwa Yule binti ni nani ambapo Sophia alimjibu kwa makini kabisa na kwa kujiamini,
“Huyo ndio Jane Yule mchawi maarufu”
Yule mganga akamtazama kwa makini Jane kisha akatikisa kichwa halafu akawageukia wakina Sophia na kuwaambia kuwa wamwambie Yule Jane aondoke kwani atawaharibia kazi ila Ibra akahamaki na kuuliza,
“Kazi gani sasa mganga wakati huyo nyoka hayupo tena”
“Nyoka hayupo tena? Unaweza kuangalia wewe kuwepo au kutokuwepo kwa nyoka?”
“Kama yupo yuko wapi sasa?”
Sophia akamuangalia mumewe kwa jazba na kumkazia macho kisha akamwambia,
“Ibra tafadhali acha kubishana na mtaalamu”
Kisha Sophia akamtazama Jane na kumwambia,
“Jane tunakuomba uondoke tafadhali”
Jane hakutaka kubishana nao na wala hakuongea lolote zaidi ya kutoka kwenye nyumba ile na kuondoka.
Sasa alibaki mganga na wakina Sophia ambapo Siwema nae akatia chumvi kuhusu Jane,
“Mmh halafu kale katoto kanaonekana ni kachawi haswaa yani haiwezekani kawe kanajiamini kiasi kile jamani”
“Umeona dada eeeh kale katoto sio ka kawaida kabisa”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Mganga akaanza kuongea kuwa inaonekana nyoka kuna mahali kajificha kwahiyo alitakiwa afanye jitihada za kumuita kwanza nyoka huyo ili amteketeze ila katika kumuita huyo nyoka alihitaji wachinje kuku wa kienyeji watatu ili apate nguvu ya kufanya hivyo.
Kwakweli Ibra alijiona akizidi kupoteza pesa kwa uzembe wa mke wake ila hakuwa na namna yoyote ya kufanya kwa muda huo. Ikabidi atoe pesa za hao kuku kisha Yule msaidizi wa mganga akaenda kuwanunua kuku hao.
Na baada ya muda kidogo Yule msaidizi alirudi na hao kuku watatu, kisha Yule mganga akawachinja wale kuku na kuanza kama kuita ila aliita na ukapita muda mrefu sana bila ya hilo joka kujitokeza wala nini tena haikuonyesha kama kulikuwa na dalili yoyote ya kuwepo nyoka katika eneo lile, ndipo Yule mganga alipowauliza tena jina la binti aliyetoka pale.
“Yule binti niliyesema aondoke anaitwa nani?”
“Yule anaitwa Jane”
“Jamani ngoja niwaambie ninachokiona”
Wote wakatulia kumsikilizia Yule mganga anachotaka kusema, kisha Yule mganga akaanza kuwaambia
“Nimekazana hapa kumuita Yule joka lakini hajatokea, mizimu yangu imenionyesha kitu ambacho kilikuwa kimeendelea mahali hapa. Swala ni kwamba Yule binti anaelewa kila kitu tulichokuja kukifanya hapa halafu yeye hataki tukifanye. Sasa jambo alilolifanya Yule binti ni kuondoka na lile joka kwa madai kwamba ataenda kulitumia kwenye shughuli zake. Ila nyie hata msihangaike nae, mimi nampa siku tatu tu za kuendelea kunusa harufu ya dunia hii. Kazi ya kummaliza sasa nitaifanya mimi mwenyewe baada ya kunisumbua hivi, nyie ngojeni baada ya siku tatu tu mtaitwa kwenye msiba wa huyo binti. Ngoja sisi tuondoke.”
Ibra akataka kuwapeleka ila waliomba kukodiwa usafiri wa kukodi ambapo ilimbidi Ibra afanye hivyo kisha Yule mganga na msaidizi wake wakaondoka.
Ibra akiwa pamoja na Sophia na Siwema wakafungua mlango wa ndani sasa na kuingia ndani ambapo walikaa sebleni huku wakimlaani Jane mwanzo mwisho, kwakweli Sophia alionekana wazi wazi akimchukia huyo Jane,
“Kwakweli naichukia ile siku ya kwanza kumfahamu yule mama Jane maana ndio kaniletea yote haya”
“Tena inaonyesha huyo mama ni mchawi kushinda mwanae maana haiwezekani mtoto awe mchawi halafu mama asiwe”
“Najuta kuwafahamu dada maana wamenieleleza balaa”
Ibra nae akachangia yak wake sasa,
“Mimi najuta kumfahamu huyo mganga wenu maana bila yeye hizi pesa zote ziizonitoka leo zisingenitoka”
Ikabidi Siwema atetee kuhusu hiyo mada,
“Usiseme hivyo shemeji, uhai ni bora kuliko mali”
Wakaongea ongea kisha Ibra akamuitia na huyo Siwema usafiri wa kukodi ambapo nae aliondoka kwa stahili hiyo.
Ndani walibaki wawili sasa huku Ibra akiwa na swala lake lile lile la kulaumu kuhusu mganga,
“Yani inamaanisha mganga ndio amekukera kiasi hicho mume wangu!”
