KAKA KAKA KUMBUKA MIMI NI DADA YAKO
PART 11
👉 Alinikata mtama huo dah yani…👇
Nilidondoka chini kaka akanyanyua juu mguu anataka anikite na mguu wa tumboni.
” Mimi nikabimbirika ndio ikawa nimejiokoa yani nimekwepa ule mguu.
Kaka akakita chini.
” Akaniambia nitakutoa mavi mshenzi mkubwa wewe unadiriki kumpiga mke wangu.
” Jamani moyoni niliumia mimi yani uyu mwanamke kasababisha mimi nifanyiwe ivi na kaka.
” Jamani kaka akanivuta akaenda kunifungia kwenye tundu la kuku.
” Yani niliumia sana nikawa nawaza msaada nitapata wapi mimi wa kunisaidia kupata aki yangu hii nyumba kaka ajajenga kwa pesa yake.
Ni pesa ya ulithi wa wazazi wetu.
” Jamani kaka akanifanyia ukatiri mkubwa sana alinifungia mlango yeye na mkewe wakaenda kula bata.
” Jamani mavi ya kuku yananuka mimi ndio nipo kwenye banda la kuku mpaka sasa sijui saizi saa ngapi naona giza na mmbu wananing’ata mimi nalia tu.
” Nasikia kaka amerudi na mkewe wanaongea maneno mabaya juu yangu.
” Mke akasema uyu dada yako amekosa heshima kabisa na wewe kwa sababu inawezekana kashapata bwana nje makamo yako ndio maana anakuchukulia wewe poa.
” Kaka anasema kwaiyo sasa unasemaje tumfanyaje uyu maana mimi sijapenda tabia yake kabisa.
” Mke wa kaka akasema mfukuze aende akakae kwa bwana ake uko yeye si kakua.
” Kaka akasema sasa subiri usiku sana ndio nimfukuze saizi si unaona uwanjani pale watu wamejaa wanamsubiri chizi yule anayeongea ongea aongee arafu watawanyike.
Subili wakitawanyika tu watu saa Saba tunamfukuzia mbari.
” Jamani naumia moyoni nikiona kaka yangu kasaau mimi ni dada yake Leo anapanga mipango mibaya juu yangu inauma jamani inauma nikawa nalia uku najua usiku nafukuzwa na sijui nitaenda wapi?.
” Sasa chizi alifika kwenye huo uma wa watu mimi nilikuwa natamani chizi aongee mpaka asubui hili mimi nisitolewe umu ndani.
Ila ndio aiwezekani lazima aonge amalize watu watawanyike.
Chizi aliwapa somo hili wale watu…👇
NAKWAMBIA..
______________
“Uhuru wa kuamua maisha yako yaweje upo mikononi mwako, usikubali wakuamulie kwakua wanaangalia faida upande wao katika kile watachokushauri. Kwani katika maisha yako washauri ni wengi na ukiwatazama hawana tofauti na wachezaji wa kinyenga ambao hukithamini tu pindi kinyenga, kikiwa kipya kikichakaa wanakitupa. Hata wao watakushawishi na kukushauri ufanye jambo fulani ILA ukikosea tu! watakutenga”
” Jamani akatoa na somo hili..👇
Jihadhari na kuwadanganya wanawake kwani wana uhodari wa kujua ukweli na uwezo mkubwa wa kujifanya hawajajua
mwenye kupoteza penzi la mwanamke muaminifu, basi amepoteza maisha yake yote.
” Mimi moyoni masomo yale ayana msaada kwangu ni kwa ao waliomzunguka chizi na chizi akasema natoa somo la mwisho.
” Moyoni nasema sasa ndio muda wa mimi kutolewa kama mbwa unakalibia maana chizi anamaliza somo la mwisho watu watawanyike.
Chizi akamaliza na somo hili…👇
Unaweza kuwa na furaha na ukalia. Unaweza ukawa na huzuni na ukatabasamu. Kinacho onekana kwa nje wakati mwengine
Huwa hakina mahusiano na kile kinacho endelea ndani.
” Yani nilitamani aweke somo refu ila ndio wapi kapiga fupi walio kuwa kwenye mkusanyiko wanajua maana ya masomo ayo.
” Watu wakatawanyika sasa.
” Jamani kaka kwa mikono yake ndio kaja kunivuta kwenye banda ananitoa nje usiku saa 7.
