Tuesday, April 29, 2025

Kumteka Mumeo na Kumuweka kwenye Mikono yako - Fanya haya Mambo

 Jiunge na Magroup yetu

TELEGRAM | FACEBOOK


 MAMBO 23 YA KUFANYA ILI KUMWEKA MUMEO KWENYE MIKONO YAKO MUDA WOTE


1. Mwite jina lake kimapenzi

2. Mruhusu atumie mamlaka yake akiwa kama kichwa cha familia.

3. Usimuongezee changamoto anapokuwa hayupo sawa.

4. Jaribu kujishusha anapokuwa na hasira. Unaweza kuutumia muda wakati atakapokuwa katika wakati wa utulivu na atakuomba msamaha na kukuelezea kwa nini alifanya hivyo ambayo vilikukasirisha.

5. Kuwa mwepesi wa kusema neno"Samahani mpenzi" wakati wowote unapomkosea, msisitizie msamaha wake, thamini na kumbusu anapokukosea.

6. Mzungumzie vizuri mbele ya Marafiki zake na ndugu zake.

7. Waheshimu wazazi wake

8. Jitahidi kuwanunulia wazazi wake zawadi na hivyo hakikisha kwamba nayeye anafanya hivyo kwa wazazi wako

9. Mshangaze kwa kutumia sahani au vyombo anayopenda hasa wakati akiwa hana pesa mkononi na usicheleweshe chakula chake.

10. Usimruhusu kijakazi kumhudumia chakula mmeo unapokuwa nyumbani. Kwa sababu unaweza kumpoteza mme kwa kijakazi wako.

11. Mpe mapokezi mazuri kwa kumkumbatia anaporudi nyumbani, kwa kumpokea mizigo yake na kumsaidia kumvua nguo.

12. Tabasamu unapomtazama na kumpa midomo ya hapa na pale mnapokuwa nje ya jamii.

13. Msifie mbele ya watoto wenu nyakati fulani.

14. muogeshe mgongo wake mkiwa bafuni wakati wa kuoga.

15. kuna wakati uwe unaweka ujumbe wa upendo kwenye meza ya chakula cha mchana au usiku.

16. Piga simu na mwambie kuwa umemumis.

17. Piga simu yake na ukisikia neno "hello" mwambie tu unampenda.

18. Ikiwa yeye ni mtu wa umma au mwanasiasa, mwamshe kwa upole asubuhi na mapema na umuandalie vitu kwa kiwango cha mahitaji yake..

19. Mwambie jinsi unavyojisikia kuwa na bahati yeye kuwa mume wako.

20. Mkumbatie bila sababu.

21. Mthamini Mungu kwa ajili ya Adamu wa maisha yako.

22. Kumbuka daima kumwombea dua.

23. Ombeni pamoja na pia salini pamoja kabla ya kwenda kulala usiku

Add Comments


EmoticonEmoticon