“Amenikera sana, kiukweli Sophia zamani ulikuwa ni mwanamke mwenye akili sana na ulikuwa na uchungu na pesa zetu. Nakumbuka hukutaka kabisa tufanye mambo ya kijinga kwani muda wote ulikuwa ukiwaza maendeleo, sasa siku hizi umekumbwa na nini mke wangu? Hebu fikiria isingekuwa wewe kwenda kwa mganga kwa mara ya kwanza na kupewa ile dawa ya kumuangamiza Jane je yote haya yangetokea? Na je huyu mganga alikuwa na ulazima gani wa kuchinja Yule ng’ombe, mbuzi na kondoo nyumbani kwake halafu huku akaja na damu tu! Kwanini asingekuja kwanza eneo la tukio na kuona hali halisi ilivyo kisha ndio awachinje? Kwakweli mmeniingiza hasara sana ten asana hadi sina hamu na huyo mganga tena”
“Nisamehe mume wangu ila mimi nilifanya yote haya kwa lengo la kuikomboa familia yetu.”
“Hapa hata ulikuwa hukomboi ila ulikuwa unatudidimiza tuwe maskini tena. Yani siamini kabisa kama leo nimepoteza milioni moja na nusu kwa ujinga tu dah!”
“Pole mume wangu”
“Ngoja tusaidiane kupika tule tupumzike”
Kisha wakaenda jikoni na kuanza kuandaa chakula ambapo Ibra alipofungua friji aliona kuna nyama na kuchukua nyama hiyo na kuanza kuikatakata kisha kuibandika wakati huo Sophia alikuwa akishughulika na mchele ili waweze kupika kwa haraka.
Haikuchukua muda mrefu sana wakawa tayari wamemaliza kuandaa chakula na kwenda kukaa mezani kisha wakakaa na kuanza kula huku wakikisifia kile chakula kuwa kitamu sana kwani kilikuwa na ladha nzuri mdomoni na kilivutia kula tu.
“Yani siku hizi humu ndani tunapika chakula kuwashinda hata wa hotelini maana chakula chetu ni kitamu balaa”
“Basi tusiwe tunakula hotelini siku hizi maana mapishi yetu ni hoteli tosha”
“Kwani huu wali umeweka viungo mke wangu?”
“Wala, ni maji, mafuta na chumvi tu”
“Mmh unavyonukia na kunoga balaa”
“Kwakweli hata mimi nashangaa chakula kilivyokitamu dah”
Walikula huku wakisifia muda wote kisha walipomaliza Sophia alitoa vyombo na kwenda na mumewe chumbani kujimwagia kisha moja kwa moja kupumzika kwani walikuwa wamechoka sana na mizunguko ya siku hiyo ukizingatia ni tangu jana na lile varangati la nyoka.
Wakiwa wamelala Sophia alijiwa na ndoto na kuwa kamavile analiona tukio lote ambalo lilitokea usiku wa jana yake wakati wamelala hotelini, alijiona akiwa anaitwa na jinsi ambavyo mume wake alimkataza asiitike. Kisha akamuona binti njiani akionyesha kushtushwa na lile jina la Sophia lililokuwa likiitwa na moja kwa moja akaonyesha kuitika huku akielekea mahali ambapo anaitwa ila mbele kidogo akakiona kile kitoto ambacho huwa wanakutana nacho njiani ila kilionyesha kuwa na sura kama ya kiutu uzima na gafla alitoa vitu vya ajabu na kumwagia Yule dada ambaye alianguka chini.
Sophia alishtuka sana na kupiga kelele ambazo moja kwa moja zilimshtua mume wake pia na kumfanya aamke kutoka usingizini huku akiuliza kwa mshangao kuwa mkewe ameona kitu gani.
Sophia alikuwa akitetemeka sana kisha akaanza kumueleza mumewe kile ambacho alikuwa amekiona kwenye hiyo ndoto,
“Mmh hayo ni makubwa mke wangu kwakweli tunatakiwa kuwa makini maana hiyo hali ni mbaya, unajua nini kwakweli kale katoto huwa sina imani nacho kabisa yani, kale katoto nahisi ni jini”
Sophia akashtuka sana na kumuangalia mumewe, kisha akamuuliza kwa mshangao,
“Jini tena mume wangu jamani dah! Mbona unaniletea habari za kutisha?”
“Sio habari za kutisha ila ndio ukweli huo mke wangu maana haiwezekani tuwe tunakutana nae njiani tena katika mazingira ya kutatanisha kiasi kile. Ila usijali mke wangu maana swala hili lazima nitalitafutia ufumbuzi tu.”
Kwakweli ile habari ya jinni ilimkosesha raha Sophia ingawa hata pale mumewe alipomtaka warejee kulala alijilaza tu bila ya kujiwa na usingizi tena kwani alijikuta akiwa na mawazo sana huku akikumbuka stori za zamani kuwa majini yanakuwaga marefu sana yani huoni mwisho wao halafu chini yanakuwa na kwato za ng’ombe ila akawa anajiuliza kuwa mbona kale katoto ni kafupi sana je ni jamii gani ya jini, alikosa jibu kabisa huku usingizi wake nao ukiwa umekata kabisa.
Masaa yakapita akiwa macho tu kwa muda mrefu kitu kilichomfanya aboreke pale kitandani hivyo akaona vyema hata awahi kuamka zaidi ya siku zote. Ilipofika saa kumi na moja alfajiri aliona ni vyema aende kukaa sebleni tu kuona kama ataweza kusinzia labda na kuweza kulipiza usingizi wake wa usiku.
Akainuka pale kitandani na kwenda mpaka mlangoni ambapo alifungua mlango ila akasikia kama sauti ya Tv ikiongea sebleni kwakweli aliogopa sana ukizingatia mara ya mwisho mumewe alichomoa nyaya zote za kwenye Tv hiyo. Sophia akarudi chumbani kwa kasi ya uoga kwani hakutaka kushuhudia kile kitu, moja kwa moja akaenda kumuamsha Ibra aliyeonekana kuwa na usingizi mzito sana.
