NILAMBE HUMO HUMO
ONYO: Wakubwa tu, kuanzia Miaka 18, ndio wasome hii Hadithi
Sehemu Ya 1
…ulikuwa mduara wa Segere kwa lugha isiyo rasmi. Au ‘mnanda’ kama ilivyozoeleka. Baadhi ya wakazi wa kitongoji hicho walikuwa wakizunguka kwa pozi huku wakizungusha viuno vyao taratibu kwa ustadi mkubwa.
Mirindimo ya ngoma sambamba na kiuno cha mwanamama mmoja kilichokuwa kikizunguka vitamu vikayafanya macho yangu yamuandame! Yakamwandama kila alipokwenda.
Halafu ngoma ikazimwa.
Yule mwanamama ambae wakati huo alikuwa ameshagundua kuwa nilikuwa nikimtazama akanitupia jicho na kuachia tabasamu. Ngoma ikapigwa upya na kurindima kwa robo saa hivi. Ilipozimwa tena na moto ulio kuwa ukitoa mwanga pekee hapo uwanjani nao ukazimwa!
Kabla mshangao wangu haujaisha, nikajikuta ninashikwa mkono na kuvutwa kuelekea migombani kwenye kiza. Nikaweka mgomo kiasi, lakini nilipogundua kuwa kwamba jimama lililokuwa likizungusha kiuno vitamu ndilo lililokuwa likinivuta, nikatabasamu na kulifuata mithili ya mwanakondoo.
Kisha macho yangu yakazoea giza.
Huko Migombani nikashangaa kukuta seti mbilimbili za watu wakiwa wameng’ang’aniana huku wakitoa milio ya ajabu ajabu! Nilipowatazama vizuri, nikataharuki! Walikuwa wakifanya mapenzi!.
Nikatolewa ndani ya taharuki na jimama lililokuwa likinivuta, ambalo lilikuwa tayari likinishinikiza nasi tufanye mapenzi! Loh! My God ‘Gobbah…!’
Tembeeni muone.
* * *
Naweza kusema nilikuwa na bahati mbaya maishani, ndio mwenyewe nilijiona kuwa na sura ya wastani isiyo mbaya sana wala nzuri sana.
Sura ambayo unaweza kumtongoza msichana huyu akakukatalia na yule akakukubalia! Lakini haikuwa kwangu. Kila niliyemtongoza alinikatalia, Kila niliyemtongoza!
Hali hii haikuanza leo wala jana, ilianza kitambo toka ningali kinda lisilojua adha wala starehe ya tendo hilo la ndoa. Wakati huo akili za utoto zikinifanya niamini kwamba sikuwa mtaalamu wa kupangilia vyema mashairi yangu wakati nilipotaka kufikisha ujumbe wangu kwa mlengwa.
Nilipoingia primary wewe iite shule ya msingi na tatizo hilo kujirudia tena, sikutilia maanani sana. Nilikuja kuadhirika mwishoni mwa kidato cha pili na mwanzoni mwa kidato cha tatu.
Nadhani kuathirika kwangu kisaikolojia kulitokana na ukweli kwamba kipindi hicho ndicho kilikuwa kipindi kipevu kwangu, kipindi cha masham sham na matamanio ya hamu. Kipindi cha mifadhaiko na majaribio, kipindi cha kupevuka.
Naam kilikuwa kipindi cha balehe. Kipindi cha kutoka utotoni na kuingia katika utu uzima. Ndugu yangu kipindi hiki kisikie hivyo hivyo, kama mwenzetu ulifanikiwa kukipita salama, hongera yako.
Lakini wale wenzangu na mimi tuliopelekwa na kupelekeshwa na kipindi hicho ambacho kila anayebahatika kupewa uhai na manani lazima akipitie, wanazielewa fika tamu na chungu za kipindi hiki hatari.
Wakati huo mheshimiwa sana kule ikulu alikuwa akinisumbua vilivyo nyakati za usiku muda mfupi kabla ya kulala, kila wakati akitaka kukagua gwaride la heshima.
Hata hivyo bahati ilikuwa upande wangu mara nyingi usingizi uliponichukua ndoto nyevu ziliniokoa!
Ingawa shida za usiku hazikuwa za kupatiliza, adha nilizokuwa nikizipata mchana katika maeneo mbali mbali kila nilipokuwa nikikutana na mwanamke aliyeumbika vizuri, aliyevaa nguo za kubana sana, aliyevaa kimini na kitopu na hata wale waliovaa robo tatu uchi; hazikuwa na mfano.
Pengine ni hili lililoniingiza katika mkumbo waliopitia vijana wengi. Mkumbo wa kujichua! Potelea mbali kama unalegeza mishipa na kuathiri nguvu za kiume baadae!
Ndiyo, niliamua kufanya mapenzi na mikono yangu kwa msaada wa sabuni, mafuta au chochote nilichokiona kinafaa au kunirahisishia kazi. Hii ikaendelea kuwa mkombozi pekee kwangu katika masuala ya kupoza makali ya ukware!
Kumbe ningelifanyaje? hasa ukizingatia ukweli kwamba nilikuwa mwanafunzi nisiye na uwezo wowote kifedha, muoga wa kuwakabili viumbe hawa uzao wa Eva? Hakika hilo lilikuwa suluhisho kwangu.
Sikushauri uwe kama mimi, lakini mwenzako suluhisho hilo lilinifanya nihitimu elimu ya sekondari vizuri salama usalimini.
Sikupata alama nzuri ambazo zingeniwezesha kuendelea na masomo ya juu ngazi ya A – level, kidato cha tano na sita. Na hili nilitarajia kabisa. Unadhani? Ningewezaje kupata alama nzuri hali nikiona mguu uliojaziajazia chini ya sketi basi hata kama nilikuwa ninasoma na wenzangu ni lazima nitafute mahali nijichue kwanza ndipo mambo yaende sawa?
