Tuesday, April 29, 2025

Alama Kuu za Uaminifu katika Mahusiano ya Kimapenzi

 Jiunge na Magroup yetu

TELEGRAM | FACEBOOK


HIZI NDIYO ALAMA KUU ZA UAMINIFU NA MAANA ZAKE...

1. Kulala karibu na mwenzi wako bila uoga, na kuwa na uhakika kwamba hatokudhuru.

2. Kuzaa watoto mkiwa pamoja nyakati zote za malezi pasipo kumtelekezea mmoja majukumu ya ulezi

3. Kutambulishana kwa wazazi na familia zenu, ikiwa unauhakika kwamba utawaheshimu na kuwapenda wazazi wake kama wako.

4. Kula chakula ambacho amepika mwenzi wako bila uoga, ukijiamini kuwa hakiwezi kuwa na sumu.

5. Kukutazamana hasa mmoja wenu akipita mlango wa nyumba, ili kuhakikishiana kuwa hatafanya chochote cha kuhatarisha familia yenu isije kuingia kwenye maisha hatarishi.

6. Kuwekeza mapenzi thabiti pasipo kuingiza uwezo wa kipesa ni kufanya juhudi kwa hisia zenu wenyewe, huku mkijua kuwa kuna msingi thabiti unaofanya penzi lenu liende

7. Kukabidhiana miili yenu kitandani bila hofu ya kuwa mwenzio sio mwaminifu kuwa anakuchezea tu au kuhisi kuletewa magonjwa ya zinaa .

8. kuishi na mwenzio pasipo na haja ya kukagua simu ya mwenzio kila mara simu na meseji zinavyoingia, kwa sababu huenda akawa hafanyi chochote cha aibu huko nje.

9. kutokujali kiburi cha mwenzio hasa akiwa na ww

10. Kuwa na amani unapokuwa mbali na na mwenzio kimwili na kiakili, na kuondoa mawazo ukijua utafanya ujinga

11. kuhifaddhi maneno mnayozungumza mkiwa wote maana kesho mengine hujirudia

12. kujipa ujasiri wa Kufumba macho yako kwa kujiamini, ukijua upo salama mikononi mwake.

13. Kukuteteana pale wengine wanapowashambulia bila sababu za msingi, hasa mkijua kwamba mnafaa kupiganiana.

14. Kupeana maisha na kuishi pamoja, huku mkijua hamtajuta kwa maisha mliyoyachagua.

 

Add Comments


EmoticonEmoticon