” Mimi namwita kaka kaka umejisaau mimi ni dada yako.
” Kauri ilimuuzi mke wake jamani mke wa kaka akanivua nguo zangu anasema toka nenda kwa bwana ako akakununulie na nguo wewe si jeuri.
” Jamani nilidhani kaka atanitetea udhalilishaji anaonifanyia wifi.
Nashangaa kaka ndio kachana brauzi yangu.
Mkewe kachana sketi yangu.
Na akanitoa mpaka nguo ya ndani akanisukuma nje nikiwa uchi kabisa.
” Jamani jamani dah dk 2 NYINGI vijana wa kiuni wakanikamata.
” Wakawa wanasema dah mtembea bule si sawa na mkaa bule jamani tumepata nyama mbichi yani Leo FULL raha.
” Jamani wananinyanyua mmoja wao akanishika matuta yangu.
Dah wanapanga kunibaka mimi yani…
PART 12
👉 Dah wanapanga kunibaka mimi yani…👇
Sasa kabla awajafikia dhamira yao mbaya kwangu.
Chizi anatokea ananiokoa mimi jamani.
” Wale vijana walikimbia mbio.
Chizi akavua shati lake akanivalisha mimi kama sketi lakini juu maziwa yapo wazi.
” Akaniambia twende nyumbani kwangu ukaniambie yaliyokusibu.
” Nikaenda na chizi mpaka anapoishi kwake chumbani kwake kuna godolo la mwanafunzi na neti tu akaniambia aya kaa hapa uniambie mwanzo mwisho.
” Jamani nilikaa kwenye kile kigodolo nimeziba maziwa yangu uku naongea sasa mwenyewe mwanzo wa maisha yangu mpaka pale nilipofikia.
” Chizi alilia sana arafu akanipa picha.
” Sasa mimi ili nipokee picha inabidi nitoe mkono mmoja kwenye maziwa yangu.
Ilibidi nitoe mkono mmoja nipokee picha tu ambayo ata sijui maana yake.
Naona picha ya mwanamke.
” Chizi akaniambia unaona iyo picha uyo ni dada yangu.
Sasa acha nianze na kuichambua stoly ya maisha yako.
Wewe mjomba wako na baba yako mdogo wanausika kabisa kwenye vifo vya wazazi wenu wewe na kaka yako.
Sasa nia yao ni Mari za wazazi wenu ila kaka Yako akauza Mari zile akawaalibia mipango yao.
Wakaamua wamloge kaka yako akubake wewe hili akikupa mimba mpate aibu ndani ya hili jiji.
Sasa uyo mama mage alikuwa mkombozi kwenu ila waswahili wanasema kizuri akidumu usemi umetimia kwenye maisha ya mama mage baada ya kuwaokoa nyinyi yeye akafa.
Sasa narudi kwenye iyo picha uliyoshika arafu nitakuja kwenye maisha yako ya kaka yako ya sasa ivi.
Uyo ni dada yangu na mimi kama nyinyi wazazi wetu walikufa.
Sasa tumezaliwa wawili dada akataka tuuze nyumba kila mtu awe na 50 zake.
Mimi nilimwambia dada wewe utaolewa na mume si ndugu yako je tumeuza nyumba umeachwa kwenye ndoa yako utaenda wapi.
Tuache nyumba hii iwe kimbilio letu labla mimi naweza kuumwa hapa ndio niwe naugulia.
Sasa kumwambia dada yangu ayo ndio akaona sasa kaka ananibania mimi maisha ya kula bata.
Dada yangu uyo akaenda kwa mganga kuniloga niwe chizi ili yeye awe na uwezo wa kuamua juu ya hii nyumba.
Na kwanini kawa na nguvu ya kuniroga nyuma yake kuna kitu kinaitwa mapenzi yani alikuwa na bwana ndio alimshawishi huo ujinga.
Sasa tunafunika stoly yangu nakuja kwa kaka yako.
Yule kaka yako kwa sasa ajarogwa ila ichi kitu kinaitwa mapenzi ndio kakivamia kwa pupa kinamfanya awe mnyama juu yako yani pale anajiona yupo sawa kukutesa wewe kumfuraisha mkewe amesaau wewe ni dada yake.