Wazazi wangu wakaamua kunipeleka Veta kuchukua mafunzo ya ufundi umeme!
Kazi ambayo awali niliona inawastahili wanaume pekee, lakini nilipofika huko matokeo yakawa kinyume! Wanawake na labda niwaite wasichana walikuwa wamefurika isivyo kawaida katika darasa hilo.
Pongezi kwa wanaharakati wanaopigania usawa wa kijinsia, harakati zao zinazaa matunda ati! Kwa mujibu wa waalimu wa hapo, kipindi cha nyuma ilikuwa aghalabu kukuta wanawake wengi wakijitokeza katika fani kama hizi zilizoonekana kama zina harufu ya uume uume!
Wengi ungewakuta ama katika mafunzo ya ufundi wa ususi, urembaji mapambo, mabatiki, ushonaji nguo, upishi na aina zote zenye mwelekeo huo lakini sasa hali ni tofauti, tena tofauti sana.
Ni huko nilikokutana na rafiki yangu Akimu Yusuph, huyu alitokea kuwa rafiki wa kweli na mfariji mkuu wa maradhi yangu ambayo sina shaka kwamba sasa unayafahamu fika.
Halafu ilifika siku moja, siku isiyo na jina!
Siku ambayo hatukuwa na masomo hapo chuoni. Nadhani itapendeza zaidi nikiita siku ya mapumziko. Mchana wa siku hiyo ulinikuta katika grosari moja jirani na chuo chetu pale chang’ombe nikipata kinywaji laini cha baridi. Mimi sio mtumiaji wa vikali na ninaomba Mungu anisaidie nisijaribu kuvigusa, usiulize sababu tafadhali.
Mchana huo ukiendelea kuyoyoma taratibu sambamba na kinywaji changu, mkononi nilikuwa na gazeti la Ijumaa wikienda nikiendelea kupata elimu ya kutakata ya namna ya kuyafikia mafanikio toka kwa Brother Erick Shigongo.
“Hai Ibra?” Sauti nyembamba na laini ikaniharibia pozi.
Nikageuka taratibu kabla ya kujibu. Ni utaratibu nilio jiwekea toka enzi na enzi ili kuepuka kujibu salamu isiyonihusu na hivyo kumkwaza msalimiaji. Ndiyo! Kuna akina Ibra wangapi jijini?
Macho yangu yakakumbana na tabasamu zuri lililopachikwa kiufundi katika sura murua ya binti huyu mantashau. Hakuwa mgeni kwangu. Hili lilidhihirisha kwamba salamu ile ilikuwa yangu. Nami nikachanua tabasamu bomba kujibu tabasamu lake pamwe na salaam pia.
“Hai Shamsa! Mambo?”
“Kama mgambo kasoro kirungu!”
“Hivi bado hamjamuelewa Karl P tu? Kwanini hukujibu kama mgambo kasoro bunduki na pingu?”
Tukacheka.
Shamsa Nuhu alikuwa mmoja kati ya wanafunzi wenzangu tuliokuwa tukichukua mafunzo ya umeme pale VETA. Katika muziki Shamsa alikuwa akimpenda sana msanii Karl P, ingawa Karl P mwenyewe hayuko tena kwenye chati siku hizi .
Shamsa pia ni mmoja wa wasichana wachache walio kuwa wakiwapelekesha puta wanaume ndani na nje ya darasa letu.
Alikuwa na akili za kutosha, hilo lazima nilikiri. Masomoni alikula sahani moja na wale unaoweza kuwaita majiniazi. Kifedha pia alikuwa njema kiasi kile ambacho usingeweza kumrubuni akubaliane na wewe kwa kwa kumringishia vijisenti! Kama hujui vijisenti, usiniulize mimi; muulize Chenge!
Kwa uzuri sijui wengine, lakini kwangu alikuwa na uzuri ulio shinda malaika! Alikuwa na sura nzuri, tabasamu zuri, ‘dimples’ nzuri, shingo ya miraba miraba, umbo zuri, mzigo wa uhakika nyuma yake, usafiri mzuri na hata mwendo wake ulikuwa mzuri. wachilia mbali sauti, roho na vitendo vyake. Alikuwa mzuri hasa, mzuri fika.
Alikuwa mmoja kati ya wengi waliowahi kuumong’onyoa moyo wangu! Unadhani? Sio yeye tu, wako wengi waliowahi kupata hifadhi moyoni mwangu, lakini mimi nilipotaka kuingia katika mioyo yao wakagoma kunipa hifadhi!
Nilihofia kumueleza nilivyojisikia juu yake kutokana na ile hofu ya kawaida, hofu ya kukataliwa kwamba kama watu wanaoonekana; wenye akili zao darasani, fedha zao Benki na heshima zao katika jamii wamejaribu wameshindwa mimi mtoto wa msaka nyoka kama sio msaka tonge nitaweza kweli?
Niliendelea kuumia kwa muda mrefu mpaka siku fulani nilipopata ujasiri wa aina yake na kumkabili. Hii ilikuwa ni baada ya kujishauri sana na kuamua kwamba mwanaume anakufa siku moja.
Aidha ilikuwa ni baada ya kujiuliza ni mara ngapi nimetongoza na kufaulu, nikagundua ni mara 0.05! Nikakubali kuishi siku moja kama simba kuliko kuishi siku mia moja kama inzi! Kwamba hata akinikatalia atakuwa tayari anajua ninampenda! Itatosha .
Nikamvaa!
Unadhani nilifanikiwa kuinua domo langu na kumwambia japo ninakupenda tu? Thubutu! Kila nilipojitahidi kusema sasa nimwambie, ulimi ulikuwa mzito na pale ulipokuwa mwepesi maneno yalifanya mgomo!
Mgomo ulipojisahau yalitoka maneno mengine tofauti kabisa na ninakupenda!
