HAYA MATESO NINAYO PITIA MUNGU NAOMBA ULEGEZE KITANZI
Mimi na mume wangu tumebarikiwa watoto wa 2 japo mimi alivonioa nilikua na watoto wawili teali kwaiyo mimi nimezaa na mume wangu huyu mpya watoto wa 2 ukichanganya na wakwangu wanakua wa 4
Kwakweli mwanzoni alikua anawapenda sana wanangu Ila nilipozaa naye tu huyo mtoto ndo ikawa chanzo cha kuwachukia wanangu Mala nyingi tukigombana alikua ananiambia niwapeleke kwa baba yao
Sasa basi huyu mume wangu kidogo uchumi wake upo vizuri ni mpambanaji sana sasa aliongea na mimi kuhusu kuongeza mtoto wa pili nilikubali maana nilikua nampenda sana japo toka nizae nae mtoto wa kwanza nikama alibadilika Ila niliona labda majukumu yameongezeka
Kweli nilimzalia mtoto wa pili apo ndo niliona roho mbaya ya huyu mwanaume yaani anaweza Kuja na chipusi mayai na chipusi kavu watoto wake anawapa chipusi yai na wanangu anawapa kavu aiseee nilikua naumia sana mda mwingine alikua anakuja na pikipiki anawabeba anaenda nao kuogelea huko wakirudi wanasimulia kila kitu kwakweli alinifanya nianze kumchukia huyu mwanaume
Watoto wake aliwanunulia baisikeli Ila wakwangu hakuwanunulia nilimuuliza mbona unabagua akaniambia hao watoto Wana baba yao kwaiyo hapo nilipo walea inatosha sasa warudishe kwa baba yao aiseee majibu haya yaliniumiza sana nililia sana
akawanunulia mpka simu zile za kuchezea Game Ila wangu nikama aliwatenga sana nikimuuliza mbona hivo we mwanaume unaroho mbaya habijibu anawabeba watoto wake anaenda nao kutembea kwa kweli nilijisikia vibaya sana mpka pale niliona nifanye maamuzi ili tuishi kama mwanzo na niliwaza kuwa Hawa watoto nisipo waondoa siwezi Lea watoto wangu. Kwa furaha nilienda kununua sumu nikawapa Hawa watoto nilie zaa nae mume wangu wa sasa ili niondoke na watoto niliozalishwa ambao alikua hawapendi kwaiyo niliweka sumu kwenye juice
Pia nilikua najua PIN ya dro ya kuwekea pesa nilichota pesa yote milioni 4 nikatokomea huku nikimuachia mizoga ya watoto wake aendelee kuwa penda na kuwanunulia vitu vya thamani
Kuja kwenu ni hivi ni miaka mi tatu sasa imepita kwakweli ukisikia damu ya mtu ni mbaya ukiimwaga yamenitokea mimi tangu nifanye tukio hilo uzao wetu watoto wakiume wote nishawazika hata na watoto wangu pia nimewazika juzi Kama ni kwenda makanisani nimeenda sana na kama ni Toba nimefanya sana ila haikubadilisha matokeo ukoo wetu umeisha watoto wa kiume wote nikajifunza kitu usimwage damu ya mtu wala kwenye hii dunia usilipize kisasi moyo wangu umejawa na huzuni na machozi yasiyo Isha