Sasa nakurudisha tena kwa dada yangu na yeye alijiona yupo sawa kuniloga mimi kumfuraisha bwana ake.
Sasa mimi mganga aliyemfata akaja kuniambia kwa sababu ajajua tu yule mganga ni rafiki yangu.
Na mganga akaniambia wewe mimi siwezi kukuroga ila naomba uwe chizi kwa muda hili dada yako afurahi na maisha yake auze nyumba pesa nitamwambia alete kwa mizimu arafu nitakupa wewe asilimia 75 ya pesa yeye nitampa asilimia 25 tu azitamsaidia chochote wewe pesa yako utanunua nyumba.
Sasa mimi kwa sababu dada kafikia atua ya kutaka mimi niwe chizi kwa sababu ya Mari nikasema moyoni kama angeenda kwa mganga nisiyemjua si ningekuwa chizi kweli.
Sasa nilianza kuwa chizi uku najitambua nimeamua kuwa chizi misemo.
Dada aliuza nyumba na akapeleka pesa kwa mganga nakwambia siri yangu wewe mimi mganga alinipa kweli pesa na nikanunua hii nyumba.
Na mimi nimekaa chumba ichi cha uwani naishi maisha ya kama chizi kweli.
Dada uyo pesa alimpa bwana ake na bwana ake alikimbia na pesa zote sasa yeye ndio karukwa na akili kweli kweli.
Mimi sio kama siwezi kumsaidia dada yangu matatizo aliyonayo ni chizi kweli kwa msongo wa mawazo.
Mpaka anaongea mwenyewe nimemloga kaka yangu analopokwa ovyo ila nimemuacha ili wengine wajifunze kupitia yeye.
Mapenzi yasifanye uwe katili kwa ndugu yako.
Mimi nachofanya kumlinda asibakwe na wauni tu ndio maana unaona saizi natoka kumwangalia yeye usalama wake.
Yupo kwa babu mzaa mama amemstiri na ujinga wake.
Sasa narudi upande wa kaka yako inapoendea wewe utataka mari ya wazazi wako kwa sababu ile nyumba na mtaji wa biashara ni Mari zenu wote.
Ila zile ndio zitafanya kaka yako aende kwa mganga ili akuue au akupe uchizi sasa saizi ni usiku sana naomba ulale.
Kesho nitakwambia nini ufanye sawa?.
” Jamani niliona dunia ina mambo mengi sana na kumbe kuna watu awana akili ya fikra kweli umtie uchizi kaka yako kwa ajili ya mapenzi.
Sasa ayo nimejifunza.
Mtihani unakuja nalala vipi na mwanaume kwenye godolo la mwanafunzi wale wasiojua godolo la mwanafunzi ni lile dogo.
Watu wawili mkilala lazima mgusane je uyu kaka ambaye mwanzo nilidhani chizi sasa najua yeye sio chizi.
Atopata isia juu yangu na akanilazimisha tendo lile la kikubwa zaidi.
Nawaza nawazua sina chupi ndani nimevaa shati lake.
Nashangaa yeye anasema joto Kari anavua shati na suluali amebaki na pensi tu nyepesi analala.
Ananiambia mimi lala sasa acha kukaa kitako.
” Mimi nimekaa kitako nimejiinamia nawaza itakuwaje?.
Naona kanishika bega kanilaza kifuani kwake anasema.
” Acha kujiinamia.
Mimi nipo kwa ajili yako nakupenda sana naomba unipe k….
PART 13
👉 Mimi nipo kwa ajili yako nakupenda sana naomba unipe k…👇
Kitu unachowaza Kwenye kichwa chako nishirikishe mimi kama nilivyo kushilikisha maisha yangu.
” Jamani nipo kifuani kwake nimelala sasa nimelala nimeangalia juu yani nimempa mgongo.
” Nikamwambia mimi nawaza mengi nitakwambia kesho.
” Akataka kuniambia kitu ila anasikia kuna mtu anatoa somo kupitia kwenye TV ya nyumba nyumba ya pili ila kaweka sauti kubwa na saa zile usiku sauti inatoka nje.
Kaka yule akasema uyo aliyepandisha sauti ya TV ni kiziwi kidogo yani ata mtu akimsalimia inabidi aongee kwa nguvu ndio amsikie.
Sasa akipenda kitu kwenye TV kazi mnayo majilani yani anafungua sauti ya juu aijalishi Kwake saizi saa ngapi.