Mpaka muda wa maongezi niliomuomba tuongee unakwisha na yeye kuniaga sikuwa nimemwambia lolote la maana. Nilibaki nimeduwaa kwa muda wakati wakati akiyoyoma na kunipa nafasi ya kuyafaidi maungo yake kwa nyuma.
Ghafla akageuka na kunitazama.
Macho yetu yakagongana.
Akatahayari, labda kwa vile alivyogundua kwamba alikuwa akitazamwa kifisifisi. Akageuza na kurudi kwa madaha akitumia hatua zilezile za miss Tanzania wa mwaka huu mpaka pale nilipokuwa nimesimama. Akaniangalia kwa muda kabla hajaniuliza kwa wasiwasi.
‘’Una nini Ibra?’’
“Sina kitu Shamsa!’’
‘’Kweli?’’
“Haki ya Mungu vile!’’
“Au nimekukatili?! Bado hujamaliza kiu yako ya maongezi na mimi?”
“Nilishamaliza kabisa. Amini nilitaka tu kujua kidogo kuhusu utendaji kazi wa Socket Bracker na vitambuzi vya Short, lakini jinsi ulivyonielekeza inatosha kabisa. Ahsante sana Da! Shamsa, Mungu akujaalie!”
“Amina” Akajibu akitabasamu, wasiwasi ukiondoka pole pole. Dimples zake zikabonyea na kukitonesha kidonda changu tena. Mshituko mdogo nilioutoa ambao nilijitahidi kuuficha asiuone, ukawa umeurudisha wasiwasi wake kwangu tena.
‘’Sikiliza Ibra!’’ akaniambia kama aliyechoshwa na kitu fulani.
“Mimi ni mwanadamu mwenye hisia timilifu kama wewe! Kama una lolote ambalo labda unahisi litahitaji msaada wangu we niambie tu. Acha kuteseka kipumbavu na njaa na wakati chakula unachodhani ni cha watu kipo karibu yako! Huwezi jua may be Mungu amepanga kukuokoa kwa chakula hicho.!”
Akazidi kunionyesha kwamba yuko tayari kwa lolote binti wa watu. Masikini laiti angelijua jinsi alivyozidi kuniweka mbali kwa kauli ile, asingeendelea.
“Da’ Shamsa, msaada niliouhitaji umekwisha nisaidia, tena umenisaidia kiukamilifu. Nikiwa na tatizo jingine nitakwambia tu. Naomba nawe usichoke kupokea miito yangu!”
‘’Usijali!’’ akaniwahi kwa pupa.
Ukapita ukimya mfupi tukiwa bado tumesimama hivyo hivyo tukiangaliana kwa zamu tena kwa wizi, mwishowe Shamsa akaniita tena.
‘’Ibra?” Sasa alinitulizia macho usoni moja kwa moja.
‘’Naam!’’ Nikaangalia pembeni, nikisugua vidole vyangu kama jinga vile
‘’Au… Au… Au unanipenda na unashindwa kuniambia?”
“Mmmm, mmmm!” Nikatikisa kichwa kushoto na kulia kukataa.
Shamsa akanipuuza na kuendelea “Kama umenipenda niambie tu. Niambie dia, niambie nijue! Hizi ni zama za ukweli na uwazi niambie usiogope!’’
Ooops! nikashusha pumzi ya faraja ndani kwa ndani, kwa namna ya mtu aliyeshusha mzigo mzito. Shamsa aliamua kuweka ile Msondo ngoma wanaita mambo hadharani. Ndiyo! Alikuwa amegusa mzizi, amegusa pale nilipotaka aguse.
Pengine ingelikuwa wewe ilikuwa ni kiasi cha kuongeza maneno machache tu ndio ni kweli ninakupenda, lakini kutokana na uzuri wako, uwezo wako kiakili na kifedha nimekuwa nikihofia kukwambia kwa kuwa nilijua utanikataa na hivyo nitaaibika lakini ninakupenda sana na ninataka uwe mpenzi wangu please please naomba upokee ombi langu na kunipokea mimi mwenyewe,
Lakini kwangu thubutu! Haikuwa hivyo nikajichekeshachekesha kiwazanga pale huku nikiona aibu kupindukia pengine kwa Shamsa kuligundua lile lililomo moyoni mwangu, nikaropoka.
“Hapana Da’ Shamsa! Wewe ni dada yangu, kwamwe siwezi kukutamkia maneno kama hayo, nikiwa na mengine nitakwambia si hili!’’ Nilizidi kujiweka mbali na kujikaanga kwa mafuta yangu mwenyewe.
Shamsa akaniangalia vizuri asiamini lile nililoongea, kutaka uhakika akaniuliza tena. ‘’Unasemaje?”
Nikarudia nilichokisema awali mithili ya muigizaji aliyeiva vyema baada ya kumeza scripts kikamilifu. Nikaona Shamsa akiishiwa nguvu kwa staili ileile ya kukata tamaa, alipogundua nimemgundua katika hilo, haraka akajirekebisha na kusema.
“Ok! Nafurahi kwa mawazo yako yaliyokwenda shule Ibra, laiti kama wanaume wote wangelikuwa kama wewe…! Ndio maana ninakupenda Ibra, wewe sio muhuni, hupendi mambo ya kipumbavu!
Angelikuwa mwanaume mwingine, tayari angeisha nitongoza zamani. Lakini wewe akah! Keep it up. Keep it real Ibra. Endelea na moyo wako huo huo siku moja nitakuja kukupa tuzo. Bye!’’
Akaondoka bila kunipa nafasi ya kujibu tena, nadhani maneno yale aliyasema kwa uchungu kiasi cha machozi kumlenga na nilihisi aliondoka upesi akihofia kulia mbele yangu!
Kulia? Nikajiuliza kwa mshangao, kwa ajili yangu! Maana yake nini? Sikupata jibu! Niliendelea kumwangalia mpaka alipotoweka kwenye upeo wa macho yangu. Ndio kwanza nikapambazukiwa na ukweli wa kile nilicho kifanya.
