KAKA KAKA KUMBUKA MIMI NI DADA YAKO
PART 16
👉 dah kilichoendelea jamani dah yani…👇
Mikono yake ikawa inavuka mpaka sehemu ya mgongoni inafika kiunoni yani ananiminya kiuno mimi.
Jamani nasikia raha.
Sasa natamani animinye na matuta yangu yani naisi nitasikia raha zaidi.
Mimi niliacha kumchezea nikawa nasikilizia utamu naousikia.
” Basi aliniminya kama dk 20 mimi nikasikia aja ndogo nikaenda kujisaidia jamani wakati nanawa naona utelezi kwenye sehemu zangu za siri mbele.
Nikasema jamani ule mchezo mtamu ila nitamuomba anioe awe mwanaume wangu wa kwanza kunifungua bikra na aniingize kwenye ulimwengu wa mapenzi nishampenda tayari.
Nikaludi namkuta usingizi ushamkamata na mimi nikalala nikajifunika shuka.
” Sasa upande wa kaka na mkewe kwa kitendo walichofanyiwa kaka anaona aibu kweli kweli wao wenyewe wakashauliana Wauze nyumba.
Wahame kabisa kwenye huu mji kwa aibu.
” Sasa kumbe yule mwanamke wake ni mtoto wa mjini kashapanga wezi siku nyumba ikiuzwa ata mshauri kaka walipwe keshi selekali za mtaa.
Sasa kitendo cha kutoka selekali ya mtaa kwenda benk hapo njiani ndio kinuke.
Yani lugha nyepesi tukio lifanyike la wizi yani njama inapangwa na mkewe kaka ajui.
” Sasa kaka biashara zake ni kuuza duka kwa tukio lile akawa anaona aibu kwenda kufungua duka lake akaanza kuliuza duka ilo pesa kaludi nazo anasubiri auze nyumba achanganye pesa zote apeleke benk.
” Sasa upande wetu siku ya pili tunaenda kuchukua zawadi kwa tajiri.
Sasa tajiri kumbe alisambaza lile somo kwa matajiri wenzie.
Na wenzie wakaona ni fursa.
” Kaka chizi anafika pale anaambiwa atapewa zawadi alizoaidiwa na atapewa mkataba wa kazi awe anafanya masomo yake kwenye kongamano tofauti tofauti akaulizwa je unajua mambo ya kikilisto maana kongamano linakusanya dini tofauti.
” Kaka chizi akasema vyote vipo kichwani hapa.
” Wale matajili wakasema tupe moja la kikilisto.
” Kaka chizi akaanza moja kwa moja yani aina kuangalia kitabu akasema…👇
MACHACHE KUHUSU MT.YOHANE PAULO II.
1.Mmoja ya viongozi waliosafiri zaidi duniani kwa shughuli za kimisionari.*
alisafiri zaidi ya nchi 129(zikiwemo Tanzania na Uganda).
2.Alikuwa Papa wa I asiye muitaliano( anatoka nchi ya Poland).*
3.Alinusurika kufa kwa kupigwa risasi, kwa msaada wa Bikira Maria akapona.(1981)*
4.Ni mmoja ya Mapapa waliodumu kwenye madaraka kwa kipindi kirefu zaidi.* Wengine ni Papa wa I, Mt.Petro aliyehudumu kwa miaka 37, Papa Pius IX aliyehudumu miaka 31 na yeye Papa Yohane Paul II aliyehudumu miaka 26.
5.Alipokea Sakramenti ya Kitubio kutoka kwa Padri Pio,* ambaye alikuja kumtangaza Mtakatifu baada ya miaka 55.
6.Ni Papa wa kwanza kutembelea Msikiti*(Omayyad mosque- Damascus.)
7.Kauli mbiu yake ilikuwa “Totus Tuus” maana yake “Yote ni Yako”.
Karibuni nyote kwa chochote mnachokumbuka kwa Mtakatifu huyu.Leo ni siku yake, karibuni tuindee haki.
” Wote walikaa kimya kwa ajabu walisema wewe ni kichwa meneja wa kazi zako unataka awe na nani?.
” Kaka chizi akasema meneja wake nitakuwa mimi.
” Matajiri wakasema meneja kwanza unatakiwa uwe na nyumba Kari sema wapi unataka ununuliwe nyumba iwe yako uwe unasimamia kazi za uyu kwa utulivu zaidi.