Ila kipindi icho watu wengi wanakipenda na sasa ivi ni marudio yeye ndio anaangalia.
” Sasa mimi nasikia ni sauti ya yule kijana ambaye ata mimi wakati nipo kwa kaka nikipika namsikilizaga na amenifanya nimsikilize kwa sababu niliwai kumuona kwenye basi.
Sasa akawa anatoa somo hili…👇
Usiwe mfungwa kwa mambo yaliyokwishapita
Yalopita ndio yamepita na huna njia ya kuyarekebisha, hivyo kubaliana na hali
Ila yabaki ni funzo kwako na sio kifungo cha maisha
Lazima uruhusu maisha yanaendelea.
” Mimi nikamuuliza uyu kaka ivi mbona anafanana na wewe mambo yenu ya kuongea misemo masomo.
” Akaniambia unajua ata chizi kweli kweli anafanana na wewe au mtu yoyote pale anapokuwa amelala ila utofauti unakuja pale anapolala kalala wapi.
Ila usingizi ni ule ule.
Ata mimi na uyo tunafanana kabisa kazi zetu ila yeye anafanya kwenye vyombo vya habari mimi mtaani acha tumsikilize anasema nini.
” Jamani majibu yalinitosheleza nikaendelea kumsikiliza anachosema.
Sasa akawa anatoa somo hili…👇
Matokeo ya kuwadharau wanaume bora na kujichanganya na wanaume matapeli
Utakuja kujuta na kuchaganyikiwa pale utakapo ona wale wanaume bora ulio wadharau
Wanaoa wanawake ambao uliwaona hawana uzuri wowote mbele yako.
” Jamani mimi nikawa nacheka kweli kwenye ilo somo.
” Sasa uyu kaka akaniambia geuka basi tucheke wote.
” Jamani nawaza nikigeuka maziwa yangu yanagusana na kifua chake arafu naisi analo garden love kwenye kifua chake.
Maana hapa nimemlalia kwa mgongo nasikia galden love linanigusa mgongoni.
Jamani jamani uyu kaka ana makusudi mimi nawaza yeye kanigeuza.
Na shati nililolifunga kiunoni limefunguka na sijavaa kitu chochote ndani kwa sababu nilifukuzwa na kaka nikiwa uchi kabisa.
Sasa ili shati alinipa uyu uyu kaka msaada kwangu na ndio limefunguka nipo juu ya kifua chake.
Aliponigeuza madodo yangu yameshagusana na kifua chake kilichojaa nywele ambazo zinaitwa galden love.
Sasa nashangaa ananivutia Kwake zaidi.
Yani amenishika kichwa changu ananivutia kwake hili mdomo wangu ukutane na mdomo wake.
” jamani jamani dah yani mdomo wangu na wake ukakutana nga nga nga…
PART 14
👉 jamani jamani dah yani mdomo wangu na wake ukakutana nga nga nga…👇
Arafu yule kaka akaukwepesha kidogo mdomo wake ukawa umekuja kwenye sikio langu na mimi mdomo wangu umeenda kwenye sikio lake.
” Akaanza kuninong’oneza ivi.
Naomba uniache autakuwa na chuki kwenye moyo wako bari mapito unayopitia yatakuwa yanakomaza akili yako uyachukulie kama upo shule naongea na wewe kwenye sikio hili nia yangu maneno yapenye yakae kwenye nafsi yako.
” Jamani najishangaa na mimi nasema kwenye sikio lake ivi.
Sawa sitakuwa na chuki mimi na kisasi juu ya kaka bari nitaona kama nipo shule nasoma.
” Basi jamani nilivyojibu ivyo akanikumbatia kwa nguvu.
Sasa jamani naisi mwili wangu kama unaanza kuwa tofauti ivi kwa sababu maziwa yangu yamegusana na kifua chake.
Jamani na mimi ni mwanamke na yeye ni mwanaume kuna vitu vilikuwa vinajiseti vyenyewe.
Nikaona hapa nitashawishika kujalibu nisivyo vijua nikamuomba nitoke kifuani kwake lakini kwa kutumia akili ili asichukie.
Nikamwambia kaka naona joto naomba nilale hapo pembeni.
” Jamani sasa ndio nikapewa vitu vyengine vitamu.