“Shit!” Nikaguta ghafla nikijipiga makonde ya nguvu kichwani. “Nimefanya nini sasa? Ama kweli mimi ndio mjinga wa wajinga No! Mwenyekiti wa wajinga. Mtoto tayari alishakaa katika laini namba moja, mie nimemrudisha line namba ziro! Tena ziro pointi ziro tano! Kamwe siistahili kusamehewa!” Nikajiambia nikizidi kujipiga makonde kichwani.
‘’We vipi Ibra?’’ sauti niliyoifahamu sana ikanishtua kutoka nyuma yangu. Nikageuka haraka huku nikitahayari mithili ya mtu aliyefumaniwa, ni kweli rafiki yangu Yusuph alikuwa amenifumania, nikijipiga makonde kichwani kama chizi.
“Vipi nini?” Nikasaili kipumbavu nikizidi kuona hatia na kuongeza
“Mbona mie mambo yangu yako safi?
‘’Unahakika ni safi?’’ Akimu akanitulizia macho asiyapepese walau kiduchu.
Nikazidi kuona soo.
“Sikiliza Ibra, mimi ni rafiki yako wa damu, rafiki wa dhati rafiki wa kufa na kuzikana. Unaponificha jambo ni kama unajificha mwenyewe!”
‘’Hakuna Akimu! Hakuna kabisa. Nothing!”
‘’Kweli?’’
‘’Kweli tupu!
‘’Sasa mbona unajipigapiga makonde kichwani huku ukikita miguu chini utafikiri umepoteza kitu fulani kama sio kufeli mitihani!”
Eh! Hii kali! Nikawaza. Kumbe nilikuwa nikikitakita na miguu chini? Sekunde kadhaa zikapita huku Akimu akiniangalia na mimi nikiangalia chini kwa tahayari wakati huo kichwa changu kikizunguka kutafuta jambo la kumuongopea Akimu, sikulipata.
“Ukingali unajaribu kunificha Ibra! Any way haya ni maisha yako. Wewe ni mwamuzi wa mwisho kwayo. Ukiona ninastahili kuambiwa utaniambia, Ukiona sistahili usiniambie na sitolalamika kwaheri!”.
Akimu akamaliza na kuondoka kwa haraka kama alivyoondoka Shamsa. Nahisi nae aliongea kwa uchungu kwa kuwa tangu nianze masomo yeye ndio amekuwa rafiki na mwandani wangu mkuu.
Sasa nitawakorofisha watu wangapi jamani? Kwa kule tu kukataa kwangu kusema ukweli! Kwa Shamsa naweza kustahimili kuishi bila ya kuwa na mahusiano nae mazuri. Lakini Akimu?! Itanichukua muda gani kutengeneza urafiki mzuri na bora kama yeye?
Liwalo na liwe! Nikaanza kumkimbilia huku nikimwita, alikuwa amefika mbali kidogo, aliposikia akasimama na kugeuka .
‘’Unasemaje?” Akaniuliza nilipo mfikia.
“I am so sorry kaka!’’
‘’Samahani ya nini Ibra?! Si umesema hakuna kitu?”
‘’Nilikuwa wrong Akimu, nina tatizo! Tena tatizo kubwa!’’
‘’Tatizo la mapenzi sio? Linamuhusu Shamsa bila shaka!’’
Nikasikia moyo unafanya pah! Amejuaje? Nikatikisa kichwa chini na juu kuafiki,
’’Nilijua tu lipo tatizo, nikashangaa na kuchukia ulipotaka kunificha. Ulipotoka bwenini nilikuwa na shida na wewe, nikawa nimekufuatilia ili nikujuze shida yangu. Nikakukuta na Shamsa, na kutokea hapo nimeshuhudia kila lililojiri baina yenu ingawa sikuweza kusikia maneno mliyokuwa mkizungumza!’’
Unaona? Siku nyingine mtu unaweza kufungwa hivi hivi. Kumbe amenichora A to Z halafu mie nakomaa tu hakuna kitu, hakuna kitu!
“Haya niambie ni tatizo gani?
Nikabakia nikiumauma meno kwa muda nisijue nianzie wapi. Maana haya matatizo mengine wewe unaona tatizo, hali mwenzako haoni kama ni tatizo. Nikaamua kumweleza ukweli.
‘’Tatizo ni Shamsa Akimu, Nampenda sana, tena sana !’’
“Amekukataa? kwa kadiri nilivyoona na ninavyohisi kama sio kufahamu Shamsa nae anakupenda kupita kiasi, kwani bado haujamwambia kama unampenda?”
‘’Bado!’’
‘’Sasa tatizo liko wapi si ungemwita ukamwambia?! We mwambie tu Shamsa zungu yule hana tatizo!’’
“Tatizo lipo hapo kwenye kumwambia!”
“Unaogopa?”
‘’Naweza kusema hivyo, maana naweza kujipanga kwa sasa namwambia nikikutana nae tu nageuka zezeta kama sio bwege. Kujiamini kote kunatoweka na maneno yanakimbia kabisa!’’
Akimu akatabasamu.
‘’Wakati mwingine unapaswa kujiamini Ibra!’’
“Tatizo ni kwamba…” Nikamkumbusha kwa karaha, ’’Sio kwamba sijiamini, najiamini sana lakini ninapofika mbele yake tu ndipo hali hii inapo jitokeza! Unaweza kudhani Shamsa anadawa vile!’’
“Huko unakoenda mbali Shamsa hana dawa. Tatizo liko kwako tu tatizo ni kwamba hujiamini! Hilo tu. Lakini sio lazima umtongoze kwa kuongea nae, ziko njia nyingi za kufikisha ujumbe wako,
Nikazibuka masikio. “Kama zipi?”