“Ibra Ibra tafadhali amka”
“Kwani vipi Sophia kuna nini jamani? Mi si nilisema leo siendi kazini, niache nipumzike”
“Najua kama huendi Ibra ila kuna kitu nataka ushuhudie”
“Kitu gani jamani?”
Ikabidi Ibra aamke na kumuangalia mkewe kisha kumuuliza tena kuwa ni kitu gani ambapo Sophia akamuomba Ibra moja kwa moja kwa muda huo aelekee sebleni ili akaone yeye mwenyewe, Ibra akainuka na kuelekea sebleni ila hakuona chochote ambapo Sophia nae alimfata nyuma. Kisha Ibra akamuuliza Sophia kuwa kulikuwa na kitu gani,
“Mbona hamna chochote kipya hapa sebleni! Ni kinini hiko ambacho ulikiona?”
“Tv ilikuwa inaongea yani kamavile ilikuwa imewashwa”
“Uliiona kabisa ikionyesha?”
“Hapana ila nilisikia sauti ndio nikakimbilia ndani kukuamsha”
“Mmmh maruweruwe hayo mke wangu ukizingatia na ndoto ambayo ulikuwa umeota usiku. Hapa hakuna lolote la kutisha mke wangu hata usiwe na uoga wa aina yoyote ile, uwe na amani tu”
“Lakini nilisikia kabisa”
“Ilimradi hujaona ujue basi ni maruweruwe tu mke wangu. Umefanya na nini usingizi wangu wote ukatike jamani saa kumi na moja hii bado giza totoro nje”
“Nisamehe mume wangu lakini kwakweli sikuwa na jinsi zaidi ya kukuamsha tu.”
“Usijali, mi nakuelewa sana Sophy wangu”
Kisha Ibra akamuomba Sophia kuwa warudi tena chumbani kulala tu hadi saa moja maana sikunhiyo hakuwa na mpango wowote wa kutoka asubuhi asubuhi.
Wakarudi chumbani ambapo Ibra alipojilaza tu usingizi ulimchukua tena na kufanya Sophia awe macho peke yake huku akiwa na mawazo mbalimbali.
Alikuwa akijiuliza kama kweli alisikia sauti ya tv au yalikuwa ni mawazo yake tu na maruweruwe kama mumewe alivyosema ila ilikuwa ni kweli kabisa kuwa alisikia mlio wa Tv kabisa, kwa mbali yale maneno ya Yule bibi aliyekutana nae kwa Siwema na kumwambia kuwa nyumba yake ni ya maajabu yakaanza kumuingia akilini na kuona kama kuna kaukweli flani ambako alikuwa akipingana nako ila alijiuliza kuwa je hayo maajabu yanaletwa na Jane au kuna mtu mwingine anayewafanyia mambo hayo ili kuwatisha kwenye nyumba yao?
Alipokuwa akiwaza hayo, kwa mbali akasikia tena sauti ya Tv na kufanya akurupuke pale kitandani ila kwa muda huu akajipa moyo wa ujasiri ambapo aliamua kwenda sebleni na kushuhudia kabisa kama ni Tv kweli au ndio maruweruwe yake kama mumewe alivyosema.
Sophia alitoka hadi sebleni ambapo kila aliposogea ile sauti ya Tv nayo ndio ilisikika zaidi, alipofika karibu na kuchungulia alikuta ni kweli Tv iliwaka na ilikuwa ikionyesha vizuri kabisa.
Sophia alitoka hadi sebleni ambapo kila aliposogea ile sauti ya Tv nayo ndio ilisikika zaidi, alipofika karibu na kuchungulia alikuta ni kweli Tv iliwaka na ilikuwa ikionyesha vizuri kabisa.
Kwakweli Sophia alipatwa na uoga sana safari hii, hali hiyo ilipekea aanze kuoiga makelele na kufanya mumewe atoke chumbani mbio hadi pale sebleni.
Moja kwa moja Ibra alimuuliza mkewe kuwa amekubwa na kitu gani,
“Nini tatizo mke wangu?”
“Ona Tv inawaka”
Ibra aliiangalia ile Tv ambayo ilikuwa ikionyesha vizuri kabisa kisha akamuangalia mkewe na kusema,
“Si nilichomoa nyaya zote kwenye hii Tv mimi!”
“Ndio ushangae sasa inawaka”
Ibra akaisogelea ile Tv na kuangalia vizuri akakuta nyaya zote zimechomekwa vizuri kabisa, kisha akamuangalia tena mke wake na kumuuliza,
“Nani kachomeka tena hizi nyaya za Tv?”
“Hakuna aliyechomeka itakuwa zimejichomeka zenyewe”
Ibra akacheka kama kwa dharau hivi kisha akamwambia mkewe,
“Nyaya zinajichomekaje zenyewe Sophy mke wangu? Unajua wewe huwa unabaki hapa nyumbani hebu kumbuka nani kachomeka nyaya? Au Siwema jana alichomeka hizo nyaya?”
“Ibra hakuna aliyechomeka, mimi nina uhakika na ninachoongea. Kwakweli nimeanza kuamini maneno ya Yule bibi kuwa hii nyumba ni ya maajabu na siwezi tena kubaki humu ndani peke yangu”
“Kwamaana hiyo unataka mimi nifanyaje? Je tuwe tunaenda wote kazini au nikuletee msichana wa kazi?”