Aliniweka pembeni akaanza kunipuliza kwa kupitia nguo yake.
Kumbe upepo wa kupulizwa mtamu kuliko wa feni jamani nasikia raha nikalala usingizi.
” Saa 11 alfajil akaniamsha akaniambia.
Sasa inatakiwa uvae izi nguo za kiume hili twende pale sokoni nitakupa pesa utakuwa unasubiri maduka ya funguliwe ununue nguo za kike.
Lakini mimi nitaenda kwa kaka yako kumwambia ukweli juu ya ukatiri aliokufanyia na wewe utakuwa upo sokoni mimi unajua misemo yangu inanipa pesa sana japo wao wanaona ndogo ila wanajisaau pesa ndogo ndio chanzo cha kubwa.
” Basi mimi nilivaa suluali na shati yani zimenitoa kama katuni maana ni kubwa sana.
Na kweli alinipa pesa na yeye akavaa mavazi yake ya uchizi tukaondoka.
Kweli kufika sokoni kuna mtu akampa 500 akamwambia nipe usemi ndugu yangu.
” Kaka yule ambaye wanamuona chizi akampa usemi mmoja mdogo tu na usemi wenyewe ulikuwa ni huu..
ukiona mwenye zamu ya kununua umeme kaludi na mshumaa jiongeze sio umkumbushe kitu jibu unalo.
” Yule jamaa aliyetoa pesa akacheka akasema hapo giza linausika maana jibu lake pesa ana hahahahahaha wewe ndugu yangu una misemo sana.
” Basi kaka chizi uyo akaondoka kwa kaka yangu kumwambia yale aliyopanga kumwambia.
” Bahati mzuri alimkuta na mkewe.
Akamwambia maneno aya..
” Samahani ndugu yangu ivi umewezaje kupata usingizi wakati umemfukuza mdogo wako au tuseme dada yako akiwa uchi wa mnyama?.
” Kaka akasema wewe usitake kuniambukiza uchizi wako kama nimemfukuza mimi zakia wewe anakuusu nini unamjua yule au unaleta nuxsi zako asubui asubui hapa.
” Kaka chizi akasema acha nikwambie kitu wewe ni limbukeni wa mapenzi na mapenzi ukiyavamia kichwa kichwa ilo neno ulilotamka hapo la kuwa mimi nataka nikuambukize uchizi nakwambia mapenzi yatakutia uchizi uyu mwanamke tena si mwanamke Bora ni mwanamke asiyefaa kwenye jamii asiyetaka kujua chimbuko lenu yeye kaja na yake na atatimiza yake na wewe utajuta nakwambia nione chizi kuna siku utakumbuka maneno yangu haya.
Naondoka na neno moja waliosema damu mzito kuliko maji awakumaanisha vyuma awajaviona au majabari mazito awakuyaona bari wana maana kubwa juu ya ule usemi naondoka.
” Yule mwanamke wa kaka akamwambia kaka NYAMAZA mwezi mchanga uyo anatafuta sababu amng’ate mtu.
” Na kaka akanyamaza.
” Sasa kaka chizi akaja sokoni wakamchangia pesa awape somo yeye ayo ndio maisha yake.
Wakati huo mimi nishaenda kununua nguo za kike nishaenda choo cha kulipia nikabadirisha zile nguo jamani pesa aikutosha kununua na chupi nilinunua taiti na sketi na blauzi tu.
Nguo zile za kaka chizi nimezitia kwenye mfuko nimezibeba namsikiliza na mimi kaka chizi kwenye kazi yake anayofanya pale akawa anaongea somo hili…👇
Inaelezwa Kuwa Wanawake wa Zamani Walikuwa na Utamu Asilia….Hali Hiyo Ilipelekea kutokuvunjika kwa Mahusiano Hovyo Kutokana na Ubora Waliokuwa Nao wa Ladha Zao.
Miaka ya Hivi Karibuni Wanawake Wamekosa Vitu vya Ziada Kwa Wapenzi wao Hali Ambayo Inapelekea Mahusiano Mengi Kuvunjika Mara Baada tu ya Tendo la Ndoa Inaelezwa Sababu kubwa ni Kutokuwa na Ladha Inayoeleweka Kwa Wanawake Kutokana na Ulimbukeni wa Vitu Vingi Wanavyoweka/ Kuingia Ukeni Unakuta Binti Kila Mwanamume Anayemtaka Basi Hajui Kukataa.