“Unaweza kumuandikia barua, ukamnunulia kadi za mapenzi, ukamtumia mauwaridi mazuri yenye ujumbe mzuri na hata kumwandikia sms za mapenzi na ujumbe ukafika, akaelewa na mkawa wapenzi. Shamsa hana ubavu wa kukukataa wewe Yule, sure am telling you!!
‘’Kumbe?!”
“Eeh!’’ Akakubali kwa msisitizo. Moyo wangu ukazizima kwa furaha nikajua naweza kutumia moja wapo kati ya njia hizo, mambo yakajipa na nikaweza kummiliki Shamsa Nuhu moja kwa moja.
‘’Ila’’ Akimu akanizindua tena, “Itakubidi usubiri muhula huu wa mitihani uishe ili usichanganye mapenzi na masomo. Ukianza wewe kuvichanganya vyenyewe vitamalizia, na hupata zaidi ya hasara!’’
‘’Nitasubiri!” Nikamwambia
“Good!’’ Akashangilia baadae akaniambia lile alilokuwa akinitafutia, nami nikampa ushauri alioutaka. Mpaka tunaagana tabasamu lilikuwa bado limeupamba uso wake.
Sehemu Ya 2
“Eeh!’’ Akakubali kwa msisitizo. Moyo wangu ukazizima kwa furaha nikajua naweza kutumia moja wapo kati ya njia hizo, mambo yakajipa na nikaweza kummiliki Shamsa Nuhu moja kwa moja.
‘’Ila’’ Akimu akanizindua tena, “Itakubidi usubiri muhula huu wa mitihani uishe ili usichanganye mapenzi na masomo. Ukianza wewe kuvichanganya vyenyewe vitamalizia, na hupata zaidi ya hasara!’’
‘’Nitasubiri!” Nikamwambia
“Good!’’ Akashangilia baadae akaniambia lile alilokuwa akinitafutia, nami nikampa ushauri alioutaka. Mpaka tunaagana tabasamu lilikuwa bado limeupamba uso wake.
* * *
Usiku ule hali ilikuwa ngumu Sana niliufikiria mlolongo wa maisha yangu, mahusiano yangu na wanawake hatimaye Shamsa “…ndio maana nakupenda Ibra…!” Mvumo wa sauti yake tamu ukatetema akilini mwangu na kuendelea ’’…wewe sio muhuni na hupendi mambo ya kipumbavu!’’
Mambo yepi wakati mie nampenda? Hivi wakati anaongea yale alikuwa seriously au? Sasa kama aliyasema kwa dhati itakuwaje atakapopokea sms yangu ya mapenzi? Atasemaje atakapopata barua au kadi kama sio uwaridi?
Maswali yalikuwa mengi majibu yakiwa haba. Dakika kadhaa zikapita kichwa kikinichemka. Kutahamaki nikawa nimeinuka na kuikabili kabati nikaifungua na kuitwaa albamu ya picha nikarejea nayo kitandani.
Katikati ya albamu ile kulikuwa na picha nzuri ya Shamsa akiwa ufukweni ndani ya mavazi ya kuogelea. Picha hii nilimpigisha kwa wizi baada ya kumuomba mpigapicha mmoja ampige kwa siri na kuniletea picha hiyo kwa malipo ya kutakata.
Vile alipigwa bila ya kuwa na taarifa, alitoka vizuri sana! Rangi yake adimu ya chocolate iliupendezesha mwili wake na kutokeza kwa mng’aro uliovutia hasa katika yale maeneo ambayo ni aghalabu kuonekana wazi hovyo hovyo, ila pale anapoamua kubaki na chupi na sidiria tu.
Vishimo vya kuvutia vya hapa na pale katika kidevu na mashavu yake, miraba miraba mizuri yenye ukubwa wa wastani iliyoizunguka shingo yake na kuikata kata vizuri sana, achilia chuchu zilizosimama vizuri; vilikuwa ni baadhi tu ya vitu viliyoyafanya mate ya uchu yaanze kujaa mdomoni.
Wakati nikiyameza, macho yakashuka chini tumbo dogo na zuri lenye kitovu maridhawa lilikuwa likinisubiri! Mwili ukaanza kupata joto hali mheshimiwa akianza kushtuka, niliposhuka chini zaidi kwenye mapaja. My God! Shamsa!? Acheni niwe zezeta.
Hali niliyoiona pale chini ikayafanya mapigo yangu ya moyo yaende joshi kana kwamba yanataka kuzimika. Yule mheshimiwa kule ‘somewhere’ sasa akasimama barabara kutaka kukagua gwaride la heshima.
Nikatazama mbele ya dressing table yangu kulikuwa na kopo la Rays, sabuni ya Give na Lotion ya E9. Akili ikafanya kazi kuchagua niende bafuni na nyenzo ipi kati ya zile.
Kabla sijachagua, masikio yangu yakanasa kitu. Macho yangu yakageuka haraka kuiangalia TV iliyokuwa humo chumbani. Nikaona polisi wakifanya kuwasukuma watu kwenye Defender. Ilikuwa ile Operation maalum iliyoendeshwa na Mkuu wa Mkoa wa Dare s salaam ya kuondoa machangudoa waliozagaa huku na huko katika jiji la Dar es salaam.
Akili yangu ikapata chaji mpya.
Kumbe kuna mahala ninakoweza kupata tiba muafaka bila taabu, mahali ninakoweza kutibiwa bila kuangaliwa usoni, nikasuuzika mimi na mtima wangu hata nikaona raha na utamu wa dunia.
Bila ya kufikiria mara mbili nikachukua pesa kiasi, nikaweka ndala miguuni na kutimkia stendi. Ilikuwa saa mbili usiku. Nikaparamia daladala moja, baadae nikashuka na kupanda nyingine, niliposhuka nikatemba kidogo nikiuliza hapa na pale, nikiingia kichochoro hiki na kile, hofu ya kukabwa ikawa puani kabisa.