Sophia akawa kimya kwa muda bila ya kujibu lile swali la Ibra, kisha Ibra akaisogelea ile Tv na kuizima halafu akachomoa tena nyaya zote za T vile, halafu akaanza kuongea na mkewe tena
“Unajua zamani watu walipokuwa wakiniambia kuwa wamama wajawazito wana vituko sana nilikuwa siwaamini kabisa ila sasa najionea mwenyewe kwa macho yangu. Kwakweli vituko vyako Sophy imezidi sasa”
“Jamani vituko gani ambavyo mimi navifanya Ibra?”
“Hebu kumbuka toka umeshika hiyo mimba ni vituko mwanzo mwisho, mara useme vyombo vimeosha kimiujiza sijui chakula kimepikwa kimaajabu mara nguo zimejifua zenyewe. Sasa ya saivi ndio kali hii ya kujiwasha kwa Tv duh! Tutafika kweli kwa mtindo huu mke wangu? Sophy hukuwa mtu wa kwenda kwa waganga ila kupindi hiki umeenda hadi kwa mganga na kuniletea makubwa zaidi, kiela chetu kimekwenda na maji. Ulitaka umuue Jane, hivi unaweza kuua wewe? Hiyo roho umeitoa wapi mke wangu? Wewe sio Sophy niliyekuzoea jamani!”
“Ibra najua unanishangaa kwavile mambo mengi ni mimi ninayeyaona ila ungeona na wewe ungeelewa kwanini nakuwa hivi”
“Kwahiyo unataka turudi yale maisha ya zamani? Unataka yale maisha yaw ewe kutembeza karanga na kurudi na mia tano ndani? Unayataka maisha yale ya kukosa hata hela ya kula ndani? Mumeo nimepambana na kufanya maisha yetu yabadilike ili angalau mke wangu uweze kuishi yale maisha ambayo wanawake wengine wanaishi ila matokeo yake ndio haya kukosa amani ndani! Nilikuwa najiuliza sana kwanini wanaume wengine huwarudisha wake zao nyumbani hadi watakapo jifungua ila sasa nimepata jibu kabisa, kwakweli wewe Sophia ni miongoni mwa wanawake wanaotakiwa kurudi nyumbani kwao hadi uatakapojifungua”
Sophia hakuongea chochote kwani kauli ya mumewe kuwa anastahili kurudi kwao hadi atakapojifungua ilimkera sana ukizingatia maisha ya kwao aliyajua mwanzo mwisho.
Ibra alirudi tena chumbani ambapo moja kwa moja akaenda kuoga huku akili yake ikimueleza kuwa lazima Sophia alienda sebleni na kuchomeka nyaya za Tv kisha akaiwasha na kujifanya kuwa imejiwasha ili kumfanya yeye awe anaamini maneno yake kuwa kuna maajabu katika nyumba hiyo.
Ibra alikuwa akioga huku akiwaza cha kufanya kwa huyu mkewe kwani alimuona kama anaanza kuchanganyikiwa na akili, alimaliza kuoga na kurudi chumbani alianza kuvaa huku akiongea peke yake,
“Kwakweli kama mimba zenyewe ndio hivi sijui kama nitaweza jamani, ndio kwanza mimba ya mtoto wa kwanza je akifika mpaka huyo wan ne anayehitaji yeye dah sijui kama sitabaki kijiti mimi kwa mawazo jamani mmh! Mwanamke ananieleleza huyu sijapata kufikiria.”
Wakati akiwaza hayo, salimsikia Sophia akimuita tena kwa sauti ya juu kabisa na kumfanya atoke na kuelekea Sophia alipo ambapo alimkuta jikoni,
“Eeh kuna nini kipya huku jikoni?”
“Vyombo vya jana vimeoshwa vyote”
Safari hii Ibra hakushtuka wala nini bali alicheka tu na kumwambia mkewe,
“Kama vimeoshwa si ndio vizuri umepunguziwa kazi au unaonaje mke wangu!”
“Ibra unachukulia masikhara wewe, sasa hutaki hata kujiuliza kuwa vimeoshwa na nani ikiwa ndani tuko wawili tu mimi na wewe!”
“Ingekuwa tunakuta vyombo visafi vimechafuliwa hapo sasa ndio ningechukua hatua ila kukuta vyombo vichafu vimeoshwa sasa nichukue hatua gani wakati kazi zetu zinajifanya zenyewe tu. Hakuna hata sababu ya kushtuka kwa hilo mke wangu kuwa kawaida tu”
Sophia alimuangalia mumewe kwa hasira kiasi na kuhisi kuwa mumewe kuna vitu anafahamu kuhusu yanayotokea ila amemficha tu maana muda wote yeye ndio anaonekana kuridhishwa kabisa na kinachotokea.
Kisha akamuuliza anapoelekea maana alimuona akiwa amemaliza kujiandaa kabisa,
“Kwahiyo ndio unataka kwenda wapi?”
“Nataka kwenda kumleta fundi wa Tv”
“Kipindi kile ulisema hivyo hivyo ila mpaka leo kimya haonekani fundi wala nini”
“Fundi ningemletaje na yale majanga yako? Tatizo lako kila leo unazua jipya yani hatupumui humu ndani.”
“Kwahiyo mimi unaniacha na nani?”
“Nilikuuliza nikuletee msichana wa kazi au uende kwenu ukapumzike? Hakuna ulilonijibu sasa unafikiri mimi nasemaje tena!”