DADA TUNZA HIYO MALI ULIYOPEWA BURE NA MWENYEZI MUNGU NA KUMBUKA ALIIWEKA MOJA TU SEHEMU HIYO KWA AJILI YA MTU MMOJA TU (MWANAMUME) AMBAYE NDIYE CHAGUO ULILOCHAGULIWA NA ALLAH KUWA NA SUBRA MWANAMUME WAKO YUPO USIWE NA HARAKA YA NDOA MAANA UKIFANYA HARAKA UTAJIKUTA SEHEMU ZAKO ZA SIRI HAZINA MVUTO TENA HATA KWA MWANAMUME WA MAISHA YAKO.
” Watu walipiga kelele Weweeeeee.
Uku wanamuongeza pesa.
” Kaka chizi akasema somo lengine ni hili…👇
Si kila mwanaume anayechelewa kufanya malengo kwa Mwanamke basi hana malengo na huyo mwanamke hapana , wanaume wengine wanahitaji muda ili
kutimiza malengo hayo kulingana na hali zao . Muda mwingine ukosefu wa subira na uvumilivu
kwa wanawake wnafanya kuwaacha watu sahihi na kuingia kusiko sahihi .
” Watu wanapiga kelele sana yani sokoni kuna mambo mimi nikawa nacheka nikisema kimoyoni watu wanamchukulia chizi kumbe mzima na anajua anachofanya akamaliza na somo hili…👇
Taa Nyekundu
Ukiona taa nyekundu kwenye mahusiano yako ni bora ujitoe mapema, ili usije kuumia zaidi, amini akupendae kwa dhati utaona matendo yake na maneno machache ya kusindikiza ule upendo wenu. Kama mtu anakuambia anakupenda halafu huoni matendo yoyote, ujue mwenzio anakufanya wa “Mazoezi”, Mechi anaenda kuchezea kwingine.
” Hapo wote walifurahi akuna aliyejutia pesa yake kutoa.
” Sasa akaniambia mimi chukua pesa hii nenda kale kwanza mimi naenda kumtafuta dada nimstili na yeye na chai sawa?.
” Basi nikaenda kutafuta chai.
Jamani navuka barabara tu naingia mtaa ambao unayo mgahawa nakutana na kaka na mkewe.
” Sasa mkewe akamwambia kaka wewe si unaona nilikwambia anaye bwana uyu Jana si tulimuacha uchi Leo amevaa nguo mpya.
” Wakati huo yule mke wa kaka akaninyang’Anya ule mfuko wenye nguo za kaka chizi.
Sasa akasema unaona nguo za bwana ake izi hapa.
” Sasa kaka akanikamata anasema wewe umeanza umaraya sasa uyo bwana ako atakukuta tena uchi.
” Mimi namwambia kaka kaka kumbuka mimi ni dada yako.
” Kaka ajasikia ilo akanichania brauzi yangu yule mke wa kaka akaichana sketi yangu.
Jamani nilibaki na taiti ndani sina chupi.
” Sasa kaka akaishika taiti yangu aivute aichane na mkewe akaishika taiti yangu.
Yani wanataka kuivuta kwa pamoja waichane waniache uchi mimi dah yani….
PART 15
👉 Yani wanataka kuivuta kwa pamoja waichane waniache uchi mimi dah yani….👇
Sasa bahati mzuri akatokea mama mmoja mtu mzima alimtandika Kofi moja mke wa kaka.
Uku anasema wewe mpuuzi sana unapomvua nguo uyu binti unamdharirisha nani?.
” Jamani mara wakatokea wale wauni waliotaka kunibaka Jana usiku.
Wakasema uyu kumbe ndio alimvua uyu dada nguo sasa kama kukaa uchi kuzuri Leo atakaa yeye na tutamzungusha sokoni hapa.
” Jamani wauni walimkamata mke wa kaka wakamvua nguo na bahati mbaya kwake alikuwa kwenye siku zake.
Sasa kaka akataka kumtetea mkewe na yeye akavuliwa nguo.
Jamani mimi nilifumba macho tu.
” Jamani wauni si watu wazuri walichukua pedi ya mke wa kaka wakambandika nayo kaka kwenye makalio yake.