Kutahamaki nikawa nimeibukia nilipopataka
Uwanja wa fisi!
Harufu ya nyama choma ikanipokea, kelele za kanisa hali kadhalika. Katikati kulikuwa na uwanja mkubwa uliosheheni visichana vidogo vidogo vya wastani na wanawake kadhaa ambao mavazi, vitendo na jinsi walivyo walikuwa mwito tosha.
Macho ya wengi wao yalikuwa malegevu mithili ya mtu aliyekula kungumanga. Wengi walikuwa na ndala na miguu yao ilikuwa michafu wenye mchanganyiko wa vumbi masizi na pumba ambazo nyingi zilikuwa zikingali zimeanikwa hadi usiku huo.
“Hoyaaa…!’’ Mmoja akaita.
“Bro!” Mwingine akadakia.
Nikainua macho kuangalia huyo aitwae, mmoja akajaribu kunikonyeza. Nikajikuta nikitabasamu! Sio kwa kufurahishwa na konyezo lake, hasha! Yale macho. Alikuwa na macho mabaya ajabu.
“Twenzetu tuka…!’’ likamtoka neno baya yule wa kwanza. Yule wa pili akajaribu kutabasamu. Likaondokea kuwa tabasamu lililokosa ladha. Zaidi lililochusha na kuudhi. Kicheko kidogo kikaniponyoka.
Vibinti hivi vilikuwa viathirika vikubwa vya madawa ya kulevya. pamoja na kiu yangu kubwa ya ngono, nikavipuuza macho yangu yakasafiri tena na kufanya ziara ndefu katika maeneo anuai ya viwanja vile vilivyolaaniwa.
Muziki mkubwa uliokuwa ukitoka katika baa mbili tatu za kienyeji zilizolizunguka eneo hilo, lile kundi la wachoma nyama ambazo hazikujulikana ni za mnyama gani, walevi waliotamalaki huku na kule wakiyumba, kutukana na kucheza muziki, wacheza kamari, vile visichana vichangudoa pamoja na zile kelele za kanisa kwa pamoja zilipafanya mahala pale sio tu uwanja wa fisi hasa. Bali uwanja wa fujo! Tena fujo lililo chukizo.
Katika kuendelea kuperuzi, nikaona vijana wengi waliokuwa wakiingia na kutoka katika uchochoro mmoja uliokuwa ukipita pembezoni mwa kanisa. Wengi mno.
Pasipo kujitambua na pengine bila ushirikiano maalumu na akili yangu ambayo kwa kawaida ndio mwenyekiti wa mwili wangu, kwa maana ya mfanya maamuzi, miguu yangu ikaanza kurefuka na kupiga hatua ndefu ndefu kuelekea kule kulipokuwa na sumaku iliyokuwa ikiwavuta na kuwatema vijana.
“Sasa vipi mpenzi?” Sauti moja ikaniwahi
’’Mchumba niko hapa, njoo tuyamalize!!” Nyingine ikadakia. Sikuwasikiliza, niliendelea kupiga hatua ndefu kama ninayewahi kitu fulani
“Achana nae!’’ Mmoja akafoka
’’Anawahi kwa wahaya! Angejua kama wahaya ni spare tire! He he he halooow!” wakacheka kishangingi kwa sauti zao zilizo toka mfano wa sauti ya redio yenye betri zisizo na nguvu. Sikuwasikiliza!
Nikaingia katika uchochoro ule. Mungu wangu! nikamudu kutamka. Sekunde chache baada ya kuingia nikatokezea katika mnada wa machangudoa hasa, ilikuwa ni mitaa miwili myembamba sana yenye vyumba vidogo vilivyotazama nje.
Ukingoni mwa kila nyumba, mwanamke mmoja aliketi juu ya stuli au kigoda akiwa na kijivazi kilichoacha nje sehemu kuubwa ya mapaja yake, taa inayoyowaka ndani iliachwa iyamulike mapaja yale makubwa na mazuri na kutufanya wakware kutokwa na mate ya uchu.
Mapaja wazi mtaa wote!
Kazi yako ni kupita mbele ya nyumba hiyo huku ukichagua mapaja yaliyonona kupita yote, huku kila uliyemkaribia akikurabisha kwa tabasamu taamu, tabasamu maridhawa. Nikachoka! nisikuamni macho yangu. ‘’Eeeh Tanznia hii hii, tena Dare s salaam!” Nikawaza kwa mshangao
Nikapiga moyo konde na kupita taratibu nikitazama mapaja hayo kushoto na kulia kwangu, kundi la vijana nilioingia nao katika mtaa huo mwembamba wakipotea mmoja baada ya mwingine kwa zamu na ndani ya vyumba vile na milango kufungwa nyuma yao.
Wakati haya yakitokea; milango mingine iliyokuwa imefungwa, inafunguliwa mmoja baada ya mwingine kwa zamu. Ndani yake wanatoka vijana kama sio wanaume wanaovuja jasho, wengine wakiwa vifua wazi.
Nikaendelea kutembea, kutahamaki nikatokea mtaa mwingine.
Huu haukuwa na vituko, mbele yangu kulikuwa na vijana fulani kama wanne hivi waliokuwa wakitafuta kitu fulani. Nami bila ya kuwaambia nikawa nimewageuza kuwa wenyeji wangu. Nikawafuata kila walipokwenda. Tutukaingia mtaa mwingine.
Huu ulikuwa wa mijimama tipwa tipwa mikubwa yenye maumbo makubwa ya kibantu. Hawa walikuwa ni wazuri maradufu kuliko wale wa awali nikafanya kukaza moyo na kuwapita.
Mtaa uliofuata ulikuwa wa wazee! Hawa sikuwatupia macho japo marambili, nikiwa na wenyeji wangu tukaingia mtaa wa tatu, huu ulikuwa wa mashoga!! nikasikia kinyaa na kutoka mara moja nikawaacha wenyeji wangu wakishughulikiwa katika mtaa huo.