“Ila mimi si nilishakwambia sitaki msichana wa kazi nataka aje mdogo wangu”
“Sophy, mdogo wako Yule Tausi unamjua vizuri kabisa kwakweli siwezi kumleta hapa maana mambo yatakuwa ni yale yale tu. Lini Tausi ametulia nyumbani? Hebu usitake kuleta makubwa zaidi. Cha muhimu hapa ni mdada wa kazi tu.”
“Sawa siwezi kukupinga si umeamua bhana, sasa tutampatia wapi huyo mdada wa kazi?”
“Tutampata tu hata usijali, ngoja nianze kuulizia kwa wadau mbali mbali.”
“Ila kwa leo mimi sibaki hapa peke yangu”
“Kwahiyo unataka nikusubiri twende wote kwa fundi?”
“Ndio nisubiri”
“Mmh kweli kazi ninayo, haya kajiandae nakusubiri”
Ilibidi Ibra akae sebleni akimngoja mkewe amalize kujiandaa waende huko kwa fundi.
Sophia alipomaliza kujiandaa alitoka, kisha yeye na mumewe wakatoka nje ambapo Ibra aliona ni vyema wakamfate fundi kwa miguu tu kwani hapakuwa na umbali wowote,
“Ni vyema maana itakuwa pia ni zoezi tosha kwangu”
Wakaanza kutembea kwa mwendo wa kawaida tu ila mbele kidogo walimuona binti kajiinamia tena alionyesha wazi kuwa alikuwa akilia, kwakweli Sophia huruma ilimjaa kwa binti Yule na kumuomba mumewe kuwa wamsogelee na wamuulize kuwa alikuwa na tatizo gani ila kama kawaida ya Ibra na roho yake ngumu alikuwa akipinga,
“Sophy, kila mtu ana matatizo yake hapa duniani utayaulizia ya wangapi jamani?”
“Ibra jamani mbona huwa huna huruma! Unakuwa na roho mbaya hivyo kwanini?”
“Roho mbaya kushinda wewe uliyekuwa unataka kumuua Jane!”
“Jamani hayo mambo si yaliisha! Hebu tukamuulize Yule binti inaonekana ana matatizo”
Ibra aliamua kukubaliana na mkewe kisha wakamsogelea Yule binti ambaye ni kweli alikuwa akilia, Sophia akainama na kumuuliza kuwa ana matatizo gani
“Nina matatizo mengi sana dada yani hapa nilipo hata kula sijala njaa nayo inaniuma sana”
Sophia akaingiwa na imani na kumuomba mumewe kuwa warudi na binti huyo nyumbani kwao ili waweze kumpatia chakula na awaeleze yale yaliyomsibu ili kama wataweza kumsaidia zaidi basi wamsaidie. Ibra hakupinga swala hilo kisha wakamsaidia Yule binti kuinuka na kuanza kuelekea nae nyumbani kwao.
Walifika na kuingia nae ndani ambapo Sophia alienda kupasha kile chakula cha usiku na kumpatia ili ale, kisha na wao wakapakua cha kwao na kuanza kula kwani walikuwa wakienda kwa fundi wakati hata kula walikuwa hawajala.
Walikuwa kwa pamoja pale na kumaliza kisha wakatulia kabisa kusikiliza kuwa huyu binti alikuwa na matatizo gani, Sophia alianza kwa kumuuliza,
“Kwanza kabisa unaitwa nani na ni kitu gani kilichokupata mpaka ukawa umekaa pale unalia?”
“Mimi kwa majina naitwa Neema, kwakweli nina matatizo sana yani tangu alipokufa mama yangu nimekosa kabisa furaha ya maisha kwani nilikuwa nikiishi na bibi tu ila ndugu wote walikuwa hawanitaki nyumbani”
Akainama tena na kuanza kulia ambapo Sophia alimsogelea na kumbembeleza,
“Pole sana Neema jamani dah pole sana, eeh ikawaje?”
“Tatizo la sasa ni kuwa Yule mtetezi wangu yani bibi yangu nae amekufa na kuniacha na ukiwa halafu ndugu wakanifukuza. Nimejikuta nikitangatanga tu kisha nilipanda gari la mizigo lililoniacha mjini ila nimejikuta sina pa kuelekea na hata sijui cha kufanya”
“Khee jamani binadamu wabaya sana, pole sana. Ngoja na sisi tuangalie namna ya kukusaidia Neema”
“Nitashukuru sana jamani maana sina uelekeo mimi”
Ibra akaona ni vyema amuache Sophia na huyo Neema ili yeye aende huko kwa fundi, kwahiyo akawaaga pale na kutoka nje ambapo kabla hajaondoka Sophia alimfata nje na kumuuliza kuhusiana na wao kumsaidia binti huyo.
“Unaonaje tukiishi na huyu binti mume wangu?”
“Sophy, tutazungumza nikirudi ngoja saivi nishughulikie hili swala la fundi”
“Sawa basi badae”
Ibra akaondoka na kumfanya Sophia arudi ndani.
Sophia alienda kukaa karibu na Yule binti ili hata kujaribu kuongea nae kama ataweza kuishi hapo nyumbani kwao,
“Je tukikwambia ukae hapa na sisi unaonaje?”
“Nitafurahi sana dada, unaonekana una roho nzuri sana dada yangu”
“Usijali, jisikie huru kabisa yani jisikie upo nyumbani. Ila kazi za nyumbani unaweza kufanya?”
