Tuesday, April 29, 2025

Vidokezo 18 Muhimu kuhusu Ndoa - Fahamu haya Mambo

 Jiunge na Magroup yetu

TELEGRAM | FACEBOOK


 VIDOKEZO 18 VYA NDOA


1. Ukiolewa utawavutia sana wanaume wengine. Jifunze kuweka mipaka


2. Kila ndoa ina changamoto zake, zitambue njia za kuzitumia changamoto hizo kutunza ndoa yako


3. Unaweza kuwa tayari kuwa kwenye ndoa lakini ukiolewa na mtu ambaye hayuko tayari kuwa chaguo lako utachanganyikiwa sana. Usiwe unampenda mtu asiye sahihi kwako kwa njia sahihi


4. Tambua Kuna maisha ukiwa kwenye ndoa, Jaribu kufuata lengo lako binafsi lakini timiza kwa pamoja na mumeo


5. Mkioana lakini mkawa mnapenda ushindani tambua kuwa ndoa hiyo haitakufaa


6. Tafuteni shughuli za kufanya nyinyi nyote kwa pamoja kama wanandoa. Upendo hujengwa na shughuli mbalimbali


7. Kuwa mwangalifu unayependa kumsikiliza mmeo/mkeo. Baadhi ya watu hawafurahii kuwa katika ndoa zao au katika uchumba wao na huwafanya wenza wao kukosa furaha katika ndoa zako


8. Ndoa ina vipindi mbalimbali tofauti. Msimu wa pamoja, msimu wa migogoro ambapo nyote wawili mtastahili kutafuta suruhisho zenu ndani ya ndoa yenu kupitia mizozo mnayokutana nayo mara nyingi, kuna msimu wa majaribu ambpo nyinyi wawili mtakabiliana na sababu za kuachana na msimu huo wenye nguvu kwa pamoja na hapo mtapata ushindi wa pamoja.


9. Usipojitayarisha kwaajili ya watoto wako, watoto watakuwa na sababu ya kupunguza upendo na umakini mliokuwa nao kwa kila mmojawenu. Ndoa nyingi huingia kwenye mateso pale uzazi unapoanza tu


10. Kuna mtu anaangalia ndoa yako na anajifunza kutoka kwako. sasa jiulize anajifunza nini?


11. Masuala yote katika maisha yako ambayo hukuyamaliza ukiwa single, yatakuletea shida kipindi umeoa katika ndoa yako.


12. Kwa sababu ndoa ya baba yako ilifeli, haimaanishi kuwa na ndoa yako itafeli. na haimaanishi kuwa ndoa ya baba yako ilisitawi na kuwa njema basi na yako itakuwa hivyo. jifunze kupigania majukumu yako kibinafsi


13. Usimpe mke wako madaraka makubwa kiasi cha kukufanya upoteze maadili ndani ya ndoa yako, utaakakosa usingizi, utaishi maisha duni ya kimaskini na kuua ndoto zako.


14. Ndoa yoyote inaweza kustahimili anguko lolote ili mradi tu wawili hao wakiwa tayari kusameheana, kubadilika, kujitahidi kuhakikisha kwamba upendo unadumishwa, kuinuka na kuyashinda mapito.


15. Unapoanza kuzingatia sana na kuyaweka akilini madhaifu na mapungufu ya mwenzi wako, utayumbishwa na vituko vya muda mfupi.


16. Pesa inaweza kuwa sababu ya nyinyi kutoelewana chukua maamuzi ya kushughulikia hilo swala mnapokuwa wekeni urafiki ndani ya ndoa yenu na kuchukulia kuwa ndiyo msingi wa ndoa yenu.


17. Ukaribu ni zaidi ya kufanya mapenzi. Unganishaneni ndani zaidi ya kufika kileleni hasa miguso, kukumbatiana, kubembelezana, busu na mazungumzo mazuri


18. Wazazi wako wanaweza kuwa na nia njema lakini wanaweza kuharibu ndoa yako wanapofanya au kusema kwa kuzingatia mapendekezo yao, chuki, upendeleo, ukabila, kurudi nyuma, uchungu, ubinafsi, maumivu ya zamani au habari potofu. kumbuka wao Walikuwa na maisha yao, sasa na wewe ni wakati wa kujenga maisha yako.

Add Comments


EmoticonEmoticon