” Jamani mimi nikasema nyumba ile ile anayouza kaka nataka iwe yangu.
” Jamani likapitishwa kesho naenda kukununuliwa.
Kaka chizi akaingia mkataba pale vizuri na pesa alipewa akafungua akaunti akapeleka benk.
Sasa tukaludi hotelini.
” Jamani nina furaha nikaona kaka chizi kashanipa mwanga mpya kwenye maisha yangu sasa Leo natamani nimwambie aniingize kwenye ulimwengu wa mapenzi jamani nampenda sasa.
” Kaka chizi akaniuliza Leo utaki nikukumbatie.
” Nikamwambia nataka ila naona aibu kukwambia kila siku naisi umechoka.
” Akaniambia wala sijachoka njoo nikukumbatie.
” Nikamwambia kaka mimi nataka unikumbatie kama ulivyonikumbatia Siku ya kwanza.
” Kaka chizi akakumbuka akaniambia aya vua nguo uvae shati uje juu ya kifua.
” Jamani mimi nataka kitu kwa kaka chizi nishampenda nikavua nguo nikavaa shati nikatanua miguu nikaenda kumlalia kaka chizi juu.
” Jamani namwambia mgongoni kunawasha.
” Akaanza kunikuna mgongoni nikamwonyesha muwasho umefika mpaka kwenye matuta.
” Jamani akapeleka mkono kwenye matuta yangu.
Sasa ananikuna kwa kuniminya minya.
Mimi nimefumba macho nasikia raha sana.
” Namsikia kaka chizi anasema zakia naomba nikufanye…
PART 17
👉 Nasikia kaka chizi anasema zakia naomba nikufanye..👇
Uwe mke wangu naisi kuwa wako ndani ya moyo.
” Mimi nilidhani anataka anifanye sasa yani aniingize kwenye ulimwengu wa mahaba ya kikubwa.
Nikawa namwambia kaka mimi sijawai kufanya ata siku moja.
” Kaka chizi akasema dah utakuwa umetimiza ndoto zangu mimi nataka niwe wa kwanza kwako na nisikuonyeshe uchungu wa mapenzi nakupenda unanipenda?.
” Jamani nasema bila uoga.
Nakupenda na mimi.
” Kaka chizi akasema sawa unajua toka nikusaidie wewe na ndio Mungu kaninyanyua mimi nina mda mrefu natoa masomo misemo sijawai PATA kuinuliwa kama ilivyo kuwa ivi.
Sasa basi naomba kesho twende ukanunue ile nyumba ya kaka yako kama walivyosema arafu naomba twende kijijini kwenu tukatembelee makabuli ya wazazi wako vile vile nikutane na baba yako mdogo na mjomba wako wewe nikuoe kisheria uwe mke wangu.
” Nilimwambia sasa baba mdogo na mjomba si maadui zetu mimi na kaka.
” Kaka chizi akasema ayo tunafanya atuyajui nachotaka mimi wanipe ndoa wewe unaona kama anakupendi kwenye uzima tu mfano japo sio mzuri wewe ufe ndani ya hii hoteli yule kaka yako anakuwa wa kwanza kunishitaki.
Wale baba yako mdogo na mjomba wako wanaungana kwenye kunifunga mimi.
Waswahili wanasema nyoko nyoko ya kuonana.
Sasa naomba ndoa yetu tukafunge kwenye kijiji chenu my sawa.
” Nikamwambia sawa.
” Akaniambia my naomba ulale tusimuuzi mungu tukaja kuzini wewe ni wangu ndoa inakuja nakula tunda kwa halali.
” Nikamwambia sawa.
” Basi tulilala.
” Kesho yake nyumba ya kaka ikanunuliwa.
Na kaka akapewa pesa yake akaondoka kwenye ile nyumba.
” Sasa makabiziano ya nyumba kuwa yangu kaka ajayaona.
Ayo yalikuwa kwenye uongozi wa matajiri.
” Sasa kaka anapanga mipango ya kwenda mbari na mji huu yani akaanzishe maisha mapya bila kufikiria ile pesa na mimi nausika.
Afikirii mimi nipo wapi nafanya nini je akiondoka itakuwaje.
Yeye anafikiria maisha yake.
” Upande wetu mimi na kaka chizi ndio tushapewa nyumba yani ushakuwa yangu.