“Hakuna kazi ambayo mimi inanishinda, maisha niliyokulia yamefanya niwe naweza kazi zote dada yangu kwahiyo hata usiwe na hofu kuhusu mimi.”
Sophia alijikuta akiwa na huruma sana kwa huyu binti na pia akivutiwa nae sana na kuona lile swala lake na mumewe la kuhitaji mdada wa kazi limepata ufumbuzi kwa stahili hiyo.
Muda kidogo Ibra alirudi akiwa na kijana ambaye alimtambulisha kuwa ni fundi, Yule kijana moja kwa moja alienda kuiangalia ile Tv kisha akaanza kuwaorodheshea matatizo ya ile Tv n kuhitaji wampatie pesa ili aende akanunue vifaa kwaajili ya kurekebisha Tv hiyo.
“Inahitajika kama laki moja na nusu hapa ili tatizo lisijirudie tena, yani msingekuwa makini siku moja ingewalipukia hii”
“Ila mbona gharama sana mtu wangu?”
“Ndio hivyo, ni kutokana na kifaa ambacho kimeharibika huwa kinauzwa gharama sana tena hapo nimekupunguzia sababu wewe wangu bhana, yani hela ya ufundi hapo nitachukua elfu kumi tu maana laki na arobaini yote nitaenda kununulia hicho kifaa”
Ibra akafikiria kidogo, ila kwavile hapendi malalamiko ya kila siku kuhusu ile Tv aliamua kujitoa muhanga kwa kutoa hiyo pesa ili amkabidhi huyo fundi kwaajili ya kununua hicho kifaa. Ila kabla fundi hajapokea ile pesa, huyu Neema akamwambia Ibra,
“Kaka hata usitoe hiyo pesa maana hii Tv sio mbovu”
“Kwani wewe hii Tv unaijua?”
“Siifahamu ila moyo wangu unaniambia kuwa hii Tv sio mbovu”
Kisha akamuangalia Yule fundi na kumwambia,
“Kwanini unakuwa muongo hivyo? Au ukubwa wa hii nyumba ndio unafanya na wewe utake kuponea hapa! Hebu waambie ukweli kuwa hii Tv sio mbovu na wala hakuna kifaa chochote kilichoharibika, sema ukweli”
Huyu fundi alionekana akitetemeka na kujieleza kuwa ni kweli ile Tv haikuwa mbovu ila yeye alishikwa na tama ya pesa tu na ndiomana akasema vile, Ibra alimshangaa sana huyu fundi kwani alikuwa ni kati ya watu aliowaamini sana, kisha huyu fundi aliondoka bila kuaga.
Ibra alimuangalia Neema na kumshukuru kisha akamuuliza kuwa amejuaje kuwa ile Tv sio mbovu na amejuaje kuwa Yule fundi ni muongo,
“Bibi yangu alinifundisha kuwa mtu muongo akiongea macho yake huwa anapepesa pepesa, sasa nilipomuangalia huyo fundi nikamuona akipepesa macho na moja kwa moja nikagundua kuwa ni muongo.”
Sophia aliyekuwa amekaa kimya kwa kipindi chote nae aliamua kuchangia mada kwa kumshukuru sana Neema maana ilikuwa kama amewasaidia katika kupoteza pesa zingine, ila bado alimwambia kuwa ile Tv ina tatizo la kujiwasha na kujizima ndiomana wakaita fundi awasaidie.
“Msijali, ilimradi mimi nipo hapa hilo tatizo halitajitokeza tena”
Sophia hakuongeza neno zaidi ya kwenda kumuonyesha Neema chumba ambacho atakuwa analala kwa kipindi chote atakachokuwa anaishi hapo.
Alimpeleka kwenye chumba ambacho kilikuwa na kitanda na godoro tu kisha Sophia akatoka na kumuacha huyo Neema kwenye chumba hicho, Sophia alienda chumbani kwake na kumchukulia Neema mashuka ili aweze kutandika vizuri pale kitandani na kufanya papendeze kulala.
Sophia akiwa na mashuka yake mkononi kwa lengo la kumpelekea Neema, aliingia kwenye kile chumba na kumkuta Neema akiwa amesimama tu ila kitanda kilikuwa kimetandikwa vizuri kabisa tena kwa mashuka mazuri.
Sophia akiwa na mashuka yake mkononi kwa lengo la kumpelekea Neema, aliingia kwenye kile chumba na kumkuta Neema akiwa amesimama tu ila kitanda kilikuwa kimetandikwa vizuri kabisa tena kwa mashuka mazuri.
Kwakweli Sophia alishangaa sana na kumtazama Neema kwa mshangao zaidi ila huyu Neema hakuonekana na hofu yoyote ile na kufanya Sophia amuulize,
“Neema, kitanda kimetandikwa na nani? Na je mashuka yametoka wapi hayo?”
Neema hakujibu ila naye alimuuliza swali Sophia,
“Kwani umeyapenda dada haya mashuka?”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Sophia alizidi kushangazwa kwani hakutegemea na yeye kuulizwa swali badala ya kujibiwa swali lake kwahiyo ilikuwa kamavile ni kitu kinachomchanganya zaidi, kisha kabla hajaongeza neno lolote akamshangaa tu Yule Neema akimpokea yale mashuka na kisha kumshukuru sana kwa kumletea,
“Asante dada kwa haya mashuka kwani nayo ni mazuri sana dada yangu”
Bado Sophia hakuweza kuongeza neno lolote zaidi ya kutoka mule chumbani na moja kwa moja akaelekea chumbani kwake kwani hata sebleni alipitiliza, Ibra alikuwa ametulia tu pale sebleni akimuangalia mkewe akipitiliza chumbani na kuhisi kuwa huenda kuna vitu ambavyo mkewe alivisahau huko chumbani kwani kwa matarajio yake alihisi kuwa mkewe alipomaliza kupeleka yale mashuka angerudi pale sebleni waweze kuzungumza.