Nikarudi kuzunguka mara ya pili na hatimaye nikajikuta nikiangukia katika mikono ya jimama moja lililokatika kibantu khaswaa ambalo lilikuwa na weupe wa papai bivu.
‘’Mambo?’’ Nikalisalimia
‘’Safi, vipi unataka huduma?’’ Akarembua na kutabasamu, alikuwa na mwanya alikuwa na dimples!! My God, ugonjwa wangu!.
‘’Ndiyo! Nikakubali haraka
‘’Basi karibu ndani!’’ Akafanya kunipisha niingie ndani
‘’Kiasi gani?’’
“We mgeni hapa?”
‘’Ndiyo! Hii ni mara yangu ya kwanza kufika hapa!
’’Si siunataka mapenzi ya kawaida tu?!”
Sikujua mapenzi ya kawaida ni mapenzi gani. Ila kulingana na ukubwa wa mama huyu ambae alinizidi umri kwa kila namna, hali weupe na uzuri wake ukinitisha, nikajikuta nikitikisa kichwa kukubali.
‘’Elfu tatu tu’’ Nikajibiwa.
Nikaingiza mkono mfukoni
‘’Nimekwambia uingie ndani ebo?” Akanikaripia na kuongeza “Kama umetumwa ujue kutuchunguza, sijui kutuchoma ujue hutatoka salama! Tutakupigia kelele za mwizi, wakutwange wakutie mafuta na kukuchoma moto!’’ Akanihitimisha
Nikaogopa na kuruka ndani haraka.
Chumba kilikuwa cha wastani chenye ndoo kadhaa za maji kitanda cha wastani futi nne kwa sita, jiko la mchina beseni lenye vyombo vichache nadhifu na stuli moja tu.
Ukutani kulikuwa na picha kubwa za wanawake wa kizungu walio uchi ambao walikuwa wamelala kitandani katika namna ya kutamanisha kulikovuka mipaka, yule mheshimiwa akaanza fujo tena.
Jimama likaingia na kufunga mlango!!!
Likaondoa kanga kifuani na kile kijisketi kilichokuwa kimemsitiri kwa chini na kubaki kama lilivyozaliwa. Mwanga hafifu uliotoka katika balbu ukimpiga vilivyo katika mwili wake mtepe na kuufanya uwe mwekundu na kuvutia vitamu, jimama likapiga hatua za maringo na kuketi kitandani.
Mkono wake ukazama uvunguni na kuibuka na boksi la kondomu!
‘’Changamka! Hesabu haijatimia, nataka niendelee kula vichwa na kijua ndio hiki nisipouanika nitautwanga mbichi!’’ Nikaelewa nikavua shati, wakati najiandaa kuvua suruali akaniuliza
“Unataka kulala hapa hapa?”
‘’Hapana!’’
‘’Sasa unatoa nguo za nini?’’
‘Nikamshangaa ‘’si tunataka ku…ku…!’’
“Najua’’ akaniwahi kwa karaha ‘’Haina haja ya kuvua nguo shusha tu suruali kidogo kama huwezi kuipitisha hapo katika zipu! Halafu nipe hela yangu kabisa!”.
Nikatoa hela na kumpa nikimwambia “Lakini hapa hatuwezi…”
‘’Ukitaka starehe kamili kaoe! Mimi niko kazini na nilishakwambia hesabu haijatimia hivyo sitaki mizungu!’’
Nikamtumbulia macho
Alipoona simuelewi akanisogelea pale akaivuta chini sarawili yangu na kumkamata jamaa aliyekuwa nusu akilia na nusu akitetemeka akamvisha koti la mvua na kumkaribisha uwanjani akague gwaride.
Hakukuwa na busu, sijui romance wala kunyonyana ndimi. Nikaanza kazi mara moja. Alikuwa fundi wa kuzungusha viuno na kunung’unika. unadhani nilichukua round basi!? dakika zangu mbili unusu tu, ikawa kitu na boksi! Akanitoa kunisukumia pembeni. Kazi ikawa imekwisha.
‘’Ukitaka kurudia je?” Nikamuuliza nikimwangalia kwa matamanio. Kusema kweli nilikuwa sijaridhika hata kidogo.
‘’Haturuhusu! Hapa goli moja, unatambaa!“
Nikamuelewa.
Dakika iliyofuata nikawa nje katika upande mwingine.
Elfu kumi niliyoichukua kwa kazi hii ilibaki elfu saba! Kwa bei ya elfu tatu ningeweza kupata wanawake wengine wawili na kubaki salio la elfu moja ambayo ningelitumia kama nauli na kurudi bwenini chuoni Chang’ombe.
Katika chumba hiki cha pili nikiwa na mwanamke mwingine tena nilikuwa nimeshakaa kifuani kwa zaidi ya dakika tano pasipo jibu kuonekana, ndipo mambo yalipoanza kwenda mrama.
‘’Changamka bwana muda wako umeisha!’’ Alinihimiza nikazidisha spidi. Dakika zingine tatu yule mama akanisukumia pembeni na kuliangalia koti la baridi alilonivika akidhani namuongopea.
‘’Alipokuta halijaloa akaniangalia vizuri na kunitwanga swali
“Umeshatoka kupata sehemu nyingine siyo?”
‘’Ndiyo!” Nikamjibu.
Akaachia mfyonzo mrefu uliotoka vizuri haswaa. Halafu akainuka kwa ghadhabu na kuvaa nguo zake, alipomaliza akaniambia “Haya toka!’’
‘’Lakini hatujamaliza bado!’’
‘’Tumemaliza umeniongopea kuwa hujapata kumbe umeshapata toka nakwambia!’’ Sasa alinifuata na kuniinua pale kitandani.
‘’Hatukuongea hivyo!’’