Na kaka chizi ambaye sasa ndio mchumba wangu uongozi ukasema atoe somo moja ambalo litachukuliwa na kurushwa kwenye vyombo vya habari.
” Kaka chizi akakaa mbele ya camera akatoa somo hili…👇
Endelea kumwambia mwanao kuwa ile kauli isemayo ‘tone moja la ubaya huchafua bahari ya wema’ ni ya ukweli na pekee aiamini asilimia 100. Akikuuliza kwanini?
Mwambie amtazame vizuri Golikipa katika mchezo wa mpira wa miguu ⚽, bila kujali ataokoa hatari ngapi, bila kujali atacheza kwa juhudi kiasi gani ila mwishoni mashabiki watamlaumu kwa goli moja alilofungwa.
Asipokuelewa usimshangae, yawezekana akili yake bado haijapevuka hivyo mfafanulie kuwa.
Ana uwezo wa kutenda mema kwa moyo wake wote mbele ya wanadamu, lakini siku akija kukosea kitu kimoja basi watasahau yote aliyowahi kuwatendea hapo awali.
Tafadhali usisahau kumwambia kuwa aache majivuno na kujiona fahari katika mgongo wa dunia hii, maana bila kujali Mungu kaumbaje viumbe wake ila kila kiumbe kina kikomo chake. Eeh! Ndio maana tunazaliwa tuna miguu miwili, lakini hatuwezi kukwea miti miwili kwa wakati mmoja.
Najua hii hatoilewa vizuri, wala usiwe na shaka. Mueleze tu taratibu kuwa, Mungu katuumba na uwezo wa tofauti kwa kila kiumbe ila lazima kuwe na kikomo chetu.
Na ndio maana hata kinyonga ana rangi ya kumfanya ahimili kila mazingira, lakini siku msitu ukiwaka moto 🔥 kinyonga lazima ataungua maana hana rangi ya kumfanya ahimili moto.
Akiwa bado anawaza hilo☝ we endelea kumhusia kuwa, awe na shukrani na roho ya kuridhika kwa kila kidogo apatacho. Yaani hata kama ana kiu yenye kuhitaji lita nzima ya maji, ila kila apatapo tone moja ni lazima ashukuru maana wapo tayari waliokufa kwa kiu .
Mwambie mwanao kuwa asipende kubishana na wanadamu kwa kila kitu, kwani maisha si mtihani wa mashindano.
Msihi tu saa nyingine kuna faida kubwa kwenye kujishusha kuliko kujaribu kushindana kwa kila kitu… Akikuuliza kivipi?
Muache na hii kauli kuwa👇
“Nyani aokotapo jiwe akamrushia, kisha na yeye akaliokota kumrudishia wote wanaonekana manyani.
” Jamani uongozi mzima walicheka wakasema hapa ichi kichwa.
” Basi upande wa kaka ndio wanaenda kupeleka pesa benki ajui mpango mbaya juu yake.
” Gali walilopanda yani tax lilikuwa ndani ya mpango kaka anashangaa deleva wa tax ile kapeleka sehemu gali wamepanda watu wawili.
Arafu wamewekewa midomo ya bunduki.
Yeye na mkewe.
” Jamani walipelekwa mbali arafu wakavuliwa nguo wote yani mwanamke anajifanya kama ayupo kwenye mpango vile.
Kupigwa anapigwa kaka mwanamke anaguswa guswa.
Arafu walichofanya wakamshusha kaka akiwa uchi wa mnyama uku wanasema uyu mwanamke wako tunaenda kumbaka.
” Maskini kaka ndio kashaachwa ivyo na umaskini mbaya ata nguo moja ana na mkewe ndio wanaenda kugawana pesa ivyo.
” Kaka akili zilimluka alipiga kelele kama mweu uku kashika kichwa cha juu cha chini kinaning’inia.
” Wanawake sio wastaharabu wanacheka wanavyomuona wanasema jamani wake za watu sio kitu cha kuchukua jamani muoneni uyu mkaka wa watu anavyofedheeka.
” Jamani wabongo kwa kutunga stoly kwenye tukio wapo sawa sana hapo yani washa mtengenezea tukio lake.
Kaka ajui chochote kashachanganyikiwa.
” Wanaume wakamstili wakampeleka hospital.