Muda kidogo ni Neema aliyetoka na kwenda kukaa sebleni ambapo alimtazama tu Ibra bila ya kuongea chochote kile, Ibra nae hakuchukua muda mrefu akainuka pale sebleni na kuelekea chumbani.
Alipofika chumbani alimkuta mkewe akiwa amelala kabisa kamavile ni muda mrefu aliingia kulala, mija kwa moja Ibra alihisi kuwa ni uchovu wa mimba ndio umemfanya mkewe awe katika ile hali kwani haikuwa kawaida yake hapo zamani, ila Ibra nae alipanda kitandani na kujilaza karibu na mkewe ambapo kwa muda mchache tu naye usingizi ulimpitia.
Walipokuja kushtuka muda tayari ulikuwa umeshaanda tena aliyeanza kushtuka alikuwa ni Ibra na kumuamsha mkewe,
“Sophy, Sophy tumelala sana mke wangu amka”
Sophia nae aliamka na kuanza kujinyoosha kwa uchovu huku akijihisi kuchoka sana, kwa pamoja wakainuka na kutoka chumbani ambapo walimkuta Neema akiwa pale sebleni tena alionekana kuyazoea sana mazingira yale kupita maelekezo kwani alikuwa sawa na binti ambaye amekuwa pale kwa siku zote. Ambapo walipofika tu sebleni aliwakaribisha mezani kuwa chakula tayari, hakuna aliyehoji kati yao kuwa ni nani aliyemwambia Neema kupika au kumuelekeza cha kupika bali walielekea mezani wote na kuanza kula huku huyu Neema akiwa anaendelea na shughuli zingine.
Alianza Sophia kukisifia kile chakula kuwa ni kitamu sana huku akiyasifu mapishi ya Neema kuwa ni binti aliyefundwa vyema, Ibra nae alimsapoti mkewe kwa kummwagia sifa za kutosha huyu Neema. Hadi wanamaliza kula ilikuwa ni kumsifia Neema tu pale mezani.
Walipomaliza tu Neema alikuja na kutoa vile vyombo na kuvipeleka jikoni moja kwa moja kisha Sophia na Ibra wakarudi sebleni na kukaa ambapo neema alikuwa ameiwasha ile Tv ambayo walikuwa wakiogopa kuiwasha kwa siku zote mule ndani.
Hakuna aliyemuuliza chochote Neema kwani wote walitulia na walionekana kuridhishwa na uwepo wake mule ndani, ingawa mara nyingi sana walimuona huyu Neema akiwaangalia sana ila hawakuweza kuhoji kitu chochote kile zaidi ya kutabasamu tu.
Usiku ulipoingia zaidi, Sophia na Ibra walielekea chumbani kwao huku Neema nae akielekea chumbani kwake.
Walipokuwa chumbani, Ibra aliamua kumuuliza mkewe kilichompelekea mchana kwenda kulala bila ya kumtaarifu.
“Ilikuwaje kwani maana nilikukuta umelala hoi kabisa au ndio mambo ya mimba tena?”
“Naelewa basi! Hata sielewi, nilikujs chumbsni sijui hata kufanya nini nikashangaa usingizi ulipotokea loh yani nimelala usingizi mzito kupita maelezo ya kawaida.”
“Duh pole mke wangu, najua ni mimba hiyo inayokusumbua ila mambo yatakuwa sawa baada ya miezi kadhaa tu.”
“Na hapa tumbo halijakua vizuri je likikua sijui itakuwaje”
“Utazoea tu mke wangu ila ni vyema kama ukianza kliniki si unajua wanasema ni bora kuanza mapema!”
“Naelewa mume wangu nitaanza tu hata usijali”
“Ila unasemaga hivyo kila siku halafu wala huonyeshi huitaji wa kuanza kabisa hata sijui kwanini?”
“Ngoja tumbo litokee tokee kwanza”
“Mmh jamani Sophy, mbona watu wanaanzaga mapema unataka tumbo litokeaje?”
“Khee Ibra hao wanaoanza mapema umewaona wapi? Ushawahi kukaa na mwanamke mjamzito wewe?”
“Basi yaishe mke wangu ila ni vyema kuanza kliniki”
“Sawa nitaanza hata usijali”
Sophia akajinyoosha pale kitandani na kulala, muda huo huo ikawa kama amelala kwa muda mrefu kwani alikuwa na usingizi mzito sana na kufanya Ibra amtazame tu kisha na yeye akalala.
Ibra alipolala tu akajiwa na ndote, ile ndoto ilimuonyesha kuwa Yule nyoka mkubwa waliyemuona mlangoni kwao hakuwa nyoka kweli bali alikuwa ni huyu Neema waliyekuwa nae ndani kwani alivyokuwa akimuona kwenye ndoto alimuona akibadilika badilika mara akiwa mtu na mara akiwa joka. Kisha akamuona Jane akiingia pale ndani kwao na gafla Yule nyoka akayeyuka halafu akaonekana chini ya mti mahali ambapo ndio pale pale walipoenda kumkuta Neema akiwa amejiinamia.