‘’Toka nitakupigia kelele za mwizi!’’ Sauti yake haikuwa ndogo, alikuwa akipayuka.
“Basi nipe chenji yangu nakudai elfu mbili, nimekupa elfu tano!’’
“Elfu tatu ni dakika tatu wewe umetumia kumi! Nikingali nakudai elfu tano!” Akabweka.
Nikachoka. “Haiwezekani!” Nami nikapandisha na kukomaa. “Lazima unipe chenji yangu’’
Akaufuata mlango na kuufungua nje kulikuwa na shehena ya kutosha ya watu, Baadhi wakitaka kujua kulikoni wengine wakipaza sauti nikomeshwe! “Betty mtoe fasta tumjeruhi!” Sauti kutoka nje ikaomba.
Akanivuta na kunisukumia nje akawageukia wale wanawake na kuwaambia “Alitaka kunitumia dabo dabo bila malipo!”
kufikia hapo moyo ulikuwa ukinipiga vibaya nikijua sasa ndio naadhirika. Kwa ajili ya ngono! Nikawaza kwa uchungu. Maana sikupewa hata nafasi ya kujieleza.
Pale nje nilipokelewa kama mpira wa kona, nikatukanwa matusi ya kila aina waloweza kunitia singi walinitia, walioweza kunipiga na viatu na makopo ya mkojo pia walifanya hivyo.
Mara wakatokea watoto kadhaa machokoraa wakanikwapua kama kipanga na kunipeleka mahala walipopaita Chakabovu! Kule wakanisachi na kunipokonya kila nilichokuwa nacho.
Simu, fedha kidogo, viatu, kofia! Halafu halafu wakaniambia nipotee!
Niliondoka roho ikiniuma na nikiwa nimewachukia wanawake wote wa Uwanja wa fisi. Niliwachukia isivyo kawaida. Kutoka pale Manzese Bahresa hadi magomeni makonda waliweza kunielewa na kunipa lifti.
Lakini kutoka Magomeni hadi Chang’ombe hawakunielewa ikanilazimu nitembee kwa mguu kutoka Magomeni baada ya kuona masaa yakiyoyoma bila kupata lifti. Nilifika chuoni usiku nikiwa hoi bin taaban.
Siku ya pili sikuingia darasani nikabaki bwenini nikijisomea na kuuguza majeraha madogo toka kwa wale machangu pamoja na machokoraa wao.
Jioni Akimu na Shamsa walikuja kunitazama na kunipa pole. Nikajisingizia ugonjwa. Shamsa akanisisitiza kwenda hospitali kuangalia afya pengine nina malaria
‘’Nitakwenda!’’ nikawaambia kuwapa moyo.
* * *
Miezi kadhaa baadae nilishaweza kuyasoma mazingira na kwenda nayo sawasawa. Niligundua kuwa uwanja wa fisi sio mahala pa’ kwenda na fedha nyingi, simu ya kifahari, mavazi mazuri sana na kadhalika.
Sio mahala pa’ kusema utapata bao mbili kwa mwanamke mmoja. Na muda wa kuwa na mwanamke kitandani usizidi dakika kumi,
Niligundua pia kuwa yako mamia kwa mamia ya wanaume wanaofuata ngono za bei raisi katika maeneo hayo kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Dar es Salaam ambapo hapo hakuna haja ya kutongoza.
Hakuna pia kuombwa hela ya vocha, Saloon, hela ya mtindo mpya n.k pale ni mahala pa’ kulipa, kupata huduma utakayo na kutoweka! Mahala pa nipe nikupe.
Niligundua pia kwa siku moja pale mwanamke ambae mapato yake sio mazuri hulala na angalau wanaume kumi kwa siku na kupata elfu thelathini! Wale wenye mapato mazuri hupata wanaume kati ya ishirini na ishirini na tano kwa siku.
Hawa pato lao kwa mwezi lilifukuzia pato la mafisadi kwa karibu tu kwa vile ni kati ya milioni 1.2 na milioni 5, ambapo pia nao hulazimika kulala na wanaume 600 hadi 750!
Unashangaa nini? Wewe endelea tu kuhudhuria huko uwanja wa sifa kama ibada ujue hauko peke yako.
Niligundua mbali ya walevi, wanywa pombe na wabwia unga; wapo baadhi ya wanawake ambao wamelitumia pato hilo kwa kujenga makwao kusomesha watoto na n.k.
Niligundua tena kuwa wengi walikuwa ni waathirika wa ukatili wa kijinsia ambao uliwakumba katika familia zao na mikondo ya maisha waliokuwa wakiishi.
Wengine ndugu zao wa kiume walikuwa wamewadhulumu mali za urithi walioachiwa na wazazi wao, wengine walikuwa yatima walioondokewa na wazazi wao na kukosa mtu wa kuwaangalia! Wengine walikuwa wametupwa na wazazi wao baada ya kuzaliwa wengine… wengine!
Basi ilimradi kulikuwa na mlolongo wa matatizo ambayo kwa hakika yalichusha na kuudhi.
Hofu ya ukimwi je?
Walikuwa nayo lakini wangefanyaje? Waliona bora waishi kwa furaha leo kwa kuwa hata kesho wasipokufa kwa ukimwi kama watajitunza, basi watakufa kwa njaa, umasikini na adha zingine kadha wa kadha.
Ugunduzi huu ukanifanya nisiwatizame kwa jicho baya tena, bali nikawaona kama wahanga fulani hivi!
Nikajitengenezea utaratibu mzuri wa kwenda pale na kuhudumiwa mara nne kwa wiki! ulikuwa utaratibu nilioupenda na kuufuatisha kama ibada, utaratibu mtamu kweli, mtamu haswaa.
* * *
**IBRA keshagundua mambo kadhaa juu ya Uwanja wa fisi…sasa amejiwekea utaratibu wa mara 4 kwa wiki…….HATARIII…
INAENDELEA