Jamani akawekwa wodi ya vichaa ajitambui yani mstuko mkubwa aliopata umefyatua mpaka akili.
” Sasa tahalifa zimenifikia mimi.
” My wangu ananiuliza je utamsaidia kaka yako lishampata la kumpata aliniita mimi chizi sasa yeye yupo milembe mimi nipo na wewe mtaani nani chizi?.
Sasa je utamsaidia?.
” Dah nikiwaza alichonifanyia jamani jamani dah yani….
PART 18
👉 dah nikiwaza alichonifanyia jamani jamani dah yani..👇
Nilimwambia mchumba wangu mimi namsamehe kaka yangu tupo wawili tu tulioachwa na wazazi wetu.
” My wangu akasema sawa iyo ndio akili na unajua kuna usemi huu..
Ni heri kufa mwili hautosikia wanayoongea, kuliko kufa moyo, unakuwa maiti inayotembea.
Huu usemi ni mkubwa sana maana kaka yake alikufa moyo na amekuwa maiti inayotembea sasa kaka yako yupo sehemu salama twende kijijini kwenu tukafunge ndoa arafu tuje tuwashughulikie kaka yako na dada yangu wote ni wagonjwa wa akili ila wapo sehemu mbili tofauti.
” Basi tulienda kijijini.
Jamani tunafika kijijini tunakuta kuna mpasuko mkubwa yani mjomba na baba mdogo wameweuka.
Wameshaongea ubaya wote waliofanya juu ya familia yetu.
Sasa kijiji kizima wamewatenga na wamesema awa wana lana.
” My wangu akaongea na wazee wa kijijini na kuwaambia awa walikuwa ni wafuasi wa shetani na shetani ana urafiki wa kudumu kwenye maisha ya binadamu.
Naomba tuwapate watu wa dini wafanye dua na maombi mungu atawapa njia salama.
” Wazee walisema ngoja tumuulize zakia kwa kitendo walichofanya mjomba na baba yake mdogo anawasamehe.
” Mimi nilisema nishawasamehe.
” Basi walifanyiwa dua kubwa na maombi atimaye mungu amejibu wamepona.
Wale wazee walinipa shamba ndani ya kijiji kile nilichozaliwa nimeludi tena na kumiliki shamba.
Wazee wote waliudhulia ndoa yangu na mjomba na baba mdogo waliniomba msamaha na wakawa ni watu wa kuswali na kuomba msamaha mbele ya mwenyezi mungu.
Wao ndio wakawa wafagiaji wakubwa kwenye makabuli ya wazazi wangu.
” Tuliludi mjini tulienda kwa mashekhe na wachungaji walifanya dua na maombi.
Kaka na dada wa mume wangu wakapona.
” Kaka alilia kama mtoto mdogo alipokumbuka aliyonifanyia.
” Dada wa mume wangu na yeye alilia kama mtoto mdogo akikumbuka alivyomfanyia kaka yake.
” Kaka akimwangalia mume wangu anazidi kumuomba msamaha maana anakumbuka jinsi alivyomjibu.
” Mume wangu akamuuliza unakumbuka kauli gani ambayo itakuliza ambayo zakia alikwambia.
” Kaka akasema nakumbuka kauli hii..
KAKA KAKA, KUMBUKA MIMI NI DADA YAKO.
“Mume wangu akamwambia aya basi kuwa mtu wa amani na hii nyumba utakaa wewe japo si yako ila ndio nyumba uliyoizoea kupitia maisha uliyoishi itakuwa funzo kwa watu wengine wenye kudhalau ndugu zao kisa mapenzi.
Na vile vile dada yangu utaenda kukaa kwenye nyumba hile yangu.
Mimi na mke wangu tunaenda kuishi kwenye Fukwe uko ya bahari kwa sababu kazi yangu inaitaji utulivu hili niweze kuhelimisha jamii nawatakia maisha mema.
” Mimi sasa naondoka na mume wangu kwenda kuishi sehemu yenye utulivu na ndugu zetu wakawa shamba darasa kwenye jamii.
Nawaomba tuwe makini sana kwenye ndoa zetu na usihukumu ndugu yako kwa hila.
Usiloge ndugu yako kwa sababu ya Mali.
Ushirikina si kitu cha kukimbilia nawaomba sana tuwe watu wa kuabudu mungu.
* MWISHO*