Kwakweli Ibra alishtuka sana kwani hakutegemea kama anaweza kupata ndoto ya namna ile ukizingatia huyo Neema ndio wanaishi nae ndani kwa kipindi hiko, jasho lilikuwa likimtoka sana Ibra na kumfanya ashindwe kuendelea kulala kabisa kwani alikaa tu kitandani kwa muda huo, kisha akakumbuka jinsi mkewe nae anavyopataga ndoto ambazo huwa zinamfanya akose usingizi kabisa kwakweli na leo ilikuwa zamu yake yeye.
Kulipokucha Ibra aliamka na kujiandaa kwaajili ya kwenda kwenye shughuli zake, kisha akamuamsha na mkewe kwa kumuaga kuwa anatoka kwa muda huo, hivyo Sophia aliinuka ili aweze kufunga mlango pale mumewe anavyotoka ila walipofika sebleni walimkuta Neema akiwa tayari ameshaamka, alikuwa amekaa tu akiangalia Tv ikabidi wamsalimie huku Sophia akimuuliza kuwa mbona mapema sana.
“Ndio kawaida yangu kuamka mapema huwa silali kupitiliza”
“Sawa ndio vizuri ila duh unawahi sana”
“Hata usijali kitu dada yangu”
Ibra akawaaga pale na kuondoka, ndani alibaki Neema na Sophia ambapo Sophia alirudi chumbani na kuendelea kulala.
Ibra akiwa njiani kwakweli alijikuta akikosa imani kabisa kumuacha mkewe na Neema ukizingatia mkewe ni mjamzito halafu Neema ni mgeni kwenye ile nyumba yao, akajiwa na wazo kuwa ni bora akamwambie Jane nae aende pale kwake ili awe nao pamoja kuliko mkewe kubaki mwenyewe na Yule Neema ambayo hawamfahamu vizuri.
Ibra aligeuza gari na moja kwa moja akaelekea kwakina Jane ambapo kama kawaida alimkuta mama yake Jane akiwa ndiye pekee aliyeamka huku akifanya shughuli za nyumbani kwake, hivyo akamsalimia na kuomba aitiwe Jane, ila leo mama Jane nae alifunguka
“Ila nyie mpaka mumtoe mwanangu ngeo ndio mtaona raha maana sio kwa kumuita ita huko halafu akifika kwenu mnamfanyia vituko. Au unafikiri habari zenu sikuzipata? Kwanza mwanangu Jane bado kalala labda uje badae.”
Ibra hakutaka kupingana na huyu mama ukizingatia ni kweli mambo ambayo walimtendea Jane hakuna mzazi yeyote anayeweza kuridhishwa au kufurahishwa nayo, hivyo Ibra akawa mpole tu na kumuaga huyu mama kuwa atarudi tena badae.
Ibra akaondoka pale kwakina Jane na kuelekea kwenye shughuli zake ila mawazo yake yalikuwa ni juu ya mkewe kwani alijikuta gafla akikosa amani kabisa dhidi ya uwepo wa Yule Neema pale nyumbani kwao ukizingatia na ile ndoto aliyoota ndio kabisa yani.
Sophia sasa aliamka vizuri na kwenda sebleni tena ambapo alimkuta Yule Neema akiangalia tu Tv ila kazi za mule ndani zote zilikuwa zimefanyika, Sophia alikaa nae huku akizungumza nae kwa furaha sana.
“Kwakweli Neema nimekupenda bure maana wewe ni mchapakazi sana na hata sikukutegemea kabisa kama utakuwa hivi”
“Usijali dada mbona utazidi kufurahia uwepo wangu, yani utafurahia sana na kujilaumu kuwa kwanini umechelewa kugundua uwepo wangu”
“Ni kweli kabisa maana wewe hata sio mtu wa kupigishana kelele ukizingatia unafanya kazi zako kwa wakati.”
Neema akatabasamu tu, kisha akamwambia Sophia kuwa hata chai alishamuandalia mezani ambapo Sophia alienda moja kwa moja kunywa chai ile ambapo alikuta ni chai ya maziwa, chapati na mayai. Sophia alikunywa bila hata ya kuhoji kuwa vile vitu vimenunuliwa muda gani hadi kupikwa kwani alihisi huenda mumewe alinunua bila hata ya kusema.
Alipomaliza kunywa chai alirudi chumbani kuoga ili kupata nguvu mpya ambapo alioga na kwenda kukaa kitandani huku akijikuta akifikiria mambo mawili matatu.
“Inamaana Neema zile chapatti kazipika au kazinunua? Kama kazipika unga ametoa wapi? Na kama amezinunua basi pesa alipewa na nani? Hivi Ibra anaweza kutoa pesa bila ya kunishirikisha kweli? Vipi kuhusu yale mayai mmh! Itakuwa ni ibra tu ila hatahivyo chakula kilikuwa kitamu sana.”
Sophia akatulia na kuanza kuvaa kisha akatoka tena na kwenda sebleni ambapo Yule Neema alikuwa pale pale sebleni akiwa ametulia akiangalia Tv tu, ambapo Sophia alimuuliza
“Huchoki Neema kuangalia Tv?”
Neema akatabasamu tu na kudai kuwa anapenda sana kuangalia Tv kuliko kitu chochote na kama akichoka basi ataizima, Sophia hakutaka kuongea zaidi kwani alihisi anaweza kumfanya Neema achukie bure ukizingatia hoja yake ilikuwa ni kumwambia kuwa tv inahitaji kupumzika kwani sio vizuri kuwa inaonyesha muda wote.
INAENDELEA