” Jamani wakaanza kuwatembeza sokoni.
Mpaka wagambo wa sokoni wanakuja kutoa msaada washatembezwa eneo kubwa la soko.
” Mimi sasa kaka chizi alikuja akaninunulia nguo zengine uku anasema acha wadhalilike.
” Sasa Sisi tunaondoka likasimama gali moja la kifahali wakamwita kaka chizi.
Wakampa Dili kubwa ya kuwa akatoe somo kwenye ndoa ya tajiri mmoja mjini amependa masomo yake.
” kaka chizi akasema sawa.
Walimpangia Siku na wakamwambia aje ivi ivi na mavazi yake yule tajili amependa sana masomo yako tofauti tofauti.
” Basi tuliludi kwake tukalala vizuri siku ikafika kaka chizi tukaenda wote kwenye iyo sherehe ya tajiri.
Sasa jamani kaka chizi siku iyo aliongea somo kila mmoja alimshangaa maana ata mimi nilimshangaa alitoa somo hili hapa…👇
Naam vipenzi vya Allah
WAJIBU WA MUME KWA MKEWE
Mahitaji ya lazima.
Ni katika jumla ya haki za mke zilizo katika dhima ya mumewe kupata mahitaji yake yote ya lazima.
Mume anawajibika kutoa gharama zote za mahitaji ya lazima ya mkewe, ikiwa ni pamoja na chakula bora cha kulinda, kujenga na kutia mwili nguvu. Ni wajibu wa mume kuhakikisha kuwa mkewe anapata maji safi na salama ya kunywa.
Ampatie mavazi yatakayomfaa katika vipindi/majira yote ya mwaka; nguo za masika na kiangazi.
Ni haki ya mke kupatiwa maskani yatakayomsitiri na kumpa amani na usalama wa nafsi, mali na akili. Kadhalika ni wajibu wa mume kumpa matibabu mkewe anapougua na kushirikiana nae kwa kumliwaza katika kipindi kigumu cha maradhi au ujauzito. Haya yote yamo katika agizo tukufu la Allah Mtukufu.
Nae Bwana mtume-Rehema na Amani zimshukie-amesema katika kuuonyesha wajibu huu wa mume ambao kwa mkewe ni haki:
Wana (hao wanawake) juu yenu (haki ya) chakula chao na nguo zao kwa wema (sharia) [Tirmidhiy]
Siku moja Bwana Mtume-Rehema na Amani zimshukie-aliulizwa ni ipi haki ya mke wa mmoja wetu juu yake, akasema:
Ni kumlisha utakapokula na kumvisha utakapovaa. Na wala usiupige uso (wake), wala usimtolee maneno machafu na wala usimuhame ila ndani ya nyumba (yenu)”.* [Ahmad, Abuu Daawoud na Ibn Maajah.]
Allah akurehemu ewe mume ikiwa utajua kwamba juhudi na uchovu wako katika kuhangaika kumpatia mkeo mahiataji yake haya. Hazipotei bure bali Allah anakulipa thawabu na ujira mkubwa._
Imekuja katika hadithi ya Sa’ad Ibn Abiy Waqaasw-Allah amuwiye radhi-kwamba Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-alimwambia:
Na hakika wewe hutotoa matumizi/gharama zo zote ukiikusudia dhati ya Allah ila utalipwa kwayo (gharama hizo). Hata (gharama za) kile unachokitia katika kinywa cha mkeo (yaani chakula)
Allah atutangulie
Sote ktk hilo
Aammyn.
” Watu wote walikuwa kwenye utulivu na somo limewaingia kisawa sawa.
” Basi kaka chizi aliambiwa kesho atapewa pesa na zawadi atachagua yeye anataka afanyiwe nini.
” Basi tulitoka pale tukaenda kuchukua chumba hotelini jamani ndio siku nimelala na kaka chizi kwenye godolo kubwa.
Sasa ndani kuna baridi Kari mimi sijui kumbe ac.
Namwambia kaka chizi nasikia baridi.
Yeye akaniambia sogea nikukumbatie.
” Na mimi nikasogea akanikumbatia tupo kitandani mikono yake anachezesha mgongoni kwangu nasikia raha.
Jamani najikuta na mimi nachezesha mikono mgongoni kwa kaka chizi.
” Dah kilichoendelea jamani dah yani..
INAENDELEA